Medical Stores Department (MSD)

Medical Stores Department (MSD) MSD is annually audited by CAG and has fully-fledged competent internal audit Unit that oversees internal controls effectiveness.

Medical Stores Department (MSD) was established by the Act of Parliament No.13 of 1993 as an autonomous department under the Ministry of Health, responsible for developing, maintaining and managing an efficient and cost effective system of procurement, storage and distribution of approved medicines and medical supplies required for use by the public health services as the Ministry of Health may from time to time approve. Board of Trustees is the highest decision-making body that governs and set the directions of MSD on behalf of the Minister for Health, The Board composed of nine(9) members appointed every three years. The Chairman appointed by the President of the United Republic of Tanzania, eight (8) members are appointed by the Minister responsible for health.The Board is comprising of a multidisciplinary team including eminent public servants, scientists, practicing medical doctors, lawyers, accountants, professors and renowned economists. To implement its responsibilities the Board operates through three committees namely; Audit and Risk Management Committee that provides the management with accurate information on the effectiveness of risk management and internal controls including regulatory compliance by the Department; Technical Services Committee that handles all matters related to quality of medicines and medical supplies together with management expired medicines. Finance and Administration Committee tha is mandated in handling all matters related to MSD Financial Management, Human Resources Management and Administrative functions of the Department. The Board delegates the day to day management of the department operations to Director General who is appointed by the President of the United Republic of Tanzania. The administrative functions and operations of Department are carried by and through the Executive Management Team (EMT).The EMT is constituted by the Director General, Director of Human Resources and Administration, Director of Finance and Planning, Director of Logistics, Director of Procurement, Director of Information and Communication Technology, Director of Customer Service and Zonal Operations as well as Chief Legal Counsel. The departnment operates through eight zonal stores in Dar-es-salaam, Mwanza, Iringa,Moshi,Mbeya,Tabora, Dodoma and Mtwara suppoted by two Sales Points in Tanga and Muleba.

16/04/2026
15/04/2026

Fuatilia Simulizi za usambazaji wa bidhaa za afya mkoani Morogoro

Mwenyekiti wa Kamati ya Ustawi wa Jamii ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Hussein Ibrahim Makungu ameipongeza Bohar...
15/04/2026

Mwenyekiti wa Kamati ya Ustawi wa Jamii ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Hussein Ibrahim Makungu ameipongeza Bohari ya Dawa (MSD) kwa maboresho makubwa iliyofanya kuwezesha kuimarika kwa mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya, hasa kuwezesha vifaa na mashine za kisasa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini.

Mwenyekiti huyo na wajumbe wake ambao wamefanya ziara ya kubadilishana uzoefu na Bohari ya Dawa (MSD) wameeleza kuwa, MSD kusambaza bidhaa za afya kwa vituo 8,900 nchi nzima hadi mlangoni kwa mteja mara sita kwa mwaka ni hatua kubwa, na ya kupongezwa.

Ameongeza kuwa, vifaa vya kisasa na vinavyoendana na teknolojia ya kisasa vinavyonunuliwa na serikali kupitia MSD na kuwezesha matibabu ya kitaalam kufanyika nchini ni jambo la kujivunia, kwani wananchi sasa wanapata huduma nyingi za kibingwa ndani ya nchi.

Kwa upande mwingine, wamepongeza juhudi za ujenzi wa maghala mapya na ya kisasa Mkoani Dodoma na Mtwara ambayo yameongeza ukubwa wa mita za mraba 12,000 na kuongeza uwezo wa uhifadhi na huduma kwa wananchi, huku ujenzi mwingine ukiendelea Wilayani Chato.

*“Tuna la kujifunza hapa kwani huko Zanzibar Bohari Kuu ya Dawa ina changamoto ya eneo la uhifadhi wa bidhaa za afya, na zipo nyingi” alisema Mhe. Makungu”.*

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa MSD Elisamehe Macha ameeleza kuwa maboresho ya huduma za MSD yanaendana na malengo ya serikali ya kusogeza huduma kwa wananchi, ndio maana MSD imenunua na kusambaza bidhaa za huduma za kusafisha damu kwa wagonjwa wa figo, kinywa na meno, vifaa vya upasuaji, mashine za uchunguzi, pamoja na mama na mtoto.

Ameongeza kuwa, hali ya upatikani wa bidhaa za afya pia imeimarika, kwani kwa sasa MSD inakidhi mahitaji ya wateja kwa wastani wa asilimia 83.

@mchengerwa .hmwinyi

15/04/2026

Baadhi ya wateja na wadau wa MSD wakiwa na nyuso za furaha, baada ya kutunukiwa vyeti mbalimbali na MSD, kufuatia uongoz...
14/04/2026

Baadhi ya wateja na wadau wa MSD wakiwa na nyuso za furaha, baada ya kutunukiwa vyeti mbalimbali na MSD, kufuatia uongozi na utendaji wao bora katika kuimarisha mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya.

MSD iliwatunuku vyeti viongozi hao k**a ishara ya kutambua na kuthamini mchango wao katika kusimamia na kuimarisha mnyororo wa ugavi katika mikoa ya Mbeya, Songwe, Rukwa na Wilaya ya Makete.

  cha Wateja na Wadau wa MSD Kanda ya mbeya 2026Baadhi ya wateja na wadau wa MSD wakiwa na nyuso za furaha, baada ya kut...
14/04/2026

cha Wateja na Wadau wa MSD Kanda ya mbeya 2026

Baadhi ya wateja na wadau wa MSD wakiwa na nyuso za furaha, baada ya kutunukiwa tuzo mbalimbali na MSD, kufuatia utendaji wao bora katika maeneo muhimu ya mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya.

Tuzo hizo zilitolewa kwa washindi walioonesha ubora katika vipengele tofauti ikiwemo ulipaji wa madeni kwa wakati, matumizi ya vyanzo vya ndani (own source) katika ununuzi wa bidhaa za afya, matumizi bora ya mifumo katika kuagiza bidhaa, uwasilishaji wa mahitaji kwa wakati, pamoja na umahiri katika ununuzi wa bidhaa za afya.

Hatua hii inaonesha dhamira ya pamoja ya kuimarisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wananchi.

*DC CHUNYA AHIMIZA UBORESHAJI WA MNYORORO WA UGAVI WA BIDHAA ZA AFYA NCHINI*Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mbaraka Batenga, a...
13/04/2026

*DC CHUNYA AHIMIZA UBORESHAJI WA MNYORORO WA UGAVI WA BIDHAA ZA AFYA NCHINI*

Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mbaraka Batenga, amewataka wataalamu wa sekta ya afya nchini kuimarisha maoteo ya mahitaji ya bidhaa za afya kwa ajili ya vituo vya kutolea huduma za afya, ili kuhakikisha Bohari ya Dawa (MSD) inafanya kazi kwa ufanisi na kutoa huduma bora kwa wananchi.

Batenga ametoa wito huo hii leo, alipokuwa akifungua kikao cha wateja na wadau wa MSD Kanda ya Mbeya kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo, akisisitiza umuhimu wa kuwepo kwa usambazaji thabiti na upatikanaji wa kutosha wa bidhaa za afya kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.

Amewaasa watoa huduma za afya nchini, kuwaelimisha wananchi na kutoa ufafanuzi juu ya huduma na bidhaa za afya zinazopatikana kwenye ngazi tofauti za vituo vya kutolea huduma za afya nchini, ili kuepusha sintofahamu na malalamiko ya kukosa bidhaa za afya.

“Ni muhimu kila mdau akatimiza wajibu wake ipasavyo ili takwimu zinazokusanywa ziwe sahihi na ziweze kusaidia kupanga mahitaji halisi ya dawa na vifaa tiba,” alisisitiza Batenga.

Aidha, amewataka watoa huduma za afya nchini kulipa madeni wanayodaiwa na MSD, akieleza kuwa ucheleweshaji wa malipo hayo unaathiri uwezo wa MSD kununua na kusambaza bidhaa za afya kwa wakati.

“Mrundikano wa madeni unaathiri mnyororo mzima wa ugavi, ikiwa ni pamoja na uwezo wa MSD kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi, sambamba na kushindwa kulipa wash*tiri na wazalishaji” aliongeza.

Awali, akitoa salamu za Menejimenti ya MSD, Mkurugenzi wa Ugavi na Uendeshaji, Hassan Ally, alisema MSD imefanikiwa kufikia asilimia 96 ya usambazaji wa bidhaa za afya nchini, kutokana maboresho yanayoendelea ndani ya bohari.

Alibainisha kuwa taasisi hiyo pia inaendelea kuboresha huduma zake kupitia mikakati mbalimbali ikiwemo ujenzi wa maghala mapya, uboreshaji wa mifumo ya utoaji huduma, ununuzi wa magari ya usambazaji, matumizi ya nishati mbadala pamoja na kuanzisha viwanda vya uzalishaji wa bidhaa za afya.

Kwa upande wake, Meneja wa MSD Kanda ya Mbeya, Egidius Rwezaura, aliwahimiza wadau kutumia mifumo ya kidijitali k**a “MSD Customer Portal” ili kuongeza ufanisi na kurahisisha upatikanaji wa huduma.

Pia ali

MSD imeendelea na zoezi la usambazaji wa vyandarua mkoani Morogoro pamoja na kuwepo kwa changamoto za mvua kubwa zinazoe...
12/04/2026

MSD imeendelea na zoezi la usambazaji wa vyandarua mkoani Morogoro pamoja na kuwepo kwa changamoto za mvua kubwa zinazoendelea kunyesha. Mvua hizo zimesababisha zoezi hilo kuwa na changamoto nyingi ikiwemo kuharibika kwa miundombinu.

Bohari ya Dawa (MSD) imepata leseni  ya usalama na afya mahala pa kazi (Osha Compliance license )  2025/2026 kutoka Maml...
12/04/2026

Bohari ya Dawa (MSD) imepata leseni ya usalama na afya mahala pa kazi (Osha Compliance license ) 2025/2026 kutoka Mamlaka ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) ikiwa ni mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwake MSD.

Kupatikana kwa leseni hii ni uthibitisho kuwa MSD imepiga hatua kubwa kuzingatia kikamilifu sheria, taratibu, kanuni na miongozo ya afya na usalama mahali pa kazi k**a inavyotakiwa.

Mafanikio haya yanaonesha dhamira ya dhati ya MSD kuhakikisha inalinda afya na usalama wa watumishi, wadau pamoja na jamii kwa ujumla.

MSD itaendelea kuboresha mifumo ya usalama ili kudumisha viwango hivi na kuvuka zaidi ya matarajio.

Kuokoa Maisha*

Watumishi wa MSD kanda ya Tabora wamekutana ndani ya Jiji la Mwanza kwaajili ya mafunzo maalum yanayolenga kuboresha ute...
12/04/2026

Watumishi wa MSD kanda ya Tabora wamekutana ndani ya Jiji la Mwanza kwaajili ya mafunzo maalum yanayolenga kuboresha utendaji kazi wa taasisi na kuongeza ufanisi wa majukumu ya kila siku.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa programu hiyo, Meneja wa MSD Kanda ya Tabora Bw.Rashid Omary alisisitiza umuhimu wa kujengeana uwezo ili kuendana na mabadiliko ya kiutendaji na mahitaji ya kisasa ya huduma.

Aliongeza kuwa Mafunzo hayo ni sehemu ya mkakati wa taasisi wa kuimarisha weledi, ushirikiano, na ubunifu miongoni mwa washiriki.

Mafunzo hayo yanatarajiwa kuleta matokeo chanya kwa washiriki na kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kuboresha utoaji wa huduma kwa jamii.

Matukio mbalimbali ya Kikao kazi cha watumishi wa MSD Kilimanjaro.
11/04/2026

Matukio mbalimbali ya Kikao kazi cha watumishi wa MSD Kilimanjaro.

Watumishi wa MSD Kanda ya  Kilimanjaro wanashiriki mafunzo maalum ya kuimarisha uwajibikaji wa ushirikiano,umoja, upendo...
11/04/2026

Watumishi wa MSD Kanda ya Kilimanjaro wanashiriki mafunzo maalum ya kuimarisha uwajibikaji wa ushirikiano,umoja, upendo na kuimarisha utendaji kazi. Mafunzo hayo yanayofanyika Mkoani Arusha yanalengo la kuongeza ufanisi wa utoaji huduma kwa wateja wake, ambao ni vituo vya kutolea huduma za afya takribani 991 vilivyopo Kilimanjaro, Arusha na Manyara.

Katika mafunzo hayo watumishi wanafundishwa masuala mbalimbali k**a mikakati ya huduma kwa wateja, maadili na uadilifu, mpango mkakati na uelekeo wa taasisi, namna ya kukabiliana na msogo wa mawazo na uwiano wa maisha.

Hata hivyo watumishi watashiriki kwenye michezo ya kujenga umoja na ushirikiano kwa pamoja.

Address

Off, Nyerere Road, Keko Mwanga
Dar Es Salaam
9081

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Medical Stores Department (MSD) posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram