05/05/2025
Mhe sana na anguko lake la kisiasa yaani (KUFA KISIASA) Arusha ni miongoni mwa mikoa michache nchini Tanzania yenye watu wenye itikadi na misimamo yao, sitaki kuingia kwenye upande wa siasa moja Kwa moja japo siasa ni maisha, ila Leo nitaangazia anguko LA Mh sana kwenye upande wa maisha ya kawaida. Roho mbaya pamoja na misimamo ya hovyo imemfikisha hapo alipo Leo, joto la kisiasa limemfanya atumie nguvu ili kujaribu kurudisha Imani Kwa watu kumbe ndio anajitengenezea mazingira magumu sana. NYOTA ni maisha, nyota ikififia au kufunikwa Kila utakalofanya haliendi.
Mh sana ni kiongozi mwenye msimamo ya Hovyo, moyo wa choyo, chuki na visasi hivi vimemfanya kuumizwa leo kisiasa, hata na wana ccm wenzie Leo wanampiga mawe. Hapa chini ya jua ogopa sana visasi, chuki na choyo leo vinamtafuna yeye mwenyewe, tukisema tumchambue Mh sana nazani neno sahihi utasema ni mtu mbaya mno kuwahi kutokea tuache huko Kila mtu anamapungufu yake.
Mh sana Yale aliyomfanyia Mh Lema Leo yanamtafuna kwa nguvu Kwa sababu ni mwepesi kinyota, na hii sio bahati mbaya amepigwa na kitu kizoto, sisi wasukuma tunaamini kwenye miti na hasa dawa za mivuto, huyo aliumiza sana watu nazani aliona kawaida na hakufanya lolote yaani kutambua kosa na kufanya TOBA au k**a Hana Imani huyo alitakiwa kunuwisha nyota yake Kwa kusafishwa mwili kutoa mikosi, Sasa wamekuja watu wanataka Jimbo lake umempiga mkosi (SALALA) ya mako hii SALALA ni kuchafuliwa Kwa mwili na ukitaka kuamini muangalie usoni amejawa na aibu SONI Hana Nuru. Anatia huruma.
Mtazame Mh. Sana Sura imemshuka Nuru Hana kabisa, chini ya jua nyota ndio Kila kitu, watu wakichukua nyota unakuwa maiti inayotembe, utapuuzwa Kwa Kila kitu hata k**a kuna jambo unalijua na lina ukweli kiasi Gani utazomewa k**a BUNDI, Mh Sana yeye Hana kinga, SIO KINGA ZINDIKO, nyota inaweza kuchukuliwa Kwa njia nyingi yaweza kuwa Kwa kusemwa vibaya na watu Kwa matendo yako mabaya (ZONGO) kuchafuliwa mwili kwa kuoshwa dawa za mikosi bila wewe kujua au kulishwa dawa za mikosi hii Huwa ni mbaya zaidi, msomaji wa makala hii MTU anaweza kukuchafua mwili lakini usiombe ukachafuliwa mwili wako Kwa dawa za mikosi kwa kulishwa au Kuzioga (SALALA) kitiba lazima utumie nguvu kubwa sana kujitengeneza njia zingine ni pamoja na kuchotwa mchanga sehemu uliyokanyaga au kivuli Cha mwili wako.
Tungeweza kuandika hata gazeti juu yake, lakini afanye Nini Kwa Sasa!? Huyu anatakiwa kuutakasa mwili wake Kwa vyovyote vile iwe Kwa maombi au mizimu njia zote ni njia sahihi kulingana na Imani yake pia kuomba na kutubu na kumwangukia Mungu ili mwili urudishe Nuru yake ila ni ngumu Kwa kuwa aliyemiibukia na kuliitaji Jimbo lake ni mtu mshika dawa kuliko yeye. Kingine Hali aliyonayo kinyota na mda huu mchache kuelekea uchaguzi k**a hajajiweka sawa asijiusishe na siasa kabisa mpaka atakapo weka mwili sawa, akikaidi pesa yote itapotelea kwenye mikoni ya watu na kura hawatampa nimesema nyota ni maisha, nyota ikipotea Kila kitu kitagoma.
Sasa kitiba MTU k**a huyu ambaye sio Tu nyota yake imepotea yenyewe, huyu nyota yake imechukuliwa kabisa au imefunikwa kwa kutumia madawa mabaya (MAZUMO) Pia kusemwa vibaya na watu Kwa mabaya yake lakini wakati mwingine Kwa kufanyiwa maombi Maalum, DUA na hata Ibada ili kumuomba Mungu atende kulingana na uovu wake, Mungu hujibu maombi kulingana na kipimo Cha uovu Wake, kwani chozi la mtu aliendi Bure, ndio maana Sasa Kila akifanya jambo Akizani unajitengeneza inakuwa kinyume GUNDU wengine wakiita KIMAVI, hii itamfanya akose Hali ya kujiamini Kwa kawaida hii aiji TU Kwa kusemwa vibaya na watu, hii watu wanaongia chimbo na wanakutungua (KUROGWA) yaani NYOTA WANAIZIMA kabisa. Ndio maana unakuwa mwepesi utaambiwa simama una simama, utaambiwa Kaa na unakaa k**a zezeta. Sasa huyu kitiba anatakiwa kupitishwa kwenye njia sahihi za kitiba na dawa zenye vionjo (JINGILA) vya maana siwezi kuandika hapa watu watachukua maujuzi.
Imeandikwa na Ntuzu Traditional Clinic