28/08/2015
MASHARTI KUMI YA KUZINGATIA
UWEZO KUPUNGUZA KITAMBI NA
UZITO MKUBWA BY DR MKUMBO
1-ULAJI
Ipo mifumo miwili ya kula. Chakula unachokula na
namna unavyokila.
Unavyokula.
-Kuna kula vyakula vidogo vidogo vyenye madini,
vitamini, mafuta nk mara nyingi kwa siku; au kula
milo michache (mmoja au miwili) mikubwa ili
kujaza tumbo. Ulaji mdogo mdogo husaidia afya
na kuingia mwilini vyema kuliko ulaji mkubwa wa
mara chache. Tumbo lina musuli zinazofanya kazi
k**a mashine au mnyama. Gari likijaa sana
hupata taabu kwenda. Punda hivyo hivyo. Ulaji
mdogo mdogo unaosambazwa mara kadhaa kwa
siku ni bora maana mwili unachambua kila kitu
kwa wepesi na haraka. Unapokula milo michache
mikubwa unapalilia zaidi mafuta mwili.
(PENDEKEZO la kwa
nza. Asubuhi, kunywa maji kwanza, matunda,
kisha ndiyo chai na vitu vingine k**a mkate au
maandazi…)
-Wapo wanaodai kwamba wanakula matunda na
mboga.
Tatizo ni kwamba mipangilio yao huwa ya
makosa. Mathalan wengi hula matunda baada ya
chakula. Vimeng’enya chakula (enzymes)
tumboni hufanya kazi namna tofauti. Mathalan vile
vinavyonyambua matunda ni tofauti na
vinavyomeng’enya vitu vigumu zaidi k**a nyama
au wanga. Matunda hunyambuliwa haraka zaidi
kuliko vyakula vingine. Hivyo ni bora kula
matunda dakika10-20 kabla ya chakula. Ukila
baadaye matunda hugeuzwa aina fulani ya pombe
(fermented food) inayoelea tu juu ya chakula na
kubakia kitu kingine badala ya kuingizwa haraka
ndani ya damu kupitia utumbo mdogo, uwengu,
moyo, ini, nk.
Tatizo jingine ni kupika sana mboga hadi
zikapoteza nguvu.
-Mseto wa vyakula pia ni muhimu. Kwa mfano
vyakula vyenye uchachu (“acid”) na vile
vinavyomumunyuka haraka (“alkaline”) havitakiwi
viliwe pamoja. Mfano ni matunda. Matunda
chachu k**a machungwa, mananasi na maembe
yatakiwa yawe pamoja; na yale laini zaidi: ndizi
mbivu, matikiti maji, mapapai, matufaha, nk
Hali hiyo pia iko katika nyama. Nyama nyeupe
(ndege na samaki) tofauti na nyama nyekundu
(ng’ombe, kondoo, nk) ziliwe tofauti.
Chakula unachokula
Waafrika hatuna tabia ya kula mboga mboga
mbichi. Tunafuata ladha na mazoea kuliko
thamani.
Bara letu lina mboga na vyakula bora kuliko bara
lolote duniani lakini sisi tunakufa mapema na kwa
utapia mlo kuliko wale wanaotoka nchi kame.
Ulaya nzima imejazana mboga mboga
zinazoagizwa toka Afrika. Kenya na Tanzania
zinauza mboga za maharagwe mabichi (green
beans), matunda toka Afrika Kusini na Ivory
Coast; nk. Waafrika tunapenda kujaza matumbo.
Unene umekithiri hata wale walio matajiri
waliosoma bado wanakufa kwa kisukari shauri ya
kutokula mboga mbichi.
Ulaji wa mboga mbichi ni upi?
Ni mathalani ulaji wa salad. Tanzania tunaita
kachumbari. Lakini si lazima iwe kachumbari ya
nyanya, vitunguu na chumvi tu. Waweza
kuchanganya matango, nyanya kwa maparachichi;
au vitunguu saumu, giligilani na karote. Huu
mseto wa mboga mbichi ni mzuri ukienda na
chakula chenye nyama za minofu na wanga (ugali,
wali, ndizi za kupika nk). Ulaji wa wanga asubuhi,
mchana na jioni kila siku huchangia sana katika
unene.
(PENDEKEZO LA 2. Ugali kwa samaki; mboga ya
majani ya matango kwa nyanya. Usiweke chumvi
kwenye chakula
2-UNYWAJI MAJI
Waafrika hatunywi maji, hasa wanawake.
Wanaokunywa maji zaidi ni wacheza michezo.
Wengi wetu hunywa zaidi soda (vinywaji baridi
k**a Cocacola, Pepsi, Mirinda ,Tangawizi na gesi
za kisasa k**a Red Bull) zilizojaa gesi inayoleta
vidonda tumboni; na chai. Kuliko maji. Na maji
haya hutakiwa dakika 10-20 kabla ya chakula au
nusu saa kuendelea baada ya chakula. Ukila
chakula huku unasakatia maji huimanisha mtu
una kiu. Ulaji chakula na unywaji maji ni vitu
viwili tofauti. Ila utawaona watu wanakula huku
wakibugia maji. Unapokula chakula huku unabugia
maji unapunguza nguvu za chakula, unajaza
tumbo maji na kuchelewesha mmeng’enyo wa
chakula (digestion).
Chakula kisipomeng’enywa vizuri kinaketi tu
tumboni. Matokeo wengi wetu tuna matumbo
makubwa. K**a hufanyi mazoezi lile tumbo
linakwenda pembeni (chini ya mbavu) hasa kwa
watu wa makamo linaleta maradhi k**a kisukari,
kiungulia, kuvimbiwa, uyabisi wa tumbo, nk.
Kizungu huitwa “love handles.”…
3-SUALA LA UMENG’ENYAJI
Chakula huanza kumeng’enywa au kusagwa (kwa
lugha iliyozoeleka) mdomoni. Mate yako mdomoni
ni chanzo cha uchambuaji chakula. Unapobugia
chakula bila kutafuna sawasawa unasababisha
mambo mawili. Moja chakula kutochambuliwa
vizuri, pili chakula kwenda kukaa tu tumboni, au
k**a kikipita hakisaidii lolote mwilini. Utafunaji
wa taratibu husaidia umeng’enyaji. Chakula
kinapofika tumboni hukaa pale dakika ishirini.
Hapo huchanganywa na asidi (ya manjano iitwayo
Hydrochloric) inayokibadilisha tayari kupelekwa
utumbo mkubwa, kupitia kongosho. Kule uchafu
utapelekwa chini na rutuba kusafirishwa na
utumbo mdogo kuelekea katika uwengu, moyo.
Moyo utadunda chakula kilichoshageuzwa damu
kuelekea mwilini kufanya kazi na akiba
hubakishwa katika ini.
Sasa k**a usipotafuna vizuri, ukila huku
unakunywa sana maji au vinywaji vingine chakula
hakimeng’enywi vizuri. Ndiyo maana unawaona
watu wengine wanakula sana lakini hawana afya.
Wanaugua ovyo ovyo, wanatoka jasho ovyo,
wanajamba ovyo, wana matumbo makubwa,
wanavimbiwa, wanakaa siku nyingi bila kwenda
choo (inatakiwa mtu kwenda haja kubwa mara
moja au mbili kwa siku) nk.
4-ULAJI WA VYAKULA VYA MAFUTA
Mafuta ni suala muhimu sana mwilini. Ila ulaji
wake shurti uwe wa mpangilio. Yaani unaowiana.
Lazima mtu uwe na wastani mzuri wa vyakula vya
nguvu, yaani “wanga” (ugali, ndizi, wali, viazi
mbalimbali, mikate, mahindi, nk), ujenzi yaani
“protini” (mboga na nyama), “madini” (mbegu
mbegu mbichi si za kukaanga sana na chumvi) na
“vitamini” (matunda, maziwa, mayai, nk).
Waafrika tunapenda nyama. Nyama ni muhimu
sana maana ina madini aina ya chuma (nyama
nyekundu) protini,nguvu na mafuta. Ila mafuta
yaliyoko katika nyama mara nyingi si mazuri
shauri hayatoki, huganda. Chukua nyama ya kuku
na samaki ambayo huwa na ngozi. Wengi wetu
hupenda sana kula ile ngozi ya wanyama hawa
kwa kuwa tamu. Lakini haya ni mafuta mabaya.
Mafuta ya samaki lakini ni mazuri. Samaki anayo
mafuta ya Omega-3 ambayo husaidia mwili na
kinga maradhi mwilini.
Tunapokula nyama choma au ya kukaanga, lazima
tule pia mboga za majani (mbichi) na si vizuri
kula nyama kila siku. K**a huwezi kukaa bila
nyama kila siku, fanya mazoezi ya mwili.
PENDEKEZO LA 3- Kula mbegu mbegu za
korosho, karanga au mlozi (ziwe mbichi badala ya
kukaanga na chumvi) kati kati ya siku. Haya ni
mafuta yenye rutuba mwilini kuliko nyama za
mafuta.
5-MAZOEZI YA MWILI NA VIUNGO
Mazoezi ni mfalme wa kupunguza unene.
Ukiwauliza wengi watakuambia wanafanya kazi
ngumu za sulubu (wanachuruzikwa jasho) kwa
hiyo hayo ni mazoezi. Ila kazi na mazoezi ni vitu
viwili tofauti. Ingekuwa kufanya kazi ni mazoezi
basi kusingekuwa na wastani mfupi wa maisha
kwa maskini hasa sisi Waafrika.
Wengine watadai kwamba walipokuwa wadogo
shuleni walifanya mazoezi sasa wamekuwa watu
wazima (miaka 40 kuendelea) kwamba eti
mazoezi ni suala la ujana; kumbe kadri
unavyokuwa ki umri ndivyo kadri unavyotakiwa
kufanya mazoezi na kujitazama zaidi kiafya.
Watazame Wachina na Wajapani wanavyoishi
maisha marefu.
Mazoezi ni shughuli inayokufanya kwanza uheme
(mapafu na moyo kwenda kasi), viungo na mifupa
kujinyoosha (stretching), kutoka jasho na
usafishaji wa damu. Mazoezi yanayosaidia haya ni
pamoja na kutembea kasi, kukimbia, kuogelea,
michezo mbalimbali ya riadha (k**a mpira wa
miguu, nyavu, kikapu, mikono, nk); michezo ya
kupigana na kujilinda yaani masho ati(karate,
kung fu, judo, capoeira, krav maga, jiu jitsu,
systema, kickboxing, thai boxing, kempo, kalari
payatu, aikido, nk) …
Ni muhimu mwanadamu ufanye mazoezi makali
ya viungo mara mbili tatu kwa juma. Si vizuri
kufanya kila siku kwani musuli na mishipa
inahitaji kupumzika na kukua.
K**a unapenda kuinua vyuma lazima uwe na
mwalimu wa kukuelekeza; na si vizuri kufanya kila
siku. Wastani wa mara mbili tatu kwa juma
inatosha kabisa.
6-UPO UFANYAJI MAZOEZI WA AINA MBILI
Mazoezi ya nguvu ya kuhema niliyotaja hapo juu
(cardio-vascular) na yale laini ya kujinyoosha
yaani ambayo hutumia zaidi nguvu za ndani na
pumzi. Haya ya pili ni k**a Yoga (India) , Tai Chi
Chuan (China) na aina mpya mazoezi iliyoanza
Majuu miaka ya karibuni yaani Pilates (hutamkwa
hivyo hivyo ilivyoandikwa Pilates). Haya laini
yanawafaa zaidi watu wazima na nchini China na
Japan mathalan utawakuta wazee wa miaka 80
hadi 90 bado wanayafanya. Husaidia moyo, damu
na akili.
Michezo na mazoezi ya mwili ni njia kuu ya
kupunguza unene, kurefusha maisha,
kuchangamsha ubongo, kupunguza ulevi, uvutaji
sigara, dawa za kulevya, tabia mbaya za uvivu,
ugomvi, nk. Mataifa yenye watu wanaofanya
mazoezi k**a Japan, Brazili, India, China nk
huwa na wachapa kazi wengi na wananchi
wanaoipenda jamii yao.
7-KULA SANA CHUMVI SI VIZURI
Ulaji chumvi mwingi hutokana na suala la ladha.
Kisayansi vyakula vyote vina chumvi asilia sema
tu tumezoea kuongezea madini hii iitwayo
Sodium. Sodium inachangia sana kufupisha
maisha. Huifanya mishipa ya damu ichoke; ni
k**a bomba lolote la maji ukilitazama baadaye
hugeuka rangi kutokana na yale maji kupita pale
kila siku.
Kwa wale tunaoishi nchi za joto na kutoka sana
jasho kula chumvi ni muhimu. Ila tatizo letu ni
kwamba hatunywi maji ya kutosha. Mtu ukiwa na
kiu unakunywa soda au kinywaji cha sukari;
inakuwa k**a unaendelea kuutesa mwili. Kwa
vipi? Mishipa inayopitisha damu mwilini badala ya
kusaidiwa kwa maji inawekewa kazi zaidi ya
kusafisha sukari na chumvi. Ndiyo maana vifo
vingi vinatokea mapema; wastani wetu wa maisha
haupiti miaka 50.
Utafiti uliofanywa chuo kikuu cha California,
Marekani mwanzoni mwa 2010, umethitibisha
kwamba vifo vingi duniani husababishwa na
maradhi ya moyo na saratani ambavyo hutokana
na uvutaji sigara, unene, ulevi na ulaji sana wa
chumvi na sukari. Tukipunguza ulaji wa chumvi
tunasaidia pia kupunguza maradhi ya moyo, utafiti
unasema.
8-TAFITI ZA VYUO KADHAA ULIMWNGUNI
KUHUSIANA NA AFYA
-Jarida la Kimarekani la sayansi lilieleza mwaka
jana kwamba utapunguza ugonjwa wa moyo
(ambao husababishwa na unene , wasiwasi na
purukshani) kwa asilia mia 42 k**a utakula
matunda na mboga za majani peke yake kila siku,
juu ya msosi wa kawaida.
(PENDEKEZO LA KULA- Na 4- Kula mlo wako.
Baada ya saa mbili au tatu, sakatia tunda au
matunda; baada ya mlo mwingine, kula sahani ya
mseto wa mboga mbichi k**a karote na
matango. Utaona tofauti ya afya, ngozi, wajihi,
kinyesi, usingizi, nk. Kidesturi tumezoea kunywa
chai au soda za sukari sukari na gesi kati kati
nya milo badala ya matunda na mboga mbichi za
majani).
-Utafiti uliofanywa na wanasayansi chuo kikuu
cha South Carolina mwanzo wa mwaka 2010
kuhusu faida za kuogelea.
Zoezi la kuogelea lina faida zaidi ya kukimbia au
kutembea kwa vile huchanganya mazoezi makali
na pumzi, kusaidia mapafu na moyo. Utafiti
ulithibitisha kuogelea hupunguza hatari za kifo
kwa asili mia hamsini.
-Utafiti wa jarida la chuo cha uganga Ulaya
umeeleza (desemba 2009) kwamba kulala nusu
saa kila mchana (“nap”) husaidia kupunguza
ugonjwa wa moyo kwa asilimia 37.
-Uchunguzi wa chuo cha michezo cha Hispania
mwanzoni mwa 2010 umethibitisha kwamba
ukikimbia mara tatu kwa juma (jogging)
unaongeza nyege mwilini kwa asili mia 75. Hasa
kwa watu wa makamo mnaoanza kupoteza nguvu
za urijali.
-Uchunguzi chuo kikuu cha Leeds, Uingereza
mwanzoni mwa 2010 umeonyesha unapotembea
kwa miguu, ukikwepa barabara kubwa zisisokuwa
na mioshi ya magari (pollution) unapunguza
matatizo ya maradhi ya hewa chafu k**a pumu,
mapafu na appendix.
-Uchunguzi wa chuo kikuu cha Texas mwaka
2010 umegundua kwamba kula tunda la divai
nyekundu mara kwa mara husaidia kupunguza
kupata ugonjwa wa kisukari.
-Hapo hapo tunaelezwa kwamba watu weusi na
bara la Asia wanakumbwa zaidi na ugonjwa wa
kisukari kutokana na vinywaji vya sukari sukari na
gesi (fizzy drinks). Ukinywa kiasi cha miligramu
300 za vinywaji hivi (Cocacola, Red Bull, Fanta
)
9-KUFUNGA
Neno kufunga linatambuliwa rasmi kuhusiana na
Waislamu (mwezi Ramadhani) au Wakristo (Lenti
nk). Ufungaji huo una masharti mengine ya kidini
tofauti na haya ya kiafya.
Mathalani wafungaji hawa hula chakula kingi
usiku; ukihesabu wanafunga wastani wa saa 12
tu. Kawaida ukitaka virusi na takataka nyingine
mwilini zitoweke, au viungo vipumzike wahitaji
saa 20 kuendelea.
Ufungaji ninaouongelea ni ufungaji wa kutokula
kabisa kwa saa 24, 36 hadi 48 kuendelea…
Ufungaji ni nini?
K**a mashine yeyote mwili wa mwanadamu
unahitaji kupumzika na kujisafisha. Hata tukiwa
tumelala bado viungo mbalimbali mwilini
vinafanya kazi. Kwa hiyo faida ya kwanza kabisa
ya kufunga ni kuupumzisha mwili k**a
mfanyakazi yeyote anapokwenda likizo.
Faida ya pili ya kufunga ni kusafisha mwili
kutokana na uchafu ambao haukutoka (kinyesi
hakitoi mabaki yote toka utumbo mkubwa), dawa
na takataka za mazingira tunayoyavutia hewa,
virusi au kuyanywa katika maji na vyakula
mbalimbali na pia uchafu wa hisia, yaani hasira,
huzuni, nk.
Kuna ufungaji wa aina mbalimbali.
1-Kufunga kwa kunywa maji tu, saa 24
kuendelea…
2-Kufunga kwa kutokunywa maji au kula
chochote, saa 24 kuendelea…
3-Kufunga kwa kula tu matunda au mboga
zilizopondwa k**a karote, matango nk, saa 24
kuendelea…
Ufungaji huu unatakiwa ufanywe kwa mpangilio.
Kitu muhimu si tu kufunga bali NAMNA
unavyofungua. Ukianza kula tena, unaanza
taratibu. Kawaida ni vizuri kuanza na maji,
kikombe au bilauri ya kwanza taratibu. Subiri tena
nusu saa, bilauri nyingine, halafu hadi ya tatu,
halafu ndiyo matunda yasiyo ya chachu, na
kadhalika. Kuanza kufungua kwa kunywa chai ya
maziwa, uji au vyakula vingine vya wanga
hakusadii sana mfungo huu.
Maana lengo lake ni kusafisha mwili.
PENDEKEZO LA 5- Kwa wenye imani za kidini.
Unaweza pia kufunga hivi ukawa pia unasali au
kuvaa mavazi yanayokufanya mtu wa amani.
Ukifanya hivi unajitakasa kimwili na kiroho. Si
lazima ungojee ile miezi ya kufunga na wengine.
10-USINGAJI
Usingaji au masaji ni njia nzuri sana ya
kupunguza unene. Ikiwa unaangalia namna
unavyokula, unafanya mazoezi na kusingwa mara
moja au mbili kwa mwezi unaupalilia mwili vizuri.
Nini faida ya usingaji? Kusinga husaidia ngozi,
mishipa ya damu na sura nzima ya mwili na
taswira yako mwanadamu. Wengi wetu
tunaposikia neno kusinga tunafikiria usingaji wa
mapenzi. Hivi ni vitu viwili tofauti kwani usingaji
wa mapenzi unaimanisha mahusiano ya kihisia.
Kifupi mwanadamu unatakiwa uwe unautunza na
kuungalia mwili wako k**a nyumba au hekalu
lako. Wengi wetu tunaoga, tunajipaka marashi,
tunasuka, tunanyoa nywele au ndevu; lakini miili
yetu kiundani inaoza taratibu…
Kwa maswali ya kiafya chakula k**a tiba
unaweza kunitumia sms kupitia no 0754509936