TAEFI

TAEFI A youth lead a non-governmental organization dedicated to providing education and support on epilepsy.

Our vision is to become the number one youth platform in Tanzania that advocate, support, research and provide new therapies and education for epilepsy.

SHINE Project ni mradi uliotekelezwa na Comunità Solidali nel Mondo (COM-SOL TZ) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na P...
19/08/2025

SHINE Project ni mradi uliotekelezwa na Comunità Solidali nel Mondo (COM-SOL TZ) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na PORALG, ukiungwa mkono na Italian Agency for Development Cooperation (AICS) kuanzia mwaka 2023 hadi sasa.

Mradi huu umejikita katika:
✅ Kushughulikia changamoto za kifafa (epilepsy) na lishe duni (malnutrition), hasa kwa watu wenye ulemavu.
✅ Kuimarisha huduma katika kliniki maalum nne zinazotoa huduma za kifafa na lishe.
✅ Kutoa mafunzo kwa mfumo wa cascade katika mikoa 10 ya Tanzania kwa wahudumu wa afya na wadau wa jamii.
✅ Kuandaa mapendekezo ya sera na vitendo kwa ajili ya huduma jumuishi za afya.

Mnamo 18 Julai 2025, TAEFI ilishiriki katika Final Conference ya SHINE Project jijini Dar es Salaam. Ushiriki huu ni hatua muhimu kwani unawakilisha sauti za watu wanaoishi na kifafa na changamoto za ulemavu katika mjadala wa kitaifa kuhusu huduma jumuishi za afya.

Kupitia ushirikiano na wadau mbalimbali, tunajivunia kuona mapendekezo ya mwisho ya mradi huu yakizinduliwa rasmi, yakilenga kuimarisha huduma za kifafa na lishe nchini.

👉 TAEFI itaendelea kusimama pamoja na wapambanaji wa kifafa kuhakikisha hakuna anayeachwa nyuma.

💜


Happy International Youth Day! 🌍💜Leo tunasherehekea nguvu na mchango wa vijana duniani kote hasa wale wanaothubutu kuvun...
12/08/2025

Happy International Youth Day! 🌍💜
Leo tunasherehekea nguvu na mchango wa vijana duniani kote hasa wale wanaothubutu kuvunja vikwazo na kufuata ndoto zao licha ya changamoto. Kupitia miradi yetu wa SPEAK UP, STANDING STRONG , tunaendelea kuwajengea uwezo wanafunzi wenye changamoto ya kifafa, tukiwapa maarifa, ujasiri, na nafasi za kujitambua.

Kila kijana ana sauti na thamani. Wakati vijana wenye changamoto wakipata msaada na fursa, dunia inapata viongozi wapya wenye maono na moyo wa kubadilisha jamii. 💪✨

Kwa vijana wote, Tunaweza!




Miaka inaenda, upendo wa mama hauchuji! 🌷 ‘Mom Forum’ imetupa somo la jinsi ya kumuwezesha kila mama kuwainua watoto wen...
19/05/2025

Miaka inaenda, upendo wa mama hauchuji! 🌷 ‘Mom Forum’ imetupa somo la jinsi ya kumuwezesha kila mama kuwainua watoto wenye changamoto za ukuaji.

Furaha iliyoje kuwa shule ya sekondari Vijibweni jana! Kupitia clubs ya MRC Youth Books Club Tulifanya programu ya kuwah...
22/03/2025

Furaha iliyoje kuwa shule ya sekondari Vijibweni jana! Kupitia clubs ya MRC Youth Books Club Tulifanya programu ya kuwahamasisha watoto kupenda kusoma vitabu na kuwapa elimu muhimu kuhusu kifafa . Ni muhimu kwa jamii yetu kuelewa kifafa na kuondoa unyanyapaa. Tulipenda sana shauku yao ya kujifunza na tunafurahi kuwa tumeweza kuwapatia vitabu vya "Mimi na Rafiki Mwenye Kifafa" kwa shule, tukitumaini vitawasaidia wanafunzi na walimu. Tushirikiane kueneza uelewa kuhusu kifafa

💜

"Leo nimepata heshima ya kushiriki Siku ya Epilepsy (Epilepsy Day), iliyofanyika katika Ukumbi wa Ummy Mwalimu, Muhimbil...
10/02/2025

"Leo nimepata heshima ya kushiriki Siku ya Epilepsy (Epilepsy Day), iliyofanyika katika Ukumbi wa Ummy Mwalimu, Muhimbili, na kuandaliwa na Tanzania Epilepsy Association. Hafla hii muhimu ilihudhuriwa na wadau mbalimbali wa afya na jamii, ikiongozwa na Mgeni Rasmi, Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel.

Kwa kaulimbiu ya mwaka huu, "Unite for Better Care in Tanzania", tunasisitiza mshikamano katika kuhakikisha watu wanaoishi na kifafa wanapata huduma bora za afya, elimu sahihi, na kuondolewa kwa unyanyapaa. Pamoja, tunaweza kuleta mabadiliko chanya kwa jamii!




"Tarehe 25 Januari 2025, Tanzania Epilepsy Fighters (TAEFI) tulipata heshima ya kushiriki katika uzinduzi wa Kanzidata n...
10/02/2025

"Tarehe 25 Januari 2025, Tanzania Epilepsy Fighters (TAEFI) tulipata heshima ya kushiriki katika uzinduzi wa Kanzidata na Mfumo wa Taarifa za Watu Wenye Ulemavu, unaotokana na Sensa ya Watu na Makazi ya 2022. Hafla hii muhimu iliongozwa na Mgeni Rasmi, Mheshimiwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Tunapongeza Serikali Sikivu ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa hatua hii kubwa katika kuhakikisha watu wenye ulemavu wanajumuishwa ipasavyo katika mipango ya maendeleo ya taifa. Hii ni hatua muhimu kuelekea usawa, fursa, na ustawi kwa wote!


Mapema leo nilipata nafasi ya kushiriki katika programu ya SAUTI, ambapo kupitia ushairi mtaani tulitoa elimu kuhusu kif...
13/09/2024

Mapema leo nilipata nafasi ya kushiriki katika programu ya SAUTI, ambapo kupitia ushairi mtaani tulitoa elimu kuhusu kifafa kwa jamii na wafanyabiashara. Ni fursa ya kipekee kuona sanaa ikiunganisha watu na kuleta uelewa kuhusu afya ya akili na kifafa.


Tulijumuika na wafanyabiashara na kuwaelimisha kuhusu kifafa, tukifungua milango ya uelewa na ushirikiano katika kusaidi...
13/09/2024

Tulijumuika na wafanyabiashara na kuwaelimisha kuhusu kifafa, tukifungua milango ya uelewa na ushirikiano katika kusaidia jamii yetu. Kila hatua ni muhimu katika kuhakikisha watu wanaishi kwa uelewa na msaada sahihi.



tunakukaribisha kwenye tukio la kipekee SAUTI—  "ushairi mtaani" kwa ajili ya kuelimisha jamii kuhusu kifafa. Karibu tuu...
13/09/2024

tunakukaribisha kwenye tukio la kipekee SAUTI— "ushairi mtaani" kwa ajili ya kuelimisha jamii kuhusu kifafa. Karibu tuungane katika safari ya kupaza sauti ya kifafa itakayofanyika katika Ofisi ya Mtendaji, Mtaa wa Bora, Keko siku ya ijumaa Usiikose, "pamoja tunaleta mabadiliko!"



Join Us for *Mji Mwema Beach Cleanup*! Join us this Saturday, let's come together for a Pre-World Cleanup Day 2024! We'r...
12/09/2024

Join Us for *Mji Mwema Beach Cleanup*! Join us this Saturday, let's come together for a Pre-World Cleanup Day 2024! We're calling out all volunteers, ocean lovers, and environmental champions to participate in the Mji Mwema Beach Cleanup on September 14, 2024, from 6:00 AM to 10:00 AM.

🗓️ Date: Saturday, 14th September 2024
🕕 Time: 6:00 AM - 10:00 AM
📍 Location: Mji Mwema Beach, Kigamboni

Bring your energy and passion to protect our coastline, and let's leave the beach cleaner and safer for all. We can’t wait to see you there!
organisationtanzania .forminglife

08/05/2024
HELLO TAKA IS JUST AROUND THE CORNER Don't have a BIKE?Kindle register today through the link on  instagram  page  and  ...
22/04/2024

HELLO TAKA IS JUST AROUND THE CORNER

Don't have a BIKE?

Kindle register today through the link on instagram page and will organize one for you.

For non-cyclers you are all welcome straight to Coco Beach B (Opposite oyster bay hotel) from 07:00am

Karibu sana and see you all 👋♻️🏖️⛱️

♻️💚⛱️🌅



_
.organisationtanzania

Address

Kigamboni

Telephone

+255754839583

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TAEFI posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to TAEFI:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram