05/04/2019
HORMONAL IMBALANCE (KUBADILIKA KWA VIWANGO VYA HOMONI)
Hormonal imbalances hutokea endapo kuna kiwango kikubwa au kidogo (kupungua) cha homoni katika damu. Homoni ni muhimu sana katika mwili, hata kiwango kidogo kikipungua au kuongezeka kinaweza kusababisha madhara katika mwili.
Homoni husaidia mwili kufanya kazi zake vizuri. Husaidia kupunguza (regulate); mmeng'enyo wa chakula na hamu ya kula, Mapigo ya moyo, Kulala, Kuzaa na viungo vy uzazi, Ukuaji wa mtu, Kutunza joto la mwili, n.k
Wanawake na Wanaume hawafanani matatizo yao ya hormonal imbalance. Wanaweza kusubuliwa katika nyongo, steroids, homoni za ukuaji na adrenalini
Wanawake wanaweza pia kusumbuliwa na tatizo hili hasa kwa homoni za estrogeni na progesteroni, wakati wanaume mara nyingi wanasumbuliwa na homoni ya testosteroni.
DALILI ZA HORMONAL IMBALANCE
Dalili za tatizo hili hutegemea na mtu anayeumwa na pia aina ya gland (kizalisha homoni) yenye matatizo. Dalili zake zinaweza kua, kuongezeka au kupungua uzito, kutokwa na jasho mara kwa mara bila kutarajia au bila kazi, kulala kwa tabu, kubadilika kwa msukumo wa damu (blood pressure), kubadilika kwa kiwango cha sukari mwilini, mwili kuchoka sana, kiu kali, msongo wa mawazo, kiu kali, kupoteza uwezo wa kuona n.k
kwa wanawake mara nyingi hua inatokea wakati wa mimba. pia hutokea wakati wa kubalehe, hedhi kunyonyesha, kuzaa, menopause.
VYANZO VYA TATIZO
Kila mtu anaweza kutokewa na tatizo hili mara moja katika sehemu ya maisha yake. Hili tatizo linaweza kutokea endapo gland (sehemu ambayo homoni huzalishwa) zilizopo ndani ya mwili hazifanyi kazi vizuri.
Baadhi ya matibabu au dawa zinaweza kusababisha tatizo hili (Vidonge vya kuzuia mimba) au aina fulani ya maisha na mazingira pia yanaweza kusababisha tatizo hili
Vyanzo vinaweza kua; msongo wa mawazo, kisukari aina ya 1 na 2, kutokula mlo kamili, kua na uzito mkubwa, kupungua au kuongezeka kwa homoni za glucagoni na parathyroid, vidonge vya uzazi, kansa za gland, sumu mbalimbali (dawa za wadudu na wanyama)
MATIBABU
Matibabu yake yanategemea na aina ya hormonal imbalance ambayo mtu anaumwa.
1. Metformin (kwa aina ya 2 ya kisukari) au Levothyroxine. ni dawa anazoweza kupewa mgonjwa mwenye hormonal imbalance
2. Mwanamke anaweza kupewa vidonge vya homoni (estrogen na progesterone), vitanzi au vifaa vya kupitisha njia ya mkojo hasa wakati wa ujauzito.
2. Kukauka kwa sehemu za siri, mgonjwa anaweza kupewa mafuta (cream) ambayo ina estrogen
3. Mwanamke anaweza kupewa Anti-androgen. Ni matibabu ambayo huharibu homini za kiume kwa mwanamke hasa androgen.
Pia watu hutumia njia za asili k**a karafuu nyekundu, kupunguza vyakula vya sukari na wanga, kula mlo kamili, kupunguza au kuzuia msongo wa mawazo