IJALI AFYA YAKO

IJALI AFYA YAKO Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from IJALI AFYA YAKO, Medical and health, Dar es Salaam.

Tunasaidia kutatua Matatizo yote ya mfumo mmbovu wa mmeng'enyo wa chakula kama Choo kigumu, Bawasili, Vidonda vya Tumbo, Tumbo kujaa gesi, Kiungulia, kukosa hamu ya kula, kutapika damu n.k

*JINSI YA KUEPUKANA NA VIDONDA VYA TUMBO* 🥑Kunywa maji mengi *Kila uamkapo asubuhi hakikisha unakunywa maji ya kutosha y...
15/01/2025

*JINSI YA KUEPUKANA NA VIDONDA VYA TUMBO*

🥑Kunywa maji mengi

*Kila uamkapo asubuhi hakikisha unakunywa maji ya kutosha yasiwe ya baridi sana au ya moto.*
*Hakikisha maji unakunywa kabla ya kusafisha kinywa.*

🥑Punguza mawazo, fanya mazoezi yatakayo kupunguza mawazo
*Fanya kitu ambacho unaweza kuwa na furaha na Kusahau Mambo yote yanayokusumbua.*

🥑Punguza (balansi) kiwango cha lehemu (choresterol)
*Epuka vyakula vyenye mafuta mengi au vya kusindikwa viwandani*

🥑Usivute sigara
🥑Punguza au acha kunywa pombe
🥑Kula vizuri vyakula bora hasa asilia na sio vyakula vyenye kemikali
🥑Lala vizuri kwa muda mzuri – masaa 7 hadi 9

K**a tatizo hili limekua sugu sana au unahisi kuwa na dalili za vidonda vya tumbo
Tuwasiliane kwa simu namba 0749800898

*KUTOPATA CHOO KWA MUDA MREFU AU KUPATA CHOO KIGUMU - (CONSTIPATION) - SULUHISHO* *CONSTPATION NI NINI ?**Hili ni Tatizo...
04/01/2025

*KUTOPATA CHOO KWA MUDA MREFU AU KUPATA CHOO KIGUMU - (CONSTIPATION) - SULUHISHO*

*CONSTPATION NI NINI ?*

*Hili ni Tatizo la kutopata Choo Kwa *Muda Mrefu au Kupata Mara Chache*
*Lakini Kwa Shida Sana na Nguvu* *Kubwa huwa inatumika.*

*CHANZO CHA CONSTIPATION NI NINI ?*
*Constipation inasababishwa na mfumo mbovu wa mmeng'enyo wa chakula*
*Kwenye utumbo mdogo ambao una urefu wa takribani mara 10 mpaka 13 ya urefu wa mtu husika , Kwenye Utumbo huo kuna Villars , hivi ni k**a vidole ambavyo muda Wote huwa vinachezacheza ili kumeng'enya chakula*

*K**a Unapata Choo Mara Moja(1) Kwa SIKU Na Unakula Mara Tatu (3) Upo Kwenye Hatari Kubwa Ya Kupata Magonjwa Yafuatayo:*

~*Kansa ya Utumbo.*
~*Uzito uliozidi.*
~*Bawasir i(Vinyama sehemu ya haja kubwa).*
~*Maumivu ya Kiuno , Mgongo , Mabega , Kichwa , Misuli.*
~*Kukosa usingizi(Insomnia)*
~*Kukosa hamu ya kula (Loss of appetite).*
~*Tumbo kujaa gesi.*
~*Vidonda vya tumbo (Ulcers).*
~*Upungufu wa nguvu za kiume.*
~*Kushindwa kubeba mimba au kuzaa ( Ugumba ).*

Kwa huduma zaidi 0749800898

28/11/2024

Tatizo la bawasili limekua ni tishio kubwa miongoni mwa watu,
Pale Inapofikia hatua ya kulazimika kwenda kufanyiwa upasuaji wa kuondoa kile kinyama sehemu ya haja kubwa.
Kuna hatari yankupoteza maisha pale unapofanyiwa upasuaji,
endapo tu yakifanyika makosa ya kukatwa kwa mshipa wa damu wa sehemu ile ya haja kubwa, uwezekano wa kupoteza maisha unakuwa mkubwa, kutokana na damu amabazo zitachuruzika sehemu ile.

Ondokana leo na tatizo hili kwa kutumia tiba, amabazo zitaenda kudeal moja kwa moja na chanzo cha tatizo hili
Wasiliana nami kwa namba 0749800898 kupata tiba yako.

FAHAMU KUHUSU KIUNGULIA.⭐ KIUNGULIA ni Hali ya kuwaka moto ambayo hupelekea maumivu kwenye kifua na Koo kutokana na asid...
04/11/2024

FAHAMU KUHUSU KIUNGULIA.
⭐ KIUNGULIA ni Hali ya kuwaka moto ambayo hupelekea maumivu kwenye kifua na Koo kutokana na asidi ya tumboni kupanda juu kwenye Koo la chakula.

SABABU ZINAZOPELEKEA KUPATA KIUNGULIA.
👉Ulaji wa vyakula vyenye pilipili na viungo vingi.
👉Ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi.
👉Ulaji wa chocolate.
👉Kula Milo mikubwa na kulala mara baada tu ya kumaliza kula.
👉Ujauzito.
👉 Unywaji uliopitiliza wa vinywaji vya kaboni k**a soda.
👉Ulaji wa matunda yenye asidi k**a machungwa,nanasi.

NJIA ZA KUEPUKANA NA KIUNGULIA.
👉Kula kwa kiasi na kwa utaratibu.
👉Kula vyakula vya alkali k**a parachichi, karanga na ndizi.
👉Pendelea kutumia chai ya tangawizi.
👉Kuacha kulala mara baada tu ya kumaliza kula.
👉Punguza unywaji wa vinywaji vyenye gesi k**a soda na pombe.

Kwa ushauri zaidi na tiba kwa kutumia virutubisho lishe
Wasiliana nami 🤗.
0749800898

Bawasiri, kwa kitaalamu inajulikana k**a hemorrhoids, ni hali ambapo mishipa ya damu iliyoko katika eneo la rektamu (seh...
23/10/2024

Bawasiri, kwa kitaalamu inajulikana k**a hemorrhoids, ni hali ambapo mishipa ya damu iliyoko katika eneo la rektamu (sehemu ya mwisho ya utumbo mkubwa) au kwenye puru (mkundu) huvimba na kutokea nje. Mishipa hii inapovimba inaweza kusababisha maumivu, kuwasha, na kutokwa na damu wakati wa kujisaidia.

Kuna aina mbili za bawasiri:

1. Bawasiri za ndani (internal hemorrhoids): Hizi zinatokea ndani ya rektamu na kwa kawaida hazisababishi maumivu makali, lakini zinaweza kusababisha damu wakati wa kujisaidia.
2. Bawasiri za nje (external hemorrhoids): Hizi zinatokea kwenye eneo la nje la puru na mara nyingi husababisha maumivu, kuwasha, na hata kuganda kwa damu ndani yake, jambo linaloweza kuleta maumivu makali zaidi.

Sababu za Bawasiri

• Kushinikiza wakati wa kujisaidia: Hii ni sababu kuu ya bawasiri, kwani inaongeza shinikizo kwenye mishipa ya damu katika eneo la puru.
• Kukaa kwa muda mrefu chooni: Kukaa muda mrefu chooni au kushindwa kupata choo inaweza kusababisha shinikizo kwenye mishipa ya damu.
• Kukosa nyuzinyuzi (fiber) kwenye chakula: Ulaji mdogo wa vyakula vyenye nyuzinyuzi huchangia kupata choo kigumu na kusababisha kushinikiza zaidi wakati wa kujisaidia.
• Uzito mkubwa au ujauzito: Mambo haya yanachangia shinikizo kwenye eneo la chini la mwili, hali inayoweza kusababisha bawasiri.
• Kuharisha au kuvimbiwa kwa muda mrefu: Hali hizi zinaweza kuongeza hatari ya bawasiri.

Dalili za Bawasiri

• Kutokwa na damu nyekundu wakati wa kujisaidia
• Maumivu au kuwasha kwenye eneo la puru
• Kuvimba au kuwa na donge kwenye eneo la puru
• Maumivu makali wakati wa kujisaidia, hasa kwa bawasiri za nje

Matibabu na Kinga

• Ulaji wa vyakula vyenye nyuzinyuzi k**a matunda, mboga, na nafaka zisizokobolewa huweza kusaidia kulainisha choo na kupunguza shinikizo wakati wa kujisaidia.
• Kunywa maji ya kutosha: Hii husaidia kulainisha choo na kuzuia kuvimbiwa.
• Kuepuka kukaa muda mrefu chooni: Kupunguza muda unaotumia chooni husaidia kupunguza shinikizo kwenye mishipa ya damu ya eneo la puru.
• Kutumia dawa za kutuliza maumivu k**a vile krimu au mafuta maalum kwa ajili ya bawasiri, ambazo hupunguza kuwasha na maumivu.

Kwa bawasiri sugu au kali, mara nyingi madaktari wengi ufanyiwe upasuaji au utaratibu wa dawa za kupooza bawasiri.

Wasiliana nasi leo tukupe tiba ya kudumu ya kuondokana na tatizo hili.!
Wasiliana nami kwa namba ya simu 0749800898

Habari zenu wapendwa Leo tujifunze kuhusu constipation (kupata choo kigumu)🟤 Constipation ni Hali ya Ugumu wa kutoa kiny...
20/10/2024

Habari zenu wapendwa
Leo tujifunze kuhusu constipation (kupata choo kigumu)
🟤 Constipation ni Hali ya Ugumu wa kutoa kinyesi unapoenda haja kubwa kutokana na kinyesi kuwa kigumu na kikavu.

Sababu:
🟤Ulaji wa vyakula vyenye kiwango kidogo Cha kambakamba/fibres k**a parachichi,mboga za majani,nafaka zisizokobolewa

🟤Kutokunywa maji mengi.

🟤Msongo wa mawazo

🟤Kutoshughulisha mwili kwa kufanya mazoezi.

🟤Uzito mkubwa.

🟤 Matumizi ya dawa za kupunguza maumivu(opioids), antidepressants na shinikizo la damu.

🟤 Matatizo ya kiafya K**a ugonjwa wa kisukari.

Dalili
🟤Kupata kinyesi kigumu na kikavu.

🟤 Kwenda haja kubwa mara chache

🟤Kukosa hamu ya kula.

🟤 Maumivu wakati wa haja kubwa.

🟤Kutoa kinyesi chenye damu

🟤Tumbo kujaa gesi.

Madhara ya kupata choo kigumu kwa muda mrefu.
🟤 Bawasiri (vinyama vinavyoota kwenye njia ya haja kubwa)

🟤Mwili kudhoofu.

🟤 Saratani ya utumbo mpana

🟤Michubuko kweny njia ya haja kubwa(anal fissure)

Kwa ushauri zaidi na tiba kwa kutumia virutubisho lishe
Wasiliana nami.
kwa namba 0749800898

VIDONDA VYA TUMBO   ULCERS🌱✨ Vidonda vya Tumbo (Peptic Ulcers): Sababu, Dalili, na Njia za Kujisaidia ✨🌱Vidonda vya tumb...
10/10/2024

VIDONDA VYA TUMBO ULCERS

🌱✨ Vidonda vya Tumbo (Peptic Ulcers): Sababu, Dalili, na Njia za Kujisaidia ✨🌱

Vidonda vya tumbo ni vidonda vinavyotokea katika ukuta wa tumbo au sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo (duodenum). Hali hii inaweza kusababisha maumivu makali na usumbufu.

Sababu za Vidonda vya Tumbo:

- 🦠 Bakteria ya H. pylori: Bakteria hii ni sababu kuu ya vidonda vya tumbo.

- 💊 Matumizi ya Dawa: Dawa za anti-inflammatory (NSAIDs) zinaweza kuharibu ulinzi wa ukuta wa tumbo.

- 🥵 Mizigo ya Stress:Stress inaweza kuongeza uzalishaji wa asidi tumboni, ikichangia kuunda vidonda.

Dalili za Vidonda vya Tumbo:

- 😖 Maumivu ya Tumbo:Maumivu yanayokuja na kuondoka, mara nyingi yanajitokeza baada ya chakula.

- 🤢 Kichefuchefu: Huwa na dalili za kichefuchefu na kutapika.

- 🍽️ Kukosa Hamu ya Chakula: Watu wengi hupata matatizo ya kula kutokana na maumivu.

Njia za Kujisaidia kwa Matunda na Mbogamboga:

- 🍌 Banana: Husaidia katika kupunguza asidi tumboni na kuimarisha kinga ya mwili.

- 🍏 Mizizi ya Ginger: Ina mali za kuzuia uchochezi na husaidia katika kumeng’enya chakula.

- 🥬 **Spinach:** Ina virutubisho vinavyosaidia kuimarisha afya ya tumbo.

- 🍊 Machungwa: Vitamini C husaidia katika kuimarisha mfumo wa kinga.

Kumbuka: Ikiwa unakabiliwa na dalili za vidonda vya tumbo, tafadhali usisite kuwasiliana nasi kwa matibabu na ushauri zaidi. 🌿💚

Tupigie kwa namba ya simu 0749800898

ZIJUE VIASHIRIA VYA TATIZO LA BAWASIRIBawasiri (au hemorrhoids) ni uvimbe wa mishipa ya damu kwenye eneo la puru. Viashi...
03/10/2024

ZIJUE VIASHIRIA VYA TATIZO LA BAWASIRI

Bawasiri (au hemorrhoids) ni uvimbe wa mishipa ya damu kwenye eneo la puru. Viashiria vya bawasiri ni pamoja na:

1. Maumivu au usumbufu wakati wa kujisaidia - Maumivu haya ni makali zaidi wakati wa kinyesi.

2. Kuvimba au kuwasha eneo la puru - Kuwasha au hisia za uchomekevu katika eneo la puru.

3. Kutokwa damu - Wakati mwingine kunaweza kuwa na damu nyekundu kwenye kinyesi au karatasi ya choo baada ya kujisaidia.

4. Uvujaji au hisia ya uvimbe - Unaweza kuhisi uvimbe mdogo au mkubwa unaojitokeza nje ya puru (bawasiri za nje).

5. Kuhisi kinyesi hakijaisha - Hisia k**a kwamba haja kubwa haijaisha kikamilifu hata baada ya kujisaidia.

Ikiwa unahisi dalili hizi, ni muhimu kuwasiliana na mtaalamu wa AFYA kwajili ushauri wa matibabu, ikiwemo kupata tiba ya kudumu .
Kwa mawasiliano zaidi piga simu number
0749800898

NOTE ✍️
Kadri unavyozidi kukaa na tatizo ndivyo unavyozidi kuhatarisha Afya, pamoja na gharama ya matibabu
Tatizo hili haliishi kwa kufanyiwa upasuaji.
Na upasuaji huatarisha uhai wako.

NJOO LEO UCHUKUE TIBA, ITAKAYOMALIZA TATIZO LAKO BILA UPASUAJI📌....0749800898

*BAWASIRI {HEMORRHOIDS/PILE*➖ Ni ugonjwa unaotokana na kuvimba kwa mishipa ya damu katika mfereji wa njia ya haja kubwa ...
29/09/2024

*BAWASIRI {HEMORRHOIDS/PILE*
➖ Ni ugonjwa unaotokana na kuvimba kwa mishipa ya damu katika mfereji wa njia ya haja kubwa na kuoelekea kuota kinyama sehemu ya haja kubwa

*CHANZO CHA BAWASIRI*
➖ Tabia ya kuketi sehemu moja kwa muda mrefu mfano; madereva
➖ Tatizo sugu la kuharisha
➖ Ujauzito
➖ Uzito wa mwili kupita kiasitt
➖ Kufanya ngono kupitia tundu la haja kubwa (kulawitiwa)
➖ Kupata haja kubwa ngumu
➖ Kua na mgandamizo mkubwa tumboni
➖ Kunywa pombe
➖ Kula sana nyama nyekundu
➖ Vidonda vya tumbo
➖ Ngiri(Chango/Hernia
➖ Kula sana pilipili
➖ Kunyanyua vitu vizito

*DALILI ZA BAWASIRI*
➖ Kupata muwasho mkali katika eneo la juu la haja kubwa
➖ Kujitokeza kwa kinyama eneo la haja kubwa
➖ Kutokewa na kiuvimbe katika tundu ya haja kubwa
➖ Kupata kinyesi chenye damu
➖ Kupata maumivu makali wakati wa
kujisaidia haja kubwa
➖ kutokwa na uteute sehemu ya haja kubwa
➖ Kupata maumivu makali wakati wa kujisaidia kutokana na choo kigumu aunmichubuko n.k

Tatizo hili linatibika vizuri sana bila upasuaji
ila jitahidi usiendelee kuka nalo kwani itakugharimu sana

Kwa tiba ya na ushauri wasiliana nami kwa namba 0749800898

Zijue Sababu, Madhara na Tiba ya Kukosa Choo/Choo Kigumu ‘Constipation’✍🏻Tatizo la kukosa choo (constipation) ni tatizo ...
26/09/2024

Zijue Sababu, Madhara na Tiba ya Kukosa Choo/Choo Kigumu ‘Constipation’

✍🏻Tatizo la kukosa choo (constipation) ni tatizo ambalo limekuwa likiwakumba watu wengi sana katika dunia, watu wamekuwa wakiteseka bila kujua nini chanzo cha tatizo hili na vipi kuliondoa tatizo hili na wengine wamekuwa wakilipuuzia bila kujua madhara ambayo wanaweza kuyapata kutokana na tatizo hili.

✍🏻Kukosa choo hutokea pale mtu anakula vizuri lakini unakata siku tatu hadi nne bila kupata choo. Ukiona unakula kutwa mara tatu na unakaa siku mbili hadi tatu huendi chooni au unatoa choo kigumu k**a mbuzi hilo ni tatizo kwako.

✍🏻Tafiti zinaonyesha mtu anaweza kupoteza maisha k**a atakosa choo kwa siku tano hadi saba mfululizo. Watu wengi hulidharau tatizo hili lakini linamadhara makubwa tofauti na wanavyofikiria.

Sababu za Kukosa Choo/Choo Kigumu

👉🏿Kupenda kula sana vyakula vilivyokobolewa k**a vile ugali wa sembe, mikate.
👉🏿Ukosefu wa mbogamboga za majani na matunda ya nyuzi nyuzi/faiba k**a machungwa huongeza tatizo hili. Kila mtu unatakiwa kula matunda aina mbili na mboga za majani aina mbili kila siku.
👉🏿Matumizi makubwa ya pombe na sigara.
👉🏿Unywaji mdogo wa maji, Kila mtu anapaswa kunywa maji kwa kiwango cha chini lita 3 kila siku na usinywe maji wakati unakula, kunywa maji nusu saa kabla au baada ya kula.
👉🏿Matumizi mabaya ya madawa. Mfano dawa za presha, aleji n,k.
👉🏿Kuugua kisukari au ugonjwa wa misuli.
👉🏿Kansa ya utumbo mpana.
👉🏿Msongo wa mawazo: watu wanaopata msongo mkubwa wa mawazo huharibu mpangilio wa homone zao pamoja na kuathiri uzalishaji wa visambaza taarifa kwenye mwili na hivo kusababisha shida kwenye misuli, kupata mcharuko/mpambano ndani ya mwili (inflammation) nakuathiri ufanyaji kazi wa enyzmes ambazo husaidia kumeng’enya chakula.

👉🏿Kutoshughulisha mwili: mazoezi yanasaidia kuimarisha mzunguko wa damu kwenye mfumo wa chakula na kuimarisha misuli na hivo kurahisisha utolewaji wa kinyesi. Utafiti unasema watu wanaotumia mda mwingi wakiwa wamekaa hasa maofsini wanaongoza kwa kuapata matatizo ya kukosa choo kwa mda mrefu.
👉🏿Matumizi ya baadhi ya vidonge: baadhi ya vidonge husababisha kukosa choo kwa muda mrefu na kupata choo kigumu, mfano dawa za kupunguza maumivu, dawa za kuconrtol stress, dawa za kulevya, virutubisho vya calcium na magnesium na antiacids.

👉🏿Ukuaji wa bacteria wabaya kwenye mfumo wa chakula: bacteria wazuri/normal flora waliopo kwenye mfumo wa chakula tunawaita probiotics husaidia kwenye uchakataji wa chakula. Ndio maana kuna umuhimu wa kula vyakula vye kambakamba kwa sababu ni mbolea nzuri kwa bactetia wazuri kukua na kufanya kazi.

👉🏿Matatizo ya tezi ya Thyroid na matatizo mengine ya homoni: matatizo k**a kisukari, kukoma hedhi, maumivu kabla ya hedhi na ufanyaji kazi hafifu wa tezi ya Thyroid huweza kusababisha kupata constipation. Magonjwa mengine ni k**a Pakinson disease, ajali ya uti wa mgongo na matatizo mengine ya neva yanaweza kusababisha Constipation.

Madhara Yatokanayo na Kokosa Choo

➡️Unaweza kuugua saratani ya utumbo mpana.
➡️Unaweza kupata tatizo la tumbo kujaa gesi.
➡️Figo yako inaweza isifanye kazi vizuri.
➡️Unaweza sababisha magonjwa ya moyo.
➡️Unaweza pata tatizo la kukak**aa mishipa ya damu ambapo utasababisha miguu kuwaka moto na ganzi miguuni au mikononi
➡️Unawezasababisha magonjwa ya ini
➡️Unawezapata kisukari
➡️ Upungufu wa nguvu za kiume na kulegea uke baada ya Msuli wa Pelvic kulegea

Tiba Ya Lishe Kwa Tatizo La Constipation

➡️Vyakula vyenye kambakamba/fibers kwa wingi; karanga, nafaka isiyokobolewa, maharage, mboga za majani, na mbegu. Parachichi, broccoli, apple na viazi vitamu
➡️Mbogamboga za kijani: zina madini mengi ya magnesium ambayo husaidia katika ufanyaji kaz mzuri wa misuli na hivo kupunguza tatizo la constipation.
➡️Tumia kinywaji cha uvuguvugu: k**a una tatizo la constipation jaribu kutumia chai ya moto asubuhi, au tumia maji yaliyochanganywa na limau.

Vyakula vya Kuacha Kabisa Kutumia kwa Mgonjwa wa Constipation ni pomoja na:
👉🏿Vyakula vilivyokaushwa kwenye mafuta
👉🏿Pombe
👉🏿Vyakula na vinywaji vilivyopikwa kwenye joto kali sana mfano maziwa yaliyosindikwa
👉🏿Unga uliokobolewa na kusafishwa kupita kiasi
👉🏿Vinjwaji vyenya caffeine kwa wingi k**a kahawa na baadhi ya chai.

✍🏻 Tatizo Hili linatibika kabisa. K**a utalizembea, utakaribisha Ugonjwa wa Bawasiri na utakusumbua. Nipigie / WhatsApp

0684 899 587

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255749800898

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when IJALI AFYA YAKO posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram