dr.singano_afya

  • Home
  • dr.singano_afya

dr.singano_afya Elimu ya afya na ushauri juu ya afya

📌Kumeza folic acid (au folate) kabla ya kubeba mimba kuna faida nyingi muhimu sana kwa afya ya mama na mtoto. Hapa chini...
09/06/2025

📌Kumeza folic acid (au folate) kabla ya kubeba mimba kuna faida nyingi muhimu sana kwa afya ya mama na mtoto. Hapa chini ni baadhi ya faida kuu:

1. Kuzuia matatizo ya neva ya mtoto (neural tube defects)
Folic acid husaidia kuzuia matatizo k**a:
Spina bifida (mgongo wa mtoto kutokufunga vizuri)
ubongo wa mtoto kutokukua vizuri
📌Haya matatizo hutokea wiki za mwanzo kabisa za ujauzito (wiki ya 3 hadi 4), mara nyingi hata kabla mama hajajua k**a ni mjamzito — ndiyo maana ni muhimu kuanza kutumia kabla ya kushika mimba.

2. Kusaidia ukuaji mzuri wa mtoto tumboni
Folic acid ni muhimu kwa ukuaji wa seli mpya, hasa wakati mtoto anapokua haraka mwanzoni mwa ujauzito.

3. Kupunguza hatari ya mimba kuharibika (miscarriage)
Utafiti unaonyesha kwamba wanawake wanaotumia folic acid qwana uwezekano mdogo wa mimba kuharibika mapema.

4. Kuzuia matatizo ya kuzaliwana matatizo ya moyo
Inaweza kusaidia kupunguza hatari ya matatizo ya moyo kwa mtoto.

5.kumsaidia mama kutokupata changamoto ya upungufu wa damu kipind cha ujauzito.singano_afya

Kuhudhuria clinic wakati wa ujauzito inakusaidia wewe na mwanao aliyeko tumboni kuwa na afya njema.1.Madaktari wanaweza ...
23/01/2025

Kuhudhuria clinic wakati wa ujauzito inakusaidia wewe na mwanao aliyeko tumboni kuwa na afya njema.
1.Madaktari wanaweza kugundua matatizo ya kiafya mapema wanapokuona clinic mara kwa mara. Hii itafanya upate matibabu mapema na hivyo kuzuia ugonjwa usiendelee au kuzuia madhara zaidi yasitokee.
2.Daktari au mhudumu wa afya atakuelezea ni mambo gani ya kuzingatia wakati wa ujauzito ikiwemo lishe, madawa ya kuepuka na vitu vingine hatarishi wakati wa ujauzito.
3.Utapata nafasi ya kuuliza mambo mbalimbali yanayohusu ujauzito na kupata ufafanuzi kutoka kwa mtaalamu wa afya.
4.Kupata chanjo mbalimbali ikiwemo chanjo za tetenasi
5. Utapewa Folic acid ili kupunguza hatari ya kuzaa mtoto mwenye mgongo wazi.
6.Utafanyiwa uchunguzi na kutibiwa magonjwa ya zinaa k**a utakutwa nayo.singano_afya

Address


Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when dr.singano_afya posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to dr.singano_afya:

Shortcuts

  • Address
  • Alerts
  • Contact The Practice
  • Claim ownership or report listing
  • Want your practice to be the top-listed Clinic?

Share