17/04/2026
βββππππππ ππ πππππππ ππππππ.πππππ
π¨Kiungo wa Ecuador Moises Caicedo ameafikiana mkataba mpya wa muda mrefu na Chelsea wa miaka 7 wenye mshahara nono, ambao utamuweka klabuni hadi mwaka 2033.
π Chanzo: BBC Sport
π¨ Makubaliano hayo yameshakamilika na yamekubalika kwa pande zote, kilichobaki ni tangazo rasmi tu ambalo linatarajiwa kutolewa muda wowote.
π Chanzo: Ben Jacobs
π¨ FC Barcelona hawana uhakika kulipa β¬30m (Β£21.1m) ili kumchukua mshambuliaji wa England Marcus Rashford kutoka Manchester United kwa mkataba wa kudumu.
π Chanzo: Marca
π¨ Winga wa Newcastle United Anthony Gordon yuko tayari kuangalia chaguo nyingine msimu huu wa joto, huku Bayern Munich wakimtamani.
π Chanzo: Telegraph
π¨ Lakini Arsenal wanaongoza kwenye mbio za kumsajili Anthony Gordon, ambaye anapendelea kuhamia London kuliko miji mingine.
π Chanzo: The Sun
π¨ Manchester City na FC Barcelona wanaongoza mbio za kumsajili mshambuliaji wa Brazil mwenye miaka 16 Eduardo Conceicao kutoka Palmeiras.
π Chanzo: Mail+
π¨ Newcastle United wanajiandaa na majira ya joto yenye shughuli nyingi, huku wachezaji 7 wa kikosi cha kwanza wakihusishwa na kuondoka klabuni.
π Chanzo: The Sun
π¨ Liverpool wana wachezaji 9 wanaoweza kuondoka, akiwemo kiungo wa Argentina Alexis Mac Allister (27), anayevutiwa na vilabu vya Ulaya.
π Chanzo: Telegraph
β‘οΈ Beki wa England Joe Gomez (28) anahitajika na Crystal Palace, Brighton & Hove Albion na AC Milan.
π Chanzo: Telegraph
π¨ Jurgen Klopp na Mauricio Pochettino ni wagombea wa ukocha wa Real Madrid iwapo Alvaro Arbeloa ataondolewa.
π Chanzo: Daily Mail
π¨ Beki wa England Matt Targett (30), anayekipiga kwa mkopo Middlesbrough kutoka Newcastle United, anafuatiliwa na Everton na Leeds United.
π Chanzo: Teamtalk
π¨ Tottenham Hotspur wako tayari kumuuza kiungo wa England Conor Gallagher (26), ambaye alijiunga Januari.
π Chanzo: Football Insider
π¨ Beki wa England Levi Colwill (23) anatarajiwa kusaini mkataba mpya wa muda