Amana Hospital Ilala

Amana Hospital Ilala Amana Hospital take your health in safe place

  ya kisukari Duniani
14/11/2025

ya kisukari Duniani

13/11/2025

DKT. KIWELU AKIONGEA NA MKUU WA WILAYA KWENYE HHUDUMA ZA AFYA ZA KGA NA KOFIH DODOMAMganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufa...
13/11/2025

DKT. KIWELU AKIONGEA NA MKUU WA WILAYA KWENYE HHUDUMA ZA AFYA ZA KGA NA KOFIH DODOMA

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana, Dkt. Bryceson Kiwelu, ambae ni rais wa Korea Global Alumni KGA akizungumza naa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma katika huduma za magonjwa yasiyoambukiza zilizoendeshwa na Korea Global Alumni (KGA) kwa ufadhili wa Korea Foundation for International Healthcare (KOFIH).

Huduma hizo maalum zinaendele kufanyika jijini Dodoma, zikiwa na lengo la kutoa uchunguzi, ushauri na matibabu ya magonjwa yasiyoambukiza k**a vile kisukari, shinikizo la damu, saratani na matatizo ya moyo.

Zoezi hilo linaendelea kufanyika katika viwanja vya Nyerere Square na limevutia mamia ya wananchi waliokuwa na hamasa kubwa ya kupata huduma bure kutoka kwa wataalamu wa afya kutoka hospitali mbalimbali nchini.

Akizungumza wakati wa tukio hilo, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana, Dkt. Bryceson Kiwelu, alisema KGA Tanzania Chapter imeendelea kuwa mstari wa mbele katika kuchochea maendeleo ya afya nchini kupitia programu za kijamii na ushirikiano wa kimataifa unaolenga kuinua ustawi wa jamii.

Aidha amesisitiza umuhimu wa wananchi kujenga utamaduni wa kupima afya zao mara kwa mara ili kuepuka madhara makubwa yanayotokana na magonjwa yasiyoambukiza.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma aliipongeza KGA na wadau wote walioshiriki katika zoezi hilo kwa mchango wao mkubwa katika kuboresha huduma za afya kwa Watanzania. Alibainisha kuwa jitihada k**a hizi zinaunga mkono malengo ya serikali ya kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma bora za afya bila vikwazo vya kifedha.

Korea Global Alumni (KGA) Tanzania Chapter, chini ya uongozi wa Dkt. Kiwelu, imekuwa ikitekeleza miradi mbalimbali ya kijamii ikiwemo utoaji wa elimu ya afya, kampeni za upimaji bure na programu za mafunzo kwa wataalamu wa afya. Kupitia ufadhili wa KOFIH, KGA imepania kuendelea kuleta mabadiliko chanya katika sekta ya afya nchini Tanzania.

MGANGA MFAWIDHI HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA ASHIRIKI KAMPENI ZA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA YALIYORATIBIWA NA KGA JIJIN...
12/11/2025

MGANGA MFAWIDHI HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA ASHIRIKI KAMPENI ZA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA YALIYORATIBIWA NA KGA JIJINI DODOMA

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Amana, Dkt. Bryceson Kiwelu, ameshiriki katika maadhimisho ya Wiki ya Magonjwa Yasiyoambukiza yanayoendelea kufanyika jijini Dodoma, ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kitaifa ya kuhamasisha wananchi kujali afya zao na kujikinga na magonjwa hayo.

Katika maadhimisho hayo, KGA Tanzania Chapter imeendesha huduma ya bure ya upimaji wa magonjwa yasiyoambukiza katika viwanja vya Nyerere Square, ikiwemo uchunguzi wa shinikizo la damu, kisukari, uzito na ushauri wa lishe bora kwa wananchi wa Dodoma na maeneo jirani.

Zoezi hilo la utoaji huduma za huruma limeandaliwa na KGA Tanzania Chapter kwa ushirikiano na Ofisi ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, likiwa na lengo la kuongeza uelewa kuhusu hatari na namna ya kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza kupitia mtindo bora wa maisha na uchunguzi wa mara kwa mara.

Dkt. Kiwelu amepongeza juhudi hizo akisisitiza kuwa elimu na uchunguzi wa mapema ni nguzo muhimu katika kupunguza vifo na athari zitokanazo na magonjwa yasiyoambukiza, huku akitoa wito kwa jamii kujenga mazoea ya kupima afya mara kwa mara na kufanya mazoezi ili kudumisha afya bora.

Hongera
12/11/2025

Hongera

Wiki ya magonjwa yasiyoyakuambykiza
10/11/2025

Wiki ya magonjwa yasiyoyakuambykiza

Huduma kwa wateja
10/11/2025

Huduma kwa wateja

Kila pumzi yao ni ishara ya ushindi
10/11/2025

Kila pumzi yao ni ishara ya ushindi

Hudhuria kliniki ya Macho kuanzia jumatatu hadi ijumaa saa 2:00 - 8:00 mchana
09/11/2025

Hudhuria kliniki ya Macho kuanzia jumatatu hadi ijumaa saa 2:00 - 8:00 mchana

08/11/2025
MADAKTARI TARAJALI HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA WATAKIWA KUJITUMA NA KUZINGATIA MAADILI YA TAALUMA YAOMadaktari tara...
07/11/2025

MADAKTARI TARAJALI HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA AMANA WATAKIWA KUJITUMA NA KUZINGATIA MAADILI YA TAALUMA YAO

Madaktari tarajali Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana wametakiwa kujituma na kufanya kazi kwa weledi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, na Maadili ya taaluma yao ili kutimiza azma ya hospitali hiyo ya kutoa huduma bora nchini.

Wito huo umetolewa na Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt. Jumanne Mafele wakati akifungua mafunzo ya elekezi kwa madaktari tarajali 36 ambapo ameeleza kuwa hospitali ya Amana ni miongoni mwa hospitali za rufaa zinazoongoza kwa kutoa huduma bora hivyo ujio wa madaktari hao utaenda kuwa chahu katika kuendelea kuboresha huduma utoaji wa huduma za afya hospitalini hapo.

" Kuwa daktari si kazi tu ni wito wa moyo na uaminifu mkubwa, nawasihi mkafanye kazi kwa uaminifu, mtunze siri za wagonjwa na mkawahudumie wateja kwa upendo ”amesema Dkt. Mafele

Pamoja na hayo amewahimiza madaktari hao kutumia fursa hiyo k**a daraja la kujifunza kutoka kwa wataalamu waliobobea, huku akisisitiza umuhimu wa kushirikiana na timu nzima ya afya kwa lengo la kuboresha huduma kwa wananchi.

Follow us on social media platforms
07/11/2025

Follow us on social media platforms

Address

Ilala
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Amana Hospital Ilala posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Amana Hospital Ilala:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram