Amana Hospital Ilala

Amana Hospital Ilala Amana Hospital take your health in safe place

WAZIRI WA AFYA MHE. MOHAMED MCHENGERWA AFANYA ZIARA YA KIMKAKATI HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANAWaziri wa Afya, Mohamed...
27/02/2026

WAZIRI WA AFYA MHE. MOHAMED MCHENGERWA AFANYA ZIARA YA KIMKAKATI HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA

Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa, leo Februari 27, 2026, amefanya ziara ya kimkakati katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana kwa lengo la kukagua utolewaji wa huduma za afya pamoja na maendeleo ya uboreshaji wa miundombinu ya hospitali hiyo.

Katika ziara hiyo, Mhe. Mchengerwa ameambatana na Katibu Mkuu Dkt. Seif Shekalaghe pamoja na menejimenti ya Wizara ya Afya, ambapo alikagua hali ya upatikanaji wa huduma, kusikiliza changamoto zinazowakabili watumishi na wagonjwa, na kueleza mikakati madhubuti ya serikali katika kuimarisha ubora na ufanisi wa huduma za afya kwa wananchi.

Aidha, Waziri Mchengerwa amesisitiza umuhimu wa uwajibikaji, nidhamu ya kazi na matumizi sahihi ya rasilimali zilizotengwa na Serikali ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora, salama na kwa wakati.

Sambamba na hayo Mhe. Mchengerwa Amesema Serikali itaendelea kuwekeza katika ununuzi wa vifaa tiba vya kisasa, kuongeza wataalamu wa afya na kuboresha mazingira ya kutolea huduma ili kukidhi mahitaji ya wananchi wanaotegemea hospitali hiyo na vituo vingine vya afya nchini.

WANANCHI WAPATIWA ELIMU JUU YA UMUHIMU WA KUMALIZA DOZI ZA DAWA YA ANTIBIOTICWananchi wametakiwa kutumia dawa za antibio...
26/02/2026

WANANCHI WAPATIWA ELIMU JUU YA UMUHIMU WA KUMALIZA DOZI ZA DAWA YA ANTIBIOTIC

Wananchi wametakiwa kutumia dawa za antibiotics kwa kuzingatia maelekezo sahihi kutoka kwa daktari na kuacha tabia ya kukatisha dozi punde wanapoona kuwa wamepata nafuu.

Wito huo umetolewa leo na Wafamasia wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana waliokuwa wakitoa elimu juu ya umuhimu wa kumaliza dozi ya dawa za antibiotics kwa Wateja waliokuja kupata huduma za matibabu hospitalini hapo

Akitoa elimu kwa Wateja hao Mfamasia wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Bi. Saada Khalid amesema dawa za antibiotics ni dawa zinazotumika kutibu maambukizi yanayosababishwa na bakteria na hutolewa kwa muda maalum kulingana na aina y amaambukizi lakini watu wengi huacha kutumia dawa wanapohisi kuwa wamepata nafuu.

Pamoja na hayo amongeza kuwa kuna umuhimu wa mtu kumaliza dozi ili kuhakikisha kuwa bakteria wote wameangamizwa, kuzuia maambukizi kurudi tena na kupunguza hatari ya kupata usugu wa dawa.

“Mtu asipomaliza dozi aliyoandikiwa anaweza kupata madhara mbalimbali ikiwemo maambukizi kurudi kwa nguvu zaidi, Bakteria kuwa sugu kwa dawa,kuongezeka kwa gharama za matibabu pamoja hatari ya kulazwa hospitalini”amesema Bi. Saada

Aidha ameongeza kuwa watu wamekuwa wakifanya makosa mbalimbali ya antibiotics ikiwemo kuacha dawa baada ya siku chache, Kuhifadhi dawa zilizobaki kwa matumizi ya baadaye, kushirikiana dawa na mtu mwingine, pamoja na kununua antibiotics bila kupata ushauri wa daktari.



  za kazi ‼️
25/02/2026

za kazi
‼️

Ramadan Kareem 🕌
19/02/2026

Ramadan Kareem 🕌

Kwaresma njema ✝️
19/02/2026

Kwaresma njema ✝️

Heri ya jumatano ya Majivu
18/02/2026

Heri ya jumatano ya Majivu

AMANA WAOMBOLEZA KIFO CHA MTOTO ALIYETELEKEZWA NA WAZAZI WAKE BAADA YA KUZALIWA NA UZITO PUNGUFU NA ULEMEVU WA MIKONOMto...
17/02/2026

AMANA WAOMBOLEZA KIFO CHA MTOTO ALIYETELEKEZWA NA WAZAZI WAKE BAADA YA KUZALIWA NA UZITO PUNGUFU NA ULEMEVU WA MIKONO

Mtoto aliyetelekezwa na wazazi wake baada ya kuzaliwa na uzito pungufu na ulemevu wa mikono katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Perpetua Amana amefariki baadaya ya kuugua ghafla katika kituo cha kulelea Watoto cha Msimbazi Centre jijini Dar es Salaam.

Mtoto huyo alizaliwa akiwa na uzito wa Kg 1.2 na baadaye mama yake kutoweka na kumuacha wodini hivyo uongozi wa Hospiatali ya Amana uliamua kuchukua jukumu kumpatia uangalizi wa karibu na baadaye msamaria mwema aliamua kujitokeza na kuamua kumkumbati mtoto huyo aweze kupata joto la mama.
Mtoto huyo alizaliwa tarehe 13 Machi, 2025 na tarehe 26 Desemba, 2025 alipokea sakramenti ya ubatizo katika Kanisa Katoliki lililopo Msimbazi Centre na kupatiwa jina la Perpetua Amana.

Mtoto huyo aliendelea kulelewa hospitali hapo kwa takribani miezi kumi na moja na afya yake iliimarika vizuri na baadaye uongozi uliamua kumpeleka katika kituo cha kulelea Watoto Msimbazi Centre kwaajili ya uangalizi zaidi, tarehe 14 Februari, 2026 aliugua ghafla na kukimbizwa hospitali ya Amana ambapo wataalam walijitahidi kumpatia matibabu lakini tarehe 15 Februari, 2026 mtoto huyo alifariki dunia.

Perpetua Amana amezikwa tarehe 17 Februari, 2026 katika viwanja vya Makaburi ya Msimbazi Centre Jijini Dar es Salaam.



TANZIA 🕊️
16/02/2026

TANZIA 🕊️

HOSPITALI YA AMANA YAPOKEA MSAADA WA VIFAA TIBA VYENYE THAMANI YA TAKRIBANI  TZS.42 MIL KUTOKA SIGN FRACTURE CARE INTERN...
16/02/2026

HOSPITALI YA AMANA YAPOKEA MSAADA WA VIFAA TIBA VYENYE THAMANI YA TAKRIBANI TZS.42 MIL KUTOKA SIGN FRACTURE CARE INTERNATIONAL

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana imepokea msaada wa vifaa tiba vyenye thamani ya takribani TZS.42 Mil ambao unalenga kusaidia kuboresha huduma za afya kwa wagonjwa wa mifupa na ajali kutoka taasisi ya Sign Fracture Care International ya nchini Marekeni.

Akipokea msaada huo Daktari Bingwa Mwandamizi wa Magonjwa ya Mifupa na Ajali Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Nsajigwa Mwamwitwa ameishukuru taasisi hiyo na kusema kuwa msaada huo utasaidia *kuwadumia* wagonjwa wenye matatizo ya mifupa na waliopata ajali.

“Hospitali ya Amana ipo katikati ya jiji na inapokea wagonjwa wengi waliopata ajali mbalimbali hivyo vifaa hivi vitasaidia kuboresha huduma za afya kwa wagonjwa wanaofika hospitalini hapa”amesema Mwamwitwa.

Pamoja na hayo ameipongeza taasisi hiyo kwa kuunga mkono juhudi za serikali za kuboresha huduma za afya nchini na kuwataka wadau wengine kuendelea kujitokeza zaidi kwakuwa juhudi *za zitasaidia* katika kuhakikisha kuwa kila Mtanzania anayehitaji huduma za afya anapata huduma bora bila kikwazo chochote.

10/02/2026

@

WATUMISHI WA HOSPITALI YA AMANA WASHIRIKI KATIKA HAFLA YA KUMPOKEA NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA AFYA ANAYESHUGHULIKIA MAS...
09/02/2026

WATUMISHI WA HOSPITALI YA AMANA WASHIRIKI KATIKA HAFLA YA KUMPOKEA NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA AFYA ANAYESHUGHULIKIA MASUALA YA DAWA NA VIFAA TIBA

Watumishi wa Hospitali ya Rufaa Mkoa Amana wameshiriki katika hafla fupi ya kumpokea na kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Bw. Emmanuel Tayari mara baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kushika nafasi hiyo.

Hafla hiyo imefanyika leo tarehe 9 Februari, 2026 katika katika Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) jijini Dar Es Salaam.

Leo tarehe 4 Februari, 2026, Tanzania inaungana na mataifa mengine duniani kuadhimisha Siku ya Saratani Duniani, siku mu...
04/02/2026

Leo tarehe 4 Februari, 2026, Tanzania inaungana na mataifa mengine duniani kuadhimisha Siku ya Saratani Duniani, siku muhimu ya kuongeza uelewa kwa jamii kuhusu ugonjwa wa saratani, kuhimiza kinga, uchunguzi wa mapema na upatikanaji wa matibabu kwa wote.

Maadhimisho haya yanawakumbusha wananchi kuwa saratani inaweza kuzuilika, kutibika endapo itagundulika mapema, na kwamba kila mmoja ana wajibu wa kuchukua hatua ikiwemo kubadili mtindo wa maisha.

Address

Ilala
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Amana Hospital Ilala posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Amana Hospital Ilala:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram