Amana Hospital Ilala

Amana Hospital Ilala Amana Hospital take your health in safe place

Heri ya kumbumbuku ya Mapinduzi ya Zanzibar Hospital ya Rufaa ya Mkoa Amana tunaungana na Watanzania wote kuadhimiwha si...
12/01/2026

Heri ya kumbumbuku ya Mapinduzi ya Zanzibar
Hospital ya Rufaa ya Mkoa Amana tunaungana na Watanzania wote kuadhimiwha siku hii

π—›π—’π—¦π—£π—œπ—§π—”π—Ÿπ—œ 𝗬𝗔 π—₯𝗨𝗙𝗔𝗔 𝗬𝗔 π— π—žπ—’π—” 𝗔𝗠𝗔𝗑𝗔 π—¬π—”π—œπ—¦π—›π—¨π—žπ—¨π—₯𝗨 π—¦π—›π—œπ—₯π—œπ—žπ—” π—Ÿπ—” π— π—”π——π—”π—žπ—§π—”π—₯π—œ π—ͺπ—”π—¦π—œπ—’ 𝗑𝗔 π— π—œπ—£π—”π—žπ—” π—žπ—ͺ𝗔 π—žπ—¨π—¦π—”π—œπ——π—œπ—” π—žπ—¨π—•π—’π—₯π—˜π—¦π—›π—” 𝗛𝗨𝗗𝗨𝗠𝗔 𝗭𝗔 π— π—”π—šπ—’π—‘π—...
09/01/2026

π—›π—’π—¦π—£π—œπ—§π—”π—Ÿπ—œ 𝗬𝗔 π—₯𝗨𝗙𝗔𝗔 𝗬𝗔 π— π—žπ—’π—” 𝗔𝗠𝗔𝗑𝗔 π—¬π—”π—œπ—¦π—›π—¨π—žπ—¨π—₯𝗨 π—¦π—›π—œπ—₯π—œπ—žπ—” π—Ÿπ—” π— π—”π——π—”π—žπ—§π—”π—₯π—œ π—ͺπ—”π—¦π—œπ—’ 𝗑𝗔 π— π—œπ—£π—”π—žπ—” π—žπ—ͺ𝗔 π—žπ—¨π—¦π—”π—œπ——π—œπ—” π—žπ—¨π—•π—’π—₯π—˜π—¦π—›π—” 𝗛𝗨𝗗𝗨𝗠𝗔 𝗭𝗔 π— π—”π—šπ—’π—‘π—π—ͺ𝗔 𝗬𝗔 𝗗𝗛𝗔π—₯𝗨π—₯𝗔 π—žπ—ͺ𝗔 π—ͺπ—”π—‘π—”π—‘π—–π—›π—œ

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana imeishukuru Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) kwa kusaidia uboreshaji wa utoaji wa huduma za magonjwa ya dharura na ajali hospitalini hapo.

Pongezi hizo zimetolewa na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Bryceson Kiwelu alipokuwa akikabidhi cheti cha shukrani kwa Mkuu wa Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka nchi Tanzania Bw.Tommaso Santo ikiwa ni ishara ya kuthamini mchango mkubwa walioutoa kwa kipindi chote walichokuwa hospitalini hapo.

Dkt. Kiwelu ameeleza kuwa shirika hilo limekuwa na mchango mkubwa kwa hospitali hiyo ambapo hivi karibuni ilitoa msaada wa gari la kubebe wagonjwa, vifaa tiba pamoja na kuwaleta baadhi ya wataalam wa afya wakiwemo Madaktari Bingwa wa Magonjwa ya Dharura, Wauguzi na Madereva ambao wamesaidia kuongeza nguvu kazi ya utoaji wa huduma za dharura hospitalini hapo.

β€œLeo Hospitali ya Amana inahitimisha ushirikiano baina ya Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka, ushirikiano huu umekuwa na manufaa makubwa sana katika kusaidia kuokoa maisha ya wananchi, shirika hili limetujengea uwezo wa namna ya kujiandaa na kukabiliana na magonjwa ya dharura na mlipuko punde yanapotokea” amesema Dkt. Kiwelu

Aidha, ameongeza kuwa kwa sasa Idara ya Magonjwa ya dharura katika hospitali hiyo imejitosheleza katika nyanja zote na iko tayari kufungua milango kwa hospitali yoyote ambayo iko tayari kuja kujifunza kwa kuwa kuna wataalam wabobezi wenye uzoefu wa kutoa huduma za dharura kuanzia eneo la tukio hadi mgonjwa anapofikishwa hospitali.

Asia Saidi Saidi, mkazi wa Mtongani jijini Dar es Salaam, ameishukuru Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana kwa huduma bora a...
02/01/2026

Asia Saidi Saidi, mkazi wa Mtongani jijini Dar es Salaam, ameishukuru Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana kwa huduma bora aliyopata wakati wa kujifungua watoto wake mapacha watatu siku ya sikukuu ya mwaka mpya.

Bi Asia amesema kuwa tangu alipofika hospitalini hapo alipokelewa kwa upendo, uangalizi wa karibu na huduma za kitaalamu kutoka kwa madaktari na wauguzi, hali iliyompa faraja na matumaini katika kipindi kigumu cha kujifungua.

Aisha, ameongeza kuwa kujifungua mapacha watatu si jambo rahisi, lakini kwa msaada wa wataalamu wa afya wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana, alijifungua salama yeye pamoja na watoto wake. Asia amepongeza juhudi za madaktari kwa kufuatilia afya yake na ya watoto tangu ujauzito hadi kujifungua, akisisitiza kuwa walikuwa makini, wavumilivu na wenye moyo wa kujali wagonjwa.

Kwa furaha na shukrani, Asia Saidi Saidi ametoa wito kwa kina mama wengine wajawazito kutumia huduma za Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana, akisema ni hospitali yenye vifaa vya kisasa na wataalamu wenye uwezo mkubwa. Ameeleza kuwa tukio lake ni ushuhuda wa namna hospitali hiyo inavyoendelea kutoa huduma bora za afya na kuokoa maisha ya mama na mtoto.

Tunawatakia heri ya mwaka mpya wa 2026
01/01/2026

Tunawatakia heri ya mwaka mpya wa 2026

Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana wamepatiwa mafunzo maalum kuhusu mbinu za kuzuia na kudhibiti maambukizi y...
30/12/2025

Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana wamepatiwa mafunzo maalum kuhusu mbinu za kuzuia na kudhibiti maambukizi ya magonjwa ya mlipuko katika maeneo yao ya kazi. Mafunzo hayo yalilenga kuwaongezea uelewa na ujuzi wa vitendo watumishi ili kuhakikisha usalama wa wagonjwa, wahudumu wa afya pamoja na jamii kwa ujumla, hususan wakati wa utoaji wa huduma za afya.

Usalama barabarani
29/12/2025

Usalama barabarani

Mtoto Perpetua Amana aliyetelekezwa akiwa na uzito pungufu na ulemavu wa mikono amepokea sakramenti ya ubatizo katika Ka...
26/12/2025

Mtoto Perpetua Amana aliyetelekezwa akiwa na uzito pungufu na ulemavu wa mikono amepokea sakramenti ya ubatizo katika Kanisa Katoliki lililopo Msimbazi Centre, ambapo ibada hiyo ilihudhuriwa na madaktari, wauguzi na watumishi wengine wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana pamoja na waumini wa kanisa hilo.

Ubatizo huo uliendeshwa kwa utaratibu wa kanisa, ukiwa ni ishara ya imani, matumaini na baraka kwa maisha ya mtoto huyo.

Aidha, watumishi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana wakieleza shukrani zao kwa Mungu pamoja na wadau wote wanaoendelea kumuunga mkono mtoto huyo katika safari yake ya maisha.

Tunawatakia Krisimasi njema
25/12/2025

Tunawatakia Krisimasi njema

Tunakutakia maandalizi mema ya Christmas 🎁
22/12/2025

Tunakutakia maandalizi mema ya Christmas 🎁

20/12/2025
Huduma Bora kwa wateja ndio nguzo yetu
20/12/2025

Huduma Bora kwa wateja ndio nguzo yetu

Address

Ilala
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Amana Hospital Ilala posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Amana Hospital Ilala:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram