IJUE AFYA

IJUE AFYA Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from IJUE AFYA, Medical and health, Mbeya.

Jifunze na tambua masuala ya Uzazi pamoja na Afya ya mfumo Wa Uzazi: matatizo na magonjwa yanayoshambulia mfumo Wa Uzazi yaani via vya uzazi kwa wanawake, bila kusahau Afya ya mtoto, lishe bora na maendeleo ya ukuaji

"Obstetrics & Gynaecology"

31/05/2022

Elimu ya uzazi ni muhimu Sana kwa jinsia zote mbili, baadhi ya matatizo mengi ya mfumo wa uzazi kwa wanawake husababishwa na wanaume, ingawa badhi ya wanaume huwa mabali na wengine hukataa kabisa kujihusisha na suala la kujifunza Afya ya uzazi na kudhania kuwa ni jukumu la wanawake pekeyao, kitu ambacho siyo kweli Wala si haki na hii ni kutokana na kukosa Taarifa sahihi, ushauri ama elimu Bora ya uzazi. Tambua jukumu ni letu sote kwa Afya Bora ya uzazi

29/12/2021
Je wajua ni wakati gani Wa kumuona mtaalamu Wa Afya ya UZAZI ama kwenda kliniki unapohisi hali ya utofauti pale unapo ku...
27/06/2020

Je wajua ni wakati gani Wa kumuona mtaalamu Wa Afya ya UZAZI ama kwenda kliniki unapohisi hali ya utofauti pale unapo kuwa MJAMZITO?

Zipo dalili ama viashiliya vingi vya kukufanya uweze kumuona mtaalamu wa Afya ya Uzazi, ama kufika kliniki ikiwezekana hospitali kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi na kubaini tatizo na hatimaye kulitibu. Hapa nimeorodhezesha baadhi ya dalili (5) ingawa zipo nyingi lakini hizi nimezipa kipaumbele.

1.Mara unapojihisi kuwa mjamzito inakupasa wewe na mwenza wako kufika sehemu ya kutolea Huduma za Afya (clinics),hospitali ili kuweza kupewa ushauri, kufanyiwa vipomo na uchunguzi mbalimbali ili kubaini k**a kuna shida yeyote ya kiafya na kuweza kupatiwa matibabu na namna ya kutunza huo ujauzito n.k.

2.unapo hisi maumivu ya kichwa,macho kuuma ama kushindwa kuone vizuri, kuvimba kwa miguu, kujihisi kizunguzungu, inakupasa ufike clinic ama Hispitali ili uweze kutibiwa kwani hilo ni tatizo

3.unapopata maumivu makali ya tumbo hasa chini ya kitovu, kuharisha zaidi ya Mara tatu ndani ya muda mfupi, nyonga (kiuno) kuuma kupita kiasi, inakupasa umuone mtaalamu Wa Afya (uzazi) ili kuweza kufanyiwa uchunguzi.

4.kutokwa na damu ama maji sehemu za sili wakati Wa ujauzito pia ni dalili mbaya hivyo inakupasa umuone mtaalamu Wa Afya ama kliniki, fika hospitali iliyokaribu na wewe kwa uchunguzi zaidi

5. Unapohisi mabadiliko ya kucheza ama kutosikia mtoto akicheza fika kliniki iliyokaribu yako kwa uchunguzi zaidi.

19/09/2019
19/09/2019

Kwa kuanza nilazima Tujue nini maana ya AFYA na UGONJWA ama TATIZO manaake nini?

UNAPOSEMA AFYA:
ni hali ya kutokuwa na hitirafu yoyote ile katika mwili wako. Ama ni hali ya kutokuwepo kwa ugonjwa ama tatito lolote lile.

UGONJWA:
ni kitu chochote kile kinachoweza kuingilia utendaji kazi wa mwili,, yaani mwili ama kiungo kubadilisha mfumo wake wa utendaji kazi wa kawaida huo ndo ugonjwa ama tatizo,,

Zipo sababu nyingi zinasababisha magonjwa ama matatito Mbalimbali yatokee na kusababisha mwili kufanya kazi tofauti na ilivyo kawaida, nikusii mwana Ijue Afya, kuwa sambamba na ukurasa huu kwani utajifunza mengi juu ya Afya na utajua ni namna gani ya kuweza kuzuia,kukabiliana, kutatua ugonjwa ama tatizo juu ya Afya.

Tutakuwa na mijadala ama masomo mbalimbali juu ya Afya asante.

Address

Mbeya

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when IJUE AFYA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to IJUE AFYA:

Share