Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI

Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI Tunatoa matibabu ya Kibingwa na bobezi ya Mifupa, Upasuaji wa Ubongo,Mgongo, Mishipa ya fahamu, huduma za dharura na ajali

The Muhimbili Orthopaedic Institute (MOI) is an autonomous Institution established through an Act of Parliament No 7 of 1996 with the main objective of providing primary,secondary and Tertiary care for preventive and curative health services in the field of Orthopaedic,Traumatology and neurosurgery
The management of the Institute is based on Public/Private Mix concept geared towards performance improvement and and self sustainability.

WAGONJWA 783 WAPATA HUDUMA ZA KIBINGWA, WIKI YA KUJIKINGA NA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA MOINa Abdallah Nassoro - Mnazi Mmoj...
16/11/2025

WAGONJWA 783 WAPATA HUDUMA ZA KIBINGWA, WIKI YA KUJIKINGA NA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA MOI

Na Abdallah Nassoro - Mnazi Mmoja

Wagonjwa 783 wamefaidika na huduma za matibabu ya kibingwa na bobezi zilizotolewa na Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) katika wiki ya kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Kaimu Meneja wa Magonjwa ya Ndani na huduma za Dawa wa MOI Dkt. Deodata Matiko amebainisha hayo wakati wa ufungaji wa maadhimisho Novemba 15, 2025.

Dkt. Deodata amebainisha kuwa wagonjwa hao walifaidika na huduma za vipimo vya awali bila malipo, kuonana na madaktari bingwa, bobezi, elimu ya lishe, mazoezi tiba na viungo saidizi.

“Muitikio ulikuwa mkubwa sana, hadi leo tunahitisha kambi hii wagonjwa 783 wamepatiwa matibabu, wapo tuliowapa rufaa ya kuja MOI kuendelea na matibabu zaidi, wapo waliopata elimu na ushauri katika kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza” amesema Dkt. Deodata

Ameongeza kuwa “Baada ya kukamilisha kambi ya wananchi, Novemba 18, 2025 tutatoa matibabu k**a hayo kwa watumishi wa MOI na ndugu wa wagonjwa waliopo pale”

Amesema katika utoaji wa huduma hiyo bima za afya zitatumika kwa watumishi na huduma za vipimo vya awali bila malipo kwa wasio na bima ya afya.

“Lengo ni kuhalikisha huduma hii inawafilia si wananchi pekee bali kwa watumishi kwakuwa magonjwa haya hayachagui mtu...huduma kwa upande wa MOI zitatolewa hadi Ijumaa Novemba 21,2025” amefafanua

Tunatafuta ndugu zake
15/11/2025

Tunatafuta ndugu zake

14/11/2025

MGONJWA KUTOKA MALAWI AISHUKURU MOI KWA KUPATA MATIBABU YA KIBINGWA BOBEZI

MAMIA WAJITOKEZA KUPATA MATIBABU MNAZI MMOJANa Abdallah Nassoro-Mnazi MmojaMamia ya wakazi wa Dar es Salaam na viunga vy...
10/11/2025

MAMIA WAJITOKEZA KUPATA MATIBABU MNAZI MMOJA

Na Abdallah Nassoro-Mnazi Mmoja

Mamia ya wakazi wa Dar es Salaam na viunga vyake wamejitokeza kupata matibabu ya bila malipo ya uchunguzi wa awali wa magonjwa yasiyoambukiza yanayotolewa na madaktari bingwa na bobezi kutoka Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza.

Kaimu Meneja wa Magonjwa ya Ndani na Dawa Dkt. Deodata Matiko amesema zaidi ya wagonjwa 260 wamejitokeza kupata matibabu katika siku ya kwanza ya matibabu hayo

“Muitukio ni mkubwa, ukiacha hawa 260 tuliowasajili wapo wengine wengi tumewaomba waje kesho ili kutoka nafasi ya madaktari bingwa na bobezi kuhudumia hawa waliofika mapema” amesema Dkt. Deodata

Ameongeza kuwa “Tunaomba wateja wetu wasiwe na wasiwasi tupo hapa kuwahudumia hivyo waendelee kujitokeza kupata matibabu, hii ni fursa adhimu kwao”

Amesema huduma hizo zitaendelea kutolewa hadi jumamosi Novemba 15, 2025, hivyo ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kupata vipimo vya awali, matibabu na elimu ya kujikinga.

Kwa upande wake Hadija Mrisho ambaye ni mmoja wa wagonjwa ameishukuru MOI kwa kutoka huduma hizo bure ili kuwafukia wananchi wenye kipato cha chini.

“Tunafahamu kumuona daktari bingwa ni gharama kubwa lakini hapa leo ni bure, vipimo vya awali bure, Sina cha kusema zaidi ya kuishukuru MOI”

09/11/2025

“Tutafanya kambi maalum ya matibabu kwa magonjwa yasioambukiza katika viwanja vya Mnazi mmoja tarehe 10 mpaka 15 Novemba 2025 kuanzia saa 2 asubuhi mpaka saa 10 jioni, huduma ni bure na wenye bima zitatumika”

Dkt. Deodata Matiko
Daktari bingwa wa magonjwa ya ndani - MOI

Siku ya radiolojia duniani
08/11/2025

Siku ya radiolojia duniani

Taarifa kwa umma
07/11/2025

Taarifa kwa umma

MOI KUENDESHA KAMBI YA MAALUM YA UCHUNGUZI WA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA BILA MALIPO   Na Abdallah Nassoro-MOI Taasisi ya T...
07/11/2025

MOI KUENDESHA KAMBI YA MAALUM YA UCHUNGUZI WA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA BILA MALIPO

Na Abdallah Nassoro-MOI


Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) inautaarifu umma kuwa itaendesha zoezi la uchunguzi, elimu na ushauri wa magonjwa yasiyoambukiza kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam na viunga vyake, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza Duniani ambayo hufanyika kila wiki ya pili ya mwezi Novemba.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Mhe: Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya wakati akiongea na waandishi wa habari leo Ijumaa Novemba, 7, 2025 na kufafanua kuwa uchunguzi huo utafanywa na madaktari bingwa na bobezi kutoka MOI katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam kuanzia Jumatatu tarehe 10 mpaka Jumamosi tarehe 15 Novemba 2025, saa 2:00 asubuhi hadi saa 10:00 jioni.

“Huduma zitakazotolewa ni pamoja na uchunguzi wa awali, ushauri na elimu kwa magonjwa ya mifupa, ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu, kisukari, magonjwa ya moyo, shinikizo la damu na kiharusi. Pia kutakuwa na huduma za mazoezi tiba (Fiziotherapia) pamoja na ushauri wa tiba lishe “ amesema Dkt. Mpoki na kuongeza kuwa

“Huduma hizo zitatolewa bure kwa wagonjwa wasio na bima ya afya, na kwa wale wenye bima ya afya, bima zao zitatumika kupata huduma hizo ili kurahisisha muendelezo wa matibabu iwapo mgonjwa atatakiwa kufanya hivyo”

Kwa upande wake Kaimu Meneja wa kitengo cha magonjwa ya ndani na dawa, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya ndani Dkt. Deodata Matiko ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kupima afya zao ili wajue afya zao, kupata matibabu na kujikinga na magonjwa hayo.

Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MO) itaendesha zoezi la uchunguzi, elimu na ushauri wa magonjwa yasiyoamb...
06/11/2025

Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MO) itaendesha zoezi la uchunguzi, elimu na ushauri wa magonjwa yasiyoambukiza kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam na viunga vyake kuanzia tarehe 10 hadi 15 Novemba 2025 katika Viwanja vya Mnazi Mmoja vilivyopo Dar es Salaam.

Zoezi hizo zitatolewa bure kwa wagonjwa wasio na bima ya afya, kwa wale wenye bima ya afya, bima zao zitatumika kupata matibabu.

Salamu za pongezi
04/11/2025

Salamu za pongezi

Address

P. O. BOX 65474
Dar Es Salam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category

Our Story

The Muhimbili Orthopaedic Institute (MOI) is an autonomous Institution established through an Act of Parliament No 7 of 1996 with the main objective of providing primary,secondary and Tertiary care for preventive and curative health services in the field of Orthopaedic,Traumatology and neurosurgery The management of the Institute is based on Public/Private Mix concept geared towards performance improvement and and self sustainability.