MNH-Mloganzila

MNH-Mloganzila Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from MNH-Mloganzila, Medical and health, Kibamba, Dar es Salaam.

14/04/2026

Fahamu kuhusu homa ya rheumatic na ugonjwa wa moyo wa rheumatic.

Ungana na Daktari Bingwa Bobezi wa Magonjwa ya Moyo kwa watoto,Dkt. Grace Ng’waida, kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila.

13/04/2026
11/04/2026

Fahamu hatua za ukuaji kwa mtoto aliezaliwa kabla ya wakati.

Ungana na Daktari Bingwa wa Watoto, Dkt. Lucy Mpayo kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila kwa ufafanuzi zaidi.

10/04/2026

Je! Unafahamu lishe muhimu kwa mgonjwa alieungua?

Ungana na Bw. Abubakari Abushiri, Afisa lishe kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili - Mloganzila kwa ufafanuzi zaidi.

MAFUNZO YA USIMAMIZI WA RASILIMALI WATU YAFUNGULIWA MUHIMBILI-MLOGANZILANaibu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ...
09/04/2026

MAFUNZO YA USIMAMIZI WA RASILIMALI WATU YAFUNGULIWA MUHIMBILI-MLOGANZILA

Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila, Dkt. Julieth Magandi amefungua mafunzo ya namna ya kusimamia rasilimali watu kwa lengo la kuwaongezea uelewa na ujuzi wa kisasa katika usimamizi bora wa watumishi.

Mafunzo hayo ya siku mbili yamehusisha washiriki kutoka idara mbalimbali hospitalini hapo, ambapo Dkt. Magandi ameeleza kuwa mafunzo hayo ni muhimu katika kuboresha utendaji kazi na kuongeza tija kwa wafanyakazi.

Amefafanua kuwa uwekezaji katika rasilimali watu ni msingi wa mafanikio ya taasisi yoyote, hivyo ni vyema washiriki wakayachukulia kwa uzito huku akisisitiza umuhimu wa kujifunza mbinu mpya za usimamizi zitakazosaidia kuleta mabadiliko chanya katika mazingira ya kazi.

08/04/2026

“Epuka dhana potofu kuhusu ugonjwa wa kifafa, tembelea vituo vya afya kwa uchunguzi na matibabu zaidi”.

Dkt. Brighton Mushengezi,
Daktari Bingwa Bobezi wa Ubongo na Mishipa ya Fahamu,
Hospitali ya Taifa Muhimbili -Mloganzila.

04/04/2026

Fahamu umuhimu wa madini chuma mwilini.

Ungana na Bw. Charles Massawe, Afisa Lishe kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila akifafanua zaidi.

MUHIMBILI–MLOGANZILA YAPOKEA MASHINE YA (G-BREATHE NA CPAP)YA KUMSAIDIA MTOTO KUPUMUA Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloga...
02/04/2026

MUHIMBILI–MLOGANZILA YAPOKEA MASHINE YA (G-BREATHE NA CPAP)YA KUMSAIDIA MTOTO KUPUMUA

Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imepokea kifaa cha kisasa cha kusaidia upumuaji (G-Breathe n CPAP kwa ajili ya watoto wachanga, kilichotolewa na kampuni ya Gina Medical Limited kwa lengo la kuendelea kuboresha matibabu ya watoto.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo,kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa MNH, Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Tiba Dkt. Elineema Meda ameeleza kuwa upatikanaji wa vifaa tiba vya kisasa ni hatua muhimu katika kuboresha sekta ya afya na kuokoa maisha.

Kwa upande wake Muwakilishi wa Kampuni hiyo Mhandisi Bonaventure Kitalonja amesema kampuni hiyo imeamua kushirikiana na taasisi za afya ili kuboresha huduma za matibabu nchini hasa kwa makundi yenye uhitaji mkubwa k**a watoto wachanga.

Mashine ya CPAP ina uwezo wa kusaidia watoto wachanga wenye matatizo ya mapafu kupumua kwa urahisi zaidi bila kuhitaji huduma za hali ya juu zaidi, hatua hiyo inatarajiwa kuleta mabadiliko chanya katika matibabu ya watoto na kupunguza changamoto zinazowakabili wahudumu wa afya katika kuwahudumia wagonjwa hao.

01/04/2026

“Wauguzi mnatakiwa kuleta mabadiliko chanya katika sekta ya Uuguzi na Ukunga kwa kuzingatia weledi, ubunifu na kujituma katika majukumu yenu”.

Dkt. Delilah Kimambo, Mkurugenzi Mtendaji Hospitali ya Taifa Muhimbili.

01/04/2026

“Wauguzi tunatakiwa kujivunia kwa taaluma yetu na juhudi kubwa tunazozifanya katika kuwahudumia wagonjwa”.

Dkt. Ezekiel Mbao, Rais wa Chama Cha Wauguzi Tanzania (TANNA).

01/04/2026

“Wauguzi mnatakiwa kufanya kazi kwa ushirikiano na kuendelea kuzingatia maadili ya taaluma yenu pamoja na kanuni za Utumishi wa Umma ili kuhakikisha mnatoa huduma bora”.

Bi. Ziada Sellah, Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi na Ukunga Tanzania.

Address

Kibamba
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MNH-Mloganzila posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to MNH-Mloganzila:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram