TFNC Tanzania

TFNC Tanzania Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from TFNC Tanzania, Nutritionist, Next to Moshi AirPort, Ilala.

VACANCY ANNOUNCEMENT
11/09/2025

VACANCY ANNOUNCEMENT

Mafunzo kwa njia ya mtandao kuhusu Matibabu ya Ukondefu kwa Wagonjwa wa Nje kwa kuzingatia Mwongozo  Mpya wa Shirika la ...
10/09/2025

Mafunzo kwa njia ya mtandao kuhusu Matibabu ya Ukondefu kwa Wagonjwa wa Nje kwa kuzingatia Mwongozo Mpya wa Shirika la Afya Duniani (WHO 2023)

K**a wewe ni Daktari, Muuguzi, Afisa Lishe ama Mkuu wa Mradi wa Lishe unakaribishwa kujiunga katika mafunzo haya kwa kuskani QR kodi katika tangazo au kwa kupitia kiunganishi kifuatacho: https://www.tfnc.go.tz/announcements/kozi-4

TFNC YAENDELEA KUBORESHA MAABARA YAKE YA CHAKULA NA LISHE.Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) imeendelea kuwekez...
08/09/2025

TFNC YAENDELEA KUBORESHA MAABARA YAKE YA CHAKULA NA LISHE.

Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) imeendelea kuwekeza katika Maabara yake ya Chakula na Lishe iliyopo Mikocheni jijini Dar es Salaam, ikiwemo kuongeza vifaa vya kisasa zaidi vya kimaabara vitakavyoongeza ufanisi katika kuchakata na kuchambua sampuli mbalimbali inazopokea kutoka ndani na nje ya nchi.

Mkurungezi Mtendaji wa TFNC Dkt.Germana Leyna amesema Maabara hiyo imefanikiwa kuongeza mashine nyingine aina ya Real Time PCR Machine ambayo itatumika kupima vinasaba vinavyosababisha matatizo ya lishe.

Mkurugenzi Mtendaji pamoja na Menejimenti ya Taasisi leo Septemba 8,2025 wametembelea Maabara hiyo na kufanya kikao na watumishi wa Idara ya Sayansi ya Chakula na Lishe ikiwa ni sehemu ya kujadili kwa pamoja masuala mbalimbali yanayohusiana na utendaji wao.

Heri ya Sikukuu ya Mawlid
05/09/2025

Heri ya Sikukuu ya Mawlid

TUNAONJA. Baadhi ya washiriki wakionja sampuli za uji uliotengezwa kwa unga wa mchicha ikiwa ni sehemu ya utafiti unaoen...
03/09/2025

TUNAONJA.
Baadhi ya washiriki wakionja sampuli za uji uliotengezwa kwa unga wa mchicha ikiwa ni sehemu ya utafiti unaoendelea kufanywa na Taasisi ya Chakula la Lishe Tanzania (TFNC) wa kutengeneza chakula cha nyongeza kwa watoto wenye umri miezi sita na kuendelea ili kuboresha hali zao za afya na lishe.

WATUMISHI TFNC  WAPATIWA MAFUNZO YA USALAMA BARABARANIWatumushi wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania  (TFNC), wamepat...
27/08/2025

WATUMISHI TFNC WAPATIWA MAFUNZO YA USALAMA BARABARANI

Watumushi wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), wamepatiwa mafunzo ya Usalama Barabarani na wakufunzi wa Jeshi la Polisi kutoka Chuo cha Polisi Ufundi kilichopo jijini Dar es Salaam.

Mafunzo hayo yameoongozwa na Mkufunzi wa masuala ya usalama barabarani kutoka chuo hicho SP. Hamisi Membe, yamelenga kutoa elimu kwa madereva na watumiaji wa barabara ili kupunguza ajali zitokanazo na kujua au kutojua matumizi sahihi ya barabara.
tanzania @

SIMAMIENI MPANGO WA MMS KWA KUZINGATIA MAHITAJI YA WAJAWAZITONa WAF - DodomaMganga Mkuu wa Serikali Dkt. Grace Magembe a...
23/08/2025

SIMAMIENI MPANGO WA MMS KWA KUZINGATIA MAHITAJI YA WAJAWAZITO

Na WAF - Dodoma

Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Grace Magembe amemtaka Mkurugenzi wa Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto Dkt. Ahmad Makuwani pamoja na viongozi wengine wa Wizara ya Afya kwa kushirikiana na OR-TAMISEMI, kusimamia Mpango wa kuanzishwa matumizi ya virutubishi lishe kwa uadilifu, umahiri na kwa kuzingatia mahitaji ya wajawazito hapa nchini.

Dkt. Grace ametoa maelekezo hayo Agosti 20, 2025 kwenye kikao chenye lengo kuu la kuongeza kasi ya uboreshaji wa huduma za afya ya uzazi na lishe kwa akina mama wajawazito chini ambao utajumuisha kuanzishwa kwa matumizi ya virutubishi vya nyongeza kilichofanyika mkoani Dodoma.

Aidha, Dkt. Magembe amesema Tanzania imekuwa miongoni mwa nchi za kwanza Duniani kutambua njia bora ya kuimarisha huduma za lishe pamoja na kutoa virutubishi vya ‘Multiple Micronutrient Supplements’ (MMS), hivyo kuifanya nchi kuwa mano wa rejea kwa nchi nyingine katika eneo hilo.

“Katika utekelezaji wa lengo hilo, naelekeza pia kikao hiki kitumike katika kujengeana uelewa wa pamoja kuhusiana na umuhimu wa kuboresha huduma za lishe kwa wajawazito ikiwemo uandaaji wa chakula na mpangilio
sahihi wa mlo na sio tu utoaji wa virutubishi vya lishe,” amesema Dkt. Magembe.

Pia, ameelekeza kikao hicho kijadili kwa kina na kukubaliana juu ya mbinu na namna bora ya kuandaa na kutekeleza mpango huo wa Kitaifa ili uwe endelevu ikiwemo ushiriki wa sekta binafsi katika kuzalisha virutubishi hivyo, kupitia viwanda vya ndani na kuhakikisha taarifa za utekelezaji zinawasilishwa kila baada ya miezi miwili ili kufahamu hatua zilizofikiwa.

Tunaendelea kuwakumbusha zimebaki siku tatu tu kabla ya kuanza mafunzo ya Huduma bora za Afya na Lishe kwa mama mjamzito...
22/08/2025

Tunaendelea kuwakumbusha zimebaki siku tatu tu kabla ya kuanza mafunzo ya Huduma bora za Afya na Lishe kwa mama mjamzito, anayenyonyesha, mtoto mchanga na mdogo yanayotolewa kwa watoa huduma za afya kuanzia tarehe 25-28/08/2025 kwa njia ya mtandao.

Endelea kujisajili kwa kuskani QR code au kwa kubonyeza https://www.tfnc.go.tz/announcements/kozi-2

Endelea kujisajili zimebaki siku tano tu kabla ya kuanza mafunzo ya Huduma bora za Afya na Lishe kwa mama mjamzito, anay...
20/08/2025

Endelea kujisajili zimebaki siku tano tu kabla ya kuanza mafunzo ya Huduma bora za Afya na Lishe kwa mama mjamzito, anayenyonyesha, mtoto mchanga na mdogo yanayotolewa kwa watoa huduma za afya kuanzia tarehe 25-28/08/2025 kwa njia ya mtandao.

Jisajili kwa kuskani QR code au kwa kubonyeza https://www.tfnc.go.tz/announcements/kozi-2

Afisa Lishe Mtafiti, Fatma Juma (aliyevaa ushungi) kutoka TFNC akifanya mahojiano na watangazaji  wa Hope Channel (TV na...
19/08/2025

Afisa Lishe Mtafiti, Fatma Juma (aliyevaa ushungi) kutoka TFNC akifanya mahojiano na watangazaji wa Hope Channel (TV na redio) kuzungumzia uandaaji na ulaji sahihi wa matunda kwa afya bora katika kipindi cha Anza na Bwana kinachorushwa kila siku asubuhi

Tunaendelea kuhesabu zimebaki siku sita tu kabla ya kuanza mafunzo ya "Huduma bora za Afya na Lishe kwa mama mjamzito, a...
19/08/2025

Tunaendelea kuhesabu zimebaki siku sita tu kabla ya kuanza mafunzo ya "Huduma bora za Afya na Lishe kwa mama mjamzito, anayenyonyesha, mtoto mchanga na mdogo" itakayotolewa kwa watoa huduma za afya kuanzia tarehe 25-28/08/2025 kwa njia ya mtandao.

Jisajili sasa kwa kuskani QR code au kwa kubonyeza https://www.tfnc.go.tz/announcements/kozi-2

Je, wewe ni mtoa huduma za afya,  au Afisa miradi ya lishe kutoka taasisi za Serikali na zisizo za Serikali na unatamani...
18/08/2025

Je, wewe ni mtoa huduma za afya, au Afisa miradi ya lishe kutoka taasisi za Serikali na zisizo za Serikali na unatamani kuongeza ufanisi katika kutoa huduma bora za afya kwa mama mjamzito, anayenyonyesha, mtoto mchanga na mdogo?

Hii isikupite zimebaki siku saba tu kabla ya kuanza kwa kozi fupi kwa njia ya mtandao inayotolewa na *Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania* jisaliji sasa kwa kubonyeza https://www.tfnc.go.tz/announcements/kozi-2

Address

Next To Moshi AirPort
Ilala

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00

Telephone

0658990996

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TFNC Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category