Afya ya Mama

Afya ya Mama MTAALAMU NA MSHAURI WA MATATIZO SUGU YA KIAFYA KWA WANAWAKE KARIBU NIKUSAIDIE

22/05/2023

SIKU YA KUSHIKA MIMBA MZUNGUKO MFUPI
Mungu ndiye muumba watu wote na viumbe vyote juu na chini ya jua, hilo halina pingamizi wala ubishi na lazima tumshukuru Mungu kwa hilo, ila alitoa amri ya ndoa kwamba ZAENI MKAONGEZEKE kwa hiyo kila mtu anayependa kutimiza amri hii yafaa awe na maarifa.kuendana na maswali mengi ya mzunguko mfupi na kushika mimba nimeona nikuletee somo hili hapa chini.

Kwa wale wasiojua namna ya kuhesabu mizunguko yao basi ni muhimu kurudi katika maada zilizopita na kisha kujifunza namna ya kuhesabu mzunguko wako. Tambua ya kwamba mzunguko wa bleed (hedhi) ni tofauti sana na siku za bleed (hedhi).

JIFUNZE ZAIDI VITU VYA KUJUA
1. Siku za bleed (hedhi) ni kuanzia na siku ya kwanza unapopata bleed hadi siku ile unamaliza bleed.
2. Wakati mzunguko wa bleed huanza siku umepata bleed mpaka siku moja kabla hujapata bleed nyingine.
Mfano umepata bleed tarehe 1 mwezi wa saba na bleed hiyo ikaisha tarehe 05 basi siku za bleed ni 5 na zimeanza tarehe moja na zikaisha tarehe 5.
K**a bleed nyingine umeipata tarehe 29 mwezi wa 7, basi mzunguko wako wa bleed ya mwezi wa saba umeanza tarehe 01 mwezi wa saba na ukaisha tarehe 28 mwezi wa saba. Mzunguko huo ni wa siku 28. Mzunguko wa mwezi wa 8 Umeanza tarehe 29 mwezi wa 7.
Ukiwa na mzunguko mfupi usiogope kwa kuwa bado unayo nafasi kubwa ya kupata mtoto na watu wengi tu wapo wana watoto.

Lazima ujue mzunguko wako kwanza ni wa siku ngapi.
Mfano k**a umekuwa na mzunguko wa siku 21 kwa muda wa miezi mitatu mfululizo na mfano umepata bleed tarehe 10 mwezi wa saba basi siku yako ya uzazi haiwezi kuwa siku ya 14 tangu kupata bleed. Bali ni siku ya 7 tangu umepata bleed.

HEBU ZAMA NDANI HAPA UJIFUNZE
Mzunguko wa siku 21 siku ya uzazi ni siku ya (7) tangu upate bleed. Kwa hiyo k**a utapata bleed siku 3 basi siku ya tano unatakiwa uanze tendo la ndoa.
Mfano mzuri ni k**a ufuatao. ANNA ameingia bleed leo tarehe 16 mwezi wa 7 na mzunguko wake kila mwezi unamchukua siku 21.
Huyu ANNA anachukua siku 3 za bleed.
Basi siku zake atahesabu hivi tarehe 16 ni siku ya kwanza yaani leo tarehe16 ni siku ya kwanza ya bleed, kesho tarehe 17 ni siku ya pili ya bleed, kesho kutwa tarehe 18 ni siku ya tatu ya bleed, tarehe 19 ni siku ya nne bleed imeisha, tarehe 20 siku ya tano bleed imeisha - anza hapa kukutana na mwenzako, tarehe 21 ni siku ya sita endelea na tendo na tarehe 22 siku ya saba endelea na tendo yai linatoka. Unashauriwa kuanza mapema ili kuongeza nafasi ya mbegu kulikuta yai.

MZUNGUKO WA SIKU 22,23,24,25 na 26
Mzunguko wa siku 22 yai linatoka siku ya 8 wewe anza tendo siku ya 6, 7 na 8
Mzunguko wa siku 23 yai linatoka siku ya 9 wewe anza tendo siku ya 7
Mzunguko wa siku 24 yai linatoka siku ya 10 wewe anza tendo siku ya 8
Mzunguko wa siku 25 yai linatoka siku ya 11 wewe anza tendo siku ya 9
Mzunguko wa siku 26 yai linatoka siku ya 12 wewe anza tendo siku ya 10

Kumbuka kuanza siku moja au mbili kabla ya siku ya yai kutoka pia unaweza ongeza siku 1 au mbili baada ya siku yenyewe hii ni kwa sababu mizunguko huwa inabadilika badilika kutokana na sababu mbalimbali k**a ugonjwa na dawa nzitonzito msh*tuko k**a wa kufiwa, kubadilika kwa hali ya hewa na pia mabadiliko ya mwili k**a kunenepa.

Kumbuka k**a umekaa muda mrefu hujapata mtoto ni lazima ufike hospitalini na kupima na kupata majibu sahihi. Ni muhimu pia ukawa uko karibu na mwenzako, una afya nzuri na mko vizuri kiuhusiano.

UJUE UMUHIMU WA CHAKULA BORA
Ni muhimu ule chakula bora na sio bora chakula. Imethibitika ya kwamba asilimia zaidi ya 50 ya matatizo ya hedhi hutokana na kutokula vizuri. Ulaji wa chips, soda, pombe kupindukia, kula wanga mwingi na sukari ni hatari kwa maisha ya ndoa.
Unatakiwa kula chakula halisi (Real Food) chakula fresh na chakula cha asili. Vyakula hatari ni pamoja na vyakula vya paketi na makopo na kuku wa kisasa (chicken)

TUNAKUSAIDIAJE?
1.TUNATOA USHAURI JUU YA AFYA YAKO.
Endelea kufuatilia mada zetu hapa hapa kwenyepage yetu ukipenda kuwekwa kwenye group ili kujifunza mengi zaidi whatsapp 0713051747

22/05/2023

UJUE MZUNGUKO WAKO WA HEDHI NA UFAHAMU SIKU ZA KUSHIKA MIMBA
Habari za leo rafiki yangu, ni matumaini yangu unaendelea vizuri na kufurahia elimu uipatayo hapa pia napenda kuwapongeza wote wachukuayo hatua kwa kutumia virutubisho na pads zetu za neplily sanitary pads, kutokana na maoni yenu juu ya kufunzwa jinsi ya kuweza kuhesabu mzunguko wa wenu wa hedhi kupanga na kuepuka mimba leo nipo hapa kuwajuza haya
Kutokana na wanawake wengi kutokujua mizunguko yao ya hedhi hivyo huwawia vigumu kujua ni siku gani akutane na mumewe au aepuke ili kubeba mimba au kutoshika mimba
Ni muhimu sana mwanamke kujua mzunguko wake wa hedhi, hii pia itakusaidia kujua siku hatari za kushika mimba na vile vile kukusaidia kuepuka mimba usiyoitarajia kwa kutumia kalenda yako kupanga tarehe yako.
NAMNA YA KUHESABU MZUNGUKO WAKO WA HEDHI
ili kujua siku nzuri ya kupata mimba au kuepuka ni lazima kwanza ujue siku ya KILELE (productive/fetal day) kwa maana kwamba ujue siku ambayo huitwa SIKU YA KUMI NA NNE
 Rafiki napenda mtambue kuwa wanawake mnatofautiana katika swala la urefu wa mzunguko wa hedhi (menstrual periods) yani idadi ya siku ya kwanza ya period mpaka hedhi ya pili
 wanawake wengi huwa mnafall Kwenye tarehe 22-35 ingawa wapo walio kawaida wanachukua siku 28 vilevile wengine Wana mizunguko miwili yani mfupi na mrefu hivyo walio na mzunguko mfupi mathalani wale wenye siku 22 huwa Wana kipindi kifupi cha utokaji damu yan damu inaweza kukatika ndani ya siku mbili huwa ni tofaut na mtu mwenye mzunguko wa siku 31_35 kwani wao huwa na kipindi kirefu cha utokaji damu
JE, UNAIJUA SIKU YA MIMBA???
watu wengi huwa hatujui na kuishia kuchemka katika swala hili la mzunguko wa hedhi na kutambua siku ya mimba ni ipi wao hufikiri siku ya mimba ni Ile siku ya kumi na nne baada ya Dalili za kwanza za damu, wao huhesabu kuanzia Ile siku damu ilipoanza kutoka hadi siku ya kumi na nne, kwa utaratbu huu wengi wanafall hii ni kwasababu wanawake Wana mizunguko tofauti kwa urefu hivyo basi nakuelekeza ili ujue siku ya mimba ni ipi
 Kwanza inabid ujue mzunguko wako ni upi??? Yan mfupi /mrefu /wa kawaida
 Baada ya kujua urefu wa mzunguko wako chagua (pin_ point) yani siku Ile ya mwisho halafu uhesabu kurudi nyuma (backwards) siku kumi na tano kuanzia siku Ile ya mwisho yani siku kumi na tano kuanzia mwisho ndio siku ya mimba, hapa namaansha ukishafahamu siku ya kumi na tano kutoka mwisho hukuwezesha kufaham siku ya kupata ujauzito
 kwa utaraitbu huu mdogo msomaji utagundua karibia wanawake wote au wew mwenyew unatumia njia za Zaman ambazo huwafaa watu wenye mzunguko wa siku 28 tu hivyo nakupa mifano Hai jinsi ya kutumia kalenda kwa mizunguko yote
MZUNGUKO WA SIKU 28
tengeneneza kalenda yako ya siku 28 yani hivi 1,2,3,4,5,6,7,8,9,10,11,12,13,14,15,16,17,18,19,20,21,22,23,24,25,26,27,28
Baada ya kuandaa hesabu kuanzia 28 mpaka siku ya kumi na tano ambayo itaangukia Kwenye (14th) day sasa hiyo ndio siku ya kubeba mimba kwa mwanamke yoyote mwenye mzunguko wa siku 28 Lakin kwakua kipindi cha ovulation kinaanza siku ya 4_5 kabla ya ovulation na humalizika masaa 24_48 hivyo unapaswa kujikinga kuanzia tareh 12_16 kuepuka mimba hii ni kwasababu mbegu za mwanaume Zina uwezo wa kudumu kwa masaa 24_48 baada ya kujamiiana,
kumbuka :siku ya kwanza ndio siku unayoanza kubreed
MZUNGUKO WA SIKU 22
tengeneneza kalenda yako ya siku 22 yani hivi
1,2,3,4,5,6,7,8,9,10,11,12,13,14,15,16,17,18,19,20,21,22,Baada ya kuandaa hesabu kuanzia 22 kurudi nyuma mpaka siku ya kumi na tano ambayo itaangukia Kwenye (8th)hivyo siku hiyo ni siku ya hatar kubeba mimba ila kwa kuangalia ovulation inabid ujikinge kuanzia tarehe 6_10 kuepuka mimba hii ni kwasababu mbegu za mwanaume Zina uwezo wa kudumu kwa muda wa masaa 24_48 kumbuka tareh moja ndio siku unayoanza kubreed
MZUNGUKO WA SIKU 35
Tengeneneza kalenda yako ya siku 35 yani k**a hivi
1,2,3,4,5,6,7,8,9,10,11,12,13,14,15,16,17,18,19,20,21,22,23,24,25,26,27,28,29,30,31,32,33,34,35.Baada ya kuandaa hesabu kuanzia 35 kurudi nyuma mpaka sku ya kumi na tano ambayo itaangukia Kwenye (21th)hivyo hiyo siku ni ya hatar kubeba mimba ila kutokana na ovulation inabid uanze kujizuia kuanzia tareh,19_23 kuepuka mimba hii ni kwasababu mbegu za mwanaume Zina uwezo wa kudumu kwa masaa 24_48 baada ya kujamiiana
MZUNGUKO USIO WA KAWAIDA WA SIKU KUMI NA TANO
Mara nyingi Watu Hawa huwa na mzunguko wa siku 15-18 Hawa huwa na wa kutokushika mimba hivyo kwanza tengeneneza mzunguko wa siku zako
1,2,3,4,5,6,7,8,9,10,11,12,13,14,15 Kisha Anza kuhesabu kuanzia 15 kurud nyuma mpaka ufike siku kumi na tano Bila Shaka itaangukia Kwenye (1st) hivyo siku ya kwanza ya mzunguko wa mwanamke yoyote mwenye mzunguko wa siku 15 ndio siku hyo mimba inaingia (hata wa siku kumi na nane follow above) kumbuka siku ya kwanza ndio siku unayoanza kubreed pia ndio siku hyo unaweza kupata mimba hii inamaanisha kwamba siku ambayo linaharibika lile yai la kwanza ndio siku hyo hiyo yai la upande wa pili linapevuka n kuwa tayar kurutubishwa, Mara nyingi mwanamke wa kundi hili anaweza kupata mimba k**a atakutana na mwanaume wake siku Ile anayoanza hedhi kwani n siku ambayo yai linaharibika na ndio siku hyo yai moja linapevuka na kuwa tayar kurutubishwa
 Mara nyingi wanawake wa kundi hili huwa hawapati ute wa Uzazi ambao wenzao huwa wanapata siku Ile yai linapevuka wao hupata ute uliochanganyikana na damu kwakua ndio siku hyo ya kuanza breed
 Rafiki yangu ni matumaini yangu umejifunza na kuelewa jinsi ya kupanga kupata mimba au kuepuka nimeamua kuandaa somo hili ili kupunguza utoaji wa mimba na madhara wanayoyapata wanawake wanaotumia vidonge vya Uzazi wa mpango hivyo ni vizuri KUTUMIA KALENDA ILI KUEPUKANA NA MADHARA YA SINDANO NA VIDONGE VYA UZAZ WA MPANGO AMBAYO NI MAKUBWA K**A VILE KUPATA SARATAN YA MATITI, KUWA MGUMBA, KUPATA UVIMBE KATIKA KIZAZI, HUSABABISHA KUBLEED SANA NK,
Asante kwa kusoma kupata elimu hii na wewe unaweza kuwafundisha wenzako kwa kushare hii post na kuwatag marafiki zako
Jipatie neplily sanitary pads ,pads salama kwa hedhi yako, na virutubisho vya kutibu magonjwa tabia na sugu k**a presha,asthma,joint maumivu ya viungo,kuongeza kinga yako,vidonda vya tumbo ,alleji na kadhalika usisite kunitafuta .
NOTED :NDUGU MSOMAJI K**A UNA MAONI USHAUR NIANDIKIE UJUMBE KUPITIA NAMBA YANGU HAPO CHINI 0713051747/ 0783148453
PLEASE USISAHAU KUSHARE /KULIKE NA KUWAALIKA WENZAKO KATIKA PAGE HII

IFAHAMU HALI YA UTE WA MLANGO WA UZAZI KWA AKINAMAMA(VAGINAL MUCUS)KABLA NA WAKATI WA HEDHI NA NAMNA UTE HUO UNAVYOCHANG...
12/04/2023

IFAHAMU HALI YA UTE WA MLANGO WA UZAZI KWA AKINAMAMA(VAGINAL MUCUS)KABLA NA WAKATI WA HEDHI NA NAMNA UTE HUO UNAVYOCHANGIA KUPATIKANA KWA MIMBA

katika mlango wa uzazi hubadilika kulingana na siku mwanamke yupo katika mfumo wake wa uzazi (reproductive system circle),
Hii hufanyika ili kuweza kuruhusu mbegu za mwanaume ziweze kwenda kwa kasi na kulifikia yai la mwanamke hivyo kurahisisha mwanamke kupata mimba.
Hivyo basi ni muhimu kujua hili k**a mwanamke kwa ajili ya kujilinda dhidi ya mimba usiyoitarajia au siku maalum za kulenga ili upate mimba k**a unatafuta mtoto

HALI YA UTE.
UTE UKIWA MKAVU AU UNANATA;
aina ya ute k**a huu hauruhusu mbegu za kiume kusafiri na kuingia katika kizazi cha mwanamke hivyo mimba haiwezi kutungwa hapa, Huu ute huwepo mwanamke akiwa hayupo katika kipindi cha joto au kipindi ambacho yai yake bado halijapevuka.

UTE UKIWA NA RANGI YA KRIMU (Cream)
hapo mwanamke anakaribia kuingia katika kipindi cha joto pia yai linakaribia kupevuka bado hawezi kupata mimba.

UTE UKIWA MAJIMAJI AU YENYE UNYEVU UNYEVU;
huu unaweza kusafirisha mbegu ya mwanaume hadi kizazi cha mwanamke na k**a imebaki siku mbili au tatu yai kupevuka ukifanya tendo la ndoa hapa kuna uwezo utashika mimba kwa sababu yai likipevuka litakutana na mbegu ya mwanaume ndani ya kizazi kuna uwezo mimba itatungwa.
Mwanamke hupata hisia za kufanya mapenzi lakini siyo sana

UTE UKIWA NA RANGI NYEUPE K**A YAI BICHI;
ute ukiwa katika hali hii ndiyo mzuri kabisaa kwa kusafirisha mbegu za kiume, pia hapa mwanamke ameshafika katika kipindi cha joto hapa tendo la ndoa likifanyika mimba inapatikana kwa asilimia zote k**a hakuna vizuizi kutoka Mungu muumba na vizuizi vingine vya afya vinavyozuia mimba kutunga.
Hapa hisia za mwanamke za kufanya tendo la ndoa huwa juu sana na hutamani kufanya mapenzi kila mara especially yai likikaribia kushuka na likishuka.
Ni muhimu sana mwanamke aangalie ute (va**nal mucus) katika kuzifahamu siku zake za kuweza kushika mimba na kutoshika mimba kuliko kutumia calendar ya damu ya mwezi.
Siku za ute ni siku 30 kinyume na siku za damu ya mwezi na pia ni muhimu sana mwanamke kushika ule ute kila siku kwa mkono wake kuangalia rangi na utelezi na harufu.

Ongeza uwezekano wa kupata mimba kwa kutumia virutubisho vya tiba mbadala

Mwanamke Jithaminishe maana wewe ni wa thamani sana

Nitafute 0713051747 kwa ushauri zaidi nakujipatia virutubisho asilia.

Ndugu wasomaji wa page yangu Leo nimewaletea bidhaa mpya kwa wale wote wanaopitia changamoto ya kukosa hamu ya kula kwa ...
12/04/2023

Ndugu wasomaji wa page yangu Leo nimewaletea bidhaa mpya kwa wale wote wanaopitia changamoto ya kukosa hamu ya kula kwa watu wazima adi watoto wanaweza kutumia bidhaa hii bila madhara yoyote, Na wew K**a umehangaika Sana na ushatumia kila dawa kurudisha hamu ya kula lakini bado haujafanikiwa njoo utumie STENAPO hutojutia hata kidogo hurudisha hamu ya kula kuanzia siku kadhaa unapoanza kutumia dawa Ila mabadiliko ya mwili kuanzia week ya pili..karbu tukuhudumie 0713051747

K**a unasumbuliwa na changamoto mojawapo Kati ya hizo usisite kuwasiliana nasi karibu tukusaidie kutatua tatizo lako 071...
12/04/2023

K**a unasumbuliwa na changamoto mojawapo Kati ya hizo usisite kuwasiliana nasi karibu tukusaidie kutatua tatizo lako 0713051747

INAKUHUSU HII MTOTO WA K**E AU KIUME ANATOKEAJEHabari rafiki yangu kuendana na maswali mengi ya jinsi gani mtoto wa k**e...
01/03/2023

INAKUHUSU HII MTOTO WA K**E AU KIUME ANATOKEAJE

Habari rafiki yangu kuendana na maswali mengi ya jinsi gani mtoto wa k**e au kiume hutokea. Inakuwa hivi nifatilie.

Katika urutubishaji yai la mwanamke linabeba chromosome X yaani XX

Na mbegu ya mwanaume inabeba chromosome XY

Chromosome X kutoka kwa mwanamke ikikutana na Y kutoka kwa mwanaume mtoto wa kiume hupatikana.
Chromosome X kutoka kwa mwanamke ikikutana na X kutoka kwa mwanaume mtoto wa k**e hupatikana

*FAHAMU SIFA ZA CHROMOSOMES X na Y za mwanaume*

Ili uweze kufanikiwa kuchagua mtoto wa kiume au wa k**e lazima ujue sifa za chromosomes hizi zinazoamua jinsia ya mtoto.

*SIFA ZA CHROMOSOMES Y*

Zina spidi kubwa sana kwa hiyo k**a yai lipo tayari zenyewe zitawahi kwenda kurutubisha

Zina maisha mafupi sana kulinganisha na X

*SIFA ZA CHROMOSOMES X*

Zina spidi ndogo sana

Zina maisha marefu kulinganisha na Y
Baada ya kujua sifa za chromosome ambazo ndo zinatusaidia kuamua jinsia twende moja kwa moja kwenye jinsi ya kupata mtoto wa jinsia unayotaka

*MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA KUAMUA JINSIA*

Lazima mwanamke ajue mzunguko wake (menstrual cycle)siku ya 1-28

Lazima mzunguko wako uwe na mpangilio sahihi(unaweza ukachunguza mzunguko wako kwa miezi minne mfululizo)

PH ya uke lazima iwe kiwango sahihi 4-5.5(Tumia neplily pads kwa kuwa na PH sahihi

Ushirikiano kati ya mwanamke na mwanaume

*JINSI YA KUPATA MTOTO WA KIUME*
Ili uweze kupata mtoto wa kiume kisayansi unashauriwa kushiriki tendo la ndoa siku ambayo yai litakuwa limetoka k**a mzunguko wako uko sahihi ni siku ya 14.

Njia nyingine ya kujua yai limetoka baba anaingiza vidole viwili ukeni wakati wa asubuhi na ukikuta uteute ujue yai limetoka kwa hiyo jioni mnashiriki tendo la ndoa kwa ajili ya kupata mtoto wa kiume

*KWANINI USHIRIKI TENDO LA NDOA WAKATI YAI LIMETOKA ILI KUPATA MTOTO WA KIUME?*
Kisayansi chromosome Y ambayo inahusika katika kutunga mimba ya mtoto wa kiume ina spidi kubwa sana ni nyepesi na haiwezi kuishi muda mrefu kwa hiyo ukishiriki tendo la ndoa wakati yai limetoka maana yake unaongeza nafasi ya kupata mtoto wa kiume.

*JINSI YA KUPATA MTOTO WA K**E*
Ili ufanikiwe kupata mtoto wa k**e utatakiwa ushiriki tendo la ndoa siku tatu kabla ya yai kupevuka yaani hapa ni baada ya kujua mzunguko

*KWANINI USHIRIKI TENDO LA NDOA SIKU TATU Kabla. ?*

Hii ni kwasababu chromosome X ambazo ndo zinaunda mtoto wa k**e huwa zina sifa ya kuwa na maisha marefu na kutembea taratibu hivyo yai likitolewa litakuta chromosome X ziko hai

KUNA BAADHI YA WAZEE WA ZAMANI WANAAMINI HAYA KATIKA KUPATA MTOTO WA JINSIA UNAYOTAKA

KUPATA WA K**E
Kula samaki, mboga za majani, matunda, bidhaa za maziwa, mbegu za matikiti maji, alzeti n.k

-Wakati wa kufanya tendo la ndoa mwanamke akae juu n.k

KUPATA WA KIUME
Kula nyama, ndizi, Vyakula vya chumvi k**a chips ila usizidishe chumvi, karanga na vyakula vingine vya potassium na sodium.
Chromosomes Y zinahitaji pH ya alkane kuliko asidi ndio maana wazee waliona hili.

Kuna mengi kuhusu wazee wa zamani ila tumeongelea haya ya mlo kwa maana yana mantiki kibaiolojia

MAMBO YANAYOWEZA ATHIRI KUPATA MTOTO UNAYEMTAKA

Kushindwa kuhesabu siku

Mzunguko mbovu wa hedhi(Tumia neplily pad)

Kutokuwa na PH sahihi ukeni tumia Neplily

WANAUME:
Kumekuwa na ongezeko kubwa la wanaume kutoweza kubebesha mimba au kuishiwa nguvu za kiume. Sababu ni nyingi tumekuwa tukizitaja katika makala zetu zilizopita ikiwemo upigaji holela wa punyeto

Baada ya mambo mengi kupita nimeanza kutoa mwongozo ambao mtu akiufuata atarudisha kabisa uwezo wake katika tendo la ndoa. Huu ni mwongozo salama kiafya kwani utatumia vitu salama na vyenye faida katika mwili wako.

Ambavyo ni virutubisho vya tiba mbadala sahihi kabisa bila Kemikali.

ZIFAHAMU DALILI ZA SARATANI YA UZAZISaratani ya kizazi huwa na dalili zake za awali ambazo tutakuja kuziona. Tunapozungu...
26/02/2023

ZIFAHAMU DALILI ZA SARATANI YA UZAZI
Saratani ya kizazi huwa na dalili zake za awali ambazo tutakuja kuziona. Tunapozungumzia saratani ya kizazi tunalenga zaidi saratani ya shingo ya uzazi ‘Carcionoma of Cerix’ na saratani ya mfumo wa uzazi au ‘Endometrial Carcinoma.

Saratani ya mfuko wa kizazi hushambulia zaidi tabaka la ndani la kizazi ‘Endometrium’ na kusababisha maumivu ya tumbo kwa muda mrefu na hata tumbo kuvimba.

Saratani hii siyo kubwa sana hivyo hatutaelezea kwa undani ila endapo utakuwa na maumivu chini ya tumbo na yanasambaa kulia na kushoto na upande wa juu, tumbo likiwa linaongezeka ukubwa na siku za hedhi zinavurugika, basi muone daktari wa kinamama kwa uchunguzi wa kina.

Saratani ya shingo ya uzazi huwapata wanawake walio katika umri wa kuzaa wenye wapenzi zaidi ya mmoja au ambao mara leo kaolewa na huyu, anaachana naye anaishi na mwingine, yaani mara kwa mara hana msimamo, anabadilibadili wanaume, wanawake wanaofanya ngono na wanaume wasiofanyiwa tohara pia hupatwa na tatizo hili la saratani ya shingo ya uzazi.

Saratani ya shingo ya uzazi pamoja na kuchangiwa na mambo yote hayo hapo juu, husababishwa hasa na kirusi kiitwacho ‘Human Papilloma virus’ au kwa kifupi ‘HPV’. Kirusi hiki huenezwa kwa njia ya ngono, mwanaume huwa hakimuathiri bali yeye hukibeba na kukisambaza kwa wanawake kwa hiyo mwanamke anayechanganya wanaume hajui wapi atakipata.

*Ukubwa wa tatizo*
Saratani ya shingo ya kizazi ina tabia ya kusambaa endapo haitagundulika na tiba haitafanyika mapema. Saratani husambaa katika kizazi, nyonga hadi katika mapafu. Ikishambulia nyonga, mwanamke hulalamika maumivu chini ya tumbo.

Saratani hii ina tabia ya kusambaa kwa kasi na endapo hatua za haraka hazitachukuliwa husababisha kifo kwa mwanamke. Saratani huwa haiambukizi.

*Dalili za awali za saratani ya shingo ya uzazi*
Mwanamke mwenye tatizo hili hulalamika maumivu ya tumbo chini ya kitovu, kutokwa na majimaji yenye harufu ukeni na muwasho mara kwa mara. Tatizo hili hutibiwa na kujirudia
Kwa ushauri zaidi wasiliana nasi 0713051747

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease).Pelvic Infalammatory Disease (PID) ni maambukizi kwenye viungo vya uza...
26/02/2023

Ujue Ugonjwa Wa PID (Pelvic Inflammatory Disease).

Pelvic Infalammatory Disease (PID) ni maambukizi kwenye viungo vya uzazi vya mwanamke. PID hutokea pale bakteria waenezwao kwa ngono wanaposambaa kutoka kwenye uke (va**na) hadi kwenye nyumba ya uzazi (uterus), mirija ya uzazi (fallopian tubes) na ovari.

Dalili Za PID
Maumivu – yanayoweza kuwa madogo au makali – maeneo ya chini ya tumbo au nyonga Uchafu usio wa kawaida au mzito ambao unaweza kuwa na harufu mbaya Kutokwa damu kusiko kwa kawaida, hasa wakati wa tendo la ndoa, au katikati ya siku za hedhi Maumivu wakati wa kujamiiana Homa, wakati mwingine kusikia baridi Maumivu wakati wa haja ndogo, haja ndogo ya mara kwa mara au haja ndogo kutoka kwa shida.

Chanzo Cha PID

Kuna bakteria wa aina nyingi wanaoweza kusababisha PID, lakini maambukizi ya gonorrhea na chlamydia ndiyo yanayoonekana zaidi.

Aghalabu, bakteria hawa huingia kwenye viungo ya uzazi vya mwanamke pale ulinzi wa kwenye shingo ya kizazi (cervix) unapovurugwa. Hii inaweza kutokea mathalani, wakati wa hedhi na baada ya kuzaa, mimba kuharibika au kutoa mimba. Mara chache bakteria huweza kujipenyeza wakati kifaa cho chote cha tiba kinapoingizwa kwenye nyumba ya uzazi.

Mazingira Hatarishi

Kuna vipengele ambavyo huweza kukuweka kwenye hatari kubwa zaidi ya kupata PID, navyo ni:
Kuwa mwanamke uliye chini ya miaka 25 unayeshiriki ngono Kuwa na wapenzi zaidi ya mmoja Kuwa na mahusiano na mpenzi mwenye wapenzi zaidi ya mmoja Kufanya mapenzi bila kinga Kujisafisha na maji mara kwa mara Kuwa uliwahi kupata PID kabla au magonjwa mengine ya ngono



Madhara Yatokanayo Na PID
Madhara yanayoweza kutokea ni pamoja na:
Mimba nje ya mirija (ectopic pregnancy). PID ndiyo sababu kubwa ya mimba kutunga nje ya kizazi.
Ugumba. Uharibifu wa viungo vya uzazi huweza kusababisha ugumba – kushindwa kupata ujauzito. Kadiri unavyozidi kupata PID mara nyingi zaidi, ndivyo hatari ya ugumba inavyozidi. Kuchelewa kupata tiba ya PID kunaongeza ha

ZIJUE FAIDA ZA TUNDA LA PERA PAMOJA NA MAJANI YAKEKati ya mimea yenye faida kubwa katika mwili wa mwanadamu ni tunda la ...
10/03/2022

ZIJUE FAIDA ZA TUNDA LA PERA PAMOJA NA MAJANI YAKE

Kati ya mimea yenye faida kubwa katika mwili wa mwanadamu ni tunda la pera ni moja wapo. Majani ya tunda la mpera yakitumiwa vizuri yanaweza kukuletea matokeo ya kushangaza katika nywele hasa kwa watu wenye tatizo la kukatika kwa nywele na mwili kwa ujumla
Majani ya mpera yana kiwango kikubwa cha Vitamin C, Vitamin A, fiber na potassium.
Wanawake wengi wanaopenda urembo wa nywele wamekuwa wakihangaika na ‘steaming’ za bei mbaya kisa tu kujaza nywele kichwani na kuzifanya zisikatike,
Wasiokuwa na muda wa saluni na wasiokuwa na hela hizi ni habari njema kwao kwamba majani ya mpera ni mazuri kwa kukuza nywele na kuzitibu zile zinazokatika.

Jinsi ya kuyatengeneza k**a dawa
Chukua majani yanayotosha kwenye kiganja chako kisha weka kwenye sufuria yenye lita moja ya maji, chemsha kwa muda wa dakika 15 mpaka 20.
Baada ya hapo, yaache yapoe kisha paka kwenye nywele zako kuanzia kwenye mzizi wa nywele mpaka mwisho.


Ukimaliza fanyia masaji nywele zako k**a mtu anayepaka mafuta nywele zote.
Baada ya hapo unaweza kuacha kwa muda k**a steaming kisha ukaosha.
Fanya hivi mara kwa mara, walau mara 3 kwa juma, naamini utaona mabadiliko.

FAIDA PIA ZA MATUNDA YAKE (MAPERA YENYEWE)
Mapera ni miongoni mwa matunda yenye kiwango kizuri cha vitamin C pamoja na vitamin A na inaelezwa kuwa kiwango cha vitamin C kinachopatikana ndani ya pera ni mara nne ya kiwango cha vitamin hiyo kinachopatikana kwenye chungwa.
Pia mapera yamesheheni virutubisho mbalimbali ikiwa ni pamoja na vitamin B2, E na K pamoja na madini ya chuma, ‘copper’, ‘potassium’ na ‘manganese.’
Kwa mujibu wa utafiti uliowahi kuchapishwa na Jarida la Journal of Human Hypertension mwaka 1993 ulieleza kuwa tunda aina ya pera hupunguza kiwango cha msukumo mkubwa wa damu ndani ya mwili yaani ‘High Blood Pressure’ hii ni kwa sababu ya madini ya potassium na vitamin C ambayo husaidia kuweka sawa msukumo wa damu ndani ya mwili.
1. Utajiri wa Vitamin C:


Mapera yana utajiri mkubwa wa Vitamin C ambayo ni muhimu sana katika mwili wa mwanadamu.
2. Ni kinga nzuri ya kisukari.
Ulaji wa watu wengi unawaweka katika hatari ya kupatwa na ugonjwa wa kisukari lakini matumizi ya mapera yatakupunguzia hatari ya kupatwa na ugonjwa wa kisukari Hii ni kwa sababu mapera yana utajiri mkubwa sana wa Fibre.
Fibre ni muhimu sana katika kupunguza kiasi cha sukari kwenye damu. Vilevile ni muhimu sana katika kuusafisha mfumo wa usagaji
3. Kuimarisha Uwezo Wa Kuona
Mapera yana utajiri mkubwa sana wa Vitamin A au Retinol ambayo ni muhimu sana katika kusaidia kuona vizuri.
Hivyo basi k**a ilivyo kwa karoti, mapera yanasaidia sana katika kuongeza na kuimarisha uwezo wa mtu kuona.
4. Kusaidia katika Uzazi
Mapera yana madini yaitwayo Folate ambayo husaidia katika kurutubisha mayai ya uzazi..
5. Kurekebisha Kiwango Cha Shinikizo la Damu
Madini ya Potassium yaliyomo ndani ya mapera yanasaidia katika ku-normalise shinikizo la damu (Blood Pressure)
Ndizi na mapera vina kiwango cha potassium sawa.
6. Utajiri mkubwa wa Madini Ya Shaba
Mapera yana madini ya shaba (Trace element copper) ambayo ni mazuri sana katika ku- maintain ufanyaji kazi wa tezi ziitwazo thyroid.
Tezi za thyroid zisipofanya kazi vizuri zinaweza kusababisha matatizo mengi ya kiafya kwa mwanadamu.
7. Utajiri wa Madini Ya Manganese
Mapera yana utajiri mkubwa wa madini ya manganese ambayo yanausaidia mwili katika kunyonya ama kupata virutubisho muhimu kutoka kwenye vyakula tunavyo kula.
Chakula tunachotumia kikitumika vizuri mwilini, tunapata virutubisho vyote muhimu k**a vile biotini, vitamin nakadhalika
8. Kuusadia mwili na akili katika ku–relax
Mapera yana utajiri mkubwa wa madini ya magnesium ambayo hufanya kazi ya kuvifanya akili na mwili wa mwanadamu viweze ku relax. Unashauriwa kutumia mapera baada ya kazi nzito. Hii itasaidia katika kuufanya mwili na akili yako kupumzika
9. Mapera ni muhimu katika afya ya akili ya mwanadamu.
Vitamin B3, Vitamin B6 ambazo zinapatikana ndani ya tunda la mpera muhimu katika kuimarisha afya ya akili ya mwanadamu.
Mapera yatasaidia kuufanya ubongo wako u relax
10. NI MUHIMU KATIKA NGOZI YA MWANADAMU
Vitamin C, viondoa sumu na karotini ambavyo vyote vinapatikana ndani ya tunda la mpera ni muhimu sana katika kuimarisha afya ya ngozi.
K**a hiyo haitoshi, kokwa la mpera huwa linatumika katika kutengeneza vipodozi na losheni kwa ajili ya matumizi ya mwanadamu.
FAIDA 16 ZA MAJANI YAKE
1. Chai ya majani ya mpera inaponyesha kifua na kikohozi,
Majani ya mpera yaliyosagwa vizuri yanatumika kutibu muwasho uliotokana na mzio (allergy)
Pia majani haya ya mpera yakichemshwa k**a chai yanaondoa cholesterol iliyozidi mwilini
Chai ya majani ya mpera inapunguza kiwango cha tatizo la sukari mwilini
Chai ya mpera ni dawa nzuri kwa wenye matatizo ya nguvu za kiume
Pia inatumika k**a scrub ya uso chukua majani ya mpera saga kisha tia maji kiasi na inasaidia kuondoa uchafu usoni
7. Pia majani ya mpera yakichemshwa ni dawa ya kuponyesha tumbo la kuhara
8. K**a umejikata kidogo unaweza kutumia majani ya mpera yaliyoshwa na kusagwa vizuri kwa kupunguza maumivu na kukulinda na maambukizi ya bakteria
9. Majani ya mpera yaliyosagwa vizuri yanatumika kutibu eneo la mwili lililong’atwa na mdudu na kupunguza maumivu
10. Chai ya majani ya mpera inaaminika kuwa ina uwezo wa kutibu tezi dume
11. Kutokana na kuwa na vitamini C kwa wingi majani ya mpera yana uwezo mkubwa wa kutibu chunusi
12. Chai ya majani ya mpera inasaidia kupunguza uzito mwilini na kuzuia uharibifu ndani ya sukari mwilini
13. Majani ya mpera yanajaza nywele na kurefusha nywele kwa watu wenye tatizo la kukatika kwa nywele, unasaga na kuchemsha kisha acha yapoe ndio upake kichwani kutoka chini ya ngozi ya kichwa hadi kwenye ncha ya nywele zako
14. Ukiwa na tatizo la vidonda kwenye ufizi, maumivu ya jino na ufizi tafuna majani ya mpera na utaona maajabu ya majani haya
15. Chukua majani ya mpera saga vizuri mpaka yawe laini kabisa ongeza na maji kidogo kisha tumia kupaka usoni k**a scrub inatibu ngozi inayoanza kuzeeka mapema
16. Chai ya mpera inasaidia kwa kutibu mvurugiko wa tumbo.
Pamoja na majani hayo kuwa msaada wa kutibu maradhi mbalimbali , halikadhalika juisi ya mapera nayo husaidia sana kutibu mgolo au bawasiri, figo na hata kuondoa mafuta katika moyo.
Kimsingi mti wa mpera karibu kila sehemu yake ni tiba kwani hata mizizi yake inapochemshwa na kutumia kwa kunywa huenda kuwasaidia wanawake wenye matatizo ya hedhi au wenye matatizo ya kutokwa na maji yenye harufu mbaya sehemu zao za siri.
Sanjari na hayo, watoto wadogo wenye matatizo ya kutopata choo zaidi ya siku mbili, wakinyweshwa maji ya majani hayo baada ya kuchemshwa huwasaidia kuondokana na shida hiyo, lakini ni vyema kuwasiliana na wataalam wa tiba asili kabla ya kuamua kutumia majani hayo k**a tiba kwa mtoto.

Tunda la ukwaju ni tunda lenye faida nyingi sana kwa afya ya mwanadamu. Tunda hili huweza kutumika kutengeneza juisi amb...
10/03/2022

Tunda la ukwaju ni tunda lenye faida nyingi sana kwa afya ya mwanadamu. Tunda hili huweza kutumika kutengeneza juisi ambayo matumizi yake yana faida kubwa sana katika afya ya mwili wa mwanadamu.

NAMNA YA KUTENGENEZA JUISI YA UKWAJU.

Nunua ukwaju wako, ukwaju unapatikana kwa wingi sana masokoni na kwenye supermarkets
Andaa maji kwenye dishi na uoshe kidogo tuu baada ya kuuosha chukua ukwaju wako weka kwenye sufuria yenye maji ya saizi na injika jikoni uache uchemke kwa dakika 10/15 ili uuwe vijidudu
Ipua ukwaju wako jikoni na uache kwa muda upoe andaa maji yako masafi na chujio ili uweze kuchuja juice yako kwa uangalifu zaidi ili upate juice yenyewe
Weka sukari kwa kiasi unachopendelea pia ili kupunguza ukali unaweza ukaweka hiliki au vanila ili kupata taste weka juice yako kwenye fridge ili ipoe tayari kwa kunywa.

FAIDA YA JUISI YA UKWAJU.

Chanzo kizuri cha viuasumu mwilini 'antioxidants' ambavyo huzuia Saratani (cancer)
Chanzo cha Vitamini B na C vile vile "carotentes"
Hushusha joto la mwili na kuondosha homa, hasa homa ya malaria na homa ya matumbo
Huulinda mwili dhidi ya mafua na kero za mafua kooni
Husaidia myeyusho na mmengenyo wa chakula na kuondosha kuvimbiwa
Husaidia kutibu matatizo ya nyongo (bile disorders)
Husaidia kurahisisha choo (laxative)
Husaidia kupunguza wingi wa lehemu (cholesterol) na hivyo kuimarisha moyo
Husaidia ngozi kuwa nyororo, vile vile husaidia ngozi inayopona baada ya kuungua au yenye vidonda
Husaidia kuua minyoo tumboni (kwa watoto wadogo)

Address

Mabibo
Dar Es Salaam

Telephone

+255713051747

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Afya ya Mama posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Afya ya Mama:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram