10/01/2026
KUTOKWA UCHAFU UKENI WA RANGI ISIYO KAWAIDA (Vaginal Discharge)
Kutoka uchafu ukeni ni hali ya kawaida, ingawa kuna uchafu unaotoka ambao unaashiria uwepo wa maambukizi, hasa pale unapotoka mwingi kupita kiasi, wenye rangi ya njano au kijani na ukiwa na harufu isiyo ya kawaida, mfano harufu kali, au harufu k**a ya samaki.
Uke wa mwanamke hufanya kazi ya kutoa njia kati ya sehemu ya nje ya mwili na viungo vya uzazi vya ndani vya mwanamke.
Hali ya kawaida ya majimaji yaliyomo katika uke wa mwanamke huwa ni ya tindikali ili kuzuia maambukizi ya vijidudu wa kuleta maradhi. Hali hii ya utindikali huletwa na bacteria waishio katika uke wa mwanamke. Bacteria hawa ni wa kawaida na hawana madhara kwa mwili.
Uke ulio katika hali nzuri hutoa majimaji haya ili kujisafisha. Majimaji haya yanayotengenezwa katika uke na kwenye eneo la cervix hufanya kazi ya kuondoa seli zilizokufa na bacteria waharibifu nje ya mwili na huu ndio uchafu wa kawaida ambao mwanamke hutoa ukeni.
Kutoa uchafu huu sehemu za siri ni njia ya kuusafisha uke na kuzuia maambukizi ya magonjwa. Kitu cho chote ambacho kitaharibu uwiano wa utengeneaji wa majimaji haya ndani ya uke kinaweza kujenga mazingira ya maambukizi katika uke.
Kila mwanamke anapaswa kujichunguza kila siku ya maisha yake maeneo yake ya uzazi na matiti, vile vile kuichunguza nguo ya ndani aliyokuwa ameivaa siku hiyo k**a kuna uchafu wowote.
Kufanya hivi kunaweza kumsaidia kugundua kuwa ana tatizo la kiafya, kwani wapo baadhi ambao hawafahamu kuwa kila siku huwapo ute ute unaomtoka ambao ni hali ya kawaida.
Ute huo unaweza kuwa na ujazo wa nusu kijiko cha chai na huwa na harufu asilia ya uke na huwa na rangi nyeupe au kahawia mpauko k**a chai isiyokolea rangi bila kuwa na harufu mbaya.
Utokaji wa ute huo ni mojawapo ya njia ya uke kujisafisha kwa kutiririka pamoja na mabaki ya hedhi au takataka za mwili au zilizotoka nje ya mwili. Ute huu huzalishwa na kuta za nyumba ya uzazi na huzifanya tezi za ukeni kushuka chini kutokana na kani ya nguvu za uvutano (gravity).
Uchafu wa kawaida ukeni (Normal va**nal discharge)
Wanawake wote hutoa uchafu ukeni, Kiwango cha uchafu unaotoka, rangi yake na harufu yake vitabalikabadilika kutoka kipindi kimoja hadi kingine kulingana na muda mwanamke aliopo katika mzunguko wake wa mwezi.
Uchafu huu utabadilika vilevile k**a ananyonyesha, atakuwa na hisia za kufanya mapenzi, atakuwa na mabadiliko ya lishe, anatumia madawa hasa ya mpango wa uzazi au atakuwa na ujauzito.
Kwa kawaida uchafu huu huwa usio na rangi, wenye rangi yenye weupe wa mawingu au njanonjano pale unapokaukia kwenye nguo.
Unaweza kuwa na vijipande vidogovidogo na mara nyingine ukawa wa kunatanata.
Clear and watery
Uchafu usio na rangi huu ni wa kawaida, Hutokea muda wowote katika mwezi, unaweza kuwa mwingi baada ya kumaliza kufanya mazoezi.
Clear and stretchy
Wakati uchafu usio na rangi lakini unaovutika na kunatanata, mzito kidogo unapotoka, huashiria uchevushwaji (Ovulating). Huu huwa ni uchafu wa kawaida.
Uchafu wa Ukeni usio wa kawaida (Abnormal va**nal discharge).
Ishara Na Dalili za uchafu wa Ukeni usio wa kawaida.
Mabadiliko ya uwingi wa uchafu unaotoka au katika rangi ya uchafu unaotoka ni dalili ya maambukizi ya magonjwa katika uke.
Maambukizi katika uke ni tatizo la kawaida kwa wanawake na wanawake wengi wameshapata tatizo la maambukizi angalau mara moja katika maisha yao.
Ukiona yafuatayo, ujue unaweza kuwa na tatizo la maambukizi ya vijijidudu vya maradhi katika uke wako:
🖋️Kutokwa na uchafu ukeni kunakoambatana na kuwashwa au vijipele.
🖋️Kutokwa na uchafu ukeni ambako ni endelevu na kwa kiwango kinachozidi kila siku.
🖋️Kusikia maumivu wakati wa kutoa haja ndogo.
🖋️Kutokwa na uchafu mweupe, mzito k**a jibini.
🖋️Uchafu wa kijivu/mweupe au njano/kijani unaotoa harufu mbaya.
Aina za uchafu wa ukeni usio wa kawaida (Abnormal va**nal Discharge).
Aina nyingine za uchafu huwa ni za kawaida, Na nyingine zinaashiria hali zisizo nzuri zinazohitaji matibabu.
1. Uchafu Mweupe (White discharge).
Kutoka uchafu mweupe, hasa mwanzoni au mwishoni mwa mzunguko wa hedhi, ni kawaida. Ingawa, k**a itaambatana na miwasho na uchafu Mweupe Mzito K**a Jibini, sio kawaida inahitaji matibabu.
Aina hii ya uchafu inaweza kuwa ni dalili ya maambukizi ya Yeast infection na dalili nyingine ni kuvimba na maumivu kwenye mashavu ya uke (v***a), kuwashwa na maumivu wakati wa kufanya tendo la ndoa.
2. Uchafu wa kahawia au wenye damu (Brown or bloody discharge).
Uchafu wa kahawia au uliochanganyika na damu mara nyingi huwa ni kawaida, hasa inapotokea kipindi cha hedhi au baada ya mzunguko wa hedhi.
Uchafu utakaotoka mwishoni mwa mzunguko wako wa siku unaweza kuonekana wa kahawia au uliochanganyikana na damu, unaweza kuwa unapata kiasi kidogo cha uchafu wenye damu katikati ya mzunguko wa hedhi. Hii hujulikana k**a spotting.
K**a spotting ikitokea wakati wa kawaida wa mzunguko wa hedhi na ikiwa ulifanya mapenzi pasipo kutumia kinga, hii inaweza kuwa dalili ya ujauzito, Na Spotting kipindi kabisa cha mimba changa inaweza kuwa dalili ya mimba kuharibika (miscarriage), ni vema ukaongea na daktari.
Katika hali isiyo ya kawaida, uchafu wa kahawia au uliochanganyikana na damu inaweza kuwa ni dalili ya Maambukizi katika tabaka la ndani la kizazi (Endometrial) au kansa ya shingo ya kizazi (cervical cancer).
Inaweza kuwa matatizo mengine k**a vile uvimbe (fibroids) au hali nyingine zisizo za kawaida. Ndio maana ni muhimu kufanya uchunguzi kila mwaka wa afya ya uzazi (Pelvic exam and Pap smear).
Daktari wako atchunguza k**a kkuna ukuaji usio wa kawaida katika fupanyonga (cervical abnormalities). Mwanamke mwenye tatizo hili atatoa damu nyingi ukeni na kuumwa nyonga.
3. Uchafu wa njano au kijani (Yellow or green discharge).
Uchafu wenye rangi ya kijani au njano, ikiwa uchafu utatoka k**a mapovu, unaombatana na harufu mbaya, sio kawaida, aina hii ya uchafu dalili ya Trichomoniasis, Maambukizi yatokanayo na ngono isiyo salama. Dalili nyingine ni maumivu na kuwashwa wakati wa kukojoa.
4. Uchafu wa rangi ya mawingu au njano (Cloudly or yellow discharge).
Hii ni dalili ya ugonjwa wa kisonono (Gonorrhea). Mwanamke atatokwa na damu katikati ya siku zake, atatokwa na mkojo bila kukusudia na kupata maumivu ya nyonga.
Uchafu mweupe, wa njano au kijivu wenye harufu ya samaki
Kutokwa na uchafu mweupe au wa kijivu ulio k**a maziwa ya mgando ukeni ni tatizo la kiafya, ni dalili mojawapo ya ugonjwa wa fangasi za ukeni kitabibu hujulikana k**a 'Vaginal Candidiasis'.
Sababu ya uchafu wa aina hii ni Bacterial vaginosis chanzo cha maambuzi ya bacteria hawa hakijulikani, kinachotokea ni ongezeko la kutoka kwa uchafu mweupe, njano au kijivu na wenye harufu k**a ya samaki, ingawa kwa upande mwingine haioneshi dalili,
Wanawake wanaofanya ngono kwa mdomo au wenye wapenzi wengi wako kwenye hatari kubwa ya kupata maambukizi haya.
Uchafu wa aina hii ni dalili za maabukizi ya Bacterial Vaginosis. Mwanamke mwenye tatizo hili atasikia miwasho au maumivu, kuvimba kwa uke au sehemu ya nje ya uke (v***a).
Aina ya Maambukizi ya ukeni.
Baadhi ya maambukizi hayo ni pamoja na Bacterial Vaginosis, Trichomoniasis na Monilia (Yeast) Infection.
Bacterial Vaginosis.
Chanzo halisi cha ugonjwa huu hakifahamiki. Kinachotokea ni kuongezeka kwa ghafla kwa idadi ya bacteria hawa ambao ni kawaida kupatikana kwenye uke na kubadilisha uwiano wao kwenye mazingira ya uke.
Wanawake wenye wapenzi wengi au wanaofanya mapenzi kupitia midomo wanakuwa kwenye hatari kubwa zaidi ya kupata maambukizi ya Bacterial Vaginosis.
Dalili za Bacterial Vaginosis.
Kuongezeka kwa uchafu unaotoka ukeni
Kutokwa na uchafu wa kijivu/mweupe, mwepesi au wa majimaji
Harufu k**a ya samaki ikiambatana na uchafu
Harufu inayozidi au uchafu unaozidi mara baada ya kufanya tendo la ndoa,
Tiba kwa tatizo la bacterial vaginosis zipo za aina mbili. Tiba ya aina ya kwanza ni kutumia metronidazole (Flagyl) na tiba ya pili ni kutumia antibiotic ya vidonge au ya cream.
Trichomonas Vaginalis – (TV).
Hiki nacho ni kijidudu cha bacteria, kidogo kinachoambukiza kupitia ukeni na kwenye mrija wa kupitishia mkojo. Ugonjwa wa Trichomoniasis unasababishwa na vimelea vya jamii ya protozoa vinavyojulikana kitalaamu k**a Trichomonas va**nalis.
Ugonjwa huu huathiri mrija wa kupitisha mkojo (urethra) na tupu ya mwanamke (va**na).
Huathiri sana wanawake kuliko wanaume na wanawake wenye umri mkubwa wako katika hatari zaidi kuliko mabinti wadogo. Hupatikana kwa njia ya kujamiana bila kutumia kinga na mtu aliyeathirika na Trichomoniasis.
Ishara na dalili (Signs and symptoms).
Dalili za Trichomoniasis, huanza kuonekana kuanzia siku ya 4 mpaka ya 28 baada ya mtu kupata maambukizi, Wanaume huwa hawaonyeshi dalili zozote lakini baadhi wanaonyesha dalili k**a;
Dalili kwa mwanamke aliyeambukizwa ni;
🖋️Kutokwa na uchafu wa rangi ya njano/kijani ulio k**a mapovu huenda ukawa na harufu k**a ya samaki .
🖋️Harufu mbaya inayoambatana na kutokwa na uchafu,
🖋️Kuongezeka kwa uwingi wa uchafu wa ukeni.
🖋️Maumivu ya ukeni au sehemu za nje ya uke (v***a).
🖋️Kujisaidia haja ndogo mara nyingi zaidi.
Kuwashwa sehemu za siri.
Maambukizi haya hutokana na aina ya protozoa wa seli moja. Trichomoniasis maranyingi huambukizwa kwa kufanya ngono.
Protozoa huyu huweza kukaa kwenye mazingira ya unyevunyevu kwa muda wa saa 24 bila kufa hivyo kufanya taulo na nguo nyingine za kuogea kuwa chanzo kingine kikuu cha maambukizi.
Matibabu;
Ugonjwa huu unaweza kutibiwa kwa urahisi, kwa madawa maalam ya kupambana na viini antibiotics metronidazole. Ili kuepuka kuambukizwa upya, na kusambaa zaidi kwa ugonjwa huu inabidi mpenzio pia naye atibiwe.
Monilia (Yeast) Infection.
Kwa kawaida kuna kiwango kidogo cha yeast (Candida albicans) katik uke.
Tunasema kuna maambukizi ya yeast pale kiwango chao kinapozidi hali ambayo inatokana na kubadilika kwa hali ya ukeni (change in the pH balance of the va**na).
Maambukizi ya yeast hayatokani na tendo la ngono. Kuna mambo ambayo yanaweza kusababisha kuongezeka kwa yeast katika uke, nayo ni; msongo wa mawazo, matumizi ya dawa za kuziua mimba, kisukari, ujauzito na matumizi ya antibotics.
Dalili za Monilia (Yeast) Infection.
🖋️Ongezeko la uchafu unaotoka ukeni.
🖋️Uchafu mweupe unaotoka katika vifungu vidogo k**a vya jibini.
🖋️Kuwashwa na mauvivu ya ukeni au sehemu za nje (v***a).
Tiba ya Monilia (Yeast) Infection inalenga kuzuia mwongezeko wa yeast katika uke na kuwarudisha kwenye kiwango kinachofaa na si kuwaondoa. Tiba ni kutumia vidonge vya antifungal na cream za kupaka ukeni, Kuna dawa nyingi za kuweza kuondoa tatizo hili.
Cytolytic Vaginosis.
Hii ni hali inayojitokeza pale kunapotokea kuongeka kwa bakteria aitwaye Lactobacillus acidophilus kwenye uke.
Lactobacilli ni bakteria wazuri wanaoishi ukeni bila kuleta matatizo ya aina yo yote. Kwa kawaida uwepo wa bakteria hawa unasaidia sana katika kupambana na wadudu aina nyingine wenye madhara kwa mwili – huongeza kinga ya mwili .
Lakini endapo mazingira dhalili ya uke yatabadilika, bakteria hawa wazuri wanaweza kuzalina kupita kiwango kinachotakiwa.
Hii inaweza kutokea, kwa mfano, kunapotokea matumizi ya mara kwa mara ya antibiotics au dawa za kuzuia na kuua fungus.
Ni tatizo ambalo linalowapata zaidi wanawake walio katika umri wa kuzaa – miaka 25 – 40 – kwa sababu ya uwepo wa homoni ya estrogen.
Dalili za cytolytic vaginosis
Kutoka uchafu kwa wingi wenye rangi nyeupe, wa maji maji au mzito k**a maziwa ya mgando
Miwasho ya sehemu za ndani au nje ya uke
Maumivu wakati wa kutoa haja ndogo
Maumivu wakati wa kufanya tendo la ndoa
Dalili za tatizo hili ni rahisi sana kuzichanganya na zile za matatizo mengine ya hapo juu na hasa va**nal candidiasis (monilia).
Tatizo hili halina tiba bali kufanya yafuatayo:
-Kuacha kutumia antibiotics au dawa za fungus
- Kuacha kutumia sabuni ukeni na kutumia maji ya uvuguvugu tu.
-Kutovaa nguo za ndani usiku.
-Kutofanya tendo la ndoa.
-Kupunguza kiwango cha sukari katika mlo.
-Kujiosha mara kwa mara ukeni kwa kutumia baking soda.
Unaweza vile vile kuchanganya baking soda na maji ukatengeneza namna ya uji na kuuweka kwenye pedi.
MUHIMU;
TUNAFANYA KAZI KUPITIA ONLINE, HIVYO UAMINIFU NI KIPAUMBELE CHETU KIKUBWA, HATUNA MAWAKALA POPOTE, ILA TUNATUMA POPOTE KWA UHAKIKA NA UAMINIFU MKUBWA.
Kwa tiba zisizo na kemikali kwa maambukizi ukeni, wasiliana nasi kwa;
0769247626.