21/06/2014
TATIZO LA KUTOKUWA NA UWIANO MZURI WA HOMONI KWA WANAWAKE
Kwa mwanamke, mabadiliko katika mfumo wa homoni ni jambo la kawaida kutokea, si kwamba mtu abaye amefika au kuelekea kwenye menopozi (kufika ukomo wa hedhi) ndiye anayekutana na mabadiliko haya.
Ingawa mabadiliko haya hutokea kwa mwanamke ambaye tayari keshafika umrii wa miaka kati ya 40 hadi 50, pia inaweza kutokea kwa mwanamke ambaye amefikisha umri wa miaka 25.
SABABISHO:
1. Vyakula, vinywaji vinakuwa na mambo mengi ambayo yana madhara k**a vile sumu, mafuta mengi, kemikali zinazowekwa kwenye vyakula/vinywaji
2. Dawa: zipo dawa tutumiazo kunywa au kupakaa kwenye ngozi ambazo huwa zina sumu ndani yake
3. Mchafuko wa mazingira (pollution), hewa chafu itokanayo na moshi wa magari, uchomwaji wa madampo, moshi wa viwanda (kuna kemikali zinatumika viwandani mfano uchanganywaji wa rangi mbalimbali, uchomwaji wa vyuma, utengenezaji wa nondo, n.k)
Mambo hayo hapo juu hueanda kuzivuruga homoni ambazo zina kazi ya kufanya mambo mengi katika mwili wa mwanamke, mfano homini inayofanya kazi ya kuhakikisha maziwa kwa mwanamke yanakuwepo, homoni inayoweka hedhi kwa mwanamke kuwa sawa (kuhakikisha yai linapevuka kwa wakati unaotakiwa).
DALILI ZA MWANAMKE AMBAYE ANA MABADILIKO YA HOMONI:
1. Ongezeko la uzito mara kwa mara: mwanamke atajitahidi kuhakikisha anaondokana na ongezeko la uzito, lakini hali hii inakuwa na kujirudia rudia
2. Mafuta kwenye tumbo na upungufu wa homoni
3. Low libido
4. Uchovu
5. Hasira, kukasirika, kukosa mudi kwa kupitiliza, au mara kwa mara
6. Shida kwenye usingizi (aidha kupata usingizi sana au kukosa usingizi)
7. Kutokwa jasho isivyo kawaida hasa nyakati za usiku
8. Shida kwenye mfumo wa kumeng’enya chakula
9. Hamu ya kupenda kula vyakula vya aina Fulani mfululizo (mfano vyakula vyenye sukari kwa wingi ambavyo)
10. Mabadilko katika hedhi, wengine wanafikia ukomo wa hedhi kabla ya wakati wake
11. Kutopata hisia za kufanya tendo la ndoa, au kutopenda kupata tendo hilo
NINI CHA KUFANYA
1. Kula vyakula ambavyo vinasaidia kuleta uwiano sawia wa homoni (k**a vile soya, maziwa,
2. Kunywa maji kwa wingi kwa ajili ya kuondoa sumu mwilini
3. Pata virutubisho mbadala kwa ajili ya kuleta uwiano sawia k**a vile milk calcium, soy isoflavonoids, nk)