04/03/2026
Mapigo ya moyo kwenda mbio kwa mjamzito (moyo kudunda haraka) ni jambo linaloweza kutokea mara nyingi wakati wa ujauzito. Wakati mwingine ni kawaida, lakini wakati mwingine linaweza kuashiria tatizo.
1.Sababu za kawaida (zisizo hatari)
Hizi hutokana na mabadiliko ya mwili kipindi cha ujauzito:
-Kuongezeka kwa ujazo wa damu mwilini (Blood volume)(moyo hufanya kazi zaidi)
-Homoni za ujauzito
- Hali ya Wasiwasi au msongo wa mawazo kwa mjamzito
-Uchovu au kukosa usingizi
-Kunywa kahawa/ chai nyingi au vinywaji vyenye caffeine
2.Sababu zinazoweza kuwa hatari
-Upungufu wa maji mwilini (dehydration)
-Upungufu wa damu (anemia)
-Kiwango cha sukari mwilini kuwa chini (low blood sugar)
-Shinikizo la juu la damu au dalili za kifafa cha mimba(preeclampsia/eclampsia)
MUONE DAKTARI k**a kuna dalili hizi kwa pamoja:
1.Mapigo ya moyo yanaenda kwa kasi sana na hayapungui na Dalili zinaendelea muda mrefu,Ikiambatana na;
2.Kizunguzungu au kuzimia
3.Maumivu ya kifua
4.Kupumua kwa shida
5.Kuvimba sana mwili(Uso,mikono,miguu)
6.Homa n.k..