Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI

Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI Taasisi ya Mifupa MOI
Huduma za Kibingwa za Mifupa, Upasuaji wa Ubongo,Mgongo ,Mishipa ya Fahamu na Ajali

The Muhimbili Orthopaedic Institute (MOI) is an autonomous Institution established through an Act of Parliament No 7 of 1996 with the main objective of providing primary,secondary and Tertiary care for preventive and curative health services in the field of Orthopaedic,Traumatology and neurosurgery
The management of the Institute is based on Public/Private Mix concept geared towards performance improvement and and self sustainability.

MOI YATAMBUA WIKI YA USTAWI WA JAMII KWA MAFUNZO MAALUM KWA WATUMISHI WA TAASISI HIYONa Amani Nsello- MOIIkiwa Wiki ya U...
28/08/2025

MOI YATAMBUA WIKI YA USTAWI WA JAMII KWA MAFUNZO MAALUM KWA WATUMISHI WA TAASISI HIYO

Na Amani Nsello- MOI

Ikiwa Wiki ya Ustawi wa Jamii Kitaifa ikiendelea kuadhimishwa kuanzia tarehe 25 hadi 30 Agosti 2025 katika viwanja vya Chuo cha Ustawi wa Jamii jijini Dar es Salaam chini ya kauli mbiu “Pata Msaada wa Kisaikolojia; Imarisha Afya ya Akili,” Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) imetambua umuhimu wake kwa kutoa mafunzo maalum kwa watumishi wake.

Mafunzo hayo yalilenga kuwajengea uelewa juu ya nafasi na majukumu ya Afisa Ustawi wa Jamii hospitalini, ili kila mtumishi aweze kushirikiana ipasavyo katika kuwahudumia wagonjwa wenye changamoto za kijamii na kisaikolojia.

Mafunzo hayo yalifunguliwa Agosti 27, 2025 na Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi MOI, Bw. Fidelis Minja ambaye alisema kwamba ni vema kwa kila mtumishi kufahamu majukumu ya Afisa Ustawi wa Jamii ili kuweza kutoa huduma bora kwa wagonjwa wenye mahitaji ya kijamii.

“Ni muhimu kila mtumishi kumfahamu Afisa Ustawi wa Jamii anafanya nini?... ili tuwajue mapema wagonjwa wenye changamoto kubwa kabla gharama za matibabu hazijawa kikwazo,” alisema Bw. Minja

Kwa upande wake, Afisa Ustawi wa Jamii Mwandamizi wa MOI, Bi. Stella Kihombo alieleza kwa kina majukumu makuu ya kada hiyo, ikiwemo kutoa msaada wa kisaikolojia kwa wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji, kufanya tathmini ya kijamii na kiuchumi, kufuatilia wagonjwa majumbani (outreach), kuunganisha wagonjwa na familia zao pamoja na kusimamia sera ya msamaha wa matibabu.

“Wapo wagonjwa wanaopoteza viungo kutokana na upasuaji, hawa wanahitaji msaada mkubwa wa kisaikolojia ili kuimarisha afya ya akili na kuendelea na maisha yao,” alisema Bi. Stella

Naye, Bi. Furaha Godfrey, mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo, alisema kupitia mafunzo hayo yamemjengea uwezo wa kutambua mchango mkubwa wa Afisa Ustawi wa Jamii katika masuala ya afya na tiba kwa ujumla.

MENEJIMENTI MOI YAPIGWA MSASA UTEKELEZAJI BAJETI 2025/6 Na Amani Nsello- MOIMenejimenti ya Taasisi ya Tiba ya Mifupa na ...
28/08/2025

MENEJIMENTI MOI YAPIGWA MSASA UTEKELEZAJI BAJETI 2025/6

Na Amani Nsello- MOI

Menejimenti ya Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) imepatiwa mafunzo ya utekelezaji bora wa bajeti ya maendeleo ya Taasisi hiyo ya mwaka wa fedha 2025/26 ili kuendelea kuboresha huduma kufikia dira ya taifa ya 2050.

Hayo yalibainishwa Agosti 26, 2025 na Meneja Mipango, Ufuatiliji & Tathimini wa MOI, Bw. Elisha James Sibale wakati wa mafunzo ya utekelezaji wa mpango na bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026 kwa wajumbe wa menejimenti ya MOI.

Bw. Sibale alisema taasisi imejipanga kuhakikisha rasilimali zilizotengwa zinatumika kwa ufanisi mkubwa

“Bajeti ya MOI kwa mwaka wa fedha 2025/2026 imejikita katika uwekezaji wa huduma za kibingwa, tafiti na matumizi ya teknolojia ya kisasa. Hatua hii inalenga kuhakikisha tunachangia moja kwa moja kufikia azma ya Taifa iliyoainishwa kwenye Mpango wa Taifa wa miaka mitano pamoja na kujipanga vema kuanza utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2050 kupitia Mpango na Bajeti utakao andaliwa kwa mwaka wa fedha 2026/2027” alisema Bw. Sibale

Kwa upande wake, Mchumi Mkuu kutoka Wizara ya Afya, Bw.Mintanga Milulu, alisema kuwa wizara itaendelea kusimamia na kuhakikisha taasisi za afya zinatekeleza bajeti kwa kuzingatia vipaumbele vya kitaifa.

“MOI ni moja ya nguzo muhimu katika sekta ya afya, hivyo utekelezaji wake wa mpango na bajeti lazima uendane na dira ya taifa. Wizara itaendelea kutoa usimamizi wa karibu na msaada wa kitaalamu,” alisema Bw. Milulu

Aidha, Mtakwimu Mkuu kutoka Ofisi ya Msajili wa Hazina, Bi. Mary Mshangila, alisema kwamba serikali imeweka mkazo kwenye matumizi sahihi ya fedha za umma, kuhakikisha taasisi zinabaki na uendelevu wa kifedha

“Ofisi ya Msajili wa Hazina itaendelea kuhakikisha taasisi k**a MOI zinapata usimamizi bora wa kifedha. Tunataka kila shilingi inayotolewa ichangie moja kwa moja katika kufikia malengo ya maendeleo ya taifa ifikapo mwaka 2050,” alisema Bi. Mary

26/08/2025
26/08/2025
DKT. NJEKELA APONGEZA MOI KWA UTOAJI HUDUMA KATIKA KIKAO CHA WENYEVITI WA BODI NA WAKUU WA TAASISI ARUSHANa Mwandishi we...
25/08/2025

DKT. NJEKELA APONGEZA MOI KWA UTOAJI HUDUMA KATIKA KIKAO CHA WENYEVITI WA BODI NA WAKUU WA TAASISI ARUSHA

Na Mwandishi wetu- Arusha

Mwenyekiti wa bodi ya wadhamini MOI Dkt. Marina Njelekela ameipongeza menejimenti ya MOI kwa uamuzi wake wa kushiriki na kutoa huduma kwa washiriki wa mkutano wa wenyeviti wa bodi na wakuu wa Taasisi unaofanyika katika ukumbi wa AICC Arusha.

Dkt. Njelekela ametoa pongezi hizo Leo 25/08/2025 alipotembelea eneo la kutolea huduma la MOI katika ukumbi wa AICC

“Nawapongeza menejimenti nzima ya MOI ikiongozwa na Mhe. Balozi Dkt. Mpoki Ukisubisya kwa uamuzi huu mzuri wenye tija wa kuja kutoa huduma kwa ashiriki wa mkutano huu mkubwa na muhimu, hongereni sana “ Alisema Dkt. Njelekela

Pia , Dkt Njelekela amepongeza ushirikiano kati ya Taasisi ya MOI, Taasisi ya Moyo JKCI na Hospitali ya AICC katika kuwahudumia washiriki wa mkutano huo.

Awali, Mkurugenzi mtendaji wa MOI Mhe. Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya alimuarifu Dkt. Njelekela kwamba MOI imeleta madaktari bingwa wa mifupa, Ubongo, Mgongo, viungo na mishipa ya fahamu ili watoe huduma za ushauri (Consultation) kwa washiriki wa mkutano huo ambapo wale watakaohitaji uchunguzi zaidi watapewa rufaa kwenda MOI

Taasisi ya MOI imeanza kutoa huduma kwenye kikao kazi cha Wenyeviti wa bodi na wakuu wa Taasisi za umma 2025 jijini Arusha kuanzia Agosti 23, 2025 na kutamati Agosti 26, 2025.

MADAKTARI  BINGWA WA MIFUPA 43 WANOLEWA MBINU MPYA ZA KUTIBU MIFUPA ILIYOVUNJIKA NA MADHARA YATOKANAYO NA AJALINa Amani ...
24/08/2025

MADAKTARI BINGWA WA MIFUPA 43 WANOLEWA MBINU MPYA ZA KUTIBU MIFUPA ILIYOVUNJIKA NA MADHARA YATOKANAYO NA AJALI

Na Amani Nsello- Dar es Salaam

Jumla ya madaktari bingwa 43 wa mifupa kutoka nchi za Tanzania, Uganda, Rwanda, Zambia na Zimbabwe wamepatiwa mafunzo ya kitaalam ya Teknolojia mpya na za kisasa za kutibu mifupa iliyovunjika.

Mafunzo hayo yaliyoendeshwa kwa siku 3 na taasisi ya AO Alliance ya nchini Marekani kwa kushirikiana na Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) katika hoteli ya Protea (Courtyard), jijini Dar es Salaam, yalihusisha mbinu mbalimbali za kibingwa na za kisasa katika matibabu ya mifupa iliyovunjika pamoja na madhara yatokanayo na ajali.

Hayo yamebainishwa leo Jumapili Agosti 24, 2025 na Mratibu wa mafunzo hayo ambaye pia ni Daktari Bingwa Mbobezi wa Upasuaji wa Mifupa kutoka MOI Dkt. Joseph Mwanga, ambaye ameeleza kuwa mafunzo hayo ni sehemu ya mkakati wa kuwajengea uwezo wataalam wa tiba ya mifupa barani Afrika ili kuhakikisha wagonjwa wanapata huduma bora na za viwango vya kimataifa.

“Kozi hii imelenga kuwajengea uwezo na kuwakumbusha madaktari bingwa katika kutumia njia sahihi zinazoheshimu baiolojia ya mfupa na tishu laini, huku zikihakikisha mgonjwa anapona haraka na kurejea katika shughuli zake za kila siku.” amesema Dkt. Mwanga

Kwa upande wake, mmoja wa wakufunzi wa kimataifa kutoka Marekani katika Taasisi ya AO Alliance Dkt. Coscia Michael , amesema mafunzo hayo ni ya kipekee kwani yanawaandaa madaktari bingwa wa Afrika kushiriki katika mabadiliko makubwa ya kitaalam duniani.

“Tunawapa madaktari hawa nyenzo mpya ili waendane na mabadiliko ya kimataifa katika tiba ya mifupa... Hii ni hatua muhimu ya kuboresha huduma za afya barani Afrika na kupunguza changamoto za muda mrefu za wagonjwa.” amesema Dkt. Michael

Nao washiriki wa mafunzo hayo wameeleza namna walivyonufaika. Dkt. William Mgisha, Daktari bingwa wa upasuaji wa mifupa MOI, amesema kuwa mafunzo hayo yamemsaidia kupata uelewa wa mbinu za upasuaji usio na madhara makubwa kwa wagonjwa.

Mshiriki mwingine, Dkt. Kuzivakwesha Mbiriri kutoka Hospitali ya Parirenyatwa ya nchini Zimbabwe, amesema kwamba mafunzo hayo yatawezesha kuboresha huduma kwa majeruhi.

Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) inashiriki katika kikao kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Waku...
24/08/2025

Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) inashiriki katika kikao kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma (CEOs Forum 2025) kinachofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), kwa ajili ya kutoa na kuonesha Huduma za Kibingwa na Kibobezi

DKT. MPOKI APONGEZA USHIRIKIANO WA UTOAJI HUDUMA KATI YA MOI, JKCI NA AICCNa Erick Dilli- ARUSHAMkurugenzi Mtendaji wa T...
24/08/2025

DKT. MPOKI APONGEZA USHIRIKIANO WA UTOAJI HUDUMA KATI YA MOI, JKCI NA AICC

Na Erick Dilli- ARUSHA

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI), Mhe. Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya, amepongeza ushirikiano mzuri wa utoaji huduma za afya kati ya MOI, Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na Hospitali ya AICC, katika kikao kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Wakuu wa Taasisi za Umma kinachoendelea jijini Arusha.

Dkt. Mpoki ametoa pongezi hizo leo, Agosti 24, 2025, mara baada ya kutembelea maeneo ya utoaji huduma kwa washiriki wa kikao kazi hicho kinachofanyika katika Ukumbi wa AICC, Arusha.

“Mpangilio wa utoaji huduma umekaa vizuri, kuanzia sehemu ya viongozi kusubiria matibabu hadi hatua ya mwisho... Kinachofurahisha zaidi ni kuona kila Taasisi inashirikiana kwa namna yake kuhakikisha huduma inatolewa kwa ubora,” amesema Dkt. Mpoki.

Aidha, Daktari Bingwa wa Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu kutoka MOI, Dkt. zarina Shabhay, ametoa wito kwa viongozi wanaoshiriki mkutano huo kujitokeza kwa wingi kupata huduma.

Dkt. Mpoki aliambatana na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo (JKCI), Dkt. Peter Kisenge, ambapo wote waliridhishwa na maandalizi bora na namna huduma zinavyotolewa kwa washiriki wa kikao kazi hicho.

FAMILIA YA MURO YATOA TUZO YA PONGEZI KWA WATAALAMU WA WODI 4B MOINa Martha Kimaro- MOIFamilia ya Dkt. Abraham Muro wa T...
20/08/2025

FAMILIA YA MURO YATOA TUZO YA PONGEZI KWA WATAALAMU WA WODI 4B MOI

Na Martha Kimaro- MOI

Familia ya Dkt. Abraham Muro wa Tegeta jijini Dar es Salaam imetoa tuzo ya pongezi kwa madaktari na wauguzi wanaohudumu katika wodi namba 4B ya Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI), k**a ishara ya shukrani kwa huduma bora walizozitoa kwa mama yao aliyekuwa akipatiwa matibabu katika taasisi hiyo.

Tukio hilo lilifanyika tarehe 18 Agosti 2025, ambapo Bi. Isabella Muro, kwa niaba ya familia, aliwashukuru viongozi na wataalamu wa wodi hiyo kwa kumhudumia kwa upendo mama yao Desphoria Muro aliyekuwa amelazwa katika wodi hiyo kwa matibabu.

“Katika kutambua huduma bora zinazotolewa na MOI, familia yetu imeona ni vyema kuwakabidhi cheti hiki cha pongezi k**a shukrani kwa matibabu bora yaliyotolewa kwa mama yetu aliyekuwa na changamoto ya goti. Hakika moyo wenu wa kujituma umeacha alama njema katika familia yetu,” alisema Bi. Isabella.

Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo, Kiongozi wa Wodi 4B MOI, Bi. Sada Mbilinyi, aliahidi kuendelea kutoa huduma bora kwa wagonjwa wote k**a sehemu ya misingi ya taasisi hiyo.

“Kwa kushirikiana na uongozi na watumishi wenzangu, tunaahidi kuendelea kutoa huduma bora kwa wagonjwa wetu na kuhakikisha wanarejea katika shughuli zao wakiwa na amani ya moyo,” alisema Bi. Mbilinyi.

Address

P.O.BOX 65474
Dar Es Salam
+255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category

Our Story

The Muhimbili Orthopaedic Institute (MOI) is an autonomous Institution established through an Act of Parliament No 7 of 1996 with the main objective of providing primary,secondary and Tertiary care for preventive and curative health services in the field of Orthopaedic,Traumatology and neurosurgery The management of the Institute is based on Public/Private Mix concept geared towards performance improvement and and self sustainability.