25/07/2024
TEZI DUME NA KANSA YA TEZI DUME INATIBIKA by Dr M***A
( 0756 560 562)
Dalili za kupanuka kwa tezi dume
Dalili huonekana baada ya umri wa miaka ya hamsini . Karibu wanaume wote wenye umri wa sabini na themanini huwa na tatizo hili.Dalili huanza polepole na kuzidi jinsi miaka inavyoongezeka.Dalili hizi ni k**a zifuatazo:
📌Kukojoa mara nyingi hasa nyakati za usiku.Hii ni dalili ya mapema sana.
📌Kulazimisha, mara nyingi hasa nyakati za usiku, kutumia nguvu kuanzisha mkojo kutoka. Hata pale mgonjwa anahisi kibofu kimejaa. Hii ni dalili ya mapema sana.
📌Mkojo kutiririka polepole, hukatikakatika na hutumia nguvu kutoka.
📌Mkojo kushidwa kutoka hata wakati mtu anapohisi kukojoa.
📌Mkojo kuendelea kutoka kidogokidogo baada ya kukojoa, matone ya mkojo huendelea kutoka hata baada ya kukojoa hivyo nguo za ndani hulowa.
📌Kibofu hakiishi mkojo.
📌Matatizo ya tezi dume iliyotanuka
Tezi dume ikitanuka sana huleta matatizo mengi kwa wagonjwa wengine hali hii isipotibiwa. Matatizo hayo ni k**a yafuatayo:
📌Mkojo kukosa kutoka kabisa
Wagonjwa wenye tatizo hili lazima wawekewe katheta ili kumimina mkojo.
📌Madhara kwenye kibofu na figo
Kwa sababu ya kibofu kuwa na mkojo wakati wote, ukuta na misuli yake hupanuka na mwishowe hudhoofika hivi kwamba haiwezi kuzuia mkojo.
Kwa sababu ya kibofu kujaa
📌mkojo hurudi kwenye figo na mwishowe huharibu figo.
📌Ugonjwa wa tezi dume husababisha mkojo kutiririka polepole na mtu kukojoa mara nyingi hasa usiku.
📌Maambukizi na mawe
Kwa sababu kibofu hakimimini mkojo wote kuna hatari kubwa ya maambukizi kwenye njia ya mkojo nakuwa na mawe kwenye kibofu.
✍️Kumbuka
Kutanuka kwa tezi dumehakusababishi ugonjwa wa saratani.
Utambuzi wa kupanuka kwa tezi dume
Historia na dalili zikiashiria uwepo wa hali hii, basi uchunguzi ufuatao hufanywe.
Uchunguzi wa ukubwa wa tezi
Uchunguzi huu hufanywa kwa kuingiza kidole chenye glavu nyuma hadi kwenye tezi dume. Daktari huweza kujua ukubwa na hali yake. Iwapo mtu ana ugonjwa huu tezi dume ni kubwa kuliko kawaida, laini na gumu yote pamoja. Iwapo tezi lina vifundo basi inaweza kuwa na kansa (saratani)au inaweza kuwa na
Dalili za tezi kilichopanuka na saratani hufanana.Lazima uchunguzi wa kina ufanywe ili kujua ni ugonjwa upi.
PIGA (0756 560 562) KWA USHAURI ZAIDI