AFYA MAMA NA MTOTO

AFYA MAMA NA MTOTO Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from AFYA MAMA NA MTOTO, Dar es Salaam.

JE! NITARAJIE KUJIFUNGUA LINI?🤔Moja kati ya maswali yanayowasumbua wajawazito wengi ni “je! Nitarajie kujifungua lini?” ...
02/07/2024

JE! NITARAJIE KUJIFUNGUA LINI?🤔

Moja kati ya maswali yanayowasumbua wajawazito wengi ni “je! Nitarajie kujifungua lini?” k**a ww ni mmojawapo unayejiuliza swali k**a hili, usihofu majibu yako yatapatikana hapa.

FAIDA YA KUJUA TAREHE YA KUJIFUNGUA

*Humsaidia mjamzito kujiandaa kimwili na kisaikolojia kwa ajili ya mapokezi ya mtoto, mf; kupanga likizo ya kutoka kazini , kuandaa chumba cha mtoto n.k.

*Humsaidia mjamzito kuandaa vifaa vya kujifungulia mapema.

*Inasaidia kujipanga kifedha ili kujilinda na kumlinda mtoto kutokana na changamoto za uzazi.

*Inasaidia kuwezesha ufuatiliaji mzuri wa ujauzito na kuhakikisha unaenda kliniki kwa wakati unaofaa.

*Inasaidia kupanga safari ya kujifungua k**a utajifungulia kwenye hospitali husika.

JE! WIKI ZA KUJIFUNGUA NI ZIPI?

Mjamzito anatakiwa au anatarajiwa kujifungua kati ya wiki ya 36 hadi 40, ndani ya wiki hizi mtoto huwa salama zaidi. Haitakiwi kupungua au kuzidi wiki, ikiwa wiki zitapitiliza inabidi kumuona daktarin kwa ushauri.

N/B; lakini mara nyingi k**a unahudhuria kliniki k**a inavyotakiwa itajulikana mapema zaidi.

USHAURI / CHANGAMOTO MBALIMBALI ZA UJAUZITO NA UZAZI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0627292775


DALILI ZA HATARI KIPINDI CHA UJAUZITOKila mama mjamzito pamoja na familia yake wanapaswa kufahamu hatari zinazoambatana ...
04/03/2023

DALILI ZA HATARI KIPINDI CHA UJAUZITO

Kila mama mjamzito pamoja na familia yake wanapaswa kufahamu hatari zinazoambatana na ujauzito pamoja na kujua dalili zinazoashiria matatizo yanayoweza kuhatarisha mimba.

Zifuatazo ni dalili ambazo zikionekana kwa mama mjamzito anapaswa kuwahishwa hospitali kwa ajili ya kupata matibabu ya haraka kutoka kwa wataalamu wa afya;

●Kutokwa na damu ukeni wakati wa ujauzito
●Mtoto kutokucheza baada ya miezi mitano
●Maumivu makali ya kichwa
●Kutapika sana kupita kiasi
●Uvimbe usio wa kawaida wa uso , miguu au mikono
●Maumivu makali ya tumbo
●Kukak**aa kwa viungo
●Kupata homa kali
●Chupa kupasuka kabla ya kutimia kwa muda wa kujifungua [Maji mengi kutoka ukeni ]
●Harufu mbaya ukeni [Hii ni dalili ya maambukizi ]

KARIBU KUJIUNGA NA DARASA LETU LA WHATSAPP KWA MAFUNZO MENGI ZAIDI.

ADA YA KUJIUNGA
SH 5000/= TUU



Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255782885172

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when AFYA MAMA NA MTOTO posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram