21/11/2025
Moja ya tabia inayoboa na chanzo cha magonjwa ya njia ya hewa ni mtoto kubebwa na kila mtu, mtoto kubusiwa busiwa na mtu pasipo kuzingatia hali yake ya afya mtu ana mafua lakini unakuta anapiga busu mtoto mwa mwa mwa, ana miwasho na upele lakini bado anang'ang'ana ambebe mtoto kidogo, kumrusharusha mtoto juu eti asiporushwa rushwa hachangamki awi mjanja mwisho unamrusha anapata mtikisiko wa ubongo (brain shake syndrome), kuweka vitu vya ajabu kwenye kitovu wapo uweka majivu, mate ya bibi nk. Baadhi ya mambo 7 ambayo humweka mtoto katika hatari;
▪️ Kumlazia mtoto tumbo wakati wa kulala.
Wengi hufikiri ni vizuri, lakini huongeza kukosa hewa(suffocation) .
▪️ Kutumia poda au mafuta kupita kiasi au vipodozi vikali
Kutumia talc marashi kunaweza kusababisha vipele, matatizo ya kupumua, au maambukizi. Tumia mafta yenye harufu kiasi siyo mchanganyiko mingi pia yawe mazuri na salama kwa Afya ya mtoto.
▪️ Kupuuza utunzaji wa kitovu
Kugusa kitovu kwa mikono michafu au kupaka vitu visivyo salama kunaweza kusababisha maambukizi.
▪️Kuchelewa kumpeleka mtoto kuanza chanjo
Baadhi ya wazazi huahirisha chanjo wakidhani mtoto yuko sawa.
Chanjo humlinda mtoto dhidi ya magonjwa iwe utotoni hadi utu uzima .
▪️ Kushirikiana chupa za kulisha au dawa
Hii inaweza sababisha ugonjwa kuenea kutoka mtoto mmoja kwenda mwingine pia kushea dawa kunaweza sababisha mtoto kutopona kwa kutopata dozi stahiki
Kila mtoto anahitaji vitu vyake vya kulisha na hakikisha vifaa hivyo vinafanyiwa usafi baada ya kuvitumia.
▪️ Kila mtu kumshika, kumbeba mtoto kuna weka kwenye hatari kubwa ya kuambukizwa baadhi ya magonjwa.
Wageni wenye kikohozi, mafua, au miwasho na upele siyo vizuri kuwagusa au kuwashika watoto kwakuwa wanaweza kuwaambukiza ugonjwa kwa njia ya mgusano (contact) kumbuka Watoto wachanga wana kinga dhaifu.
▪️Kutofuatilia halijoto ya mtoto
Homa kali au baridi sana inaweza kuwa hatari kwa maisha ya mtoto .
Mchunguze mtoto mara kwa mara na avae ipasavyo ili kumkinga dhidi ya baridi ambayo inaweza pelekea pneumonia nk .
Tabia ipi huwa inakukera ukiwa na mtoto mdogo...!?