Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI

Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI Tunatoa matibabu ya Kibingwa na bobezi ya Mifupa, Upasuaji wa Ubongo,Mgongo, Mishipa ya fahamu, huduma za dharura na ajali

The Muhimbili Orthopaedic Institute (MOI) is an autonomous Institution established through an Act of Parliament No 7 of 1996 with the main objective of providing primary,secondary and Tertiary care for preventive and curative health services in the field of Orthopaedic,Traumatology and neurosurgery
The management of the Institute is based on Public/Private Mix concept geared towards performance improvement and and self sustainability.

14/01/2026

Daktari bingwa mbobezi wa Mionzi kutoka MOI, Dkt. Mwanaabas Sued ameanza kutoa huduma mbalimbali za kibobezi za radiolojia kwa njia ya matundu madogo baada ya kurejea kutoka masomoni.

13/01/2026

"Naishukuru sana Serikali yetu chini ya Rais wetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan lakini pia hospitali ya MOI kwa ushirikiano wao wameweza kumpokea mtoto ameshaanza matibabu"

Bw. Simon Bryson
Mkazi wa Dar es Salaam

13/01/2026

“Tumepokea maelekezo kutoka kwa Mhe. Rais aliyeguswa na hali ya mtoto na tayari kashaanza kupatiwa matibabu ya kibingwa na kibobezi ya Ubongo, Mgongo na Mishipa ya fahamu katika Taasisi yetu”

Dkt. Mpoki Ulisubisya
Mkurugenzi Mtendaji- MOI

AMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUGHARAMIA MATIBABU YA MTOTO WAKENa Erick Dilli- MOIMkazi wa  Dar es Salaam, Simon Bryson amems...
13/01/2026

AMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUGHARAMIA MATIBABU YA MTOTO WAKE

Na Erick Dilli- MOI

Mkazi wa Dar es Salaam, Simon Bryson amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kugharamia matibabu ya mtoto wake Nilsa Simon kufuatia ombi lake kupitia mitandao ya kijamii mtoto wake asaidiwe matibabu .

Bw. Simon ametoa shukurani hizo leo Januari 13, 2025, wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Taasisi ya MOI ambako mtoto wake anaendelea na matibabu.

“Ninamshukuru sana Rais wetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa moyo wake wa upendo na utu... Bila msaada wa serikali, isingekuwa rahisi kumpatia mtoto wangu matibabu haya ya kibingwa. Mwenyezi Mungu ambariki Rais wetu na aendelee kuwasaidia Watanzania wenye uhitaji.” amesema Bw. Simon

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Mhe. Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya amesema Serikali imeendelea kuonyesha dhamira ya dhati katika kusaidia wananchi, hususani wenye changamoto za kiafya zinazohitaji matibabu ya gharama kubwa.

“Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Samia imeweka kipaumbele katika afya za wananchi. Tumeendelea kupokea wagonjwa wengi wanaosaidiwa kupitia mifumo mbalimbali ya serikali, jambo linaloonesha dhamira ya kweli ya kuwahudumia Watanzania,” amesema Dkt. Mpoki.

Naye Dkt. Hamis Shabani, Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo wa MOI, amewataka wanawake kuchukua tahadhari mapema kabla ya ujauzito ili kuepuka matatizo ya kiafya kwa watoto wachanga.

“Tunawasihi wanawake wote walio kwenye umri wa kuzaa kunywa madini ya folic acid kabla na wakati wa ujauzito. Hii husaidia kwa kiasi kikubwa kuzuia watoto kuzaliwa na matatizo k**a kichwa kikubwa na mgongo wazi,” amesema Dkt. Shabani

HERI YA MIAKA 62 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR
12/01/2026

HERI YA MIAKA 62 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

12/01/2026

MHE. NKINGWA APONGEZA HUDUMA BORA ZA MOI

MBOGWE NSOGA YAWAFARIJI WAGONJWA  MOINa Erick Dilli – MOIKampuni ya ushonaji nguo ya Mbogwe Nsoga imewafariji wagonjwa w...
11/01/2026

MBOGWE NSOGA YAWAFARIJI WAGONJWA MOI

Na Erick Dilli – MOI

Kampuni ya ushonaji nguo ya Mbogwe Nsoga imewafariji wagonjwa waliolazwa katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) kwa kuwapatia zawadi ya nguo.

Faraja hiyo imetolewa leo Januari 11, 2026, wakati kampuni hiyo ilipotembelea MOI ikiongozana na Mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Jimbo la Mbogwe, Mkoa wa Geita, Mhe. Ferguson Nkingwa, kwa lengo la kuwafariji na kuwatia moyo wagonjwa.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Mhe. Nkingwa amesema kuwa asilimia kubwa ya wagonjwa waliopo MOI ni majeruhi wa ajali, ambapo wengi wao wanatoka katika familia zenye kipato cha chini, hali inayowafanya washindwe kumudu mahitaji ya msingi wakiwa wodini.

“Tumekuja hapa MOI kwa kushirikiana na kampuni ya Mbogwe Nsoga ili kuwafariji wagonjwa. Tumewapatia nguo mbili hadi tatu kwa kila mgonjwa kuanzia wodi za watoto, watu wazima, ICU pamoja na HDU,” amesema Mhe. Nkingwa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kampuni ya Mbogwe Nsoga, Bw. Peter Deus, amesema kuwa kampuni hiyo inatambua mahitaji makubwa ya wagonjwa waliolazwa hospitalini, jambo lililoisukuma kutimiza ahadi yake ya kufanya tendo la huruma.

“Kama kampuni, tuliahidi siku moja tutafanya jambo la kuwafariji wagonjwa, na leo tumeanza kutekeleza ahadi hiyo hapa MOI,” amesema Bw. Deus.

Naye mmoja wa wanufaika wa faraja hiyo, Bi. Asha Juma, ameishukuru kampuni hiyo kwa kujitolea na kuonesha upendo kwa wagonjwa waliolazwa wodini.

“Tunawashukuru sana kwa kutuona na kutufariji. Tunaomba muendelee na moyo huo wa kusaidia hata wengine wenye uhitaji,” amesema Bi. Asha.

TUNATAFUTA NDUGU ZAKE
09/01/2026

TUNATAFUTA NDUGU ZAKE

Je unasumbuliwa na maumivu ya mgongo,kichwa na nyonga?
08/01/2026

Je unasumbuliwa na maumivu ya mgongo,kichwa na nyonga?

Matukio katika picha wakati ambapo Wataalamu wa MOI wakisikiliza na kujibu maoni, ushauri, changamoto, mapendekezo na po...
07/01/2026

Matukio katika picha wakati ambapo Wataalamu wa MOI wakisikiliza na kujibu maoni, ushauri, changamoto, mapendekezo na pongezi kutoka kwa wagonjwa na ndugu wa wagonjwa .

Tukio hilo limefanyika leo Jumatano Januari 07, 2026 katika eneo la kusubiria huduma lililopo katika Taasisi hiyo.

WATU 602 WAREJESHEWA TABASAMU BAADA YA KUPEWA MIGUU NA MIKONO BANDIA BURENa Abdallah Nassoro-MOIZaidi ya watu 602 waliop...
07/01/2026

WATU 602 WAREJESHEWA TABASAMU BAADA YA KUPEWA MIGUU NA MIKONO BANDIA BURE

Na Abdallah Nassoro-MOI

Zaidi ya watu 602 waliopoteza miguu au mikono kutokana na sababu mbalimbali wamerejeshewa tabasamu baada ya kupatiwa viungo bandia bure katika kambi maalum ya utoaji wa huduma hizo iliyoandaliwa na Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) kwa kushirikiana na SBMVSS Jaipur India na Ubalozi wa India Nchini.

Kambi hiyo iliyoanza November 26, 2025 imefungwa rasmi jana Januari 06, 2026 na Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Mhe. Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya ambaye amepongeza mafanikio yaliyofikiwa na kambi hiyo.

“Tumeambiwa hapa kuwa hadi kufikia leo Januari 6, 2025 watu 602 wamepatiwa viungo bandia, lengo lilikuwa kuwahudumia walengwa 600…hili ni jambo la kujivunia kwasababu huu ni msaada wa kibinadamu unaogusa utu, upendo na kurejesha tabasamu kwa wahitaji” amesema Dkt. Mpoki na kuongeza kuwa

“Sisi MOI tumesajili zaidi ya wahitaji 1,350 kwahiyo hawa waliofaidika na kambi hii ni k**a asilimia 45, kuna asilimia 55 bado hawajafikiwa, hivyo wakati tukihitimisha kambi hii tunakwenda kujipanga ndani ya mda mfupi kuona namna ya kuwafikia hawa waliobaki”

Amefafanua kuwa wataalam wa MOI wameshirki kubadilishana ujuzi wa teknolojia mpya ya utengenezaji wa viungo hivyo kwa bei nafuu na kwamba kutokana na wahitaji kutoka mikoa yote, kambi zitakazofuata zitaangalia namna ya kusogeza huduma hizo karibu na wahitaji ili kuwapunguzia adha ya kusafiri umbali mrefu.

“MOI tutafanya ufuatiliaji kwa waliofaidika na kambi hii ili kuona maendeleo yao na kwa wale watakaobainika kuwa na changamoto za utumiaji, vifaa vyao vitarebishwa ili kuendeleza tabasamu lao” amesisitiza Dkt. Mpoki

Kwa upande wake Balozi wa India Nchini Tanzania Mhe. Bishwadip Dey amesema kambi hiyo licha ya kufungwa rasmi jana bado watoa huduma watendelea kutoa viungo bandia hadi kufikia Januari 10, 2025.

“Tabasamu ndiyo lugha inayounganisha Dunia, inavunja vikwazo vya lugha zetu na leo taasisi ya SBMVSS Jaipur India, Ubalozi wa India, Chama cha Wagonjwa wa Kisukari na MOI tumeweza kurejesha tabasamu kwa wahitaji hawa, kwa tabasamu lao wameweza kuwasiliana na Dunia” amesema Mhe. Dey na kuongeza

“Msaada huu h

Address

P. O. BOX 65474
Dar Es Salam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category

Our Story

The Muhimbili Orthopaedic Institute (MOI) is an autonomous Institution established through an Act of Parliament No 7 of 1996 with the main objective of providing primary,secondary and Tertiary care for preventive and curative health services in the field of Orthopaedic,Traumatology and neurosurgery The management of the Institute is based on Public/Private Mix concept geared towards performance improvement and and self sustainability.