Dr. Christopher Cyrilo

Dr. Christopher Cyrilo Medical Doctor| Health Literacy expert | Social Activist | Writer
(1)

KUNA NINI ZANZIBAR Nafuatilia kisa cha Haji Manara kishaa nawaza!Moja ya maukumu muhimu kwenye tasnia ya 'Intelligence' ...
22/02/2026

KUNA NINI ZANZIBAR
Nafuatilia kisa cha Haji Manara kishaa nawaza!
Moja ya maukumu muhimu kwenye tasnia ya 'Intelligence' ni kutumia taarifa za wazi ili kupata taarifa zilizofichwa. Unakusanya taarifa, unazifanyia upembuzi - unazitathmini na kuzichakata, halafu unapata 'taswira' ya taarifa zilizofichwa. Kisha unaweza kufanya uchunguzi ili kubaini ukweli usio na shaka.

Taarifa za wazi ni kwamba, Simba na Yanga zina mashabiki wengi kutoka Mikoa yote ya Tanzania na Zanzibar. Simba na Yanga, pamoja na kudhaminiwa na matajiri bado wanahitaji mapato kupitia tiketi za kutazama mechi zao. Mechi za ligi ya mabingwa Afrika na Mechi za Derby ndio mechi zenye mahudhurio na mapato makubwa. Mbali na mapato, Simba na Yanga bila shaka zinafanya kila liwezekanalo kuongeza mashwbiki, na kuwatunzana kuwafurahisha wale waliopo. Naam! Kitu kikubwa cha kuwapa mashabiki ni raha na furaha.
Bila shaka aya hiyo ya pili imenyooka, hakuna mawaa. Nimeandika mambo ya wazi kabisa ambayo kila mtu mzima anayafahamu.

Sasa, Kwanini Simba na Yanga wanapeleka mechi zao Zanzibar hata pale Uwanja wa Mkapa unapokuwa katika mazingira ya kuruhusu mchezo?
Je! Kuna taarifa gani ya siri ambayo inaweza kujibu swali hilo?
Wengine watasema ni maamuzi binafsi!
Wengine watasema Wanafuata bahati kwenye uwanja wa Amaan!
Wengine watasema wameagizwa na waganga wao!
Kila mtu anaweza kuwa na majibu yake.
Lakini maswali hayaishi.

Kwanini Simba na Yanga waache mapato makubwa Benjamin - Mkapa kwa ajili ya Zanzibar?
Kwanini Simba na Yanga wasumbue mashabiki kusafiri hadi Zanzibar, na kuwanyima mashabiki wengi zaidi fursa ya kutazama mchezo wao?
Kwanini Simba na Yanga watumie muda mrefu na nguvu kubwa kuvuka maji wakati makazi yao ni Dar es Salaam na kuna uwanja bora na mkubwa zaidi?
Kunani Zanzibar?

Je! Kuna makubaliano ya siri kati ya serikali ya Zanzibr na vilabu vya Simba na Yanga?
Je! Serikali ya Zanzibar inawalipa Simba na Yanga pesa kubwa kiasi cha wao kutojali mapato ya Benjamin Mkapa?
Je! Serikali ya Zanzibar inawalipa Simba na Yanga pesa ya kuwafanya waone mashabiki wao si kitu?

Je! Ni 'mpango wa siri' wa Serikali ya Zanzibar kuitangaza Zanzibar, kuchochea ukuaji wa michezo, buashara na utalii?

Cardinal Pengo, Gallery.
20/02/2026

Cardinal Pengo, Gallery.

Serikali ya CCM ilipoanza kupambana na wapinzani wake kwa kuwateka na kuwaua, tumelia  hadi macho yamevimba wakati wanaC...
19/02/2026

Serikali ya CCM ilipoanza kupambana na wapinzani wake kwa kuwateka na kuwaua, tumelia hadi macho yamevimba wakati wanaCCM wakitucheka na kutukebehi eti tunajiteka wenyewe!

Pamoja na vilio vyetu tulionya pia, kwamba uovu unaambukiza, uovu unasambaa, uovu ni kansa inayosambaa! Tulionya kwamba, WanaCCM pamoja na dharau zao na kejeli zao juu yetu sisi tunaotekwa na kuuawa, na wao pia hawapo salalama. Na kweli, ametekwa Waziri wa Zamani Ndg. Mwambe na kufanyiwa vitu vibaya, wapo mawaziri wengine wamewahi kuwekwa house arrest, na kwenye uchaguzi wao wa ndani wanafanyiana mambo haya na mengine ya ajabu. Hakuna aliye salama ndani ya uovu!

Tulionya tena, kwamba hao vijana wanaotumiwa kuteka na kuua wapinzani wataanza kutumia mbinu hizo kutafuta pesa. Kana kwamba watu hawa wanaotumiwa na baadhi ya viongozi wakisiasa na wale wa vyombo vya ulinzi na usalama wanaogopwa na hawaguswi, na kwakuwa wao ni sehemu ya ulinzi wa madaraka ya CCM basi hakuna kitu watafanywa na viongozi CCM. Tukio maaurufu la kuthibitisha madai haya ni tukio kutekwa na kupotezwa kwa baadhi ya wafanyabiashara wa Kariakoo, na jaribio la kutekwa mfanyabiashara Tarimo kule Kiluvya. Wahusika wa matukio haya wametajwa kuwa ni watumishi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama.

Tulionya pia, kwakuwa serikali ya CCM imeruhusu matukio haya; kwanza kwa kutochukua hatua stahiki na pili kutoa kauli zinazochochea matukio haya (mfano, kauli kwamba hata nchi nyingine matukio haya yapo); basi tutarajie hata raia binafsi wenye roho chafu huko mitaani wakikosana wataanza kutekana na kuuana! Yes! Kwa sababu uovu, k**a ulivyo wema, unaambukiza, unasambaa!

Hata leo, wapo vijana ambao wanahisi matukio haya ni kwa watu fulani tu na wao hayawahusu! Nawajua vijana wa CCM wanaotukana wapinzani na wasiojali maovu wanaofanyiwa wakosoaji, wanaokejeli na kusema eti tunajiteka, nawajua ambao na wao yamewakuta. Waovu hawa, wameruhusiwa na serikali ya CCM, lakini uovu wao utawaumiza wote wakiwemo hao walioruhusu!

Shetani limeshika hatamu, Shetani halishibi damu.
Nawasilisha.
Dr. Chris Cyrilo.
--------------------------
Usikose kusoma kitabu cha ISTILAHI ZA UHALIFU NA USALAMA popote Tanzania.
Nicheki kwa 0713933736 / 0745830775

17/02/2026

VIDEO
Msikilize Mtanzania aliye vitani huko Urusi akitoa maelezo yake juu ya hali ilivyo. Tofauti na wengine, yeye anaonekana yupo salama, na hajutii kuwa huko.
Huyu hajakutana na maguruneti au mwenetu anatuita tukaumie wote?

Zingatia! Warusi hawataki kupoteza nguvu zao, wanataka kubaki kuwa super power. Mapema kabisa walipoona mataifa ya magharibi yanamimina silaha kusaidia Ukraine, Warusi walibadili mbinu haraka; moja kutumia silaha za gharama nafuu kutoka Iran, Korea Kaskazini, ili kulinda silaha kali za gharama kubwa, na pili kutumia mamluki (mercenaries) mfano; Wagner Group na wanadamu wengine kutoka kokote duniani wanaoweza kupigana kwa ajili ya ujira. Lengo ni kulinda idadi ya askari wao raia wa Urusi.

Funzo; usitumie nguvu kubwa kupambana na adui mdogo wakati kuna maadui wakubwa zaidi wanakutamani. Ni funzo la kijeshi na maisha pia.

Msikilize mwamba! Anawaita! Halafu huyu mwanangu wa Tanga kabisa mitaa ya Majani Mapana!
Maisha ni nini?
Oyaa! Anayetaka kwenda Urusi au Ukraine anicheki tuongee atanilipa ngapi? 😂

Nawasilisha!
Dr. Chris Cyrilo.

Namuonea huruma!
16/02/2026

Namuonea huruma!

16/02/2026

VIDEO; UTEKAJI MUHEZA.
Kuhusu watekaji na wauaji!
Kwanza, namuonea huruma huyu jamaa anaelekeza malalamiko yake kwa watu walewale!

Pili, niliwahi kuandika madhara ya serikali za vyama tawala kutumia makundi ya watekaji na wauaji ili kukandamiza upinzani; madhara ambayo kila mtu anaweza kuyaona ni serikali kukosa uhalali wa kuongoza raia, na raia kuichukia serikali na kutengeneza uadua mkali kati ya raia na viongozi wa serikali. Hilo linaonekana kirahisi lakini watekelezaji wa matukio haya hawajali kwa sababu kipaumbele chao sio ustawi wa taifa moja lenye amani na utulivu, kipaumbele chao ni kushikilia madaraka ili waendelee kutapanya mali za umma kwa gharama za damu za wapinzani.

Sasa kuna madhara ambayo si rahisi kuyaona;
Moja, ni wale vijana wanaotumiwa kuteka na kuua wapinzani wanapoanza kufanya matukio hayo bila kutumwa. Kwa kuwa wana silaha na kwa kuwa ni marafiki wa wenye madaraka katika uhalifu, basi hakuna wa kuwagusa wanapoteka mfanyabiashara, kupora pesa zake na kumuua, halafu wanasingizia siasa.
Pili, ndani ya serikali, viongozi wa ngazi tofauti wa kisiasa na wale wa vyombo vinavyoitwa vya ulinzi na usalama, na marafiki zao kujiundia magenge ya uhalifu kwa ajili ya manufaa yao ya kisiasa na kibiashara. Na kwakuwa serikali tayari ilishabaliki matukio haya, nani wa kumnyooshea mwenzia kidole?
Viongozi wa kisiasa na wale wa vyombo vya ulinzi; wakuu wa mikoa na wilaya, mawaziri, ma RPC na ZCO, wakimiliki magenge ya uhalifu ya kuteka na kuua watu nani atakayemkemea mwingine?

Unajikuta kwenya hatari ya kutekwa na genge la kiongozi mmoja, unapeleka malalamiko yako kwa kiongozi mwenye genge kubwa na katili zaidi! Unahisi kuna usalama? Ole wako magenge hayo yanashirikiana.

Walianza kwa upinzani, wakakubaliana hiyo ndio mbinu ya kushikilia madaraka, wamenogewa, sasa wanatumia mbinu hizo kwenye kufanya mambo yao binafsi.
Mbegu imechepua!
Jiti limemea!
Matunda tutakula!
Matunda machungu! Mabaya! Ufala
Nchi yenye ufala!

Shetani limevimbiwa damu!
Shetani litatapika damu!
Nawasilisha
Dr. Chris Cyrilo.

15/02/2026

VIDEO
Mtoto "muhaini aliyechoma vituo vya mafuta" akisimulia alivyopigwa risasi Oktoba 29.

Shetani limevimbiwa damu!
Shetani litatapika damu!
Nawasilisha.
Dr. Chris Cyrilo.

Yes! Ni upumbavu.
02/02/2026

Yes! Ni upumbavu.

Una mdada wa kazi, ni msichana wa miaka 18 au zaidi), maana yake ana mahitaji yake ya kiutu uzima! Sio?Je! Unampa muda w...
01/02/2026

Una mdada wa kazi, ni msichana wa miaka 18 au zaidi), maana yake ana mahitaji yake ya kiutu uzima! Sio?

Je! Unampa muda wa kutoka kwenda ku-refresh mwili na akili au unamfungia ndani k**a mfungwa?
Unahakikisha anapata elimu na ushauri juu ya masuala ya mahusiano, maradhi ya zinaa, ujauzito nk? Au yeye ni wa kupika, kutunza nyumba na watoto ila mambo mengine ya kibinadamu hayamuhusu?

Halafu akipewa mimba na vijana huko nje, unamfukuza. Kumbe ulikuwa na nafasi ya kumsaidia kiakili.
Akilala na kijana wako wa kiume?
Akianza kumtega Baba wa familia?

Umewahi kufikiria kwamba mfanyakazi wako wa k**e k**a ni mtu mzima atahitaji muda wake wa mambo binafsi? Tena ikibidi umwambie akipata boy friend amlete amtambulishe kwako. Ni salama! Ni utu uzima.
Sasa endelea kuamini huyo ni mtoto wa miaka 14, mnyime uhuru, mdhibiti ndani ya geti, subiri surprise.

Pombe kistaarabu!
Sigara acha.
Nawasilisha!
Dr. Chris Cyrilo.

Na Naitwa Dr.A.C. Namuombea msaada huyu binti Neema (22) mzaliwa wa Bukoba lakini mkazi wa Shinyanga kwa sasa.Historia y...
01/02/2026

Na
Naitwa Dr.A.C. Namuombea msaada huyu binti Neema (22) mzaliwa wa Bukoba lakini mkazi wa Shinyanga kwa sasa.

Historia yake ni ndefu kidogo. Ni yatima aliyelelewa na baba mdogo huko Ifakara Morogoro. Mwaka 2022 mlezi wake alifariki, hivyo akalazimika kurudi Bukoba kwa bibi yake.

Akiwa Bukoba alikutana na kijana mmoja ambaye alimpa ujauzito akajifungua 2024. Baadae alianza kupata maumivu na uvimbe kwenye taya. Mzazi mwenzie alimuaga anaenda Shinyanga kutafuta kazi ili aweze kumhudumia yeye na mtoto.

Uvimbe ulizidi kuongezeka hivyo akalazimika kumfuata mwenzie Shinyanga. Kijana alipoona hali ya uvimbe alimkimbia na hadi leo hajulikani alipo. Baada ya muda alifukuzwa walipokuwa wakiishi kwa kushindwa kulipa kodi. Akaanza kuhangaika mtaani akiwa na mtoto wa miezi 18 na uvimbe ukizidi kukua.

Muuguzi mmoja alimsaidia kumleta hospitalini. Vipimo ilionesha ana saratani ijulikanayo k**a “Ameloblastoma” yani seli za “ameloblasts" kukua na kuharibu mfupa wa taya na kusababisha sura ya uso kubadilika.

Akifanyiwa upasuaji anaweza kupona kwa sababu ni saratani isiyosambaa. Tumempa rufaa ya kwenda Bugando, lakini hana uwezo wa kumudu gharama. Maisha yake ni magumu na tumekuwa tukimsaidia yeye na mwanae kuanzia malazi, chakula na matibabu.

Anahitaji upasuaji wa kuondoa uvimbe na sehemu ya taya iliyoathirika (Wide local excision). Kisha kurejesha muonekano (aesthetics) na kazi ya taya (function). Kwa cash gharama inaweza kuwa kubwa lakini akipata bima ya NHIF kifurushi cha juu cha Tanzanite (TZS 2,712,000/=) kinaweza ku-cover sehemu kubwa ya matibabu, zikabakia gharama ndogondogo.

:
Maisha ya Neema hayajawa rahisi tangu utotoni. Kufiwa na wazazi na kuachwa yatima, kulelewa na baba mdogo naye akafariki, kurudi kwa bibi Bukoba, kupewa ujauzito, kuugua saratani, kukimbiwa na mwenzie kutokana na ugonjwa. Yote hiyo ni mitihani ya maisha. Hana ndugu wa kumlilia. Sisi ndio ndugu zake.

Tumchangie angalau 5M ili apate matibabu na kiasi kingine kimsaidie kujiuguza. Tuma sadaka yako kupitia M-PESA #0752581983, Tigopesa #0719744954, CRDB #0150633516500, NMB #24110012109 Gifted Hearts Foundation. RudishaTabasamu LetLoveLead.

29/01/2026

VIDEO
Kijana, raia wa Kenya akiwa vitani kupigania maslahi ya Urusi katika eneo la Donesky, mashariki mwa Ukraine. Eneo hilo kwa sasa linakaliwa na Urusi baada ya uvamizi wa Februari 2022.

Warusi, baada ya kuona vita dhidi ya Ukraine inakuwa ngumu kutokana na misaada ya kijeshi kutoka Ulaya na Marekani, waligundua vita hii itakuwa ndefu na kwahiyo walichukua hatua kadhaa;
Moja, walianza kutafuta silaha za gharama nafuu katika mataifa rafiki, hasa Iran na Korea Kaskazini. Kwahiyo, badala ya kutumia makombora ya mamilioni ya dola wakageukia drones kutoka Iran zinazogharimu dola 20,000 tu kwa kila moja.

Pili, walianza kukarabati silaha zao za zamani enzi za Sovieti ili kufidia mahitaji ya muda mrefu.

Tatu, waliitisha upya, kwa nguvu zaidi wito wa vijana kujiunga na jeshi ili kuongeza idadi ya wapiganaji.

Nne, Walianza kutumia mamluki wa kijeshi. Mfamo wa mamluki hawa ni Wagner Group. Mamluki wengi walitoka katika nchi za kiarabu za Mashariki ya Kati na Afrika.

Somo! Matukio ya dunia ya sasa yameanza kutupa ishara kwamba mataifa makubwa yanapotaka mambo yao hayaangalii sheria za kimataifa. Lakini raia wa mataifa madogo nao wamekuwa mashabiki na wafuasi wa mataifa makubwa. Hili ni kumbusho kwa mataifa madogo. Pengine kuna raia wengi wa Urusi na/au Marekani waliozaliwa Tanzania/Kenya na wanaoishi TZ, Kenya nk.
Mfano halisi ni huyu kijana wa k**enya aliyaemua kufa au kuua kwa ajili ya Urusi. Wapo watanzania pia wanaopigana huko Urusi (na kwenye vikosi vya kijeshi vya mataifa mengine ya Ulaya na Marekani).

Hii ni Wake-up call kwa mataifa madogo. Kwamba kadiri siku zinavyoenda, mipaka ya ardhi inapoteza umuhimu wake. Dunia inaendelea kukumbatiwa pamoja. Siasa zinakuwa za kidunia zaidi kuliko kitaifa. Raia wa nchi moja wanaweza kuamua kufa kwa ajili ya nchi nyingine. Vijana wanapata mbinu za kijeshi na uzoefu kutoka kwenye vita kubwa, wakati viongozi wao wa kijeshi katika nchi zao wanapata vitambi.

Ole wao serikali za mataifa madogo zinazochochea mivunjiko ya amani ndani ya nchi zao wenyewe na kufanya kila jitihada za kuwafanya vijana wasiwe wazalendo; wizi, ufisadi, dhuluma, uzembe, utekaji, mauaji na matusi kwa vijana.

Nawasilisha!
Dr. Chris Cyrilo

Nauliza!
27/01/2026

Nauliza!

Address

Zip Code 00083
Dar Es Salaam

Telephone

+255713933736

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dr. Christopher Cyrilo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Dr. Christopher Cyrilo:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category