Njombe RRH

Njombe RRH Ukurasa Rasmi wa Hospitali ya
Rufaa Mkoa wa Njombe
59017 Ramadhani -Njombe
P. O Box 1044 Njombe

MKURUGENZI WA HOSPITALI YA KIBONG’OTO AITEMBELEA NJOMBE RRHMkurugenzi wa Hospitali Maalum ya Tiba ya Magonjwa Ambukizi k...
16/07/2025

MKURUGENZI WA HOSPITALI YA KIBONG’OTO AITEMBELEA NJOMBE RRH

Mkurugenzi wa Hospitali Maalum ya Tiba ya Magonjwa Ambukizi kibong’oto, Dkt. Leonard Subi leo hii Julai 16 ametembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe na kukutana na Menejimenti ya Hospitali ambapo amepata wasaa wa kutembelea maeneo mbalimbali ya utoaji huduma ikiwemo Kitengo cha Uchunguzi wa Magonjwa ya Mfumo wa Chakula na Maabara.

Ziara ya Dkt. Subi, imelenga kuangalia na kutoa ushauri wa namna nzuri ya kujikinga na magonjwa ya mlipuko na magonjwa ambukizi kwa kuimarisha huduma ya utambuzi na uchunguzi wa magonjwa hayo ikiwemo ugonjwa hatari wa Kifua kikuu.

Amepongeza Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe kwa kuendelea kusimamia uimara wa miundombinu ya Hospitali, ubora wa Huduma za Afya ikiwemo vipimo vya maabara , pamoja na kupata Ithibati ya Ubora wa Huduma za Maabara kutoka SADCAS.

Ameahidi kuwa Hospitali ya Kibong’oto itaendelea kushirikiana na Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe ikiwemo kuwajengea Uwezo wataalamu mbalimbali wa afya katika maeneo mbalimbali ya taaluma zao hususani eneo la uchunguzi wa maabara ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za Afya na utambuzi wa mapema wa magonjwa haya.

Kwa upande wake Mganga Mfawidhi, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe Dkt. Gilbert Kwesi amemshukuru Dkt. Leonard Subi na ujumbe alioambatana nao kwa ujio wake, kwa kile alichoeleza kuwa Uongozi wa Njombe RRH upo tayari kuendelea kushirikiana na Hospitali ya Kibong'oto kuimarisha afua za Kifua kikuu na magonjwa ambukizi kwa ujumla ikiwemo kutoa wataalamu wake ambao watapata nafasi ya kwenda kujengewa uwezo, kujifunza na kuongeza ujuzi, ili kuongeza ubora katika utoaji huduma.

Happy Sabasaba Day | 07, July
07/07/2025

Happy Sabasaba Day | 07, July

Jovin Binamungu ni Afisa Lishe, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe.Leo ametupitisha katika Dondoo chache na muhimu za ...
04/07/2025

Jovin Binamungu ni Afisa Lishe, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe.

Leo ametupitisha katika Dondoo chache na muhimu za kufahamu juu ya Uhusiano uliopo kati ya Afya ya Ngozi na Hali ya Lishe katika mwili.

Pindi unapohisi unahitaji ushauri wa masuala ya Lishe na Elimu kwa ujumla, usisite kufika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe, au wasiliana naye kwa namba

0782 367 247

"Huduma Bora ndio Kipaumbele chetu"

Dkt. Edward Mhina, ambaye ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake na Uzazi, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe anatu...
03/07/2025

Dkt. Edward Mhina, ambaye ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake na Uzazi, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe anatupitisha katika Dondoo muhimu za kufahamu kuhusu Ugonjwa wa Saratani ya Mlango wa Kizazi.

➡️Fasili

➡️Visababishi

➡️ Namna ya Kujikinga

➡️ Namna ya kuzuia Saratani ya Mlango wa kizazi.

Bunge la Tanzania limepitisha kwa kishindo Mapato na Matumizi ya fedha ya Wizara ya Afya kwa  mwaka wa fedha 2025/26 Shi...
03/06/2025

Bunge la Tanzania limepitisha kwa kishindo Mapato na Matumizi ya fedha ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2025/26 Shilingi Trilioni 1.6 ambapo Fungu namba 52 ikiwepo matumizi ya kawaida Shilingi Bilioni 626.4 na miradi ya maendeleo Bilioni 991.7

Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akiwaongoza viongozi na watumishi wa Wizara ya Afya katika ibada fupi viwanja vya Bu...
02/06/2025

Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akiwaongoza viongozi na watumishi wa Wizara ya Afya katika ibada fupi viwanja vya Bunge kabla ya kuwasilisha Bajeti ya Wizara ya Afya ya mwaka wa fedha 2025/26 leo Juni 2, 2025.

Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akiwasili katika viwanja vya bunge leo Juni 2_ 2025_ jijini Dodoma kwa ajili ya kuwa...
02/06/2025

Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama akiwasili katika viwanja vya bunge leo Juni 2_ 2025_ jijini Dodoma kwa ajili ya kuwasilisha bajeti ya Wizara ya Afya.

UJUMBE MUHIMU S**I YA HEDHI SALAMA DUNIANI
28/05/2025

UJUMBE MUHIMU S**I YA HEDHI SALAMA DUNIANI

TAARIFA MUHIMU KWA UMMA✍️✍️
20/05/2025

TAARIFA MUHIMU KWA UMMA✍️✍️

MOH YAWAJENGEA UWEZO WATAALAMU WA MAABARA, NJOMBE RRHWataalamu watano wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe kutoka Ida...
16/05/2025

MOH YAWAJENGEA UWEZO WATAALAMU WA MAABARA, NJOMBE RRH

Wataalamu watano wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe kutoka Idara ya Maabara na Kitengo cha Afya, Kinga na Mazingira wamejengewa uwezo katika ufuatiliaji wa magonjwa (Laboratory Based Surveillance) zoezi lililodumu kwa siku nne kuanzia Jumatatu, Mei 12 – hadi Alhamisi Mei 15.

Mafunzo hayo yameongozwa na wataalamu wawili kutoka Wizara ya Afya akiwemo Rais wa Chama cha Wataalamu wa Maabara (MELSAT) Bw. Yahaya R. Mnung’a na Mlezi wa Maabara Kanda ya Mashariki, Bw. Hamza Matimba.

Akifunga mafunzo hayo Rais wa MELSAT alisisitiza wataalamu wa Maabara kufanya kazi kwa kufuata miongozo iliyowekwa huku akiacha ujumbe wa mshikamano na umoja miongoni mwa wataalamu hao.

 

Kwa upande wake Mratibu wa Maabara Kanda ya Mashariki amesema kuwa Idara ya Maabara ni eneo nyeti na muhimu sana katika kugundua na kuthibitishwa kwa milipuko ya magonjwa kwa haraka, hivyo akaasa wataalamu hao kuitumia taalamu yao katika kuhakikisha taaluma yao inaleta tija kwa jamii.

 

Naye Mratibu wa Huduma za Maabara Mkoa wa Njombe, Bw. China Mbilinyi, amewaasa wataalamu wa Maabara Njombe RRH, kuwa na tabia ya kujisomea na kujiendeleza katika masomo ili kuendana na mabadiliko ya teknolojia katika maabara ikiwemo matumizi ya akili mnemba katika utoaji huduma za maabara.

WAUGUZI HALMASHARI YA MJI NJOMBE WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI.Wauguzi mbalimbali ndani ya Halmashauri ya Mji Njom...
12/05/2025

WAUGUZI HALMASHARI YA MJI NJOMBE WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI.

Wauguzi mbalimbali ndani ya Halmashauri ya Mji Njombe wamefanya maandamano ya Amani leo Mei 12, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya wauguzi duniani, yanayoambatana na kuuenzi mchango mkubwa uliofanywa na muuguzi wa kwanza duniani Florence Nightingale.

Maandamano hayo yamefanyika kuanzia Zahanati ya Idundilanga iliyopo Halmashauri ya Mji Njombe hadi Soko Kuu la Mji Njombe, ambapo wauguzi pia wametoa mahitaji mbalimbali kwa wagonjwa katika kituo cha Afya Njombe mjini.

Mgeni Rasmi katika maadhimisho hayo ni Afisa Tarafa ya Njombe Mjini Bi. Lilian Nyemele.

Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi duniani kwa mwaka huu, yamebebwa na kaulimbiu isemayo “Uuguzi nguvu ya Mabadiliko"

03/05/2025

Address

Njombe

Telephone

+255678888654

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Njombe RRH posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Njombe RRH:

Share