Social Medical Online

Social Medical Online Health for "choice" not for chance
SOCIAL MEDICAL ONLINE health education counsel o

SARATANI_YA_TEZI_DUMESaratani ya tezi dume inashika nafasi ya tatu kwa kusababisha vifo vinavyotokana na kansa kwa wanau...
28/11/2019

SARATANI_YA_TEZI_DUME

Saratani ya tezi dume inashika nafasi ya tatu kwa kusababisha vifo vinavyotokana na kansa kwa wanaume duniani. Ugonjwa huu ni chanzo kikuu cha vifo vinavyosababishwa na saratani kwa wanaume wenye umri wa kuanzia miaka 45 na kuendelea, hata hivyo, satarani ya tezi dume kwa sasa inawapata sana wanaume kuanzia miaka 25. Kwa ufahamisho tu ni kwamba neno saratani ni jina la ugonjwa ambalo hutokea wakati chembechembe za hai au seli katika sehemu fulani ya mwili zinapoanza kukua bila kufuata utaratibu wa mfumo wa mwili na kutengeneza vijiuvimbe vidogo vidogo. Kwa kawaida seli huwa zinajigawa, kupevuka na baadaye zinakufa. Sasa Utokeaji wa saratani ni pale ambapo sili zilizotakiwa kufa hazifi zinaendelea kuishi wakati zile mpya zinazidi kuzaliwa. Sasa ni kwamba Wanaume wote wanazaliwa na tezi dume lakini baada ya BALEHE Tezi dume huongezeka ukubwa mara Mbili. Na ikifika miaka 30 Tezi dume huanza kukua haraka zaidi maaana ukuaji wa Tezi dume huenda sambamba na Umri.
Kuna vihatarishi vingi vinavyochangia mwanamume kupata saratani ya tezi dume. Vifuatavyo ni baadhi yake;
1. Kwanza kabisa ni umri. Nafasi ya kupata saratani ya tezi dume huongezeka sana hasa ukifikia umri wa karibu miaka 50 na kuendelea.
2. Nasaba ni kihatarishi kingine ambapo wanaume wenye historia ya tatizo hili kwenye familia zao, yaani wale ambao mmoja wa ndugu zao wamewahi kuugua ugonjwa huu huwa katika hatarini ya kupata kansa hiyo kutokana na kurithi jeni za ugonjwa huo.
3. Suala jingie ni lishe ambapo wanaume wanaopenda kula nyama au (red meat) na walaji wa chakula chenye kiasi kikubwa cha mafuta hasa ya wanyama huwa katika hatari kubwa ya kupata saratani ya tezi dume.
4. Vilevile wataalamu wanatumbia kuwa, wanaume wasiopenda kufanya mazoezi, wanene na wenye upungufu wa virutubisho vya Vitamin E pia wako kwenye hatari zaidi ya kupata saratani ya kibofu cha mkojo. Wanaume wengine walio katika hatari kubwa ya kupata saratani ya tezi dume ni pamoja na wale wenye asili ya Afrika (Weusi) ikilinganishwa na wazungu, wakulima wanaotumia aina fulani ya mbolea za kemikali, wanaofanya kazi katika viwanda vya kutengeneza matairi na wachimbaji madini, hususan aina ya cadmium

DALILI ZA SARATANI YA TEZI DUME
Hayo yote yakiwa ni tisa, kumi ni je, dalili za saratani ya tezi dume ni zipi?Katika hatua zake za awali, dalili za saratani ya tezi dume hazitofautiani na zile za kuvimba kwa tezi dume au BPH. Dalili hizo ni pamoja na, 1) Kupata shida wakati wa kuanza kukojoa. 2) Kutiririka kwa mkojo baada ya kumaliza kukojoa. 3) Kukojoa mkojo wenye mtiririko dhaifu. 4) Kukojoa mara kwa mara hasa nyakati za usiku. 5) Kujikakamua wakati wa kukojoa na kushindwa kumaliza mkojo wote na 6) kutoa mkojo uliochanganyika na damu.
Lakini kitaalamu imethibitika kuwa endapo Mwanaume huyu hasa mwenye miaka kuanzia 30 atapata Virutubisho maalumu vya Vitamin na Madini anaweza kuepuka Tatizo hili. Kwani kuna Madini Maalumu na Vitamin Maalumu ambazo Mwanaume ataweza kuwa anatumia k**a Kinga dhidi ya Saratani ya TEZI DUME. Pia virutubisho hivi vinauwezo mkubwa wa kupambana na Saratani changa ya Tezi Dume kwani zikiingia Mwilini bidhaa hizi huenda kuondoa uvimbe na kuua zile seli za saratani zilizoanza kuzaliwa. Wanaume waliopo hatarini zaidi ni kuanzia miaka 45 na kuendelea. Kwani katika kila wanaume 6 inakadiriwa kuwa mmoja atakuwa na Saratani hii.

“True emotional healing doesn't happen without feeling. The only way out is through.”
20/11/2019

“True emotional healing doesn't happen without feeling. The only way out is through.”

FAHAMU UGONJWA WA U.T.I NA MATIBABU YAKEUTI, yaani Urinary Tract Infections, ni magonjwa au maambukizi katika njia ya mk...
07/11/2019

FAHAMU UGONJWA WA U.T.I NA MATIBABU YAKE
UTI, yaani Urinary Tract Infections, ni magonjwa au maambukizi katika njia ya mkojo. Maambukizi hayo huletewa na vimelea (bakteria) au kitu chochote kinachoweza kusababisha shida katika njia ya mkojo.Vitu hivi vinaweza kuingia kwenye njiaya mkojo kutoka nje au ndani ya mwili. Maambukizi haya hayabagui jinsia wala umri, kwani yanaweza kumpata yeyote.UTI usipotibiwa, unaweza kuenea na kuadhiri viungo vingine vinavyoshikana na njia hii k**a vile kibofu cha mkojo (bladder), mirija inayoshikanisha kibofu cha mkojo na figo (ureter) na sehemu inayotoa mkojo kutoka kwenye kibofu na kuutoa nje (urethra). Kwa ufupi, UTI huadhiri viungo ambavyo hupitisha mkojo kutoka mwilini na kuutupa nje.Wanawake huadhirika zaidi na UTI ikilinganishwa na wanaume. Hii ni kwasababu za kimaumbile. Maambukizi haya huweza kusababishwa na historia ya familia au kufanya mapenzi na watu kadhaa bila kutumia kinga.Wasichana wadogo walio chini ya umri wa miaka miwili na wavulana ambao hawajatahiriwa pia huupata ugonjwa huu mara zaidi.Vimelea vinavyosababisha UTI ni k**a vileStaphylococcus saprophyticusnaEscherichia coli(E Coli). Asimilia chache ya maambukizihaya huweza kuletwa na virusi au fangasi (fungus).Dalili za UTIDalili za UTI ambazo mtu hupata hulingana na sehemu ambayo imeathirika. Hivyo basi, dalili zitakua tofauti wakati mrija wa mkojo, kibofu au figo zimeathirika.
Dalili hizo zimeelezwa kwa kina hapa.Dalili iwapo mrija wa kutoa mkojo kwenye kibofu umeathirika
*.Mtu huhisi k**a kwamba anaungua wakati anapokojoa. Kuchomeka huko huweza kuzidi na kuwa uchungu (maumivu).
*.Shida wakati wa kukojoa k**a vile kushindwa kudhibiti kasi ya mkojo.
*.Mtu anaweza kukawia sana kabla yamkojo kutoka.
*.Mtu kuhisi kukazwa sana lakini aendapo chooni, mkojo kidogo tu ndio hutoka.
*.Kukojoa kiasi kidogo cha mkojo mara nyingi.Dalili za UTI iwapo kibofu cha mkojo kimeathirika
*.Mtu huweza kuona damu kwenye mkojo anapoenda haja. Hii huweza ikawa dalili ya UTi ingawaje magonjwa mengine pia huleta dalili sawa na hii*.Pia mtu huweza kuhisi maumivu kwenye nyonga (hip area). Hii huathiri wanawake zaidi.
*.Kuhisi k**a kibofu kimejaa wakati wote.
*.Dalili ingine ni kuwa na maumivu chini ya kitovu.
*.Dalili ya mwisho ni mtu kukujoa mara kwa mara na kuhisi uchungu anapokojoa.
Dalili iwapo figo zimeathirika
*.Mtu hupata kichefuchefu mara kwa mara iwapo ugonjwa wa UTI umemwathiri.
Kichefuchefu ni hali ya kuhisi kutapika.
*.Maumivu kwenye mbavu.
*.Dalili hii ya kichefuchefu huweza kuzidi na mwathiriwa kuanza kutapika anapokula chakula.
*.Dalili ingine ni mtu kuumwa na upande wa juu wa mgongo. Hii inaweza kuwa kuanzia katikati ua utiwa mgongo, kwenye mabega na kwenye shingo.
*.Dalili hizi huweza kuambatana na homa kali.
*.Dalili ya mwisho ni mtu kuhisi baridi kali na kutetemeka sana pasi na kuwepo kwa baridi.
Kuna dalili za UTI ambazo hutokea wakati ugonjwa huu umeathiri mahali popote kwenye njia hii ya kutoa mkojo.
Rangi ya mkojo kugeuka na kuwa mawingu mawingu, pia unaweza ukawa rangi ya brauni aupinki.Maradhi yanapozidi, mkojo huwa na rangi nyekundu na wenye harufu kali.
Wanaume huweza kupata maumivu wakati wa kwenda haja kubwa.Hatari za UTIMagonjwa yanayosababisha UTI ni rahisi kutibiwa kutumia dawa za antibaotiki.
Hata hivyo, mtu huhimizwa kupata matibabu mara moja na kumaliza dawa k**a alivyoagizwa na daktari.
Maradhi hayayasipotibiwa huweza kuleta shida zaidi k**a vile:
*.Maradhi kujirudia baada ya kutibiwa na kupona kabisa. Hii hutokea sana sana kwa wanawake ambao wanaathirika na UTI zaidi ya mara tatu.
*.Kuharibika kwa figo kutokana na shida zinazotokea k**a vilekidney infection(Pyelonephritis). Hii huweza kutokea mtu asipopokea matibabu.
*.Wanawake huweza kuwazaa watoto mapema (premature birth) au kuzaawatoto wenye uzani mdogo zaidi.
*.Njia ya mkojo (urethra) kwa wanaume hufinyika na kuwa ndogo. Hii hutokana na ugonjwa waUrethritiskutokea mara kadhaa. Pia maradhi k**agonococcal urethritishuweza kusababisha shida hii.
*.Mwisho, ugonjwa wa UTI unapofika kwenye figo kupitia mshipa wa kutolea mkojo, mtu huweza kupata Sepsis. Hii ni shida inayokumba figo na kuziangamiza kabisa. Hii ni mojawapo ya shida hatari kabisa kwani inaweza kumfanya mwathiriwa kuaga.Hali zinazochangia kupata maradhi ya UTI
*.Maumbile: Wanawake huwa na njia fupi ya kutoa mkojo (urethra) kuliko wanaume. Hivyo basi, vimelea na vitu vinavyosababisha UTI huweza kuingia kwenye njia ya mkojo haraka.
*.Ngono: Watu wanaofanya mapenzi huambukizwa UTI zaidi ya wasiofanya mapenzi k**a vile watoto. Walio na wapenzi wengi huwa hatarini ya maambukizi zaidi.
*.Njia za kupanga uzazi: Wanawake wanotumia njia zadiaphragmkupanga uzazi hupata maambukizi zaidi ya wanaotumia kinga aina yaspermicidals.
*.Kufunga uzazi: Wanawake waliofikisha miaka ya kufunga uzazi huwa hatarini zaidi kutokana na upungufu waestrogen.
*.Kukosa kinga mwilini: Mtu anapokua na maradhi yanayopunguza kinga ya mwili k**avile ugonjwa wa sukari au Ukimwi, anaweza kuupata ugonjwa huu kwa urahisi.
*.Upasuaji: Iwapo mtu amefanyiwa upasuaji karibu na njia ya mkojo, inaongeza uwezekano wake wa kupata UTI.
*.Kufungika kwa mishipa ya figo: Mawe yanayokuwa kwenye figo huleta shida za kufungika kwa mishipa ya kutoa mkojo kwenye fig

If you dont kill pollution,it will kill you and your child   a part of solution not a part of the pollution"
29/10/2019

If you dont kill pollution,it will kill you and your child a part of solution not a part of the pollution"

Knowledge = Prevention
25/10/2019

Knowledge = Prevention

Warning: too much fruit causes: health!  MEDICAL ONLINE
24/10/2019

Warning: too much fruit causes: health!
MEDICAL ONLINE

HEALTH tips........for more contract with us
23/10/2019

HEALTH tips........for more contract with us

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Social Medical Online posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share