ERY Herbal Clinic

ERY Herbal Clinic Huu ni ukurasa maalumu kwa ajili ya elimu ya tiba za magonjwa kupitia mimea | piga simu 0658505671

Ulipougua vidonda vya tumbo ulitumia tiba gani asili ukapona? Weka kwenye comment hapo na wengine wajifunze.Mdharau asil...
29/09/2025

Ulipougua vidonda vya tumbo ulitumia tiba gani asili ukapona? Weka kwenye comment hapo na wengine wajifunze.

Mdharau asili hufa kikatili

Kuwa tu mkweli —Lunch ya leo unakula nini?
29/09/2025

Kuwa tu mkweli —Lunch ya leo unakula nini?

Mapenzi ya kweli yapo vijijini tu—mjini ni full mipasho Vijijini mwanamke akichepuka kijiji kizima kinajuaAutomatically ...
29/09/2025

Mapenzi ya kweli yapo vijijini tu—mjini ni full mipasho

Vijijini mwanamke akichepuka kijiji kizima kinajua
Automatically mwanamke wa kijijini hata awe na hamu vipi hawezi chepuka kwa kuhofia aibu ya kijiji
Ikumbukwe baadhi ya vijiji mwanamke akichepuka anafukuzwa kwenye kijiji.

Wa mjini sasa😆

Yaan anaweza kuchepuka, na majirani zako wasikwambie
Anaingiza mpaka mwanaume ndani, majirani wakaona na wasikwambie ngoma inatembea kimyakimya.

Kijijini hawana roho ya kufumbia macho uovu.

Mitracarpus hirtus ni mmea mdogo wenye uwezo mkubwa wa kupambana na saratani—nimeuelezea vizuri kwenye kile kitabu cha k...
29/09/2025

Mitracarpus hirtus ni mmea mdogo wenye uwezo mkubwa wa kupambana na saratani—nimeuelezea vizuri kwenye kile kitabu cha kwanza. K**a ulikikosa nitafute mapema.

Huu mmea ni mzuri kwa kutibu maumivu ya jino, ng’oa pamoja na mizizi yake safisha
Pondaponda na ukamue maji yake
Tia sehemu ya jino linalouma/kutoboka

Mdharau asili hufa kikatili

Kujifukiza ni tendo la kuvuta mvuke wa mitishamba au dawa za asili kwa njia ya kuvuta puani au kuipokea kwenye ngozi. Ni...
29/09/2025

Kujifukiza ni tendo la kuvuta mvuke wa mitishamba au dawa za asili kwa njia ya kuvuta puani au kuipokea kwenye ngozi. Ni maarufu sana katika tiba za asili, hasa kwa wanawake baada ya kujifungua, lakini pia kwa watu wote k**a tiba ya kinga au tiba ya kuondoa uchafu mwilini.

Nini faida ya kujifukiza?

1. Husaidia kufungua njia za hewa.
—Inasaidia kwa mafua, kikohozi, baridi na pumu

2. Huondoa sumu na taka mwilini
—Kupitia jasho na ngozi, mwili hutolewa uchafu

3. Huboresha mzunguko wa damu
—Joto la mvuke husaidia damu kusambaa vizuri

4. Huimarisha afya ya kizazi (kwa wanawake)
—Husaidia kuondoa uchafu baada ya hedhi au kujifungua
—Huchangamsha misuli ya nyonga na uke

5. Kupunguza maumivu ya mwili au viungo
—Hasa maumivu ya mgongo, kiuno, na viungo baridi

6. Huondoa msongo wa mawazo na uchovu.
—Harufu ya mitishamba k**a mchaichai au mkaratusi hutuliza akili

🌿 Mitishamba mizuri kwa kutumia kujifukiza:
- Mchaichai
- Mlonge
- Majani ya mpera
- Mkaratusi (eucalyptus)
- Mdalasini
- Karafuu
- Kivumbasi

ZINGATIA:
- Usijifukize ukiwa na presha, mimba au magonjwa ya moyo bila ushauri
- Usikae karibu sana na mvuke mkali – unaweza kuchoma ngozi au macho
- Kwa watoto, fanya kwa uangalizi mkubwa

Mdharau asili hufa kikatili

KUTOKWA NA UTEUTE/ USAHA KWENYE UUME (Pe**le Discharge)Hali hii mara nyingi huwa ni sababu ya maambukizi yatokanayo  na ...
29/09/2025

KUTOKWA NA UTEUTE/ USAHA KWENYE UUME (Pe**le Discharge)

Hali hii mara nyingi huwa ni sababu ya maambukizi yatokanayo na Magonjwa ya kuambukizana kupitia kufanya ngono - Haya kwa kimombo yanaitwa STIs au Sexually Transmitted Infections.

Mambukizi hutokea pale maji maji ya mwili k**a vile mate, damu, manii, majimaji ya ukeni n.k – ya mtu ambae tayari ameambukizwa, yatatangamana na ya mtu ambae hajaambukizwa. Hii mara nyingi hufanyika wakati wa ngono ya kuingiliana kimwili au ya kunyonyana sehemu za siri.

Baadhi ya magonjwa hayo (lakini sio yote) yanatibika, lakini yasipotibiwa yanaweza kusababisha madhara ya kudumu. Kumbuka maambukizi ya ukimwi na virusi vya HIV pia mara nyingi hufanyika kupitia kufanya ngono.

Ishara na Dalili (Symptoms & Signs).

—Kutokwa na uteute kwenye uume inaweza kuwa ni Maji, usaha au damu.
—Maambukizi kwenye njia ya mkojo (UTI) au magonjwa ya zinaa (STIs) ni sababu kuu zinazochangia kutokwa na uteute/usaha kwenye uume.
—Kutokwa na uteute au usaha kwenye uume huambatana na maumivu au miwasho/kuunguza wakati wa kukojoa na huhitaji kukojoa mara kwa mara.
—Miwasho sehemu za siri inaweza kuambatana na kutokwa na usaha au uteute kwenye uume.
—Maambukizi ya Klamidia (Chlamydia), kisonono ( gonorrhea) na Trakoma (Trichomonas) ni moja ya vyanzo vikuu vinavyochangia kutokwa na usaha au uteute kwenyeuume.

Muone daktari (to see a doctor).
Muone daktari endapo utabaini haya;

✓Unatokwa na usaha au maji maji meupe, njano au mchanganyiko na damu.
✓Unapata miwasho au mkojo kuunguza wakati wa kukojoa.
✓Kupata vipele na malengelenge kwenye uume.
✓Uume kuwasha .
✓Miwasho sehemu za siri .

K**a umefanya mapenzi bila kutumia kinga na una wasi wasi huenda umeambukizwa, nenda ukafanyiwe uchunguzi na daktari.

Kumbuka, baadhi ya maambukizi huenda yasiwe na dalili, Hii haimaanishi kwamba huwezi kumwambukiza mpenzi wako, au kwamba hayawezi kukudhuru kiafya. K**a una wasi wasi, ni vyema kuchunguzwa na daktari haraka iwezekanavyo, ama kliniki.

Vihatarishi (Risk factors)
Ngono nzembe bila kinga wala tahadhari,
Kuwa na wapenzi wengi.
Kushiriki mapenzi na mtu zaidi ya mmoja.

Je unahitaji tiba? Piga simu au njoo whatsap https://wa.me/255658505671

Kaka kwenye game hakikisha ukimfunga gori analia —vinginevyo ujue ni offside😆Hii nayo inahitaji D2 wadau?
29/09/2025

Kaka kwenye game hakikisha ukimfunga gori analia —vinginevyo ujue ni offside😆

Hii nayo inahitaji D2 wadau?

Kila Ofisi Kuna yule mwana kila kukicha mnajadili namna ya kuacha kazi, Ila mtaondoka wote yeye yupo TU 😂🤣😂🤣
29/09/2025

Kila Ofisi Kuna yule mwana kila kukicha mnajadili namna ya kuacha kazi, Ila mtaondoka wote yeye yupo TU 😂🤣😂🤣

Uvivu wa kuhudhuria vikao ona sasa usiku kucha umeshinda porini unachoma mkaa ukikwepana na wamayama wakali, na game. —M...
29/09/2025

Uvivu wa kuhudhuria vikao ona sasa usiku kucha umeshinda porini unachoma mkaa ukikwepana na wamayama wakali, na game. —Muda huu umeuza mkaa na pesa yote imeliwa na haka ka bidada😆

Rudi tena porini ukateseke mpaka umasikini ukunyooshe s h e n z i kabisa

“Pombe na wanawake huwapotosha wanaume wenye akili; mwanamume afanyaye urafiki na malaya ni mpotovu kabisa. Huyo mwisho wake ni kuoza na kuliwa na wadudu; na maisha yake ya aibu yataondolewa. —Sira 19:-3”

“Achyranthes aspera” ni dawa nzuri ya jaundice (homa ya manjano) - Chuma majani ya kutosha - Chemsha katika maji kwa dk ...
29/09/2025

“Achyranthes aspera” ni dawa nzuri ya jaundice (homa ya manjano)

- Chuma majani ya kutosha
- Chemsha katika maji kwa dk 15
- Kunywa kikombe cha chai kutwa mara mbili

Mmea huu unatibu magonjwa mengi ikiwemo fistula—umeelezwa vizuri zaidi kwenye kitabu cha Rejesha afya yako bila gharama sehemu ya II

Mdharau asili hufa kikatili

Leo kikao cha wanaume  kimesoma hii misitari ya biblia—k**a haukuhudhuria nakukumbusha😁
29/09/2025

Leo kikao cha wanaume kimesoma hii misitari ya biblia—k**a haukuhudhuria nakukumbusha😁

*NAMNA NYINGINE YA KUTIBU HOMA YA INI (HEPATITIS)*Kuna njia nyingi za kutibu homa ya ini. Hii ni mojawapo, na inahitaji ...
28/09/2025

*NAMNA NYINGINE YA KUTIBU HOMA YA INI (HEPATITIS)*

Kuna njia nyingi za kutibu homa ya ini. Hii ni mojawapo, na inahitaji viambato vifuatavyo:-

- Papai la kijani (lisiloiva) pamoja na mbegu zake
- Jani la mpapai (la kijani)
- Mzalia nyuma
- Mchai chai (lemon grass)

*Matayarisho:*
✅Kata papai isiyooiva vipande vidogo kisha ongeza pamoja na mbegu zake. —K**a utapata iliyo na mbegu nyeupe ni bora zaidi.
✅Weka kwenye sufuria yenye maji safi
✅Ongeza majani ya mchai chai, mzalia nyuma na ya mpapai pamoja,
✅Chemsha kwa dakika 20, kisha acha ipoe.

- Kunywa mara mbili kwa siku kwa muda wa mwezi mmoja au zaidi.

Pia zingatia kila siku, kula tango (cucumber) baada ya chakula chako cha mchana na jioni.

Mdharau asili hufa kikatili

Address

Geita

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ERY Herbal Clinic posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram