The Afya

The Afya 🔘 TUZUNGUMZE KUHUSU AFYA.
🔘 VIFAA TIBA NA DAWA.
🔘 USAHURI WA KITAALAM.
🔘 NAMBA: 0717174151

Kwanini wagonjwa huwa wanakatazwa wasile kabla ya upasuaji..!?Wakati wa upasuaji, mgonjwa anapopewa dawa za usingizi mwi...
15/02/2026

Kwanini wagonjwa huwa wanakatazwa wasile kabla ya upasuaji..!?

Wakati wa upasuaji, mgonjwa anapopewa dawa za usingizi mwili huwa unapoteza uwezo wa kujlinda matapishi yasiingie kwenye njia ya hewa. Sasa mgonjwa anapokuwa amekula muda mfupi kabla ya upasuaji, tumboni huwa kuna mabaki ya chakula na asidi nyingi. Anapopewa dawa za usingizi atatapika na hayo matapishi yataingia kwenye njia ya hewa hivyo yanaweza kuharibu mapafu, mgonjwa kulazwa ICU na wakati mwingine anaweza kupoteza maisha. Sasa hili kuzuia hali hiyo, ndio maana wagonjwa wanakatazwa wasile au kunywa kitu kabla ya upasuaji.

Sasa ule muda gani kabla ya kuingia kwenye chumba cha upasuaji..!?

1. Maji ya kunywa, chai ya rangi, maji ya sukari, juice ya apple au kinywaji chochote ambacho unaweza kuona chini ya kikombe
- Unaweza kutumia vinywaji hivi masaa mawili kabla ya kuingia kwenye chumba cha upasuaji. Vinywaji hivi havihusishi pombe kwa sababu pombe hufanya tumbo lchelewe kumwaga chakula.

2. Maziwa ya Mama
- Mtoto anaweza kunyonya masaa matatu kabla ya kuingia kwenye chumba cha upasuaji.

3. Maziwa ya Unga na Maziwa ya ng'ombe
- Mtoto anaweza kutumia vinywaji hivi masaa manne kabla ya kuingia kwenye chumba cha upasuaji.

4. Vinywaji vingine ambavyo haviko hapo juu, mfano juice ya embe, juice nzito nzito.
- Mgonjwa anaweza kutumia vinywaji hivi masaa 6 kabla ya kuingia kwenye chumba cha upasuaji.

5. Milo laini mfano chai na mkate, chai na viazi nk.
- Mgonjwa anaweza kutumia vyakula hivi masaa 6 kabla ya upasuaji.

6. Vyakula vyenye mafuta mfano chips, nyama..
Mgonjwa anaweza kutumia vyakula hivi masaa 8 kabla ya upasuaji.

Kufunga muda mrefu o haina faida yoyote isipokuwa inaongeza usumbufu kwa wagonjwa na wazazi hasa kwa watoto wadogo. Pia huongeza hatari ya wagonjwa kupata matatizo hasa sukari kushuka wakati wa upasuaji. Wahudumu wanaohudumia wagonjwa waliopangiwa upasuaji wanahimizwa kuwasaidia wagonjwa hawa na kutowaweka na njaa kwa muda mrefu.
Kwa mfano mgonjwa wa mwisho kwenye list ambaye inatarajiwa ataingizwa theatre saa 8 mchana anaweza kuambiwa anywe kikombe cha maziwa na mkate na yai kabla ya saa 1 asubuhi.

Kuna mwenye swali..!?

“Ubongo ni kiungo pekee katika mwili ambacho hakijakomaa kikamilifu wakati wa kuzaliwa. Hii ina maana kwamba unaendelea ...
15/02/2026

“Ubongo ni kiungo pekee katika mwili ambacho hakijakomaa kikamilifu wakati wa kuzaliwa. Hii ina maana kwamba unaendelea kukua na kubadilisha muundo na maudhui yake katika maisha yote.
Ubongo huchakata takribani biti bilioni mia nne za taarifa kwa kila sekunde. Taarifa yoyote inayowekwa kwenye kichakataji hiki lazima itachakatwa.”
Hello 👋

Maandalizi Na Vifaa Kujifungua.
11/02/2026

Maandalizi Na Vifaa Kujifungua.

Ona shilingi ilivyokwama kwenye koo la mtoto...kuna mambo ambayo wazazi huwa wanafanya k**a njia ya kuonyesha upendo lak...
26/01/2026

Ona shilingi ilivyokwama kwenye koo la mtoto...kuna mambo ambayo wazazi huwa wanafanya k**a njia ya kuonyesha upendo lakini kwa upande mwingine huwa ni kuhatarisha maisha ya mtoto...kwa mfano kumpa mtoto hela kwenda kununua p**i... au kumpa hela kuchezea au kumpa vitu k**a karanga, mahindi, korosho...ni vitu ambavyo havina faida yoyote kwa mtoto mdogo hasa wenye umri chini ya miaka 4....hawa mara nyingi kila kitu wanaweka mdomo... sasa ikikwama kwenye njia ya hewa unajikuta unampoteza mtoto kizembe sana.. lakini pia mtihani mwingine huwa upo kwenye kuvitoa hivyo vitu vilivyokwama kwenye njia ya hewa ni matibabu ya hatari sana ambayo ni rahisi sana kumpoteza mgonjwa akiwa theatre...tuepuke kuwapa vitu ambavyo havina manufaa yoyote watoto kwenye ukuaji wao...kwa mtoto muhimu ni chakula...!

Credit

HATA WEWE UNAWEZA KUITWA MAMA.KWA KUTUMIA WOMEN FERTILITY KIT (DOZI YA UZAZI ) UNAWEZA KUBEBA UJAUZITO NDANI YA SIKU 30....
26/01/2026

HATA WEWE UNAWEZA KUITWA MAMA.

KWA KUTUMIA WOMEN FERTILITY KIT (DOZI YA UZAZI ) UNAWEZA KUBEBA UJAUZITO NDANI YA SIKU 30.

Women fertility KIT ni dozi ambayo humsaidia mwanamke mwenye changamoto ya kupata ujauzito kubeba ujauzito kwa muda wa siku 30 tu.

Faida za Women fertility Kit inafanya Yafuatayo kumsaidia mwanamke mwenye shida ya uzazi

▶️inasaidia kupevusha mayai
▶️inasafisha mirija,ready kabisa kupitisha Yai/mayai(kwa mapacha),na mbegu za kiume zinapita vizur kabisa
▶️inaweka kizazi vizuri kabisa,ready kupokea mtoto
▶️inaweka PH ya uke,vagina ile nzur inafaa kupitisha mbegu za kiume bila kuziua.
▶️inakufanya mwanamke upate ule UTE special unaovutika k**a ute mweupe wa mayai ukiwa siku za hatari,huu ute ni muhimu maana ndio ute special mbegu za kiume zinapitia kuingia ndani....
▶️zinaweka hormones Zikae sawa ka bisaaaaaa zinazofanya upevushe mayai,udake mimba na ukipata mimba,Isitoke.
▶️INATIBU PID.inasafisha infection na uchafu wote.
Na k**a imeonekana hupati MIMBA,lakini shida haijaonekana,basi unahitaji sana hii kit

WOMEN FERTILITY KIT ITAKUSAIDIA KUBEBA UJAUZITO NDANI YA MUDA MFUPI SANA.


res Salaam



morogoro

0717 174 151

KUTOKWA NA UCHAFU UKENI.FANGASI UKENI (VAGINAL CANDIDIASIS)1️⃣ Fangasi ukeni ni nini?Fangasi ukeni ni maambukizi yanayos...
26/01/2026

KUTOKWA NA UCHAFU UKENI.

FANGASI UKENI (VAGINAL CANDIDIASIS)

1️⃣ Fangasi ukeni ni nini?

Fangasi ukeni ni maambukizi yanayosababishwa na ukuaji kupita kiasi wa fangasi aina ya Candida albicans ndani ya uke.
Ni tatizo la kawaida, wanawake wengi hukumbana nalo angalau mara moja katika maisha.

2️⃣ Dalili za fangasi ukeni

🔹 Kuwashwa sana ukeni
🔹 Maumivu wakati wa kufanya tendo la ndoa
🔹 Kujisikia k**a kuchoma au kuungua ukeni
🔹 Kutokwa uchafu mzito mweupe k**a maziwa mtindi (cottage cheese)
🔹 Kukosa raha wakati wa kukaa au kutembea
🔹 Kubana au kuuma wakati wa kukojoa

3️⃣ Sababu zinazosababisha fangasi ukeni

⭐ (a) Kushuka kwa kinga ya mwili
Mfano: msongo wa mawazo, usingizi mdogo, magonjwa yanayoshusha kinga.

⭐ (b) Mabadiliko ya homoni
• Wakati wa ujauzito
• Wakati wa hedhi
• Matumizi ya vidonge vya uzazi wa mpango

⭐ (c) Matumizi ya antibiotics
Antibiotics huua bakteria wazuri wanaolinda uke → fangasi wanaongezeka.

⭐ (d) Mavazi ya ndani yasiyoruhusu hewa
K**a nailoni, kufanya uke kuwa na unyevunyevu muda mrefu.

⭐ (e) Usafi kupita kiasi
Kuosha uke kwa sabuni kali, kuosha ndani ya uke (douching) hupunguza bakteria wazuri.

⭐ (f) Kisukari kisichodhibitiwa (diabetes)
Sukari nyingi kwenye uke husaidia fangasi kukua.

4️⃣ Madhara ya fangasi ukeni ikiwa hayajatibiwa

🔸 Maumivu makali ukeni na wakati wa tendo la ndoa
🔸 Vidonda ukeni kutokana na kukuna sana
🔸 Kutokea fangasi mara kwa mara (recurrent infections)
🔸 Uchafu kuongezeka na usumbufu wa kudumu
🔸 Kwa wajawazito: kuongezeka kwa hatari ya kujifungua mapema au mtoto kupata thrush

5️⃣ Jinsi ya kujikinga

✔ Vaa chupi za pamba (cotton)
✔ Epuka sabuni kali na manukato ukeni
✔ Kausha uke vizuri baada ya kuoga
✔ Kunywa maji ya kutosha
✔ Epuka kuvaa nguo za kubana muda mrefu
✔ Usitumie antibiotics bila sababu
✔ Dhibiti kisukari k**a unacho

K**a unasumbuliwa na changamoto hii piga simu moja kwa moja kupitia nmba hii upate suluhisho lako leo 0717 174 151

“Usijipe mawazo kwa watu ambao hata hawastahili kuwa tatizo kwenye maisha yako. Waachie waende.”_Usiruhusu maneno, tabia...
26/01/2026

“Usijipe mawazo kwa watu ambao hata hawastahili kuwa tatizo kwenye maisha yako. Waachie waende.”

_Usiruhusu maneno, tabia au mawazo ya watu wasiokujali yakuharibie amani yako.

_Sio kila mtu anastahili nafasi kwenye akili na moyo wako.

_Kujiachia ni njia ya kujilinda kisaikolojia na kihisia.

Wanasayansi wa China wapunguza ukubwa wa chipu ya semikonda na kuifanya kuwa nyuzi nyembamba k**a unywele wa binadamu.Ha...
26/01/2026

Wanasayansi wa China wapunguza ukubwa wa chipu ya semikonda na kuifanya kuwa nyuzi nyembamba k**a unywele wa binadamu.

Hatua hii ya kiteknolojia inaruhusu nyuzi hizo kufanya hesabu k**a chipu au kuonyesha taarifa k**a transista, jambo linalofungua njia kwa utengenezaji wa nguo janja (smart textiles) zinazoweza kuvaliwa k**a nguo.

Rudisha Furaha ya Tendo;​Tendo la ndoa linapaswa kuwa la kufurahisha na lenye kutosheleza pande zote mbili ndani ya muda...
12/01/2026

Rudisha Furaha ya Tendo;

Tendo la ndoa linapaswa kuwa la kufurahisha na lenye kutosheleza pande zote mbili ndani ya muda muafaka. Ukiona unatumia zaidi ya nusu saa na bado hufiki mwisho, mwili wako unahitaji marekebisho. Usiteseke kwa ukimya, suluhu ipo na ni ya uhakika.

📞 Mawasiliano: 0717174151

Address

Mlimani City
Dar Es Salaam
+255

Opening Hours

Monday 09:00 - 20:00
Tuesday 09:00 - 20:00
Wednesday 09:00 - 20:00
Thursday 09:00 - 20:00
Friday 09:00 - 20:00
Saturday 09:00 - 16:00
Sunday 00:00 - 18:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when The Afya posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram