Herbal Impact

Herbal Impact Research on various natural products with therapeutic value, creation of medicinal natural products formulations, and health and wellness training & coach

Herbal Impact was founded in 2007 by Juma Killaghai as a vehicle for exploiting nature’s treasure, especially in the area of phytochemicals. Juma Killaghai is an organic natural products research chemist based in Dar es Salaam. The firm he founded is the maker of HAIIBA brand. The brand comprises natural medicinal products that includes:

1. Haaiba Dental Guard;
2. Haiiba IG;
3. Haiiba Skin Guard

;
4. Haiiba GlucoMaster; and
5. Haiiba Timamu Tea. Haiiba Dental Guard:

This is a highly potent mouth wash. It kills millions of germs, especially gram positive bacteria, on contact. The product is known for its ability to permanently cure severe tooth aches within 15 minutes of using;

Haiiba IG:

This is a very potent anti HIV product. The product can reduce the viral load in HIV infected people by millions of HIV copies within six (6) months of use;

Haiiba Skin Guard:

This is highly effective for a variety of skin infections, including fungi;

Haiiba GlucoMaster:

This product is good for diebetics in the sense that it helps to reduce insuline resistance, and corrects damage caused by prolonged elevated blood sugar such as nerve damage, weakened libido, etc. ; and

Haiiba Timamu Tea:

This tea is very powerful body tonic. It is a great help for people with certain medical conditions including the following:

1. Chronic inflammation;
2. Muscle and joint pains;
3. Chronic fatigue;
4. Gaut;
5. Arithrites;
6. Indigestion;
7. Catarracts;
8. Slow metabolism;
9. Skin disorders;
10. Fast aging;
11. Compromised immunities;
12. Cancer disposition;
13. Multiplesclerosis;
14. Elevated Cholesterol;
15. Nerve damage;
16. High Blood Pressure;
17. Liver disfunction;
18. Malignant Tumors;
19. Heart Disease; and
20. Migranes. With more research and experience to back it up, the firm in 2012 redefined its mission to include provision of health and wellness education as its core activity. The change was brought about by mounting evidence that shows that for the most part people fall ill simply because they lack the right kind of health information.

18/12/2024
Want to make a great first impression? Discover our professional resume template! It’s designed to highlight your streng...
13/12/2024

Want to make a great first impression?

Discover our professional resume template! It’s designed to highlight your strengths and achievements. Perfect for job seekers at any level! Visit here: https://payhip.com/b/ENqvl

This professional resume template has a sleek, modern design. It's made to showcase your skills, experience, and achievements. You can customize it to fit your needs, making your qualifications stand out.It's ideal for those looking to make...

Maumivu ya Jino yanaweza kuwa Jinamizi baya!Maumivu yanaweza kuwa makali hadi ukahisi kuwa uko jahanam. Kutana na Haiiba...
05/12/2024

Maumivu ya Jino yanaweza kuwa Jinamizi baya!

Maumivu yanaweza kuwa makali hadi ukahisi kuwa uko jahanam. Kutana na Haiiba Dental Guard; kitakasa kinywa chenye uwezo wa kuua mamilioni ya bakteria aina ya Gram positive kwa mguso tu, ambao ndiyo hupelekea maradhi ya meno na fizi.

Agana kabisa na maumivu ya meno ndani ya dakika 15 -20 baada ya kutumia Haiiba Dental Guard. Haiiba Dental Guard pia hutoa ulinzi wa muda mrefu.

Agiza sasa! Simu/whatsApp 0754281131/0655281131

AU

Tembelea HERBAL IMPACT: Mosque street, Kitumbini, Dar es Salaam (makabala na msikiti wa Sunni Muslim Jamaat)

A tooth Ache is Really Scary!The pain is so intense it turns your life into hell. Meet Haiiba Dental Guard, an oral disi...
05/12/2024

A tooth Ache is Really Scary!

The pain is so intense it turns your life into hell. Meet Haiiba Dental Guard, an oral disinfectant that permanently eliminates toothache within 15 to 20 minutes. Get it now!

Order here: https://payhip.com/b/hxvAR

ILI KUIMARISHA SIHA NA AFYA: PAISHA KINGA ZAKO ZA MWILITumezungukwa na vitu vingi vyenye uwezo wa kudhuru na kuathiri af...
04/12/2024

ILI KUIMARISHA SIHA NA AFYA: PAISHA KINGA ZAKO ZA MWILI

Tumezungukwa na vitu vingi vyenye uwezo wa kudhuru na kuathiri afya zetu.

Vitu hivi ni pamoja na vimelea mbalimbali vya maradhi k**a vile bakteria, kuvu, virusi, minyoo, nakadhalika; na sumu mbalimbali kutoka kwenye lishe na mazingira.

Mfumo wa Kinga za mwili

Muumba wetu ametujaalia ulinzi kupitia kile kinachoitwa mfumo wa kinga mwilini.

Bila huu mfumo huenda maisha yetu yangeishia muda mfupi tu baada ya kuzaliwa, au tusingezaliwa kabisa.

Ili tuendelee kuishi na kudumu katika hali ya siha na afya njema, tunapaswa kuchukua hatua za makusudi za kuuenzi huu mfumo na kuhakikisha kuwa siku zote unafanya kazi kwa ufanisi wa hali ya juu.

Hatua za kuchukua ni pamoja na:
1. Kula lishe sahihi;
2. Kupata usingizi wa kutosha;
3. Kukabiliana kikamilifu na msongo wa mawazo;
4. Kuhakikisha kuwa mwili una maji ya kutosha kila wakati;
5. Kupata mwanga wa jua wa kutosha kila siku;
6. Kuushughulisha mwili kila siku na kila wakati (kutobweteka);
7. Kuondosha sumu mwilini zinazotokana na uvunjifu na ujenzi wa kemikali ndani ya mwili, na zile zinazoingia mwilini kupitia chakula, vinjwaji, na muingiliano na mazingira; na
8. Kuchukua hatua za kukarabati seli chakavu.

Haiiba Timam Tea

Moja ya njia bora sana za kuondosha sumu ndani ya mwili (detoxing) na kukarabati seli zilizochakaa ni matumizi ya chai ya ajabu inayoitwa Haiiba Timam Tea.

Chai hii ambayo imesheni viini lishe vingi tofauti, ina uwezo mkubwa wa kuondosha sumu zinazolundikana kwenye ini na katika tishu nyingine mbalimbali za mwili.

Aidha, chai hii kupitia kuwa na mkusanyiko mkubwa wa vijenzi vya protini (amino acids) na kiasi kikubwa cha vizuia vioksidishaji (antioxidants), ina uwezo mkubwa sana wa kukarabati seli za mwili zilizoharibika.

Kuondoa sumu na kukarabati seli kunasaidia sana kuimarisha uwezo wa kinga za mwili.

Kudhihirisha uwezo wa Haiiba Timam Tea katika jukumu hili wako wagonjwa wa UKIMWI waliokuwa wamezidiwa na kulala kabisa lakini leo wanatembea, na wanaendelea na shughuli zao baada ya kutumia Haiiba Timam Tea kwa majuma machache.

Aidha, watumiaji wengi wanadai kuwa baada ya kuanza kutumia chai hii sasa hawaugui tena ugonjwa wa malaria, tofauti na ilivyokuwa huko nyuma.

Je ungependa kuijaribu chai hii?

Tupigie/whatsApp 0754281131/0655281131

AU

Tutembelee: mtaa wa Mosque, Kitumbini, Dar es Salaam (mkabala na msikiti wa Sunni)

TIBA YA MAAMBUKIZI KWENYE SIKIOK**a umepata maambukizi ya sikio yanayopelekea mwasho mkali, maumivu na kutoa usaha au ha...
02/12/2024

TIBA YA MAAMBUKIZI KWENYE SIKIO

K**a umepata maambukizi ya sikio yanayopelekea mwasho mkali, maumivu na kutoa usaha au harufu kali, tiba ni hapa!

Bofya kiungo (link) ifuatayo kujifunza tiba hii bure kabisa:

Kuna maambukizi mengi yanayoweza kulikabili sikio lako. Maambukizi mengi yanahusisha bakteria au fangasi.

TUMIA HAIIBA IG GEL KUAGANA KABISA NA VIDONDA VYA TUMBO K**a una vidonda vya tumbo huna haja ya kuambiwa adha yake. Maum...
30/10/2024

TUMIA HAIIBA IG GEL KUAGANA KABISA NA VIDONDA VYA TUMBO

K**a una vidonda vya tumbo huna haja ya kuambiwa adha yake. Maumivu huwa ni makali, tena makali sana wakati mwingine!

Kwa wale ambao hawana bahati, kiwambo cha mfuko wa tumbo hufikia kutoboka.

Hali ikifikia hapo siyo tu kwamba maumivu yanakuwa makali mno, bali pia yanaambatana na kutapika kiasi kikubwa cha damu pale mtu anapokabiliwa na shambulizi.

JIPONESHE LEO!

Uwezekano wa kutibu vidonda vyako vya tumbo hadi vikapona kabisa upo.

Inawezekana hilo lilikuwa bado halijakutokea kwa sababu ulikuwa hujakutana na tiba sahihi.

K**a unasoma makala hii fupi, mshukuru Mungu na ujipongeze pia.

Kwa nini? Kwa sababu makala hii fupi ni ya kuitambulisha tiba yenye nguvu inayoitwa HAIIBA IG GEL.

Tiba hii imewaponya wengi vidonda vya tumbo pamoja na magonjwa mengine mengi.

Miongoni mwa magonjwa hayo ni k**a:

1. Bawasir (Hemorhoids);
2. UTI sugu;
3. Muwasho mkali huko kikeni (Va**na Candida Infection);
4. Homa ya mapafu (Pneumonia);
5. Maambukizi katika njia ya hewa;
6. Muwasho wa ngozi kutokana na mizio (Allergies);
7. Vijiwe vya mfuko wa nyongo na figo; na
8. Maumivu ya misuli, kani na mifupa.

HAIIBA IG GEL pia ni adui mkubwa wa virusi na kwa maana hiyo pia ni tiba nzuri kwa wenye virusi vya ukimwi na vile vya homa ya ini.

K**a unaamini kwamba unaweza kunufaika na tiba hii mujarabu sana basi usisite kuwasiliana nasi.

Simu/WhatsApp 0754281131/0655281131

Misukosuko - Sura ya NneKilikuwa kipindi cha saba, somo la Jiografia. Mwalimu alikuwa hajaingia darasani na watoto wenza...
28/10/2024

Misukosuko - Sura ya Nne

Kilikuwa kipindi cha saba, somo la Jiografia. Mwalimu alikuwa hajaingia darasani na watoto wenzangu wote walipiga makelele. Sikuwa nina tabia ya kupiga makelele darasani; nilikuwa mtulivu, akili safi kwa upande wa masomo na siyo mwoga.

Tabia zangu mbili za mwanzo zilijionyesha kwa kila mtu, ile ya kutokuwa mwoga nahisi mpaka wakati huo ni mimi mwenyewe niliyekuwa nikiifahamu. Si jambo la kawaida kwa mwanafunzi wa darasa la nne ku*ifahamu tabia alizo nazo, lakini mimi nilizifahamu za kwangu. Hivyo ndivyo ilivyokuwa.

Kutokana na tabia zangu hizo zilizojitokeza, nilipendwa sana na walimu kwa upande mmoja na kwa upande mwingine watoto wenzangu hawakuisha kunipa misukosuko.

Ni kipindi hiki cha saba, somo la Jiografia wakati mwalimu hajaingia, wakati misukosuko niipatayo kwa hawa wanafunzi wenzangu iliponizukia tena. K**a kawaida nilikuwa nimekaa kimya. Watoto wenzangu waliokuwa wakipiga makelele na kukimbia kimbia huku na huko darasani ghafla waliacha makelele wakawa wananiangalia na kucheka. Sikuwajali kwanza. Waliendelea kucheka mpaka nikakerwa, nikaanza kujikagua kagua kutaka kujua kisa cha hivyo vicheko. Tendo langu la kujiangalia angalia liliwamaliza wenzangu mbavu, walicheka mpaka wengine wakawa wanatoa machozi. Sikuona dosari yeyote niliyokuwa nayo, hivyo niliamua nijikalie kimya. Vicheko viliendelea.

Ghafla Yakobo aliyekuwa mlangoni alitoa tahadhari kuwa mwalimu wa Jiografia alikuwa anakuja na wabaya wangu wote walikimbilia kwenye nafasi zao na kukaa kimya! Mwalimu aliingia akaanza kufundisha na kila mmoja pamoja na mimi alisahau vicheko vya muda mfupi uliopita.

Katikati ya somo, mwalimu alinitoa mbele nikaonyeshe kitu fulani kwenye ramani aliyokuwa amechora ubaoni. Nusu ya njia kabla sijafika ubaoni miguno ya hapa na pale ilianza kusikika, halafu ghafla darasa zima likaangua kicheko. Mwalimu alishtuka, akauliza kilichokuwa kinawachekesha. Badala ya kupata jibu kicheko kilizidi.

Mwalimu akiwa amekasirika alichukua fimbo toka mezani akatoa amri wanafunzi wanyamaze. Darasa likawa kimya. Alimnyooshea Joakim aliyekuwa akikaa deski la mbele kidole.

“Simama wewe!”

Joakim alisimama.

“Nieleze mnachocheka.”

Joakim alibaki kimya.

“Kwa mara ya mwisho! Unacheka nini?” Alifoka mwalimu akipepea pepea fimbo yake.

“Eeh…..ni…..ni Jakob, Mwalimu. Amevaa kijikaratasi kimening’inia k**a mkia nyuma.”

Jibu la Joakim, lilileta kicheko kipya darasani. Mwalimu alinigeukia kwa ghadhabu pale nilipokuwa nimesimama. Alinitazama akakiona hicho kikaratasi kilichokuwa kimefungwa kwa u*i na kuning’inia nyuma yangu, akakinyofoa na kukisoma kimya kimya. Alinikabidhi mimi hicho kikaratasi nami nilipata fursa ya kusoma hayo yaliyoandikwa. Kiliandikwa kwa herufi kubwa hivi. MIMI JAKOB NI MJINGA SANA. MBALI YA KUTOA MAKAMASI HOVYO, NAKOJOA KITANDANI!!!

Fuata kiungo (link) kifuatacho kuendelea kusoma hadithi hii ya kusisimua....
https://wellbizsolutions.org/blog/f/misukosuko---sura-ya-nne

Understanding Stress and Its Impact on HealthAs a professional, you are likely familiar with stress. For executives, the...
27/10/2024

Understanding Stress and Its Impact on Health

As a professional, you are likely familiar with stress. For executives, the pressure to make the right decisions, meet deadlines, and motivate teams can be overwhelming. For employees, the constant demands from higher-ups and the drive to achieve performance objectives create a similar environment of stress. This cycle is often exacerbated by the desire to climb the corporate ladder and secure pay raises.

With our workdays stretching to 8 hours a day, 5 days a week for 48 weeks a year, it’s no surprise that many of us carry a heavy burden of stress, leading to high blood pressure.

When faced with this reality, many people find themselves relying on daily medication to manage their blood pressure. While these pills can be life-saving, isn't there a better way to address the root cause?

The answer is stress management. Learning to control and reduce stress can be a more sustainable solution for your health.

If you're unsure how to begin, I recommend checking out "The Nuts and Bolts of Stress Management and Mindful Cultivation," available for free at this link: https://wellbiz2023.gumroad.com/l/axrvnf

Misukosuko - Sura ya TatuSIKUWEPO: NIMEHADITHIWATofauti na watoto wengine wengi mimi sijapata kufaidi hata chembe ya uta...
26/10/2024

Misukosuko - Sura ya Tatu

SIKUWEPO: NIMEHADITHIWA

Tofauti na watoto wengine wengi mimi sijapata kufaidi hata chembe ya utamu wa kuishi na wazazi; yaani baba na mama. Nimehadithiwa kwa kifupi na mjomba Joseph kwamba Leah, yaani mama yangu alifariki wakati akinizaa mimi. Baba yangu ambaye nadhani bado yuko hai, baba wa haramu kwa kuwa hakuwa mume wa ndoa wa mama yangu – Mungu amlaani!, anaitwa John Lengia.

Baba huyu ni afisa wa ngazi ya juu serikalini, kwa maneno mengine anakula nchi. Huyu baba nimewahi kuonana naye siku moja na Mungu anijalie nisionane naye tena! Kuonana kwetu kumeniacha na mashaka mpaka leo hii. Kweli John Lengia ndiye baba yangu?
Hivyo sijawahi kufaidi utamu wa wazazi. Maisha yangu yote nimeishi katika hali ambayo si ya kujivunia hata! Utafahamu ni kwa nini kadri utakavyozidi kupitia mfululizo wa maisha yangu machanga lakini yaliyooza!

KISA CHA LEAH

Leah kwa moyo mkuu alijitahidi asilie tena. Alifahamu kwamba k**a ni kulia ameshalia sana na ataendelea kulia sana atakapofika nyumbani, si kwa kupenda ila kwa kulazimika. Ataachaje kulia naye alifahamu kwamba asingepata hata chembe ya utu toka kwa mzee Onesmo, baba yake, pindi atakaposikia kisa kilichomfuku*isha binti yake shule?

Wakati Leah anajitayarisha kuondoka na kurudi nyumbani, alimkumbuka mtu aliyemsababishia matatizo yote hayo. John Lengia. Alikumbuka kuwa baada ya ahadi za kufa na kupona toka kwa John, zilizomlegeza na kumwachia auchezee mwili wake, alichoambulia ni mimba na kufukuzwa shule. John alikuwa ameikana mimba hiyo na kumtahadharisha ‘akome’ la sivyo! Alikuwa amediriki kumwita hata kinyango! Leah alikumbuka wazi wazi sentensi ya John aliyomweleza kwenye barua ya kumtahadharisha.

“Sikiliza binti, nafikiri umekosea. Umewezaje kufahamu jina na anuani yangu? Nafiri kuna mtu amekudanganya na kukupa jina na anuani yangu kwa makusudi. Mimi sikujui na wala sijapata kukuona. Mungu! Ukathubutu hata kuniletea picha ya kinyago unachodai ni wewe na kunishauri eti kwa kuwa una mimba tuoane! Usinichekeshe! Picha inarudi na barua hii. Angalia sana usifanye makosa siku nyingine na kutuma barua zako kwa watu wasio husika.”

Fuata kiungo (link) ifuatayo kuendelea kosoma hadithi hii ya kusisimua: https://wellbizsolutions.org/blog/f/misukosuko---sura-ya-tatu

Misukosuko – Sura ya PiliJAKOB MSAFIRINilizungusha macho yangu huku na kule, chumba cha mahak**a ilikokuwa ikisikilizwa ...
25/10/2024

Misukosuko – Sura ya Pili

JAKOB MSAFIRI

Nilizungusha macho yangu huku na kule, chumba cha mahak**a ilikokuwa ikisikilizwa kesi yangu kilikuwa kimejaa kiasi.
Kila macho yangu yalipotua yaliona watu ambao nilihisi ni walewale niliokuwa nikiwaona siku zote tangu kesi yangu ianze kusilikilizwa. Nilitabasamu kidogo baada ya fikra za ajabu kidogo kuniingia kichwani.

Je? Hawa watu walikuwa wamekosa la kufanya kiasi cha kupoteza muda wao na kuja kusikiliza kesi ya lofa k**a mimi? Huenda nao walikuwa wakitoka katika familia ile ile nilikotokea; familia ya wale tuishio kwa misukosuko tangu siku tunapouonja uso wa dunia. Misukosuko tuliyozaliwa tuishi nayo bila kujua sababu hasa!

Nilisikia miguno kadha toka kwa hawa wasikilizaji nami kwa juhudi kubwa niliyarudisha mawazo yangu kwa yule mtu aliyekuwa kavaa mavazi ya kijaji. Mtu ambaye muda si mrefu tokea sasa angeamua namna ambavyo ningekuwa baada ya hukumu yake.
Angeweza akanihukumu kifo! Sikuwa nikifahamu sheria, lakini nilikuwa na fununu kuwa kwa kosa nililohusiana nalo hukumu ya kifo ingeweza kutolewa. Angeweza akanihukumu kifungo cha maisha au vyovyote! Vyovyote iwavyo sikujali hata kidogo. Hapana, nilijali! Hukumu ya kifungo ilikuwa na maana ya kuendelea na maisha haya yasiyo na uhakika, maisha ya bahati nasibu. Ni afadhali hukumu ya kifo, ndiyo… Hukumu ya kifo.

Kwa kuwa mawazo yangu yalikuwa yakitembea huku na huko sikuwa nimesikia maelezo yaliyotangulia ya hukumu yangu. Wakati ndiyo kwanza nayaweka mawazo yangu katika hali ya usikivu, ghafla jaji alisita na kunikazia macho yake yaliyokuwa yamevishwa miwani.

“Msh*takiwa Jakob Msafiri, kabla sijatangaza hukumu una lolote la kusema?

Nilijiuliza k**a nilikuwa na lolote la kusema. Yaa, nilikuwa nalo.

“Asante sana Ndugu Mheshimiwa Jaji. Ndiyo ninalo la kusema. Naomba unipungu*ie adhabu Ndugu Mheshimiwa Jaji, kwa kunihukumu adhabu ya kifo. Nastahili kupungu*iwa adhabu kwani nakataa kutupiwa lawama yote ya kosa lililonifikisha hapa. Ni sehemu ndogo tu ya lawama hizo, k**a ipo basi! Ambayo naikubali, sehemu iliyobaki ni lazima imwendee mhalifu halisi. Na huyo mhalifu halisi ni nani? Ni HALI. Ni kosa la hali …………...

Nilinyamaza baada ya kugundua kuwa kote mahak**ani mle kumekuwa kimya kabisa, kila mtu ikiwa ni pamoja na Jaji mwenyewe na maafisa wengine wa mahak**a, wamedumaa wakinitumbulia macho.

Baada ya kimya cha ziada cha sekunde kadhaa Jaji alikohoa kidogo akasema:
“Bwana msh*takiwa sidhani k**a nimekuelewa. Hata hivyo ni matumaini yangu kwamba hukuwa na lengo la kuiletia mahak**a dhihaka…... k**a ilivyosikika katika maelezo yaliyotangulia ya hukumu, mahak**a imeridhika na maelezo yaliyotolewa na upande wa mash*taka na mahak**a hii inakutia hatiani kwa kosa la kuwa mwanachama wa genge hatari la kufanya biashara haramu mpakani, kosa la kushikwa na mali isiyothibitika kisheria na kosa la kuhusiana na mauaji yaliyotokea wakati wa kusafirisha mali hiyo....

Fuata kiungo (link) hiki kuendelea kusoma hadithi hii ya kusisimua: https://wellbizsolutions.org/blog/f/misukosuko--sura-ya-pili

MISUKOSUKOSURA YA KWANZAJakob Msafiri – kipande cha mwanaume, mrefu, mweusi na mkak**avu wa maungo, alisimama pembeni ki...
24/10/2024

MISUKOSUKO

SURA YA KWANZA

Jakob Msafiri – kipande cha mwanaume, mrefu, mweusi na mkak**avu wa maungo, alisimama pembeni kimya akiungalia mlolongo wa wafungwa wenzake, katika gereza la Ngathi, wakati wakienda kupokea chakula chao.

Jakob alikuwa na ada ya kuzungumza machache na kufikiri mengi. Ingawa amekuwa katika gereza hili si zaidi ya miezi kumi sasa, amepata sifa au cheo cha mfungwa wa pekee – mfungwa ambaye hakusita kutumia nguvu zake katika kuwafunza adabu wale wote alioona wanamletea upumbavu bila kujali matokeo ya tabia hiyo.

Aghalabu ni wafungwa wachache sana ambao hufikia kuwa na sifa aliyokuwa nayo Jakob sasa, kwani k**a hawakufa kabla hawajapata sifa hiyo, wengi wao, k**a askari jela wengi walivyokuwa wakisema kwa utani, “nguvu za soda huwaishia’, wakatubu na kufuata amri k**a gereza lilivyowataka.

Kwa Jakob ilikuwa kinyume. Miezi minne ya mwanzo gerezani aliipitia katika purukushani na adhabu za kila aina – adhabu ambazo zilikuwa zimebuniwa na uongozi wa gereza kwa madhumuni mawili. Moja, kumtoa mkaidi anayejidai ameshindikana kiburi alichonacho na kumfanya atubu, au mbili, kumuua yule anayejifanya ni mkaidi wa kupindukia lakini hana nguvu na afya ya kutosha kuhimili adhabu hizo. Hata hivyo ni wachache waliokufa kwani wengi walitubu haraka. Jakob hakutubu wala hakufa. Vyovyote ilivyokuwa athari ya adhabu hizo ilikuwa ni kuongezeka kwa kiburi na jeuri aliyokuwa nayo.

Huenda Jakob alikuwa na bahati kwamba adhabu na purukushani alizokuwa akizipitia zilikoma ghafla miezi minne kamili tangu aingie gerezani hapo. Ni vigumu kutabiri kile ambacho kingetokea iwapo muda ambao Jakob angepitia hizi purukushani na adhabu ungezidi hiyo miezi minne. Angeweza akatubu, akafa au hata akaendelea kudumu katika tabia yake hiyo bila kuathirika.

Siku ambayo Jakob alitimiza miezi minne kamili tangu aingie gerezani aliamua kutoamka asubuhi k**a ilivyokuwa ada kwa wafungwa kila asubuhi; tayari kwa kuhesabiwa na kwenda kwenye sulubu mbali mbali. Matokeo yake ni kwamba wakati wa kuhesabiwa alikosekana hivyo ikabidi atafutwe. Kikundi cha askari jela kilichoingia alikokuwa analala kiliudhika vibaya sana baada ya kumkuta humo akiwa ameamka anafanya mazoezi mepesi ya viungo.

Baadhi ya wale askari jela walitaka kumvamia lakini kiongozi wao, mzee mmoja ambaye alikuwa na uzoefu wa muda mrefu sana k**a askari jela, aliwazuia akanong’ona.

“Hakuna haja. Ni kweli mtamk**ata na huenda mtafanikiwa kumvunja mkono, mguu au hata shingo, lakini ninavyohisi ni kwamba hajali. Zaidi ya hapo mmoja wenu au hata wawili ataishia vilevile na kutokuwa na meno au jicho au vyovyote. Nawajua sana viumbe wa aina yake.”

Walibaki wakimwangalia Jakob kwa muda ambaye hakuonyesha dalili yoyote ya kuwajali, kisha yule mzee akapaaza sauti na kusema.

“Mfungwa Jakob, hutakiwi kuwapo humu saa hizi.”
“Nafahamu”
Alijibu Jakob akaendelea na mazoezi yake.

“Sasa k**a unafahamu, mbona uko humu?”
“Nimeamua tu”. Alijibu Jakob, ghafla akaacha mambo aliyokuwa anafanya na kuwageukia.

“Nyie mbwa. Naona mna bunduki, kwa nini mmoja wenu asiitumie yake?.” Aliuliza kwa dharau.

“Hivyo ndivyo unavyotaka?”

“Ni dhahiri. Kwani huoni? Hiyo ndiyo njia pekee ambayo itakupungu*ieni kazi.” Alijibu Jakob.

Yule mzee alimkazia jakob macho kwa muda akatikisa kichwa.
“Hatuna haja ya kujipungu*ia kazi. Zaidi ya hayo, k**a una hamu sana ya kufa, kwa nini usijitundike?. Siyo jambo geni unajua? Ni jambo linalotendeka mara nyingi gerezani.”

Jakob alicheka.
“Nijitundike? Siwezi kujitundika. Mimi sio mwoga kiasi hicho.”

“Sawa Jakob, tumeshakusikia maoni yako. Lakini hatuhitajiwi kuendelea na soga hapa. Unachotakiwa kufanya ni kutoka humu na kwenda kazini k**a unavyopaswa.
Jakob alitikisa kichwa.

“Itabidi mnichukue na kwenda kuniadhibu k**a mnataka. Mtakuwa mnatimiza wajibu wenu. Unajua jana usiku wakati nimejilaza nilikuwa nawaza nini? ‘K**a kesho nisipokwenda kazini watakuja kunifuata humu. Tutaongea kwa muda lakini hatutaelewana.

Huenda mmoja wao akashawishika kunipiga risasi. Isipotokea hivyo itabidi wanichukue kwa nguvu, na katika harakati hizo virungu itabidi vitumike. Virungu vingi vinavyorushwa kwa pamoja, kimoja wapo, kwa bahati nzuri kinaweza kupiga kichwani chini ya kisogo, kwenye maungio ya shingo na kichwa……”

“Lazima ana wazimu!.” Alipayuka mmoja wa wale askari jela akikatiza kauli ya Jakob.

“Labda. Lakini sidhani. Ni mmoja wa wale wanafalsafa wasio na bahati.”
Alijibu kiongozi wa wale askari jela kisha akaendelea.

“Sawa Jakob. Kirungu kimoja chini ya kisogo, kwenye maungio ya shingo na kichwa, kitakuwa na athari ile ile ya kupigwa risasi ya moyo au kichwa. Nimekuelewa. Unaonaje tukifuatana kwenda ofisini?

“Ofisini? Tukafanye nini ofisini?.” Aliuliza Jakob uso wake ukionyesha kutatizwa.

“Ukweli ni kwamba sijui. Lakini vilevile ukweli ni kwamba kwa kuwa sasa najua nia yako, sitakupa furaha ya kuona risasi yoyote ikipigwa au virungu vyovyote vikipiga chini ya kisogo kwenye maungio ya kichwa na shingo. Tunakwenda au sisi tuondoke zetu?”

Jakob alisita kwa muda kisha akasema.
“Umeshazeeka. Hunda umeshafanya kazi hii kwa miaka ishirini au zaidi. Karibu utastaafu. Unajua unaweza ukafukuzwa kazi na kupoteza muda wako bure kwa kutofuata taratibu?”

“Miaka ishirini na mitano kazini. Nakaribia kustaafu. Naweza kufukuzwa kazi na kupoteza muda wangu, yote hayo ni kweli. Lakini, - lakini wewe siyo mwanafalsafa pekee asiye na bahati humu. Twende zetu.”

Jakob alitikisa kichwa kwa masikitiko.
“Sitapenda kukuona ukifukuzwa kazi. Lazima utakuwa na mke na watoto wanaokutegemea. Tunaweza tukakubaliana jambo moja. Mwanzoni ulinitaka niende kazini na haya mambo yaishilie mbali nikakataa. Unaonaje iwapo nitakwenda kazini leo k**a ulivyotaka, lakini na wewe kwa upande wako ukubali kwamba kesho au siku nyingine yeyote hutaongoza kundi lolote litakalotakiwa kunitafuta?”

“Hakuna makubaliano yoyote Jakob” alijibu yule kiongozi wa wale askari jela.

“Sawa. Wewe ni mtu mzuri lakini mjinga, k**a unadhani kufuatana na wewe kwenda ofisini itasaidia, twende.”

Dakika chache baadaye Jakob alikuwa akikabiliana na Mkuu wa Gereza. Walikuwa wako wenyewe wawili kwenye ofisi ya Mkuu huyo. Yule mzee askari jela aliyekuwa amemleta Jakob alikuwa ameamriwa na mkuu wake aondoke.

Mkuu wa gereza la Ngathi, Thomas Oringe, alikuwa ni mtu aliyepata umri wa miaka arobaini na mitano. Kulikuwa na minong’ono kwamba hakuipenda sana kazi yake, minong’ono ambayo ilizuka kutokana na kule kushindwa kwa juhudi zake za kubadilisha hali na mazingira ya magereza. Kushindwa kwa juhudi zake hakukuwa ni makosa yake. Mapendekezo yake mengi yalikuwa yamerudishwa na wakuu wake yakiwa yameambatana na taarifa fupi.

“Shukrani kwa mapendekezo yako, lakini tunasikitika kuwa hayazingatii hali halisi. Unalopendekeza ni sawa na kuligeuza gereza kuwa k**a shule au hospitali, hilo haliwezekani. Vilevile tutashukuru k**a hutatoa mapendekezo ya aina hiyo siku za baadaye”

Thomas Oringo, kiutaalam akiwa ni mwanasaikolojia aliyejigeuza askari aliendelea na juhudi zake kwa muda bila mafanikio na hatimaye ilibidi shauku aliyokuwa nayo itoweke kabisa baada ya kukumbushwa kuwa yeye alikuwa askari na ilimbidi aishi kwa ku*ingatia mila na desturi za kiaskari, k**a hazimfurahishi kwa nini asifungashe mizigo yake akaondoka?

Thomas Oringo hakufungasha akaondoka, lakini vilevile ilikuwa ndio mwisho wa juhudi zake. Walikuwepo watu wachache waliokijua kisa hiki cha Thomas. Kati ya hawa baadhi walimuona ni mjinga na wengine walimwonea huruma. Waliomuonea huruma walijua kuwa mbali ya juhudi zake nzuri kushindwa, alikuwa amewaudhi wakuu wake na kutokana na hali hiyo, asingetarajia cheo chochote zaidi ya kuishia na ukuu wa gereza.

Askari yule mzee aliyeongoza kikundi kilichomkuta Jakob akifanya mazoezi alifahamu kisa hiki cha Thomas Oringo na alikuwa miongoni mwa wale waliomuonea huruma. Hii ndiyo sababu iliyomfanya amwambie Jakob kuwa hakuwa mwanafalsafa pekee aliyekosa habati.

Thomas Oringo alimtaza Jakob kwa makini kwa muda mfupi kisha akamwashiria kiti kilichokuwa mbele ya meza yake.
“Keti tafadhali.” Alisema, akatoa paketi la sigara mfukoni akachomoa sigara mbili na kumkaribisha Jakob moja.
“Unavuta? Aliuliza.

Jakob aliketi akapokea sigara na kukubali kiberiti ambacho alikabidhiwa na Thomas.
“Kwa kawaida sivuti lakini gerezani unaweza ukafanya jambo lolote.” Alijibu Jakob akajiwashia sigara aliyopewa.
“Wakati mwingine ni kweli, wakati mwingine si kweli. Inategemea.” Alisema Thomas naye akajiwashia sigara yake.

“Kwa nini unasema wakati mwingine ni kweli na wakati mwingine si kweli.” Aliuliza Jakob.

“Nasema hivyo kwa sababu mabadiliko yanayompata mtu gerezani yanategemea kwa kiasi kikubwa mtizamo wa mtu mwenyewe. Tunachukulia tu kuwa magereza yanawabadilisha watu kwa sababu tunaona watu wengi wanaofungwa magerezani wakikumbwa na mabadiliko hayo. Lakini ni vizuri vilevile tukakumbuka kuwa watu walio wengi ni dhaifu na kwa kwa urahisi kabisa watajiachia wapate nafuu kidogo inayoambatana na mabadiliko ambayo mazingira yamelazimisha juu yao, hata k**a nafuu hiyo inaambata na kudhalilika na kujipotezea heshma. Wako watu wachache, tena wachache sana, ambao wako radhi kufa lakini wasiruhusu mabadiliko katika kile wanachokiamini.”

Thomas alinyamaza kwa muda akamkazia macho Jakob kisha akamnyooshea kidole cha shahada.

“K**a wewe Jakob. Unajaribu kujiua kwa sababu unaamini ndani ya tendo la kujiua na nimeshaona kuwa vyovyote tutakavyofanya hapa hutaacha kuamini hivyo. Wewe ni jasiri, na hilo hakuna mtu anayeweza kubisha; lakini kinachonishangaza ni kwamba ni kwanini hujaamua kujitundika?”

Jakob alivuta sigara yake kwa muda bila kujibu kisha akasema.
“Unajuaje kuwa nataka kujiua?”

“Wafungwa wote wenye tabia k**a yako napata taarifa zao na ku*ichunguza kwa makini. Tangu ufike hapa umekuwa ukitafuta kifo kwa nguvu sana lakini bahati imekuwa si yako. Bado nakuuliza. Kwa nini hujitundiki?.

“Sijitundiki kwa sababu, kufanya hivyo ni woga. K**a wewe ulivyo askari, na mimi kwa mtizamo wangu mwenyewe binafsi naamini kuwa ni askari. Napigana na yale yote ambayo katika mtazamo wangu naamini hayanifai. Situmaini kushinda, lakini kutokutumainia ushindi hakunifanyi niache kupagana. Nitaendelea kupigana mpaka atakapotokea mtu ambaye naye ana mtizamo wa aina yake aamue kunimalizia. Kwa mfano tu afande, wewe unaweza ukawa mtu k**a huyo. Hapo ulipo una bastola. Unaweza ukaichomoa na dakika chache baadaye nikawa marehemu. Utaandika ripoti k**a inavyotakiwa na kuelezea ilikuwaje n.k. huo ukawa ndiyo mwisho wa Jakob mwenye usumbufu.”

Fuata kiungo (link) hiki kuendelea kusoma hadithi hii ya kusisimua: https://wellbizsolutions.org/blog/f/misukosuko---sura-ya-kwanza

Address

Mosque Street, No. 1574/144, Kitumbini
Dar Es Salaam
11105

Opening Hours

Monday 08:30 - 07:30
Tuesday 08:30 - 07:30
Wednesday 08:30 - 07:30
Thursday 08:30 - 07:30
Friday 08:30 - 07:30
Saturday 08:30 - 07:30

Telephone

+255754281131

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Herbal Impact posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Herbal Impact:

Share

Our Story

Herbal Impact was founded in 2007 by Juma Killaghai as a vehicle for exploiting nature’s treasure, especially in the area of phytochemicals. Juma Killaghai is an organic natural products research chemist based in Dar es Salaam. The firm he founded is the maker of HAIIBA brand. The brand comprises natural medicinal products that includes: 1. Haaiba Dental Guard; 2. Haiiba IG; 3. Haiiba Skin Guard; 4. Haiiba GlucoMaster; and 5. Haiiba Timamu Tea. Haiiba Dental Guard: This is a highly potent mouth wash. It kills millions of germs, especially gram positive bacteria, on contact. The product is known for its ability to permanently cure severe tooth aches within 15 minutes of using; Haiiba IG: This is a very potent anti HIV product. The product can reduce the viral load in HIV infected people by millions of HIV copies within six (6) months of use; Haiiba Skin Guard: This is highly effective for a variety of skin infections, including fungi; Haiiba GlucoMaster: This product is good for diebetics in the sense that it helps to reduce insuline resistance, and corrects damage caused by prolonged elevated blood sugar such as nerve damage, weakened libido, etc. ; and Haiiba Timamu Tea: This tea is very powerful body tonic. It is a great help for people with certain medical conditions including the following: 1. Chronic inflammation; 2. Muscle and joint pains; 3. Chronic fatigue; 4. Gaut; 5. Arithrites; 6. Indigestion; 7. Catarracts; 8. Slow metabolism; 9. Skin disorders; 10. Fast aging; 11. Compromised immunities; 12. Cancer disposition; 13. Multiplesclerosis; 14. Elevated Cholesterol; 15. Nerve damage; 16. High Blood Pressure; 17. Liver disfunction; 18. Malignant Tumors; 19. Heart Disease; and 20. Migranes. With more research and experience to back it up, the firm in 2012 redefined its mission to include provision of health and wellness education as its core activity. The change was brought about by mounting evidence that shows that for the most part people fall ill simply because they lack the right kind of health information.