Lishe yako, Afya yako

Lishe yako, Afya yako Ukurasa huu ni mahususi kwaajili ya Afya lishe, ushauri kwa wale wanaosumbuliwa na magonjwa sugu yasiyoambukizi na kutoa majibu ya nini kifanyike kua salama

Lengo kuu la Mungu kukuumba ni Ili apokee Utukufu kupitia wewe.Isaya 60:21cMungu aliweka kusudi ndani yako ambalo kwa hi...
15/09/2024

Lengo kuu la Mungu kukuumba ni Ili apokee Utukufu kupitia wewe.

Isaya 60:21c

Mungu aliweka kusudi ndani yako ambalo kwa hilo kusudi, Utukufu wake utadhihirika.

Kusudi limebeba kazi ndani yake,

Hivyo Kila kazi unayoiona duniani inawakilisha kusudi la Mungu.

Na kila kazi ni lazima impe Mungu Utukufu maana ndilo lengo kuu la Mungu.

Ikiwa kazi yako haimpi Mungu Utukufu tambua kuwa shetani amekubadilishia mfumo wa kuitumikia kazi hiyo,

Na hii ni hatari sana kwako na kwa kizazi chako.

Hakikisha kazi yako inatimiza Kusudi aliloweka Mungu ndani yako.

*FOR GOD'S GLORY*

05/04/2022
03/04/2022

*NILICHOKITHIBITISHA KWENYE NDOA Miezi 6*

*Kuna kitu nimekuja kukihakikisha kwenye ndoa, hichi kitu bhana alinambiaga mentor wangu M***a Suleiman enzi hizo nikiwa single wakati ule sikumwelewa lakini saizi ndio namwelewa...
Sasa from experience ya ndoa ya miezi 6 ngoja nishuhudie kitu, hapa nataka kuongea na Wanawake wenye bonge za ndoto walioolewa na wanaotarajia kuolewaga....

Maana ya kuwa mke ni kuwa msaidizi na sio hivyo tu Biblia inasema Waefeso 5:22"Enyi wake watiini waume zenu k**a kumtii Bwana wetu.23:Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe,k**a Kristo naye ni kichwa cha kanisa, naye ni mwokozi wa mwili. (English version inasema"Wives, submit to your own husband,as to the Lord." Hapa nilitaka tu hili Neno "Submit"neno submit limetokana na Neno "Submission"
Hili neno submit kwa namna nyingine tunaweza sema "Wives understand and support your husband in ways that show your support for Christ"
Submit iliyoelezewa Kwa Kiswahili Kwa maana ya kutii ina maana nyingi.
Kutii haimaanishi kuheshimu tu,bali ina upana mkubwa Sana unaobeba uhalisia wa mume Kwa ujumla.
Sasa hapa mimi katika kusoma soma na kutafakari nikagundua Submission ndani yake ina maana ya "submit your vision, under his vision"
Ili mwanamke uendane na kusudi la Mungu la Ndoa,
Ili ndoa yako iwe na Amani,
Ili Ndoa yako ibarikiwe,
Ili uendelee kutimiza ndoto zako hata kwenye ndoa( maana hapa kuna wanaosema Mimi siolewi, maana nikiolewa ndoto zangu zitakufa. Hii hata Mimi nilikuwa nayo.
Yani nilikua na ndoto hizo jamani😄mpaka nyingine kuziongea tu zinaweza kukuangusha chini, sijui nifungue mashule, makampuni, mahotel, nawaza ndoto zangu, nikiolewa zitakufa, nilikua naangalia walioolewa wakiwa Moto baada ya ndoa wakazima ghafla, nikajisemea siunaona fulani,fulani kumbe nilikuwa na mawazo mgando,)
Sikuzote napenda kusema *Ukimjua Mungu atakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea atakushauri jicho lake likikutazama* Mungu si akaanza kunifundisha na sio tu kunifundisha alininyoosha haswa mpaka yale mawazo yangu ya alinacha yakayeyuka, akanipondaponda akanifanya k**a atakavyo Yeye lakini ni baada ya Kumwambia BABA nimefika mwisho wa akili zangu naomba akili zako🙇‍♀️🙌🏽 )
Nikaja kugundua sio kwamba vinakufa lakini ni wao hawajaelewa maana ya Submission k**a mke ndani ya ndoa, hasa ukitaka kuishi katika ndoa ya Kusudi la Mungu.
Nikagundua tena kumbe ndio maana ndoa nyingi za Leo zina migogoro na talaka,yani kila kukicha talaka, mpaka mahusiano tu sikuizi yana talaka🙆🏻‍♂️.

Hii inatokana na mfano k**a huu, utamkuta mwanamke anaingia kwenye ndoa na ndoto zake/ huduma na anataka asimamie ndoto zake tuu asiambiwe kitu kingine, na mwanaume ukimwambia kitu utasikia niache nina ndoto zangu, my dear hapa utalia sana na hakuna siku hiyo ndoto itatimia na mwisho wa siku utaishia kupigwa vibuti.
Hujawahi kuona mtu ameolewa ana huduma/kipaji mwisho ndoa inamshinda??

*Sasa tuendelee kwenye submission*
Ili Ndoa yako iwe Sawa na vile tulivyoviona pale juu ikiwemo ndoto zako mwanamke kutimia ni lazima ukubali kusubmit vision/ndoto zako chini ya vision za mume wako.
Kivipi???
Ni Rahisi sana, Ukishajua mume wako ana vision gani, hakikisha unaisimamia vision yake kwa kuchomeka vision yako ndani yake mpaka vision/ndoto zake zitimie.
Kumbuka Mwanzo Mungu alipomuumba Adamu alimpa Kazi ya kufanya, kazi Mungu aliyompa Adamu ndio vision yenyewe, Mungu akaona Adamu pekee hatoweza kuikamilisha vision hiyo ni lazima amfanyie msaidizi wa kumsaidia kuitimiza.
Ndipo akamuumba mwanamke.

Wakati Mungu anamuumba mwanamke alimpa vifaa vyote(equipments) za kuhakikisha maono ya Mungu kwa Adamu yanatimia, mfano kuna (enqubation ability, hichi ni kifaa mojawapo walichopewa wanawake chenye nguvu na Uwezo wa kuatamia ndoto/maono ya mume,watoto, yakwake mpaka yatimie)
*Kuna kitabu kimoja nakiandika ni bonge ya kitabu kwa wanandoa✍🏼hasa Wanawake..stay tuned*

Sasa turudi kwetu, waume zetu wamepewa maono na MUNGU na Sisi ndio wenye vifaa vya kukamilisha maono hayo, ikitokea mwanamke umeligundua hili nakuhakikishia utakuwa na ndoa ya baraka na mfano duniani na Mbinguni.

Cha kufanya mwanamke, yale maono yako uliyokuwa nayo tokea ukiwa single ukiolewa hakikisha unayasubmit kwenye maono ya mumeo sio uyaache hapana, nakupa mbinu hapa👇🏼
*Simamia,Fanya, Pambania,Ombea, Tia moyo, sisitiza, wekeza nguvu, muda wako,akili yako Kwa maono ya mume wako*
Nakuhakikishia ukipambania maono ya mume wako yakatimia, yakwako yanakuwa yameshatimia automatically yani pasipo hata kutumia nguvu.

Mimi nimeanza kuiishi hii baada tu ya kuolewa, na nimejikuta kuna vingine vizuri zaidi vinaongezeka kwenye maono yangu, kuna vitu mume wangu ananiambia tufanye ambavyo ndio Vilevile vilivyokuwa ndoto zangu na nguvu imekuwa kubwa kuliko ambavyo ningepambana mwenyewe lakini hii ni baada tu ya kukubali kusubmit my vision under his vision. Kitu ambacho nisingesubmit ningebaki palepale na kudumaa na huenda hayo mandoto yangu yasingekaa yatimie.

"Make your man's vision shine and your vision will shine automatically"

*Mwisho*
Nikwambie bonge la Siri
Hakuna kitu kinamshinda Mzee wa Siku nikmaanisha Mungu, Jamani Mungu anabadilisha, Mungu anaweza kufanya mambo ambayo akili zetu zilishafikaga mwisho.
Na kingine hakuna ndoa ngumu, hakuna mwanaume mkorofi, hakuna mwanamke mbabe mbele ya huyu Mwamba💪🏼, wewe mpeleke tu mbele zake uone.

*USHUHUDA WANGU*
Jamani hakuna mtu alikuwa mkorofi, mbabe na mjeuri hasa kwenye mahusiano k**a Mimi, Kwa nje ulikua ukiniona hutaamini.
Yaani tunaweza ingia kwenye mahusiano asubuhi na mchana tukaachana🙄
Ilikuwa ni Mimi na misimamo yangu ninachokitaka Mimi ndio kitafuatwa, ukileta mchezo hasa ukiingia kwenye 19 za ndoto zangu yaani hutaamini.
Yaani utanikosea wewe msamahaa utaomba wewe na kuachana naanza mimi🙆🏻‍♂️.
Ulifika wakati nikaona mahusiano yananichelewesha kwenye ndoto zangu, nikafunga ukurasa huo na sio tu nilifunga ukurasa wa mahusiano Bali nilifunga mpaka wa ndoa, nikasema sitaki kabisa kuolewa maana nikiolewa ndoto zangu zitakufa🙄.
Nilikua nikiwaza mwanaume gani atanioa Mimi maaana ukorofi ule nilikuwa namuonea huruma sana, nikasema labda nipate mwanaume mkali, mbabe, mkorofi zaidi yangu tofauti na hapo ningekuja piga mtoto wa watu afu nivunjwe mbavu bure😨maana ukorofi gunia mwili sindano😄.
*Lakini nilipotaka na kutafuta kumjua sanaaa Mungu maana nilikua namjua lakini siyo Ile aliyosema yeye sanaa,Ile ya kushuka mpaka mavumbini, kunyenyekea mbele zake,kuwa si kitu kabisa mbele zake, Ile ya kupungua haswa na Mungu aongezeke sana Kwa maisha yako* nikamwambia BABA naomba unifinyange unifanye k**a utakavyo wewe nikasurrender🙇‍♀️🙌🏽mbele zake.

Kweli Mungu ni mwaminifu sana kwa wale wamtafutao Kwa bidii ni lazima aonekane, Mungu akaingila Kati maisha yangu akashuka Yeye mzima mzima🙌🏽🙌🏽hakusema hata amtume malaika, Mungu akaninyoosha haswaaa, akanipondaponda akanifanya k**a atakavyo Yeye, akaniondolea ukorofi wote, ubabe, misimamo ya hovyoo, sijui ndoto za mavitu gani sijui magari, manyumba, makampuni kwamba niyapate kwanza haya ndio niolewe tofauti na hapo nilikuwa nasema siolewi.

Wakati Mungu ananifundisha alinibananishaga kwenye Kona hiyo sitasahau na akanambia
"Winnie mwanangu hivyo unavyovitaka hutokaa uvipate mpaka utakapoolewa, Akaendelea kuniambia si unaona unavyopambana na hakuna ulichopata, kanambia Kwa jinsi ulivyo na juhudi usingekuwa mtu wa kukosa hata kagari wala kanyumba lakini vyote hivyo sikupi maana nikikupa hutowaza kabisa kuolewa na ujeuri utaongezeka na ili kusudi langu kwako litimilike na kile nilichoweka ndani yako kiwe chenye Utukufu wangu ni lazima uolewe.
Akaendelea kuniambia nakuahaidi hivi unavyovitaka siku ukiolewa utavipata na zaidi maana ulivyonavyo akilini mwako ni tuvitu tudogo saaaanaa kuliko vile nilivyoweka mbele yako ukiwa na familia.
Mfano wa kwanza akanioneshea, kweli nilivyoinua mikono nikasema Baba nakubali🙌🏽 kufuata ratiba yako, nikamkubali kijana aliyemleta kwangu wakati ule, nikashangaa🙄lile gari langu nilikuwa nimelichora kichwani Mungu siakampa huyo jamaa🤨
Sijakaa sawa process za ndoa zikaanza, Ile nyumba yangu iliyokuwa kwenye ndoto zangu ikamdondokea tena huyo jamaaa🤨, nikasema kweli Mungu ni hatari🙌🏽🙌🏽
Nikakubal ndoa ikafungwa baada ya ndoa tukahamia kwetu, Mungu kanikumbusha unaona uliyokuwa unapambana mwenyewe ungezeekea kwenu pasipo baiskeli wala banda la kuku🙆🏻‍♂️.
(Hii ni kwangu sisemi masingle ladies msinunue magari wala kujenga nyumba, mkiweza jengeni haswaa lakini k**a ratiba ya Mungu inataka tofauti lazima usarende).

Sasa juzi hapo nilikuwa naenda kanisani bodaboda akachelewa kunifuata, nikakasirika kweli😣
Nikasikia sauti ndani ikiniambia "yaani wewe siulikuwa unalilia gari haya leo gari imepack hapo huna hata mpango nayo, ona Sasa ivi unavyoiona ya kawaida!kitu kidogo hivi ndio kilikuwa kinakufunga usifikilie hatima alizokuandalia Mungu?? !
*Mungu akanifundisha kitu kikubwa Sana hapa, kwamba tunakuwa na vijimipango vyetu ambavyo vinatufunga kufikilia makusudi yake makubwa Sana hasa mabinti/Wanawake kumbe Mungu katuandalia mabonge ya mipango ni sisi tu kumwambia Mungu nataka kutembea kwenye mipango yako🙌🏽 niongoze Baba.*

Turudi baada ya ndoa Sasa,baada ya kukubali kufuata ratiba ya Mungu, niulize leo zile ndoto zangu naziona kumbe vilikuwa vijindoto tu, kuna mabonge ya mindoto bhana na mavision ukitembea kwenye mipango ya Mzee wa Siku🙌🏽
Yaani tena hiyo mindoto mnaijadili wawili kila mmoja anaweka point mezani mkianza kuitekeleza acha kabisa huwa ni kutelezaa tuuu. Hapa ndipo nilithibitisha kumbe ni haikika na kweli Ndoa ni Kusudi halisi na kuu Sana la Mungu Kwa maisha yetu.

Na uzuri mmoja mkijua Sana Mungu yaani anawaambia kabisa hapa wanangu fanyeni hivi na anakupa mtu ambaye mtaendana hata kimandoto unashangaa mume anakuambia Kwa ukubwa wa hili mke wangu hapa tuweke ghorofa kitu wewe uliwaza room moja na store😄.

Mabinti, Wanawake, Wanaume tujifunze Kumkabidhi Mungu njia zetu na mawazo yetu yatathibitika tukaze Sana kumjua Yeye ili atufundishe na kutuonesha njia tutakazoziendea atatushauri jicho lake likikutazama🙌🏽🙌🏽🙌🏽
*FOR GOD'S GLORY*

NINI UFANYE ILI KUPUNGUZA TUMBO? ¶¶Katika jamii yetu wanawake ndio wanaohangaika zaid kutoa matumbo yao makubwa, utawasi...
28/08/2020

NINI UFANYE ILI KUPUNGUZA TUMBO?

¶¶Katika jamii yetu wanawake ndio wanaohangaika zaid kutoa matumbo yao makubwa, utawasikia mara nyingi wakiulizia kuhusu dawa ya kupunguza tumbo kwa wanawake, lakini si kwa ajili ya kukwepa madhara ya kiafya, bali kwa ajili ya kuboresha mwonekano wao kiurembo-kwao ni suala la urembo tu na si suala la afya. Kwa upande mwingine akina baba huona fahari kuwa na vitambi, kwao kitambi ni dalili ya kunyookewa na maisha.

¶¶Katika mada ya leo tutazungumzia hayo matumbo makubwa na vitambi ambapo tutaona matumbo hayo au vitambi hivyo ni nini, tutaeleza madhara ya kuwa na matumbo hayo makubwa na mwisho kutoa ushauri wa jinsi ya kuyapunguza matumbo hayo.


✓✓Nini Maana Ya Tumbo Kubwa Au Kitambi


¶¶Leo utasikia neno la ajabu kuwa “kila mtu ana kitambi, hata yule ambaye tumbo lake kwa nje linaonekana kuwa flat kabisa na kuwa kitambi kina madhara makubwa kwa afya yako kuliko aina nyingine yo yote ya mafuta yaliyo ndani ya mwili wako.”

✓✓Hii ina maana gani?

¶¶Kitambi ni mafuta na mafuta haya yanaweza kuwa chini ya ngozi yako au ndani kabisa kuzunguka moyo, mapafu, maini na viungo vingine. Ni mafuta haya ya ndani (visceral fat) ambayo yanaweza kuwa tatizo kubwa kwa afya yako hata k**a mwili wako ni mwembamba kiasi gani. Mwili huhitaji mafuta haya ya ndani kwa ajili ya kutenganisha viungo vya ndani ya mwili visigusane na kusuguana, lakini yakizidi huleta matatizo ya kiafya. Ukiwa na mafuta mengi mno utakuwa kwenye hatari ya kukumbwa na magonjwa k**a ya high blood pressure, kisukari (Type 2 Diabetes), magonjwa ya moyo, kansa (kansa ya maziwa na kansa ya utumbo) na mengine. Kuongeza uzito au kunenepa kunasababisha mwili ushindwe kupata sehemu ya kutosha ya kuhifadhi mafuta na hivyo kuanza kuyatunza mafuta hayo kwenye sehemu za ndani ya mwili, kuuzunguka moyo, na ndipo matatizo yanapoanza.



✓✓Utapimaje tumbo lako?

¶¶Kuna njia za kitaalamu za kupima kiasi cha mafuta ya ndani uliyo nayo ambazo ni CT Scan au MRI lakini pia unaweza kujipima mwenyewe ukapata picha nzuri tu ya hali yako. Chukua kipimo cha utepe, kile kinachotumiwa na mafundi cherehani (measuring tape), jipime eneo la kitovuni ukiwa umesimama huku ukihakikisha kuwa utepe ni mnyoofu. Kwa afya nzuri, kipimo kisizidi nchi 35 kwa mwanamke na kisidi nchi 40 kwa mwanamme.

Kuwa na mwili wenye umbo la pears “pear shape”, hips na mapaja makubwa, kunafikiriwa kuwa ni bora zaidi ya umbo la apple ambalo linamaanisha kiuno kipana zaidi. Kuwa na kiuno kipana kuna uwiano na kiasi cha mafuta ya ndani (visceral fat) uliyo nayo.



✓✓Namna Ya kuondoa Matumbo


¶¶Tumeona hapo juu kuwa hata watu wembamba wana mafuta ya ndani ambayo yanaweza kuwasababishia matatizo ya kiafya. Uwingi wa mafuta unakuwa ni wa kiurithi, utalingana na style ya maisha unayoishi na jinsi gani mwili wako unafanya mazoezi – mafuta haya hupenda mtu asiyejishugulisha yaani yule ambaye anaufanya mwili wake kubweteka.

Maandiko mengi sana yameandikwa kuhusu namna ya kupunguza unene wa mwili na makampuni mengi yamekuja na dawa za kupunguza unene wa mtu. Kimsingi ili mwili upungue unene, unahitaji kutumia kalori nyingi kuliko unazozipokea. Hili ni la kweli vilevile kwa mada yetu ya leo ya kupunguza tumbo kwani si rahisi kupunguza tumbo peke yake bila kupunguza sehemu nyingine za mwili. Ili kufanikisha azma ya kutumia kalori nyingi zaidi ya zile unazozipokea, hapa nashauri njia 4 za kuzitumia:



1• Mazoezi Ya Viungo Ya Kupunguza Tumbo

°Unaweza kufanya mazoezi ya aina nyingi ili kupunguza tumbo. Mazoezi yo yote ya nguvu yatapunguza mafuta ya mwili wako pamoja na mafuta ya ndani (visceral fat).

°Mazoezi ya kadri ya dakika 30 mara tano kwa wiki yanafaa, k**a vile kutembea, ili mradi unatoa jasho, yatakufanya uheme kwa haraka na kuongeza mapigo ya moyo wako.
Unaweza kupunguza muda kwa kufanya mazoezi ya nguvu zaidi k**a jogging kwa dakika 20 mara nne kwa wiki.

°Unaweza kupata matokeo mazuri vile vile kwa kufanya mazoezi ya ndani ukiwa nyumbani mwako. Cha msing ni kuanza na mazoezi mepesi na taratibu, kuongeza ugumu wake hadi kufikia mazoezi ya nguvu.


2 •Chakula

°Kuna maandishi mengi mno kuhusu somo hili la kupunguza mafuta ya mwili kwa kuwa na mpango mzuri wa ulaji chakula. Unaweza pia kusoma ukurasa wetu wa “Punguza Unene“. Kwa kifupi unahitaji kuzingatia yafuatayo:

••••Kula mboga za majani kwa wingi sana kulijaza tumbo lako

••••Kunywa maji mengi sana

••••Weka chakula cha kukutia hamu mbali na nyumba yako

••••Tafuta shughuli za kukufanya uwe busy kila wakati

••••Kula kutoka kwenye sahani tu ukiwa umeketi mezani

••••Kula milo yote, acha tabia ya kuruka milo

3 • Kupata Usingizi Wa Kutosha

Kupata usingizi kwa muda mzuri kumeonyesha kuwa na mchango katika kudhibiti kiwango cha mafuta katika mwili wa binadamu. Katika utafiti mmoja, watu waliopata usingizi kwa saa 5 hadi 6 kwa siku katika kipindi cha miaka 5, walionyesha kuwa na mafuta mwilini kidogo zaidi ukilinganisha na wale waliopata usingizi kwa pungufu ya saa 5 kwa siku au wale waliolala kwa saa 8 au zaidi kwa siku.

4 • Kuepusha Msongo Wa Mawazo

Kila mmoja wetu hapatwa na mawazo. Jinsi unavyoyachukulia mawazo hayo huwa na mchango mkubwa katika kujaza mafuta mwilini. Jaribu kushiriki katika mazungumzo na ndugu katika familia na marafiki zako. Mazoezi ndiyo ndiyo bora kabisa kwani hukutoa kwenye msongo wa mawazo wakati huo huo yakikupunguzia unene. Ukipungukiwa na mawazo utaweza kufanya maamuzi mazuri zaidi kuhusu maisha yako.

5. Kutumia Virutubishi

Kuna virutubishi ambavyo vimethibitika kusaidia kupunguza uzito wa mwili. Virutubishi vinafanya kazi vizuri ikiwa mwili utakuwa na kiwango kizuri cha madini ya calcium katika damu. Tafiti zimeonyesha kuwa asilimia moja ya madini ya calcium ndani ya mwili huwa katika mzunguko wa damu. Kiwango hiki cha calcium kikipungua, homoni ya parathyroid huzuia uvunjwaji wa mafuta katika mwili. Hivyo basi, k**a kiwango cha calcium katika damu kitakuwa kimepungua, zoezi la kupunguza mafuta mwilini halitafanikiwa.

Baadhi ya virutubishi vya kupunguza mafuta mwilini ni k**a:

1. Choleduz

Kupunguza Kasi ya UZEE
2. Restolyfe

Kuweza kupata maelezo ya virutubishi hivyo, wasiliana nasi kupitia njia yo yote iliyo rahisi kwako kati ya hizi zilizoorodheshwa hapa chini.

Soma mada nyingine zinazolingana na hii kwenye kurasa za "Lishe yako,Afya yako".

✓✓ Ndugu msomaji unakaribishwa sana kuuliza maswali uliyonayo au kutoa maoni yako kuhusu mada yetu ya leo. Itakuwa ni furaha kubwa kwetu kukujibu.



✓✓Kwa maoni, maswali au ufafanuzi zaidi wasiliana nasi kupitia barua pepe winng4363@gmail.com.
¶Pia Unaweza kutupigia simu moja kwa moja kupitia namba 0763042588 au kufika ofisini kwetu ... MOROGORO KITUO CHA FIRE, JENGO LA SABA GENERAL FLOOR NUMBER 2.

27/08/2020

¶¶Karibu katika kipengele Cha darasa la leo, linalohusu kujikinga na UTI Sugu.

✓✓Zifuatazo Ni njia ambazo zinaambatana na vyakula tulivyosoma;

¶¶Unywaji wa maji ya uvuguvugu kila siku asubuhi kabla ya kutia chochote kinywani. Pia zingatia unywaji wa juisi badala ya vinywaji vikali.

¶¶Epuka vinywaji baridi, pombe, chai ya rangi na kahawa.

¶¶Mara zote jinawishe kutoka mbele kurudi nyuma hasa kwa mwanamke na uepuke kuchangia vifaa vya bafuni nk

¶¶Usikae na mkojo kwa muda mrefu, Mara usikiapo kupata haja ndogo unapaswa kwenda Mara moja.

¶¶Vaa nguo za ndani zilizotengenezwa na pamba.

¶¶Epuka tendo la Ndoa kinyume na maumbile.

Hongera Sana kwa wewe uliefwatilia somo hili hata hapa tulipofikia hitimisho katika kipengele hiki Cha UTI.

Usikose kufwatilia page na masomo yetu

✓✓Kwa ushauri zaidi wasiliana nasi kwa namba 0763042588

Karibu tuendelee na darasa la kujikinga na UTI Sugu. Leo tutaangalia;¶¶Mshubiri (Aloe-vera)Kwanza kabisa Jeli ya Aloe Ve...
26/08/2020

Karibu tuendelee na darasa la kujikinga na UTI Sugu. Leo tutaangalia;

¶¶Mshubiri (Aloe-vera)
Kwanza kabisa Jeli ya Aloe Vera huongeza Kinga ya mwili kutokana na mu-aloe-vera kua na viinilishe vingi Sana muhimu kwa Afya ya binadam. Aloe-vera Ina vitamin A, B, C na E.

¶¶Namna ya kutumia Aloe-vera kutibu na kujinga na UTI Sugu;

✓✓Chukua Jeli ya mshubiri(Aloe-vera) vijiko vikubwa vinne Kisha changanya na maji ya kawaida ili kupata kikombe kimoja (ml 250) au robo Lita .
Changanya vizuri mchanganyiko huu na unywe kutwa Mara 2 kwa siku ndani ya wiki 3 mpka 4. Unaweza kuongeza asali ndani take vijiko vikubwa vitatu ili kupunguza ukali wa dawa hii.

¶¶Usikose darasa linalofwata.
✓✓ Kwa ushauri zaidi wasiliana nasi kwa namba 0763042588 au
fika katika ofisi zetu Morogoro-Kituo Fire, Jengo la Saba General floor number 2.

¶¶Kiboko nyingine ya UTI sugu hii hapa✓UBUYU✓Inaelezwa kuwa unga wa ubuyu una vitamini C nyingi mara 6 zaidi ya ile inay...
25/08/2020

¶¶Kiboko nyingine ya UTI sugu hii hapa
✓UBUYU✓
Inaelezwa kuwa unga wa ubuyu una vitamini C nyingi mara 6 zaidi ya ile inayopatikana katika machungwa.
¶¶Vitamin C husaidia kuzuia uzalishwaji wa bacteria wabaya Mwilini.

¶¶Baadhi ya madaktari wanashauri mtu atumie mpaka mg 5,000 za vitamin C kwa siku kwa mgonjwa anaesumbuliwa na maambukizi ya Mara kwa Mara kwenye njia ya mkojo.

¶¶Vitamin C hukifanya kibofu Cha mkojo kubaki na Afya kutokana na asidi yake Safi kwenye mkojo, kitendo ambacho ni muhimu katika kuwazuia bacteria wabaya kufanya makazi kwenye kibofu Cha mkojo.
Ukiacha machungwa, vitamin C inapatikana kwa wingi katika juisi ya ubuyu na kwenye mlonge

¶¶Hakikisha unapata kiasi Cha kutosha Cha vitamin C kila siku ili kujikinga na kujitibu na UTI
¶¶Tumia glass moja mpaka mbili za juisi ya ubuyu kila siku.
✓✓✓Usikose kipindi kinachofwata Tutaangalia aina nyingine ya kupambana na UTI Sugu.

✓✓✓Kwa ushauri zaidi wasiliana nasi kwa namba 0763042588

Karibu tuangalie tiba nyingine ya UTI Sugu¶¶MAJI YA KUNYWA¶¶Maji yakunywa Ni Kinga ya kipekee sana Ikiwa unasumbuliwa na...
24/08/2020

Karibu tuangalie tiba nyingine ya UTI Sugu

¶¶MAJI YA KUNYWA¶¶

Maji yakunywa Ni Kinga ya kipekee sana Ikiwa unasumbuliwa na UTI na inakutokea unapatwa na ugonjwa huu Mara kwa Mara, unapaswa kuhakikisha unakunywa maji ya kutosha kila siku walau glass 8 mapka 10 kwa siku.

¶Unapaswa kunywa maji kwa utaratibu huu:
✓✓✓Maji ya uvuguvugu kila siku asubuhi unapoamka kabla yakutumia chochote. Baada yakunywa maji Hakikisha unakaa nusu saa ndipo upige mswaki au kupata kifungua kinywa.

••••Kwa kila wiki unapaswa kuzingatia utaratibu huu wa maji ya uvuguvugu muda wa asubuhi;
°°°°Wiki ya kwanza= Glass 3
°°°°Wiki ya Pili. =Glass 4
°°°°Wiki ya tatu. =Glass 5
°°°°Wiki ya nne. =Glass 6

✓✓✓kunywa maji jioni baada ya shughuli zako zote, kabla ya kupata chakula Cha jioni.

•••Pata maji glass 2 mpaka glass 3.

Kwanini maji yanauwezo Mkubwa Sana wakuondoa na kukinga na UTI?

✓✓✓Mara nyingi mtu mwenye UTI hua ana upungufu wa maji mwililni na Ikiwa utachunguza mkojo wake utaona ni wa rangi ya njano.
Hivyo kunywa maji yakutosha kila siku hupelekea bacteria wote wanaokupelekea upatwe na UTI kulazimika kutoka nje ya mwili kupitia mkojo utakaoupata kutokana na kukojoa Mara kwa Mara K**a Matokeo ya kunywa maji mengi na utaona baada ya siku 4 mpaka 7 hata rangi ya mkojo itaanza kubadilika.
..Usikose darasa linalofwata..Kwa mawasiliano zaidi wasiliana nasi kwa namba 0763042588

Kiboko nyingine ya UTI hii hapa¶¶¶Limau ni tunda ambalo ndani yake hupatikana vitamini C ambayo Ni muhimu San katika kuk...
19/08/2020

Kiboko nyingine ya UTI hii hapa

¶¶¶Limau ni tunda ambalo ndani yake hupatikana vitamini C ambayo Ni muhimu San katika kukinga na kuzuia maambukizi ya UTI.

¶¶¶Weka vijiko vikubwa vitano vya juice ya limau au ndimu na uongeze maji ili kupata robo Lita(250ml) na unywe kutwa Mara tatu.

¶¶¶Pia unaweza kuongeza asali vijiko vikubwa vitatu ndani yake. Mchanganyiko huu wa limau na maji ya uvuguvugu utakuondolea maumivu yatokanayo na UTI na hata kuzuia kutokwa na damu K**a Matokeo ya maambukizi ya UTI hasa kwenye kibofu Cha mkojo.

¶¶¶Hakikisha unakunywa Mchanganyiko huuasubuhi mara tu baada ya kuamka kabla ya kutia chochote kinywani, Kisha tulia ndani ya lisaa limoja ndipo uswaki na kupata kifungua kinywa.

✓✓✓Usikose kipindi kinachofwata, tutaangalia Aina nyingine ambazo zinafanya kazi kwa pamoja na tulizokwisha ziona katika kukinga na kutibu UTI sugu.

•••••Kwa ushauri zaidi wasiliana nasi kwa namba 0763042588

✓✓✓Karibu tuangalie Aina nyingine ya chakula ambacho ni muhimu Sana katika kutibu UTI sugu..¶¶¶Kitunguu swaumu ni mojawa...
18/08/2020

✓✓✓Karibu tuangalie Aina nyingine ya chakula ambacho ni muhimu Sana katika kutibu UTI sugu..

¶¶¶Kitunguu swaumu ni mojawapo ya tiba mbadala ya nguvu katika kutibu maambukizi kwenye njia ya mkojo .

¶¶¶Ni dawa nzuri dhidi ya bacteria na virusi hivyo ni muhimu na inao Uwezo wa kutibu na kuzuia maambukizi ya UTI ya jumla na hata Yale ya kibofu Cha mkojo.

¶¶¶Kwakua moja ya kazi ya kitunguu swaumu ni kusafisha mkojo Basi ni dhahiri kua inafaa Sana katika kutibu UTI.

¶¶¶Namna yakutumia;Chukua kitunguu swaumu kimoja na ukigawe Mara 2 kisha menya nusu yake(Punje 10au 15). Menya Punje moja baada ya nyingine na kisha ikateate vipande vidogo vidogo kwa kutumia kisu.
Baada ya hapo Chukua vipande hivyo na uvimeze K**a unavyomeza dawa na maji vikombe viwili (2) kila unapoenda kulala na mapema uamkapo asubuhi kwa siku Saba mfululizo.

✓✓Usikose kipindi kinachofwata, tutaangalia Aina nyingine ya tiba ya UTI.

✓✓Kwa ushauri na mawasiliano zaidi, wasiliana nasi kwa namba 0763042588

Kinga madhubuti ya UTI¶¶Nanasi ni mojawapo ya tunda linalokinga na kuondoa maambukizi ya UTI.¶¶Kula nanasi Mara kwa Mara...
14/08/2020

Kinga madhubuti ya UTI

¶¶Nanasi ni mojawapo ya tunda linalokinga na kuondoa maambukizi ya UTI.

¶¶Kula nanasi Mara kwa Mara ni mbinu nzuri kabisa katika kudhibiti maambukizi katika njia ya mkojo.

¶¶Kwenye nanasi Kuna kimeng'enya muhimu Sana kijulikanacho kwa kitaalam K**a Bromelain.

¶¶Katika utafiti mmoja wa watu wenye UTI waliopewa hii Bromelain samabamba na antibiotics zao walifanikiwa kuondokewa na maambukizi ya UTI.

¶¶Kula vipande vitatu mpaka vitano vya nanasi kila siku kutakuweka mbali na maambukizi ya ugonjwa huu.

✓✓✓Kwa ushauri zaidi wasiliana nasi kwa namba 0763042588

Kiboko ya UTI Sugu na maambukizi ya uzazi kwa Wanawake...Kwa maelezo na ushauri namna yakutumia wasiliana nasi kwa namba...
12/08/2020

Kiboko ya UTI Sugu na maambukizi ya uzazi kwa Wanawake...
Kwa maelezo na ushauri namna yakutumia wasiliana nasi kwa namba 0763042588

07/08/2020

Karibu katika darasa letu,,leo tutaangalia ;;
UGONJWA WA U.T.I (URINARY TRACT INFECTION) NA TIBA YAKE.

U.T.I ni maambukizi kwa njia ya mkojo na huathiri mfumo wa mkojo na mfumo wa uzazi, wadudu huathiri sana kibofu na urethra. Jina U.T.I ni kifupi cha URINARY TRACT INFECTION (Neno la kingereza) watu wengi huzoea kuita hivyo wakijua ni jina la kiswahili, imeshazoeleka hivyo. Jinsia ya k**e wana hatari kubwa kuliko jinsia ya kiume. Maambukizi yakwenye kibofu huleta maumivu makali, madhara makubwa hutokea maambukizi yakifika mpaka kwenye figo. U.T.I husababishwa na wadudu wadogo sana ambao ni bakteria waitwao Escherichia coli (E. coli), wanapoingia mwilini na kuenda kuathiri mfumo wa mkojo.

U.T.I hutibika haraka kwa mtu ambaye atatumia dawa na pia yaweza kuleta madhara makubwa isipotibika huweza kuathiri mfumo wa uzazi, kibofu, na sehemu mbalimbali, tunashauri mtu mwenye U.T.I inatakiwa awe msafi na kubadili mienendo iliyo hatarini.

✓✓✓MGAWANYO WA U.T.I

Kuna mgawanyo wa aina mbili za U.T.I

••Maambukizi ya Upande wa juu – Hii hujumuisha Figo na Ureta
••Maambukizi ya Upande wa chini – Hii hujumuisha Kibofu na Urethra

¶¶¶CHANZO CHA MAAMBUKIZI YA U.T.I

U.T.I husababishwa na wadudu wadogo sana ambao ni bakteria waitwao Escherichia coli (E. coli), wanapoingia mwilini na kuenda kuathiri mfumo wa mkojo, vitu vifuatavyo vinaweza kukuingiza kwenye hatari ya kupata U.T.I;

1.Kinga ya mwili kutokuwa imara
2.Kutumia Vifaa au Dawa za kuzuia mimba
Kwa wa k**e; Kupungua kwa homoni ya estrogeni
3.Mtu mwenye kisukari
4.Kutumia choo kichafu na kutumia idadi kubwa ya watu
5.Kuwa na tatizo la mmeng’enyo na tatizo la choo
6.Kukaa kwa mda mrefu bila kutembeatembea
7.ngono zembe
8.kubana mkojo muda mrefu
9.wagonjwa wanaowekewa mpira wa mkojo

¶¶¶DALILI ZA MTU MWENYE U.T.I

Dalili za mtu mwenye tatizo la U.T.I hutokea tofauti kulingana na umri, jinsia na sehemu iliyoathiriwa. Hizo dalili ni k**a;

1.Kujihisi mchovu na kutokujisikia vizuri
2.Kukojoa kwa shida na kujilazimisha
3.Maumivu wakati wa kukojoa
4.Kukojoa kiasi kidogo na mara kwa mara
5.Mkojo kutoa harufu kali
6.Mkojo kuwa na rangi tofauti zisizo za kawaida kwa mfano wekundu kiasi
7.Kichefuchefu au kutapika
8.Maumivu ya tumbo, au pande za mwili karibu na tumbo mpaka sehemu za misuli
9.Joto laweza kuongezeka

¶¶¶JINSI YA KUEPUKANA NA U.T.I

1.Kunywa maji mengi
2.Acha kutumia dawa za uzazi wa mpango
3.Kula vizuri vyakula bora hasa asilia na sio vyakula vyenye kemikali
4.Kojoa hata kidogo baada ya kujamiiana
5.Punguza au acha kunywa pombe na kutumia sigara huchochea kuathiri kibofu
6.Kuwa msafi hasa sehemu za siri ili kutoruhusu bakteria
7.Usipulizie spray kwenye sehemu za siri

KWA USHAURI ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA:0763042588

05/08/2020

*UJUE UGONJWA WA P.I.D*

Maambukizi katika mfumo wa uzazi wa mwanamke kwa kitaalamu Pelvic Inflamatory Diseases au kwa kifupi PID, ni moja ya matatizo ambayo huwaathiri sana wanawake. Kwa kawaida maambukizi haya huhusisha shingo ya uzazi (cervix) hali ambayo hujulikana k**a cervicitis, nyama ya mfuko wa uzazi (endometrium) ambayo kitaalamu huitwa endometritis, na mirija ya uzazi (fallopian tubes) hali ijulikanayo kitabibu k**a salpingitis.

1⃣ *_PID husababishwa na nini?_*

Pamoja na aina kadhaa za vimelea kuhusishwa na PID, vimelea vya jamii ya Neisseria Gonorrhoeae pamoja na Chlamydia trachomatis ndivyo vinavyoongoza kwa umaarufu zaidi katika kusababisha PID kwa akina mama.

2⃣ *Je mwanamke huambukizwaje PID?* Kuna njia kadhaa ambazo mwanamke anaweza kuambukizwa PID. Njia hizo ni pamoja na
✅Kufanya ngono isiyo salama.
✅Maambukizi ya njia ya uzazi hasa kipindi mara baada ya kujifungua (au postpartum period)
✅Maambukizi ya njia ya uzazi mara baada ya kutoa mimba kwa njia zisizo salama (post abortion) au mara baada ya mimba kutoka (miscarriage)
✅Kutumia vipandikizi vya ndani ya mfuko wa uzazi (IUCD) k**a njia mojawapo ya uzazi wa mpango.
✅Kuambukizwa kupitia damu iliyo na vimelea vya PID.

3⃣ *Dalili za PID ni zipi?* Zipo dalili kadhaa za ugonjwa huu wa PID. Miongoni mwa dalili hizi ni :-
✅Mwanamke kuhisi maumivu ya tumbo hasa maeneo ya chini ya kitovu.
✅Kupata maumivu ya mgongo.
✅Mwanamke kutokwa na uchafu sehemu za siri. Uchafu huu huambatana na harufu mbaya.
✅Kuhisi maumivu wakati wa kukojoa.
✅Kupata maumivu wakati wa tendo la ndoa.

✅Kutoka damu bila mpangilio wakati wa hedhi.
✅Kupata homa.
✅Wakati fulani kuhisi kichefuchefu na
Pia kutapika.

N.B. *Maambukizi katika via vya uzazi vya mwanamke yanatibika kabisa ukipata tiba ya uhakika, usipozingatia ni chanzo cha Ugumba*

¶¶¶Usikose kipindi kinachofwata,, Tutaangalia njia zakuweza kujikinga na kutibu Tatizo hili.

✓✓✓Kwa ushauri zaidi wasiliana nasi kwa namba 0763042588

05/08/2020

*UJUE UGONJWA WA P.I.D*

Maambukizi katika mfumo wa uzazi wa mwanamke kwa kitaalamu Pelvic Inflamatory Diseases au kwa kifupi PID, ni moja ya matatizo ambayo huwaathiri sana wanawake. Kwa kawaida maambukizi haya huhusisha shingo ya uzazi (cervix) hali ambayo hujulikana k**a cervicitis, nyama ya mfuko wa uzazi (endometrium) ambayo kitaalamu huitwa endometritis, na mirija ya uzazi (fallopian tubes) hali ijulikanayo kitabibu k**a salpingitis.

1⃣ *_PID husababishwa na nini?_*

Pamoja na aina kadhaa za vimelea kuhusishwa na PID, vimelea vya jamii ya Neisseria Gonorrhoeae pamoja na Chlamydia trachomatis ndivyo vinavyoongoza kwa umaarufu zaidi katika kusababisha PID kwa akina mama.

2⃣ *Je mwanamke huambukizwaje PID?* Kuna njia kadhaa ambazo mwanamke anaweza kuambukizwa PID. Njia hizo ni pamoja na
✅Kufanya ngono isiyo salama.
✅Maambukizi ya njia ya uzazi hasa kipindi mara baada ya kujifungua (au postpartum period)
✅Maambukizi ya njia ya uzazi mara baada ya kutoa mimba kwa njia zisizo salama (post abortion) au mara baada ya mimba kutoka (miscarriage)
✅Kutumia vipandikizi vya ndani ya mfuko wa uzazi (IUCD) k**a njia mojawapo ya uzazi wa mpango.
✅Kuambukizwa kupitia damu iliyo na vimelea vya PID.

3⃣ *Dalili za PID ni zipi?* Zipo dalili kadhaa za ugonjwa huu wa PID. Miongoni mwa dalili hizi ni :-
✅Mwanamke kuhisi maumivu ya tumbo hasa maeneo ya chini ya kitovu.
✅Kupata maumivu ya mgongo.
✅Mwanamke kutokwa na uchafu sehemu za siri. Uchafu huu huambatana na harufu mbaya.
✅Kuhisi maumivu wakati wa kukojoa.
✅Kupata maumivu wakati wa tendo la ndoa.

✅Kutoka damu bila mpangilio wakati wa hedhi.
✅Kupata homa.
✅Wakati fulani kuhisi kichefuchefu na
Pia kutapika.

N.B. *Maambukizi katika via vya uzazi vya mwanamke yanatibika kabisa ukipata tiba ya uhakika, usipozingatia ni chanzo cha Ugumba*

***Usikose kipindi kinachofwata;;Tutaangalia njia zakuweza kujikinga na kutibu Tatizo hili....

¶¶¶Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kwa namba 0763042588

Address

Morogoro

Opening Hours

Monday 11:00 - 19:00
Tuesday 11:00 - 19:00
Wednesday 11:00 - 19:00
Thursday 11:00 - 19:00
Friday 11:00 - 19:00
Saturday 00:00 - 18:00
Sunday 02:00 - 21:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Lishe yako, Afya yako posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Lishe yako, Afya yako:

Share