TFNC Tanzania

TFNC Tanzania Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from TFNC Tanzania, Nutritionist, Ilala.

Afisa Lishe Mtafiti kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), Eliasaph Mwana akijibu maswali ya washiriki wa m...
07/01/2026

Afisa Lishe Mtafiti kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), Eliasaph Mwana akijibu maswali ya washiriki wa mafunzo ya namna ya kukusanya taarifa za utafiti wa kuhakiki ufanisi wa unga mchanganyiko wa mbegu za mchicha na nafaka nyingine katika kupunguza utapiamlo kwa watoto wenye umri kuanzia miezi sita hadi 59 kabla ya kuanza kufanyika kwa utafiti huo unaotarajiwa kufanyika katika Halmashauri mbili za mkoa wa Arusha (Arusha jiji na Arusha Vijijini).

Baadhi ya washiriki wa zoezi la kukusanya taarifa katika utafiti wa  kuhakiki ufanisi wa unga mchanganyiko wa mbegu za m...
06/01/2026

Baadhi ya washiriki wa zoezi la kukusanya taarifa katika utafiti wa kuhakiki ufanisi wa unga mchanganyiko wa mbegu za mchicha na nafaka nyingine katika kupunguza utapiamlo kwa watoto wenye umri kuanzia miezi sita hadi 59 wakitoa maoni yao wakati wa kupitia dodoso la kukusanya taarifa hizo, ikiwa ni siku ya pili ya mafunzo kwa wakusanya taarifa yanayofanyika jijini Arusha katika ukumbi wa Idara ya Afya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

Utafiti wa kuhakiki ufanisi wa unga mchanganyiko wa mbegu za mchicha na nafaka nyingine utafanyika kwa miezi sita katika Halmashauri mbili za mkoa wa Arusha (Arusha jiji na Arusha Vijijini).

Afisa  Mtafiti - Takwimu kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), Dillan Lyimo akiwapitisha Watoa Huduma za A...
06/01/2026

Afisa Mtafiti - Takwimu kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), Dillan Lyimo akiwapitisha Watoa Huduma za Afya ngazi ya Jamii wa jiji la Arusha na Halmashauri ya Wilaya ya Arusha katika dodoso la kukusanya taarifa za kufanya utafiti wa kuhakiki ufanisi wa unga mchanganyiko wa mbegu za mchicha na nafaka nyingine katika kupunguza utapiamlo kwa watoto wenye umri kuanzia miezi sita hadi 59 unaofanyika kwa miezi sita katika wilaya mbili za mkoa wa Arusha (Arusha jiji na Arusha Vijijini).

Baadhi ya washiriki wa zoezi la kukusanya taarifa katika utafiti wa  kuhakiki ufanisi wa unga mchanganyiko wa mbegu za m...
05/01/2026

Baadhi ya washiriki wa zoezi la kukusanya taarifa katika utafiti wa kuhakiki ufanisi wa unga mchanganyiko wa mbegu za mchicha na nafaka nyingine katika kupunguza utapiamlo kwa watoto wenye umri kuanzia miezi sita hadi 59 wakifanya mazoezi kwa vitendo ya kujaza dodoso litakalotumika kukusanyia taarifa za utafiti huo unaofanyika katika wilaya mbili za mkoa wa Arusha (Arusha jiji na Arusha Vijijini).

Afisa Mtafiti Mkuu kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), Dkt. Hoyce Mshida akitoa maelekezo namna ya kujaz...
05/01/2026

Afisa Mtafiti Mkuu kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), Dkt. Hoyce Mshida akitoa maelekezo namna ya kujaza dodoso la kukusanya taarifa za utafiti wa kuhakiki ufanisi wa unga mchanganyiko wa mbegu za mchicha na nafaka nyingine katika kupunguza tatizo la utapiamlo kwa watoto wenye umri kuanzia miezi sita hadi 59.

Utafiti huu unafanyika kwa muda wa miezi sita katika wilaya mbili za mkoa wa Arusha (Arusha Jiji na Arusha Vijijini).

Afisa  Mtafiti - Takwimu kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), Dillan Lyimo akitoa maelekezo kwa Watoa Hud...
05/01/2026

Afisa Mtafiti - Takwimu kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), Dillan Lyimo akitoa maelekezo kwa Watoa Huduma za Afya ngazi ya Jamii wa jiji la Arusha na Halmashauri ya Wilaya ya Arusha namna ya kujaza dodoso la kukusanya taarifa za kufanya zoezi la kuhakiki ufanisi wa unga mchanganyiko wa mbegu za mchicha na nafaka nyingine katika kupunguza utapiamlo kwa watoto wenye umri kuanzia miezi sita hadi 59 unaofanyika kwa miezi sita katika wilaya mbili za mkoa wa Arusha (Arusha jiji na Arusha Vijijini).

Mkurugenzi Idara ya Elimu na Mafunzo ya Lishe kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), Dkt. Esther Nkuba akio...
05/01/2026

Mkurugenzi Idara ya Elimu na Mafunzo ya Lishe kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), Dkt. Esther Nkuba akiongea na Watoa Huduma za Afya ngazi ya Jamii kutoka jiji la Arusha na Halmashauri ya Wilaya ya Arusha kuhusu mradi wa kupambana na utapiamlo wa kati kwa kutumia mbegu za mchicha na nafaka nyingine, kabla ya kuanza kwa zoezi la kuhakiki wa ufanisi wa unga mchanganyiko wa mbegu za mchicha na nafaka nyingine katika kupunguza utapiamlo nchini.

02/01/2026

Tukiendelea kusherehekea mwaka mpya 2025, leo katika dondoo za lishe tuungane na Maria Ngilisho, Afisa Lishe Mtafiti kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania akituelezea umuhimu wa kuwapatia watoto vitafunwa “snacks” vyenye afya kilishe

01/01/2026

Heri ya Mwaka Mpya, leo katika kusherehekea sikukuu ya mwaka mpya tuungane na Samila Jabiri, Afisa Lishe Mtafiti Mtafiti kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania akituelezea juu ya umuhimu kula mbogamboga

HERI YA MWAKAMPYA 2026
31/12/2025

HERI YA MWAKA
MPYA 2026

31/12/2025

Ikiwa tumebakisha masaa machache kukamilisha mwaka 2025 na kuukaribisha mwaka 2026, tuungane na *Glory Benjamini*, Mtafiti kutoka *Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania* akitueleza kuhusu *Madhara ya ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi*

RESEARCH ARTICLEEnhancing Hemoglobin Levels in Moderately Acute Malnourished Children Aged 6–59 Months: A Randomized Con...
31/12/2025

RESEARCH ARTICLE

Enhancing Hemoglobin Levels in Moderately Acute Malnourished Children Aged 6–59 Months: A Randomized Controlled Trial of a Novel Ready-to-Use Food (RUF)

Link on Bio.

Address

Ilala

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00

Telephone

0658990996

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TFNC Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category