Njombe RRH

Njombe RRH Ukurasa Rasmi wa Hospitali ya
Rufaa Mkoa wa Njombe
59017 Ramadhani -Njombe
P. O Box 1044 Njombe

13/01/2026

Pata kufahamu huduma za Kliniki ya Pua, Koo na Sikio

Daktari, Elionora Sitta kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe leo Januari 13 anatupitisha katika moja ya Huduma za Kliniki hiyo, yaani Dondoo kuhusu Sikio.



05/01/2026

Bw. Eusebius Mbilinyi kutoka Halmashauri ya Madaba amefika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe baada ya Taarifa iliyosambazwa katika kurasa za Mitandao ya kijamii za Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe kutangazwa kwa mwananchi aliyefikishwa akiwa Mahututi kisha kuhudumiwa kwa siku 42 pasipo ndugu zake kujitokeza baada ya kufikishwa na watu wema akiwa mahututi.

Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe unaungana na wazazi, ndugu, jamaa na Marafiki wa Steven Eusebius Mbilinyi (anayetibiwa) kwa jamii, na wananchi wema waliosambaza taarifa hii iliyofanikisha kupatikana kwa ndugu zake.

Mungu awabariki na akawakumbuke.

Asante.

01/01/2026
TAARIFA KWA UMMA
30/12/2025

TAARIFA KWA UMMA

IDARA YA WATOTO WAFANYA TATHMINI YA KUFUNGA MWAKAIdara ya Watoto kwa kushirikiana na Idara nyingine za Hospitali ya Rufa...
30/12/2025

IDARA YA WATOTO WAFANYA TATHMINI YA KUFUNGA MWAKA
Idara ya Watoto kwa kushirikiana na Idara nyingine za Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe imefanya hafla fupi leo Disemba 30 ya kujifanyia tathmini katika Utoaji hudumakwa mwaka 2025, ambapo wale waliofanya vizuri katika maeneo mbalimbali wamepata zawadi ikiwa ni sehemu ya motisha.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mgeni Rasmi, Kamu Mganga Mfawidhi, Dkt. Lazaro Jassely ameipongeza Idara hiyo kwa kuwa moja ya Idara zilizofanya kazi kwa mafanikio makubwa kwa mwaka 2025.

Amesema ushirikiano uliopo miongoni mwa watumishi katika Idara hiyo unapaswa kuigwa na Idara nyingine za Hospitali ili kuendelea kuboresha hali ya utoaji huduma.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara hiyo, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Watoto, Mariam Gaitani, ameomba ushirikiano ulioonyeshwa na Idara nyingine kwa Idara hiyo ubaki kuwa endelevu, huku akiahidi kuwa 2026 utakuwa mwaka wa huduma bora zaidi.

Watumishi wa idara ya watoto waliofanya vizuri katika eneo la uongozi, ukusanyaji wa mapato na Huduma bora kwaMteja walipatiwa zawadi.
Aidha Idara ilitoa zawadi kwa vitengo na Idara nyingine zilizipo hapa hospitali ikiwa ni shukrani na ushirikiano mzuri wanaoipatia idara ya watoto.

Katika hafla hiyo, wakuu wa Idara pia na watumishi mbalimbali wameshiriki kwa kula keki ya pamoja k**a ishara ya kuendeleza ushirikiano na Idara hiyo.

Viongozi na wataalamu wa Afya kutoka Hospitali ya Consolata Ikonda, wametembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe le...
23/12/2025

Viongozi na wataalamu wa Afya kutoka Hospitali ya Consolata Ikonda, wametembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe leo Desemba 23, 2025 na kujionea hali ya utoaji Huduma katika jengo la Huduma za Afya ya Mama na Mtoto ambapo pia wamepata wasaa wa kubadilishana uzoefu na kushauriana na wataalamu wenyeji katika maeneo hayo.

Timu ya wataalamu hao imeongozwa na Elide Ambrositte ambaye aliongozana na Timu ya Wauguzi, na Madaktari kutoka Hospitali hiyo iliyopo wilaya ya Makete.

Akizungumza kwa niaba ya Mganga Mfawidhi, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake na Uzazi, Edward Mhina, amepongeza uamuzi uliofanywa na wataalamu hao huku akiahidi pia Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe kuendeleza ushirikiano ambao umekuwepo na Hospitali ya Ikonda, hasa katika maeneo ya kujengeana uwezo, kushiriki uzoefu ili kuendelea kuboresha hali ya utoaji huduma za afya kwa watanzania.

Kiongozi wa msafara huo wa wataalamu kutoka Ikonda, Bi. Ambrositte, amepongeza uwekezaji mkubwa uliofanywa na serikali katika eneo la Huduma za Afya ya Mama na Mtoto, ikiwemo wataalamu wa kutosha na miundombinu ya kisasa k**a vile vifaa na dawa; ambapo amesisitiza ipo haja kubwa ya kuendeleza ushirikiano miongoni mwa wataalamu ili kujengeana ujuzi na kubadilishana uzoefu baina ya Taasisi hizo mbili.

CALL FOR EXPRESSION OF INTEREST (EOI)
20/12/2025

CALL FOR EXPRESSION OF INTEREST (EOI)

Hongera Mheshimiwa Dkt. Florence George Samizi
17/11/2025

Hongera Mheshimiwa Dkt. Florence George Samizi

Hongera sana Mheshimiwa
17/11/2025

Hongera sana Mheshimiwa

Sehemu ya Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Bunge la 13 la Jamhuri ya...
14/11/2025

Sehemu ya Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambalo limefunguliwa rasmi leo Novemba 14, 2025.

Address

Mgodechi/Ramadhani Njombe Mjini
Njombe
59107

Telephone

+255678888654

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Njombe RRH posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Njombe RRH:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram