08/01/2026
Mabibi, sikilizeni kwa makini… moja ya sababu kuu za kuchanika au michaniko ya kizazi (Cervix) wakati wa kujifungua ni kusukuma kabla ya mwili wako kuwa tayari. Kuna baadhi ya wajawazito wakifika tuu leba baada ya kutoka chumba cha kusubiri uchungu au njia ifunguke wakifika leba wao ni kusukuma ilihali njia haijafunguka hadi mwisho mwisho wanaishia kuchanika vibaya (Tear) baada ya kusukuma na da mwingine njia kuvimba
Cervix yako inahitaji kupanuka au kufunguka kikamilifu (10cm) kabla ya kusukuma. Kuhisi maumivu haimaanishi ni wakati wa kusukuma!
Kusukuma mapema sana kunaweza:
▪️ Kusababisha mchaniko makali au mbaya
▪️ Kusababisha kutokwa na damu nyingi
▪️ Ushonaji wa mchaniko utahitaji utaalamu wa hali ya juu ndo maana wengine baada ya kujifungua kutokana na kuchanika vibaya basi ili ashonwe vizuri inatakiwa akashonwe chumba cha upasuaji (Operating Theater) , huko vijijini ndiyo kabisa unapewa rufaa ya kwenda hospital kubwa ukashonwe na wengine hujikuta wanapata fistula yaani mchaniko wake unahusisha uke hadi kwenye njia ya haja kubwa hivyo basi kinyesi na mkojo vinaanza jitokea kwakuwa misuli inayoratibu kutokwa kwa mkojo na kinyesi imechanika.
Baadhi ya wanawake wanahisi k**a mtoto "anajisukuma mwenyewe." Hayo ni maumivu tu yanayokudanganya. Vuta pumzi ndefu, vuta pumzi kupitia mdomo wako, na uache mwili wako ufuate mwongozo wa mkunga wako.
✅ Sukuma tu wakati mkunga wako anathibitisha: cervix imepanuka au imefunguka kikamilifu
✅ Inapokuwa tayari, kusukuma hakutaumiza cervix yako
Ushirikiano wako unakuokoa kuchanika (tear) hivyo fata muongo on kutoka kwa mkunga wako. USIJISUKUMISHE KABLA MKUNGA WAKO AKAKWAMBIA NA SUBIRI NJIA IFUNGUKE KIKAMILIFU NDIPO USKUME.
Tuambie neno gani unalikumbuka ambalo uliambiwa na mkunga wako wakati wa kusukuma.......!?