Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI

Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI Taasisi ya Mifupa MOI
Huduma za Kibingwa za Mifupa, Upasuaji wa Ubongo,Mgongo ,Mishipa ya Fahamu na Ajali

The Muhimbili Orthopaedic Institute (MOI) is an autonomous Institution established through an Act of Parliament No 7 of 1996 with the main objective of providing primary,secondary and Tertiary care for preventive and curative health services in the field of Orthopaedic,Traumatology and neurosurgery
The management of the Institute is based on Public/Private Mix concept geared towards performance improvement and and self sustainability.

MOI YAENDELEA  KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WAGONJWANa Amani Nsello- MOITaasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (...
19/07/2025

MOI YAENDELEA KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WAGONJWA

Na Amani Nsello- MOI

Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) imeendelea kutoa matibabu kwa wagonjwa wa dharura bila kuhitaji malipo ya awali, ikiwa ni sehemu ya kujali maisha ya wagonjwa na kutekeleza wajibu wake wa kutoa huduma bora za afya kwa jamii.

Hayo yalibainishwa jana Julai 18, 2025 na Mkuu wa Kitengo cha Mapato wa MOI, Bw. Chediel Mziray wakati akijibu hoja za wagonjwa na ndugu wa wagonjwa ambapo amesema kuwa taasisi hiyo ina utaratibu wa kumhudumia mgonjwa wa dharura haraka iwezekanavyo bila kuzuia huduma kwa sababu ya malipo.

"Kwa wagonjwa wa dharura, MOI hatuzuii huduma kwa sababu ya fedha... Tunatoa huduma kwanza, malipo hufuata baadae. Kipaumbele ni kuokoa maisha ya mgonjwa. Baada ya mgonjwa kuwa katika hali tulivu, ndipo hatua za malipo hufuata kwa utaratibu rasmi wa taasisi" alisema Bw. Chediel na kuongezea

"Huu ni utaratibu uliowekwa mahsusi kusaidia kuokoa maisha na kuondoa mzigo kwa wananchi wakati wa dharura”

Aidha, alieleza kuwa mfumo huo unazingatia misingi ya utu, usawa na haki ya kila mtu kupata huduma za afya bila kujali hali yake ya kiuchumi wakati wa dharura.

Kwa upande wake, Ernest Mgogo, mkazi wa Dar es Salaam ambaye ni mmoja wa ndugu wa mgonjwa aliwapongeza watumishi wa MOI kwa kufanya kazi kwa bidii na kwa moyo wao wa kujitolea kuokoa maisha ya wagonjwa wa dharura hususani wa ajali za barabarani.

Taasisi ya MOI kupitia Menejimenti yake imetenga siku ya Jumatano na Ijumaa kuanzia saa 5 asubuhi hadi saa 6 mchana kwa ajili ya kusikiliza maoni, kero, changamoto na pongezi kutoka kwa wagonjwa na ndugu wa wagonjwa wanaopatiwa matibabu katika taasisi hiyo.

TAASISI YA FHAMAZ TRUST KUUNGA MKONO JITIHADA ZA MOI KUBORESHA HUDUMANa Erick Dilli- MOITaasisi isiyo ya Kiserikali ya F...
18/07/2025

TAASISI YA FHAMAZ TRUST KUUNGA MKONO JITIHADA ZA MOI KUBORESHA HUDUMA

Na Erick Dilli- MOI

Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Fhamaz Trust kutoka nchini Uingereza imeahidi kuchangia mashine mbili maalum za kuzalisha joto kwenye chumba cha upasuaji katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili MOI.

Hayo yamesemwa leo Julai 18/072025 na Bi. Zarnat Datoo ambaye ameambatana na mumewe ambaye pia mmiliki mwenza wa taasisi hiyo, amesema ahadi hiyo ya kuchangia mashine hizo imekuja baada ya kutembelea chumba cha upasuaji MOI.

“Kwa moyo wa amani na upendo tumeona ni vyema kuzidi kuweka alama pale ambapo mgonjwa anakuwa na furaha baada ya kufanyiwa upasuaji haswa kwa watoto wenye kichwa kikubwa na mgongo wazi” amesema Bi. Zarnat na kuongezea

“Tunaahidi kuongezea mashine hii ya kumpa mgonjwa joto wakati wa upasuaji pamoja na mashine ya kupasha joto maji au damu zinazotumika wakati wa upasuaji kwa lengo la kuwa sehemu katika kufanyikisha matibabu ya wagonjwa”

Kwa upande wake, Muuguzi Mbobezi kutoka chumba cha upasuaji MOI, Bw. Juma Rehani ameishukuru taasisi hiyo kwa kuzidi kuweka alama MOI haswa kwenye matibabu ya watoto wenye kichwa kikubwa na mgongo wazi kuanzia gharama za upasuaji na huduma nyinginezo.

FHAMAZ TRUST YACHANGIA MATIBABU YA WATOTO 25 WENYE VICHWA VIKUBWA NA MGONGO WAZI MOINa Erick Dilli- MOITaasisi isiyo ya ...
16/07/2025

FHAMAZ TRUST YACHANGIA MATIBABU YA WATOTO 25 WENYE VICHWA VIKUBWA NA MGONGO WAZI MOI

Na Erick Dilli- MOI

Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Fhamaz Trust imechangia matibabu kwa watoto 25 wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi waliolazwa na wanaoendelea kupatiwa matibabu katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI).

Akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo leo Jumatano Julai 16, 2025, Bi. Zarnat Datoo ambaye ameambatana na mume wake, pia mmiliki mwenza wa Taasisi hiyo Bw. Jamie Satchell kutoka nchini Uingereza ameeleza gharama walizochangia za matibabu na msaada mwingine wa kibinadamu.

“Mimi na mume wangu kwa uwezo wetu tumechangia gharama ya upasuaji kiasi cha shillingi milioni 10 za Kitanzania pamoja na kiasi cha shillingi milioni 3 za Kitanzania kwa ajili ya ununuzi wa dawa” amesema Bi. Zarnat na kuongezea

“Pamoja na kuchangia gharama hizo pia tumeweza kuwapatia kila mtoto na mzazi chakula pamoja na vifaa vya shejala kwa lengo la kuwapa tabasamu la moyo na pia kuwawezesha watoto kuendelea kujifunza hata wakiwepo hospitalini”

Kwa upande wake, Afisa Ustawi wa Jamii Mwandamizi wa MOI, Bi. Sophia Nasson ameishukuru taasisi hiyo kwa kuendelea kuwa wadau wakubwa kwa watoto wenye kichwa kikubwa na mgongo wazi wanaopatiwa matibabu katika taasisi hiyo.

WAJUMBE TIMU YA TATHIMINI NA UDHIBITI WA VIASHIRIA VYA HATARI MOI WANOLEWANa Abdallah Nassoro- MOITimu ya tathimini na u...
16/07/2025

WAJUMBE TIMU YA TATHIMINI NA UDHIBITI WA VIASHIRIA VYA HATARI MOI WANOLEWA

Na Abdallah Nassoro- MOI

Timu ya tathimini na udhibiti wa viashiria vya hatari ya Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) imeanza mafunzo ya siku tano ya kuainisha, kuchambua na kupendekeza njia za kukabiliana na viashiria vya hatari ili kuiwezesha taasisi kufikia malengo yake.

Mafunzo hayo yamefunguliwa leo Julai, 16, 2025 na Meneja Mipango, Ufuatiliaji na Tathimini wa MOI Bw. James Sibale kwa niaba ya Mkurugenzi wa Fedha na Mipango, ambaye amesema mafunzo hayo ni muhimu kwa ajili ya kuwajengea uwezo wajumbe wa kubainisha viashiria vya hatari vya taasisi.

“Ni jukumu letu wajumbe kuhakikisha mafunzo haya yanakuja na nyaraka muhimu ya taasisi, rejesta itakayoainisha viashiria vya hatari vya taasisi, kupima uzito wake na namna ya kukabiliana ili kuiwezesha taasisi kufikia malengo yake” Bw. Sibale amsema na kuongeza kuwa

“Ni nyaraka muhimu kwa ustawi wa taasisi yetu hivyo ni lazima tuwe makini katika kitengeneza ili mchakato wa kuipitisha uwe rahisi, nyaraka tutakayoitengeneza itapelekwa kwenye menejimenti na baadaye bodi ya wadhamini kabla ya kuwa nyaraka halali ya MOI”

Mratibu wa mafunzo hayo Getudusy Myayau amesema wajumbe kutoka kila kitengo na idara za taasisi ya MOI wanashiriki mafunzo hayo muhimu ya kuandaa rejista ya viashiria vya hatari vya taasisi na namna ya kukabiliana navyo.

“Mwisho wa mafunzo haya tunatarajia kuwa na rejista ya viashiria vya hatari vya taasisi na ndiyo maana tumechukua mjumbe kutoka kwenye kila kitengo na idara ili watusaidie kuainisha viashiria vya hatari katika maneono yao ya kazi na hatmaye tupate viashiria vya hatari vya taasisi” amesema Myayau

WANANCHI 1,908 WATEMBELEA BANDA LA MOI MAONESHO SABASABANa Erick Dilli- SABASABAWananchi 1,908 wametembelea Banda la Taa...
13/07/2025

WANANCHI 1,908 WATEMBELEA BANDA LA MOI MAONESHO SABASABA

Na Erick Dilli- SABASABA

Wananchi 1,908 wametembelea Banda la Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) katika maonesho ya 49 ya kimataifa ya biashara, Sabasaba 2025 yaliyomalizika leo Julai 13, 2025

Hayo yamebainishwa leo Julai 13, 2025 katika kilele cha Maonesho hayo na Daktari bingwa Mbobezi wa Mifupa MOI, Dkt. Tumaini Minja ambapo amesema wanamchi wenye changamoto za Mifupa, Ubongo, mgongo, nyonga, magoti wamenufaika na huduma hizo zilizotolewa kwa gharama nafuu pamoja na kupata elimu.

“Jumla ya wananchi 1,908, wametembelea katika Banda letu, kati ya hao 455 wamepatiwa matibabu na 1,503 wamepatiwa elimu ya afya wakati wa maonesho haya... Tulikuwa na sehemu mbili, ya matibabu yaani kliniki na maonesho ambapo wananchi walipata ushauri kutoka kwa watalaam wa lishe, viungo saidizi na Muuguzi kutoka chumba cha upasuaji” amesema Dkt. Minja na kuongezea

“Kwa wagonjwa ambao walihitajika kupata vipimo vikubwa vya MRI na CT Scan tumeweza kuwapa rufaa ya kwenda kupatiwa vipimo hivyo katika Taasisi yetu (MOI) kwa lengo la kuhakikisha mgonjwa tunaemuona hapa (Sabasaba) anapatiwa matibabu bora na sawa akifika katika Taasisi yetu”

Aidha, Afisa Muuguzi Mwandamizi MOI Bi. Scholastica Mansillo ameendelea kuhimiza wananchi wenye changamoto ya Mifupa, Mgongo, Ubongo na Mishipa ya fahamu kufika katika Taasisi ya MOI na kupata Matibabu kutoka kwa Madkatari bingwa na bobezi pamoja na Watalaam wengine kutoka Taasisi hiyo.

MOI yaendelea kutoa huduma za kibingwa na kibobezi Sabasaba
11/07/2025

MOI yaendelea kutoa huduma za kibingwa na kibobezi Sabasaba

*📍MOI tupo Sabasaba*Wananchi kutoka maeneo mbalimbali wameendelea kujitokeza kwa wingi katika banda la Taasisi ya tiba y...
10/07/2025

*📍MOI tupo Sabasaba*

Wananchi kutoka maeneo mbalimbali wameendelea kujitokeza kwa wingi katika banda la Taasisi ya tiba ya mifupa na ubongo Muhimbili (MOI) katika maonesho ya 49 ya kimataifa ya biashara Sabasaba kupata matibabu ya mifupa, ubongo, mgongo, mishipa ya fahamu pamoja na huduma za mazoezi tiba, tiba lishe, viungo saidizi, huduma za dawa na uchunguzi huduma za Radiolojia.

Wagonjwa wanaotembelea banda la MOI wanasajiliwa bure kwenye mfumo wa MOI.

Kliniki ya MOI inapatikana katika banda namba 12 Barabara ya Biashara Avenue katibu na banda la Woiso

Karibu MOI upate huduma za kibingwa na Kibobezi

,Kidigitali Zaidi.

Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) imepata tuzo ya kuwa mtoa huduma bora kwa wagonjwa wanaopata ajali k...
10/07/2025

Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) imepata tuzo ya kuwa mtoa huduma bora kwa wagonjwa wanaopata ajali kazini na magonjwa yatokanayo na kazi, ambao ni wanufaika na Fao la Matibabu linalo linalotolewa na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF).

Tuzo hiyo ilitolewa Julai 04, 2025 katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam katika kilele cha Maadhimisho ya miaka 10 ya mfuko huo, ikiwa ni ishara ya kutambua mchango mkubwa wa MOI katika kutoa huduma bora za haraka na zenye ufanisi kwa wafanyakazi waliopatwa na madhara wakiwa kazini.

Mgeni Rasmi wa Maadhimisho hayo alikuwa Mhe. Kassim Majaliwa (Mb), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akiambatana na Mhe. Ridhiwani Kikwete (Mb), Waziri wa Nchi - Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu). Ambapo Mhe. Ridhiwani aliongoza zoezi la utoaji wa tuzo.

MWENYEKITI BODI YA WADHAMINI  AIPONGEZA MOI KUSHUSHA GHARAMA ZA MATIBABU SABASABANa Abdallah Nassoro –SabasabaMwenyekiti...
07/07/2025

MWENYEKITI BODI YA WADHAMINI AIPONGEZA MOI KUSHUSHA GHARAMA ZA MATIBABU SABASABA

Na Abdallah Nassoro –Sabasaba

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) Dkt. Marina Njelekela leo Julai, 7, 2025 ametembelea banda la MOI katika maonesho ya kimataifa ya 49 ya biashara, Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam na kuipongeza taasisi hiyo kwa kushusha gharama za matibabu ili kuwawezesha wananchi wengi kupata huduma za kibingwa na kibobezi za mifupa, ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu.

Dkt. Njelekela amesema uamuzi wa kushusha ghalama za matibabu hadi Tsh. 5,000 kumuona daktari bingwa ni wa kupongezwa na kwamba umetoa fursa ya wananchi wenye kipato cha chini waliokuwa wanahitaji huduma za kibingwa na kibobezi lakini hawapati kutona na kushindwa kubudu gharama kuweza kupata huduma hizo katika banda la Sabasaba.

“Niwapongeze kwa uamuzi huu wa kushusha gharama za matibabu, sasa kwa Tsh. 5,000 tu mwananchi anapata huduma za kibingwa na kibobezi...usogezaji wa huduma hizi karibu na wananchi unalenga zaidi kuwapunguzia gharama za matibabu” amesema Dkt. Njelekela na kuongeza kuwa

“Muendelee kutangaza hizi huduma hapa Sabasaba nina amini wananchi wengi hawajapata taarifa hizi, ni jukumu letu kuhakikisha wananchi wanapata taarifa ili wazidi kujitokeza kwa wingi kupata matibabu haya, huduma munazotoa zinahitajika sana na wananchi wetu...nawapongeza watumishi wote waliokuja kutoa huduma katika banda hili, huduma ni nzuri na wanaonesha weledi kwa kile wanachowaeleza wananchi”

Kwa upande wake Mjumbe wa Bodi hiyo ya Wadhamini Bi, Zuhura Mawona amesisitiza umuhimu wa wananchi kupata taarifa juu ya ushiriki wa MOI katika maonesho hayo na huduma wamazotoa.

“Kuna elimu ya lishe bora inatolewa hapa, ni nzuri sana ili kujikinga na maradhi mbalimbali, elimu ya mifupa, mgongo, mishapa ya fahamu, mazoezi tiba na vipimo vya ultrasound vyote hivyo ninapatikana hapa banda la MOI” amesema Bi, Mawona

Meneja Uhusiano wa MOI, Bw. Patrick Mvungi amasema ujio huo wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini MOI umelenga kuona namna ambavyo taasisi hiyo inatoa huduma za kibingwa na kibobezi kwa wananchi na kuwatia moyo watumishi.

Yanga MOI washindi wa jumla michezo ya MOI day 2025
07/07/2025

Yanga MOI washindi wa jumla michezo ya MOI day 2025

Bodi ya Wadhamini, Menejimenti na Watumishi wote wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) tunawatakia Wata...
07/07/2025

Bodi ya Wadhamini, Menejimenti na Watumishi wote wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) tunawatakia Watanzania wote heri ya siku ya Sabasaba 2025.

Maria Magasta mshindi wa MOI talent show 2025
07/07/2025

Maria Magasta mshindi wa MOI talent show 2025

Address

Dar Es Salam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Taasisi ya Tiba ya Mifupa - MOI:

Share

Category

Our Story

The Muhimbili Orthopaedic Institute (MOI) is an autonomous Institution established through an Act of Parliament No 7 of 1996 with the main objective of providing primary,secondary and Tertiary care for preventive and curative health services in the field of Orthopaedic,Traumatology and neurosurgery The management of the Institute is based on Public/Private Mix concept geared towards performance improvement and and self sustainability.