Saikolojia akili

Saikolojia akili Ni kituo Cha masuluhisho, ni mahali sahihi pakupata ushauri wa saikolojia na ushauri wa kiroho kupitia neno la Mungu
Mawasiliano 0612001042

Tutafika tu๐Ÿคฃ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚
11/02/2026

Tutafika tu๐Ÿคฃ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

09/02/2026

VIASHIRIA HIVI NDOA INAELEKEA PABAYA ๐Ÿ‘‰๐Ÿ‘‰๐Ÿ‘‰๐Ÿ‘‰watu wengi hupitia changamoto kwenye NDOA zao hivyo inabidi kuchukua hatua ili kunusuru kuvunjika kabisa

Zifuatazo ni dalili

1. Mwenza wako hubadilika ghafla tabia bila sababu ya wazi
Unamkumbuka mume/mke wako alivyoanza mpole, mwelewa, anayesikiliza.

Lakini ghafla anakuwa mkali, anahoji kila uamuzi wako, anakataa makubaliano yenu ya zamani.

Ukichunguza kwa karibu, maneno yake hayatoi sauti yake halisi, bali sauti ya mtu mwingine.

Hapa ndipo mama mkwe, au marafiki huanza kuishi ndani ya akili ya mke wako au mume. Maana ake si akili zake Bali za kuambiwa.

2. Siri zinaanza kuingia kwenye ndoa taratibu
Mambo yaliyokuwa ya wazi sasa yanajadiliwa pembeni.

Unagundua maamuzi yanachukuliwa bila wewe kushirikishwa, lakini yanahusisha moja kwa moja maisha yenu ya ndoa.
Hapo ndoa inaanza kupasuka kimyakimya kwa sababu ndoa isiyo na uwazi hufa polepole.

3. Malalamiko ya ndugu, marafiki, mkwe yanakuwa sheria ya ndoa
Kila ukikosea kidogo, hata kisicho kosa, ghafla unahukumiwa.

Unasikia sentensi k**a, โ€œMama alisemaโ€ฆโ€, โ€œKwetu sisi hatufanyi hiviโ€ฆโ€. Badala ya maamuzi kufanywa kwa misingi ya ninyi wawili, yanaanza kufanywa kwa misingi ya kumridhisha mtu wa tatu.

Ndoa inapogeuka jukwaa la kuthibitisha utii kwa mama mkwe,rafiki au ndugu mapenzi huanza kupotea.

4. Unaanza kujiona mgeni kwenye ndoa yako mwenyewe
Unahisi k**a unaishi maisha yasiyo yako.
Huna sauti, huna nafasi ya kupendekeza, huna haki ya kukataa.

Kila kitu kinafanywa kwa hofu hofu ya kumkosea mwenza, ambaye naye ana hofu ya kumkosea mama yake.

Hii huzaa upweke wa ndoani, ambao ni uchungu zaidi kuliko upweke wa kuwa single.

5. Mwenza wako anakutetea mbele ya watu, lakini anakushambulia faraghani
Hii ni dalili kali sana.

Hadharani anaonekana yupo upande wako, lakini faraghani anakurudia kwa ukali
Hii humuumiza sana yule anayenyamaza kwa ajili ya amani.

6. Kila tatizo dogo linapanuliwa na kupewa historia ya kifamilia, kukumbushia matatizo au makosa

Hii ni kweli
07/02/2026

Hii ni kweli

Njia za kudeal na tatizo la tabia mbayaza kurithi k**a vile ulevi, wizi, uzinzi, mimba za utotoni, kukosa kuolewa, umasi...
06/02/2026

Njia za kudeal na tatizo la tabia mbaya
za kurithi k**a vile ulevi, wizi, uzinzi, mimba za utotoni, kukosa kuolewa, umasikin kutokusoma na mengine mengi

Tabia za kurithi (generational pattern)
Ni tabia / sifa ambazo hurithiwa zinaweza kuwa mbaya au nzuri.
Athari za kisaikolojia kwa mtu alierithi huonekana mapema katika utoto au baadae katika utu uzima na huendelea kurithiwa na familia na vizazi vijavyo.

ANGALIZO: endapo tu mtu ataamua kutafuta msaada ili kusaidia kuvunja mzunguko huo wa tabia za urithi basi tabia za kurithi hukoma, hupotea kuanzia kwa muathirika Hadi kizazi kijacho kitakuwa kimekombolewa

zifuatazo ni NJIA 5 ambazo mtu anaweza kufuata ili kujua na Kushughulikia tatizo la tabia mbaya za kurithi

1. Kutambua tatizo
Hapa ni kufanya mapitio ya kufahamu matatizo yanayokabili familia au ukoo kwa kuangalia ndugu, ww binafsi au watoto au wazazi. Je Kuna ulevi au umaskini nk

2. Kufatilia historia ya familia au ukoo
Mababu na mabibi, baba wakubwa au wajomba walikuwaje

3.tafakari binafsi
Je wewe binafsi umefanya au umefanyiwa jambo lolote hasi/baya ambalo linaweza kuathiri kizazi chako mfano kubakwa, kuthalilisha nk

4. Fanyia kazi uliyogundua kwa kuchukua hatua unazoamini zitafaa

5 Tafuta mtu mwenye professional ya kutatua na kukupa mwongozo namna ya kujinasua

Kwa msaada kuondokana na tatizo la tabia za kurithi na mengineyo karibu

Dk Silvano mbuya
simu 0621001042
Pia karibu ofisini tukuhudumia

MAMBO 10 YA KWELI AMBAYO TUNAJISAHAUHuu ni ukweli ambao mara nyingi tunaishi kwa kujisahau na kuona havipo lakini vipo. ...
05/02/2026

MAMBO 10 YA KWELI AMBAYO TUNAJISAHAU
Huu ni ukweli ambao mara nyingi tunaishi kwa kujisahau na kuona havipo lakini vipo. Daima ni kwa asili vipo tutake tusitake

1. Muda ni mdogo - Tuna muda mdogo tu wa kufanya mambo yote tunayotaka kufanya

2 . Sote tutakufa - Haijalishi tumefanikiwa au tajiri kiasi gani au maskini, wadhifa, cheo. hakuna kukwepa kifo.

3. Maisha hayatabiriki -
Maisha yanaweza kutuletea furaha au maumivu makubwa bila onyo kwa kutarajia au kwa gafla

4. Maana ya Mafanikio ni ya kibinafsi
- Kila mtu ana tafsiri tofauti ya mafanikio.

5. Maisha hayapo fair (usawa)--
Watu wengine huzaliwa na kupitia maisha mserereko mwingi kuliko wengine AKA kitonga au wengine hukabiliwa na magumu yasiyotarajiwa, vikwazo na changamoto za kutosha

6. Mahusiano yanapande mbili -
Kuleta furaha au kuumiza
Mahusiano na watu tunaowapenda yanaweza kuwa yenye Raha, furaha, lakini yanaweza kuwa changamoto, karaha na kuumiza.

7. Maisha ni magumu - Maisha yanatupa changamoto katika hali ngumu, na ni juu yetu kushughulikia kwa njia yenye tija na chanya.hatupaswi kukata tamaa

8. Matendo yetu yana matokeo - Kila hatua tunayochukua ina matokeo yake, yawe chanya au hasi.

9. Mabadiliko ni ya kila mara - Kila kitu kinachotuzunguka hubadilika, na ni juu yetu kuzoea na kurekebisha ipasavyo. Kushindwa kuendana na mabadiliko huleta maumivu

10. Furaha ni chaguo - Hatimaye, furaha yetu ni wajibu wetu wenyewe, na tuna uwezo wa kuchagua au la.

04/02/2026

"Kwenye maisha haya, ukitaka kuwa MTU MWENYE MAMLAKA kwenye eneo fulani au jambo fulani, hakikisha UMEJITIISHA CHINI YA MTU AU WATU WENYE MAMLAKA JUU YAKO! Mtu yeyote ambaye HANA MAMLAKA JUU YAKE ni sawa na mtu ambaye MGUU WAKE MMOJA umekanyaga GANDA LA NDIZI na MGUU WAKE WA PILI umekanyaga SAKAFU INAYOTELEZA KWA MAJI, kinachofuata ni MWELEKA KWENYE MAISHA AU JAMBO ANALOLIFANYA! Ni MPUMBAVU PEKEE anayesema ONLY GOD CAN JUDGE ME! Na ni MWEHU tu anayesema NAWAJIBIKA KWA MKE AU MUME WANGU TU! Na ni HAYAWANI PEKEE anayesema NAWAJIBIKA KWA MASHABIKI/ WAFUASI AU WASHIRIKA WANGU TU... Njia ya haraka na iliyothibitishwa ya KUHARIBIKIWA ni kujiendea mwenyewe bila SPEED GOVERNOR! K**a una mpango wa KWENDA MBALI kwenye CHOCHOTE UNACHOFANYA lazima UWE NA WATU AMBAO WAKIKUITA UNAACHA RATIBA ZAKO ZOTE KWENDA KUWASIKILIZA KWA ADABU NA UTII WA KWELI KWA NIA YA KUTENDEA KAZI"

04/02/2026

USHUHUDA:

Siku chache zilizopita kuna kijana ambaye ni mfanyakazi wa taasisi fulani alinitumia ushuhuda mzito sana.

Huyo kijana alikuwa amekaa na kifungo cha kucheza michezo hiyo ya kubahatisha kwa muda wa miaka 5.

Kabla ya kuanza kucheza michezo hiyo, alikuwa na mahusiano mazuri na Mungu, alikuwa anahudhuria sana ibada na pia alikuwa mtoaji mzuri wa sadaka.

Baada ya kuingia kwenye hiyo michezo, mahusiano yake na Mungu yakaharibika, kwenda kanisani ikawa ni ngumu na utoaji wa sadaka kanisani ukawa ni mzigo kwake.

Alikuwa akipata mshahara wake wa mwezi, anatenga kiasi cha shillingi 300,000/= hadi 500,000/= kwa ajili ya kuchezea k**ari (michezo ya kubahatisha).

Amefanya hivyo kwa miaka 5.

Alikuja kuacha baada ya kuanza maombi ya kufunga na mafundisho

Aisee chukua hatua haraka 0621001042
04/02/2026

Aisee chukua hatua haraka 0621001042

K**A WEWE NI MRAHIBU WA KUBETI NA UPO TAYARI KUACHA TUMA UJUMBE 0621001042 Nimeambiwa hawa ni WAWEKEZAJI wako kwa Ofisi ...
04/02/2026

K**A WEWE NI MRAHIBU WA KUBETI NA UPO TAYARI KUACHA TUMA UJUMBE 0621001042 Nimeambiwa hawa ni WAWEKEZAJI wako kwa Ofisi wanapambana na Muhindi/Kanjibai, ila hii kazi nayo nzito sana, utsema wako Prepo wanajiandaa na pepa

WAKATI WA TENDO LA NDOA HUPASWI KUZIMA TAA.....0621001042
03/02/2026

WAKATI WA TENDO LA NDOA HUPASWI KUZIMA TAA.....0621001042

03/02/2026

UTATA KUHUSU HARUFU YA MVUA
Mdau mmoja anauliza je ni kweli mvua hunukia kabla ya kunyesha na je k**a ni kweli Nini husababisha hiyo HARUFU
Anasema yeye hajawahi hisi.

Address

Dar Es Salaam
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Saikolojia akili posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category