Dr. Christopher Cyrilo

Dr. Christopher Cyrilo Medical Doctor| Health Literacy expert | Social Activist | Writer
(1)

Kataa UFALA.
13/01/2026

Kataa UFALA.

Au pesa za sherehe za Uhuru wa Tanganyika (9 December) ndio zinatumika kwenye sherehe za mapinduzi ya Zanzibar leo Janua...
12/01/2026

Au pesa za sherehe za Uhuru wa Tanganyika (9 December) ndio zinatumika kwenye sherehe za mapinduzi ya Zanzibar leo Januari 12?

Polisi sio chanzo sahihi cha kutoa taarifa za watuhumiwa wanaopata shida vituoni. Kwanza kwa namna muundo wa jeshi la po...
12/01/2026

Polisi sio chanzo sahihi cha kutoa taarifa za watuhumiwa wanaopata shida vituoni. Kwanza kwa namna muundo wa jeshi la polisi ulivyo, pili ni kwa sababu chombo hiki kimeshapoteza imani kwa wananchi. Mtu mwenye akili timamu hawezi kuliamini jeshi la polisi la Tanzania. Hiki chombo ni - compromised (kimeshindwa kutimiza majukumu yake), ni corrupt (Watumishi wengi ni matapeli, wala rushwa) na ni primitive (kinafanya kazi kwa mtindo wa kale/zamani).
K**a wewe unaliamini jeshi la polisi, HUNA AKILI.

Nini kifanyike;
Kwanza, mapendekezo ya tume ya haki jinai yafanyiwe kazi (ingawa kwa sasa hakuna serikali ya kufanyia kazi hiyo). Moja ya mapendekezo ni kuvunja na kusuka upya jeshi la polisi. Hili linahitaji viongozi wengine wa kujenga taasisi ya polisi, sio hawa wa sasa waliokwisha shindwa.

Pili, hata k**a polisi ikifanyiwa mabadiliko, bado ni lazima kuwe na chombo kingine cha ulinzi na usalama ambacho kinaweza kuchunguza watumishi wa jeshi la polisi. Kwa sasa, polisi wakiua mtu wakatangaza huyo mtu ni jambazi, imeisha. Wao ndio wanajua ni jambazi, wao ndio wana ushahidi na uthibitisho. Ikitokea kuna sintofahamu basi ni polisi haohao watachunguza na haohao watatoa majibu. Kwahiyo polisi wamepewa 'all power' ya kufanya chochote bila hofu ya kuwajibika.

Tunahitaji chombo kingine kitakachofanya kazi ya kuchunguza makosa ya jinai. Hapa maana yake , ofisi ya DCI pamoja na vitengo vya Forensic ambavyo vipo ndani ya polisi vinatakiwa kutenganishwa na kuwa sehemu ya hicho combo kipya. Polisi wao watabaki na kazi ya ulinzi (kulinda raia na mali zao) na sio kazi ya kuchunguza matukio ya uhalifu kwa sababu hawawezi kujichunguza wenyewe. Maana yake, watuhumiwa wanapofia vituoni/mahabusu anayechunguza asiwe polisi.

Tayari tuna TAKUKURU kwenye uhalifu wa fedha, tuna UHAMIAJI kwenye usafirishaji haramu wa binadamu, na DCEA kupambana na dawa za kulevya, vivo hivyo tunahitaji FORENSIC BUREU kwa ajili ya kuchunguza na kukusanya ushahidi wa makosa mengine ya jinai k**a mauaji, utekaji nk.
Polisi wabaki kutoa HUDUMA ya Ulinzi na Usalama wa raia.

Hata hivyo, vyombo vyote hivi na hata hicho kipya vitapaswa kujengwa kwa misingi ya HAKI na UWAJIBIKAJI.
Nawasilisha.
Dr. Chris Cyrilo

11/01/2026

Lucy Kuffa au Latifa, amevamiwa na kupigwa.
Lucy ni miongoni mwa wahuni 100 waliojivika ukatoliki ingawa sio wakatoliki, na kujifanya kuwash*taki viongozi wa Kanisa Katoliki, tukio liloibua hasira na ghadhabu kwa waumini Katoliki na wote wanaoamini katika haki, usawa na ukweli.

Ikiwa ni kweli Lucy amevamiwa, Je! Ni nani aliyefanya hivyo?

Waumini wa Kanisa Katoliki waliopitia, kuelewa na kushiba mafundisho ya Kanisa hawawezi kufanya hivyo. Na ikiwa waliofanya hivyo ni Wakatoliki basi wamekiuka mafundisho ya imani katoliki.

K**a kweli amevamiwa, Lucy aende polisi au k**a ametumwa kuendeleza drama shauri yake. Zaidi namuombea apone, aendelee na upumbavu wake. Mtu mwenye akili hawezi kuhangaika na hawa wavaa vijora vichafu.

Nawasilisha!
Dr. Chris Cyrilo.

20261. 'Kula Vizuri', Zaidi vyakula vitokanavyo na mimea vikiwa katika asili yake. Naam, mahindi ya kuchemsha ni bora ku...
10/01/2026

2026
1. 'Kula Vizuri',
Zaidi vyakula vitokanavyo na mimea vikiwa katika asili yake. Naam, mahindi ya kuchemsha ni bora kuliko ugali na mkate. Protini kiasi, mafuta kidogo, vyakula vya viwandani kwa nadra.

2. Shughulisha mwili/fanya mazoezi.
K**a maji yaliyotwama yanavyotunza uchafu chini, ndivyo mwili uliotulia unavyotunza maradhi kimyakimya. Miguu na mikono tuliopewa na Mungu si kwa ajili ya kuketi na kulala.

3. Soma vitabu;
Vitabuni ndimo kwenye maarifa na taarifa. Dunia inaongozwa na wasomaji wa vitabu na mahali penye viongozi wasiosoma hakuna uongozi. Na k**a wewe husomi vitabu huna haki ya kupinga hii dhana.

4. Amini na simama na Ukweli, Haki, na Utu.
Binadamu ili ajitofautishe na wanyama vema azingatie utashi aliopewa na Mungu. Utashi wa kuuishi UKWELI, kupigania HAKI na kuzingatia UTU. Binadamu aliye kinyume na haya ni wa kumtazama kwa tahadhari kubwa.

5. Ukiweza jiepushe na mazingira ya moshi na vumbi, epuka tumbaku (sigara, ugoro, sh**ha, nk), na kwa wanaokunywa pombe, kunywa kistaarabu.

Bonus, epuka mijadala na mabishano na watu wapuuzi!

Nawasilisha!
Dr. Chris Cyrilo

Ewe! Kijana.
09/01/2026

Ewe! Kijana.

Haki ya Mungu, huna akili.
09/01/2026

Haki ya Mungu, huna akili.

Nchi yangu!
09/01/2026

Nchi yangu!

08/01/2026

Moja ya dalili ya maradhi sugu ya ini ni kuvimba kwa mirija ya damu ya vena (veins) inayosambaza damu maeneo ya tumboni.
Ni mambo gani unadhani yanaweza kupelekea maradhi sugu ya ini?

Nauliza!
08/01/2026

Nauliza!

Neno la jioni!
07/01/2026

Neno la jioni!

Very sad.
06/01/2026

Very sad.

Address

Zip Code 00083
Dar Es Salaam

Telephone

+255713933736

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dr. Christopher Cyrilo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Dr. Christopher Cyrilo:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category