08/03/2026
NANI anapenda kuwa mgonjwa?
Hakuna anayependa, kwa kuwa ugonjwa ni kikwazo na ni chanzo cha gharama.
Unapokuwa mgonjwa, huhisi tu vibaya bali pia huenda ukashindwa kwenda kazini au shuleni, kutafuta pesa, au kuitunza familia yako.
Huenda hata ukahitaji mtu fulani akutunze, na huenda ukahitaji kulipia gharama za dawa na matibabu.
Kuna msemo usemao “Kinga ni bora kuliko tiba.”
Baadhi ya magonjwa hayaepukiki.
Hata hivyo, bado kuna mambo mengi unayoweza kufanya ili kupunguza au hata kuzuia kuanza kwa ugonjwa.
Fikiria mambo matano unayoweza kufanya ili kuwa na afya bora
1 DUMISHA USAFI
njia moja bora zaidi ya kujikinga na ugonjwa na kuepuka kueneza ugonjwa” ni kunawa mikono. Ni rahisi kupata homa au mafua k**a utagusa pua au macho yako huku mikono yako ikiwa na viini. Njia bora ya kujilinda na maambukizi ni kunawa mikono yako kwa ukawaida. Kudumisha usafi kunaweza pia kuepusha kuenea kwa magonjwa hatari k**a vile, nimonia na magonjwa ya kuharisha, ambayo kila mwaka husababisha vifo vya watoto zaidi ya milioni mbili, walio chini ya umri wa miaka mitano.
Hata kuenea kwa ugonjwa hatari wa Homa ya ini, kunaweza kupunguzwa kwa kuwa na kawaida ya kunawa mikono.
2 TUMIA MAJI SAFI
3 KULA CHAKULA KINACHOFAA
4 FANYA MAZOEZI
BILA kujali umri wako, unahitaji kufanya mazoezi kwa ukawaida ili uwe na afya nzuri. Watu wengi leo hawafanyi mazoezi ya kutosha. Kwa nini ni muhimu kufanya mazoezi? Kwa sababu kufanya mazoezi kunaweza kukusaidia:
Kulala vizuri.
Kuweza kutembea kwa wepesi.
Kuwa na mifupa na misuli yenye nguvu.
Kudumisha au kuwa na uzito wa mwili unaofaa kiafya.
Kupunguza hatari ya kuwa na ugonjwa wa kushuka moyo.
Kupunguza hatari ya kufa mapema.
Ikiwa haufanyi mazoezi, huenda ukapatwa na:
Ugonjwa wa moyo.
Ugonjwa wa kisukari aina ya 2.
Kupatwa na shinikizo la damu.
Mwili kuwa na kiwango cha juu cha kolesteroli.
Kupatwa na kiharusi
5 LALA VYA KUTOSHA
KIASI kinachohitajika cha usingizi kinatofautiana kati ya mtu mmoja na mwingine. Watoto wengi wachanga hulala saa 16 hadi 18 kwa siku, watoto kuanzia umri wa mwaka mmoja hadi mitatu hulala saa 14 na wale wenye umri wa miaka mitatu hadi minne hulala saa 11 au 12 hivi. Watoto walio na umri wa ku