20/03/2023
SHINIKIZO LA JUU LA DAMU (HIGH BLOOD PRESSURE)
MAANA:
Shinikizo la juu la damu ni pale msukumo wa Damu unapokuwa juu ya kiwango cha kawaida katika mishipa ya damu mwilini. Kwa kawaida shinikizo la damu linatakiwa kuwa 110/70- 120/80 mmHg
• Viwango vya shinikizo la juu la damu ni:
• JUU KIDOGO (MILD): 135-139/90 mmHg
• JUU KATI (MODERATE) : 140/100 to 159/109
• JUU SANA (SEVERE): mmHg 160/110 mmHg na zaidi
• SHINIKIZO LA CHINI (HYPOTENSION) : < 100/65 mmHg
UGUNDUAJI:
Mara nyingi wagonjwa wa shinikizo la juu la damu hawana dalili zinazoashiria kuwa wana tatizo hili. Na kwa kawaida wengi hugundulika kuwa na tatizo la Shinikizo la juu la damu katika uchunguzi wa kawaida tu wa magonjwa mengine wawapo hospitalini. Mara chache baadhi ya watu huja tayari wakiwa na madhara ya shinikizo la juu la damu.
Pia, Shinikizo la damu laweza kuwa juu katika baadhi ya hali k**a vile fezeha , mazoezi, hofu n.k
Kiulimwengu inakadiriwa kwamba watu billioni 1 sawa na 26% ya watu wazima wana tatizo hili. Kijinsia, Liko zaidi kwa jinsia ya kiume na hutokea zaidi kwa rika la umri wa kati (middle aged) na uzeeni (elderly).
SABABU NA VIHATARISHI:
• Vinasaba (Genetics)
• Uzito uliopitiliza (Overweight)
• Kitambi (Obesity)
• Kutumia kileo (Alcohol intake)
• Jinsia - hasa ya kiume
• Umri (hasa wazee)
• Magonjwa ya figo (RENAL diseases)
• Kisukari (Diabetes mellitus)
• Uvutaji sigara (Smoking )
• Hofu mwendelezo maishani (Stressful life) husababisha kumwagwa kwa wingi vichocheo k**a adrenaline & prostaglandins zinazoongeza mapigo ya moyo)
• Mimba (Pregnancy) - mara chache na husababisha tatizo la kifafa cha mimba - (eclampsia)
• Magonjwa ya mfumo wa vichocheo (Endocrine disorders ) k**a vile pheochromocytoma, cushing disease, thyrotoxicosis n.k
• Magonjwa ya moyo ya kuzaliwa nayo (Congenital heart diseases)
• Baadhi ya Dawa ( k**a dawa zenye kichocheo cha estrogen- za uzazi wa mpango - oral contraceptives, anabolic steroids, corticosteroids, n.k)
Inaendelea ...
Credits: Dr. Taphinez Machibya