Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI

Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI Tunatoa matibabu ya Kibingwa na bobezi ya Mifupa, Upasuaji wa Ubongo,Mgongo, Mishipa ya fahamu, huduma za dharura na ajali

The Muhimbili Orthopaedic Institute (MOI) is an autonomous Institution established through an Act of Parliament No 7 of 1996 with the main objective of providing primary,secondary and Tertiary care for preventive and curative health services in the field of Orthopaedic,Traumatology and neurosurgery
The management of the Institute is based on Public/Private Mix concept geared towards performance improvement and and self sustainability.

MOI KUWA KITUO CHA KWANZA CHA UMAHIRI MATIBABU YA MGONGO  AFRIKA YA MASHARIKI NA KATINa Abdallah Nassoro - MOITaasisi ya...
22/04/2026

MOI KUWA KITUO CHA KWANZA CHA UMAHIRI MATIBABU YA MGONGO AFRIKA YA MASHARIKI NA KATI

Na Abdallah Nassoro - MOI

Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) imekuwa ya kwanza katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati kutoa matibabu ya kisasa ya mgongo bila upasuaji.

Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Mhe: Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya amebainisha hayo leo Aprili, 22, 2026 wakati akiongea na waandishi wa habari baada ya taasisi hiyo kufanikiwa kutoa matibabu hayo ya kisasa kwa wagonjwa 20.

“Kwa muda mrefu tumekuwa tukishirikiana na chuo kikuu cha afya cha Weill Cornell cha nchini Marekani katika ubadilishanaji wa afua mbalimbali za matibabu ya ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu katika nyanja za upasuaji, lakini leo hii tumekuja na afua mpya kabisa na ya kisasa duniani, nayo ni matibabu ya mgongo bila kupasua” amesema Dkt. Mpoki na kuongeza

“Kwa afua hii MOI imekuwa taasisi ya kwanza Afrika Mashariki na Kati kutoa matibabu haya na inakwenda kuwa kituo mahiri cha kufundishia wataalam katika ukanda huu, habari hii ni faraja kwa wagonjwa wote wenye matatizo ya mgongo ambao hawatalazimika kufanyiwa upasuaji”

Kwa upande wake Mratibu wa mafunzo hayo Daktari bingwa wa upasuaji wa ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu Dkt. Hamisi Shabani amesema matibabu ya mgongo bila kufanya upasuaji ni mbinu mpya na ya kisasa inayotoa nafuu kwa wagonjwa.

“Matibabu haya ni tofauti na yale ya mazoezi tiba (Physiotherapia), hii ni teknolojia ya kisasa na ni fahari kwetu MOI kuwa taasisi ya kwanza kutoa matibabu ya aina hii, na tutakuwa taasisi ya kwanza Afrika, wagonjwa hawa 20 watakuwa mashuhuda wa matibabu haya” amesema Dkt. Shabani

Mkurugenzi wa huduma za matibabu ya mgongo kutoka Chuo Kikuu cha Weill Cornell cha nchini Marekani, Prof. Roger Hartl amesema ushirkiano wa miaka 15 na MOI umekuwa wa mafanikio makubwa na kwamba utolewaji wa afua hiyo mpya ya matibabu ya mgongo bila kupasua ni kielelezo cha ufanisi.

OUR BEST EMPLOYEE’S MOI FROM EACH DIRECTORATE YEAR 2025 - 2026
22/04/2026

OUR BEST EMPLOYEE’S MOI FROM EACH DIRECTORATE YEAR 2025 - 2026

21/04/2026

“Naamini nipata uzoefu wa kutosha katika mafubzo haya pamoja na MOI”

Dkt. Zamzam Aberuka kutoka Uganda

SALAMU ZA PONGEZI
21/04/2026

SALAMU ZA PONGEZI

21/04/2026

“Naishukuru MOI kwa kuwa Taasisi bora yenye viwango vya hali ya juu”

Dkt. Siafa Mstando kutoka Liberia

21/04/2026

“MOI ni kutoa cha umahiri wa Matibabu ya Mgongo ukanda wa Afrika MAshariki na kati”

Dkt. Apima Abeil
Daktari kutoka Kenya

20/04/2026

“MOI ni Hospitali kubwa yenye vifaa vya kisasa na watalaam wabobezi, kujifunza kwao kutanisaidia kuboresha huduma nitakaporudi nyumbani (Congo)”

Dkt. France Kakulya
Daktari kutoka Nchi ya Congo

20/04/2026

“Mafunzo na kambi hii itajikita zaidi kujadili na kutibu maumivu sugu ya mgongo”

Dkt. Hamis Shaban
Daktari Bingwa Bobezi wa Ubongo, Mgongo na Mishipa ya fahamu MOI

20/04/2026

“Mafunzo na kambi hii itasaidia kutoa matibabu bora ya mgongo kwa wananchi”

Dkt. Lemeri Mchome
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji MOI

MOI NA WEILL CORNELL MAREKANI YARATIBU MAFUNZO NA KAMBI MAALUM YA MATIBABU YA MGONGONa Erick Dilli – MOITaasisi ya Tiba ...
20/04/2026

MOI NA WEILL CORNELL MAREKANI YARATIBU MAFUNZO NA KAMBI MAALUM YA MATIBABU YA MGONGO

Na Erick Dilli – MOI

Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI), kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Weill Cornell cha nchini Marekani pamoja na jumuiya ya wataalamu, Marekani Kaskazini, ya matibabu ya magonjwa ya mgongo (NASS) imeratibu mafunzo na kambi maalum ya matibabu ya mgongo yenye lengo la kuendelea kuboresha huduma za kibobezi kwa wananchi.

Akizungumza katika ufunguzi wa Mafunzo hayo leo Aprili 20, 2026 katika Hoteli ya New Afrika jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Dkt. Lemeri Mchome, alieleza umuhimu wa kambi na mafunzo hayo katika kukabiliana na changamoto ya magonjwa ya mgongo inayowakabili Watanzania wengi.

“Tunafahamu kuwa Watanzania wengi wanakumbwa na changamoto za maumivu ya mgongo. Katika kambi hii, tumewajumuisha wataalamu kutoka kada mbalimbali ikiwemo wauguzi, madaktari wa usingizi pamoja na wataalamu wa mazoezi tiba ili kutoa matibabu jumuishi ya maumivu sugu ya mgongo,” amesema Dkt. Mchome.

Kwa upande wake, Daktari Bingwa Bobezi wa Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu, Dkt. Hamis Shaban, amesema kuwa mkutano huo utahusisha mafunzo ya darasani pamoja na mafunzo kWa vitendo, ikiwemo upasuaji kwa wagonjwa zaidi ya 20 kwa mbinu mpya na za kısasa.

Kwa upande wake mkufunzi mbobezi kutoka Chuo Kikuu cha Weill Cornell nchini Marekani, Prof. Roger Hartl, ameishukuru MOI kwa ushirikiano na kusisitiza dhamira ya kuhakikisha Watanzania wanapata matibabu bora ya magonjwa ya mgongo bila kulazimika kwenda nje ya nchi.

Mafunzo hayo yamejumuisha madaktari na wataalamu mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi, ambapo wengi wao wameisifu MOI kwa kuwa na teknolojia ya kisasa na vifaa tiba vya viwango vya juu, hali inayoiwezesha kuwa kituo cha weledi katika matibabu ya ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu barani Afrika.

MOI KUSHIRIKIANA NA WEILL CORNELL KUENDESHA KAMBI MAALUM YA MATIBABU YA MGONGONa Erick Dilli – MOITaasisi ya Tiba ya Mif...
20/04/2026

MOI KUSHIRIKIANA NA WEILL CORNELL KUENDESHA KAMBI MAALUM YA MATIBABU YA MGONGO

Na Erick Dilli – MOI

Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI), kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Weill Cornell cha nchini Marekani, imeendesha kambi maalum ya matibabu ya maumivu sugu ya mgongo yenye lengo la kuboresha huduma za afya kwa wananchi.

Akizungumza katika ufunguzi wa kambi hiyo leo Aprili 20, 2026 uliofanyika katika Hoteli ya New Afrika jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Dkt. Lemeri Mchome, alieleza umuhimu wa kambi hiyo katika kukabiliana na changamoto ya maumivu ya mgongo inayowakabili Watanzania wengi.

“Tunafahamu kuwa Watanzania wengi wanakumbwa na changamoto za maumivu ya mgongo. Katika kambi hii, tumewajumuisha wataalamu kutoka kada mbalimbali ikiwemo wauguzi, madaktari wa usingizi pamoja na wataalamu wa mazoezi tiba ili kutoa matibabu jumuishi ya maumivu sugu ya mgongo,” amesema Dkt. Mchome.

Kwa upande wake, Daktari Bingwa Bobezi wa Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu, Dkt. Hamis Shaban, amesema kuwa mkutano huo utahusisha mafunzo ya darasani pamoja na matibabu kwa vitendo, ikiwemo upasuaji kwa wagonjwa zaidi ya 20 watakaopatiwa huduma.

Naye Daktari Bingwa Mbobezi wa Ubongo kutoka Chuo Kikuu cha Weill Cornell nchini Marekani, Prof. Roger Hartl, ameishukuru MOI kwa ushirikiano huo na kusisitiza dhamira ya kuhakikisha Watanzania wanapata matibabu bora yatokanayo na magonjwa ya mgongo.

Mkutano huo umejumuisha madaktari na wataalamu mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi, ambapo wengi wao wameisifu MOI kwa kuwa na teknolojia ya kisasa na vifaa tiba vya viwango vya juu, hali inayoiwezesha kuwa kinara katika matibabu ya ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu barani Afrika.

TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI
18/04/2026

TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI

Address

P. O. BOX 65474
Dar Es Salam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI:

Share

Category

Our Story

The Muhimbili Orthopaedic Institute (MOI) is an autonomous Institution established through an Act of Parliament No 7 of 1996 with the main objective of providing primary,secondary and Tertiary care for preventive and curative health services in the field of Orthopaedic,Traumatology and neurosurgery The management of the Institute is based on Public/Private Mix concept geared towards performance improvement and and self sustainability.