21/03/2026
CONFESSION 😔
Nilikuwa na mwanaume mmoja, alinipa wakati mgumu sana mpaka ikafika siku akaniambia anataka “open relationship”… yaani yeye aendelee na mwanamke wake, na mimi nitafute mwanaume wangu halafu bado tuendelee 😳
Siku hiyo ndio niligonga muhuri… nikajua kabisa huyu sio mtu wangu.
Nilimuambia: “Nimevumilia mengi, lakini leo umenithibitishia sina thamani kwako.”
Nikaondoka… na safari hii sikurudi nyuma.
Cha ajabu, baada ya k**a wiki moja tu, mwanaume mwingine akanifuata. Sijawahi hata kuwa naye kwenye mahusiano, lakini akasema ananipenda tangu muda na anataka kunioa.
Leo hii mimi ni mke wa mtu… nashukuru Mungu kwa hilo ❤️
LAKINI… maisha hayako perfect k**a nilivyodhani.
Mume wangu: Ananilipia kodi ✔️
Anatoa pesa ya kula kila siku ✔️
Analipa umeme na maji ✔️
Lakini mimi k**a mke wake… sina matunzo kabisa.
Hajawahi kuninunulia hata mafuta ya kupaka.
Hajawahi kuninunulia hata pedi.
Kila kitu najinunulia mwenyewe.
Nikiuliza thamani yangu iko wapi, anaishia kusema nina gubu 💔
Kuna muda namuuliza kitu anakaa kimya kabisa, mpaka nirudie tena ndipo ajibu kwa hasira.
Anasema hana pesa…
Lakini najiuliza, kweli mwanaume unashindwa hata 5,000 ya kumjali mke wako?
Mpaka nimefikia hatua nimejinyoa nywele zangu nzuri kwa sababu sina hela ya kuzihudumia mara kwa mara… na yeye hajali 😔
Nawaza sana… nachoka.
Je, hii ndio ndoa kweli?
Au nimeolewa ili niwe mfanyakazi wa ndani tu?
Nisaidieni mawazo… 😭