
15/09/2022
UGONJWA WA U.T.I (URINARY TRACT INFECTION) – CHANZO, DALILI & TIBA
UTANGULIZI – UJUE UGONJWA WA U.T.I (URINARY TRACT INFECTION)
U.T.I ni maambukizi kwa njia ya mkojo na huathiri mfumo wa mkojo na mfumo wa uzazi, wadudu huathiri sana kibofu na urethra. Jina U.T.I ni kifupi cha URINARY TRACT INFECTION (Neno la kingereza) watu wengi huzoea kuita hivyo wakijua ni jina la kiswahili, imeshazoeleka hivyo. Jinsia ya k**e wana hatari kubwa kuliko jinsia ya kiume. Maambukizi yakwenye kibofu huleta maumivu makali, madhara makubwa hutokea maambukizi yakifika mpaka kwenye figo. U.T.I husababishwa na wadudu wadogo sana ambao ni bakteria waitwao Escherichia coli (E. coli), wanapoingia mwilini na kuenda kuathiri mfumo wa mkojo.
U.T.I hutibika haraka kwa mtu ambaye atatumia dawa na pia yaweza kuleta madhara makubwa isipotibika huweza kuathiri mfumo wa uzazi, kibofu, na sehemu mbalimbali, tunashauri mtu mwenye U.T.I inatakiwa awe msafi na kubadili mienendo iliyo hatarini.
UTI+Header
MGAWANYO WA U.T.I
Kuna mgawanyo wa aina mbili za U.T.I
Maambukizi ya Upande wa juu – Hii hujumuisha Figo na Ureta
Maambukizi ya Upande wa chini – Hii hujumuisha Kibofu na Urethra
CHANZO CHA MAAMBUKIZI YA U.T.I
U.T.I husababishwa na wadudu wadogo sana ambao ni bakteria waitwao Escherichia coli (E. coli), wanapoingia mwilini na kuenda kuathiri mfumo wa mkojo, vitu vifuatavyo vinaweza kukuingiza kwenye hatari ya kupata U.T.I;
Kinga ya mwili kuto kuwa imara
Kutumia Vifaa au Dawa za kuzuia mimba
Kwa wa k**e; Kupungua kwa homoni ya estrogeni
Mtu mwenye kisukari
Kutumia choo kichafu na kutumia idadi kubwa ya watu
Kuwa na tatizo la mmeng’enyo na tatizo la choo
Kukaa kwa mda mrefu bila kutembeatembea
DALILI ZA MTU MWENYE U.T.I
Dalili za mtu mwenye tatizo la U.T.I hutokea tofauti kulingana na umri, jinsia na sehemu iliyoathiriwa. Hizo dalili ni k**a;
urinary_tract_infections-1
Kujihisi mchovu na kutokujisikia vizuri
Kukojoa kwa shida na kujilazimisha
Maumivu wakati wa kukojoa
Kukojoa kiasi kidogo na mara kwa mara
Mkojo kutoa harufu kali
Mkojo kuwa na rangi tofauti zisizo za kawaida kwa mfano wekundu kiasi
Kichefuchefu au kutapika
Maumivu ya tumbo, au pande za mwili karibu na tumbo mpaka sehemu za misuli
Joto laweza kuongezeka
JINSI YA KUEPUKANA NA U.T.I
Kunywa maji mengi
Acha kutumia dawa za uzazi wa mpango
Kula vizuri vyakula bora hasa asilia na sio vyakula vyenye kemikali
Kojoa hata kidogo baada ya kujamiiana
Punguza au acha kunywa pombe na kutumia sigara huchochea kuathiri kibofu
Kuwa msafi hasa sehemu za siri ili kutoruhusu bakteria
Usipulizie spray kwenye sehemu za siri
TIBA YA UGONJWA WA U.T.I
U.T.I hutibika kwa kuwaondoa bakteria na fangasi sehemu zilizoathirika kwa kutumia dawa, mtu mwenye U.T.I hupata shida sana na mpaka humpelekea kutokuwa na raha. Mtu mwenye U.T.I asipoitibu husababisha vimelea kuzaliana na kuwa vingi hii huitwa U.T.I sugu yuko hatarini kuwa na tatizo kubwa na pia hukaribisha magonjwa mengi.
DAWA
Tuna dawa ya kutibu U.T.I ambayo ni ya asili isiyo na kemikali ambayo hufanya mtu kupona na kuimarika kabisa. : Dawa hiyo hutibu kwa mda kulingana na mda wa tatizo, tatizo halirudi tena maana huondoa chanzo pamoja na ugonjwa sio kituliza maumivu, ukianza kutumia baada ya siku 5 huonesha mabadiliko, pia mgonjwa anapewa mfumo wa maisha ambao inatakiwa autumie kwasababu kuna mtindo wa maisha unaendelea kuongeza tatizo pia kuna mtindo unapunguza hatari ya ugonjwa.
Tunamshukuru Mungu kwa uumbaji wake na kutupa dawa ambazo alizileta ili kutuimarisha na kutuponya, Mungu hakuumba dawa nyingine zaidi ya mimea na vitu vingine vya asili, japo wengi hudharau. Mungu tunaomba utuokoe na kutuponya.
MAWASILIANO
0710264170
0755804170