11/08/2021
JE,WEWE NI MWANAMKE NA UNASUMBULIWA NA MATATIZO YA UZAZI KWA MUDA MREFU SASA?
a. UGUMBA KWA WANAWAKE
Ugumba ni kile kitendo au ni ile hali ya mwanamme na mwanamke kujamiiana kwa kipindi cha mwaka mmoja pasipo njia yoyote ya uzazi wa mpango, yoyote na bado mwanamke hakuweza kupata ujauzito.
Ili mwanamke apate mimba, sehemu zote za mwili wake zinazohusika na uzazi zinatakiwa zifanye kazi inavyotakiwa; Moja kati ya ovari mbili za mwanamke lazima iyachie yai “lililokomaa”, Yai hili lazima lisafirishwe na mrija wa uzazi (fallopian tube), Mbegu za mwanamme lazima zisafiri kupitia Cervix, tumbo la uzazi (uterus) hadi kwenye mrija wa uzazi, kulifikia yai na kulipevusha.
Yai lililopevushwa lazima lisafiri kupitia mrija wa uzazi hadi kwenye tumbo la uzazi (uterus), Yai hilo lazima linate kwenye ukuta wa uterus na kuanza kukua
Ugumba kwa mwanamke unaweza kutokana na dosari katika hatua yoyote katika hizo tulizozitaja na mara nyingine kutokana na dosari katika hatua zaidi ya moja.
i. Kushindwa Kuzalisha Mayai (Anovulation):
Hili ndilo tatizo ambalo linachangia ugumba kwa wanawake kwa 30% lakini kwa bahati nzuri 70% ya wanawake wenye tatizo hili hupata tiba na kufanikiwa kupata watoto. Mwanamke mwenye tatizo hili hutoa mayai mara chache au hatoi mayai kabisa.
b. UVIMBE KWENYE KIZAZI (FIBROIDS)
Fibroid ni uvimbe ambao hutokea kwenye tumbo la kizazi ambao si kansa, ni uvimbe wa kawaida tu ambao unakua kwa kutegemea kichocheo cha estrogen hormone. Huwapata Zaidi wanawake waliopo kwenye umri wa kuzaa, kuanzia kubalehe mpaka kukoma kwa hedhi. Na mara nyingi huongezeka na kukua sana hasa wakati wa ujauzito kwani vichocheo hivi huongezeka wakati huu kulinda makazi ya mtoto. Watu waliofikia kikomo cha hedhi hawapati fibroids
c. MATATIZO YA HEDHI
Kibaiolojia hedhi ya kila mwezi, ni mchakato unaojiendesha wenyewe ndani ya mwili kwa ushirikiano wa mfumo wa homoni na mfumo wa uzazi, hivyo endapo mwanamke atashindwa kupata hedhi kikamilifu, ni ishara ya kuwa na tatizo aidha kwenye mfumo wa homoni au mfumo wa uzazi kwa ujumla wake.
Ili mwanamke aweze kuwa na mzunguko ulio sahihi wa hedhi, ni lazima matezi yake ya hypothalamus na pituitary pamoja na kiwanda cha kutengeneza mayai ya k**e (ovaries) na mji wa mimba (uterus) vifanye kazi zake sawasawa.
Hypothalamus huchochea tezi la pituitary kuzalisha hormone chochezi ya follicle au follicle-stimulating hormone (FSH) pamoja na homoni ya luteinizing (LH). Hizi FSH na LH kwa pamoja huchochea ovaries kuzalisha homoni za estrogen pamoja na progesterone.
Kazi za estrogen na progesterone ni kusababisha mabadiliko katika ukuta wa uterus yaani endometrium ikiwepo kupata hedhi. Ili damu ya hedhi iweze kutoka nje, njia ya uzazi ya mwanamke haina budi kuwa huru yaani isiyo na matatizo yeyote yale.
KUKOSA HEDHI:
Tatizo la kukosa hedhi ni jambo ambalo linawakumba wanawake wengi waliovunja ungo.Aidha suala hili limekuwa likiwaletea usumbufu mwingi wa kisaikolojia wanawake wengi waliowahi kukumbana nalo.Tatizo la kukosa hedhi au amenorrhea linaweza kutokea awali kabisa (primary) au baadaye kabisa maishani (secondary).
PRIMARY AMENORRHEA:
Hiii hali ya kukosa hedhi inayoweza kumtokea msichana aliye katika umri wa kuvunja ungo na ambayo huweza kuendana na hali ya kukosa mabadiliko ya kubalehe k**a vile kuota mat**i au nywele za kinena, au msichana anaweza kuwa na mabadiliko ya kubalehe lakini asipate hedhi.
SECONDARY AMENORRHEA:
Hii hali ya kukosa hedhi inayomtokea mwanamke ambaye si mjamzito, hanyonyeshi, na ambaye hajavuka umri wa kukosa hedhi (menopause) na wala hatumii njia za uzazi wa mpango k**a vile sindano au vidonge, na ambaye hapo awali alikuwa akipata hedhi k**a kawaida lakini akasimama kwa miezi mitatu au Zaidi.
TIBA
Ewe mwanamke tumia dawa za virutubisho ili kuepukana na changamoto hizo hizi apa..
Soybean
Soya isoflavones
Vitamin E
Gyrophola
Gynko tea
MVURUGIKO WA HEDHI:
Kuvurugika kwa hedhi ni kitendo cha mwanamke kuanza kuona siku zake bila tarehe au mzunguko maalumu na matokeo yake ni kuwa mwanamke atashindwa kutimiza malengo yake kwa kutumia mzunguko huo sababu ni haueleweki.
wakati mwingine unaweza kupitiliza mwezi hata miezi kadhaa bila kuona kabisa siku zako na hata ukipima ujauzito unakutwa huna ujauzito wala dalili huna. Utakusaidia kupata ujaouzito ulioupangilia na Utakuepusha kupata ujauzito ambao hukuupangilia Utaweza kuamua jinsia ya mtoto unayemtaka
MAUMIVU MAKALI YA HEDHI (dysmenorrhea)
Ni kawaida kwa wanawake kujisikia Maumivu pale wapatapo hedhi zao, lakini Maumivu hayo hugueka na kuitwa tatizo pale ambapo mwanamke huyu inambidi atumie njia mbadala za kupunguza Maumivu ka madawa na endapo k**a atashindwa kufanya shughuli zake za kawaida kwasababu ya Maumivu hayo.
Magonjwa yanayoweza kusababisha maumivu ya hedhi ni fibroids, infection, uvimbe ndani ya kifuko cha uzazi (polyp) na ugonjwa unaoitwa endometriosis na adenomyosis. Ugonjwa wa endometriosis na adenomyosis upo Tanzania lakini hausikiki kwa sababu vituo vingi vya huduma havina vifaa vya kugundua uwepo wake.
WASILIANA NASI KWA MATIBABU ZAIDI PIGA SIMU
WHATSAPP wa.me/+255688992401
0713688688
Jiunge na group la Afya kwa elimu zaidi gusa link👇👇
https://chat.whatsapp.com/GiCpvyeHAtb5msvZcvCO2w