AFYA YAKO NA LUCAS

AFYA YAKO NA LUCAS Elimu na Ushauri kuhusu Afya 👏🙏😷⛑️ karibu kwa ushauri wa afya

Mabibi, sikilizeni kwa makini… moja ya sababu kuu za kuchanika  au michaniko ya  kizazi (Cervix) wakati wa kujifungua ni...
08/01/2026

Mabibi, sikilizeni kwa makini… moja ya sababu kuu za kuchanika au michaniko ya kizazi (Cervix) wakati wa kujifungua ni kusukuma kabla ya mwili wako kuwa tayari. Kuna baadhi ya wajawazito wakifika tuu leba baada ya kutoka chumba cha kusubiri uchungu au njia ifunguke wakifika leba wao ni kusukuma ilihali njia haijafunguka hadi mwisho mwisho wanaishia kuchanika vibaya (Tear) baada ya kusukuma na da mwingine njia kuvimba

Cervix yako inahitaji kupanuka au kufunguka kikamilifu (10cm) kabla ya kusukuma. Kuhisi maumivu haimaanishi ni wakati wa kusukuma!

Kusukuma mapema sana kunaweza:
▪️ Kusababisha mchaniko makali au mbaya
▪️ Kusababisha kutokwa na damu nyingi
▪️ Ushonaji wa mchaniko utahitaji utaalamu wa hali ya juu ndo maana wengine baada ya kujifungua kutokana na kuchanika vibaya basi ili ashonwe vizuri inatakiwa akashonwe chumba cha upasuaji (Operating Theater) , huko vijijini ndiyo kabisa unapewa rufaa ya kwenda hospital kubwa ukashonwe na wengine hujikuta wanapata fistula yaani mchaniko wake unahusisha uke hadi kwenye njia ya haja kubwa hivyo basi kinyesi na mkojo vinaanza jitokea kwakuwa misuli inayoratibu kutokwa kwa mkojo na kinyesi imechanika.

Baadhi ya wanawake wanahisi k**a mtoto "anajisukuma mwenyewe." Hayo ni maumivu tu yanayokudanganya. Vuta pumzi ndefu, vuta pumzi kupitia mdomo wako, na uache mwili wako ufuate mwongozo wa mkunga wako.

✅ Sukuma tu wakati mkunga wako anathibitisha: cervix imepanuka au imefunguka kikamilifu
✅ Inapokuwa tayari, kusukuma hakutaumiza cervix yako

Ushirikiano wako unakuokoa kuchanika (tear) hivyo fata muongo on kutoka kwa mkunga wako. USIJISUKUMISHE KABLA MKUNGA WAKO AKAKWAMBIA NA SUBIRI NJIA IFUNGUKE KIKAMILIFU NDIPO USKUME.

Tuambie neno gani unalikumbuka ambalo uliambiwa na mkunga wako wakati wa kusukuma.......!?

Wakati wa hudhurio lako la kwanza la kliniki ya ujauzito, tarehe ya kwanza ya hedhi ya Mwisho ndiyo  hutumika ✅Kukadiria...
07/01/2026

Wakati wa hudhurio lako la kwanza la kliniki ya ujauzito, tarehe ya kwanza ya hedhi ya Mwisho ndiyo hutumika
✅Kukadiria umri wa ujauzito
✅Daktari au muuguzi hutumia LMP kujua mama ana ujauzito wa wiki ngapi.
✅Kupanga huduma muhimu za kliniki
K**a:
▫️Kipimo cha damu, mkojo
▫️Chanjo (TT)
▫️Ultrasound ya wakati sahihi
▫️Kufuatilia ukuaji wa mtoto
▫️Kutambua hatari mapema

✅Kujua umri sahihi wa ujauzito husaidia kutambua:
▫️Kujifungua kabla ya wakati (preterm)ikiwa mama atajifungua kabla ya week 37 (miezi 9)
▫️Ujauzito uliopitiliza (post-term) ikiwa mama atajifungua au ujauzito wake utakuwa na umri wa zaidi ya week 42

Baadhi ya sababu zinazo weza pelekea mama kujifungua kabla ya tarehe ya makadilio ni k**a zifuatazo:

▪️Makadirio si tarehe halisi
EDD ni makisio tu—ni takribani asilimia 5 pekee ya wajawazito hujifungua siku hiyo hiyo.
▪️Mzunguko wa hedhi si wa siku 28 kwa wote
Wanawake wenye mzunguko mfupi au mrefu huweza kupata makisio yasiyo sahihi.
▪️Kutokumbuka vizuri LMP
Mama akitoa tarehe isiyo sahihi, makadirio pia yatakuwa si sahihi.
▪️Sababu za kitabibu k**a vile Maambukizi, Presha ya juu wakati wa ujauzito, mama kuwa na Kisukari cha ujauzito, mimba kuwa ya watoto wengi (mapacha n.k.)

Baadhi ya sababu za wajawazito wengine kujifungua baada ya tarehe ya makadirio ni k**a zifuatazo :

✅Ovulation ilitokea kuchelewa
Hii husababisha mtoto kuwa bado hajakomaa vya kutosha kufika mapema.
✅Makosa kwenye LMP au ultrasound iliyofanywa kwa makosa
Ultrasound ikifanyika baada ya wiki 20, usahihi wake hupungua.
✅Urithi (genetics)
Familia zingine huwa na tabia ya ujauzito kufika wiki 41–42.

Muhimu kukumbuka
▫️Tarehe ya makadirio ni mwongozo, si ahadi
Kujifungua kati ya wiki 37–42 bado huchukuliwa kuwa kawaida
▫️Ultrasound ya mapema (wiki 8–12) ndiyo sahihi zaidi kukadiria umri wa ujauzito

Je wewe ulijifungua kabla au baada au tarehe ile ile ya makadilio......!?

“K**a mpenzi wako ni mjamzito na ana maambukizi ya gono (gonorrhea), usijaribu kabisa kununua au kumpa dawa bila ushauri...
06/01/2026

“K**a mpenzi wako ni mjamzito na ana maambukizi ya gono (gonorrhea), usijaribu kabisa kununua au kumpa dawa bila ushauri wa mtaalamu wa afya.
Kwa mjamzito, si dawa zote za gono zinaruhusiwa, baadhi zinaweza kumdhuru mtoto aliyeko tumboni. Njia salama pekee ni kwenda hospitali au kituo cha afya haraka.”

Kwa nini hospitali ni muhimu?

Daktari atathibitisha aina ya maambukizi (si kila uchafu ni gono).
Atampa dawa salama kwa mjamzito kulingana na umri wa mimba.
Atapewa dozi sahihi, si kubahatisha.

Maambukizi yasipotibiwa yanaweza kusababisha:

✅Kujifungua kabla ya wakati
✅Mtoto kuzaliwa na maambukizi ya macho au upofu kabisa
✅Mtoto kuzaliwa na Uzito mdogo
✅Maambukizi kuenea kwa mama hadi kwenye maji yanayomzunguka mtoto (chorioamnionitis) pia PID (Pelvic inflammatory disease) kwa mama mwenyewe.

Ushauri muhimu kwa mwanaume (wewe):

▪️Ninyi wote mpimwe na mtibiwe kwa pamoja hata k**a una dalili au huna.
▪️Msifanye tendo la ndoa hadi matibabu yakamilike.
▪️Usinunue dawa kiholela hizi zinaweza kuwa hatari kwa mjamzito.
“Kwenda hospitali mapema ni kumuokoa mama na mtoto. Usione aibu wala kuchelewa, hii ni hatua ya ujasiri na upendo wa kweli.”

Kwa ufupi mie wengi huwaga nawaambia nenda hospital kituo cha karibu nawe yote kutaka Daktari akuone kwa ukaribu na upate matibabu sahihi...

Sema ushauri ambao ulikusadia kutoka katika ukrasa huu...!?

Walinikata… Nilipiga kelele… Kisha Nikasikia Kilio cha Mtoto Wangu. Hakuna aliyenionya kwamba hili  linaweza kutokea wak...
05/01/2026

Walinikata… Nilipiga kelele… Kisha Nikasikia Kilio cha Mtoto Wangu.
Hakuna aliyenionya kwamba hili linaweza kutokea wakati wa kujifungua.

Hili ni jeraha ambalo wanawake wengi hugundua tu baada ya kujifungua [ Episiotomy] so kwamba mama huwa haambiwi wakati wa kujifungua kwa tuna kuongezea njia ili kichwa kiweze kutoka bali hali ya maumivu ya wakati wa kupush hata mama wakati wa kukata mama anaweza asisikie maumivu yeyote na hata kusikia hiyo sauti ya mkunga, daktari au nurse yeye huitikia tuu sawa lakini hata kuwa za kuhusu hilo hakuna.

Wakati wa uchungu wa kujifungua, wakati kichwa cha mtoto wako tayari kimetoka lakini kutoka kunakuwa kugumu sana… na mtoto kuendelea kukaa pale anaweza kumeza yale maji na uchafu mwingine hivyo kuepusha yote hayo basi ndipo njia inayotumika ni kukata msuli , mda mwingine mtoto akikaa pale anaweza kuchoka na mapigo ya moyo yanaanza kushuka hapa ndipo mkunga wako hufanya jeraha dogo, lililodhibitiwa ili kumsaidia mtoto wako atoke haraka na akiwa hai.

✅ Jeraha hili SI adhabu.
✅Halifanyiki kwa ajili ya kujifurahisha.
✅ Linafanywa ili kuokoa maisha, yako au ya mtoto wako.

Jeraha safi la kimatibabu hupona vizuri na haraka kuliko kuchanika ambako hakuja dhibitiwa ambako kunaweza kuhusisha kuchanika ovyo kunakoweza pelekea kupasuka uke hadi sehemu ya haja kubwa na maeneo mengine kuzunguka uke hata kwenda ndani ya kizazi, hali ya kuchanika amabako hakuja dhibitiwa kitalaam wanaita Perineal Tear.

Baada ya mtoto kuzaliwa, eneo hilo hushonwa vizuri
Kwa utunzaji sahihi, maumivu hupungua, uponaji huwa wa haraka sana huja.

Je umewahi ongezwa njia na ulisikia nini ulipoambiwa unaoengezwa njia...!?

Dalili za hatari hazipigi simu wala kukunong'oneza kwamba ndo naenda kutokea au kuleta shida hivyo mama mara unajiona kw...
04/01/2026

Dalili za hatari hazipigi simu wala kukunong'oneza kwamba ndo naenda kutokea au kuleta shida hivyo mama mara unajiona kwamba hiki siyo cha kawaida basi chukua hatua stahiki ili kuweza kuokoa maisha yako na mja wako, zawadi ya mja kutoka kwa mungu.. Hizi ni baadhi ya dalili 👇

▪️ Kupungua kwa ghafla kwa harakati za mtoto
Ikiwa mtoto ni mtulivu kuliko kawaida, nenda hospitalini mara moja.

▪️Kutokwa na damu katika hatua yoyote ya ujauzito
Ndogo au nzito—sio kawaida. Daima angalia.

▪️ Maumivu makali ya kichwa ambayo hayataisha
Hasa kwa kuona vibaya au kizunguzungu.

▪️Uvimbe wa uso, mikono, au macho
Uvimbe wa ghafla unaweza kuashiria shinikizo la damu.

▪️ Maumivu makali ya tumbo

▪️ Homa kali au baridi
Maambukizi yanaweza kukuathiri wewe na mtoto.

▪️Kutapika mara kwa mara
Sio kawaida inapozidi.

▪️ Kutokwa na maji ghafla au kutokwa na maji mara kwa mara
Huenda chupa maji imepasuka mapema.

▪️Maumivu makali ya mgongo pamoja na maumivu ya tumbo
Inaweza kuwa uchungu wa kujifungua kabla ya wakati, usingoje.

▪️Unahisi kuna kitu kibaya rohoni mwako
Usipuuze hisia za mama, mda mwingine wajawazito hujikatia taama kutokana na safari ya miezi 9 ilivyo ndefu, mabadiliko mbalimbali, marosoroso kibao hivyo kujisikia kukata tamaa hutokea.

Mama, kwenda hospitalini mapema kunaweza kuokoa maisha ya watu wawili.

Dalili gani umewahi au ilikutokea basi ukakimbia hospital haraka....!?

Hilo si kweli kabisa — ni imani za watu tu (hadithi za jadi) na halina ukweli wowote wa kitabibu.Kitovu (umbilical cord)...
03/01/2026

Hilo si kweli kabisa — ni imani za watu tu (hadithi za jadi) na halina ukweli wowote wa kitabibu.

Kitovu (umbilical cord) hakihusiani kabisa na:
✅uanaume wa mtoto wa kiume
✅ukubwa au uwezo wa uume
✅uwezo wa kuzaa baadaye
Kitovu huunganishwa tumboni, si kwenye sehemu za siri.

Hata k**a wakati wa kuzaliwa au baada ya kuzaliwa kitovu kitapita au kugusa sehemu za siri, hakisababishi madhara yoyote.

Uanaume huamuliwa na:
▪️Vinasaba (chromosomes) – hasa Y chromosome
▪️ Kichochezi au Homoni ya kiume inayoitwa testosterone

Tatizo la kitovu hutokea tu k**a:
kimefungwa vibaya na kusababisha maambukizi,
kuna kutokwa damu au kutokea kwa hernia ya kitovu Lakini si uanaume.

Hitimisho
✅ Kauli hiyo ni hadithi za watu
✅ Haina msingi wowote wa kisayansi au kitabibu
✅ Wazazi wasiwe na hofu isiyo na sababu

Je wewe uliwahi kusikia story gani kuhusu kitovu cha mtoto kwa ujumla...!?

Kulia  au kilio ndiyo lugha pekee ambayo mtoto anaweza kuwasilisha au kuwasiliana na mama kwamba kuna mambo hayapo sawa ...
02/01/2026

Kulia au kilio ndiyo lugha pekee ambayo mtoto anaweza kuwasilisha au kuwasiliana na mama kwamba kuna mambo hayapo sawa inaweza kuwa ugonjwa au kuachwa mpweke. Baadhi ya sababu za mtoto kulia nimekuandalia hapa 👇

▪️ Njaa (Tena!)
Tumbo la mtoto mchanga ni dogo ambalo linafanana na ukubwa wa apple 🍎, kunyonyesha kunaweza kufanywa kila saa yaani anaweza kunyonya na kanyonya teena, lakini unapita mda kidogo anaanza kulia kutokana na njaa.

▪️Anaweza kuwa k**a anasinzia lakini Hawezi Kulala
Watoto waliochoka kupita kiasi hulia zaidi na bado akachukua mda kulala baada ya kulia sana.

▪️Maumivu tumbo kutokana na kujaa Gesi
Kutokana na uchanga mtoto hawezi kunyonya vizuri hivyo wakati wa kunyonya hewa ikawa inapita nyingi na baada kusababisha mtoto kulia sana na mda mwingine, mama kutomcheulisha mtoto baada ya kunyonya hivyo baada mtoto hulia sana kutokana na maumivu ya tumbo yaliyossbabishwa na hewa iliyojaa tumboni.

▪️Baridi au joto Sana
Watoto hawawezi kudhibiti halijoto vizuri hivyo mhimu kuvalishwa nguo zinazo saidia mtoto asipatwe na baridi pia mda mwingine joto linaweza sababisha mtoto kulia, kwaiyo mama jitahidi kumvalisha mtoto kulingana na hali ya hewa.

▪️Nepi chafu
Hata mkojo mdogo unaweza kumkera na kusababisha mtoto kulia na usipomtoa kwa wakati anaweza pata maambukizi ya UTI, fangasi na kuungua ngozi.

▪️Anahitaji Faraja, Sio Chakula tuu
Wakati mwingine mtoto anataka tu kubebwa, hata mazingira ya makelele yanaweza pelekea mtoto kulia hivyo watoto wachanga hupendelea mazingira ya utulivu.

▪️ Kulia sana kunako ambatana na kupumua kwa shida, sauti k**a kimluzi flani ivi, kushindwa kunyonya , mtoto kuishiwa nguvu au kunyong'onyea, joto la mwili kupanda sana nk tafadhari nenda hospitalini.

Tuambie mbinu unazo tumia kumnyamazisha mtoto anapolia...!?

... ❤️🙏🙏
01/01/2026

... ❤️🙏🙏

Watoto, hasa wa chini ya miaka 5, hupenda kuchunguza kwa kuweka vitu mdomoni, puani au masikioni. Vitu hatarishi ni pamo...
31/12/2025

Watoto, hasa wa chini ya miaka 5, hupenda kuchunguza kwa kuweka vitu mdomoni, puani au masikioni. Vitu hatarishi ni pamoja na Punje ndogo (maharage, kunde, karanga, nafaka) mda mwingine
Sarafu, vifungo (buttons), vishanga nk.

Vitu hivi vinaweza sababisha..
▪️Kuziba njia ya hewa → kukosa pumzi
▪️Maambukizi puani au masikioni
▪️Kutoboka kwa viungo kwa vitu vyenye ncha kali k**a msumali vikimwezwa au kuingizwa puani, sikioni na mdomoni.
▪️Mtoto kupoteza fahamu au kifo (kwa hali mbaya)

Ushauri 👇
✅Usimwache mtoto acheze peke yake na vitu vidogo
✅Hifadhi sarafu, betri, dawa, shanga mahali pa juu na salama
✅Nunua toys zilizoandikwa “suitable for age”
✅Kata chakula cha mtoto vipande vidogo
✅Mfundishe mtoto (kadri anavyokua) kutoweka vitu puani/masikioni

Angalizo kitu kikiingia puani/koo/masikioni:
▪️ Usijaribu kukitoa kwa fimbo, pamba au kidole
▪️ Usimwogopeshe mtoto
✅ Nenda hospitali mara moja
Wataalamu hutumia vifaa salama kuondoa bila kuumiza.

Una mapendezo gani yaboreshwe au yafanywe kwa Mwaka 2️⃣0️⃣2️⃣6️⃣...!?

Hadithi ni nyingi za mtaani zinafurahisha sana, mhimu kuhudhuria kliniki na kufata ushauri wa wataalamu wenu wa afya kwa...
30/12/2025

Hadithi ni nyingi za mtaani zinafurahisha sana, mhimu kuhudhuria kliniki na kufata ushauri wa wataalamu wenu wa afya kwa sababu ndiyo wenye majibu yenu yote ya mkanganyiko kuhusu afya ya mama na maendeleo ya ukuaji wa mtoto aliyezaliwa au aliye tumboni kwa mama, baadhi ya hadithi hizo ni k**a hizi;

▪️TUMBO DOGO LINAMANISHA MTOTO MDOGO

Ukubwa wa tumbo hutegemea aina ya mwili, si ukubwa wa mtoto.
Ni ultrasound pekee inayoweza kukadiria uzito wa mtoto.

▪️KIUNGULIA HAKIMAANISHI MTOTO ANA NYWELE NYINGI

Kiungulia kinatokana NA mabadiliko ya vichochezi vya uzazi si mtindo wa nywele wa mtoto

▪️SI LAZIMA ULE SANA

Kula kupita kiasi husababisha usumbufu jitahidi kula milo midogo dogo siyo tu ile milo mitatu mikubwa .

▪️KUTEMBEA Sana HAKUSABABISHI KUANZA KWA UCHUNGU

Kutembea kupita kiasi kutakuchosha tu . Uchungu au leba huanza wakati mwili na mtoto kwa pamoja viko tayari au huanza kwa wakati wake siyo lazima kulazimishwa.

▪️KUJIFUNGUA KWA UPASUAJI (C-SECTION) HAIMAANISHI WEWE NI DHAIFU AU ULIFELI

C-section ni utaratibu wa kuokoa maisha ya Mama na mtoto ili watoke hai.

▪️MTOTO KUPIGA MATEKE SANA HAIMAANISHI MTOTO ANA HASIRA

Hii humaanisha mtoto yuko hai na ana maendeleo mazuri ya ukuaji .
Shukuru, usiogope.

▪️IKIWA HAKUNA MAUMIVU HAIMAANISHI KWAMBA UCHUNGU UKO MBALI

Baadhi ya wanawake njia hufunguka au hutanuka kimya kimya huku maumivu nayo yakiwa kidogo lakini njia ikiendelea kufunguka.
Kila mwili una mwitikio tofauti.

▪️KUFANYA MAPENZI (S£X) ITAMUUMIZA MTOTO

Ikiwa hupati maumivu yeyote na hali au hamu ya kushiriki tendo ipo, kwa ujumla ngono ni salama kipindi cha mimba .

▪️KUVUMILIA MAUMIVU HAIMAANISHI UTAJIFUNGUA SALAMA

Maarifa, usaidizi, na huduma kwa wakati ndiyo muhimu zaidi kuliko mateso.Vizuri kuwahi kituo cha afya mapema ili kupata huduma chini ya wataalamu wa afya.

Vipi hadithi gani uliambiwa au umewahi sikia mtaani kuhusu mimba...!?

Njia ya kalenda  au rhythm method  k**a njia ya uzazi wa mpango huwa na uwezekano mkubwa wa kumsaliti mtu, na hizi ndizo...
29/12/2025

Njia ya kalenda au rhythm method k**a njia ya uzazi wa mpango huwa na uwezekano mkubwa wa kumsaliti mtu, na hizi ndizo sababu kuu:

▪️Mzunguko wa hedhi si wa kudumu 100%
Hata mwanamke mwenye mzunguko unaoonekana “sawa” anaweza:
Kuchelewa au kuharakisha ovulation (kupevuka kwa yai)
Kuathiriwa na msongo wa mawazo, ugonjwa, safari, au mabadiliko ya homoni
Ovulation ikitokea mapema au kuchelewa → siku ulizodhani ni salama zinakuwa hatarishi.

▪️Ovulation haiwezi kutabirika kwa kalenda peke yake
Yai hutoka siku 14 kabla ya hedhi inayofuata, lakini:
Hii hubadilika kila mwezi
Kalenda huhesabu kwa makadirio, sio uhakika wa kibaiolojia.

▪️Mbegu za kiume huishi muda mrefu
Mbegu zinaweza kuishi siku 3–5 ndani ya mwili wa mwanamke
Ukifanya tendo kabla ya ovulation, mbegu zinasubiri yai → mimba hutokea hata k**a siku ilionekana salama.

▪️Majimaji ya mwanaume kabla ya kumaliza au kumwaga mbegu (pre-ejaculate)
Majimaji haya yanaweza kuwa na mbegu
Hii huongeza hatari hata bila kumwaga kamili.

▪️Ufanisi wake ni mdogo
Kwa matumizi ya kawaida:
Takriban wanawake 12–24 kati ya 100 hupata mimba ndani ya mwaka
Ikilinganishwa na:
Kondomu
Vidonge
Sindano, kipandikizi, IUD
→ Kalenda ni dhaifu zaidi.

▪️Inahitaji nidhamu na ufuatiliaji wa hali ya juu
Unahitaji:
Rekodi sahihi ya miezi 6–12
Kuepuka kabisa tendo siku hatarishi
Kosa dogo tu → mimba hutokea.

✅Hitimisho Kalenda humsaliti mtu kwa sababu mwili wa mwanamke si mashine; ovulation hubadilika, mbegu huishi muda mrefu, na makadirio ya kalenda hayatoshi kuzuia mimba kwa uhakika.

💡 Ushauri k**a mtu hataki mimba kwa uhakika → achanganye kalenda na kondomu
Au achague njia yenye ufanisi zaidi (kipandikizi, IUD n.k.)

Vipi imewahi kukusaliti au njia gani nyingine imewahi kukusaliti..?

Dalili zinazoonyesha mtoto yuko salama, anaendelea vizuri na “ana furaha” (anapata mahitaji ya msingi) akiwa tumboni mwa...
28/12/2025

Dalili zinazoonyesha mtoto yuko salama, anaendelea vizuri na “ana furaha” (anapata mahitaji ya msingi) akiwa tumboni mwa mama ni hizi zifuatazo:

Dalili kutoka kwa mama👇

▪️Mtoto kucheza/kusogea mara kwa mara
Kuanzia wiki 18–25 mama huhisi mipigo, kusukuma au kugeuka.
Mtoto anapocheza mara kwa mara ni ishara nzuri ya afya.

▪️Kuongezeka kwa tumbo kulingana na umri wa ujauzito
Tumbo hukua polepole lakini kwa mfululizo kulingana na wiki za mimba.

▪️Hakuna maumivu makali au dalili hatarishi
Kukosekana kwa damu nyingi, maumivu makali ya tumbo au homa.

Dalili kutoka vipimo vya kitabibu

✅Mapigo ya moyo ya mtoto (Fetal Heart Rate) ya kawaida
Kati ya 110–160 kwa dakika.
Husikika vizuri kwa Doppler au ultrasound.

✅Ultrasound inaonyesha ukuaji mzuri
Uzito, urefu na viungo vinaendana na umri wa ujauzito.
Mtoto anasogea vizuri ndani ya mfuko wa uzazi.

✅Kiwango cha maji ya uzazi (Amniotic fluid) ni cha kawaida
Maji ya kutosha humsaidia mtoto kusogea na kukua vizuri.

✅Placenta (kondo la nyuma) linafanya kazi vizuri
Hupitisha hewa ya oksijeni na virutubisho kwa mtoto.

Dalili za tahadhari (si kawaida)👇
Muone mtaalamu wa afya haraka ikiwa:

▪️Mtoto hachezi au anacheza kidogo sana
▪️Kuna kutokwa damu nyingi au kutokwa na damu kwa ujumla
▪️Maumivu makali ya tumbo au kichwa
▪️Mama anahisi mabadiliko yasiyo ya kawaida k**a vile kuvimba kwa miguu, uso au mwili mzima, kupumua kwa shida, kutapika kupita kiasi, mwili kuishiwa pawa, kuona maruweruwe,

Hitimisho kwa ujumla, mtoto anayecheza mara kwa mara, mwenye mapigo ya moyo ya kawaida na anayekua sawasawa kwenye ultrasound huashiria afya njema tumboni.

Nini kilikupa wasiwasi au kilikufanya ukamwona daktari chap chap kipindi cha mimba...!?

Address

Mbeya

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when AFYA YAKO NA LUCAS posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to AFYA YAKO NA LUCAS:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category