FIT Mama Healthy Family

FIT Mama Healthy Family This Page is to Educate all about Health and Welness and how we can mentain Our Optimal Health and We Aloevera Plant

11/04/2026

Jana nilipata nafasi ya kusiriki kipindi ndani ya kituo cha ZBC na kuongelea juu ya ustawi (Wellness)wa maisha ya mwanadamu.

Ustawi wa maisha ya mwanadamu ni hali ya kuwa na afya njema kimwili, kiakili, kihisia, kijamii, kiroho na kiuchumi, ambapo mtu anaishi maisha yenye usawa, furaha na tija.
Ustawi wa mwanadamu unahitaji mlinganyo sawa katika maeneo haya.

1. Ustawi wa Mwili (Physical Wellness)
β€’ Unahusisha afya ya mwili wako.
β€’ Unajumuisha: lishe bora, mazoezi, usingizi wa kutosha, na kuepuka tabia hatarishi.
β€’ Mfano: kufanya mazoezi angalau dakika 30 kwa siku.

🧠 2. Ustawi wa Akili (Mental/Intellectual Wellness)
β€’ Uwezo wa kufikiri, kujifunza na kufanya maamuzi sahihi.
β€’ Unahusisha kujisomea, kusoma vitabu, na kujifunza vitu vipya.
β€’ Mfano: kusoma au kuhudhuria mafunzo mara kwa mara.

❀️ 3. Ustawi wa Hisia (Emotional Wellness)
β€’ Uwezo wa kuelewa na kudhibiti hisia zako.
β€’ Unahusisha kujitambua, kujikubali na kushughulikia msongo wa mawazo.
β€’ Mfano: kujieleza vizuri na kutafuta msaada unapohitaji.

🀝 4. Ustawi wa Kijamii (Social Wellness)
β€’ Mahusiano mazuri na watu wengine.
β€’ Unahusisha urafiki, familia, na kushirikiana na jamii.
β€’ Mfano: kushiriki shughuli za kijamii au kusaidiana.

πŸ’° 5. Ustawi wa Kifedha (Financial Wellness)
β€’ Uwezo wa kusimamia fedha zako vizuri.
β€’ Unahusisha kupanga bajeti, kuweka akiba, na kutumia kwa busara.
β€’ Mfano: kuwa na mpango wa matumizi ya kila mwezi.

🌍 6. Ustawi wa Mazingira (Environmental Wellness)
β€’ Kuishi katika mazingira salama na safi.
β€’ Unahusisha kulinda mazingira na kuhakikisha sehemu unayoishi ni rafiki kwa afya.
β€’ Mfano: usafi wa nyumbani na mazingira ya kazi.

πŸ™ 7. Ustawi wa Kiroho (Spiritual Wellness)
β€’ Uhusiano wako na imani, maadili na kusudi la maisha.
β€’ Unahusisha amani ya ndani na kuishi kwa misingi ya maadili.
β€’ Mfano: sala, tafakari au kufanya mambo yenye maana kwa wengine.

Ustawi wa kweli unahitaji usawa katika maeneo yote 7 β€” si mwili tu, bali akili, hisia, mahusiano, fedha, mazingira na roho.

Leo nitapata nafasi ya kuongelea mambo haya kwenye mkutano wa wanawake,Ustaarabu wa mwanamke.

09/04/2026

🌸 KARIBU MWANAMKE WA THAMANI 🌸

Nakukaribisha kwa moyo mkunjufu kwenye mkutano wa wanawake
✨ USTAARABU WA MWANAMKE ✨

πŸ“ Ukumbi: Golden Tulip, Malindi – Zanzibar
πŸ—“οΈ Tarehe: 11/04/2026
⏰ Muda: Saa 4:00 asubuhi – Saa 10:00 jioni

Njoo ujifunze, uungane na wanawake wenzako, na ujijenge kiuchumi, kiakili na kijamii. Huu ni wakati wako wa kung’ara na kukuza thamani yako πŸ’«

πŸ‘‰ Nitafurahi kuwa mwenyeji wako,Karibu sana.
Nipigie kwenye namba hii 0658174101 kupata ticket yako

08/04/2026

Karibuni sana.
Nipigie kupitia 0658174101 kupata kadi yako mapema kabisa,nitafurahi kuwa mwenyeji wako.


08/04/2026

Salam Aleikum Zanzibar,kwa mara nyingine tena,kwa heshima na shahuku kubwa sana,nimepokea mwaliko wa kuja kushirikisha uzoefu wangu katika kuhudumia wanawake katika eneo la Afya katika mkutano wa wanawake maarufu kwa jina la Ustaarabu wa Mwanamke.

Wanawake wote tukutane hoteli ya Golden Tulip,karibu na uwanja wa Ndege,siku ya jumamosi tarehe 11/04/2026.

Ili kuoara kadi yako wasiliana na mimi moja kwa moja kupitia namba 0658174101


01/04/2026

Our mood for April.πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯
Happy New Month of April Family.
Ukawe mwezi wa Baraka na Fanaka.

29/03/2026

Nilikua na wakati mzuri sana wa kujifunza pamoja na team na wageni wetu,Asanteni na hongereni sana kwa kuja kujifunza na kuongeza maarifa.

Wengine walitoka mikoani ili kuja kuhudhuria siku hii maalum kabisa.
Naaiita biashara ya ukarimu na namshuru Mungu naendelea kuuona ukarimu kwa watu wanao nizunguka hivyo nitaendelea kusambaza ukarimu.

29/03/2026

Jana tulikua na Master Class yetu ya kwanza kabisa 2026.FLP Company Tanzania ni familia moja kubwa ya wafanya biashara ya mtandao kupitia FLP Company.Moja ya msingi wa kujenga biashara yetu ni elimu ya mbinu za biashara (Business Skills) na hili ni jambo linapewa kipaumbele vizuri sana.

Jana tulipata nafasi ya kujifunza na kubadilishana uzoefu katika kukuza biashara zetu.
K**a wewe ni mtu unayependa ukuaji binafsi (personal development) mbali na kuongeza kipato,hapa ni mahali pako.


28/03/2026

My Skin Lately!😍πŸ₯°

Jamani,hii kitu ni nzuri mno,ngozi yangu haijawahi kuwa nzuri zaidi ya hivi,this is the best it has ever been 😍 considering am not getting any younger!

Upo wapi uletewe Marine Collagen yako uongeze confidence kwa kuboresha ngozi yako ya asili kabisa.

27/03/2026

Huku kwetu tunaimbiwa tukiwa tunafanya manunuzi,leo nimekutana na westlife millenials mpoo?

Huyu kaka na wenzake wapo Makongo mwisho,hua wanakua na vitu mbali mbali fresh kutoka shamba,njegere,mahindi,maembe au mananasi,ukipita waunge mkono hawa vijana wabunifu.


27/03/2026

Marine Collagen ya FLP inakupa Kiungo muhimu cha kujenga ngozi yako yaani Biotin na kukusaidia kuweza kuboresha ngozi yako,nywele zako,kucha zako na viungo vyako.
Aloe moisturizing lotion inakupa collagen na elastin ya kupaka ili kulisha ngozi yako na kuilinda na athari mazingira (jua,baridi na upepo) na kuifanya ngozi yako kubaki na muonekano wa ujana hata baada ya umri kusogea.

NB.Unaona ngozi yangu ilivyo hydrated,Flexibilty ya viungo vyangu je?Mimi mwenyewe naendelea kushuhudia maajabu ya hizi bidhaa.





26/03/2026

Asante sana Mteja wangu wa thamani kutoka Dodoma.Bidhaa hizi ni za mteja ambaye amejiandikisha kwenye kampuni ili aweze kupata bidhaa kwa matumizi yake binafsi.

Ndani ya FLP Company unaweza kupata punguzo la hadi 30% kwa manunuzi yako binafsi na kizuri zaidi ni kwamba ID yako ni ya kudumu,ni ya kimataifa na hakuna kushushwa cheo,yaani wewe hapo ulipofikia unaweza kuendelea kufurahia bidhaa kadiri unavyopenda.

Uzuri wa kujiunga pia ni kuwa siku ukiamua kufanya biashara ni ID hii hii itatumika na utaanzia hapo ulipo na kukuza punguzo lako la manunuzi mpaka 48% huku ukitengeneza vipato vingine kwa kujenga timu.Kumbuka ID ya FLP inarithika kwa hiyo inaweza kutumika kwa vizazi na vizazi.

Karibu sana tujenge Afya bora za familia zetu na tuokoe pesa katika matumizi yetu.



Address

Tanhouse, Victoria
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00

Telephone

+255753174107

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when FIT Mama Healthy Family posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to FIT Mama Healthy Family:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram