Wema Herbal Clinic

Wema Herbal Clinic Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Wema Herbal Clinic, Medical and health, Mwanza.

HUDUMA BORA ZA TIBA, LISHE NA USHAURI. || Meditation & Spirituality. || Tunatuma Popote nchini kwa Uaminifu.|| Tupo Mwanza - Tanzania.

25/09/2025

This Mimosa, immune booster

25/09/2025

What nature provides

Snake plant.Ni mmea wenye faida nyingi uwapo mazingira yako, unafahamu mojawapo ya matumizi yake?Kiroho, huzui na kukuki...
24/09/2025

Snake plant.

Ni mmea wenye faida nyingi uwapo mazingira yako, unafahamu mojawapo ya matumizi yake?

Kiroho, huzui na kukukinga dhidi ya nishati mbaya, lupi unalifahamu upande wako?

UCHAFU UKENI (Vaginal Discharge)Kutoka uchafu ukeni ni hali ya kawaida, ingawa kuna uchafu unaotoka ambao unaashiria uwe...
24/09/2025

UCHAFU UKENI (Vaginal Discharge)

Kutoka uchafu ukeni ni hali ya kawaida, ingawa kuna uchafu unaotoka ambao unaashiria uwepo wa maambukizi, hasa pale unapotoka mwingi kupita kiasi, wenye rangi ya njano au kijani na ukiwa na harufu isiyo ya kawaida, mfano harufu kali, au harufu k**a ya samaki.

Uke wa mwanamke hufanya kazi ya kutoa njia kati ya sehemu ya nje ya mwili na viungo vya uzazi vya ndani vya mwanamke.

Hali ya kawaida ya majimaji yaliyomo katika uke wa mwanamke huwa ni ya tindikali ili kuzuia maambukizi ya vijidudu wa kuleta maradhi.

Hali hii ya utindikali huletwa na bacteria waishio katika uke wa mwanamke.

Bacteria hawa ni wa kawaida na hawana madhara kwa mwili.

Uke ulio katika hali nzuri hutoa majimaji haya ili kujisafisha.

Majimaji haya yanayotengenezwa katika uke na kwenye eneo la cervix hufanya kazi ya kuondoa seli zilizokufa na bacteria waharibifu nje ya mwili na huu ndio uchafu wa kawaida ambao mwanamke hutoa ukeni.

Kutoa uchafu huu sehemu za siri ni njia ya kuusafisha uke na kuzuia maambukizi ya magonjwa.

Kitu cho chote ambacho kitaharibu uwiano wa utengeneaji wa majimaji haya ndani ya uke kinaweza kujenga mazingira ya maambukizi katika uke.

Kila mwanamke anapaswa kujichunguza kila siku ya maisha yake maeneo yake ya uzazi na matiti, vile vile kuichunguza nguo ya ndani aliyokuwa ameivaa siku hiyo k**a kuna uchafu wowote.

Kufanya hivi kunaweza kumsaidia kugundua kuwa ana tatizo la kiafya, kwani wapo baadhi ambao hawafahamu kuwa kila siku huwapo ute ute unaomtoka ambao ni hali ya kawaida.

Ute huo unaweza kuwa na ujazo wa nusu kijiko cha chai na huwa na harufu asilia ya uke na huwa na rangi nyeupe au kahawia mpauko k**a chai isiyokolea rangi bila kuwa na harufu mbaya.

Utokaji wa ute huo ni mojawapo ya njia ya uke kujisafisha kwa kutiririka pamoja na mabaki ya hedhi au takataka za mwili au zilizotoka nje ya mwili.

Ute huu huzalishwa na kuta za nyumba ya uzazi na huzifanya tezi za ukeni kushuka chini kutokana na kani ya nguvu za uvutano (gravity).

Uchafu wa kawaida ukeni (Normal vaginal discharge)

Wanawake wote hutoa uchafu ukeni, Kiwango cha uchafu unaotoka, rangi yake na harufu yake vitabalikabadilika kutoka kipindi kimoja hadi kingine kulingana na muda mwanamke aliopo katika mzunguko wake wa mwezi.

Uchafu huu utabadilika vilevile k**a ananyonyesha, atakuwa na hisia za kufanya mapenzi, atakuwa na mabadiliko ya lishe, anatumia madawa hasa ya mpango wa uzazi au atakuwa na ujauzito.

Kwa kawaida uchafu huu huwa usio na rangi, wenye rangi yenye weupe wa mawingu au njanonjano pale unapokaukia kwenye nguo. Unaweza kuwa na vijipande vidogovidogo na mara nyingine ukawa wa kunatanata.

Clear and watery

Uchafu usio na rangi huu ni wa kawaida, Hutokea muda wowote katika mwezi, unaweza kuwa mwingi baada ya kumaliza kufanya mazoezi.

Clear and stretchy

Wakati uchafu usio na rangi lakini unaovutika na kunatanata, mzito kidogo unapotoka, huashiria uchevushwaji (Ovulating). Huu huwa ni uchafu wa kawaida.

Uchafu wa Ukeni usio wa kawaida (Abnormal vaginal discharge).

Ishara Na Dalili za uchafu wa Ukeni usio wa kawaida.

Ukiona yafuatayo, ujue unaweza kuwa na tatizo la maambukizi ya vijijidudu vya maradhi katika uke wako:

🖋️Kutokwa na uchafu ukeni kunakoambatana na kuwashwa au vijipele.
🖋️Kutokwa na uchafu ukeni ambako ni endelevu na kwa kiwango kinachozidi kila siku.
🖋️Kusikia maumivu wakati wa kutoa haja ndogo.
🖋️Kutokwa na uchafu mweupe, mzito k**a jibini.
🖋️Uchafu wa kijivu/mweupe au njano/kijani unaotoa harufu mbaya.

MUHIMU;

TUNAFANYA KAZI KUPITIA ONLINE, HIVYO UAMINIFU NI KIPAUMBELE CHETU KIKUBWA, HATUNA MAWAKALA POPOTE, ILA TUNATUMA POPOTE KWA UHAKIKA NA UAMINIFU MKUBWA.

Kwa tiba zisizo na kemikali kwa maambukizi ukeni, wasiliana nasi kwa;

0769247626.

19/09/2025

Available, mkaa wa packet maalumu kwa kuchomea dawa au mafusho au udi!

14/09/2025

Do you know how to use this out of smoking?

14/09/2025

Mkaa wa pakiti, maalumu kwa kuchomea dawa pamoja na udi.

0769247626

14/09/2025

Nature lovers, join here.

14/09/2025

Shule ya wapi hii? 😳, mazingira haya si rafiki kabisa.

14/09/2025

SABABU ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME.Ogani za uzazi za mwanaume ni hatua tatanisha inayohusisha ubongo, homoni, hisia, n...
13/09/2025

SABABU ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME.

Ogani za uzazi za mwanaume ni hatua tatanisha inayohusisha ubongo, homoni, hisia, neva, misuli na misuli ya damu.

Kushindwa kusimamisha uume inaweza kuwa ni matokea ya tatizo lililopelekewa na vyanzo hivi, Msongo wa mawazo na matatizo mengine ya afya ya akili ambayo yanaweza kusababisha uwezo wa kusimamisha uume kupungua na kushindwa kufanya kazi vizuri.

Wakati mwingine muunganiko sababu za kimwili na kisaikolojia zinaweza kusababibisha uwezo wa kusimamisha uume kupungua, kwa mfano uwepo wa baadhi ya matatizo ya kimwili unaweza kusababisha uwezo wa kushiriki uwezo wa kushiriki tendo la ndoa kupungua ama kushindwa kabisa uume kusimama.

Sababu za kimwili zinazosabisha kushindwa kusimamisha uume (Physical causes of erectile dysfunction)

Baadhi ya sababu za kimwili zinazopelekea kupungua kwa nguvu za kiume ni pamoja na;

Ugonwa wa moyo (Heart disease).

Kwa kuwa ili uume usimame vizuri unahitaji damu iingie kwenye mishipa na misuli kwa wingi, sasa ikiwa utakuwa na ugonjwa wa moyo mzunguko wa damu katika mishipa na misuli hbauwi katika mpangilio mzuri sana hivyo kuwa chanzo cha uume kusimama kwa ulegevu au kushindwa kusimama kabisa.

Kusinyaa na kutanuka kwa misuli ya damu (atherosclerosis).

Mafuta ya ziada (High cholesterol).
Uwepo wa mafuta ndani ya mishipa ya damu hupunguza upenyo, wingi au mwendo wa damu inayotakiwa ipite kwenye mishipa.
Presha ya kupanda (High blood pressure),
Kisukari (Diabetes).
Unene (Obesity).

Metabolic syndrome — hali inayohusisha presha, kiwango cha juu cha insulin, uzito wa mwili na kiasi cha juu cha mafuta mwilini.

-Matumizi ya tumbaku (To***co use),
-Peyronie's disease,
-Uwepo wa tishu za kovu ndani ya uume.
-Tatizo la usingizi (Sleep disorders),
-Tiba ya kansa ya tezi dume au kuvimba kwa tezi za uzazi,
-Upasuaji eneo la kinena au Athari za ajali kwenye eneo la kinena au uti wa mgongo.
-Kiwango kidogo cha homoni ya Testosterone (Low testosterone),
-Punyeto, kutokana na kuchua mara kwa mara uume tena kwa kutumia mikono ambayo ni kitu kigumu hufanya mishipa ya damu kuwa dhaifu hivyo kupelekea hata mzunguko wa damu kuwa hafifu.

Pia unapokuwa unafanya mapenzi uume ukiingia ukeni na kuhisi joto la uke hupelekea kuwa kumwaga shahawa mapema sana, muda mwingine na kushindwa kusimama tena, au ladha ya uume kuingia ukeni hupotea hivyo kushindwa kuhisi raha wakati wa kujamiiana.

Sababu za kisaikolojia za kushindwa kusimamisha uume (Psychological causes of erectile dysfunction)

Ubongo ndio unaochukua sehemu kubwa kupangilia matendo yote ya mwili yakiwemo na yanayosabisha kusimama kwa uume, huanza na hisia ya hamasa ya kujamiiana. Vitu vingi vinavyoingilia hisia za mapenzi na kuweza kupunguza au kupoteza uwezo wa kusimamisha uume kabisa ni;
Msongo wa mawazo (Stress)
Matatizo ya mahusiano k**a vile migogoro kutokana na mawasiliano hafifu au vyanzo vingine.

Vihatarishi (Risk factors)

-Umri unavyozidi na uwezo wa kusimama kwa uume hupungua, unahitajji zaidi kushika uume moja kwa moja ili uweze kusimama,Baadhii ya sababu zinazo chochea kushindwa kusimamisha uume ni pamoja na:

-Matumizi ya Dawa. Dawa za kisukari au moyo,
Matumizi ya tumbaku (To***co use), ambayo huvuruga mzunguko wa damu kwenye mishipa ya ateri na vena inaweza kuzidi na kupelekea maradhi sugu hali itakayo sababisha kushindwa kusimamisha uume.

-Uzito mkubwa hasa pale unapokuwa mnene zaidi kupita kiasi, na uzito mkubwa husababisha ongezeko la mafuta ya ziada ndani ya mwili yaani (cholestrol).

-Baadhi ya matibabu k**a vile upasasuaji wa tezi au tiba ya mionzi ya kansa.
-Ajali (Injuries), inapotokea na kuharibu neva au ateri ambazo huwezesha uume kusimama.
-Madawa hasa antidepressants, antihistamines na dawa za kutibu presha ya juu au maumivu ya tezi dume.
-Matatizo ya kisaikolojia k**a vile msongo wa mawazo (stress), wasiwasi ( anxiety) au sonona (depression)
-Utumiaji wa dawa za kulevya pamoja na ulevi wa kupindukia au vinywaji vikali hasa kwa kipindi cha muda mrefu (Drug and alcohol).

Kwa matibabu na ushauri.
Wasiliana nasi kwa namba 0769247626.

NGUVU ZA KIUME.Upungufu wa nguvu za kiume (Erectile dysfunction /impotence), Ni ukosefu wa uwezo wa kufanya na kuhimili ...
13/09/2025

NGUVU ZA KIUME.

Upungufu wa nguvu za kiume (Erectile dysfunction /impotence),

Ni ukosefu wa uwezo wa kufanya na kuhimili kikamilifu tendo la ndoa,

Hali hii hupelekea mwanaume kudumu kwa muda mfupi sana au chini ya dakika moja kwenye kkufanya mapenzi na kujikuta anamwaga shahawa mapema sana, baada ya kumwaga shahawa hizo kuna muda uume hushindwa kusimama tena, Kukosa uwezo wa kusimamisha uume mara kwa mara si jambo la kufurahisha.

Kuendelea kwa tatizo hili, linaweza kusababisha Msongo wa mawazo, kukosa ladha ya kufanya mapenzi kwa mwanaume na mwanamke. Matokeo ya kushindwa kujiamini wewe mwenyewe ambayo inaweza kuepelekea kuwa na hasira na kisirani, na kupelekea migogoro kwenye mahusiano.

Uume kushindwa kusimama inaweza kuwa ni dalili ya tatizo la kiafya linalohitaji matibabu, mojawapo ya matatizo hayo inaweza kuwa ni sababu ya ugonjwa wa moyo, kisukari, madonda ya tumbo n.k

Endapo umeona tatizo la kushindwa kusimamisha uume, muone daktari hata k**a limekuvuruga, wakati mwingine kuongea nae inatosha kukurudisha hali ya uwezo wa kusimamisha.

Kwa upande mwingine dawa au maelekezo mengine ya kitaalamu yanaweza kuhusika katika kutatua changamoto hiyo.

Kumekuwepo na wimbi kubwa la watoa dawa au matumizi holela ya dawa za kuongeza nguvu za kiume, wengi hutumia dawa hizo pasipokujua wala kuchunguza nini chanzo kilichopelekea tatizo hilo.

Epuka matumizi holela ya dawa za kuongeza nguvu za kiume bila kujua chanzo cha tatizo hilo, badala ya kutibu tatizo unaweza kujikuta unaongeza tatizo na kuleta madhara mengine mabaya ya kiafya.

Viashiria na Dalili (Signs and Symptoms)
Dalili za upungufu wa nguvu za kiume zinaweza kuwa ni pamoja na;

Kushindwa kusimamisha uume (Trouble getting an er****on),
Uume kushindwa kuendelea kusimama (Trouble keeping an er****on),
Kukosa hamu ya mapenzi (Reduced sexual desire).

Muone daktari

Kumuona daktari ni jambo la msingi sana kuanza nalo unapokuwa na tatizo la kushindwa kusimamisha. Muone daktari k**a ;
Uume unasinya na kushindwa kusimama tena, Unawahi kumwaga shahawa au unachelewa sana kumwaga.
Una kisukari, ugonjwa wa moyo au magonjwa mengine yanayoweza kupelekea uume kushindwa kusimama.
Endapo una dalili ya muda mrefu ya uume kushindwa kusimama.

Vyakula vya kuongeza hamu ya Mapenzi

Tafiti zinaonesha kuwa kuna uhusiano mkubwa kati ya vyakula tunavyokula na afya ya viungo vya uzazi.

Baadhi ya vyakula na virutubishi vimehusishwa na hamu ya kufanya mapenzi (nyege).

Virutubishi ndani ya chakula ambavyo vinasaidia hali hiyo ni antioxidants, vitamin C, vitamin E, potassium na zinc.

GKirutubishi cha zinc ambacho hupatikana ndani ya vitunguu swaumu, mbegu za maboga, ufuta na mbegu za matikitimaji, Tikitimaji lina phytonutrient citrulline ambayo hugeuzwa kuwa arginine.

Arginine ni amino acid ambayo hufanya mishipa ya damu kuwa kwenye hali ya ubora wake na kusadia damu kupita vizuri zaidi.

Tikitimaji kwa hiyo husaidia damu ifike kwa kiwango kizuri zaidi kwenye sehemu ambazo hutakiwa kutanuka wakati mtu akipata hisia za kufanya tendo la ndoa ambazo ni viungo vya ndani ya kisimi cha mwanamke na ndani ya uume wa mwanaume, kinaongeza mbegu kwa mwanaume (s***m count) hivyo humsaidia kuongeza hamu ya kufanya tendo la ndoa.

Chakula cho chote chenye virutubishi hivi kikiliwa, humfanya mlaji asikie hamu ya kufanya mapenzi au kwa maneno ya mtaani, chakula hiki kinasaidia kuongeza nyege, Strawberries– matunda haya yana antioxidants kwa kusaidia afya ya moyo na mishipa ya damu (arteri) na vitamin C ambayo huongeza kiwango cha mbegu kwa mwanaume.

Parachichi kuna vitamini E ambayo ni antioxidant.

Ndani ya tunda hili kuna potassium na vitamini B6 ambavyo huboresha afya ya moyo na kusaidia mzunguko wa damu kuwa mzuri hivyo kusaidia damu kufika vizuri maneo ya via vya uzazi na kuchochea hamasa ya kufanya mapenzi.

Kingine katika kundi hili ni broccoli, karafuu, majani ya mlonge, mdalasini, mayai na tangawizi. Viazi vitamu, vina potassium ambayo husaidia kuondoa tatizo la presha ya juu (high-blood pressure)

Ufumbuzi wa Tatizo hili.

Itaendelea.......

MUHIMU;

TUNAFANYA KAZI KUPITIA ONLINE, HIVYO UAMINIFU NI KIPAUMBELE CHETU KIKUBWA, HATUNA MAWAKALA POPOTE, ILA TUNATUMA POPOTE KWA UHAKIKA NA UAMINIFU MKUBWA.

Wasiliana nasi kwa namba 0769247626.

Address

Mwanza
10901090

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00

Telephone

+255769247626

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wema Herbal Clinic posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram