Wema Herbal Clinic

Wema Herbal Clinic Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Wema Herbal Clinic, Medical and health, Mwanza.

HUDUMA BORA ZA TIBA, LISHE NA USHAURI. || Meditation & Spirituality. || Tunatuma Popote nchini kwa Uaminifu.|| Tupo Mwanza - Tanzania.

JINSI YA KUANDAA LISHE MUHIMU KWA MTOTO NA WATU WAZIMA PIA.Somo Muhimu Uji wa Lishe kwa Ajili ya Watoto.Uandaaji wa lish...
12/07/2025

JINSI YA KUANDAA LISHE MUHIMU KWA MTOTO NA WATU WAZIMA PIA.

Somo Muhimu Uji wa Lishe kwa Ajili ya Watoto.

Uandaaji wa lishe kwa watoto ni muhimu uzingatie umri na ukuaji wa mtoto, mambo muhimu kwa mtoto ili akue katika mwelekeo mzuri ni vyema apate Virutubisho vitokanavyo na Wanga, Protini, Vitamini pamoja na Mafuta.

Jinsi ya kuandaa wa uji lishe kwa Mtoto.

Kitu cha msingi cha kuzingatia ni kuandaa uji utaoweza kumpatia mtoto virutubisho anavyohitaji kwa umri wake ili kusaidia ukuaji na maendeleo bora kwa afya ya mtoto. Virutubisho muhimu zaidi kwa mtoto ni;-

📌Wanga (Carbohydrates) - Chanzo chake Mahindi/ Mchele,/Ulezi/Ngano, Umuhimu wake Kuupatia mwili nguvu.

📌Protini (Protein) - Chanzo chake Soya/Maharage, Umuhimu wake Hujenga mwili.

📌Mafuta (Lipids) - Chanzo chake Ufuta/Karanga, faida zake Kutia joto mwilini.

Lakini pia kwa ajili ya kuboresha Afya ya ubongo/Akili yake, Anahitaji kupata vyakula vyenye kiwango cha kutosha cha OMEGA-3,

Moja wapo ya vyakula vyenye OMEGA-3 ndani yake ni Samaki na Mbegu za Haradali (Musturd Seeds). Hali kadhalika unaweza kuongeza ndani yake mbegu za Maboga ( Pumpkin Seeds) kwa ajili ya matokeo bora kwa afya ya akili ya Mtoto.

Zingatia Haya katika uandaaji wa lishe ya mtoto.
Tumia aina moja ya nafaka kwa kila kirutubishi.

Uwiano sahihi wa vyanzo vya nafaka.
Kiwango cha virutubishi anavyohitaji mtoto hutofautiana kulingana na mahitaji ya ukuaji na maendeleo ya mtoto.

Mahitaji.

-Mahindi ya njano - chanzo cha wanga.
-Soya - chanzo cha protini.
-Ufuta - chanzo cha mafuta.

Uwiano.

Katika kuchanganya Virutubisho hivi inatakiwa angalau wanga iwe nyingi Kwa maana inasaidia katika Kuupatia mwili nguvu.

-Chanzo cha Wanga kilo moja - 1kg.
-Chanzo cha Protini nusu kilo - ½kg.
-Chanzo cha Mafuta robo kilo - 1/4 kg.

MUHIMU;

TUNAFANYA KAZI PIA KUPITIA ONLINE, HIVYO UAMINIFU NI KIPAUMBELE CHETU KIKUBWA, HATUNA MAWAKALA POPOTE, ILA TUNATUMA POPOTE KWA UHAKIKA NA UAMINIFU MKUBWA.

Wasiliana nasi kwa 0769247626.

Itaendelea..........

UCHAFU UKENI (Vaginal Discharge).Kutoka uchafu ukeni ni hali ya kawaida, ingawa kuna uchafu unaotoka ambao unaashiria uw...
20/06/2025

UCHAFU UKENI (Vaginal Discharge).

Kutoka uchafu ukeni ni hali ya kawaida, ingawa kuna uchafu unaotoka ambao unaashiria uwepo wa maambukizi, hasa pale unapotoka mwingi kupita kiasi, wenye rangi ya njano au kijani na ukiwa na harufu isiyo ya kawaida, mfano harufu kali, au harufu k**a ya samaki. Uke wa mwanamke hufanya kazi ya kutoa njia kati ya sehemu ya nje ya mwili na viungo vya uzazi vya ndani vya mwanamke.

Hali ya kawaida ya majimaji yaliyomo katika uke wa mwanamke huwa ni ya tindikali ili kuzuia maambukizi ya vijidudu wa kuleta maradhi. Hali hii ya utindikali huletwa na bacteria waishio katika uke wa mwanamke. Bacteria hawa ni wa kawaida na hawana madhara kwa mwili.

Uke ulio katika hali nzuri hutoa majimaji haya ili kujisafisha. Majimaji haya yanayotengenezwa katika uke na kwenye eneo la cervix hufanya kazi ya kuondoa seli zilizokufa na bacteria waharibifu nje ya mwili na huu ndio uchafu wa kawaida ambao mwanamke hutoa ukeni.

Kutoa uchafu huu sehemu za siri ni njia ya kuusafisha uke na kuzuia maambukizi ya magonjwa. Kitu cho chote ambacho kitaharibu uwiano wa utengeneaji wa majimaji haya ndani ya uke kinaweza kujenga mazingira ya maambukizi katika uke.

Kila mwanamke anapaswa kujichunguza kila siku ya maisha yake maeneo yake ya uzazi na matiti, vile vile kuichunguza nguo ya ndani aliyokuwa ameivaa siku hiyo k**a kuna uchafu wowote.
Kufanya hivi kunaweza kumsaidia kugundua kuwa ana tatizo la kiafya, kwani wapo baadhi ambao hawafahamu kuwa kila siku huwapo ute ute unaomtoka ambao ni hali ya kawaida.

Ute huo unaweza kuwa na ujazo wa nusu kijiko cha chai na huwa na harufu asilia ya uke na huwa na rangi nyeupe au kahawia mpauko k**a chai isiyokolea rangi bila kuwa na harufu mbaya. Utokaji wa ute huo ni mojawapo ya njia ya uke kujisafisha kwa kutiririka pamoja na mabaki ya hedhi au takataka za mwili au zilizotoka nje ya mwili. Ute huu huzalishwa na kuta za nyumba ya uzazi na huzifanya tezi za ukeni kushuka chini kutokana na kani ya nguvu za uvutano (gravity).

Uchafu wa kawaida ukeni (Normal va**nal discharge)

Wanawake wote hutoa uchafu ukeni, Kiwango cha uchafu unaotoka, rangi yake na harufu yake vitabalikabadilika kutoka kipindi kimoja hadi kingine kulingana na muda mwanamke aliopo katika mzunguko wake wa mwezi. Uchafu huu utabadilika vilevile k**a ananyonyesha, atakuwa na hisia za kufanya mapenzi, atakuwa na mabadiliko ya lishe, anatumia madawa hasa ya mpango wa uzazi au atakuwa na ujauzito.

Kwa kawaida uchafu huu huwa usio na rangi, wenye rangi yenye weupe wa mawingu au njanonjano pale unapokaukia kwenye nguo. Unaweza kuwa na vijipande vidogovidogo na mara nyingine ukawa wa kunatanata.

Clear and watery
Uchafu usio na rangi huu ni wa kawaida, Hutokea muda wowote katika mwezi, unaweza kuwa mwingi baada ya kumaliza kufanya mazoezi.

Clear and stretchy
Wakati uchafu usio na rangi lakini unaovutika na kunatanata, mzito kidogo unapotoka, huashiria uchevushwaji (Ovulating). Huu huwa ni uchafu wa kawaida.

Uchafu wa Ukeni usio wa kawaida (Abnormal va**nal discharge).

Ishara Na Dalili za uchafu wa Ukeni usio wa kawaida.

Mabadiliko ya uwingi wa uchafu unaotoka au katika rangi ya uchafu unaotoka ni dalili ya maambukizi ya magonjwa katika uke. Maambukizi katika uke ni tatizo la kawaida kwa wanawake na wanawake wengi wameshapata tatizo la maambukizi angalau mara moja katika maisha yao.
Ukiona yafuatayo, ujue unaweza kuwa na tatizo la maambukizi ya vijijidudu vya maradhi katika uke wako:

🖋️Kutokwa na uchafu ukeni kunakoambatana na kuwashwa au vijipele.
🖋️Kutokwa na uchafu ukeni ambako ni endelevu na kwa kiwango kinachozidi kila siku.
🖋️Kusikia maumivu wakati wa kutoa haja ndogo.
🖋️Kutokwa na uchafu mweupe, mzito k**a jibini.
🖋️Uchafu wa kijivu/mweupe au njano/kijani unaotoa harufu mbaya.

Aina za uchafu wa ukeni usio wa kawaida (Abnormal va**nal Discharge).

Aina nyingine za uchafu huwa ni za kawaida, Na nyingine zinaashiria hali zisizo nzuri zinazohitaji matibabu.

1. Uchafu Mweupe (White discharge).

Kutoka uchafu mweupe, hasa mwanzoni au mwishoni mwa mzunguko wa hedhi, ni kawaida. Ingawa, k**a itaambatana na miwasho na uchafu Mweupe Mzito K**a Jibini, sio kawaida inahitaji matibabu. Aina hii ya uchafu inaweza kuwa ni dalili ya maambukizi ya Yeast infection na dalili nyingine ni kuvimba na maumivu kwenye mashavu ya uke (v***a), kuwashwa na maumivu wakati wa kufanya tendo la ndoa.

2. Uchafu wa kahawia au wenye damu (Brown or bloody discharge).

Uchafu wa kahawia au uliochanganyika na damu mara nyingi huwa ni kawaida, hasa inapotokea kipindi cha hedhi au baada ya mzunguko wa hedhi. Uchafu utakaotoka mwishoni mwa mzunguko wako wa siku unaweza kuonekana wa kahawia au uliochanganyikana na damu, unaweza kuwa unapata kiasi kidogo cha uchafu wenye damu katikati ya mzunguko wa hedhi.

Hii hujulikana k**a spotting. K**a spotting ikitokea wakati wa kawaida wa mzunguko wa hedhi na ikiwa ulifanya mapenzi pasipo kutumia kinga, hii inaweza kuwa dalili ya ujauzito, Na Spotting kipindi kabisa cha mimba changa inaweza kuwa dalili ya mimba kuharibika (miscarriage), ni vema ukaongea na daktari.

Katika hali isiyo ya kawaida, uchafu wa kahawia au uliochanganyikana na damu inaweza kuwa ni dalili ya Maambukizi katika tabaka la ndani la kizazi (Endometrial) au kansa ya shingo ya kizazi (cervical cancer). Inaweza kuwa matatizo mengine k**a vile uvimbe (fibroids) au hali nyingine zisizo za kawaida. Ndio maana ni muhimu kufanya uchunguzi kila mwaka wa afya ya uzazi (Pelvic exam and Pap smear).

Daktari wako atchunguza k**a kkuna ukuaji usio wa kawaida katika fupanyonga (cervical abnormalities). Mwanamke mwenye tatizo hili atatoa damu nyingi ukeni na kuumwa nyonga.

3. Uchafu wa njano au kijani (Yellow or green discharge).

Uchafu wenye rangi ya kijani au njano, ikiwa uchafu utatoka k**a mapovu, unaombatana na harufu mbaya, sio kawaida, aina hii ya uchafu dalili ya Trichomoniasis, Maambukizi yatokanayo na ngono isiyo salama. Dalili nyingine ni maumivu na kuwashwa wakati wa kukojoa.

4. Uchafu wa rangi ya mawingu au njano (Cloudly or yellow discharge).

Hii ni dalili ya ugonjwa wa kisonono (Gonorrhea). Mwanamke atatokwa na damu katikati ya siku zake, atatokwa na mkojo bila kukusudia na kupata maumivu ya nyonga.

Uchafu mweupe, wa njano au kijivu wenye harufu ya samaki
Kutokwa na uchafu mweupe au wa kijivu ulio k**a maziwa ya mgando ukeni ni tatizo la kiafya, ni dalili mojawapo ya ugonjwa wa fangasi za ukeni kitabibu hujulikana k**a 'Vaginal Candidiasis'.

Sababu ya uchafu wa aina hii ni Bacterial vaginosis chanzo cha maambuzi ya bacteria hawa hakijulikani, kinachotokea ni ongezeko la kutoka kwa uchafu mweupe, njano au kijivu na wenye harufu k**a ya samaki, ingawa kwa upande mwingine haioneshi dalili, Wanawake wanaofanya ngono kwa mdomo au wenye wapenzi wengi wako kwenye hatari kubwa ya kupata maambukizi haya.

Uchafu wa aina hii ni dalili za maabukizi ya Bacterial Vaginosis. Mwanamke mwenye tatizo hili atasikia miwasho au maumivu, kuvimba kwa uke au sehemu ya nje ya uke (v***a).

Aina ya Maambukizi ya ukeni.

Baadhi ya maambukizi hayo ni pamoja na Bacterial Vaginosis, Trichomoniasis na Monilia (Yeast) Infection.

Bacterial Vaginosis.

Chanzo halisi cha ugonjwa huu hakifahamiki. Kinachotokea ni kuongezeka kwa ghafla kwa idadi ya bacteria hawa ambao ni kawaida kupatikana kwenye uke na kubadilisha uwiano wao kwenye mazingira ya uke.

Wanawake wenye wapenzi wengi au wanaofanya mapenzi kupitia midomo wanakuwa kwenye hatari kubwa zaidi ya kupata maambukizi ya Bacterial Vaginosis.

Dalili za Bacterial Vaginosis.

Kuongezeka kwa uchafu unaotoka ukeni
Kutokwa na uchafu wa kijivu/mweupe, mwepesi au wa majimaji
Harufu k**a ya samaki ikiambatana na uchafu
Harufu inayozidi au uchafu unaozidi mara baada ya kufanya tendo la ndoa,

Tiba kwa tatizo la bacterial vaginosis zipo za aina mbili. Tiba ya aina ya kwanza ni kutumia metronidazole (Flagyl) na tiba ya pili ni kutumia antibiotic ya vidonge au ya cream.

Trichomonas Vaginalis – (TV).

Hiki nacho ni kijidudu cha bacteria, kidogo kinachoambukiza kupitia ukeni na kwenye mrija wa kupitishia mkojo. Ugonjwa wa Trichomoniasis unasababishwa na vimelea vya jamii ya protozoa vinavyojulikana kitalaamu k**a Trichomonas va**nalis. Ugonjwa huu huathiri mrija wa kupitisha mkojo (urethra) na tupu ya mwanamke (va**na).

Huathiri sana wanawake kuliko wanaume na wanawake wenye umri mkubwa wako katika hatari zaidi kuliko mabinti wadogo. Hupatikana kwa njia ya kujamiana bila kutumia kinga na mtu aliyeathirika na Trichomoniasis.


Ishara na dalili (Signs and symptoms).

Dalili za Trichomoniasis, huanza kuonekana kuanzia siku ya 4 mpaka ya 28 baada ya mtu kupata maambukizi, Wanaume huwa hawaonyeshi dalili zozote lakini baadhi wanaonyesha dalili k**a;

Dalili kwa mwanamke aliyeambukizwa ni;
🖋️Kutokwa na uchafu wa rangi ya njano/kijani ulio k**a mapovu huenda ukawa na harufu k**a ya samaki .
🖋️Harufu mbaya inayoambatana na kutokwa na uchafu,
🖋️Kuongezeka kwa uwingi wa uchafu wa ukeni.
🖋️Maumivu ya ukeni au sehemu za nje ya uke (v***a).
🖋️Kujisaidia haja ndogo mara nyingi zaidi.
Kuwashwa sehemu za siri.

Maambukizi haya hutokana na aina ya protozoa wa seli moja. Trichomoniasis maranyingi huambukizwa kwa kufanya ngono. Protozoa huyu huweza kukaa kwenye mazingira ya unyevunyevu kwa muda wa saa 24 bila kufa hivyo kufanya taulo na nguo nyingine za kuogea kuwa chanzo kingine kikuu cha maambukizi.

Matibabu;
Ugonjwa huu unaweza kutibiwa kwa urahisi, kwa madawa maalam ya kupambana na viini antibiotics metronidazole. Ili kuepuka kuambukizwa upya, na kusambaa zaidi kwa ugonjwa huu inabidi mpenzio pia naye atibiwe.

Monilia (Yeast) Infection.

Kwa kawaida kuna kiwango kidogo cha yeast (Candida albicans) katik uke. Tunasema kuna maambukizi ya yeast pale kiwango chao kinapozidi hali ambayo inatokana na kubadilika kwa hali ya ukeni (change in the pH balance of the va**na).

Maambukizi ya yeast hayatokani na tendo la ngono. Kuna mambo ambayo yanaweza kusababisha kuongezeka kwa yeast katika uke, nayo ni; msongo wa mawazo, matumizi ya dawa za kuziua mimba, kisukari, ujauzito na matumizi ya antibotics.


Dalili za Monilia (Yeast) Infection.

🖋️Ongezeko la uchafu unaotoka ukeni.
🖋️Uchafu mweupe unaotoka katika vifungu vidogo k**a vya jibini.
🖋️Kuwashwa na mauvivu ya ukeni au sehemu za nje (v***a).

Tiba ya Monilia (Yeast) Infection inalenga kuzuia mwongezeko wa yeast katika uke na kuwarudisha kwenye kiwango kinachofaa na si kuwaondoa. Tiba ni kutumia vidonge vya antifungal na cream za kupaka ukeni, Kuna dawa nyingi za kuweza kuondoa tatizo hili.

Cytolytic Vaginosis.

Hii ni hali inayojitokeza pale kunapotokea kuongeka kwa bakteria aitwaye Lactobacillus acidophilus kwenye uke. Lactobacilli ni bakteria wazuri wanaoishi ukeni bila kuleta matatizo ya aina yo yote. Kwa kawaida uwepo wa bakteria hawa unasaidia sana katika kupambana na wadudu aina nyingine wenye madhara kwa mwili – huongeza kinga ya mwili.

Lakini endapo mazingira dhalili ya uke yatabadilika, bakteria hawa wazuri wanaweza kuzalina kupita kiwango kinachotakiwa. Hii inaweza kutokea, kwa mfano, kunapotokea matumizi ya mara kwa mara ya antibiotics au dawa za kuzuia na kuua fungus.

Ni tatizo ambalo linalowapata zaidi wanawake walio katika umri wa kuzaa – miaka 25 – 40 – kwa sababu ya uwepo wa homoni ya estrogen.

Dalili za cytolytic vaginosis

Kutoka uchafu kwa wingi wenye rangi nyeupe, wa maji maji au mzito k**a maziwa ya mgando
Miwasho ya sehemu za ndani au nje ya uke
Maumivu wakati wa kutoa haja ndogo
Maumivu wakati wa kufanya tendo la ndoa

Dalili za tatizo hili ni rahisi sana kuzichanganya na zile za matatizo mengine ya hapo juu na hasa va**nal candidiasis (monilia).

Tatizo hili halina tiba bali kufanya yafuatayo:

-Kuacha kutumia antibiotics au dawa za fungus
- Kuacha kutumia sabuni ukeni na kutumia maji ya uvuguvugu tu.
-Kutovaa nguo za ndani usiku.
-Kutofanya tendo la ndoa.
-Kupunguza kiwango cha sukari katika mlo.
-Kujiosha mara kwa mara ukeni kwa kutumia baking soda. Unaweza vile vile kuchanganya baking soda na maji ukatengeneza namna ya uji na kuuweka kwenye pedi.

Kwa tiba zisizo na kemikali kwa maambukizi ukeni,

MUHIMU;

TUNAFANYA KAZI KUPITIA ONLINE, HIVYO UAMINIFU NI KIPAUMBELE CHETU KIKUBWA, HATUNA MAWAKALA POPOTE, ILA TUNATUMA POPOTE KWA UHAKIKA NA UAMINIFU MKUBWA.

Wasiliana nasi kwa;

0769247626

MAAMBUKIZI MJI WA MIMBA (Pelvic Inflammatory Disease—PID).PID ni maambukizi yanayotokea  kwenye mji wa mimba, ovari na m...
20/06/2025

MAAMBUKIZI MJI WA MIMBA (Pelvic Inflammatory Disease—PID).

PID ni maambukizi yanayotokea kwenye mji wa mimba, ovari na mirija ya uzazi kwa mwanamke, mara nyingi hutokea pale bacteria wa magonjwa ya ngono wanaposambaa kutoka ukeni mpaka kwenye mji wa mimba, mirija ya uzazi pamoja na mayai.

Dalili za Maambukizi ya PID zinaweza kuwa wazi au zisionekane, Baadhi ya wanawake hawapati ishara au dalili yoyote. Huwezi kugundua k**a unayo mpaka pale utakapopata ugumu wa kubeba mimba, maumivu makali ya nyonga au chini ya kitovu.

Ishara na Dalili (Signs and Symptoms).

Ishara na dalili za maambukizi ya mji wa mimba pamoja na mirija ya uzazi huwa wakati mwingine ni ngumu kuzibainisha, Baadhi ya wanawake hawaoneshi dalili yoyote, wakati dalili za PID zinapoonekana, mara kadhaa huhusisha;-

-Maumivu makali chini ya kitovu.
-Majimaji/uteute ukeni muda mwingine wenye harufu mbaya.
-Maumivu makali wakati wa kufanya tendo la ndoa.
-Homahoma.
-Maumivu mara kwa mara au kupata shida wakati wa kukojoa.

Muone daktari unapoona au kupata hali zifuatazo.

-Maumivu makali chini ya kitovu (Severe pain low in your abdomen).
-Kutokwa damu puani na kutapika.
-Homa na joto la mwili kupanda zaidi ya 101F˚ (38.3C˚).

K**a ishara na dalili si za kawaida, muone daktari haraka iwezekanavyo.
Usaha wenye harufu, maumivu wakati wa kukojoa au damu katikati ya mzunguko wa siku pia inaweza kuwa ni dalili ya magonjwa yanayoambukkizwa kwa njia ya kujaamiana (STIs), k**a ishara na dallili hizi zitaonekana acha kufanya mapenzi, muone daktari, anza matibabu ya magonjwa hayo yanayoambukizwa kwa njia ya kujamiana inaweza kusaidia kupunguza PID.

Sababu za PID (Causes).

Aina nyingi za bacteria zinaweza kusabisha PID, lakini gonorrhea na kaswende ni vyanzo vikubwa. Bacteria hawa husambazwa kwa urahisi na mtu anayefanya ngono zembe. Mara chache bacteria huingia kwenye mfuko wa uzazi, wangeweza kuingia kupitia mlango wa kizazi wakati wowote k**a wasingezuiliwa na cervix.

Hii hutokea wakati wa mzunguko wa hedhi au kipindi cha kujifungua, kutoa mimba au mimba kuporomoka. Vile vile bacteria wanaweza kuingia kupitia uwekewaji wa vitanzi (Intrauterine Device —IUD) kwa ajili ya kuzuia mimba au kupitia hatua za uwekeji au uingizwaji wa dawa kwenye uterus.

Sababu zinazoweza kuuongeza hatari ya maambukizi ni pamoja na;-

-Mapenzi ya mara kwa mara chini ya miaka 25.
-Wapenzi wengi (Having multiple s*xual partners).
-Kuwa na mahusiano na mtu mwenye wapenzi wengi.
-Kufanya mapenzi bila kondomu (Having s*x without a condom).
-Kuosha ukeni kwa kutumia maji (Douching regularly).
-Kuwa na historia ya maambukizi mji wa mimba au magonjwa yanayoambukizwa kwa njia ya ngono.
-Maambukizi katika tabaka la ndani la kizazi (Endometriosis).

Kuna sababu ndogo ndogo zinazoongeza hatari ya maambukizi ya PID baada ya kupandikiziwa vitanzi (Intrauterine Device —IUD). Viashiria hivi kiujumla hubainika wiki tatu baada ya upandikizwaji wa kitanzi.

Madhara ya PID (Complications).

Pelvic inflammatory disease (PID) isipotibiwa husababisha makovu na vifuko vyenye maambukizi (abscesses) kundelea kuwepo kwenye mfuko wa mimba. Hii inaweza kusababisha uharibifu wa via vya uzazi.
Madhara yatokanayo na maambukizi haya ni pamoja na;-

01; Ujauzito kutungia nje ya mfuko wa mimba (Ectopic pregnancy).

PID ni sababu inayapelekea ujauzito kkutungia nje ya mfuko wa mimba, na hii hutokea pale PID inapoacha kutibiwa na kusababisha kuwepo kwa makovu kwenye mirija ya uzazi.

Makovu haya huzuia yai lililopevushwa kushindwa kkupita kwenye mirija ya uzazi kuelekea kwenye mji wa mimba, badala yake yai lililo pevushwa hujipandikiza kwenye mirija ya uzazi (fallopian tube). Mimba ya nje ya mfuko wa uzazi inaweza kusababisha usumbufu mkubwa na kuhatarisha maisha ya mjamzito, damu kutoka na kupelekea mama mjamzito kuwekwa chini ya uangallizi maalumu.

02; Ugumba (Infertility).

Uharibifu wa sehemu za via vya uzazi unaweza kupelekea ugumba —hali ya kushindwa kupata ujauzito. Kipindi kirefu utakachokuwa na PID ndivyo kadiri unajiweka kwenye hatari kubwa ya ugumba, kuchelewa kutibu PID ni kuongeza hatari ya kuwa mgumba.

03; Maumivu sugu (Chronic pelvic pain).

PID inaweza kusababisha maumivu ya chini ya tumbo yanayoendelea kwa miezi au miaka. Makovu kwenye fallopian (mirija ya uzazi) na via vingine vya uzazi inaweza kusababisha maumivu wakati wa kufanya mapenzi na upevvushwaji wa yai.

04; Uvimbe wenye usaha kwenye mfuko wa mayai (Tubo-ovarian abscess).

PID inaweza kupelekea kuwepo kwa vimbe zenye usaha kwenye mfuko wa mimba, usaha huu unaathiri mirija ya uzazi pamoja na mayai, lakini unaweza kuendelea kwenye uterus na maeneo mengine ya uzazi, Hali ikiachwa ikaendelea inaweza kupelekea maambukizi zaidi.

Jinsi ya Kuzuia (Prevention).

Kupunguza hatari ya kupata PID (pelvic inflammatory disease):

(i); Shiriki Ngono salama (Practice safe s*x).

(ii); Tumia kondomu kila mara unapofanya mapenzi, zuia kuwa na wapenzi wengi na chunguza kuhusu historia ya mpenzi uliye nae.

(iii); Ongea na daktari kuhusu vikinga mimba (contraception). Idadi nyingi ya vikinga mimba haviwezi kukinga mwendelezo wa uwepo wa PID, tumia njia ya vizuizi k**a vile kondomu ili kupunguza hatari zaidi. Hata k**a umeshatumia dawa za uzazi wa mpango, tumia kondomu unapokutana na mpenzi mpya ili kujizuia na maambukizi ya magonjwa ya ngono (s*xual transmission infections —STIs).

(iv); Pata vipimo, K**a upo kwenye hatari itokanayo na maambukizi ya magonjwa ya ngono, muone daktari kwa ajili ya uchunguzi. Tiba ya mapema dhidi ya magonjwa ya ngono inakupa nafasi ya kuzuia maambukizi wa kwenye mji wa mimba (PID). Mshirikishe na mpenzi wako mpime wote, endapo una maambukizi kwenye mji wa mimba (Pelvic inflammatory disease au STI), mshauri mpenzi wako kupima na kutibiwa. Hii itasaidia kuzuia kusambaa kwa STIs na kuondoa hatari ya PID kujirudia.

(v); Usioshe uke wako kwa vifaa vya kuoshea uke (Don't do**he). Kuosha uke wako kwa kutumia kemikali au hufanya bacteria wa kulindauke wako kushindwa kuwa kwenye mazingira mazuri.

Tafuta kujua chanzo cha maambukizi haya, ikiwa ni magonjwa ya zinaa shughulikia matibabu ya magonjwa hayo, wakati ukiendelea kutafuta namna ya kujua chanzo cha maambukizi haya, unaweza kuendelea na Matumizi ya tangawizi ya unga ndani ya glasi moja maji ya vuguvugu kamlia limao moja ongeza vijiko viwili vya asali, mdalasini wa unga na asali, pamoja na ndimu ya unga kwa kukoroga ndani ya maji baridi kijiko kimoja cha chai itakusaidia kwa sehemu kubwa kuboresha hali yako ya kiafya,

Tembelea Hospital iliyo karibu na wewe kwa msaada zaidi, njia iliyo bora ni kuzingatia kanuni za afya bora, kuepuka kuosha uke wako kwa kutumia kemikali, kuepuka kuwa na wapenzi wengi na kuzingatia ngono iliyo salama, hii itakuweka katika mazingira mazuri ya kuepuka maambukizi ya magonjwa ya ngono ambayo ndio kichochea kikubwa cha maambukizi haya ya mji wa mimba yaani PID.

Kwa huduma za matibabu, kwa wenye changamoto za kiafya, Wasiliana nasi namba zipo kwenye ukurasa huu lakini pia hata kwenye post hii. Zingatio la muhimu kuwa makini epuka kutapeliwa, hakikisha namba zinatoka kwenye kurasa zetu rasmi,

MUHIMU;

TUNAFANYA KAZI KUPITIA ONLINE, HIVYO UAMINIFU NI KIPAUMBELE CHETU KIKUBWA, HATUNA MAWAKALA POPOTE, ILA TUNATUMA POPOTE KWA UHAKIKA NA UAMINIFU MKUBWA.

Piga/SMS au WhatsApp kwa 0769247626.

11/06/2025
MAGONJWA YA ZINAA (Sexually Transmitted Infections −STIs)Yapo magonjwa mengi yanayosababisha mtu kukojoa udenda (usaha),...
26/05/2025

MAGONJWA YA ZINAA (Sexually Transmitted Infections −STIs)

Yapo magonjwa mengi yanayosababisha mtu kukojoa udenda (usaha), uume kuuma au kuwasha wakati wa kukojoa. Magonjwa yanayosababisha hali hiyo kwa sana ni pamoja na klamidia (Chlamydia), kisonono (Gonorrhea), Trichomoniasis na magonjwa mengine yanayoathiri njia ya mkojo (Nongonococcal Urethritis).

Klamidia (Chlamydia)

Klamidia (Chlamydia) ni moja ya magonjwa ya zinaa. Ugonjwa huu unasababishwa na viini vya bakteria wanaojulikana kitalaamu k**a Chlamydia Trachomatis na waweza kuathiri uke, mrija wa kupitisha mkojo, uume au sehemu ya kupitishia haja kubwa.

Klamidia (Chlamydia) ndio ugonjwa wa zinaa unaotokana na bakteria unaoongoza kwa maambukizi mengi zaidi duniani ukifuatiwa na ugonjwa wa kisonono (gonorrhea).
Ugonjwa wa Klamidia (Chlamydia) huweza kuambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kujamiana. Ugonjwa huu ni wa hatari kwa sababu mama mjamzito anaweza kumuambukiza mtoto wake wakati wa ujauzito.

Njia nyingine za maambukizi ni pamoja na,
Kuchangia vifaa vya kuogea k**a taulo vya mtu mwenye maambukizi,

Kuchangia vyoo vya kukaa na mtu mwenye maambukizi na
Kukumbatiana na mtu mwenye maaambukizi.

Vile vile ugonjwa huu unaweza kuambukizwa kupitia mbwa, kupitia vinyesi vya ndege k**a kuku, bata na kasuku walioambukizwa klamidia (chlamydia) inayopatikana kwa wanyama ijulikanayo kitaalamu k**a Chlamydophila psittaci na kusababisha aina ya homa ya mapafu au homa ya kasuku (psittacosis).

Klamidia huathiri sehemu tofauti za mwili wa binadamu k**a macho, mfumo wa upumuaji, sehemu za siri k**a makalio, viungo vya uzazi na tezi (lymph nodes).

Huchukua siku 1-14 tangu maambukizi hadi kuonekana kwa dalili. Asilimia 75 ya wanawake na asilimia 50 ya wanaume wanaopata maambukizi ya ugonjwa huu huwa hawaonyeshi dalili za moja kwa moja.

Ishara na dalili (Signs and symptoms).

Kwa wanaume,

Ugonjwa huu huathiri mrija wa kupitishia mkojo uzuri ni kwamba dalili huonekana wazi, k**a vile;
Uume kuwasha,

Uume kutokwa na ute na kusikia maumivu wakati wa kukojoa.

Sehemu ya tundu kwenye uume kuwa nyekundu,
Kuvimba na kuwasha pia kuhisi maumivu kwenye korodani.
Tezi zilizopo sehemu za uume ambazo huvimba na kuambatana na maumivu.

Kwa wanawake dalili hazionekani kwa urahisi.
Ubaya ni kuwa ugonjwa huo unaweza kuathiri fallopian tubes – yaani mirija ya kupitia mayai kutoka kwenye Ovari hadi kwenye nyumba ya uzazi hivyo basi kusababisha ugumba/utasa.

Wakati mwingine dalili hii unaweza kuiona - kutokwa na majimaji ya ukeni yasiyo ya kawaida na kuhisi maumivu wakati wa kukojoa.

Dalili za ugonjwa huu k**a umeathiri makalio (puru) kwa wanawake na wanaume ni k**a

Kuwashwa na kutokwa na damu kwenye puru,
Maumivu wakati wa kujisaidia haja kubwa.
Kutokwa uchafu k**a k**asi kutoka kwenye puru.

Iwapo vimelea vya klamidia vitaathiri macho, wanawake na wanaume huwa na dalili k**a;

Kuvimba macho,
Macho kuwa mekundu, Kuwasha na hata kutokwa na majimaji machoni.

Klamidia inayoambukiza kwenye macho hujulikana kitaalamu k**a Chlamydia conjunctivitis au Trakoma (trachoma) na ndiyo inayoongoza kwa kusababisha upofu duniani.

Dalili za klamidia kwa watoto wachanga hutokea katika kipindi cha wiki mbili kwenye macho, na iwapo ni homa ya mapafu dalili zake hujitokeza katika kipindi cha wiki mbili hadi miezi 3 baada ya kuzaliwa.

Husababishwa na viini vya bacteria na waweza kuathiri uke, mrija wa kupitisha mkojo, uume au sehemu ya kupitishia haja kubwa.

Matibabu: Ni pamoja na kufanyiwa uchunguzi wa mkojo au damu.

Unapotambuliwa daktari hupendekzeza dawa maalum ya kumeza, K**a umefanya mapenzi hivi karibuni basi yafaa mpenzi huyo aarifiwe ili naye atibiwe pia.
Kisonono (Gonorrhea)

Ugonjwa wa Kisonono (gonorrhea) husababishwa pia na bakteria waitwao kitalaamu Neisseria gonorrhea unapofanya mapenzi na mtu mwenye kisonono.

Ugonjwa huu unaweza kuaathiri viungo k**a vile Uke, Uume, sehemu ya haja kubwa na ya haja ndogo, Koo au Mdomo k**a ukifanya Mapenzi ya kunyonyana.

Ishara na dalili (Signs and symptoms).

Wanaume huwa na dalili k**a;

Uume kutoa ute wa njano au kijani.
Kupata maumivu wakati wa kukojoa (mkojo kuchoma).

Pia kuna uwezekano wa kuwashwa ama kutokwa na maji maji katika sehemu ya kupitishia haja kubwa. Ingawa hivyo baadhi ya watu hawaoni dalili zozote kabisa lakini bado wanaweza kuwaambukiza wanaofanya mapenzi nao.

Trichomonas Vaginalis – (TV)

Hiki nacho ni kijidudu cha bacteria, kidogo kinachoambukiza kupitia ukeni na kwenye mrija wa kupitishia mkojo.

Ugonjwa wa Trichomoniasis unasababishwa na vimelea vya jamii ya protozoa vinavyojulikana kitalaamu k**a Trichomonas va**nalis.

Ugonjwa huu huathiri mrija wa kupitisha mkojo (urethra) na uke wa mwanamke (va**na).

Huathiri sana wanawake kuliko wanaume na wanawake wenye umri mkubwa wako katika hatari zaidi kuliko mabinti wadogo.

Hupatikana kwa njia ya kujamiana bila kutumia kinga na mtu aliyeathirika na Trichomoniasis.

Ishara na dalili (Signs and symptoms).

Dalili za Trichomoniasis huanza kuonekana kuanzia siku ya 4 mpaka ya 28 baada ya mtu kupata maambukizi, Wanaume huwa hawaonyeshi dalili zozote lakini baadhi wanaonyesha dalili k**a;

Kuwasha ndani ya uume,
Kutokwa na uchafu au majimaji kutoka kwenye uume.
Kuwasha au mkojo kuchoma wakati wa kukojoa au baada ya kutoa shahawa.

Dalili kwa mwanamke aliyeambukizwa ni;

Kutokwa na uchafu wa rangi ya njano/kijani ulio k**a mapovu huenda ukawa na harufu k**a ya samaki .

Harufu mbaya inayoambatana na kutokwa na uchafu,
Kuongezeka kwa uwingi wa uchafu wa ukeni.

Maumivu ya ukeni au sehemu za nje ya uke (v***a),
Kujisaidia haja ndogo mara nyingi zaidi,
Kuwashwa sehemu za siri.

Matibabu; Ugonjwa huu unaweza kutibiwa kwa urahisi, kwa madawa maalam ya kupambana na viini antibiotics.

Ili kuepuka kuambukizwa upya, na kusambaa zaidi kwa ugonjwa huu inabidi mpenzio pia naye atibiwe.

Mwanaume asipopata matibabu mapema huongeza hatari ya kupata maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI na huongeza hatari ya kupata saratani ya tezi dume.

Magonjwa mengine ya njia ya mkojo
Magonjwa mengine yanayoathiri njia ya mkojo husababishwa na bakteria na huathiri mfereji wa kupitisha mkojo (urethra).

Magonjwa hayo husambazwa kwa kujamiiana. Dalili kwa wanaume ni kutokwa na ute kwenye tundu la uume na huenda akahisi maumivu wakati wa kukojoa au akahisi maumivu na kuwashwa-washwa kwa pamoja.

Cystitis

Huu ni uvimbe mgumu, Huambukiza kupitia bacteria ambao huishi chini ya ngozi, eneo la sehemu za siri na hata kwenye utumbo mkubwa.

Ishara na dalili (Signs and symptoms).

Dalili kubwa ni Maumivu makali wakati wa kukojoa.
Kujisikia kutaka kwenda chooni mara kwa mara.
Maumivu yanaweza kuendelea kuwa makali kwa haraka sana.

Huwakumba zaidi wanawake hasa wakati wa hedhi na wakati wa hali fulani nyinginezo k**a vile kuwa na Ujauzito, au kuugua ugonjwa wa Kisukari.

Usipotibiwa kwa haraka unaweza kusambaa hadi kwenye figo na kusababisha madhara mabaya zaidi.

Matibabu: Kunywa maji kwa wingi au vinywaji majimaji k**a maji ya matunda (juisi hasa ile ya cranberry) Unapoona tu dalili za kwanza kwanza, juisi hiyo inaweza kusaidia sana. Hata hivyo ni vyema kumuona daktari kwa uchunguzi na dawa zinazokufaa.

Thrush

Huu ni ugonjwa wa kuvimba vimba ndani kwa ndani mwilini. Kwa kawaida husababishwa na 'fungus'- kukua kupita kiasi kwa kitu k**a hamira. Ugonjwa huu unaweza kusambazwa kwa njia ya ngono lakini pia unaweza kutokea kutokana na sababu nyingine, kwa mfano k**a kuvaa chupi, suruali iliyokubana zaidi, au k**a unaugua ugonjwa wa kisukari.

Ugonjwa huu unaweza kuwapata wanawake kwa wanaume.

Ishara na dalili (Signs and symptoms).

Dalili kubwa kwa wanawake ni;

Kupata maumivu na kujikuna kwenye mashavu ya upenyo wa Uke na sehemu ya kupitishia haja kubwa (mkunduni).
Kuhisi mfano wa kuanza vidonda katika eneo la sehemu za siri, Hali hiyo huambatana na kutokwa na majimaji mazito meupe kutoka ukeni yenye harufu k**a hamira, Sehemu hizo huenda zikawa nyekundu zaidi.

Wanaume;
Miwasho kwenye uume, hasa ncha ya uume (kichwa cha uume).
Kuhisi k**a karaha ya kupata vidonda.
Uume hutokwa na majimaji au ute mzito wa njano.
Matibabu: Pindi ukigunduliwa ugonjwa wa Thrust hutibika kwa urahisi. Daktari hupendekeza vidonge au krimu maalum ambazo zinapatikana kwa wingi, kwenye maduka ya madawa.

Muone daktari endapo;
Ikiwa unapata dalili isiyo ya kawaida ni busara kutafuta msaada wa kitabibu na siyo kusubiri mpaka hali inakuwa mbaya au kutumia dawa kiholela bila bila ushauri wa daktari.

Wanawake:
Maji maji au ute unaotoka kwenye uke ni hali ya kawaida, lakini wanawake wanapaswa kutafuta usaidizi wa kimatibabu wakigundua lolote kati ya yafuatayo;

Majimaji ya ukeni ambayo yana harufu isiyo ya kawaida na yenye rangi tofauti na wingi kuliko ilivyo kawaida.
Maumivu au kusikia k**a unachomeka au mwasho wakati wa kukojoa.

Maumivu na miwasho katika maeneo ya Uke.
Maumivu ya ukeni wakati wa kufanya ngono.
Vidonda na malengelenge katika eneo la Uke.

Wanaume:

Mwanaume anapaswa kwenda kutafuta ushauri wa daktari k**a ana dalili zifuatazo:
Majimaji kutoka uumeni ambayo yana harufu isiyo ya kawaida, au yakiwa mengi.

Kuhisi mwasho ndani ya uume, wakati na baada tu ya kwenda haja ndogo.

Vijidonda na sugu ama malengelenge juu au kwenye uume.
Vipele au uvimbe katika sehemu za siri.

Kumbuka, baadhi ya maambukizi huenda yasiwe na dalili. Hii haimaanishi kwamba huwezi kumwambukiza mpenzi wako, au kwamba hayawezi kukudhuru kiafya. K**a una wasi wasi, ni vyema kuchunguzwa na daktari haraka iwezekanavyo, ama katika kliniki.

Ikiwa umefanya mapenzi bila kutumia kinga na una wasiwasi huenda umeambukizwa, nenda ukafanyiwe uchunguzi na daktari.

Kwa mara nyingine tena, kumbuka maambukizo mengine k**a ya virusi vya ukimwi yanaweza kuwemo mwilini kimya kimya kwa muda bila dalili zozote kujitokeza.

Unaweza kuwa hutaona dalili yoyote kwanza, lakini haimaanishi kwamba huwezi kuwaambukiza wengine.

Athari (Risk factors)

Madhara ya Magonjwa haya kwa wanaume ni kuathiri korodani na kusababisha mwanamume kukosa uwezo wa kutengeneza mbegu za uzazi (manii/shahawa) au kuwa tasa na pia husababisha maambukizi kwenye tezi dume (prostatitis).

Kwa wanawake, husababisha maambukizi kwenye mirija ya uzazi, mfuko wa uzazi, na mayai ya uzazi, kwa hivyo kusababisha ugonjwa wa uvimbe katika fupanyonga (PID).


Pia huongeza uwezekano wa wanawake kupata mimba zinazotunga nje ya mfuko wa uzazi (Ectopic pregnancies).
Mwanamke hupata maumivu sugu kwenye nyonga na ugonjwa wa mifupa (arthritis) aina ya Reiters syndrome. Vilevile, klamidia huweza kusababisha ugumba kwa mwanamke k**a hatapata tiba na kwa wanawake wajawazito, klamidia husababisha wajifungue kabla ya wakati wao.

Aidha, mtoto anaweza kuzaliwa na maambukizi kwenye masikio, sehemu za siri, macho na kwenye mapafu, yaani homa ya mapafu, na k**a mtoto hatapatiwa tiba ya haraka ya macho baada ya kuzaliwa basi anaweza kuwa kipofu.

Njia za kuzuia STIs (Prevention).

Njia sahihi ya kujikinga na magonjwa ya zinaa ni kuacha, kuepuka kujamiiana au kufanya ngono zembe na sizizo salama.

Kwa wanawake wajawazito, ni vizuri kuhudhuria kliniki mapema wakati wa ujauzito na kupimwa vipimo mbalimbali ili kubaini ikiwa mama mjamzito ameambukizwa na ugonjwa wowote wa zinaa na kupatiwa matibabu mapema.

Kwa wale wenye maambukizi wanashauriwa kuchukua tahadhari ya kutowaambukiza wapenzi wao kwa kufanya ngono salama.

MUHIMU;

TUNAFANYA KAZI KUPITIA ONLINE, HIVYO UAMINIFU NI KIPAUMBELE CHETU KIKUBWA, HATUNA MAWAKALA POPOTE, ILA TUNATUMA POPOTE KWA UHAKIKA NA UAMINIFU MKUBWA.

Wasiliana nasi kwa namba 0769 247 626

Address

Mwanza

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00

Telephone

+255769247626

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wema Herbal Clinic posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share