Navan Fertility Clinic

  • Home
  • Navan Fertility Clinic

Navan Fertility Clinic Navan Medical Care is dedicated to:-
OBGYN Consultation | Antenatal Care | Postnatal Care | Fertili

Wanawake wenye umri wa CHINI YA MIAKA 35 wanashauriwa kutafuta msaada wa kitaalamu baada ya miezi 12 ya kujaribu kupata ...
28/07/2025

Wanawake wenye umri wa CHINI YA MIAKA 35 wanashauriwa kutafuta msaada wa kitaalamu baada ya miezi 12 ya kujaribu kupata ujauzito bila mafanikio.

Wanawake wenye umri wa miaka 35+ wanashauriwa kutafuta msaada wa kitaalamu baada ya miezi 6 ya kujaribu bila mafanikio. ...
28/07/2025

Wanawake wenye umri wa miaka 35+ wanashauriwa kutafuta msaada wa kitaalamu baada ya miezi 6 ya kujaribu bila mafanikio. Kila mwezi ni nafasi muhimu.

USIKATE TAMAA – SAFARI YA UZAZI INAWEZEKANA! Changamoto za uzazi ni safari ya kipekee inayohitaji subira, matumaini na h...
25/07/2025

USIKATE TAMAA – SAFARI YA UZAZI INAWEZEKANA!

Changamoto za uzazi ni safari ya kipekee inayohitaji subira, matumaini na hatua sahihi. Kwa wale wote ambao mmekuwa mkipambana kwa muda mrefu kutafuta watoto bila mafanikio, msikate tamaa!

Tumaini ni msingi wa mafanikio katika safari ya kupata watoto. Haijalishi upo kwenye hali gani au umepitia changamoto kiasi gani – kumbuka, kila hatua ni fursa mpya ya matumaini.

Kabla ya kuanza matibabu, ni muhimu kujua sababu halisi ya changamoto za uzazi. Uchunguzi wa kina wa afya ya uzazi wa mwanamke na mwanaume ndio msingi wa kupokea tiba sahihi.

Njia sahihi zipo – kuanzia vipimo vya kitaalamu, tiba za kimaumbile, hadi teknolojia za kisasa k**a IVF na mbinu nyingine za matibabu.

Ujumbe wangu kwako leo:
* Usipoteze tumaini kwa sababu changamoto ni sehemu ya safari ya ushindi.
* Fanya uchunguzi wa kina ili ujue kikwazo halisi.
* Tafuta msaada wa kitaalamu kwa wakati.

Hakuna sababu ya kukata tamaa mpaka kieleweke!
Afya ya uzazi ni maisha – na maisha ni zawadi.

Kwa wastani, nafasi ya kupata mimba kwa kila mzunguko wa IVF ni 30% hadi 60% — ikitegemea umri wa mwanamke, ubora wa may...
21/07/2025

Kwa wastani, nafasi ya kupata mimba kwa kila mzunguko wa IVF ni 30% hadi 60% — ikitegemea umri wa mwanamke, ubora wa mayai, viinitete, hali ya mfuko wa mimba na afya ya mbegu za mume.
Hii ndiyo sababu vipimo vya awali ni muhimu kabla ya kuanza IVF.

Kazi Ninayoipenda kwa Moyo Wangu Mimi ni Dkt. Albert Robert, daktari bingwa wa afya ya uzazi na tiba za changamoto za uz...
17/07/2025

Kazi Ninayoipenda kwa Moyo Wangu

Mimi ni Dkt. Albert Robert, daktari bingwa wa afya ya uzazi na tiba za changamoto za uzazi. Kazi ninayoifanya kwa moyo wa dhati na furaha isiyoelezeka ni kuwasaidia wenza wenye changamoto za uzazi kupata zawadi ya kuwa wazazi.

Kila siku ninakutana na wanawake na wanaume waliokata tamaa, lakini tunapoweka mikono yetu pamoja, kupima, kutibu na kuwatia moyo—kisha nikathibitisha kwamba mama amepata ujauzito, moyo wangu hujaa furaha isiyoelezeka.

Kwa kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito, ninamfuatilia mama kwa karibu sana, kuhakikisha mimba inakua salama, mama yuko na afya njema, na ujauzito unaendelea vizuri.

Baada ya hapo, nampa mama ruhusa ya kuendelea na kliniki ya ujauzito kwa madaktari wenzangu hadi siku ya kujifungua. Lakini moyo wangu hubaki ukiomba baraka kwao hadi mtoto atakapozaliwa salama.

Kile ninachopenda zaidi ni kuwasaidia washike mimba. Nikifanikiwa kwenye hilo, nafsi yangu hutulia. Najua nimefanya jambo chanya kwa familia yao na kwa jamii kwa ujumla.

Kwa kila ujauzito unaopatikana kupitia msaada wangu, si tu matibabu, bali pia sala, maombi na moyo wa kujitoa, najua kwamba hii ndio kazi ya maisha yangu.

Najivunia kuwa sehemu ya safari ya uumbaji wa maisha mapya. 😁

UMUHIMU WA KUJUA AKIBA YA MAYAI WAKATI WA KUTAFUTA MTOTO Wanawake huzaliwa na idadi ya mayai ambayo hupungua hatua kwa h...
14/07/2025

UMUHIMU WA KUJUA AKIBA YA MAYAI WAKATI WA KUTAFUTA MTOTO

Wanawake huzaliwa na idadi ya mayai ambayo hupungua hatua kwa hatua kadri umri unavyosonga mbele. Tofauti na wanaume wanaozalisha mbegu kila siku, wanawake hawazalishi mayai mapya maishani, mayai waliyonayo ni yale yale tangu kuzaliwa.

Lakini kwa nini ni muhimu kufahamu akiba ya mayai (egg reserve) unapojaribu kupata watoto?

1. KUKUJULISHA HALI HALISI YA UZAZI WAKO

Vipimo vya akiba ya mayai k**a AMH na AFC kupitia ultrasound hutoa picha kamili ya:

* Akiba ya mayai kwenye ovari zako
* Uwezekano wa kupata mimba kwa njia ya kawaida au kwa matibabu k**a IVF
* Umuhimu wa kuchukua hatua mapema kabla akiba haijamalizika kabisa

2. KUSAIDIA KUCHAGUA NJIA SAHIHI YA MATIBABU MAPEMA

Kuna wanawake wengi wanachelewa kutafuta msaada kwa sababu hawajui kuwa akiba yao ya mayai iko chini, mpaka wapate changamoto kubwa k**a:
* Kushika ujauzito kunakuwa kugumu
* Kukosa vipindi vya hedhi

Kwa kujua akiba yako mapema, daktari anaweza:
✅ Kukushauri kuanza matibabu mapema
✅ Kupendekeza kuhifadhi mayai (egg freezing) au viinitete
✅ Kukushauri njia bora za kupata watoto k**a IVF au kutumia mayai ya kuchangiwa

3. UMRI UNAVYOSONGA, UBORA NA IDADI YA MAYAI HUPUNGUA

Wanawake wengi hufikia kilele cha ubora wa mayai kati ya miaka 25 hadi 32. Baada ya hapo:
* Idadi ya mayai hupungua kwa kasi
* Ubora wa mayai hushuka na kuleta matatizo ya mimba kutoka

4. INAKUPA NGUVU YA KUCHUKUA HATUA KWA MUDA SAHIHI

Kufahamu akiba yako ya mayai ni k**a kupima mafuta ya gari kabla ya safari—inakusaidia kupanga, kuchukua hatua, na kujiepusha na msongo wa mawazo unaotokana na kutokujua.

UJUMBE

K**a wewe na mwenza wako mnahangaika kupata watoto, msikate tamaa. Dunia ya sasa ina teknolojia na matibabu ya hali ya juu ambayo yanaweza kusaidia. Na hatua ya kwanza ni kupima na kujua hali yenu ya uzazi.

Mapema ni bora kuliko baadae. Afya ya uzazi huanza kwa kujitambua.

Je, unajua mirija yenye maji (hydrosalpinx) huweza kuzuia mimba? Usikimbilie kupandikiza viinitete bila kujua hali ya mi...
13/07/2025

Je, unajua mirija yenye maji (hydrosalpinx) huweza kuzuia mimba? Usikimbilie kupandikiza viinitete bila kujua hali ya mirija! Uchunguzi wa mirija kwa HSG ni hatua ya kwanza muhimu. Hydrosalpinx hupunguza mafanikio ya IVF.
Chukua hatua mapema kwa mafanikio ya baadae!

Hedhi ikikoma siyo ndoto yako ya uzazi ife pia!Kwa njia ya IVF na teknolojia za kisasa, wanawake wengi waliofikia menopa...
12/07/2025

Hedhi ikikoma siyo ndoto yako ya uzazi ife pia!
Kwa njia ya IVF na teknolojia za kisasa, wanawake wengi waliofikia menopause wanapata watoto salama. Unaweza kuwa mmoja wao.

Wewe Ni Malkia, Umri Sio Kikwazo.,Umri ni namba tu! IVF inawaruhusu wanawake waliokoma hedhi kuanzisha au kuendeleza fam...
11/07/2025

Wewe Ni Malkia, Umri Sio Kikwazo.,
Umri ni namba tu! IVF inawaruhusu wanawake waliokoma hedhi kuanzisha au kuendeleza familia wanayoiota. Ukitamani kuwa mama, njia ipo!

09/07/2025

USIKATISHWE TAMAA! Wenza wengi wanaopitia changamoto ya uzazi wamefanikiwa kupata watoto kupitia matibabu ya IVF, na wen...
09/07/2025

USIKATISHWE TAMAA!

Wenza wengi wanaopitia changamoto ya uzazi wamefanikiwa kupata watoto kupitia matibabu ya IVF, na wengi hufanikiwa katika mzunguko wa kwanza tu!

Siri kubwa ya mafanikio iko katika:
✅ Maandalizi bora ya mwili na akili kwa wenza wote wawili
✅ Kufuata ushauri wa kitaalamu na miongozo sahihi ya matibabu
✅ Kuwa na imani na kutokata tamaa

Usiruhusu hofu, presha, au maneno ya watu yakuvunje moyo.

IVF ni njia salama na ya kisayansi yenye mafanikio makubwa – endapo maandalizi na matibabu hufanyika kwa usahihi.

Safari yako bado ina matumaini. Tazama mbele kwa imani!

Wanawake wenye changamoto ya PCOS huweza kushika ujauzito kwa njia ya kawaida kwa msaada wa kitaalamu.,
08/07/2025

Wanawake wenye changamoto ya PCOS huweza kushika ujauzito kwa njia ya kawaida kwa msaada wa kitaalamu.,

Address


Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00
Saturday 08:00 - 17:00

Telephone

+255757000400

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Navan Fertility Clinic posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Opening Hours
  • Alerts
  • Contact The Practice
  • Claim ownership or report listing
  • Want your practice to be the top-listed Clinic?

Share