Suric health point

Suric health point Tunatoa ushauri na elimu ya lishe kwa wenye changamoto ya sukari .

Ugonjwa wa kisukari ni ugonjwa unaochangiwa sana na matumizi yasiyo sahihi ya vyakula.Kumekuwa na ongezeko kubwa la wago...
12/10/2023

Ugonjwa wa kisukari ni ugonjwa unaochangiwa sana na matumizi yasiyo sahihi ya vyakula.

Kumekuwa na ongezeko kubwa la wagonjwa wa kisukari ,pamoja na hali za wagonjwa wa kisukari kuzorota kutokana na kutotambua na kutokua na elimu sahihi ya matumizi ya vyakula kwa wataalamu wengi wa afya pamoja na wagonjwa.

Kwa watu kuendelea kutumia kiwango kikubwa cha nafaka na vyakula vilivyokobolewa(refined grains), mafuta, sukari na vyakula vinavyotokana na wanyama, kumepelekea ugonjwa huu kukua kwa Kasi.

Si hivyo pekee bali pia kwa wengi wa watu kuwa na maono yasiyo sahihi katika matibabu ya ugonjwa wa kisukari, watu wengi wamekuwa wakiendelea kushughulika na kiasi cha sukari katika damu kwa kuendelea kutumia dawa kadri siku zinavyokwenda, na kutoshughulika na chanzo Kikuu ili kutibu ugonjwa huu.

Kwa kufuata lishe iliyosahihi tunaweza kuita (nutrient rich diet, lower calorie diet, au nutritarian diet) pamoja na program sahihi ya mazoezi huweza kubadili kabisa mfumo wa afya wa mwili wa mwenye changamoto ya kisukari kwa kuupa mwili mazingira sahihi ya kibiokemikali na virutubisho sahihi hivyo kuamsha upya mfumo wa uponyaji wa kimwili wa asili na kuweza kuurudisha mwili katika hali ya kawaida na kuondosha changamoto ya kisukari pamoja na magonjwa mengine andamizi.

Kwa matumizi ya vyakula vyenye kiasi kikubwa cha micronutrients k**a mboga mboga za majani, Legumes (maharage,kunde n.k),seeds(flux seeds,mbegu za maboga n.k),Nuts(aina tofauti za Karanga) na matunda huweza kuzuia na kuweka sawa ugonjwa wa kisukari.

Ungana na nasi kwa kutufollow katika page zetu ,ama kwa kucomment namba yako ya WhatsApp ili kupata darasa za bure katika magroup yetu ya WhatsApp.

Kwa mujibu wa shirika la afya duniani (WHO), kuwa  kumekua na ongezeko kubwa la ugonjwa wa kisukari kwa watu wa vipato v...
02/10/2023

Kwa mujibu wa shirika la afya duniani (WHO), kuwa kumekua na ongezeko kubwa la ugonjwa wa kisukari kwa watu wa vipato vyote.

Ambapo visababishi vikubwa vya ugonjwa huu wa Aina ya pili ya kisukari ni pamoja na ulaji na matumizi ya vyakula usio sahihi, uzito uliopitiliza(obesity), kukaa bila kufanya mazoezi na mfumo mbaya wa maisha.

Takwimu zinaonyesha kumekuwa na ongezeko kubwa la wenye changamoto ya kisukari kutoka watu milioni 108 kwa mwaka 1980 na kufikia milioni 425 kwa mwaka 2014 duniani kote.

Hivyo kupelekea kuongezeka kwa idadi ya Vifo vinavyosababishwa na ugonjwa wa kisukari kwa watu wenye umri chini ya miaka sabini hasa kwa wenye kipato cha chini na cha Kati.

Si vifo pekee Bali pia ugonjwa wa kisukari umekua kisababishi kikubwa cha ulemavu wa macho ( upofu), kufeli kwa figo (kidney failure), mshtuko wa Moyo(heart attack) pamoja na kiharusi(stroke).

Katika nchi ya ya Tanzania katika utafiti uliofanywa wa STEPS mwaka 2012 katika wilaya 50 za Tanzania , uliofanywa na wizara ya afya kwa kushirikiana na Taasisi ya utafiti wa magonjwa ya binadamu (NIMR) na shirika la afya duniani (WHO), ilionyesha kuwa asilimia 9.1 ya watu wenye umri kati ya miaka 25 Hadi 64 Wana kisukari.

Hivyo ilionyesha kuwa katika kila watu 11 nchini mtu mmoja ana kisukari.

Kwa kumalizia ,kila mmoja ana wajibu wa kuzuia ongezeko la ugonjwa wa kisukari kwa kufuata mfumo Sahihi wa lishe pamoja na kubadili mfumo wa maisha ,ili kuweka miili katika afya Bora.

Wako anaejali afya yako

Mkurugenzi suric health point,Mr Suleiman Hamad

Habari!Karibu Suric health point ,usiache kutufuatilia kwa kutufollow ili kuweza kupata elimu na mafunzo ya lishe kwa we...
07/08/2023

Habari!

Karibu Suric health point ,usiache kutufuatilia kwa kutufollow ili kuweza kupata elimu na mafunzo ya lishe kwa wenye changamoto ya sukari ambapo hutayapata mahala pengine popote.

* Utajifunza umuhimu na faida za vyakula mbali mbali katika kuimarisha kinga na afya ya mwili.

* Utajifunza kuhusu madhara ya baadhi ya vyakula na vinywaji katika kuzorotesha kinga na afya ya mwili.

* Utajifunza njia rahisi ya kuandaa vyakula vyako kwa namna nzuri kwa kuzingatia kanuni za kiafya bila kupoteza virutubisho , kuwa na ladha na vitamu zaidi.

* Utajifunza namna ya kupangilia lishe yako kwa usahihi kwa kuzingatia kiasi na ubora ili kupata virutubisho sahihi.

Hongera sana kwa kutembelea suric health point, usisahau kutufollow ili kuwa wa Kwanza kupata mafunzo haya ya lishe kwa wenye changamoto ya sukari.

Mlo sahihi, Ishi kibingwa !

Address

Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 08:30 - 17:00
Tuesday 08:30 - 17:00
Wednesday 08:30 - 17:00
Thursday 08:30 - 17:00
Friday 08:30 - 17:00
Saturday 08:30 - 15:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Suric health point posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Suric health point:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram