13/11/2025
đź’ Pain Builds Men( MWANAUME USIOGOPE KUPITIA MAUMIVU)
Wanaume hawajengwi na raha.
Wanaume wanajengwa na maumivu, mapambano, na wakati ambao hawakuwa na mtu wa kuwaamini isipokuwa Mungu.
Kuna kipindi mwanaume anatulia kimya, si kwa sababu hana maneno bali kwa sababu ameumizwa sana kiasi kwamba maneno hayawezi kuelezea.
Ni pale anapojifunza kuvumilia, kujibeba, na kutabasamu ndani ya maumivu yake ndipo anaanza kukua kweli.
Maumivu humfunza mwanaume nidhamu.
Humfunza kuvumilia wakati hakuna anayemuelewa.
Humfunza kuthamini amani kuliko maneno matamu.
Na pale anapopona haponi ili arudi k**a zamani,
Anapona akiwa mpya, mwenye hekima, mwenye nguvu ya kimya na moyo wa chuma. đź’Ş
Kwa hiyo ukiona mwanaume yuko kimya, usidhani amejisahau ,
Anaumba toleo jipya la yeye, ndani ya maumivu hayo hayo.
🖋️ Pain doesn’t destroy real men it builds them.