21/09/2020
UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME, KUWAHI KUFIKA KILELENI NA KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA
Tunapozungumzia upungufu wa nguvu za kiume tunakuwa katika uwanja mpana zaidi wa tafakari za kibaiolojia na kisaikolojia walizonazo wanaume.
Lakini kwa kufupisha mlolongo wa mambo sehemu kuu tatu zinaweza kabisa kukidhi mchanganuo mzima wa jinsi tatizo hili linavyowasumbua wanaume wengi duniani.
Sehemu kubwa ya malalamiko ya wanaume katika sakata hili yanagusa zaidi maeneo matatu ambayo ni KUKOSA MSISIMKO, KUSHINDWA KURUDIA TENDO NA KUKOSA KABISA NGUVU, huku kufika kileleni mapema kukihusishwa pia k**a pacha wa janga hili ambalo linawasumbua zaidi wanaume, ingawa na wanawake wanakabiliwa na sehemu ndogo ya tatizo hili.
Hata hivyo uchunguzi wa hivi karibuni uliowahusisha wanaume wanaofika kliniki au kupata tiba za tatizo la upungufu wa nguvu za kiume umeonesha kuwa, sio wanaume wengi wenye sababu za kibaiolojia zinazowafanya wakose nguvu za kiume, isipokuwa wengi wao huwa na matatizo ya kisaikolojia zaidi ambayo wahusika wanaweza kujiponya nayo bila hata kutumia vidonge wala dawa za miti shamba.
Ingawa Matabibu wanataja magonjwa ya moyo, kisukari, shinikizo la damu, magonjwa ya zinaa, unene wa kupita kiasi, umri mkubwa kuwa ndiyo chanzo cha wanaume kupungukiwa na nguvu za kiume, lakini imebainika kuwa idadi kubwa ya wanaume wanaofika hospitalini kutafuta nguvu za kiume hawana magonjwa hayo
Huu ni ushahidi kuwa wanaokabiliwa na janga hili wamebeba tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kimawazo zaidi kuliko hali halisi.
Ukweli wa mambo ulioibuliwa na wanasaikolojia umebaini kuwa, wale wote wanaolalamikia/lalamikiwa kuwa hawana nguvu iwe ya kufika kileleni mapema, kutokuwa na msisimko na kushindwa kurudia tendo wamekosa maarifa tu ya kufahamu na hawaijui miili yao na kwamba wanaishi kwa kusikia zaidi ya kujitambua.
Katika hali ya kawaida kila mwanadamu ameumbwa kwa njinsi yake na inapotokea kushabihiana basi ni bahati, lakini mara nyingi usawa hupatikana kwa mmoja kujifunza au kusaidiwa kufikia kiwango cha mtu anayemuhitaji kuwa nae katika maisha hasa ya kimapenzi. Jambo hili wataalamu wanasema kuwa miili iko tayari kutii mafunzo na kubadilisha tabia zake kulingana na utashi wa mhusika.
Tatizo kubwa lililopo kwa wapenzi wengi wanaolalamikia upungufu wa nguvu ni kwamba maisha yao wanayachezea kwenye viwanja vya wenzao wanaokutana nao katika vijiwe na sehemu za kazi.
Usikivu wa mazungumzo toka kwa wanaume wengine wenye uwezo wa kwenda mara nne hadi saba katika tendo au wanatumia dakika arobaini kufika kileleni umewafanya wanaume wengi kujihisi tu kuwa wao wanakasoro eti kwa kuwa huishia mara mbili au moja katika kufanya tendo.
Dhana ya kujiona ni mwenye kasoro inapojengeka akilini mwa mwanaume, huchipua hofu na hatimaye kumfanya ashindwe kabisa kusisimka anapofikiria au kukutana na mwanamke. Matokeo ya hangaiko la akili hushusha uwezo wa mwili na kumuongoza mtu kwenye kuwaza ugonjwa kisha kukimbilia hospitali au kwa waganga kutafuta tiba ya ugongwa ambao kimsingi hanao.
Lakini ukweli uko wazi kwamba kukimbilia kutafuta uwezo wa kufanya mapenzi mara sita au saba hakumfanyi mwanaume awe mlinganifu mwenye kusifiwa na wanawake wengi, kwani si wanawake wote wana uwezo wa kufanya mapezi kwa raundi hizo na si wote wanapenda kutumia takika 30 kucheza mpira wa kikubwa, wengine hukinai mapema na huona kero kuwa na wanaume ving’ang’anizi wenye sifa za kuganda wanapopewa.
Kuna vitu vitatu ambavyo mwanaume unahitaji kuvifahamu ili uweze kuwa imara katika tendo la ndoa kabla ya kuanza kufikiria kutumia dawa za kuongeza nguvu za kiume
1. Fahamu sehemu ambayo inaongeza hisia katika mwili wako
Kila mwanadamu amepewa sehemu moja au mbili au zaidi ambapo sehemu hizo k**a zitatumika vizuri basi zitamfanya mwanadamu apate hisia .
Tambua sehemu hiyo au hizo kasha hakikisha uyo mpenzi wako anazifahamu pia. Ni lazima utapata hamu ya kufanya mapenzi pindi mwanamke wako atakapo chezea sehemu hizo.
Pia k**a unatatizo la kushindwa kurudia tendo basi hakikisha baada ya tendo la kwanza uyo mwanamke wako aendelee kuchezea sehemu ambazo zinaongeza hisia kwako, k**a hazifahamu basi mwambie ili azielewe, usimfiche mwanamke wako juu ya sehemu hizo ambazo zinaongeza hisia kwako.
Hakikisha unazitambua sehemu hizo.
2. Mawazo ni kitu kikubwa sana ambacho kinawafanya wanaume wengi washindwe kurudia tendo au wafike kileleni mapema
Mawazo hayo yapo ya aina mbili
i. Mawazo juu ya mambo ya binafsi ya kimaisha
Mawazo yako juu ya maisha yako ni chanzo kikubwa sana cha wewe kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa au kufika kileleni haraka au kushindwa kurudia tendo.jaribu sana kupunguza mawazo wakati unafanya tendo la ndoa au wakati unataka kwenda kufanya tendo la ndoa
ii. Mawazo juu ya mtu unayekutana naye kimwili
Kuna ile tabia ya kupania tendo, unakuta mtu anawaza siku nzima juu ya tendo ambalo anaenda kulifanya. Kwa ufupi tunasema mtu huyu anafanya tendo la ndoa akiwa peke yake na anapokutana na mwenzake anaenda kumalizia tendo , ndio maana anawahi kufika kileleni mapema na mwisho wa siku anashindwa kurudia tendo.
Hupaswi kumfikiria sana mtu unayekwenda kukutana nae kimwili kwani itakujengea mihemko ya karibu na mikali sana kitu ambacho hakifai, chukulia kawaida na usiwe na papala sana juu ya tendo
3. Kujiona kuwa unamapungufu, ukishajiona kuwa wewe huwezi kurudia tendo au huwezi kufikisha dakika 20 bila kufika kileleni na ukakubaliana na hiyo hali basi jua hutoweza kamwe.
Ondoa hizo fikra za kujiona kuwa unamapungufu, hizo ndizo zinazokumaliza.
Jambo la mwisho ni kuzingatia vyakula na mazoezi, kuna vyakula ambavyo ukitumia kwa wingi vinaongeza hamu na nguvu ya kufanya mapenzi pia kuna vyakula ambavyo ukivitumia kwa wingi vinapunguza hamu na kuondoa nguvu ya kufanya mapenzi.
Kitu kingine ni kupenda kuangalia videos za mambo ya kikubwa pia inasababisha kuleta hilo tatizo kwani linakufanya uwe namawazo ya muda wote juu ya tendo hilo na kukufanya ufike kileleni mapema na kushindwa kurudia tendo.
Naomba niishie hapo lakini kipindi kijacho nitaelezea nijinsi gani video za ngono zinasababisha matatizo ya kushindwa kurudia tendo la ndoa mara ya pili au mara ya tatu na kuendelea.
Asante
0683317836 call/sms for service