AFYA YAKO NA LUCAS

AFYA YAKO NA LUCAS Karibu kwenye ukurasa wa Elimu ya Afya 🫶
Pata maarifa sahihi kuhusu magonjwa, lishe, uzazi na mtindo bora wa maisha.⛑️

Karibu kwenye ukurasa wa Elimu ya Afya 🫶
Pata maarifa sahihi kuhusu magonjwa, lishe, uzazi na mtindo bora wa maisha.🩺

Nacheka k**a mazuri lakini mimba iache iitwe mimba... 😂😂... Hebu fikiria mtu anatafuna mwingine anafura..... Kaona kitu ...
02/03/2026

Nacheka k**a mazuri lakini mimba iache iitwe mimba... 😂😂... Hebu fikiria mtu anatafuna mwingine anafura..... Kaona kitu kwenye TV machozi.. 😂

▪️Utasahau Kila Kitu
Utaingia jikoni na kusahau kwa nini ulienda huko.

▪️ Kulia Bila Sababu isiyo na mantiki
Tangazo kwenye TV? Machozi.
Mume akitafuna kwa sauti kubwa? Machozi.
Hujui hata kwa nini unalia.... 😂😂

▪️Uchovu Ambao Usingizi Hauwezi Kurekebisha
Unaamka umechoka.
Unalala umechoka.
Umechoka tu.

▪️ Kutopenda Chakula Ulichokuwa Ukikipenda
Hicho chakula unachokipenda hapo hata huku wahi kuwaza k**a utakipenda na kile ulichokuwa unakipenda ghafla kinanuka k**a moshi wa jenereta

▪️Kukojoa K**a Ni Hobby Yako Mpya
Umesimama tu kutoka chooni…
Unarudi tena.

Kati ya hayo marosoroso lipi umepitia (umewahi)... Ongeza na mengine pia.... ⁉️😂

MAOMBI MAALUM KWA AJILI YA MWEZI MARCH.(Kwa kila ombi,omba kwa imani kwa zaidi ya dakika 5/kadiri Roho Mtakatifu atakavy...
01/03/2026

MAOMBI MAALUM KWA AJILI YA MWEZI MARCH.
(Kwa kila ombi,omba kwa imani kwa zaidi ya dakika 5/kadiri Roho Mtakatifu atakavyokuongoza)

▪️Ee Bwana Yesu,Asante kwa zawadi ya mwezi mpya,Mwezi March.
▪️Ee Bwana Mungu, Nakusihi ufanye mwezi huu uwe mwezi wa Upenyo,Ushindi,Faida,Fidia na Ongezeko kwangu na familia yangu kwa jina la Yesu.
▪️Kwa jina la Yesu,kila mishale ya mauti ya ghafla,irudi ilikotoka!
▪️Chochote kibaya kilichoelekezwa kwangu ili kuniharibia mwezi wa Tatu hakitafanikiwa kwa jina la Yesu!
▪️Kila sauti za kinyume zinazoongea kinyume changu kwenye mwezi huu wa 3,naziamuru zinyamaze kwa jina la Yesu.
▪️Kila mipango ya misiba, maumivu na vilio kwenye familia na boma letu,haitafanikiwa kwa jina la Yesu.
▪️Kila mishale ya kukandamizwa, ajali za barabarani na hasara,IRUDI ilikotoka kwa jina la Yesu!
▪️Kila sauti za mizimu zinazoongea kinyume cha mafanikio yangu mwezi huu,zinyamaze kwa jina la Yesu.
▪️Mashambulizi ya majini mahaba hayatanipata mwezi huu kwa jina la Yesu.
▪️Kila shimo walilonichimbia ili nitumbukie mwezi wa 3, watatumbukia wao kwa jina la Yesu!
▪️Nyota yangu ya mafanikio na ushindi,Nakuamuru, NG'AA mwezi huu na kuniletea faida kwa jina la Yesu.
▪️Mikono yangu,sikia sauti ya MUNGU,FUNGUKA mwezi huu March na umiliki vitu vizuri kwa jina la Yesu.
▪️Miguu yangu,pokea nguvu ya kumiliki popote utakapokanyaga kwa jina la Yesu!
▪️Kichwa changu, pokea nguvu ya mawazo mapya yenye faida mwezi huu wa 3 kwa jina la Yesu!
▪️Yeyote anayepanga anguko langu, ataanguka Yeye kwa jina la Yesu.
▪️Yeyote anayepanga aibu yangu,ataaibika yeye kwa jina la Yesu.
▪️Nyumba yangu, sikia sauti hii; Amani, furaha, kicheko na afya tele ni fungu lako mwezi huu kwa jina la Yesu.
▪️Kila madhabahu zinazoongea kinyume na ustawi wangu mwezi huu,KUFA kwa jina la Yesu.
▪️Ee Roho Mtakatifu, nipe neema ya kuomba, kukutumikia,kuishi maisha ya utakatifu mwezi huu kwa jina la Yesu.
▪️Ee Roho Mtakatifu, niongezee hekima,busara na maarifa zaidi mwezi huu kwa jina la Yesu.

●ZABURI 23

Credit © Pastor Suzzane B. G Malisa

Kuanzia week 28  za ujauzito wanaweza kulia au kuonyesha nyuso zenye kufanana na kulia kutokana na mitetemo au miitikio ...
28/02/2026

Kuanzia week 28 za ujauzito wanaweza kulia au kuonyesha nyuso zenye kufanana na kulia kutokana na mitetemo au miitikio ya nje wakiwa tumboni japo hawatoi sauti kutokana na uchanga wa mapafu yao hali hii husaidia kupumua na mawasiliano.... Hapa chini ni baadhi ya mambo ambayo hufanywa na watoto wakiwa tumboni pasipo mama kujua.. 👇

▪️ Wanalia kimya kimya, ndio, watoto wachanga hufanya mazoezi ya kulia tumboni!

▪️Wanaonja chakula chako, chenye viungo, tamu, chungu… mtoto anajua yote 😂

▪️Wanakojoa… na kumeza tena (usipige kelele, ni kawaida!)

▪️Wanaota, wanasayansi wanasema watoto huanza kuota ndoto kabla ya kuzaliwa.

▪️Wanaitikia hisia zako, unapokuwa na huzuni, mtoto pia anaihisi.

▪️ Wanatambua sauti yako, wanamjua mama kabla hata hawajafika.

Lipi limekushangaza kati ya haya.... ⁉️

●Kumbukumbu la Torati 31:6,"Iweni hodari na moyo wa ushujaa, msiogope wala msiwahofu; kwa maana BWANA,Mungu wako ndiye a...
28/02/2026

●Kumbukumbu la Torati 31:6,"Iweni hodari na moyo wa ushujaa, msiogope wala msiwahofu; kwa maana BWANA,Mungu wako ndiye anayekwenda pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha."

Baba katika jina la Yesu, tunapoianza wiki hii, tutangulie kwa nguvu na mkono wako wa neema.
Bariki kazi zetu za mikono.
Bariki mifugo na mazao yetu.
Bariki watoto wetu na jamaa zetu.
Tubariki kwa afya njema.
Baba, nyumba zetu zisipungukiwe chakula, mavazi na malazi.
Baba tunaomba, wiki hii kusiwe na taarifa mbaya kwenye familia na boma zetu.

Baba,k**a kuna safari tutaenda na tusirudi salama wiki hii, tuepushe nayo kwa jina la Yesu.
K**a kuna safari ndugu zetu wataenda na wasirudi wakiwa hai, Baba fanya jambo wasisafiri.

Baba, kwa kila manuizo mabaya dhidi yetu na dhidi ya kazi za mikono yetu, TUNAYAFUTA KWA DAMU YA YESU.

Wiki hii itakuwa nzuri, wiki hii itakuwa na ushindi, wiki hii itakuwa ya faida na fidia.
Wiki hii tutatoka salama na kurudi salama kwa jina la Yesu. Mema yote yatatufuata wiki hii sawa na Zaburi 23.Amen 🙏!

Muwe na usiku mwema.... 🙏❤️
27/02/2026

Muwe na usiku mwema.... 🙏❤️

Afya bora huanza na usafi wa chakula, maji na mwili. Yafuatayo ni mambo muhimu ya kuzingatia:▪️ Kuosha mboga na matunda ...
27/02/2026

Afya bora huanza na usafi wa chakula, maji na mwili. Yafuatayo ni mambo muhimu ya kuzingatia:

▪️ Kuosha mboga na matunda kabla ya kupika/kula

Huondoa vumbi, mabaki ya dawa za kuulia wadudu, mayai ya minyoo na vijidudu vinavyoweza kusababisha kuharisha, homa ya matumbo na minyoo. Osha kwa maji safi yanayotiririka; ikiwezekana loweka kwa dakika chache kisha suuza tena.

▪️Kunawa kabla na baada ya kula

Mikono hubeba vijidudu kutoka kwenye vitu tunavyogusa. Kunawa kwa sabuni na maji tiririka hupunguza maambukizi ya kuhara, kipindupindu na magonjwa ya tumbo.

▪️Kunawa mikono baada ya kutoka chooni

Kinyesi hubeba vijidudu hatari. Bila kunawa, vijidudu huenea kwenye chakula, watoto na vitu vya nyumbani. Nawa kwa sabuni angalau sekunde 20.

▪️Matumizi salama ya choo

Tumia choo kilichofunikwa au chenye shimo salama, funika kinyesi, na hakikisha mazingira yanakuwa safi. Hupunguza kuenea kwa nzi na uchafu unaosababisha magonjwa.

▪️Kunywa maji yaliyotibiwa au kuchemshwa

Maji yasiyotibiwa yanaweza kuwa na bakteria na vimelea. Chemsha maji yafikie mchemko kamili au tumia njia sahihi za kutibu maji kabla ya kunywa.

▪️Hatari ya kula viporo visivyohifadhiwa vizuri

Chakula kilichokaa nje muda mrefu huruhusu bakteria kuzaliana. Hifadhi kwenye jokofu ndani ya saa 2 baada ya kupika, kisha pasha moto vizuri kabla ya kula.

Hitimisho:
Usafi wa mikono, chakula na maji ni kinga rahisi lakini yenye nguvu dhidi ya magonjwa mengi ya tumbo. Kinga ni bora kuliko tiba.

Vipi kiporo gani hata uambiwe wewe ni sikio la kufa utakula tuu..... ⁉️😂

................... ⁉️❔....😂😅
26/02/2026

................... ⁉️❔....😂😅

Nawatakia usiku mwema nyote....... 🙏❤️
25/02/2026

Nawatakia usiku mwema nyote....... 🙏❤️

Kutokwa damu ukeni wakati wa ujauzito baada ya wiki ya 28 na kabla ya kujifungua. Ni tatizo la dharura (obstetric emerge...
24/02/2026

Kutokwa damu ukeni wakati wa ujauzito baada ya wiki ya 28 na kabla ya kujifungua. Ni tatizo la dharura (obstetric emergency) linalohitaji tathmini na matibabu ya haraka.

Sababu kuu za Antepartum Hemorrhage

▪️Placenta previa
Kondo la nyuma linaachia na kuja chini na kufunika au kugusa mlango wa kizazi (cervix).
Damu hutoka ghafla, mara nyingi bila maumivu.

▪️Placental abruption (Abruptio placentae)

Kondo la nyuma linajitenga mapema na mfuko wa uzazi.
Huambatana na maumivu makali ya tumbo, uterasi kuwa ngumu, na damu inaweza kuwa nyingi au kidogo

▪️Uterine rupture (kupasuka kwa mfuko wa uzazi)

Mara chache, hutokea zaidi kwa waliowahi kufanyiwa upasuaji wa tumbo (C-section).

▪️Sababu nyingine
Maambukizi ya shingo ya kizazi, vidonda, au jeraha baada ya tendo la ndoa/uchunguzi.

Dalili

✅Kutokwa damu ukeni (nyekundu au nyeusi)
✅Maumivu ya tumbo au mgongo (hasa kwenye abruption) pia kutokuwa na maumivu (placenta previa)
✅Kizunguzungu, udhaifu, mapigo ya moyo kwenda kasi
✅Kupungua au kukosekana kwa harakati za mtoto(mtoto kucheza)

Hatari/Madhara
▫️Kwa mama:
▪️Upungufu wa damu (anemia)
▪️Mshtuko wa damu (shock)
▪️Kifo endapo damu ni nyingi na matibabu hayachelewi

▫️Kwa mtoto:
▪️Kuzaliwa kabla ya wakati
▪️Kukosa hewa ya kutosha (fetal distress)
▪️Kifo cha mtoto tumboni

Kuzuia au njia za kujikinga na antepartum hemorrhage

▪️Hudhuria kliniki ya wajawazito (ANC) mapema na mara kwa mara
▪️Epuka uvutaji sigara na matumizi ya pombe
▪️Ripoti mapema damu yoyote ukeni wakati wa ujauzito
▪️Fuata ushauri wa daktari k**a uliwahi kufanyiwa upasuaji wa tumbo

✅Hitimisho

Antepartum hemorrhage ni hali hatari lakini inayoweza kudhibitiwa ikiwa itagunduliwa mapema na kutibiwa kwa haraka. Damu yoyote ukeni baada ya wiki 28 ni dharura—mwone mtaalamu mara moja.

Vipi umewahi patwa na hali hii...⁉️

Baadhi yenu huwa wanauliza au  wanapiga kelele“Daktari nisaidie.... Nianzishie Uchungu !... Nimechoka!” Lakini mwili wak...
23/02/2026

Baadhi yenu huwa wanauliza au wanapiga kelele
“Daktari nisaidie.... Nianzishie Uchungu !... Nimechoka!”

Lakini mwili wako unasema…mambo bado...Tafadhari subiri... 🚶‍♀️

Hivi ndivyo mwili wako unavyoonyesha kuwa haujawa tayari kwa leba:

▪️ Chupa bado haijapasuka yaani kifupi hakuna k**asi k**asi au maji maji hayatoki (No flow of show)
▪️ Njia (cervical dilation) bado imebana yaani haijaanza kufunguka imebana k**a kizibo cha soda.
▪️Mtoto bado yuko juu yaani hajaanza kushuka kwenye nyonga na njia haijafunguka (No engagement)
▪️Hakuna mikazo halisi ya uchungu (no strong Uterine contraction) ni maumivu madogo madogo tu ambayo ukifanya mazoezi tu yanapoa.
▪️Una wiki 40 lakini hakuna dalili za maendeleo ya kuja kwa uchungu au tayari kwa kujifungua.

Mama, tarehe ya kujifungua siyo guarantee au uthibitisho kwamba utajifungua siku hiyo hiyo bali Ni makadirio.

Kulazimisha uchungu wa kujifungua wakati mwili wako hauko tayari kunaweza kusababisha:👇

✅Uchungu wa kujifungua kwa muda mrefu
✅Uchovu
✅Kujifungua kwa upasuaji wa Dharura wakati pengine ungejifungua kawaida.
✅Hupelekea mtoto kuchoka (fetal distress) hivyo unaweza jifungua kwa upasuaji wa dharura au mtoto wako akasidiwa kupumua baada ya kuzaliwa kutokana na uchungu kuchukua mda mrefu nk.

Wakati mwingine kusubiri kidogo (wakati unafuatiliwa) ni salama zaidi kuliko kuharakisha.

Kuwa mvumilivu. Fuatilia jinsi mtoto wako anavyocheza . Jitahidi hudhuria na Nenda kliniki kwa uchunguzi k**a ulivyoandikiwa kuhudhuria au k**a utaona mabadiliko yeyote wakati wa kusubiri nenda kituo cha karibu nawe.

Sema chochote unachopitia tukufaraiji mama.. 🙏❤️

Muwe na usiku mwema..... 🙏❤️
22/02/2026

Muwe na usiku mwema..... 🙏❤️

▪️Mimi huyo nilikuwa nasafiri niliandaa nauli tsh  45000/=, nilikuwa na jero lingine nika nunua bablish (big G au banzok...
21/02/2026

▪️Mimi huyo nilikuwa nasafiri niliandaa nauli tsh 45000/=, nilikuwa na jero lingine nika nunua bablish (big G au banzoka).. Nilikuwa na 500 nikanunua bablish za 200 nikarudishiwa chenji 300, .... Ili niwe natafuna funa bwana ile chenji 300 nikachanganya na ile tsh 45000/=... Nimefika zangu stendi nikakata tiketi kabisa.. Lipa sasa nauli.. Mfukoni kuna 100 tuu, 45200 kwisha habari yake.... 😢😢.

Dah ivi itakuwa ilienda wapi....!? Ushawahi kutana na tukio k**a hili baada ya kuchanganya chenji na hela nyingine... ⁉️

▪️2️⃣0️⃣1️⃣0️⃣.... Nilienda kwenye mnada mmoja ivi... Sasa nikapita maeneo ya wale jamaa wanaorushaga nguo, akataja bei k**a kawaida yao bei ya mwanzo sikusikia kwa kweli akasema mwisho 3000 lilikuwa shati akuna aliyenyosha mkono kulitaka alivo liweka chini nikasogea nikamwambia naomba nilione maana nilikuwa mbali nilivolishika tuu jamaa ananambia bora chukua tuuu usipochukua mie nachukua hela yako.... Nikajua utani sikuchukua shati na hela alichukua k**a alivyosema... 😢😢 Aisee

Mkasa gani umewahi kutana nao kwenye nguo za kurusha hata siyo mnadani... ⁉️

Address

Mbeya

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when AFYA YAKO NA LUCAS posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to AFYA YAKO NA LUCAS:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category