YOUR Health Matters Coaching

YOUR Health Matters Coaching "Tunakusaidia kupata elimu ya afya, pia utatuzi wa matatizo ya Uzazi na magonjwa Sugu kupitia Tiba l

Je,
Ulishawahi kuugua au kujisikia vibaya katika afya yako na hujui nini sababu? Uko mbali na unatamani angalau uweze kuongea na daktari aweze kukusaidia ushauri wa kitabibu na hujui wapi pa kumpata? Unayo simu na unatamani uwe na rafiki daktari ili aweze kukupatia ushauri wa kitabibu wakati unapohitaji? Usihangaike YOUR HEALTH MATTERS COACHING inakuwezesha kuongea na daktari kupitia simu yako ya

mkononi. Unachohitaji ni wewe kutuma ujumbe wa SMS/ WhatsApp kupitia namba zetu +255789699225 Dr Sam na kuzungumza na daktari kila mara, na pindi unapohitaji msaada wa haraka zaidi.

21/02/2023
29/04/2022

Hii ndio maana ya Big Baby

Mtoto anapozaliwa na u*ito wa zaidi ya kilo nne (4kg) inasemwa kwamba huyo mtoto ni mkubwa. Hata hivyo hatari huongezeka zaidi mtoto anapozaliwa na zaidi ya kilo nne na nusu(4.5kg), wataalam wenyewe wanaita Macrosomia.

Sababu kubwa zinazosababisha mtoto kuzaliwa mkubwa ni
1.Sababu za kurithi. Mama anapoongezeka u*ito mkubwa wakati wa ujau*ito inawezekana akajifungua mtoto mwenye u*ito mkubwa
2.Ugonjwa wa Kisukari. Ugonjwa wa Kisukari ndio sababu kubwa ya mama kuzaa mtoto mkubwa
3. Mara chache mtoto anakuwa na ugonjwa ambao unamfanya awe mkubwa akiwa tumboni

Kinyume na watu wengi wanavyofikiria kuzaa mtoto mkubwa ni sifa, kitaalam sio salama. Mtoto mkubwa anafanya mama kuwa katika hatari kubwa ya kujifungua kwa njia ya upasuaji. Pia inaongeza hatari ya mtoto kuumia wakati wa kuzaliwa. Madhara mengine ni pamoja na mama kuvuja damu nyingi au mfuko wa uzazi kupasuka
-
Wewe ulipojifungua mwanao alikuwa na kilo ngapi..!? Tushare experience kwa pamoja kwa Mama wanaokuja 🤰🏽🤱

Faida za kutumia mayai kwenye kifungua kinywa.1. Huongeza Shibe,  protein iliyopo katika mayai humfanya mtu kukaa muda m...
25/04/2022

Faida za kutumia mayai kwenye kifungua kinywa.

1. Huongeza Shibe, protein iliyopo katika mayai humfanya mtu kukaa muda mrefu Bila kusikia njaa tofauti na vyakula vyengine k**a bidhaa za ngano

2. Chanzo kikubwa Cha protein.,
Mayai Yana kiasi kikubwa Cha Amino Acid, ambazo huupa mwili kiasi kikubwa Cha protein.

3. Hulinda macho., Kemikali Aina ya Leutin, na zeaxanthin zinaaminika kulinda macho dhidi ya mionzi mikali . Pia husaidia kuepuka tatizo la mtoto wa jicho kwa wazee

4. Huimarisha afya ya ubongo, kurutubisho Aina ya "Choline" ambacho hupatkan katika ubongo husaidia kuimarisha ubongo na kuweka kumbukumbu sawa.

👉🏽 Ovulation test kit.Hizi anaweza kutumia mwanamke yeyote anaehitaji kushika mimba lakini huwafaa zaidi wanawake ambao ...
24/04/2022

👉🏽 Ovulation test kit.
Hizi anaweza kutumia mwanamke yeyote anaehitaji kushika mimba lakini huwafaa zaidi wanawake ambao wanataka kupata mimba ambao;

● Mizunguko yao haieleweki yaani sio rahisi kupiga hesabu na kujua siku zao za hatari ni zipi.

● Umetafuta mimba muda mrefu hupati na hata ukipimwa unaambiwa huna shida yeyote.

● Uko bize sana na kazi kiasi kwamba huwez kutulia na kufuatilia siku zako.

● Mme wako au mpenzi wako muda mwingi hauko naye hivyo sio rahisi kulala naye mara kwa mara

● Unataka mtoto haraka.

Ni rahisi sana kukitumia na kujipima mwenye.
Ukimaliza kuona siku zako za hedhi, chukua kipimo kimoja kila siku kisha kikojolee au chukua mkojo kwenye chupa ndogo kisha tumbukiza k**a vile unavyopima mimba kisha angalia majibu,

Endelea kupima kila siku mpaka uone hedhi nyingine, k**a siku zako za hatari zifika kipimo kitaonyesha mistari miwili k**a siku zako hazijafika kipimo kitaonyesha mstari mmoja,

kutokana na matatizo mbalimbali ya uzazi unaweza usione siku zako za hatari mwezi huo hivyo unaweza kuendelea kujaribu miezi mingine lakini asilimia kubwa siku zako hu*iona baada ya kutumia kwa mzunguko mmoja tu.

Kumbuka, kipimo hichi kinatakiwa kisomwe ndani ya dakika kumi, na muda wa kupima ni saa nne asubuhi mpaka saa mbili usiku, usipime haraka baada ya kuamka kwani homoni hizi huchelewa kuongezeka mwilini baada ya kuamka, usinywe maji mengi sana kabla ya kipimo kwani mkojo utakua mwepesisana na kushindwa kusoma majibu.

Vipimo Vinapatikana Kwetu Kwa Bei Nafuu Sana, Kwa Elfu 20 tu!


*ito

MAMA MJAMZITO FANYA HAYA KILA SIKU1: Kunywa maji mengi 2. kula matunda na mboga za majani kwa Wingi3. Pata Muda wa kupum...
23/04/2022

MAMA MJAMZITO FANYA HAYA KILA SIKU

1: Kunywa maji mengi
2. kula matunda na mboga za majani kwa Wingi
3. Pata Muda wa kupumzika
4. Relax, usiwe mtu wa kuwa na stress,hasira kutukana..Mwanao anasikia😁 na unamfundisha tabia mbaya

5. kula vitu vyenye faida KIAFYA,vinampa mtu madini,ma Omega 3 k**a yote uzae mtoto mwenye Akili(samaki,vitutubisho vyenye Haya madini),vyakula vya Calcium k**a Samaki,dagaa na Virutubishi Mfano Pregnacare,prenatal etc mtoto anakuwa na mifupa ina nguvu imara...usile kujifurahisha tu,kula vitu vitamjenga mtoto afya
Vyakula vya protein vinamfanya mwanao apate pate misuli azaliwe ana Afya

6. Fanya mazoezi mepesi Mepesi,kuweka nyonga yako Sawa,kukufanya uwe Fit,maana kuwa na mimba Sio Ugonjwa(labda k**a mimba Inasumbua na umekatwa na dr kufanya chochote).

7. Fanya tendo landoa,haikatazwi labda k**a unaumwa na haitakiw kwa usalama wa mimba
8. Tumia FOLIC ACID au SUPPLIMENTS ulizopewa na dr Wako.
9. Anza Clinic Mapema na hudhuria clinic Zako zote na kufuata Unayoambiwa.
10. Fanya maandalizi ya Nguo za kumpokelea mtoto,vitu vinavyotakiwa kwenda navyo hospitali.

Wangapi tumeelewana?? SHOW LOVE ❤️, MTAG Rafiki yako au Mama K kumsaidia kupata Elimu hii🤝😍.

Mtoto anaweza kuanza kugeuka kuanzia wiki ya 32 mpaka wiki 36 Endapo hajageuka kuanzia wiki 35 kurudi chini hiyo inaweze...
22/04/2022

Mtoto anaweza kuanza kugeuka kuanzia wiki ya 32 mpaka wiki 36

Endapo hajageuka kuanzia wiki 35 kurudi chini hiyo inawezekana isiwe shida kwa sababu anaweza kugeuka mpaka wiki ya 36 ila endapo hajageuka mpaka wiki ya 36 hiyo ndio tunaita “BREECH PRESENTATION”.

Kuna aina 3 za Breech presentation.

1. Kutanguliza miguu na matako kwa pamoja huitwa COMPLETE BREECH

2. Kutanguliza Matako na kukunjua miguu sehemu ya goti huitwa FRANK BREECH.

3. Kutanguliza mguu mmoja au miwili huitwa FOOTLING BREECH

Je naweza kujifungua kwa njia ya kawaida K**a mtoto Yuko BREECH?

Hutegemeana mama moja na mwingine na mtoa huduma njia atakayo chagua lakini kwa siku hizi Madaktari wengi hupendelea kufanya operation (Cesarian section) ili kuepuka shida mbalimbali.

Lakini Kuna njia ambayo Daktari anaweza fanya maneuver kwenye tumbo la Mjamzito njia hiyo huitwa _EXTERNAL CEPHALIC VERSION_ ambayo hufanyika Kati ya wiki 36 na 38 za Ujau*ito.
-
_EXTERNAL CEPHALIC VERSION_ huu ni utaratibu unaotumika kugeuza kijusi kutoka nafasi ya breech au nafasi ya kulala-upande (transverse) kuwa nafasi ya kichwa-chini (vertex) kabla ya leba kuanza. Ukifanikiwa, hufanya iwe rahisi kwa mama kujifungua Kwa njia ya kawaida!

MWISHO;
Unaweza kuwa mwalimu kwa wengine kwa KUS-hare makala hii zaidi na zaidi ili wengi wapate Elimu hii uliyoipata wewe.

- Pia kupata masomo mengine k**a fanya kulike ukurasa wetu 🤝

BADO SIKU MOJA TU😲🏃🏽‍♀️Za KUJISAJILI NA MAMA K WATSUP GROUP.Ni group linalojumuisha Wamama wajawazito TU, Tanzania 🇹🇿 na...
19/12/2021

BADO SIKU MOJA TU😲🏃🏽‍♀️

Za KUJISAJILI NA MAMA K WATSUP GROUP.
Ni group linalojumuisha Wamama wajawazito TU, Tanzania 🇹🇿 na nchi za jiran, mpaka sasa Mama K wapo 115 ❤❤🥰 (japo kuna wengine Wameishajifungua karibun waliingia Na mimba zao kwa group).

Huku utakutana na mama wajawazito wenzako,mtashauriana juu ya mambo mbali mbali, lakin Pia tupo Doctor Mle, tunashauri kitaalamu kabisa.
Lakin pia, utajifunza Lolote unalotamani kujifunza🔥🔥.

UMUHIMU WA HILI GROUP👇🏾

1. Ushauri wa Kitaalamu wa Dr na ma nurse UNAUPATA unapohitaji masaa 24

2. Uta share safari yako na Mama K wenzako,aisee wana enjoy sana hawa Mama K,yaan hupati upweke hata kidogo.

3. kuna vitu vidogo vidogo mama k wenzako watakushaur la kufanya ili upate unafuu...

Kuna MAMA K mliniomba niwaunge, Naomba NICHEK Tena Niwaunge, Na kwa ambao mlinitafuta week hii kesho ndio Group letu la tatu linaanza rasmi 😍💃....

Lakin pia mama k wote mnaotamanI, Nafasi zipo na IMEBAKI SIKU MOJA TU YA KUJISAJILI😲🏃🏽‍♀️, wahi

DM/ inbox nikupe Utaratibu.....

Hautajuta hata kidogoooo.

Hili group wananifanya na mimi nataman ningekuwa mama K aiseee, full ku enjoy maisha yao humo ndani ya Group.

Mambo 5 Ya Ajabu Usiyoyafahamu Kuhusu Uke Wako1⃣ Uke una mfumo unaojisafisha wenyewe kwa ndani na ni sehemu moja ya mwil...
06/12/2021

Mambo 5 Ya Ajabu Usiyoyafahamu Kuhusu Uke Wako

1⃣ Uke una mfumo unaojisafisha wenyewe kwa ndani na ni sehemu moja ya mwili wako ambayo ni safi kuliko maelezo, safi kuliko hata midomo yetu.

2⃣ Uke una Mfumo unaosafisha damu ya hedhi na shahawa wenyewe, hauhijaji
msaada wa aina yeyote

3⃣ Uke wenye afya una bacteria, lactobacilli, ambao ni kawaida kuwepo humo. Hawa hupambana na vijidudu visivyopaswa kuwepo huko kulinda uke
na mfumo wa uzazi kwa ujumla.

4⃣ Uke wenye afya sio mkavu, muda wote una ute usiokua na rangi (k**a maji), mwepesi na unaonata. Uzito, wingi na mnato wa ute huu hutegemea na mabadiliko ya mwili wa mwanamke. (Jifunze kutofautisha ili ujue muda inapaswa kumuona daktari)

5⃣ Uke wenye afya una harufu, ambayo ni nzuri, murua na isiyokera
K**a harufu itakua kali na inayokera (k**a yai bovu) basi uke wako
hauko katika afya njema na unahitaji kumuona daktari.

*Tunza Uke wako Ukutunze*

kwa kufuatilia ukurasa wetu wa Afya, share ujumbe huu uwafikie watu wengi.

Imeandaliwa na Dr.Sam

(+255) 0657251686 (whatsapp) for Dr Sam 🤳

“JIFUNZE na Chukua Hatua Juu Ya Afya Yako”.

NJIA SABA ZA KUTUMIA ILI MKE APATE MIMBA KIRAHISI. 1.Kufanya tendo la ndoa katika mtindo (style) ambayo itafanya mbegu z...
16/10/2021

NJIA SABA ZA KUTUMIA ILI MKE APATE MIMBA KIRAHISI.

1.Kufanya tendo la ndoa katika mtindo (style) ambayo itafanya mbegu za kiume zikae kwa muda mrefu ukeni na hivyo nyingi kupanda kuingia kwenye kizazi na kwenda kurutubisha yai.

'missionary position' ni nzuri zaidi, ambapo mwanaume anakuwa juu, epuka positions za mwanamke kuwa juu kwani hufanya mbegu zimwagike kwa gravity. Jaribu pia kuweka mto chini ya kiuno ili kukiinua na kufanya mbegu ziingie ndani kwa urahisi zaidi.

2. Tumia ovulation prediction kit, hiki ni kifaa ambacho kitakusaidia kujua wakati hasa mwanamke ameengua yai na ndio kipindi ambacho mwanamke ana uwezo wa kushika mimba akikutana na mumewe. Ni rahisi kutumia.

3. Fanya tendo la ndoa kabla ya kuengua yai (kabla ya ovulation), huongeza uwezekano wa kushika mimba kuliko kusubiria ovulation au kufanya baada ya ovulation.

Kutaneni siku mbili au tatu kabla ya ovulation. Ukitumia ovulation test kit, mkutane kuanzia siku itakapokuwa positive kwani huwa inapredict ovulation kutokea 48 hrs after it tests positive.

4. Usitegemee njia ya kalenda kutabiri uenguaji yai, njia hii kwa kiasi fulani huweza kuwasaidia wale wenye mzunguko wa siku 28, lakini pia haina uhakika wa 100%, wengi wa wanawake hawaengui yai siku ya 14 ya mzunguko wa hedhi, kwa hiyo kutegemea kalenda kutakuchelewesha kupata ujau*ito.

5. unapotaka kushika mimba, acha au punguza kwa kiasi kikubwa matumizi ya pombe, sigara au dawa za kulevya.

6. unapotaka kupata mimba, tendo la ndoa liwe kitu 'enjoyable' na sio tendo 'mechanical' kwa ajili ya kutafuta mtoto. Plan a romantic evening or try something different to spice things up.

How you are feeling sexually may increase your chances of getting pregnancy. For women a better or**sm may help pull the s***ms into the uterus and for men a better or**sm may increase their s***m count.

7Kufanya tendo la ndoa mara kwa mara, angalau siku tatu kwa wiki, ikiwezekana on alternate days.

Kumbuka kuna asilimia 10 - 25 ya couples ambazo zina matatizo ya infertility lakini vipimo havionyeshi tatizo, inaweza kuwa namna ya kufanya mapenzi ndio ikawa shida, jaribu njia hizo 7 juu.

K**a hizi njia hazijakusaidia basi utakuwa na matatizo na unaweza kumuona daktari kwa msaada wa vipimo na matibabu. Natumaini u*i huu unaweza kuwa msaada kwa watafutao watoto...

Ndugu kwa kufatilia Makala zetu za Afya za Kila siku .K**A BADO HUJALIKE USISAHAU KULIKE NA KUSHARE UKURASA

“JIFUNZE na Chukua Hatua Juu Ya Afya Yako”.

Kwa kawaida mtoto huanza kucheza kwa mara ya kwanza, kuanzia wiki ya 16 hadi wiki ya 25 katika kipindi cha ujau*ito,K**a...
31/05/2021

Kwa kawaida mtoto huanza kucheza kwa mara ya kwanza, kuanzia wiki ya 16 hadi wiki ya 25 katika kipindi cha ujau*ito,K**a ni ujau*ito wa kwanza inawezekana usimsikie hadi ikikaribia wiki ya 25.Ujau*ito wa pili ,mama huanza kumsikia mtoto akicheza mapema kuanzia wiki ya wiki 13.

Mtoto anatakiwa kucheza mara ,6-10 ndani ya saa moja. Ile miezi 6 ya mwanzo kucheza kwa mtoto hua sio sana.Kipindi cha usiku ndio muda wa mtoto kupigapiga tumbo la mamaye kuliko mchana.

MTOTO ANAWEZA KUCHEZA MIEZI MITATU YA MWANZO?

Mtoto hua mdogo sana miezi mitatu ya mwanzo.Hua na urefu wa 7.6-10 cm (3-4 inches) na u*ito wa gramm 28g (1 ounce) ,katika kipindi hiki viungo vya mtoto hua ni vilaini na vinakua havijakomaa hivo kusababisha mtoto kutokusikika akiwa anacheza.Mtoto hua mkubwa na kuongeza mwishoni mwa mwezi wa nne (second trisemister).

SABABU ZINAZOMPELEKEA MTOTO KUTOCHEZA AKIWA TUMBONI.
1. Kukosa nguvu za kutosha kutokana na lishe duni ya mama yake.
2. Mama anapotembea sana au kusimama kwa muda mrefu ,kuna mfanya mtoto achoke hivo kumpelekea kulala na kumfanya asicheze.
3. Mama anapokua na maradhi au matatizo ya kiafya,hudhoofisha afya ya mtoto ,hivo hupelekea mtoto kukosa nguvu na kushindwa kucheza.
4. Mtoto kuwa mdogo sana na u*ito mdogo pia humfanya ushindwe kucheza.
5. Mama anapokuwa amechoka kutokana na kazi nzito,mtoto nae huchoka na huhitaji kupumzika na huwa kimya sana.
6. Kupoteza uhai kwa mtoto (kufa)

SABABU ZINAZOWEZA KUMFANYA MTOTO ACHEZE AKIWA TUMBONI.
1. Kunywa maji ya baridi.
2. Fanya kitu cha kustusha kwa sababu maalumu.
3. Kula vyakula vya sukari.
3. Kula vyakula vya pilipili.
2. Ongea na mtoto

USHAURI:
Mama mjamzito,usimposikia mtoto akicheza katika muda ambao anatakiwa acheze ni vema ukafika katika kituo cha afya na kukutana na waatalamu,kwa ajir ya uchungu*i wa hali ya mtoto.

ZINGATIA:
Matumizi ya pombe na sigara ni hatari kwa afya ya mama na mtoto.
-
MWISHO
Prepared by Dr Sam CEO/ founder of Sam Nutritional Clinic
For more help Contact with us :-
(+255) 0789699225 (Watsup/call/sms) Dr Sam 🤳👨🏻‍⚕️

Ukiwa umependa makala hii na ungepanda kupata elimu sahihi ya afya kila siku, usihaau kuliki ukurasa Wetu ili kutopitwa na makala zetu pendwa za afya.

Pia Unaweza kuwa mwalimu kwa wengine kwa KUS-hare makala hii zaidi na zaidi ili wengi wapate Elimu hii uliyoipata wewe.

26/04/2021

VITU VITATU VINAVYOPUNGUZA KIUNGULIA KWA MAMA MJAMZITO.

1. Kula kiasi kidogo cha chakula na usile ukashiba sana. Kwa kuwa mama mjamzito huwa anasikia njaa mara kwa mara na anahitajia kula vyema ili aujenge vizuri mwili wake na watoto,
basi ni bora chakula chake ukigawe katika sehemu kadhaa ndogo, na ale mara kadhaa, badala ya kula sana wakati mmoja.

Suala hilo litafanya tumbo lake lisijae na kusaidia kuzuia asidi isipande juu ya tumbo na kusababisha kiungulia na gesi.

2. Jitahidi usinywe maji mengi sana baada ya chakula au wakati wa kula,

3. Jitahidi usilale tu mara baada ya kula, subiri k**a nusu saa hivi ipite ndio ulale.
Unapolala usilaze kichwa moja kwa moja bila mto, bali tumia mito kuegemeza kichwa ili kuzuia asidi isirejee juu ya tumbo na kusababisha kiungulia.
Unapohisi kiungulia kunywa glasi ya maziwa au kula mtindi.
Na k**a hali hiyo haijatoweka kunywa maji ya moto glasi moja yaliyowekwa kijiko kimoja cha asali.
-

MWISHO
Prepared by Dr Sam CEO/ founder of Sam Nutritional Clinic
For more help Contact with us :-
(+255) 0789699225 (Watsup/call/sms) Dr Sam 🤳👨🏻‍⚕️

Ukiwa umependa makala hii na ungepanda kupata elimu sahihi ya afya kila siku, usihaau kuliki ukurasa Wetu ili kutopitwa na makala zetu pendwa za afya.

Pia Unaweza kuwa mwalimu kwa wengine kwa KUS-hare makala hii zaidi na zaidi ili wengi wapate Elimu hii uliyoipata wewe.

20/04/2021

FAIDA ZA PARACHICHI KATIKA NYWELE

✅Moisturisers hair (unyevu katika nywele)
✅Faster growth of hair (hukuza nywele haraka)
✅Protect against dandruff (kuzuia/kuondoa mmba
✅Rejuvenates hair(hufufua nywele)

Namna ya kutengeneza mchanganyiko wa parachichi

Parachichi moja+Nazi changanya, paka kwenye nywele kaa dakika 10 na zaidi, osha nywele zako. Kumbuka usichane nywele zikiwa mbichi kwa sababu nywele zikiwa mbichi huwa dhaifu.

⚠️Tumia Natural Feminine Wash isiyokuwa na kemikali Kuoshea uso, kuzuia Nywele kukatika, kung'arisha Nywele na kutoa mba na vidonda kichwani. Tuwasiliane kwa kupiga simu au WhatsApp 0789699225, Dr Sam.
-
Upendo ni kujifunza kwa pamoja, kuonyesha Upendo unaweza kushare kwa marafiki zako pia.

19/04/2021

SABABU ZA MTOTO KUPUNGUZA AMA KUACHA KUCHEZA TUMBONI

Mama mjamzito huwa anaskia raha pale mtoto anapoanza kumpiga piga tumboni kwa mara ya kwanza. kucheza kwa mtoto kunafanya kuwa na mawasiliano mazuri kati ya mama namtoto
Kwa wenye mimba ya kwanza mtoto ataanza cheza wiki ya 24 miezi (5-6), ila kwa wale walio zaa tayari mtoto mmoja au zaidi wanaskia mtoto akicheza akiwa wiki ya 18-22 mapema kidogo..

Kuna umuhimu wa mama kufatilia kujuakucheza kwa mtoto,kwa kawaida watoto wanatakiwa wacheza mara 6 -10 ndani ya lisaa limoja (1hr) ile miezi 3 ya mwisho,na ile miezi 6 ya mwanzo kucheza kwake sio sana.

Cha muhimu unatakiwa ujue pale anapocheza na asipocheza.

Kipindi cha usiku ndio muda wa watoto kupigapigakuliko mchana ,na baada ya mama kula chakula pia huwa wapiga piga sana tumbo.

SABABU ZA MTOTO KUTOCHEZA: Mtoto kukosa nguvu za kutosha kutokana na lishembaya ya mama yake,:Mtoto hapati hewa ya kutosha kutoka kwenye placenta:Mtoto kuwa mdogo sana na u*ito mdogo nayo unamfanya ashindwe kucheza au akacheza kwa mbali sana na kukufanya wewe usimskie k**a anacheza.:Mama anapokuwa na maradhi au matatizo ya kiafya, hudhoofisha afya ya mtoto na kukosa nguvu:Mama anapokuwa amechoka sana kwa safari au kazi ngumu ,mtoto nae anakuwa anachoka na kuhitaji kupumzika na huwa kimya sana:Mama anapotembea sana au kusimama kwa muda mrefu.

MWISHO
Prepared by Dr Sam CEO/ founder of Sam Nutritional Clinic
For more help Contact with us :-
(+255) 0789699225 (Watsup/call/sms) Dr Sam 🤳👨🏻‍⚕️

Ukiwa umependa makala hii na ungepanda kupata elimu sahihi ya afya kila siku, usihaau kuliki ukurasa Wetu ili kutopitwa na makala zetu pendwa za afya.

Pia Unaweza kuwa mwalimu kwa wengine kwa KUS-hare makala hii zaidi na zaidi ili wengi wapate Elimu hii uliyoipata wewe.

Utumiaji wa juisi ya limao kila siku asubuhi una faida kubwa sana katika mwili wa binadamu, kwani limao ina virutubisho ...
19/04/2021

Utumiaji wa juisi ya limao kila siku asubuhi una faida kubwa sana katika mwili wa binadamu, kwani limao ina virutubisho na madini mbalimbali k**a Calcium, Magnesiam, vitamin C, Zink, Potasiam, kopa, chuma na Protini.

Hivyo mbali na mwili kurutubika na madini tajwa hapo juu, unywaji wa juisi ya limao, kachumbali ya limao au maji ya vuguvugu yaliyonyunyiziwa limao husaidia mwili katika mambo 7 yafuatayo.

1. Limao husaidia mfumo wa mmeng’enyo wa chakula na kulainisha choo, hivyo kwa wale wanaosumbuliwa na tatizo la kupata haja kubwa wanashauriwa kila siku asubuhi kutumia juisi ya limao ili kusaidia kupata haja kubwa kwa urahisi.

2. Limao hutunza mfumo wa kinywa hasa kwa kujali afya ya meno, utumiaji wa limao kila siku asubuhi husaidia kubadilisha rangi ya meno yako hasa wale wenye meno ya njano ndimu husaidia kung’arisha meno nakuyafanya yawe katika hali ya kawaida ya uweupe, hivyo kwa lengo hili inashauriwa uweke vitone vichache katika mswaki wako wakati wa kupiga msawaki ili kupata matokeo mazuri.

2. Hutunza nywele, inashauriwa wakati mwingine kuchukua kiasi fulani cha ndimu nakupaka katika nywele hii husaidia kufanya nywele zako kuwa zenye afya na kwa wale wenye nywele chache limao husaidia kujaza nywele na ku*ing’arisha na ku*ifanya zipate muonekano wa asilia.

3. Moja ya faida kubwa ya limao ni kupunguza u*ito wa mwili, madaktari wanasisitiza kila asubuhi mtu kutumia glasi ya maji yaliyochanganywa na ndimu pamoja na asali husaidia mfumo wa kuyeyusha mafuta ndani ya mwili na kumfanya mtu apunguze u*ito.

4. Limao husaidia kuepusha kupata uvimbe kwenye figo kwani ndimu inamiliki virutubisho ambavyo huzuia figo kuathirika na uvimbe.

5. Limao mwilini hufanya kazi ya kuchuja sumu katika ini na figo kutokana na kazi yake ya kusafisha vijidudu vyote vinavyosababisha bacteria wabaya mwilini.

6. Limao inaongeza kinga mwilini ya kupigana na magonjwa mbalimbali, na ndio maana inashauriwa kwa wale wenye kinga pungufu dhidi ya magonjwa kutumia limao.

7. Limao husaidia kuepusha kupata uvimbe kwenye figo kwani ndimu inamiliki virutubisho ambavyo huzuia figo kuathirika na uvimbe.

Upendo ni kujifunza kwa pamoja, kuonyesha Upendo unaweza kushare kwa marafiki zako pia.
-
By Doctor Sam, whatsapp no. 0789699225.

.1. Mahitaji ya mloNi wazo zuri k**a utamnyonyesha mwanao. Lakini kutokana na maisha ya sasa akina mama wengi wanapendel...
05/04/2021

.
1. Mahitaji ya mlo
Ni wazo zuri k**a utamnyonyesha mwanao. Lakini kutokana na maisha ya sasa akina mama wengi wanapendelea kumtengenezea mlo tofauti utahitaji kufuata kanuni, mahitaji hayo ni k**a:
* Maziwa ya unga
* Chupa 6 za maziwa
* Kiosha chupa na begi la kuhifadhia
* Brashi ya kusafisha chupa pamoja na maji ya uvuguvugu
* Eproni
* Mto
* Kitambaa cha kumkinga mtoto akicheua
K**a utaamua kumlisha maziwa yako kwa chupa utahitaji kitu cha kukamulia maziwa na vifaa vingine k**a kiosha chupa na begi la kuhifadhia.

2. Mavazi ya msingi
Kwa siku za mwanzo mtoto atahitaji mavazi mengi, hivyo hakikisha umenunua mavazi ya kutosha. Zingatia yafuatayo unaponunua mavazi kwa ajili ya mtoto;
* Nguo za kipimo chake ingawa anakua kwa haraka
* Ovaroli zenye mikono mirefu na mifupi ambazo zina vifungo katikati
* Gloves 2 za mikono ili kumlinda mtoto asijikwaruze
* Jozi 6 za viatu na soksi pamoja na nguo za kulalia
* Jozi 6 za nguo za kutokea unapokwenda kuwaona ndugu na marafiki.
* Kofia 2 za pamba kumlinda mtoto masikio na kichwa kipindi cha baridi.
* Kwa kutegemea hali ya hewa, nunua jozi 2 za sweta.
Nguo za mtoto zisafishwe na kuhifadhiwa sehemu salama ku*ilinda kutokana na uchafu.
3. Malazi
Pindi tuu unaporudi nyumbani mtoto wako atahitaji sehemu ya kupumzikia, unaweza kuchagua sehemu kwa ajili yake pembeni ya kitanda chako. Hakikisha umepata mpangilio wa kitanda kabla ya kichanga kufika nyumbani. Uangalizi uchukuliwe kabla ya kununua neti, hakikisha unapata bora na salama. Mahitaji sahihi katika kitanda cha mtoto ni;
* Kitanda chenye ubora
* Shuka2 hadi 3 za kufiti
* Shuka3 hadi 4 zisizopitisha maji
* Blanketi 3 za pamba
K**a utaenda kuazima au kununua kwa mtumba ni vema kuangalia zilizo bora.

4. Mahitaji muhimu ya usafi wa mwili
Vifaa kwa ajili ya kumfanya kichanga awe salama na huru wakati wa kuoga. Utalazimika kuwa na vitu vifuatavyo;
* Kuandaa sehemu salama kwa ajili ya kuoga, utatakiwa kununua beseni.
* Taulo 2 za kuogea na pakiti 2 za sabuni ya kufulia nguo za mtoto
* Shampuu ya mtoto na sabuni ya kumuogeshea mtoto wako
* Losheni na mafuta ya kumpaka mtoto baada ya kuoga, Usimpulizie manukato
* Brashi ya kuchania nywele au seti ya vitana na vikatia kucha.

Prepared by Dr Sam CEO/ founder of Sam Nutritional Clinic
For more help Contact with us :-
(+255) 0789699225 (Watsup/call/sms) Dr Sam 🤳👨🏻‍⚕️

Ukiwa umependa makala hii na ungepanda kupata elimu sahihi ya afya kila siku, usihaau kuliki ukurasa Wetu ili kutopitwa na makala zetu pendwa za afya.

Pia Unaweza kuwa mwalimu kwa wengine kwa KUS-hare makala hii zaidi na zaidi ili wengi wapate Elimu hii uliyoipata wewe.

VIASHIRIA VYA  MTOTO MCHANGA KUA NA NJAASiku chache baada ya kujifungua mwili wako utaanza kutoa maziwa ya awali(colostr...
29/03/2021

VIASHIRIA VYA MTOTO MCHANGA KUA NA NJAA

Siku chache baada ya kujifungua mwili wako utaanza kutoa maziwa ya awali(colostrum).
Kwa baaadhi ya wanawake maziwa haya huwa mazito na kuwa na rangi ya njano, Kwa wengine ni mepesi na huwa ya maji maji.

Maziwa haya ya awali yana kazi kubwa ya kulinda mwili, hivyo ni muhimu sana kwa mtoto tofauti na maziwa mengine ambayo si ya mama. Maziwa haya hutiririka taratibu na hii humsaidia mtoto kujifunza jinsi ya kunyonya huku akipumua na kumeza maziwa.

Baadaya siku 3 hadi 4 za kunyonyesha, matiti yatazidi kuwa magumu kadri maziwa ya awali yanavyozidi kubadilika na kuwa maziwa ya kawaida.
Maziwa hayo yatabadilika ndani ya siku 10 hadi 14 za mwanzo na kuwa maziwa kamili.

Katika kipindi hiki kiwango cha maziwa kitaongezeka ili kukidhi mahitaji ya mwanao.
Kiwango cha maziwa hutegemeana na jinsi unavyochochewa kwa jinsi unavyonyonyesha.Hii inamaanisha kwamba mwanao anaponyonya maziwa mengi, mwili pia hutoa maziwa mengi zaidi.

Wanawake waliojifungua kwa njia ya operesheni, inaweza kuchukua muda mrefu maziwa yao kuongezeka.
Wakati mwingine bila sababu yoyote inaweza kuchukua siku chache maziwa kuanza kutoka. Hili ni jambo la kawaida kabisa na hutokea pasipo sababu yoyote lakini hakikisha unamwambia daktari kuhusiana na suala hili.

Ingawa watoto hawatahitaji chochote zaidi ya maziwa ya awali(colostrums) siku chache baada ya kuzaliwa daktari atakushauri kuhakikisha kwamba mtoto anapata maziwa ya kutosha ikiwa na pamoja na kumuweka mtoto katika matiti kila baada ya masaa mawili hadi matatu.

VIFUATAVYO NI VIASHIRIA KUA MTOTO ANA NJAA NA ANAHITAJI KUNYONYA

- Kugeuza kichwa huku na huko.
- kuachama.
- Kuweka mikono mdomoni.
- Kukunja mdomo k**a anayetaka.
- Kunyonya.
- Kujinyoosha.
- Kujisogeza karibu na matiti mama.

Prepared by Dr Sam CEO/ founder of Sam Nutritional Clinic
For more help Contact with us :-
(+255) 0789699225 (Watsup/call/sms) Dr Sam 🤳👨🏻‍⚕️

Ukiwa umependa makala hii na ungepanda kupata elimu sahihi ya afya kila siku, usihaau kuliki ukurasa Wetu ili kutopitwa na makala zetu pendwa za afya.

Pia Unaweza kuwa mwalimu kwa wengine kwa KUS-hare makala hii zaidi na zaidi ili wengi wapate Elimu hii uliyoipata wewe.

“JIFUNZE na Chukua Hatua Juu Ya Afya Yako”.

SABABU KUKOSA MAZIWA KWA MAMA ANAYENYONYESHA.A). MATUMIZI YA DAWA ZA UZAZI WA MPANGO:Wanawake wengi hutumia njia hizi ba...
25/03/2021

SABABU KUKOSA MAZIWA KWA MAMA ANAYENYONYESHA.

A). MATUMIZI YA DAWA ZA UZAZI WA MPANGO:
Wanawake wengi hutumia njia hizi baada ya kujifungua bila shida yeyote lakini kuna baadhi yao njia hizi huingilia mfumo wao wa kutoa maziwa hasa zikitumika kabla mtoto hajafikisha miezi sita. Hii husababishwa na kuongezeka kwa homoni za uzazi yaani progesterone na oestrogen ambazo hushusha homoni ya kutoa maziwa yaani prolactin hormone. K**a umekumbwa na hali hii basi acha mara moja njia hiyo na utumie njia zingine k**a kalenda.

😎. UPASUAJI WA MATITI:
K**a mama ameshawahi kupasuliwa matiti yake kwa shida yeyote labda majipu, ajari, upasuaji wa kuongeza au kupunguza matiti basi kwa namna moja au nyingine hii inaweza kuharibu mfumo wake wa matiti kupitisha maziwa na kujikuta hatoi maziwa ya kutosha

C). MATUMIZI YA DAWA WAKATI WA KUNYONYESHA:
Kuna baadhi ya dawa ni hatari kwani hushusha kiwango cha maziwa. Mfano dawa za k**a bromocriptine, methergine, pseudoephredine

D). KUTONYONYESHA WAKATI WA USIKU
Wakati wa usiku homoni inayohusika na kutengeneza maziwa yaani prolactin hutengenezwa kwa kiwango cha juu sana lakini pia ili mtoto alale usiku mzima bila kusumbua lazima anyonye vizuri usiku. Kutonyonyesha usiku hupunguza homoni hii na kumfanya mama atoe maziwa kidogo sana siku inayofuata.

E). KUTONYONYESHA KAWAIDA:
Mama anatakiwa anyonyeshe angalau mara kumi ndani ya masaa 24, sasa mwili hutengeneza maziwa unapohisi matiti hayana kitu na k**a mwili ukihisi matiti yana maziwa muda mwingi basi unajua maziwa hayahitajiki sana na kuanza kupunguza kiasi cha kutoa maziwa.

F). KUTOKULA VIZURI:
Maziwa anayotoa mama yanatengenezwa na chakula anachokula, kipindi hiki mama anatakiwa ale mlo kamili yaani matunda, protini ya kutosha, wanga, mboga za majan na maji mengi na ikiwezekana atumie virutubisho vinavyotengenezwa maalumu kwa ajili ya kuongeza maziwa.

G). MATUMIZI YA VYAKULA MBADALA:
Miezi sita baada ya kuzaliwa mtoto anatakiwa anyonye tu bila kupewa kitu chochote, kuna watu hua wanawapa maji wakidai eti watoto walisikia kiu sio kweli. Sasa kuanza kumchanganyia maziwa ya ngombe na yale ya dukani kutamfanya anyonye kidogo kwako na mwili utapunguza kiasi cha maziwa yako...hivyo siku ukikosa mbadala utajikuta huna maziwa kabisa.

Prepared by Dr Sam CEO/ founder of Sam Nutritional Clinic
For more help Contact with us :-
(+255) 0789699225 (Watsup/call/sms) Dr Sam 🤳👨🏻‍⚕️

Ukiwa umependa makala hii na ungepanda kupata elimu sahihi ya afya kila siku, usihaau kuliki ukurasa Wetu ili kutopitwa na makala zetu pendwa za afya.

Pia Unaweza kuwa mwalimu kwa wengine kwa KUS-hare makala hii zaidi na zaidi ili wengi wapate Elimu hii uliyoipata wewe.

“JIFUNZE na Chukua Hatua Juu Ya Afya Yako”.

SABABU ZA CHUPA YA UZAZI KUPASUKA KABLA YA WAKATI.Chupa kupasuka ni neno lililozoeleka katika jamii yetu likiwa na maana...
23/03/2021

SABABU ZA CHUPA YA UZAZI KUPASUKA KABLA YA WAKATI.

Chupa kupasuka ni neno lililozoeleka katika jamii yetu likiwa na maana kitabibu k**a ngozi au tando laini inayoyazungunguka maji yanayomfanya mtoto aliye ndani ya nyumba ya uzazi kuelea, imepasuka na maji hayo kutoka.

KAZI YA MAJI HAYO:
1.Kumpa kinga mtoto-kumwepusha na maradhi ya infection
2.Kumpa joto na kulihifadhi
3.Inamsaidia kwenye mmeng’enyo na upumuaji wa mtoto

Tando hili la ngozi huweza kupasuka kiasili wakati au baada ya uchungu kuanza. Katika hatua hii si tatizo bali ni hali ya kawaida kujitokeza na kitabibu hujulikana spontaneous rupture of membrane.

Pia, tando hii inaweza kupasuliwa na mtoa huduma kwa baadhi ya wajawazito, kulingana na hali zao. Kwa mfano, mtoa huduma anaweza kumtathmini mjamzito, k**a kuendelea kuwapo kwa ujau*ito huo kunaweza kuhatarisha maisha ya mtoto tumboni.

Na k**a chupa itapasuka kabla ya muda wake kufika, huenda ikawa ni tatizo la kiafya au madhara yatokanayo na hali ya ujau*ito.

Kupasuka kwa ngozi laini kabla ya mjamzito kupata uchungu halisi baada ya kukamilika kwa wiki 37 za umri wa mimba, kitabibu huitwa rupture of membrane (PROM) na kupasuka kwa chupa mapema kuliko kawaida kabla ya wiki ya 37 ya umri wa mimba, kwa neno la kitabibu huitwa preterm premature rupture of membrane (PPROM).

Inakadiriwa kati ya asilimia 8 hadi 10 ya wajawazito hupata PROM na asilimia mbili hupata PPROM. Hili ni moja ya tatizo linaloweza kuchangia kuzaliwa mtoto njiti.

VITU VINAVYOWEZA KUSABABISHA CHUPA HYO KUPASUKA KABLA YA WAKATI

1.INFECTION -k**a mama ana infection ya ukeni au kwenye mlango wa kizazi chupa itapasuka
2.UVUTAJI WA SIGARA
3.Mama mwenye matatizo ya high blood pressure -anahatari kubwa ya kupasuka kwa chupa kabla ya muda wake vizuri kuhudhuria clinic mara kwa mara na kuchukua vipimo vya pressure.
4.Mimba ya watoto mapacha – mapacha wanasababisha msukumo mkubwa kwenye membranes na chupa kupasuka kabla ya muda wake.

EPUKA YAFUATAYO:
Kutumia vyoo vya public na iwapo utatumia kuwa makini sana ,
:Usifanye mapenzi kwa kipindi hiko mpaka utakapo jifungua ,
:Usivae tamponsUsijiweka vidole ukeni

Address

Dar Es Salaam
9225

Telephone

+255789699225

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when YOUR Health Matters Coaching posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to YOUR Health Matters Coaching:

Share