AFYA YAKO NA LUCAS

AFYA YAKO NA LUCAS Elimu na Ushauri kuhusu Afya 👏🙏😷⛑️ karibu kwa ushauri wa afya

Moja ya tabia inayoboa na chanzo cha magonjwa ya njia ya hewa ni mtoto kubebwa na kila mtu, mtoto kubusiwa busiwa na mtu...
21/11/2025

Moja ya tabia inayoboa na chanzo cha magonjwa ya njia ya hewa ni mtoto kubebwa na kila mtu, mtoto kubusiwa busiwa na mtu pasipo kuzingatia hali yake ya afya mtu ana mafua lakini unakuta anapiga busu mtoto mwa mwa mwa, ana miwasho na upele lakini bado anang'ang'ana ambebe mtoto kidogo, kumrusharusha mtoto juu eti asiporushwa rushwa hachangamki awi mjanja mwisho unamrusha anapata mtikisiko wa ubongo (brain shake syndrome), kuweka vitu vya ajabu kwenye kitovu wapo uweka majivu, mate ya bibi nk. Baadhi ya mambo 7 ambayo humweka mtoto katika hatari;

▪️ Kumlazia mtoto tumbo wakati wa kulala.
Wengi hufikiri ni vizuri, lakini huongeza kukosa hewa(suffocation) .

▪️ Kutumia poda au mafuta kupita kiasi au vipodozi vikali
Kutumia talc marashi kunaweza kusababisha vipele, matatizo ya kupumua, au maambukizi. Tumia mafta yenye harufu kiasi siyo mchanganyiko mingi pia yawe mazuri na salama kwa Afya ya mtoto.

▪️ Kupuuza utunzaji wa kitovu
Kugusa kitovu kwa mikono michafu au kupaka vitu visivyo salama kunaweza kusababisha maambukizi.

▪️Kuchelewa kumpeleka mtoto kuanza chanjo
Baadhi ya wazazi huahirisha chanjo wakidhani mtoto yuko sawa.
Chanjo humlinda mtoto dhidi ya magonjwa iwe utotoni hadi utu uzima .

▪️ Kushirikiana chupa za kulisha au dawa
Hii inaweza sababisha ugonjwa kuenea kutoka mtoto mmoja kwenda mwingine pia kushea dawa kunaweza sababisha mtoto kutopona kwa kutopata dozi stahiki
Kila mtoto anahitaji vitu vyake vya kulisha na hakikisha vifaa hivyo vinafanyiwa usafi baada ya kuvitumia.

▪️ Kila mtu kumshika, kumbeba mtoto kuna weka kwenye hatari kubwa ya kuambukizwa baadhi ya magonjwa.
Wageni wenye kikohozi, mafua, au miwasho na upele siyo vizuri kuwagusa au kuwashika watoto kwakuwa wanaweza kuwaambukiza ugonjwa kwa njia ya mgusano (contact) kumbuka Watoto wachanga wana kinga dhaifu.

▪️Kutofuatilia halijoto ya mtoto
Homa kali au baridi sana inaweza kuwa hatari kwa maisha ya mtoto .

Mchunguze mtoto mara kwa mara na avae ipasavyo ili kumkinga dhidi ya baridi ambayo inaweza pelekea pneumonia nk .

Tabia ipi huwa inakukera ukiwa na mtoto mdogo...!?

Insomnia ni hali ambapo mjamzito anapata ugumu wa kupata usingizi, au kuamka mara kwa mara usiku, au kuamka mapema na ku...
20/11/2025

Insomnia ni hali ambapo mjamzito anapata ugumu wa kupata usingizi, au kuamka mara kwa mara usiku, au kuamka mapema na kushindwa kurudi kulala. Ni jambo la kawaida sana kwa wajawazito, hasa kuanzia trimester ya pili na ya tatu.

Sababu Kuu za Insomnia Kwa Wajawazito

✅Mabadiliko ya homoni

Homoni za ujauzito (k**a progesterone) zinaweza kusababisha:

Usingizi wa mchana

Kukosa usingizi usiku

✅Maumivu na usumbufu wa mwili

Maumivu ya mgongo

Kukosa mkao mzuri

✅Haja ndogo ya mara kwa mara

Shinikizo la mji wa mimba kwenye kibofu husababisha mjamzito kuamka mara nyingi kukojoa.

✅Kichefuchefu na kiungulia

Husumbua usingizi hasa trimester ya pili na ya tatu.

✅Msongo wa mawazo (stress)

Wasiwasi kuhusu:

Afya ya mtoto

Uchungu na kujifungua

Majukumu ya uzazi

✅ Ndoto nyingi au zenye nguvu

Mabadiliko ya homoni hufanya ndoto kuwa nyingi na wazi sana (vivid dreams).

▪️Dalili za Insomnia kwa Mjamzito ni pamoja na Kukosa usingizi usiku, Kuamka mara nyingi, Kukesha bila sababu, Uchovu mwingi mchana, Kukosa nguvu na Kuumwa kichwa au kukosa umakini

▪️Baadhi ya madhara ambayo mjamzito anaweza kupata Ikiwa haitadhibitiwa ni pamoja Uchovu mkali, Mood swing (kukasirika haraka), Kupungua kinga ya mwili, Kupata blood pressure kwa baadhi ya wanawake na Kuongezeka kwa hatari ya kupata msongo wa mawazo baada ya kujifungua

Namna ya Kudhibiti Insomnia Wakati wa Ujauzito

✅ Badilisha mazingira ya usingizi

Chumba kiwe kimya, salama na baridi kiasi

Lala upande wa kushoto ili kuboresha mzunguko wa damu

✅ Fanya mazoezi mepesi

Kutembea dakika 20–30 mchana

Mazoezi ya kupumua (deep breathing)

Yoga nyepesi kwa wajawazito

✅Epuka vyakula na tabia zinazosababisha kukosa usingizi

Usinywe chai, kahawa au soda zenye caffeine jioni

Epuka kula vyakula vizito usiku

Epuka kulala muda mfupi sana mchana (nap > 30 min)

✅ Tumia mbinu za kutuliza mwili

Kupumua kwa utulivu (inhale 4 sec, exhale 6 sec)

Kusikiliza muziki wa utulivu

Kuoga maji ya uvuguvugu kabla ya kulala

✅Punguza ratiba ya simu na TV

Usitumie simu saa 1 kabla ya kulala

Mwanga wa simu hupunguza usingizi (blue light)

✅Kula mlo mdogo kabla ya kulala

Kwa mfano:

Ndizi

Uji mwepesi

Tunda k**a apple
Husaidia kuzuia kiungulia.

✅Kuongea na daktari

Mwambie daktari ikiwa Insomnia inazidi na Inakuathiri kufanya shughuli za kila siku

Una maumivu, msongo, au kupumua kwa shida

Kumbuka Dawa za usingizi haziwezi kutumika bila ushauri wa daktari wakati wa ujauzito.

Vipi ulipata changamoto hii mimba ikiwa na miezi mingapi...?

Utasikia kwani nina cha kufanya sasa .... 😂😂😂😂... Nimetulia tuu nachat nawe ma mtuu .... 😂😂😂
19/11/2025

Utasikia kwani nina cha kufanya sasa .... 😂😂😂😂... Nimetulia tuu nachat nawe ma mtuu .... 😂😂😂

Kwa ujumla, mtoto anavyozidi kukua, mwili wa mjamzito hupitia mabadiliko yanayofanya kazi za kuinama sana, kubeba vitu v...
19/11/2025

Kwa ujumla, mtoto anavyozidi kukua, mwili wa mjamzito hupitia mabadiliko yanayofanya kazi za kuinama sana, kubeba vitu vizito, au kusafisha kwa kupiga magoti muda mrefu kuwa hatarishi.
Hata hivyo, hakuna mwezi maalumu unaosema “kuanzia hapa ni marufuku,” bali kuna kipindi ambacho tunashauri kupunguza sana au kuepuka:

▪️Kuanzia miezi ya katikati ya ujauzito (mwezi wa 4–5)

Tumbo linaanza kushuka mbele na uzito kuongezeka.

Mgongo unapata mzigo mkubwa, hivyo kuinama huongeza maumivu na shinikizo.

▪️Kuanzia mwezi wa 6–9 ni muhimu zaidi kuepuka

Hii ndiyo hatua ambapo:

Kiwango cha maji ya uzazi (amniotic fluid) kimeongezeka.
Mjamzito huweka presha kwenye mgongo na nyonga haraka anapoinama.

Kwa kifupi: miezi 6 kwenda juu mjamzito hapaswi kufanya kazi za kuinama mara kwa mara.

Madhara ya kufanya kazi za kuinama sana wakati wa ujauzito

▪️Hatari ya kichefuchefu, kizunguzungu na kupoteza fahamu

Shinikizo la damu hushuka ghafla unapoelekea chini au kuinuka haraka.

▪️Maumivu makali ya mgongo na kiuno

Uzito wa mtoto unavuta tumbo mbele, hivyo kuinama huongeza maumivu ya mgongo (low back pain).

▪️Kuongeza shinikizo kwenye tumbo na kizazi

Hii inaweza kusababisha:

Miscarriage (hasa miezi ya mwanzo, ikiwa ni kupiga magoti/kuinama kwa muda mrefu au kubeba vitu vizito).

Kuzaliwa kabla ya muda (preterm labor) miezi ya mwisho.

Kondo la nyuma kujitenga (placental abruption) ikiwa unainama huku ukibeba vitu vizito.

▪️Kupunguza oksijeni kwenda kwa mtoto

Kuinama sana, hasa kwa muda mrefu, husababisha mzunguko wa damu kubana, na mtoto kupata upungufu wa oksijeni kwa muda (temporary reduced uterine blood flow).

▪️maumivu ya nyonga na msuli wa nyonga (pelvic floor strain)

Hii huongeza hatari ya kuvuja mkojo au uchungu wa mapema.

Jaribu kufanya hivi ili kuepuka...
✅Omba msaada kubeba vitu vizito.

✅Gawa kazi ndogo ndogo zisizohitaji kukaa kwa muda mrefu kwa kumegemea tumbo.

✅K**a unahisi maumivu ya mgongo, tumbo kukaza au uchovu → pumzika mara moja.

Kutumia pampas (diapers/pampers) badala ya pedi za hedhi si jambo la kawaida, lakini linaweza kufanyika kwa dharura. Hat...
18/11/2025

Kutumia pampas (diapers/pampers) badala ya pedi za hedhi si jambo la kawaida, lakini linaweza kufanyika kwa dharura.

Hatari na madhara ya kutumia pampas wakati wa hedhi

▪️ Uchafuzi na maambukizi (UTI, yeast infection, bacterial vaginosis)
Pampas zimeundwa kwa mkojo, si damu ya hedhi ambayo ina wingi wa bakteria. Kutokana na joto pia unyevu vinaongeza uwezekano wa maambukizi.

▪️ Harufu mbaya
Pampas zikiwekwa muda mrefu zinaweza kutoa harufu kali kwa sababu hazitengenezwi kwa ajili ya damu ya hedhi.

▪️ Kuwashwa na upele (diaper rash)
Ngozi inaweza kupata vipele kutokana na kukaa na unyevu muda mrefu.

▪️Kutopumua kwa ngozi
Pedi nyingi za kisasa zimetengenezwa kupitisha hewa, lakini pampas zimefungika zaidi na zinaweza kusababisha joto na kukosa hewa sehemu ya uke.

▪️Kujisikia vibaya / kutojisikia huru
Pampas ni nzito na zinaonekana, hivyo zinaweza kufanya mtu ajisikie asiye na comfort au aibu.

Kutokana na sababu tajwa hapo juu Pampas Si salama wala haipendekezwi kuzitumia k**a mbadala wa pedi kwa muda mrefu, hivyo basi
▪️Tumia kitambaa safi kilichochemshwa na kukaushwa vizuri (kibadilishwe mara kwa mara)

▪️Nunua pedi za bei nafuu (kuna aina nyingi za bei ya chini)

▪️Hakikisha usafi: oga, badilisha mara kwa mara, tumia vaa nguo za ndani safi.

Vipi umewahi kutumia au huwa unatumia..!?

Wakati wa ujauzito,kizazi ( uterus) hupitia mabadiliko ya ajabu. Katika hali yake ya kawaida, ni kiungo kidogo, chenye u...
17/11/2025

Wakati wa ujauzito,kizazi ( uterus) hupitia mabadiliko ya ajabu. Katika hali yake ya kawaida, ni kiungo kidogo, chenye umbo la peazi kinachokaa chini kwenye nyonga (Pelvis) . Lakini mtoto anapokua,kizazi (uterus) hupanuka sana na huinuka juu na kuunda nafasi ya kulinda na kulisha kijusi kinachokua. Mfano huu unaonyesha jinsi mabadiliko hayo yalivyo ya ajabu, ukionyesha tofauti kati ya kizazi kabla ya ujauzito na kizazi kilivokua na kizazi kilivojaa mtoto wakati wa ujauzito.

Superfetation ni hali ya kipekee sana ambapo mwanamke anatunga mimba mpya wakati tayari ana ujauzito mwingine unaoendele...
17/11/2025

Superfetation ni hali ya kipekee sana ambapo mwanamke anatunga mimba mpya wakati tayari ana ujauzito mwingine unaoendelea. Kwa kawaida, mara tu mwanamke anapopata ujauzito, mwili huzuia kutokea kwa mimba nyingine — lakini katika superfetation, kinga hizi za mwili hazifanyi kazi k**a kawaida.Lakini hutokea ambapo Yai jingine kupevuka (ovulation) wakati tayari kuna mimba.

Hii ni ngumu sana kutokea kwa sababu:

▪️Homoni za ujauzito huzuia yai lingine kupevuka.

▪️Njia ya uzazi (cervix) hufunga na kuzalisha ute mzito unaozuia mbegu kuingia.

▪️Endometriamu (ukuta wa uterasi) tayari imeebadilika kupokea mimba ya kwanza.

Matokeo ya superfetation

Watoto hutofautiana umri wa ujauzito (gestational age) lakini huzaliwa karibu wakati mmoja.

Wanaweza kuonekana k**a mapacha, lakini si mapacha wanaofanana (identical twins) ambao mara nyingi hutokana na mgawanyiko wa yai moja ambalo lilirutubishwa na mbegu moja. Lakini kwa aina ya mapacha wanaotokana na superfetation hutofautiana kiumri kwa siku chache hadi wiki kadhaa.

Baadhi ya sababu za kutokea kwa superfetation ni kwa wanawake wanaotumia Tiba za uzazi k**a kupandikiza mimba (IVF) pia wale wanaotumia dawa za kusisimua vichochezi vya uzazi yaani hormonal treatments.
Mara chache sana kwa njia ya kawaida bila matibabu.

Baadhi ya Hatari zinazoweza Kujitokeza ni pamoja nan;

▪️Tofauti ya ukuaji katika mimba, kwani mmoja ni mdogo kuliko mwingine.

▪️Hatari ya kujifungua kabla ya wakati.

▪️Changamoto za kiafya kwa mtoto mdogo zaidi.

Mimba za namna hii ni nadra sana duniani. Kesi zinazothibitishwa ni chache sana katika historia ya tiba.

K**a una uhakika piga tangawizi yako iliyochanganyikana na karafuu na utumie asali mbadala wa sukari kisha kunywa maji h...
16/11/2025

K**a una uhakika piga tangawizi yako iliyochanganyikana na karafuu na utumie asali mbadala wa sukari kisha kunywa maji hakikisha umeoga na umejisafisha vizuri kisha hakikisha unayelala naye una hisia naye au udhaifu wako mnapendana sana.

Halafu au basi lala tu kesho nayo ni siku😀
Credit

Mimba iliyojificha au mimba isiyojulikana mapme  hutokea ambapo mwanamke ni mjamzito, lakini hajitambui au hata vipimo v...
15/11/2025

Mimba iliyojificha au mimba isiyojulikana mapme hutokea ambapo mwanamke ni mjamzito, lakini hajitambui au hata vipimo vya kawaida vya ujauzito havionyeshi kuwa ana mimba — hadi miezi kadhaa ipite, au hata hadi anapojifungua.

Hii ni hali nadra sana, lakini hutokea.

Sababu za Cryptic Pregnancy

▪️Mabadiliko madogo ya homoni

Baadhi ya wanawake hupata mabadiliko madogo ya homoni za ujauzito (k**a hCG), hivyo vipimo vya ujauzito vinaweza kuonyesha negative.

▪️Hedhi isiyo ya kawaida

Wengine hupata damu kidogo kila mwezi hata wakiwa wajawazito, wakifikiri ni hedhi ya kawaida.

▪️Matatizo ya homoni (PCOS, stress, nk.)

Magonjwa k**a Polycystic O***y Syndrome (PCOS) au msongo wa mawazo unaweza kufanya mwili usionyeshe dalili za kawaida za mimba.

▪️Matumizi ya vidonge vya uzazi wa mpango

Vidonge au sindano za uzazi wa mpango zinaweza kuficha dalili za mimba (k**a kukosa hedhi au kuongezeka uzito).

▪️Mimba ya mara ya kwanza au hali ya kisaikolojia

Wengine hawana uzoefu wa awali, hivyo hawatambui dalili, au wanakana uwezekano wa kuwa wajawazito.

Dalili za Cryptic Pregnancy

Dalili zake zinaweza kufanana na hali nyingine za kiafya, ndiyo maana hazitambuliki mapema:

▪️Kichefuchefu cha mara kwa mara

▪️Uchovu wa ajabu

▪️Tumbo kuongezeka taratibu bila mpangilio

▪️Kutopata hedhi kwa miezi kadhaa au kupata damu kidogo

▪️Maumivu ya mgongo au kiuno

▪️Hisia za mtoto kuzunguka tumboni (baada ya muda mrefu)

Matokeo au Hatari

▪️Mwanamke anaweza kutojiandaa kisaikolojia au kimwili kwa ujauzito.

▪️Kukosa huduma muhimu k**a clinic visits, vitamins (folic acid), au ufuatiliaji wa afya ya mtoto.

▪️Hatari ya kujifungua ghafla bila maandalizi.

Ikiwa una mashaka una dalili za ujauzito lakini vipimo vinaonyesha negative:

✅Fanya kipimo cha damu (serum hCG test) hospitalini.

✅Fanya ultrasound kubaini k**a kuna ujauzito.

✅ Wasiliana na daktari wa uzazi (gynecologist) kwa uchunguzi wa kina.

Wajawazito wengi hutema mate kila mara wanapokuwa matembezi, wamekaa wengine hufikia hata ya kutembea na mfuko au kutema...
14/11/2025

Wajawazito wengi hutema mate kila mara wanapokuwa matembezi, wamekaa wengine hufikia hata ya kutembea na mfuko au kutema mate kwenye chombo kidogo pia Wengine hata hubeba tishu au nailoni kila mahali,
Moja ya sababu kuu ya kutokea kwa hili wakati wa ujauzito ni kutokana ongezeko la homoni /vichochezi vya uzazi hasa estrojeni na progesterone.
Mabadiliko haya yanaweza kuathiri tezi zako za mate na kuongeza uzalishaji wa mate.
Pia, kichefuchefu cha asubuhi huwafanya baadhi ya wanawake kuepuka kumeza mara kwa mara, kwa hivyo mate hujikusanya tu!

Ni kawaida sana katika miezi 3-4 ya kwanza na kwa kawaida hupungua baadaye katika ujauzito.

Usiwe na aibu mama hauko peke yako! Wanawake wengi hupatwa na hali hiyo hata k**a hawatakubali.

Jinsi ya kukabiliana na hali hiyo ;
▪️ Weka tishu ndogo au maji ya chupa karibu.
▪️ Tafuna gum au bigijii au ili kupunguza hamu ya kutema mate.
▪️Kunywa maji kidogo mara kwa mara.
▪️ Epuka vyakula vyenye viungo vingi au asidi ambavyo huzidisha hali hiyo.

Kwa kawaida hupotea mara tu mwili wako unapozoea au baada ya kujifungua!

Kwa hivyo, ikiwa unatema mate kila wakati, usihisi aibu, ni homoni zako zinazofanya kazi yao.

Ujauzito huja na mambo mengi ya kustaajabisha, lakini kila dalili ina sababu.

Wanaume wengi hupitia mabadiliko ya kihisia na hata kimwili wakati wake zao wakiwa wajawazito, hali hii huitwa kwa kitaa...
13/11/2025

Wanaume wengi hupitia mabadiliko ya kihisia na hata kimwili wakati wake zao wakiwa wajawazito, hali hii huitwa kwa kitaalamu “Couvade Syndrome au “Marosoroso ya ujauzito kwa wanaume.”

Mwanaume anayempenda mke wake mjamzito huanza kupata dalili zinazofanana na za ujauzito, aidha kihisia au kimwili, hata k**a yeye si mjamzito.
Dalili hizi hazitokani na ugonjwa, bali zinahusishwa zaidi na muunganiko wa kihisia, huruma, na mabadiliko ya maisha wakati wa ujauzito.

Dalili ambazo wanaume wanaweza kupata

▪️Kichefuchefu na kutapika hasa asubuhi.
▪️Kuongezeka kwa hamu au kupungua kwa hamu ya chakula.
▪️Maumivu ya kichwa au mgongo.
▪️Kuongezeka uzito au tumbo kuvimba kidogo.
▪️Kuchoka, kukosa usingizi, au wasiwasi.
▪️Mabadiliko ya hisia – huzuni, woga, au hasira bila sababu.
▪️Hamu ya kuwa karibu zaidi na mke wake mjamzito.
▪️Maumivu ya tumbo wakati wa leba (mke anapojifungua) – hii hutokea kwa wachache.

Sababu za hali hii

✅Kihisia (psychological):

Wanaume wengi hujihusisha sana na ujauzito wa wake zao, hivyo wanahisi pia “mizigo” ya kihisia na hofu.

Wasiwasi wa kuwa baba, mzigo wa kifedha, au hofu ya kupoteza umakini wa mke huweza kuchangia.

✅Kihomoni (hormonal changes):

Tafiti zinaonyesha baadhi ya wanaume hupitia mabadiliko madogo ya homoni k**a vile kupungua testosterone na kuongezeka prolactin na cortisol, zinazohusiana na huruma na uangalizi.

✅Kisaikolojia (empathy connection):

Wanaume wanaohusiana kwa karibu kihisia na wake zao hupokea “athari ya kisaikolojia” kutokana na huruma na uhusiano wa karibu.

✅ Mazingira na tamaduni:

Kwa jamii fulani, mwanaume anaweza kujihusisha sana na mila au imani kuhusu ujauzito hadi kuanza kuhisi k**a na yeye anashiriki hali hiyo.

Jinsi ya kukabiliana na hali hii
▪️Elewa kuwa ni kawaida na haitoi ishara ya udhaifu.

▪️Kujadiliana na mwenzi wako kuhusu hisia na hofu.

▪️Kutafuta msaada wa kitaalamu k**a dalili zinakuwa kali (mfano: msongo wa mawazo au usingizi kupotea sana).

▪️Kupumzika na kufanya mazoezi mepesi.

▪️Lishe bora kusaidia mwili kudhibiti mabadiliko.

Kwa kifupi Marosoroso kwa wanaume ni hali halisi inayotokana na muunganiko wa kihisia, homoni, na mazingira wakati wa ujauzito wa wake zao. Ni ishara kwamba mwanaume ana huruma, uhusiano wa karibu, na ushirikiano wa kweli na mke wake katika safari ya ujauzito.

Tuambie ushawahi pitia hili au mume wako ashawahi pitia hili....!?

Watoto wachanga kufunga choo (yaani kutopata choo kwa siku kadhaa) ni jambo la kawaida kwa baadhi yao, hasa kadri wanavy...
12/11/2025

Watoto wachanga kufunga choo (yaani kutopata choo kwa siku kadhaa) ni jambo la kawaida kwa baadhi yao, hasa kadri wanavyokua — lakini inategemea sababu mbalimbali. Hapa kuna maelezo ya sababu kuu na wakati wa kuwa na wasiwasi 👇

Sababu za watoto wachanga kufunga choo

▪️Mabadiliko ya chakula

Kwa mtoto anayeanza kunyonya au kutumia maziwa ya formula, tumbo linahitaji muda kuzoea.

Kubadilisha aina ya maziwa (mfano kutoka maziwa ya mama kwenda formula) kunaweza kufanya choo kigumu au kuchelewa.

▪️Maziwa ya mama kutumika kikamilifu.Moja na mwili wa mtoto

Watoto wanaonyonya maziwa ya mama pekee mara nyingi hawapati choo kila siku, kwa sababu maziwa ya mama husagika yote vizuri.

Ni kawaida mtoto wa wiki chache kutochimba choo kwa siku 3–5, ilimradi hajapoteza hamu ya kula na tumbo si ngumu.

▪️Kukosa maji ya kutosha (dehydration)

Ikiwa mtoto anapata maziwa kidogo, mwili unaweza kufyonza maji yote tumboni, hivyo kinyesi kinakuwa kigumu.

Hii hutokea zaidi kwa watoto wanaotumia formula kuliko wanaonyonya.

▪️Mabadiliko ya mfumo wa mmeng’enyo

Wakati mfumo wa mmeng’enyo unaendelea kukua, choo kinaweza kuchelewa kupita kwa siku chache.

▪️Upungufu wa nyuzi (fiber)

Kwa watoto wanaoanza kula vyakula vigumu (zaidi ya miezi 6), ukosefu wa vyakula vyenye nyuzi k**a mboga, matunda na nafaka unaweza kusababisha kufunga choo.

Dalili za kuangalia – ishara kwamba tatizo ni kubwa

✅Mtoto analia au kuonyesha maumivu wakati wa kujisaidia.

✅Tumbo ni gumu au limevimba.

✅Kinyesi ni kigumu k**a kokoto au kuna damu.

✅Mtoto anakataa kula au anatapika.

Ikiwa dalili hizi zipo → mwone daktari mara moja.

Mambo ya kusaidia nyumbani (kwa ushauri wa daktari au nesi)

Kwa watoto wachanga (chini ya miezi 6): endelea kunyonyesha mara kwa mara.

Kwa watoto waliovuka miezi 6:

Ongeza maji kidogo kati ya milo na matunda k**a parachichi, apple, papai, au mboga laini.

Address

Mbeya

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when AFYA YAKO NA LUCAS posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to AFYA YAKO NA LUCAS:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category