13/11/2025
DKT. KIWELU AKIONGEA NA MKUU WA WILAYA KWENYE HHUDUMA ZA AFYA ZA KGA NA KOFIH DODOMA
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana, Dkt. Bryceson Kiwelu, ambae ni rais wa Korea Global Alumni KGA akizungumza naa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma katika huduma za magonjwa yasiyoambukiza zilizoendeshwa na Korea Global Alumni (KGA) kwa ufadhili wa Korea Foundation for International Healthcare (KOFIH).
Huduma hizo maalum zinaendele kufanyika jijini Dodoma, zikiwa na lengo la kutoa uchunguzi, ushauri na matibabu ya magonjwa yasiyoambukiza k**a vile kisukari, shinikizo la damu, saratani na matatizo ya moyo.
Zoezi hilo linaendelea kufanyika katika viwanja vya Nyerere Square na limevutia mamia ya wananchi waliokuwa na hamasa kubwa ya kupata huduma bure kutoka kwa wataalamu wa afya kutoka hospitali mbalimbali nchini.
Akizungumza wakati wa tukio hilo, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana, Dkt. Bryceson Kiwelu, alisema KGA Tanzania Chapter imeendelea kuwa mstari wa mbele katika kuchochea maendeleo ya afya nchini kupitia programu za kijamii na ushirikiano wa kimataifa unaolenga kuinua ustawi wa jamii.
Aidha amesisitiza umuhimu wa wananchi kujenga utamaduni wa kupima afya zao mara kwa mara ili kuepuka madhara makubwa yanayotokana na magonjwa yasiyoambukiza.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma aliipongeza KGA na wadau wote walioshiriki katika zoezi hilo kwa mchango wao mkubwa katika kuboresha huduma za afya kwa Watanzania. Alibainisha kuwa jitihada k**a hizi zinaunga mkono malengo ya serikali ya kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma bora za afya bila vikwazo vya kifedha.
Korea Global Alumni (KGA) Tanzania Chapter, chini ya uongozi wa Dkt. Kiwelu, imekuwa ikitekeleza miradi mbalimbali ya kijamii ikiwemo utoaji wa elimu ya afya, kampeni za upimaji bure na programu za mafunzo kwa wataalamu wa afya. Kupitia ufadhili wa KOFIH, KGA imepania kuendelea kuleta mabadiliko chanya katika sekta ya afya nchini Tanzania.