13/04/2026
*DC CHUNYA AHIMIZA UBORESHAJI WA MNYORORO WA UGAVI WA BIDHAA ZA AFYA NCHINI*
Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mbaraka Batenga, amewataka wataalamu wa sekta ya afya nchini kuimarisha maoteo ya mahitaji ya bidhaa za afya kwa ajili ya vituo vya kutolea huduma za afya, ili kuhakikisha Bohari ya Dawa (MSD) inafanya kazi kwa ufanisi na kutoa huduma bora kwa wananchi.
Batenga ametoa wito huo hii leo, alipokuwa akifungua kikao cha wateja na wadau wa MSD Kanda ya Mbeya kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo, akisisitiza umuhimu wa kuwepo kwa usambazaji thabiti na upatikanaji wa kutosha wa bidhaa za afya kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.
Amewaasa watoa huduma za afya nchini, kuwaelimisha wananchi na kutoa ufafanuzi juu ya huduma na bidhaa za afya zinazopatikana kwenye ngazi tofauti za vituo vya kutolea huduma za afya nchini, ili kuepusha sintofahamu na malalamiko ya kukosa bidhaa za afya.
“Ni muhimu kila mdau akatimiza wajibu wake ipasavyo ili takwimu zinazokusanywa ziwe sahihi na ziweze kusaidia kupanga mahitaji halisi ya dawa na vifaa tiba,” alisisitiza Batenga.
Aidha, amewataka watoa huduma za afya nchini kulipa madeni wanayodaiwa na MSD, akieleza kuwa ucheleweshaji wa malipo hayo unaathiri uwezo wa MSD kununua na kusambaza bidhaa za afya kwa wakati.
“Mrundikano wa madeni unaathiri mnyororo mzima wa ugavi, ikiwa ni pamoja na uwezo wa MSD kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi, sambamba na kushindwa kulipa wash*tiri na wazalishaji” aliongeza.
Awali, akitoa salamu za Menejimenti ya MSD, Mkurugenzi wa Ugavi na Uendeshaji, Hassan Ally, alisema MSD imefanikiwa kufikia asilimia 96 ya usambazaji wa bidhaa za afya nchini, kutokana maboresho yanayoendelea ndani ya bohari.
Alibainisha kuwa taasisi hiyo pia inaendelea kuboresha huduma zake kupitia mikakati mbalimbali ikiwemo ujenzi wa maghala mapya, uboreshaji wa mifumo ya utoaji huduma, ununuzi wa magari ya usambazaji, matumizi ya nishati mbadala pamoja na kuanzisha viwanda vya uzalishaji wa bidhaa za afya.
Kwa upande wake, Meneja wa MSD Kanda ya Mbeya, Egidius Rwezaura, aliwahimiza wadau kutumia mifumo ya kidijitali k**a “MSD Customer Portal” ili kuongeza ufanisi na kurahisisha upatikanaji wa huduma.
Pia ali