12/04/2026
WANAANGA JINSI WALIVYOUZUNGUKA MWEZI NA KUPATA PICHA ZA KIPEKEE ZA DUNIA
Misheni ya pili ya Shirika la Taifa la Marekani la Usafiri wa Anga na Anga za Juu yaani National Aeronautics and Space Administration (NASA) ya Safari ya wanaanga kwenda karibu na Mwezi inatarajiwa kuhitimishwa alfajiri ya leo Jumamosi tarehe 11 April 2026
Ni safari inayofahamika k**a Artemis II ikiwa ni misheni ya pili katika mpango wa NASA wa Artemis.
Safari hiyo ya Artemis II imewawezesha wanaanga kurudia karibu na Mwezi baada ya zaidi ya miaka 50 kwani Disemba 1972 chombo cha Apollo 17 ilifanikiwa kupeleka katika mwezi binadamu kwa mara ya mwisho Mwezini.
Chombo cha Orion kilirushwa kutoka Kennedy Space Center, Florida tarehe 1 Aprili 2026.
Misheni yote imechukuwa takriban siku 10,na wanatarajiwa kurejea duniani kwa kutua baharini tarehe 11 Aprili 2026 .
Kasi ya chombo hicho cha Orion ambacho kwa asilimia kubwa kinaendeshwa kutoka ardhini katika makao makuu ya NASA ni kati ya kilometa 27,000 mpaka 40,000 kwa saa moja.
Chombo hicho ambacho kitaanza safari ya kurejea dunia majira ya saa 8 usiku kinatarajiwa kutua katika bahari ya Pasific kati ya saa 9 na 9.30 usiku.
Chombo cha Orion kilifanya "translunar injection burn" na kuelekea Mwezini na kufika kwenye eneo ambalo uvutano wa Mwezi una nguvu zaidi tarehe 5 April 2026 kisha kupita upande wa nyuma wa Mwezi tarehe 6 Aprili 2026.
Ndani ya chombo cha Orion kuna wanaanga wanne ambapo mmoja wao ni mwanamke.
LENGO LA SAFARI
Ni jaribio la wanaanga wanaofanya utafiti wa mifumo ya ardhini na pia tafiti za kisayansi kuhusu afya na jinsi mwili wa binadamu unavyoathiriwa na safari ndefu angani, mionzi, usingizi, na kinga ya mwili.
MATUKIO MUHIMU
01. Wakati wakipita karibu na Mwezi tarehe 6 Aprili, walipiga picha za upande wa nyuma wa Mwezi ambazo binadamu hajawahi kuuona moja kwa moja.
02. Safari iliwawezesha kupita takribani kilometa 6,600 kutoka uso wa Mwezi. kwa kifupi Artemis II ni jaribio la maandalizi ya wanaanga kabla ya Artemis III ambayo binadamu wataweza kutua Mwezini.
03. Safari hiyo inathibitisha kuwa teknolojia iko tayari kwa safari ndefu za binadamu kwenda Mwezini na baadaye kwenye sayari ya Mars.
04 Chombo cha Orion mnamo tarehe 3 Aprili 2026, kilipiga "selfie" angani kwa kamera iliyofungwa kwenye paneli zake za sola.
05. Mnamo tarehe 4 Aprili 2026, mwanaanga alionekana kupitia dirishani mwa Orion huku akiangaziwa na mwanga wa screen ndani ya chombo chenye giza.
06. Mnamo tarehe 6 Aprili 2026, Picha ya upande wa nyuma wa Mwezi. Ni sehemu ambayo hatuoni kamwe kutoka Duniani.
SAFARI YA KUREJEA DUNIA
Baada ya kupita Mwezini kihistoria tarehe 6 Aprili 2026, wanaanga wa Artemis II waliamka na kujiandaa kwa safari ya kurudi Duniani.
HUDUMA ZA KUJISAIDIA
Wanaanga kwenye Artemis II katika kujisaidia wanatumia choo maalumu cha angani kinachoitwa Universal Waste Management System (UWMS).
Ni mfumo wa kisasa wa kuvuta taka bila mvuto wa ardhini.
01. Haja ndogo: Kila mwanaanga ana funnel yake binafsi inayounganishwa na bomba. Badala ya maji, hewa inavuta mkojo kwenda kwenye mfumo. Mkojo unatibiwa kemikali kisha unatupwa angani mara chache kwa siku.
02. Haja kubwa: Wanaanga wanatumia kiti kidogo sana kwa usahihi. Haja kubwa inavutwa na hewa kuingia kwenye mfuko unaoweza kufungwa. Mifuko hiyo uhifadhiwa kwenye kontena maalumu na kurudishwa duniani baada ya misheni.
03. Faragha: Kwa mara ya kwanza tangu Apollo 17, Artemis II ina choo chenye mlango. Lakini wanaanga ni lazima wajifunge kwa kamba miguuni ili wasiruke na kuelea wakati wanajisaidia na lazima wavae vizibo masikioni kwa sababu feni za chombo zinapiga kelele sana.
04. Changamoto: Siku chache baada ya kurushwa mnamo tarehe 1 Aprili 2026, choo cha Orion kiliharibika mara 2.
Siku ya kwanza Pampu haikupata maji ya kutosha kuanzisha mfumo. Mmoja ya wanaanga akawa fundi wa choo angani na kukirekebisha.
Lakini siku ya tatu mkojo uliganda na ukazuia bomba la kutupa taka nje. Waongozaji wa misheni wakaizungusha Orion ili jua liyeyushe barafu, na ikafunguka kwa sehemu. Pia kulikuwa na harufu ya ajabu kutoka chooni.
JE WALIJISAIDIAJE ?
Chombo hicho wakati wa dharura, wanaanga walitumia mifuko ya dharura unaokunjuka "emergency bag".Kila mwanaanga ana mifuko 2 ya akiba.
Choo cha Artemis II kiligharimu dola za Marekani milioni 23
HUDUMA YA CHAKULA
Wanaanga wa Artemis II hawapiki chakula kwani kila kitu kimepikwa na kukausishwa wakiwa Duniani.
AINA YA VYAKULA
Aina ya vyakula ni pamoja na nyama ya kuku, pasta, supu.
Wanapoitaji kula wanamwaga maji ya moto au baridi kwenye mfuko, wanasubiri dakika chache, kisha wanakula kwa kijiko chenye sumaku ili kisiruke, kuelea na kuanza kuzunguka ndani ya chombo.
Vingine ni Vyakula vikavu k**a Biskuti, karanga, matunda yaliyokaushwa k**a vitafunwa.
Vinywaji k**a Kahawa, chai, juice ya machungwa, vyote ni unga unaochanganywa na maji kwenye mfuko maalumu wenye mrija wa kunywea.
CHANGAMOTO YA KULA
01. Hakuna harufu : Angani pua uziba kidogo, hivyo chakula hakina radha sana.
02. Changamoto ya chakula kuruka na kuelea mfano k**a kipande cha mkate kikiruka, kinaweza kuingia kwenye kifaa na kusababisha moto. Hivyo wanakula kwa uangalifu ndani ya "tray" yenye sumaku.
03. Maji ni adimu : Maji yote yanatengenezwa kwa kurecycle mkojo na jasho, kwa hiyo hawayamwagi.
HUDUMA YA KULALA
Wanaanga hao hawalali kitandani kwani angani hakuna juu wala chini
JINSI YA KULALA
01. Mifuko ya kulalia : Kila mwanaanga ana mfuko wake unaofanana na "sleeping bag" uliofungwa ukutani kwa kamba. Wanaingia ndani ili wasiruke ruke usingizini na kuelea chomboni.
02. Kuziba masikioni: Orion inapiga kelele za mashine na feni saa 24. Lazima wavae vizibo masikioni au wasilale.
03. Kufunika macho : Jua linachomoza kila dakika 45 kwa sababu wanazunguka Dunia kwa kasi. Wanaanga wanafunga madirisha na kuvaa kitambaa machoni.
04. Kujifunga: Lazima wajifunge mikanda kiunoni na miguuni. K**a wasipojifunga, wanaweza kuamka wako darini au kugonga vifaa vibaya.
MAFANIKIO YA ARTEMIS II
01. Maajabu ya kuuona Mwezi kwa karibu kwani tarehe 6 Aprili 2026 walipita kilometa 6,600 tu kutoka uso wa Mwezi ambapo ni karibu mara 60 zaidi ya ndege ya kawaida kutoka Duniani.
02. Wanaanga waliweza kupiga picha za upande wa mwezi ambao hatuoni kamwe kutoka Duniani ukiwa umewaka kabisa kwa mwanga wa jua
03. Waliweza kupiga picha ya Dunia ikiinuka juu ya upeo wa Mwezi. Ni binadamu wa kwanza kuona tukio hili kwa macho tangu 1972
04. Ukanda mwembamba wa Dunia. Waliweza kuuona "ukanda mwembamba unaong'aa gizani" — mstari wa jua ukigusa Dunia kutoka umbali wa zaidi ya kilometa 380,000
UGUNDUZI WA KISAYANSI
Ugunduzi wa kisayansi kuhusu mwili wa binadamu kwani safari ya Artemis II ilikuwa ni maabara inayoruka. Walifanya tafiti hizi kwa mara ya kwanza nje ya ulinzi wa uga wa sumaku wa Dunia:
01. ARCHeR : Walifuatilia usingizi, shughuli na ustawi wa wanaanga. Waligundua kuwa angani usingizi unavurugika zaidi kwa sababu hakuna usiku wala mchana wa kawaida
02. AVATAR : Walichukuwa viungo-vidogo kwenye-chip, tishu bandia za moyo, figo na mapafu — kupima jinsi mionzi na ukosefu wa mvuto unavyoharibu seli
03. KINGA YA MWILI: Sampuli za damu na mate za wanaanga zinaonyesha jinsi kinga ya mwili inavyodhoofika haraka sana anga za mbali
04. MIONZI: Vifaa vya Orion vilipima viwango vya mionzi ndani na nje ya chombo. Hii inasaidia kubuni ngao bora za misheni ya kwenda katika sayari ya Mars
05. PICHA: Picha walizopiga zitatumika kupanga sehemu za kutua za Artemis III mwaka 2027.
Kwa kifupi: Artemis II siyo tu kupita Mwezini. Ni kuchukua vipimo vya jinsi binadamu atakavyovumilia safari ya miezi 9 kwenda katika sayari ya Mars.
MALENGO YA MISHENI ZA ARTEMIS
NASA inapanga misheni za Artemis kwa mpangilio huu:
01. Artemis I – 2022: Jaribio bila wanaanga, kuzunguka Mwezi
02. Artemis II – 1 Aprili 2026: Wanaanga kuzunguka Mwezi, k**a ilivyoendelea sasa
03. Artemis III – 2027: Kutua Mwezini tena kwa mara ya kwanza tangu 1972. Artemis III imepangwa kumpeleka mwanamke wa kwanza na mwanaanga kutoka Afrika wa kwanza mwezini.
04. Artemis IV, V - 2028 na kuendelea: Kujenga kituo cha kudumu Mwezini na kujiandaa kwenda sayari ya Mars
NOTE: USIKOSE SEHEMU YA PILI YA CHANGAMOTO ZA AJABU ZILIZOPO ANGA LA JUU