Wema Herbal Clinic

Wema Herbal Clinic HUDUMA ZA MATIBABU, LISHE & USHAURI NASAHA🥣 || Afya ya Uzazi kwa jinsia zote ||
Meditation 🧘‍♂️ ||

+255 769 247 626

KUTOKWA UCHAFU UKENI WA RANGI ISIYO KAWAIDA (Vaginal Discharge)Kutoka uchafu ukeni ni hali ya kawaida, ingawa kuna uchaf...
10/01/2026

KUTOKWA UCHAFU UKENI WA RANGI ISIYO KAWAIDA (Vaginal Discharge)

Kutoka uchafu ukeni ni hali ya kawaida, ingawa kuna uchafu unaotoka ambao unaashiria uwepo wa maambukizi, hasa pale unapotoka mwingi kupita kiasi, wenye rangi ya njano au kijani na ukiwa na harufu isiyo ya kawaida, mfano harufu kali, au harufu k**a ya samaki.

Uke wa mwanamke hufanya kazi ya kutoa njia kati ya sehemu ya nje ya mwili na viungo vya uzazi vya ndani vya mwanamke.

Hali ya kawaida ya majimaji yaliyomo katika uke wa mwanamke huwa ni ya tindikali ili kuzuia maambukizi ya vijidudu wa kuleta maradhi. Hali hii ya utindikali huletwa na bacteria waishio katika uke wa mwanamke. Bacteria hawa ni wa kawaida na hawana madhara kwa mwili.

Uke ulio katika hali nzuri hutoa majimaji haya ili kujisafisha. Majimaji haya yanayotengenezwa katika uke na kwenye eneo la cervix hufanya kazi ya kuondoa seli zilizokufa na bacteria waharibifu nje ya mwili na huu ndio uchafu wa kawaida ambao mwanamke hutoa ukeni.

Kutoa uchafu huu sehemu za siri ni njia ya kuusafisha uke na kuzuia maambukizi ya magonjwa. Kitu cho chote ambacho kitaharibu uwiano wa utengeneaji wa majimaji haya ndani ya uke kinaweza kujenga mazingira ya maambukizi katika uke.

Kila mwanamke anapaswa kujichunguza kila siku ya maisha yake maeneo yake ya uzazi na matiti, vile vile kuichunguza nguo ya ndani aliyokuwa ameivaa siku hiyo k**a kuna uchafu wowote.

Kufanya hivi kunaweza kumsaidia kugundua kuwa ana tatizo la kiafya, kwani wapo baadhi ambao hawafahamu kuwa kila siku huwapo ute ute unaomtoka ambao ni hali ya kawaida.

Ute huo unaweza kuwa na ujazo wa nusu kijiko cha chai na huwa na harufu asilia ya uke na huwa na rangi nyeupe au kahawia mpauko k**a chai isiyokolea rangi bila kuwa na harufu mbaya.

Utokaji wa ute huo ni mojawapo ya njia ya uke kujisafisha kwa kutiririka pamoja na mabaki ya hedhi au takataka za mwili au zilizotoka nje ya mwili. Ute huu huzalishwa na kuta za nyumba ya uzazi na huzifanya tezi za ukeni kushuka chini kutokana na kani ya nguvu za uvutano (gravity).

Uchafu wa kawaida ukeni (Normal va**nal discharge)

Wanawake wote hutoa uchafu ukeni, Kiwango cha uchafu unaotoka, rangi yake na harufu yake vitabalikabadilika kutoka kipindi kimoja hadi kingine kulingana na muda mwanamke aliopo katika mzunguko wake wa mwezi.

Uchafu huu utabadilika vilevile k**a ananyonyesha, atakuwa na hisia za kufanya mapenzi, atakuwa na mabadiliko ya lishe, anatumia madawa hasa ya mpango wa uzazi au atakuwa na ujauzito.

Kwa kawaida uchafu huu huwa usio na rangi, wenye rangi yenye weupe wa mawingu au njanonjano pale unapokaukia kwenye nguo.

Unaweza kuwa na vijipande vidogovidogo na mara nyingine ukawa wa kunatanata.

Clear and watery
Uchafu usio na rangi huu ni wa kawaida, Hutokea muda wowote katika mwezi, unaweza kuwa mwingi baada ya kumaliza kufanya mazoezi.

Clear and stretchy
Wakati uchafu usio na rangi lakini unaovutika na kunatanata, mzito kidogo unapotoka, huashiria uchevushwaji (Ovulating). Huu huwa ni uchafu wa kawaida.

Uchafu wa Ukeni usio wa kawaida (Abnormal va**nal discharge).

Ishara Na Dalili za uchafu wa Ukeni usio wa kawaida.

Mabadiliko ya uwingi wa uchafu unaotoka au katika rangi ya uchafu unaotoka ni dalili ya maambukizi ya magonjwa katika uke.

Maambukizi katika uke ni tatizo la kawaida kwa wanawake na wanawake wengi wameshapata tatizo la maambukizi angalau mara moja katika maisha yao.

Ukiona yafuatayo, ujue unaweza kuwa na tatizo la maambukizi ya vijijidudu vya maradhi katika uke wako:

🖋️Kutokwa na uchafu ukeni kunakoambatana na kuwashwa au vijipele.
🖋️Kutokwa na uchafu ukeni ambako ni endelevu na kwa kiwango kinachozidi kila siku.
🖋️Kusikia maumivu wakati wa kutoa haja ndogo.
🖋️Kutokwa na uchafu mweupe, mzito k**a jibini.
🖋️Uchafu wa kijivu/mweupe au njano/kijani unaotoa harufu mbaya.

Aina za uchafu wa ukeni usio wa kawaida (Abnormal va**nal Discharge).

Aina nyingine za uchafu huwa ni za kawaida, Na nyingine zinaashiria hali zisizo nzuri zinazohitaji matibabu.

1. Uchafu Mweupe (White discharge).

Kutoka uchafu mweupe, hasa mwanzoni au mwishoni mwa mzunguko wa hedhi, ni kawaida. Ingawa, k**a itaambatana na miwasho na uchafu Mweupe Mzito K**a Jibini, sio kawaida inahitaji matibabu.

Aina hii ya uchafu inaweza kuwa ni dalili ya maambukizi ya Yeast infection na dalili nyingine ni kuvimba na maumivu kwenye mashavu ya uke (v***a), kuwashwa na maumivu wakati wa kufanya tendo la ndoa.

2. Uchafu wa kahawia au wenye damu (Brown or bloody discharge).

Uchafu wa kahawia au uliochanganyika na damu mara nyingi huwa ni kawaida, hasa inapotokea kipindi cha hedhi au baada ya mzunguko wa hedhi.

Uchafu utakaotoka mwishoni mwa mzunguko wako wa siku unaweza kuonekana wa kahawia au uliochanganyikana na damu, unaweza kuwa unapata kiasi kidogo cha uchafu wenye damu katikati ya mzunguko wa hedhi. Hii hujulikana k**a spotting.

K**a spotting ikitokea wakati wa kawaida wa mzunguko wa hedhi na ikiwa ulifanya mapenzi pasipo kutumia kinga, hii inaweza kuwa dalili ya ujauzito, Na Spotting kipindi kabisa cha mimba changa inaweza kuwa dalili ya mimba kuharibika (miscarriage), ni vema ukaongea na daktari.

Katika hali isiyo ya kawaida, uchafu wa kahawia au uliochanganyikana na damu inaweza kuwa ni dalili ya Maambukizi katika tabaka la ndani la kizazi (Endometrial) au kansa ya shingo ya kizazi (cervical cancer).

Inaweza kuwa matatizo mengine k**a vile uvimbe (fibroids) au hali nyingine zisizo za kawaida. Ndio maana ni muhimu kufanya uchunguzi kila mwaka wa afya ya uzazi (Pelvic exam and Pap smear).

Daktari wako atchunguza k**a kkuna ukuaji usio wa kawaida katika fupanyonga (cervical abnormalities). Mwanamke mwenye tatizo hili atatoa damu nyingi ukeni na kuumwa nyonga.

3. Uchafu wa njano au kijani (Yellow or green discharge).

Uchafu wenye rangi ya kijani au njano, ikiwa uchafu utatoka k**a mapovu, unaombatana na harufu mbaya, sio kawaida, aina hii ya uchafu dalili ya Trichomoniasis, Maambukizi yatokanayo na ngono isiyo salama. Dalili nyingine ni maumivu na kuwashwa wakati wa kukojoa.

4. Uchafu wa rangi ya mawingu au njano (Cloudly or yellow discharge).

Hii ni dalili ya ugonjwa wa kisonono (Gonorrhea). Mwanamke atatokwa na damu katikati ya siku zake, atatokwa na mkojo bila kukusudia na kupata maumivu ya nyonga.

Uchafu mweupe, wa njano au kijivu wenye harufu ya samaki
Kutokwa na uchafu mweupe au wa kijivu ulio k**a maziwa ya mgando ukeni ni tatizo la kiafya, ni dalili mojawapo ya ugonjwa wa fangasi za ukeni kitabibu hujulikana k**a 'Vaginal Candidiasis'.

Sababu ya uchafu wa aina hii ni Bacterial vaginosis chanzo cha maambuzi ya bacteria hawa hakijulikani, kinachotokea ni ongezeko la kutoka kwa uchafu mweupe, njano au kijivu na wenye harufu k**a ya samaki, ingawa kwa upande mwingine haioneshi dalili,

Wanawake wanaofanya ngono kwa mdomo au wenye wapenzi wengi wako kwenye hatari kubwa ya kupata maambukizi haya.

Uchafu wa aina hii ni dalili za maabukizi ya Bacterial Vaginosis. Mwanamke mwenye tatizo hili atasikia miwasho au maumivu, kuvimba kwa uke au sehemu ya nje ya uke (v***a).

Aina ya Maambukizi ya ukeni.

Baadhi ya maambukizi hayo ni pamoja na Bacterial Vaginosis, Trichomoniasis na Monilia (Yeast) Infection.

Bacterial Vaginosis.

Chanzo halisi cha ugonjwa huu hakifahamiki. Kinachotokea ni kuongezeka kwa ghafla kwa idadi ya bacteria hawa ambao ni kawaida kupatikana kwenye uke na kubadilisha uwiano wao kwenye mazingira ya uke.

Wanawake wenye wapenzi wengi au wanaofanya mapenzi kupitia midomo wanakuwa kwenye hatari kubwa zaidi ya kupata maambukizi ya Bacterial Vaginosis.

Dalili za Bacterial Vaginosis.

Kuongezeka kwa uchafu unaotoka ukeni
Kutokwa na uchafu wa kijivu/mweupe, mwepesi au wa majimaji
Harufu k**a ya samaki ikiambatana na uchafu
Harufu inayozidi au uchafu unaozidi mara baada ya kufanya tendo la ndoa,

Tiba kwa tatizo la bacterial vaginosis zipo za aina mbili. Tiba ya aina ya kwanza ni kutumia metronidazole (Flagyl) na tiba ya pili ni kutumia antibiotic ya vidonge au ya cream.

Trichomonas Vaginalis – (TV).

Hiki nacho ni kijidudu cha bacteria, kidogo kinachoambukiza kupitia ukeni na kwenye mrija wa kupitishia mkojo. Ugonjwa wa Trichomoniasis unasababishwa na vimelea vya jamii ya protozoa vinavyojulikana kitalaamu k**a Trichomonas va**nalis.

Ugonjwa huu huathiri mrija wa kupitisha mkojo (urethra) na tupu ya mwanamke (va**na).

Huathiri sana wanawake kuliko wanaume na wanawake wenye umri mkubwa wako katika hatari zaidi kuliko mabinti wadogo. Hupatikana kwa njia ya kujamiana bila kutumia kinga na mtu aliyeathirika na Trichomoniasis.


Ishara na dalili (Signs and symptoms).

Dalili za Trichomoniasis, huanza kuonekana kuanzia siku ya 4 mpaka ya 28 baada ya mtu kupata maambukizi, Wanaume huwa hawaonyeshi dalili zozote lakini baadhi wanaonyesha dalili k**a;

Dalili kwa mwanamke aliyeambukizwa ni;

🖋️Kutokwa na uchafu wa rangi ya njano/kijani ulio k**a mapovu huenda ukawa na harufu k**a ya samaki .
🖋️Harufu mbaya inayoambatana na kutokwa na uchafu,
🖋️Kuongezeka kwa uwingi wa uchafu wa ukeni.
🖋️Maumivu ya ukeni au sehemu za nje ya uke (v***a).
🖋️Kujisaidia haja ndogo mara nyingi zaidi.
Kuwashwa sehemu za siri.

Maambukizi haya hutokana na aina ya protozoa wa seli moja. Trichomoniasis maranyingi huambukizwa kwa kufanya ngono.

Protozoa huyu huweza kukaa kwenye mazingira ya unyevunyevu kwa muda wa saa 24 bila kufa hivyo kufanya taulo na nguo nyingine za kuogea kuwa chanzo kingine kikuu cha maambukizi.

Matibabu;

Ugonjwa huu unaweza kutibiwa kwa urahisi, kwa madawa maalam ya kupambana na viini antibiotics metronidazole. Ili kuepuka kuambukizwa upya, na kusambaa zaidi kwa ugonjwa huu inabidi mpenzio pia naye atibiwe.

Monilia (Yeast) Infection.

Kwa kawaida kuna kiwango kidogo cha yeast (Candida albicans) katik uke.

Tunasema kuna maambukizi ya yeast pale kiwango chao kinapozidi hali ambayo inatokana na kubadilika kwa hali ya ukeni (change in the pH balance of the va**na).

Maambukizi ya yeast hayatokani na tendo la ngono. Kuna mambo ambayo yanaweza kusababisha kuongezeka kwa yeast katika uke, nayo ni; msongo wa mawazo, matumizi ya dawa za kuziua mimba, kisukari, ujauzito na matumizi ya antibotics.


Dalili za Monilia (Yeast) Infection.

🖋️Ongezeko la uchafu unaotoka ukeni.
🖋️Uchafu mweupe unaotoka katika vifungu vidogo k**a vya jibini.
🖋️Kuwashwa na mauvivu ya ukeni au sehemu za nje (v***a).

Tiba ya Monilia (Yeast) Infection inalenga kuzuia mwongezeko wa yeast katika uke na kuwarudisha kwenye kiwango kinachofaa na si kuwaondoa. Tiba ni kutumia vidonge vya antifungal na cream za kupaka ukeni, Kuna dawa nyingi za kuweza kuondoa tatizo hili.

Cytolytic Vaginosis.

Hii ni hali inayojitokeza pale kunapotokea kuongeka kwa bakteria aitwaye Lactobacillus acidophilus kwenye uke.

Lactobacilli ni bakteria wazuri wanaoishi ukeni bila kuleta matatizo ya aina yo yote. Kwa kawaida uwepo wa bakteria hawa unasaidia sana katika kupambana na wadudu aina nyingine wenye madhara kwa mwili – huongeza kinga ya mwili .

Lakini endapo mazingira dhalili ya uke yatabadilika, bakteria hawa wazuri wanaweza kuzalina kupita kiwango kinachotakiwa.

Hii inaweza kutokea, kwa mfano, kunapotokea matumizi ya mara kwa mara ya antibiotics au dawa za kuzuia na kuua fungus.

Ni tatizo ambalo linalowapata zaidi wanawake walio katika umri wa kuzaa – miaka 25 – 40 – kwa sababu ya uwepo wa homoni ya estrogen.

Dalili za cytolytic vaginosis

Kutoka uchafu kwa wingi wenye rangi nyeupe, wa maji maji au mzito k**a maziwa ya mgando
Miwasho ya sehemu za ndani au nje ya uke
Maumivu wakati wa kutoa haja ndogo
Maumivu wakati wa kufanya tendo la ndoa

Dalili za tatizo hili ni rahisi sana kuzichanganya na zile za matatizo mengine ya hapo juu na hasa va**nal candidiasis (monilia).

Tatizo hili halina tiba bali kufanya yafuatayo:

-Kuacha kutumia antibiotics au dawa za fungus
- Kuacha kutumia sabuni ukeni na kutumia maji ya uvuguvugu tu.
-Kutovaa nguo za ndani usiku.
-Kutofanya tendo la ndoa.
-Kupunguza kiwango cha sukari katika mlo.
-Kujiosha mara kwa mara ukeni kwa kutumia baking soda.

Unaweza vile vile kuchanganya baking soda na maji ukatengeneza namna ya uji na kuuweka kwenye pedi.

MUHIMU;

TUNAFANYA KAZI KUPITIA ONLINE, HIVYO UAMINIFU NI KIPAUMBELE CHETU KIKUBWA, HATUNA MAWAKALA POPOTE, ILA TUNATUMA POPOTE KWA UHAKIKA NA UAMINIFU MKUBWA.

Kwa tiba zisizo na kemikali kwa maambukizi ukeni, wasiliana nasi kwa;

0769247626.

Inspiration
25/12/2025

Inspiration

Karibu kwa huduma za tiba na ushauri.
19/12/2025

Karibu kwa huduma za tiba na ushauri.

02/12/2025

S***m vs Ovaries

02/12/2025
Una swali lolote hapa unalohitaji kujua kuhusu afya ya uzazi na maambukizi katika njia ya uzazi au njia ya mkojo?Iliza!
29/11/2025

Una swali lolote hapa unalohitaji kujua kuhusu afya ya uzazi na maambukizi katika njia ya uzazi au njia ya mkojo?

Iliza!

Dalili za Awali za UTIs (Urinal Track Infections) pamoja na magonjwa mengine ya ngono (Sexual Transmitted Diseases- STIs...
27/11/2025

Dalili za Awali za UTIs (Urinal Track Infections) pamoja na magonjwa mengine ya ngono (Sexual Transmitted Diseases- STIs) kwa Wanaume.

Kwa huduma za matibabu, wasiliana nasi 0769247626

KUTOKWA NA UTEUTE/ USAHA KWENYE UUME (Pe**le Discharge):Hali hii mara nyingi huwa ni sababu ya maambukizi yatokanayo  na...
26/11/2025

KUTOKWA NA UTEUTE/ USAHA KWENYE UUME (Pe**le Discharge):

Hali hii mara nyingi huwa ni sababu ya maambukizi yatokanayo na Magonjwa ya kuambukizana kupitia kufanya ngono - Haya kwa kimombo yanaitwa STI au Sexually Transmitted Infections.

Mambukizi hutokea pale maji maji ya mwili k**a vile mate, damu, manii, majimaji ya ukeni n.k – ya mtu ambae tayari ameambukizwa, yatatangamana na ya mtu ambae hajaambukizwa.

Hii mara nyingi hufanyika wakati wa ngono ya kuingiliana kimwili au ya kunyonyana sehemu za siri.

Baadhi ya magonjwa hayo (lakini sio yote) yanatibika, lakini yasipotibiwa yanaweza kusababisha madhara ya kudumu. Kumbuka maambukizi ya ukimwi na virusi vya HIV pia mara nyingi hufanyika kupitia kufanya ngono.

Ishara na Dalili (Symptoms & Signs).

Kutokwa na uteute kwenye uume inaweza kuwa ni Maji, usaha au damu.

Maambukizi kwenye njia ya mkojo (UTI) au magonjwa ya zinaa (STIs) ni sababu kuu zinazochangia kutokwa na uteute/usaha kwenye uume. Kutokwa na uteute au usaha kwenye uume huambatana na maumivu au miwasho/kuunguza wakati wa kukojoa na huhitaji kukojoa mara kwa mara.

Miwasho sehemu za siri inaweza kuambatana na kutokwa na usaha au uteute kwenye uume. Maambukizi ya Klamidia (Chlamydia), kisonono ( gonorrhea) na Trakoma (Trichomonas) ni moja ya vyanzo vikuu vinavyochangia kutokwa na usaha au uteute kwenyeuume.

Muone daktari (to see a doctor).
Muone daktari endapo utabaini haya;

✓Unatokwa na usaha au maji maji meupe, njano au mchanganyiko na damu.
✓Unapata miwasho au mkojo kuunguza wakati wa kukojoa.
✓Kupata vipele na malengelenge kwenye uume.
✓Uume kuwasha .
✓Miwasho sehemu za siri .

K**a umefanya mapenzi bila kutumia kinga na una wasi wasi huenda umeambukizwa, nenda ukafanyiwe uchunguzi na daktari.

Kumbuka, baadhi ya maambukizi huenda yasiwe na dalili,

Hii haimaanishi kwamba huwezi kumwambukiza mpenzi wako, au kwamba hayawezi kukudhuru kiafya. K**a una wasi wasi, ni vyema kuchunguzwa na daktari haraka iwezekanavyo, ama kliniki.

Vihatarishi (Risk factors)
Ngono nzembe bila kinga wala tahadhari,
Kuwa na wapenzi wengi.
Kushiriki mapenzi na mtu zaidi ya mmoja.

Endelea kufuatilia makala zinazokufikia mfululizo.

MUHIMU;

TUNAFANYA KAZI KUPITIA ONLINE, HIVYO UAMINIFU NI KIPAUMBELE CHETU KIKUBWA, HATUNA MAWAKALA POPOTE, ILA TUNATUMA POPOTE KWA UHAKIKA NA UAMINIFU MKUBWA.

📞Wasiliana nasi kwa 0769247626.

VIDONDA VYA TUMBO (Ulcers). Vidonda vya tumbo (Ulcers) ni ugonjwa unaompata mtu ambapo kunatokea vijitundu au michubuko ...
26/11/2025

VIDONDA VYA TUMBO (Ulcers).


Vidonda vya tumbo (Ulcers) ni ugonjwa unaompata mtu ambapo kunatokea vijitundu au michubuko katika kuta za ndani za viungo vya mfumo wa uyeyushaji chakula. Michubuko hiyo huweza kutokea katika eneo la mfuko wa tumbo, katika duodenum au katika eneo la koo.

Inakadiriwa kuwa asilimia 5 hadi 10 ya watu hupatwa na ugonjwa huu angalau mara moja katika maisha yao.

Huu ni ugonjwa ambao unaweza kumrudia mtu baada ya kupona endapo chanzo chake hakikudhibitiwa.

K**a ugonjwa huu utamrudia mgonjwa , mtu huyu atakuwa amejiweka kwenye hatari kubwa ya kupata madhara makubwa zaidi k**a kutokwa na damu au kutokea tundu kubwa katika kuta za mfuko wa tumbo.

Aina za vidonda vya Tumbo

Vidonda vya tumbo (Gastric Ulcers), Huletwa na michubuko kwenye kuta za chini za tumbo inayosababishwa na mgandamano wa mabaki ya vyakula vya kukobolewa na vyenye mafuta au samaki dagaa, aidha vidonda huletwa na matumizi yaliyokithiri ya pombe, sigara na matumizi ya madawa ya asprini kwa muda mrefu na matibabu ya kutumia cylotoxic drugs na sumu. Utumiaji holela wa dawa za kuharisha na unywaji wa kahawa kupita kiasi. Hugundulika kwa kubonyeza chini ya kifua.

Vidonda vya kwenye utumbo mfupi (Duodenum Ulcers), Huletwa na michubuko inayosababishwa na samaki na dagaa, hugundulika kwa kubonyeza katikati ya tumbo.

Vidonda vya kwenye utumbo mrefu (Peptic Ulcers), Husababishwa na Matumizi ya vyakula vyenye sumu na matibabu ya kutumia cylotoxic drugs, hugundulika kwa kubonyeza tumbo upande wa kulia.

Vidonda vya kwenye utumbo mpana (Colon Ulcers), Hutokea kwenye kuta za utumbo huu mpana na hugundulika kwa kubonyeza tumbo upande wa kushoto.

Chanzo cha vidonda vya Tumbo

Bacteria: Chanzo kikubwa cha ugonjwa wa vidonda vya tumbo ni bacteria waitwao Helicobacter pylori (H. pylori). Bacteria hawa huenezwa kwa kula chakula na kunywa maji. Katika mwili wa binadamu bacteria hawa wapo katika mate na katika ute unatanda juu ya kuta za duodenum na mfuko wa tumbo.

H pylori hutengeneza enzyme (urease) ambayo hupunguza makali ya tindikali katika tumbo, Hilo likitokea, tumbo hutengeneza tindikali zaidi na hii ndiyo husababisha michubuko katika kuta za tumbo na duodenum. Bacteria hawa pia hudhoofisha kinga ya tumbo na kusababisha maumivu mbalimbali. Kwa sababu bacteria hawa wapo katika mate ya mgonjwa huyu, njia moja ya maambukizi ya ugonjwa huu ni tendo la kubadilishana mate wakati wa kubusiana.

Madawa: Matumizi ya madawa husababisha vidonda vya tumbo.
Dawa nyingi ambazo huweza kusababisha vidonda vya tumbo ni zile za kupunguza maumivu ya kichwa na maumivu mengine madogo madogo.

Dawa hizo ni k**a aspirin, diclofenac, naproxen, ibuprofen n.k. Dawa hizi hupunguza uwezo wa tumbo wa kutengeneza utando wa ute wa kulikinga tumbo hivyo kulifanya liweze kuliwa kirahisi zaidi na tindikali. Daw hizi pia hupunguza mtiririko wa damu kuelekea kwenye eneo la tumbo hivyo kupunguza uwezo wa tumbo wa kukarabati seli zilizoharibika.

Urithi: Ugonjwa huu wa vidonda vya tumbo umeonyesha kuwa ni wa kurithishwa kwani wagonjwa wengi walibainika kuwa na ndugu wengi ambao wanaugua pia ugonjwa huu.

Pombe na Tumbaku:

Watu wanaokunywa pombe na wale ambao wanatumia tumbaku wanakuwa kwenye hatari kubwa zaidi ya kuupata ugonjwa huu wa vidonda vya tumbo.

Msongo wa Mawazo:

Haijabainishwa moja kawa moja kwamba msongo wa mawazo unaweza kusababisha vidonda vya tumbo, bali mtu mwenye vidonda vya tumbo atakuwa na hali mbaya zaidi pale atakapokuwa na msongo wa mawazo.
Dalili za vidonda vya Tumbo

Maumivu ya Tumbo:

Dalili ya kwanza kabisa ya ugonjwa huu ni maumivu ya tumbo ambayo yanaongezeka pale tindikali inapogusa eneo lililoathirika.

Maumivu haya yanaweza kutokea sehemu yoyote kuanzia eneo la kitovuni hadi kwenye mifupa ya mabega na yanaweza kuchukua muda mfupi au kuendelea kwa saa chache.

Maumivu husikika zaidi wakati tumbo ni tupu, yaani k**a hujala, na huwa makali zaidi nyakati za usiku. Maumivu hupungua kwa muda mfupi baada ya kula chakula. Mgonjwa anaweza kupata nafuu kwa siku au wiki chache halafu maumivu hurudi tena.

Madhara ya vidonda vya Tumbo

Matatizo wakati wa Kumeza: Mtu mwenye vidonda vya tumbo hupata matatizo pale anapojaribu kumeza chakula au hujisika vibaya mara baada ya kupata chakula.

Kutapika: Dalili nyingine ya tatizo la vidonda vya tumbo ni kujisikia kutapika au kutapika baada ya kupata chakula.

Kukonda: Mtu mwenye vidonda vya tumbo hukosa hamu ya kula chakula na hukonda.
Dalili za ugonjwa huu huweza kuwa mbaya zaidi k**a vile kutapika damu, kutoa haja kubwa yenye rangi nyeusi au iliyochanganyikana na damu nyeusi na kusikia kichefuchefu.

Tiba ya vidonda vya Tumbo

Tiba ya vidonda vya tumbo hutolewa kulingana na chanzo kilichosababisha ugonjwa huo k**a ni bacteria au matumizi ya dawa. Lengo kubwa ni kupunguza makali ya tindikali katika tumbo ili vidonda vipone au kuua bacteria wanaosababisha ugonjwa huu.

1. Dawa za Kuua bacteria (antibiotics) wa H. pyroli

K**a daktari atagundua kuwepo wa bacteria wa aina aina ya H. pyroli katika mfumo wako wa uyeyushaji chakula, atakuandikia mchanganyiko wa dawa za kuua bacteria hao ambazo utazitumia kwa kipindi cha angalau wiki mbili pamoja na dawa nyingine za kupunguza tindikali katika tumbo.

2. Dawa za kuzuia utengenezaji wa tindikali na kusaidia uponyaji

Dawa hizi ambazo huitwa Proton Pump Inhibitors (PPIs) hupunguza tindikali katika tumbo kwa kuzuia ufanyaji kazi wa seli zinazohusika katika kutengeneza tindikali. Dawa hizi ni k**a omeprazole (Prilosec), lansoprazole (Prevacid), rabeprazole (Aciphex), esomeprazole (Nexium) na pantoprazole (Protonix).

3. Dawa za kupunguza utengenezaji wa tindikali

Dawa hizi huitwa acid blockers au histamine (H-2) blockers, Hizi ni dawa zinazofanya kazi kwa kupunguza kiwango cha tindikali itakayoingizwa kwenye mfumo wa uyeyushaji chakula hivyo kupunguza maumivu na kusaidia uponyaji. Mfano wa dawa hizi ni ranitidine (Zantac), famotidine (Pepcid), cimetidine (Tagamet) na nizatidine (Axid).

4. Matumizi ya antacids kupunguza makali ya tindikali

Dawa hizi hupunguza makali ya tindikali ambayo tayari ipo ndani ya tumbo na kumpa mgonjwa nafuu ya mara moja. Dawa hizi si za kuponya ugonjwa huu bali kukupa nafuu ya muda mfupi tu.

5. Dawa za kulinda kuta za mfuko wa tumbo na utumbo mwembamba.

Wakati mwingine daktari anaweza kukupa dawa za kulinda kuta za tumbo lako na utumbo mwembamba.

Dawa hizi huitwa cytoprotective agents, nazo ni k**a sucralfate (Carafate), misoprostol (Cytotec) na bismuth subsalicylate (Pepto-Bismol).

Kwa huduma za matibabu, kwa wenye changamoto za kiafya, Wasiliana nasi namba zipo kwenye ukurasa huu lakini pia hata kwenye post hii.

Zingatio la muhimu kuwa makini epuka kutapeliwa, hakikisha namba zinatoka kwenye kurasa zetu rasmi, Tupo Mwanza Tanzania tu, nje ya Mwanza bidhaa tiba/dawa tunatuma kwa uaminifu kabisa , UAMINIFU NDIO MTAJI WETU.

MUHIMU;

TUNAFANYA KAZI KUPITIA ONLINE, HIVYO UAMINIFU NI KIPAUMBELE CHETU KIKUBWA, HATUNA MAWAKALA POPOTE, ILA TUNATUMA POPOTE KWA UHAKIKA NA UAMINIFU MKUBWA.

Piga/SMS au WhatsApp kwa 0769247626.

DAMU NYINGI WAKATI WA HEDHI AU KUPITILIZA SIKU ZA KAWAIDA (Menorrhagia).Ni Hali inayopelekea damu kutoka bila mpangilio ...
25/11/2025

DAMU NYINGI WAKATI WA HEDHI AU KUPITILIZA SIKU ZA KAWAIDA (Menorrhagia).

Ni Hali inayopelekea damu kutoka bila mpangilio kwa kipindi kirefu zaidi ya siku za kawaida.

Muda mwingine hali hii huendelea siku kwa siku au hadi miezi kadhaa bila matumaini ya kukata au kupungua kufuata mpangilio wa siku za kawaida sawa na asiye na tatizo la afya ya uzazi.

Kupata hedhi kupita kiasi ni moja ya Matatizo ya Uzazi yanayosumbua wanawake wengi.

Tafiti zimeonyesha kwa kila wanawake 1000, Wanawake 53 kati yao huwa na tatizo la kupata hedhi kupita kiasi.

Ni theluthi tu ya wanawake wenye shida ya Hedhi hutafuta tiba stahiki kwa Daktari wengi hukaa nayo kwa aibu au hofu.

Jinsi ya kugundua k**a unapata Hedhi iliyopita kiasi.

 Damu nyingi inayopelekea kubadili pedi ndani ya masaa mawili.
 Kutoka damu nzito inayolowesha mpaka nguo za nje.
 Damu inayotoka na Mabonge.
 Kupata hedhi inayozidi siku saba.
 Damu nzito inayolazimu kuvaa pedi zaidi ya moja.

Sababu zinazochangia Mwanamke kutokwa na damu nyingi kupita kiasi .

 Yai kupevuka bila mpangilio (Irregular Ovulation), Hali hii husababisha kuta za mji wa mimba zivimbe na kuwa nene hivyo kutoa damu nyingi, Hutokea zaidi kipindi cha kuvunja ungo na kipindi cha kukaribia ukomo wa hedhi.
 Vimbe kwenye kuta za mji wa Mimba; vimbe hizi sio saratani huitwa Fibroids
 Saratani ya mji wa kizazi; kwa kinamama waliofikia umri wa ukomo wa hedhi. Wakianza kupata hedhi isiyokoma huweza kuwa dalili ya ya saratani ya mji wa kizazi.
 Matumizi ya yasiyo sahihi ya dawa za kuzuia damu kuganda.
 Baadhi ya wanawake waliotumia vitanzi (IUD) hasa ndani ya mwaka wa kwanza.
 Maambukizi ya mji wa mimba na mirija ya uzazi (PID).
 Endometriosis.


Madhara ya Kiafya yatokanayo na kutokwa na damu nyingi kupita kiasi.

 Kudhoofisha Afya ya mwili na akili ya Mwanamke ikiwemo kupunguza kujiamini na kuongeza wasiwasi.
 Huchangia kupata upungufu wa damu kwa Wanawake wengi wenye tatizo hilo .
 Huweza kuwa ni dalili ambayo inahitaji tiba ya haraka ya Afya ya uzazi.
 Urahisi wa kupata maumbukizi kwenye mji wa mimba au kushindwa kutunga mimba.
 Kulegea kwa shingo ya kizazi.
 Maambukizi ya fangasi au bacteria kwa urahisi sehemu za siri kutoka na maeneo hayo muda mwingi kuhifadhi unyevunyevu .
 Ukibahatika kupata ujauzito kuna urahisi wa ujauzito kuporomoka/mimba kuharibika.

Ufumbuzi wa Tatizo Hili.

Matumizi ya unga wa mkaa wa mkaratusi hasa ule wenye majani ya weupe weupe, pamoja na ndimu ya unga kwa kukoroga ndani ya maji baridi kijiko kimoja cha chai itakusaidia kwa sehemu kubwa.

Lakini Endapo hali itazidi Tembelea Hospital iliyo karibu na wewe kwa msaada zaidi, Au Tutembelea na kuwasiliana nasi kwa ajili ya Matibabu kwa wenye tatizo la namna hii,

Tiba zinapatikana za uhakika zaidi na zimethibitika kusaidia wengi sana waliokumbwa na kadhia hii,

Vile vile kwa matatizo mengine ya Uzazi, wahi bila kuchelewa kwa kuwa litakapo endelea tatizo hili la damu kutoka mfululizo kuna uwezekano wa kupelekea madhara makubwa ya kiafya .

Kwa Mwanamke mwenye tatizo hili Tunalitibu kwa Uhakika zaidi na kwa Muda usio mrefu sana, Wasiliana nasi kwa taratibu zaidi kwa Namba zinazopatikana kwenye Ukurasa huu..

Zingatio na Msisitizo;
Namba zote za mawasiliano zitoke katika ukurasa huu au Inbox kupitia ukurasa huu na si vinginevyo, Kuwa makini sana na utapeli.

Tunapatikana kijiweni Nyegezi, Mwanza Tanzania,

Kwa huduma za matibabu
Piga au tuma SMS kwa namba; +255769247626.

Address

Mwanza
10901090

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00

Telephone

+255769247626

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wema Herbal Clinic posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram