03/01/2023
UJUE MAGONJWA YA MOYO – AINA, CHANZO, DALILI, GONJWA HILI HALINA UMRI NA PIA HUSABABISHWA NA MFUMO WA VYAKULA NA CHANGAMOTO ZINGINEZO.
POWER BY # Officialmoyo_uzazi
Dar es salaam
Call 0745001254
Magonjwa ya Moyo ni magonjwa yanayoambatana na kuathiri moyo. Mara nyingi magonjwa ya moyo yanaambatana na mishipa ya damu kuwa na tatizo ambapo moyo hushindwa kufanya kazi, moyo hutegemea damu ambayo hubeba oxygen, madini, vitamins, kinga ya mwili, joto, homoni na vingine vingi.
AINA ZA MAGONJWA YA MOYO
Zipo aina mbalimbali za magonjwa ya moyo hutofautiana japo yote huathiri moyo, nayo ni;
1:Ugonjwa wa moyo unaotokana na kuathirika kwa mishipa ya damu (Coronary artery disease) Hili ni tatizo linalowakuta watu wengi, mishipa ya damu hupasuka na kuharibika hii hutokana na mishipa ya damu kuwa na uchafu na mafuta mengi na kufanya damu isipite vizuri
Mapigo ya moyo kwenda tofauti (Heart Arrhythmias) Hii hutokea pale mapigo ya moyo kwenda taratibu isivyo kawaida au kwenda haraka isivyo kawaisda, pia mapigo ya moyo kwenda ovyo. Hii ni hatari sana na huua sana
2:Moyo kushindwa kufanya kazi (Heart Failure) Hii ni hali moyo hushindwa kufanya kazi yake k**a kupampu na kusambaza damu, kusambaza oxygen. Hii inaweza kutokea kwa mtu mwenye magonjwa k**a ugonjwa wa moyo wa misipa kuathirika, Shinikizo la damu, na magonjwa mengine
3:Magonjwa ya moyo ya kuzaliwa (Congenital heart disease) Haya ni magonjwa ambayo wengi huzaliwa nayo, yanaweza kuwa ni baadhi ya kasoro katika mwili k**a baadhi ya chemba za moyo kuziba au kupasuka, oxygen kupita kwa shida na vinginevyo.
4:Ugonjwa wa valvu na misuli ya moyo (Heart Valve Disease & Cardiomyopathy (Heart Muscle Disease)) Katika moyo kuna chema nne nazo zinapitisha damu na oxygen kutoka kwenye mapafu, valvu hufunguka na kufunga. Valvu na misuli ikiwa imepasuka na kuharibika husababisha tatizo la moyo.
5:Moyo kutanuka. Hii hutokea pale damu ikiingia ndani ya moyo harafu mishipa ya kutoa damu ikiwa na tatizo ikashindwa kutoa damu nje ya moyo moyo utaanza kutanuka siku hadi siku. Kutanuka kwa moyo kunatokea usipotibu baadhi ya matatizo k**a shinikizo la damu, moyo kwenda mbio, valvu na misuli ya moyo n.k.
6:Shinikizo la damu (B.P) ni shinikizo la damu yako kwenye kuta za mishipa yako kwani moyo wako unasukuma karibu na mwili wako. Unaweza kuwa na shinikizo la damu (shinikizo la damu) kwa miaka bila dalili yoyote.
7:Mshtuko/ Shambulio la moyo (Heart Attack). Ni kifo cha sehemu ya misuli ya moyo inayosababishwa na kuzuiwa wa usambazaji wa damu. Amana zilizo na mafuta huunda kwa wakati, na kutengeneza alama katika mishipa ya moyo wakoIkiwa baadhi ya misuli ya moyo inakufa, mtu hupata maumivu ya kifua na kukosekana kwa umeme kwa tishu za misuli ya moyo.
CHANZO CHA MAGONJWA YA MOYO
Magonjwa ya moyo hutokea pale ambapo moyo huathiriwa na kuharibiwa kwa vitenda kazi vyake. Kuna mitindo ya maisha inayoweza kukuweka hatarini kupata magonjwa ya moyo nayo ni pamoja na;
Heart-Disease
1:Kuwa na halemu (Cholesterol) na Shinikizo la damu (B.P)
2:Kuvuta sigala
3:Uzito kupita kiasi na unene uliozidi
4:Kisukari
5:Kukaa sehemu kwa mda mrefu bila kuufanyisha kazi mwili
6:Ulaji holela wa vyakula vyenye mafuta mengi na sukari nyingi
7:Utumiaji wa vinywaji vinavyobadili hali ya mwili
DALILI ZA UGONJWA WA MOYO
1:Mara nyingi dalili hujionesha wakati mtu kakaa na ugonjwa kwa mda mrefu kidogo, ila kuna zingine zinatangulia na mara nyingi wengi huwa wanazipuuzia.
2:Moyo kwenda mbio (Moyo kudunda kwa nguvu isivyo kawaida )
Uchovu uliopitiliza, mwili kuwa dhaifu na kuchoka haraka hata kwenye shughuri ndogo
3:Maumivu ya kifua hasa yanayotembea mpaka kwenye mabega, shingo au taya
4:Kushindwa kulala vizuri hasa kushtuka usingizini kuhisi k**a unakabwa na kukosa pumzi
5:Tumbo kujaa, kichefuchefu na kutapika
6:Kukosa pumzi au kushindwa kupumua vizuri hasa unapolala chali
Miguu, uso na tumbo kuvimba na kujaa
UGONJWA HUU NI HATARI KWA AFYA YAKO WOTE MNAKARIBISHWA UJE UPATE SULUHISHO KINGA NI BORA KULIKO TIBA
KWA MAWASILIANO: 0745001254