Afya Kamili Kwa wote

Afya Kamili Kwa wote Jukwa la Elimu na ushauri kwa wote

๐Ÿ”ตKWA MTU WA TEZI DUME UNAWEZA KUZINGATIA VYAKULA HIVI HAPA   Kwanza jitahidi kupunguza matumizi ya vyakula vya wanga (St...
14/03/2023

๐Ÿ”ตKWA MTU WA TEZI DUME UNAWEZA KUZINGATIA VYAKULA HIVI HAPA

Kwanza jitahidi kupunguza matumizi ya vyakula vya wanga (Stachi) saana na vyakula vyenye sukari zaidiii, Matumizi ya wanga yawe nikidogo sanaa.

๐Ÿ‘‰K**a utatumia ugali basi tumia Dona nzuri, na Mboga ziwe nyingi zaidi, Mboga za majani, dagaa, samaki, mayai, nyama sio mbaya.

Ongeza Matumizi ya matunda k**a Maparachichi ambayo yana vitamin E muhimu Sana kwenye Madini mengine mwili

Pia ongeza matumizi ya Tikiti Maji Kwa wingi na ndizi zakuiva k**a hauna tatizo la kisukari .

๐Ÿ‘‰Pia penda sana kutumia karanga, kwani Zina Amino asidi ambazo zinasaidia uzalishaji wa Madini ya ziki kwa wingi.

๐Ÿ‘‰Kunywa chai ya Tangawizi Kila siku ukiweza, hii Inasaidia kusisimua zaidi mwili na mfumo wa damu.

๐Ÿ‘‰Pia jitahidi kufanya Mazoezi pia hata ya kutembea au kukimbia, Epuka kutumia vyakula vya viwandani yani fast food, k**a unatumia pombe unaweza kupunguza au kuacha kabisa, au kupunguza Kwa kiasi kikubwa.

๐Ÿ‘‰Pia ongeza Matumizi ya Mboga mboga za majani

Pia k**a utapata juice ya muunganiko wa korosho, tende,N**i,Karanga mbichi,Muhogo mbichi(Kutafuna),Maziwa fresh walau glasi moja Kila siku ni nzurii zaidi

CALL/WHATSAPP 0787367182

๐Ÿ”ต KUBADILI MFUMO WA ULAJI Kula vyakula Visivyo sahihi huleta magonjwa yanayotokana na mfumo mzima wa ULAJI na kupelekea ...
12/03/2023

๐Ÿ”ต KUBADILI MFUMO WA ULAJI

Kula vyakula Visivyo sahihi huleta magonjwa yanayotokana na mfumo mzima wa ULAJI na kupelekea matatizo katika mfumo wa uzazi, ukiwa na Mvurugiko wa homoni, kitambi, uzito mkubwa, kisukari, basi kwako unakuwa kwenye nafasi finyu ya kuweza kubeba ujauzito, acha kula holela, Epuka vyakula vya kukaanga na mafuta mabaya, Acha kunywa vinywaji vya viwandani, Acha kunywa pombe, Epuka Kwa silimia kubwa vyakula vya wanga, kula kiasi kidogo mno, Acha kula fast food, chips, snacks, n.k, Zingatia vyakula hivi hapa vitakusaidia zaidi kutimiza lengo lako.

ASUBUHI- k**a unatumia chai basi,unaweza kutumia maziwa fresh, au Chai ya Tangawizi+mchai chai+ mdarasini, au supu Yako safi, nyama, au ya samaki, Acha kula maandazi, bagia, chapati, na vyakula vingine vinavyotongana na ngano zilizokobolewa.

๐Ÿ‘‰Unaweza kutumia viazi vitamu, magimbi, ndizi za kuchemsha,+ ongeza matunda, au mayai Asubuhi sio mbaya.

๐Ÿ”ต PATA ZAIDI VYAKULA HIVI HAPA CHINI๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡

1:Mboga mboga za majani, kwani Ni chanzo Cha vitamic, C usisubiri kumeza vidonge vya vitamini c, anza kutumia vyakula,Pia Ni chanzo kizuri Cha Folic Acid, Tumia zaidi kabichi, broccoli, nyanya, spinach, karoti, namboga zingine za kijani.

2:)MATUNDA.
Matunda Ni chanzo kizuri Cha Antioxidants, tumia zaidi, maparachichi ndizi, machungwa, tikiti maji, nanasi, zabibu.

3)OMEGA 3 FATS
Chanzo Cha Omega 3, Samaki, salmon fish ๐ŸŸ) mayai, pia nyama yakuku tumia zaidi.
๐Ÿ‘‰Pia tumia Sana Maziwa, kwani utapata Madini ya calcium, fats, vitamin D.

4): Pia tumia kunde, Maharage,Nataka K**a ngano,nyama,
mchele wa kahawia.

5:)Zingatia kutumia vitu Asilia (viungo)
๐Ÿ‘‰Tumia mafuta ya Mzeituni(Olive oil)kukaangia/kupikia, pia mafuta ya Samli, N**i.
๐Ÿ‘‰Tumia mbegu za maboga,unaweza kutafuna, au kuunga kwenye mboga zako.
๐Ÿ‘‰Tumia Mbegu za alizeti.
๐Ÿ‘‰Tumia karanga mbichi, unga kwenye mboga zako au tafuna.
๐Ÿ‘‰Tumia vitunguu swaumu walau meza punje saba kilasiku.
.........
Jitahidi Sana kwa asilia kubwa kufuata utaratibu...

Call/Whatsapp 0787367182

๐Ÿ”ต MAMA MJAMZITO ZINGATIA HAYA HAPA ๐Ÿ‘‡ ๐Ÿ‘‡ ๐Ÿ‘‡ ๐Ÿ‘‡ 1.Kula milo minne kwa siku na asusa au vitafunwa mara nyingi kadri uwezavyo h...
12/03/2023

๐Ÿ”ต MAMA MJAMZITO ZINGATIA HAYA HAPA

๐Ÿ‘‡ ๐Ÿ‘‡ ๐Ÿ‘‡ ๐Ÿ‘‡
1.Kula milo minne kwa siku na asusa au vitafunwa mara nyingi kadri uwezavyo hii itakuwezesha kuupa mwili nguvu na lishe ya kutosha kwa ajili yako na mtoto anayekua tumboni. Hakikisha mlo wako unakuwa na vyakula mchanganyiko vinavyopatikana katika jamii. Asusa au vitafunwa vinaweza kuwa vitu k**a vile mahindi ya kuchoma au kuchemsha, kikombe cha maziwa, viazi, mayai, karanga, matunda n.k.

2. Kuepuka kunywa kahawa au chai wakati wa mlo kwani huingiliana na ufyonzwaji wa virutubisho katika mwili.

3 Kumeza vidonge vya kuongeza damu (FEFO) kila siku kwa kipindi chote cha ujauzito.

4. Kuongeza ulaji wa vyakula vyenye asili ya wanyama mfano nyama, kuku, samaki, dagaa n.k. Vyakula vya asili ya wanyama huongeza damu kwa haraka zaidi.

5. Kula matunda ya aina mbali mbali yanayopatikana kwa msimu huo na mbogamboga kwa wingi kila siku

6. Kutumia chumvi yenye madini joto wakati wote
Kunywa maji ya kutosha kila siku (angalau glasi 8 au lita 1.5). unaweza ukaongeza ladha kwa kuweka limau au ndimu.

7. Kujikinga na Malaria kwa kutumia vyandarua vilivyowekwa viwatilifu na kutumia dawa za kuzuia malaria na minyoo k**a inavyoshauriwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.

8. Kujikinga na maambukizi ya magonjwa ya ngono na virusi vya UKIMWI
Kuepuka utumiaji wa sigara na pombe kwani inaathiri matumizi ya virutubishi na afya ya mama na mtoto.

9. Kuanza kliniki mapema mara tu ya kujihisi mjamzito na uendelee kuhudhuria ili kupata huduma na ushauri zaidi utakaoboresha lishe na afya kwa wote

Call/Whatsapp 0787367182

Address

Makumbusho
Dar Es Salaam

Telephone

+255787367182

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Afya Kamili Kwa wote posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Afya Kamili Kwa wote:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram