04/03/2026
Ujumbe kwa Wanaume Kuhusu Wanawake na Ndoa
Kila mwanamke aliyeolewa ana mwanaume mmoja anayempenda zaidi kuliko mume wakr
Najua wengi wenu mtabisha, lakini huo ndio ukweli. K**a wanawake wangepewa nafasi ya kuolewa na mwanaaume zaidi ya mmoja, wengi wao wangeolewa na zaidi ya wanaume wanne.
Mara zote imeonekana kuwa, wanawake huwawazia wanaume wengine mambo makuu na kujenga matarajio yasiyo halisi—hufikiri "huwenda yule ni bora kuliko niliyenaye".
Mwanamke mmoja aliyeolewa aliwahi kuniambia kuwa hakuolewa na mumewe kwa sababu alikuwa "aina" (spec) ya mwanamume aliyemtaka. Aliolewa naye kwa sababu ni mwanaume anayejali, anayethamini familia, na ni tajiri. Lakini kwa muonekano, umbo la mwili, na mambo mengine ya binafsi, hakuwa chaguo lake la kwanza.
K**a mwanaume, ni muhimu kuwa na ufahamu kwamba huwezi kutimiza vigezo vyote anavyovihitaji mwanamke. Ikiwa vigezo vyake ni 10 na wewe unavyo 5 au 6, atakukubali.
Lakini hiyo haimzuii kuwatamani wanaume wengine ambao wana sifa zile ambazo wewe huna. Katika hatua hiyo, atatamani mwanaume huyo angekuwa mumewe, na usipoangalia, usaliti unaweza kutokea.
K**a utamaduni ungeruhusu wanawake, wengi wao wangeolewa na wanaume zaidi ya wanne. Wanawake wana asili ya kuwa na wapenzi wengi (polygamous) kuliko wanaume, na ndiyo maana wanasaliti sana, lakini jamii haiko tayari kwa mazungumzo haya.
Hata mwanamke adai kiasi gani anakupenda, kuna mwanamume mwingine ambaye bado anampenda na kutamani angekuwa mume au mpenzi wake😀
Na ikiwa mwanaume huyo anayempenda anatokea kuwa boss wake, mfanyakazi mwenzake, au mtu yeyote aliye karibu naye—hakuna kitakachomzuia kukusaliti na mwanaume huyo.
Hivyo basi, kadiri unavyoelewa mapema kuwa kuna mwanaume mwingine ambaye mwanamke wako anampenda, ndivyo itakavyokuwa bora kwako. Weka akilini kuwa huwezi KAMWE kutimiza vigezo vyote vya mwanamke, na vile vigezo ambavyo huna, kuna mwanamume mwingine huko nje anayevitimiza.
Mahubiri yangu kila mara huonekana k**a mzaha kwa baadhi ya wanaume, lakini ni kwa wale wanaohusika. Sitaki kusema mengi zaidi,
Sheria ni Sheria 🫵