11/05/2026
Wizara ya Afya inatarajia kuongeza wigo katika eneo la Huduma za kibingwa katika Hospitali za Rufaa za Mikoa kutoka Huduma 11 zilizopo sasa hadi huduma 17 katika mwaka wa Fedha 2026/2027.
Hayo yamesemwa leo Mei 11, 2026 na Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa katika Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Afya iliyowasilishwa Bungeni jijini Dodoma.
Wizara ya Afya imeliomba Bunge kupitisha kiasi cha Tsh. Trilioni 1.8 kwa mwaka wa fedha 2026/2027