12/01/2026
Polisi sio chanzo sahihi cha kutoa taarifa za watuhumiwa wanaopata shida vituoni. Kwanza kwa namna muundo wa jeshi la polisi ulivyo, pili ni kwa sababu chombo hiki kimeshapoteza imani kwa wananchi. Mtu mwenye akili timamu hawezi kuliamini jeshi la polisi la Tanzania. Hiki chombo ni - compromised (kimeshindwa kutimiza majukumu yake), ni corrupt (Watumishi wengi ni matapeli, wala rushwa) na ni primitive (kinafanya kazi kwa mtindo wa kale/zamani).
K**a wewe unaliamini jeshi la polisi, HUNA AKILI.
Nini kifanyike;
Kwanza, mapendekezo ya tume ya haki jinai yafanyiwe kazi (ingawa kwa sasa hakuna serikali ya kufanyia kazi hiyo). Moja ya mapendekezo ni kuvunja na kusuka upya jeshi la polisi. Hili linahitaji viongozi wengine wa kujenga taasisi ya polisi, sio hawa wa sasa waliokwisha shindwa.
Pili, hata k**a polisi ikifanyiwa mabadiliko, bado ni lazima kuwe na chombo kingine cha ulinzi na usalama ambacho kinaweza kuchunguza watumishi wa jeshi la polisi. Kwa sasa, polisi wakiua mtu wakatangaza huyo mtu ni jambazi, imeisha. Wao ndio wanajua ni jambazi, wao ndio wana ushahidi na uthibitisho. Ikitokea kuna sintofahamu basi ni polisi haohao watachunguza na haohao watatoa majibu. Kwahiyo polisi wamepewa 'all power' ya kufanya chochote bila hofu ya kuwajibika.
Tunahitaji chombo kingine kitakachofanya kazi ya kuchunguza makosa ya jinai. Hapa maana yake , ofisi ya DCI pamoja na vitengo vya Forensic ambavyo vipo ndani ya polisi vinatakiwa kutenganishwa na kuwa sehemu ya hicho combo kipya. Polisi wao watabaki na kazi ya ulinzi (kulinda raia na mali zao) na sio kazi ya kuchunguza matukio ya uhalifu kwa sababu hawawezi kujichunguza wenyewe. Maana yake, watuhumiwa wanapofia vituoni/mahabusu anayechunguza asiwe polisi.
Tayari tuna TAKUKURU kwenye uhalifu wa fedha, tuna UHAMIAJI kwenye usafirishaji haramu wa binadamu, na DCEA kupambana na dawa za kulevya, vivo hivyo tunahitaji FORENSIC BUREU kwa ajili ya kuchunguza na kukusanya ushahidi wa makosa mengine ya jinai k**a mauaji, utekaji nk.
Polisi wabaki kutoa HUDUMA ya Ulinzi na Usalama wa raia.
Hata hivyo, vyombo vyote hivi na hata hicho kipya vitapaswa kujengwa kwa misingi ya HAKI na UWAJIBIKAJI.
Nawasilisha.
Dr. Chris Cyrilo