Grado company ltd

Grado company ltd for providing education to people about health and tell people oppurtunity about business of 21centu

07/10/2015

NENDA HATUA MOJA ZAIDI JE WEW UNAENDA HATUA MOJA ZAIDI KWA UNACHOKIFANYA JIFUNZE HAPA
mpendwa ili uone uzuri wa kitu lazima uweke sheria ya kwenda moja zaidi yaani namaana ujiongeze kutoka kile ulichofundishwa au unachokifanya k**a wataka kuwa bora na kufanikiwa kwa kila kitu ufanyacho nenda hatua moja ya mwenzio
mfano kam mwalimu ametoa kitabu kimoja cha kusoma wew soma viwili na zaidi
au k**a fulan kwenye biashara kaishia hapa wew nenda mbele zaidi
watu wengi wameridhika tu baada ya kuona tu kidogo alichopata hapana inabidi uende hatua nyingine mim namshukuru mkufunz wangu(mentor) lkn aliyonifundisha nimeyafanyia kazi lkn nimeenda hatua moja zaidi yaan nimejiongeza nawe pia ukiifata sheria hii itakusaidia
by grace shayo
0754509936

25/09/2015

Biashara ya mtandao (network marketing)
Biashara ya Mtandao ni njia ya kisasa ya usambazaji wa bidhaa kutoka kiwandani hadi kumfikia mteja au mtumiaji moja kwa moja. Hivyo, kiwanda kinazalisha bidhaa tu. Halafu kuna mtu mmoja tu ambaye ni msambazaji anayehusika na kufikisha bidhaa kwa mteja. Katika mfumo wa biashara za kawaida, kiwanda huzalisha bidhaa kasha huwauzia labda Depot au mawakala wakuu. Hawa huwauzia tena wasambazaji au wauzaji wa jumla, nao pia huwauzia wauzaji wa rejareja ambao watamfikishia mteja. Kwahiyo, bidhaa inaweza kuzalishwa kiwandani kwa tsh 380 lakini mteja ataipata kwa tsh 600. Kuna tsh 220 inagawanywa kwa watu wa katikati. Lakini hapo hapo utagundua kiwanda hakipati faida kubwa sana kwa sababu, katika hiyo hiyo 380 kuna gharama za usambazaji, kuwalipa macelebrities kwa ajili ya matangazo, radio, television, mabango, magazeti na hata mitandao ya kijamii, pamoja na gharama za sales department na mengineyo. Mwisho wa siku, utakuta kiwanda unaweza kukuta katika 380, baada ya kutoa gharama zote labda 180 ndiyo inaweza kubaki k**a faida.

Katika biashara ya mtandao, ile 220 ambayo inagawanywa kwa watu wa katikati, anapewa mtu mmoja tu ambaye ni msambazaji atakayenunua bidhaa toka kiwandani kwa tsh 380 na kumfikishia mtumiaji kwa tsh 600. Hivyo, kiwanda hakitalipia tena gharama za matangazo, mabango pamoja na nyingine ila kitamuelimisha huyo msambazaji kuhusu bidhaa ili yeye sasa aweze kumfikishia mtumiaji moja kwa moja. Hivyo kiwanda kinampa msambazaji uhuru wa kuwashirikisha watu wengine ambao watakuwa washirika wake katika biashara ili aweze kukuza biashara yake. Atawafundisha hao washirika wake katika biashara ili nao wawe na uwezo wa kufanya k**a yeye. Lakini atanufaika kwa kila mtu anayemshirikisha katika biashara kwa kupata asilimia za mauzo ya hao pamoja na timu zao

Atakuwa amegawa muda wake vizuri na kutengeneza kipato kizuri hata yeye asipofanya kazi, endapo atajenga timu. Lakini tambua kila mmoja ana fursa sawa ya kutengeneza kipato. Kipato kikubwa hutegemea jinsi mtu atakavyokuwa na timu kubwa kwa kuwashirikisha watu wengi katika biashara. Msingi wa hii biashara ni kushirikishana habari kuhusu bidhaa au huduma inayotolewa na kampuni halafu unanufaika na kutengeneza kipato. Lakini una uhuru wa kuanzisha kampuni yako `invisible company` ambapo utafanya biashara na kampuni na kutanua wigo wa biashara yako kwa kuwekeza muda wako kuwafundisha wengine biashara ambao watakuwa washirika wako kwenye biashara kwa kuwa na kipato kisichokuwa na kikomo.

Hayo ni maelezo mafupi tu kuhusu biashara ya mtandao japo ni biashara kubwa sana na inahitaji kujifunza kwa kina na kuielewa kwani ili ufanikiwe katika biashara ya mtandao lazima ujifunze upate kuielewa vizuri, hapo utafanikiwa. Nimekutana na watu wengi walioshindwa hii biashara, karibia wote nimegundua hawakuwa na uelewa mzuri wa biashara. Hapa huhitaji pesa ili utengeneze pesa, ila unahitaji maarifa. K**a huna maarifa ya kutafuta pesa unaweza leo ukashinda tuzo ya shilingi million 100, lakini baada ya miez 3 ukawa kapuku wa kutupwa!.

Kuna watu wengi maarufu duniani wanaoamini katika hii biashara akiwemo Robert Kiyosaki Mwandishi wa vitabu vya Rich dad poor dad pamoja na vingine k**a The business of 21st century. Ameelezea vizuri sana hii biashara. Lakini yupo Professor Pat Utomi wa Pan African University anasema `Network marketing is the futuristic way of doing business now`. Bwana Bill Clinton pia katika hotuba yake alikuwa akiyashukuru makampuni ya network marketing kwa kuwapa watu fursa sawa na kubadilisha maisha yao. Lakini pia Bill Gates, aliwahi kuulizwa k**a angefilisiwa na kuanza upya angefanyeje?. Yeye alisema tu kwamba angechagua biashara ya mtandao. Lakini wapo wengine wengi wanaoiamini na kuwashauri watu wanaotaka mabadilko waifanye.

Kuna makampuni zaidi ya 5,000 yanayofanya biashara ya mtandao duniani. Hivyo unapotaka kufanya jaribu kuangalia kampuni boraNakushauri pia wewe unayependa hii biashara, usikurupuke ilimradi biashara ya mtandao, ila angalia kampuni itayokufaa. Lakini biashara ya mtandao sio `get rich quick scheme`, japo kuna watu wanatengeneza pesa nyingi ndani ya muda mfupi sana na kubadilisha maisha yao. Ni kitu ambacho kwa wakati mwingine kitakuchukua muda kuyapata mafanikio. Inaweza kukuchukua pengine hata mwaka mmoja kuanza kuona matokeo makubwa/kutoboa k**a waswahili wanavyosema. Ila mafanikio yakija/ ukitoboa tambua huwa ni ya kudumu.

Unapoamua kufanya biashara hii usimsikilize mtu, ielewe biashara halafu uamue k**a inakufaa kwa kulinganisha marketing plan na ndoto zako. Ukiona inakufaa, nakushauri anza maramoja. Ukitaka ushauri kutoka kwa watu utakutana na watu wa aina 3. Aina ya 1 ni wale wasiojua lolote kuhusu hii biashara na watakwambia haifai. Kundi la 2 ni wale waliowahi kuisikia, huenda hata kuifanya halafu wakashindwa. Hao watakupa sababu za kushindwa. Aina ya mwisho ni wale wanaofanya na wamefanikiwa na wanakushauri uifanye na kukuahidi sapoti ya kutosha. Nakuomba usikilize hili kundi la mwisho. Tambua hili ni kundi dogo sana kwani dunia imegawanyika, wengi ni watu wenye mtazamo hasi, waoga na hawana ndoto kubwa, au wana ndoto kubwa ila huacha hofu kuwazuia kufanya maamuzi sahihi.

Mi nakumbuka nilipoambiwa mara ya kwanza kuhusu hii biashara, kuna rafiki yangu wa karibu sana nilimshirikisha. Lakini alinivunja moyo na kunikatisha tamaa. Mimi sikumsikiliza kwa sababu nilijua maisha ni yangu na nimeshaona fursa. Nilianza kuifanya na baada ya muda mi sikumwambia kitu kuhusu pesa ninayotengeneza kwa mwezi ila aliona mabadiliko. Alikuja na kunambia anataka kuanza naye biashara, hadi leo yuko kwenye biashara na anafanya vizuri sana, anafurahia kipato. Hii hunipa picha kwamba, hii biashara inaweza kumtimizia mtu yeyote ndoto zake endapo atakuwa na fikra sahihi na kujifunza biashara. Ila sisi tuko tayari kutoa sapoti kwa yeyote anayetaka kuanza hii biashara ili kuhakikisha anafanikiwa nasi tuweze kufanikiwa pia kwani huu ndio msingi wa biashara hii. K**a una roho mbaya huwezi kufanikiwa hata kidogo na hii biashara haikufai, nakushauri tafuta biashara nyingine. Hii ni biashara ya watu wanaopenda kuwasaidia wengine pia wafanikiwe. Mimi nilipoanza biashara nilianza kuwashirikisha Ndugu, jamaa na marafiki, leo hii nimegusa maisha yao kwa kiasi kikubwa sana na wananishukuru na kuniombea.

Hizi ni baadhi ya sababu, kwanini ufanye biashara ya soko la mtandao:
1. Mtaji kidogo. Hii biashara haihitaji mtaji mkubwa sana.Mfano,ukitaka kujiunga na kampuni ya Neptunus,mtaji wake wa kuanzia ni shs.26000/= tu.Lakini haihitaji duka, wala haihitaji kutembeza bidhaa mtaani k**a machinga wala haihitaji vibali.
2. Mafunzo ya biashara bure na usaidizi. Kampuni imeandaa mfumo mzuri wa biashara ambapo utapata mafunzo ya biashara na usaidizi wa karibu hadi uwe na uwezo wa kusimama na kuitanua biashara yako kitaifa au hata kimataifa.
3. Flexibility. Hapa nazungumzia uhuru wa kupanga muda wako katika kuifanya biashara yako. Unaweza kuifanya kwa muda wako wa ziada angalau masaa 10 kwa wiki au unaweza kuamua kuifanya kwa muda wako wote. Watu wengi huanza kwa muda wa ziada, wakiona wamefanikiwa hufanya kwa muda wote.
4. Vipato vikubwa. Ni biashara ambayo itakupa vipato vikubwa ndani ya muda mfupi sana ukilinganisha na biashara zingine nyingi. Jitihada zinahitajika ili kuijenga biashara yako iweze kukua na kukupa faida kubwa. Kitu cha msingi ni kuwa na uelewa mkubwa wa hii biashara. Lakini ukifanya nasi biashara katika kampuni yetu utakutana na njia zaidi ya 10 za kutengeneza vipato katika kampuni. Ndiyo maana watu wanatengeneza vipato vikubwa sana.
5. Uwezo wa kuikuza biashara yako mahali popote pale duniani. Hii ni fursa ambayo unaipata katika hii biashara bure kwa kufanya biashara na watu sehemu nyingine duniani bila ugumu hata pengine wewe usipokuwepo huko.
6. Inarithika. Kitu ambacho nakipenda sana katika hii biashara ni kuweza kuirithisha. Utakapoishia ndipo yule mrithi wako ataanzia na kuendeleza. Hivo unapofanya hii biashara tambua umefanya investment ya maisha yako na vizazi vyako.
7. Ina rasilimali muda `leverage` hii ni siri kubwa sana ya mafanikio katika biashara yeyote kubwa na ndio msingi wa mafanikio. Watu wote waliofanikiwa katika biashara zao kubwa ni wazi kuwa wamewekeza katika rasilimari muda.
8. Ni njia pekee ya kumiliki biashara kubwa duniani. Hii biashara ina sifa zote za biashara kubwa, biashara yeyote kubwa ina mambo makuu 3 yafuatayo; Bidhaa/huduma, mfumo pamoja na Timu au watu wanaofanya kazi. Kwa Tanzania ili biashara iitwe kubwa lazime uwe na watu kuanzia 100 wanaokufanyia kazi. Kidunia idadi inayotakiwa ili iitwe biashara kubwa ni kuanzia watu 500. Lakini hii biashara unaweza kuwa idadi kubwa zaidi ambapo utakuwa na watu ambao hujawaajiri wala huwalipi mshahara ila umewekeza muda wako kuwafundsha biashara ili wafanye kile unachofanya waweze kufanikiwa nawe ufanikiwe maradufu.
9. Ni biashara ya kisasa ambayo inakwenda na wakati. Kila fursa ina wakati wake. Huu ndio wakati muafaka wa hii fursa. Hapa kwetu Tanzania imeanza muda sio mrefu sana lakini imebadilisha maisha ya watu wengi.
10. Imejengwa katika dhana ya DUPLICATION ambayo kwa mujibu wa Mwanasayansi Robert Einstein aliandika katika moja ya vitabu vyake kuwa; mfumo wowote unaobeba dhana hii itakuwa ni maajabu ya 8 ya dunia. Ziko faida nyingi sana na kuna picha kubwa sana ya biashara ambayo unatakiwa kuielewa k**a wewe ni mtu makini, una ndoto kubwa na unahitaji mabadiliko ya kweli katika maisha yako 0754509936 calls/sms & whatsap

23/09/2015

JE WATAMBUA VITU VINAVYOWAKWAMISHA WAJASIRIAMALI KUENDELEA
Zifuatazo ni sababu zinazowafanya wafanyabiashara au wajasiriamali kushindwa nazo ni: 1.Mjasiriamali kukosa uzoefu wa biashara
2. Mjasiriamali kukosa ujuzi na maarifa ya
masoko
3. Kukosa nidhamu ya pesa
4. Kukosa mtaji
5. Mauzo kuwa chini
6. Kushindwa kuendana na baadhi ya
wafanyakazi wake
7. Kuchukua mkopo mwingi bila matumizi
sahihi
8. Kukosa stadi za mafanikio katika
ujasiriamali
9. Kukosa msukumo binafsi wa kufanya
mambo sahihi
10. Kujaribu kufanya biashara nyingi sana au
mambo mengi ambayo yote yanahitaji muda
na umakini ( lack of focus )
11. Kukosa ndoto na shauku ya kufanikiwa
12. Magonjwa na afya mbovu
13. Tabia ya kuahirisha mambo mra kwa mara
14. Kukata tamaa kwa urahisi mambo
yanapoonekana magumu
15. Mtazamo hasi ( negative mental attitude )
16. Hali ya kutaka kitu bila kitu.
17. Marafiki au washirika wasio sahihi katika
biashara yako ( mkeo au mumeo aweza kuwa
kikwazo)
18. Hofu na kutokuthubu
19. Kushindwa kufikiri kwa makin biashara gan ufanye
KABLA HUJAANZA AU UMEANZA BIASHARA ZINGATIA
YAFUATAYO:
• Chunguza siri za biashara zinazofanikiwa na
mifumo iliyopo nyuma yake. Jaribu
kuziangalia biashara Watu wengi huwa na wazo la
bidhaa ya kuuza au hata kutengeneza k**a
vile mshumaa , rangi , shampoo nk lakini mara
nyingi huwa hawana ujuzi wa kutengeneza
mfumo mzuri wa uletaji wa faida .hvyo angalia mafanikio ktk hiyo biashara na mfumo gani watumia
• Pata mlezi au mshauri ( Mentor )
atakayekusaidia katika safari ya ujasiriamali .
Neno mentor linamaanisha mtu ambaye
amefanikiwa kwenye jambo fulani na ana
uwezo wa kuwasaidia/kuwaelekeza watu
wengine wafanikiwe k**a yeye.
• Fanya kazi kwenye biashara ya mtu
aliyefanikiwa na ambaye unataka kuja kuwa
k**a yeye. Wakati mwingine , njia ya mkato ya
kujifunza biashara ni kukubali kutumika chini
ya mtu mwingine ili ujionee moja kwa moja
uendeshaji wa biashara kabla hujaamua
kuingia moja kwa moja.
• Jenga tabia ya kuwauliza maswali ya msingi
wajasiriamali waliofanikiwa. Kila unapopata
nafasi ya kuwa na mtu tajiri, jipe moyo mara
kwa mara halafu uliza swali hili : “ Je siri ya
mafanikio yako ni nini?”Utashangaa jinsi
ambavyo watu wengi si wachoyo wa siri zao
za mafanikio ili mradi tu uulize katika
mazingira mazuri yenye heshima na hekima .
5. Jijengee uwezo wa kuuza . Uwezo wa
kuwashawishi watu waweze kununua bidhaa
yako au kutumia huduma yako ndiyo uweze
kusimama katika ujasiriamali .
by grace shayo
0754509936

21/09/2015

habarini ndugu jamaa na marafiki karibun san ktk page yangu tuendelee kuelekezan mambo ya takayotufanikisha kimaisha karibun wote

Address

Pobox 405
Njombe

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Grado company ltd posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram