Sangulae Pharmacy CARE

Sangulae Pharmacy CARE Huu ni ukurasa unaojihusisha na utoaji elimu kuhusu afya na matumizi ya dawa. Unaweza kutembelea to

09/10/2024
SANGULAE AFYA CUP MECHI TAREHE 28/09/2024HOPE FILLING 2 - 3 UKWAMAMpira nia afya, imarisha afya yako na SANGULAE MAABARA...
29/09/2024

SANGULAE AFYA CUP
MECHI TAREHE 28/09/2024

HOPE FILLING 2 - 3 UKWAMA

Mpira nia afya, imarisha afya yako na SANGULAE MAABARA & DUKA LA DAWA - MABADAGA

SANGULAE AFYA CUP MECHI TAREHE 27/09/2024UKWAVILA 0 - 0 ITAMBA SQUADMpira nia afya, imarisha afya yako na SANGULAE MAABA...
29/09/2024

SANGULAE AFYA CUP
MECHI TAREHE 27/09/2024

UKWAVILA 0 - 0 ITAMBA SQUAD

Mpira nia afya, imarisha afya yako na SANGULAE MAABARA & DUKA LA DAWA - MABADAGA

ATTENTION:TOLEO JINGINE LA KITABU UTANGULIZI UPO HAPO CHINIUTANGULIZIKitabu hiki kimegawanyika katika sura kuu mbili; Su...
19/09/2024

ATTENTION:
TOLEO JINGINE LA KITABU UTANGULIZI UPO HAPO CHINI

UTANGULIZI
Kitabu hiki kimegawanyika katika sura kuu mbili; Sura ya kwanza inajihusisha na mfumo wa uzazi kwa wanawake, sura ya pili inajihusisha na mfumo wa homoni kwa wanaume.

SURA 1: MFUMO WA UZAZI WA MWANAWAKE
Uzalishaji wa homoni za k**e hujihusisha na mfumo mzima wa hedhi na mimba. FSH na LH ni homoni chochezi zinazopelekea kuzalishwa kwa Oestrogen na Progesterone.
Mzunguko wa hedhi kwa wanawake ni wastani kati ya siku 24 – 35, kwa mwanamke ambae yupo nje au siku zake hazieleweki humaanisha “kuvurugika kwa mzunguko wa hedhi”. Siku za hatari kupata mimba hukadiriwa kati ya siku 14 – 17 (nusu ya mzunguko wa hedhi hukadiriwa kuwa ni siku za hatari)
Changamoto za mfumo wa uzazi ni ugumba au kushindwa kushika mimba kwa urahisi na kwa baadhi ya wanawake mimba kuharibika mara kwa mara.
Ugumba ni changamoto ya kutoshika mimba mara baada ya kufanya mapenzi pasipo kinga kwa miezi 12. Changamoto ya kutoshika mimba hutokana na sababu mbali mbali k**a zifuatazo
(1) uvimbe katika ovari unaohisiwa kuwa na maji maji yenye sukari,
(2) homoni ya kuzalisha maziwa kuwa juu (hyperprolactinaemia) huepelekea kushuka kwa uzalisha wa homoni za k**e,
(3) maambukizi ya bakteria katika njia za uzazi (PID)

SURA 2: MFUMO WA UZAZI WA MWANAUME
Uzalishaji wa homoni ya kiume (Testosterone) huhusika na mambo yote ya mfumo wa kiume. Changamoto ya ugumba kwa wanaume hutokana na matatizo katika mfumo wa uzalishaji mbegu, kasoro katika vinasaba, maambukizi ya magonjwa ya zinaa ya mara kwa mara
Tatizo la nguvu za kiume kupungua linaweza kuelezwa katika namna tatu;
(1) kushindwa kupata hisia za tendo,
(2) Mishipa ya uume kushindwa kupata damu (uume kushindwa kusimamisha),
(3) Mishipa ya uume kushindwa kutunza damu (uume kushindwa kusimama kwa muda mrefu)

Kwa kutumia picha unaweza kutambua ni ugonjwa upi?Picha: www.medscape.com
21/08/2023

Kwa kutumia picha unaweza kutambua ni ugonjwa upi?

Picha: www.medscape.com

27/12/2022
ONYO; UTAPELINamba ya SANGULAE ONLINE PHARMACY CARE NI HII HII YA WHATSAPP 0659982039Yenye utambulisho wa jina la ELIA S...
18/10/2022

ONYO; UTAPELI

Namba ya SANGULAE ONLINE PHARMACY CARE NI HII HII YA WHATSAPP 0659982039

Yenye utambulisho wa jina la ELIA SANGULA (Maana halisi ya SANGULAE)

Usipokee simu wala kujibu meseji endapo namba itakuwa tofauti na hii

MAELEZO KUHUSU MUUNGANIKO WA DAWA (CHEMOTHERAPY COMBINATION)Magonjwa mengi na baadhi ya saratani hutibiwa kwa uhakika na...
02/10/2022

MAELEZO KUHUSU MUUNGANIKO WA DAWA (CHEMOTHERAPY COMBINATION)
Magonjwa mengi na baadhi ya saratani hutibiwa kwa uhakika na dawa moja. Ijapokuwa matibabu mengine hushindwa kutokana na sababu za usugu wa dawa au kuwepo kwa wadudu wengi wanaohitaji dawa tofauti tofauti au dozi ya dawa kuwa chini kwasababu za kuhofia kufikia kiwango cha usumu wake
---Sababu hizi hujitosheleza kufanya maamuzi ya kuziunganisha dawa; lakini lengo la kuunganisha dawa ni kuwapunguza wadudu au uvimbe wa saratani pasipo kuathili chembe hai za mwili. Ingawa kuziunganisha dawa ni kupanua wigo wa maudhi/athari zake

FAIDA ZA KUZIUNGANISHA DAWA
1) Kupunguza usugu wa dawa
2) Kuongeza ubora na ufanyaji kazi wa dawa katika kupambana na mdudu fulani au saratani fulani
3) Kupunguza kiwango cha usumu kinachoifikia chembe hai ya mwili
4) Kutibu magonjwa mengi kwa wakati mmoja
5) Kutibu magonjwa yanayohatarisha uhai kabla ya kumgundua mdudu husika
Kwasababu wadudu hawafanani vinasaba na binadamu, hivyo basi muunganiko wa dawa utalenga zaidi wadudu. Ingawa muunganiko wa dawa za saratani hudhibitiwa kulingana na maudhi/athari zake

UNAELEWA NINI KUHUSU KIWANGO CHA CHINI CHA DAWA CHENYE KUZUIA UKUAJI WA BAKTERIA (MIC-Minimum Inhibitory Concentration) NA CHENYE KUUA BAKTERIA (MBC-Minimum Bactericidal Concentration)
Dawa zenye kufanya kazi dhidi ya bkteria, vimelea au fangasi huwekwa kulingana na MIC na MBC. MIC ni kiwango cha chini cha dawa chenye uwezo wa kuzuia ukuaji wa bakteria mara baada ya masaa 18 – 24 wakati MBC ni kiwango cha chini cha dawa chenye uwezo wa kuua karibia 99.9% ya bakteria mara baada ya masaa 18 – 24. Kawaida MBC ni kubwa zaidi ya MIC, na mlinganisho huu huepekea dawa kuwekwa katika makundi mawili: dawa zenye kuua (cidal) na dawa zenye kuzuia ukuaji (static)

MIFANO YA DAWA ZILIZOPO KATIKA MUUNGANIKO MAALUMU NA FAIDA ZAKE
1. Matibabu ya kifua kikuu (Muunganiko ili kuepuka usugu wa dawa)
Dawa kwaajili ya matibabu haya zimesaidia kuonesha ni kwa namna gani muunganiko wa dawa unaweza kusaidia kupunguza usugu wa dawa.
Bakteria wa kifua kikuu huvutwa kwa njia ya hewa na kuingia katika mapafu, lakini kitu cha kushangaza ni kinga ya mwili kushindwa kuwaua au kuwapunguza kabisa. Uharibifu wa mapafu hutokea mara baada ya uzalishwaji wa neutral proteases na kemikali nyingine
Matibabu ya kifua kikuu yamekuwa ya mafanikio hasa kwa muunganiko wa dawa zifuatazo isoniazid, rifampin, pyrazinamide na ethambutol. Mara nyingi muunganiko huo hutumika kwa muda miezi miwili ya mwanzo kisha kufuatiwa na muunganiko wa dawa mbili ambazo ni isoniazid na rifampin kwa muda wa miezi minne. Lakini streptomycin na dawa nyingine hutumika k**a chaguo la pili endapo kukitoea usugu wa dawa katika muunganiko huu
NB: Isoniazid na rifampin hupendelewa zaidi kwasababu ya uwezo wao wa kuua aina zote za bakteria wa kifua kikuu (intracellular na extracellular mycobacteria)

2. Muunganiko ili kuongeza uwezo na ubora wa dawa
Kwa watu wenye upungufu wa kinga mwilini, uwezo wa dawa zenye kuua na kuzuia ukuaji hufanana kiuwezo. Ingawa dawa zenye kuua hupendelewa kutumika kwa wenye maambukizi ya ukimwi, waliofanyiwa upandikizaji na wenye saratani, wenye magonjwa ya moyo (bacterial endocarditis) au walioathiriwa na bakteria kwenye ubongo (meningitis). Kwanini muunganiko wa dawa zenye kuua bakteria hutumika zaidi kwa wenye upungufu wa kinga mwilini ni kwasababu hawana uwezo asilia wa kinga za mwilini wa kuzuia hata bakteria ambazo hazina uwezo wa kuzailiana kwa kujigwanya (nondividing bacteria)
Mfano mojawapo wa muunganiko ni dawa zenye kundi la penicillin na kundi la aminoglycoside katika matibabu ya endocarditis, staphylococcus aureus na streptococcus viridans. Faida ya kuziunganisha dawa hizi ni kutokana na uwezo wao, penicillin huvunja kuta za seli za bakteria na kisha kuruhusu aminoglycoside kuingia ndani ya seli ya bakteria aina ya gram-positive
Mifano mingine ya muunganiko ni k**a (1) dawa kwaajili ya fangasi ambazo ni amphotericin B na Flucytosine,ambap amphotericin huoingeza uchukuliwaji wa flucytosine na fangasi (2) dawa kwaajili ya bakteria na vimelea; kundi la sulfonamide na trimethoprim au pyrimethamine. Sulfamethoxazole na trimethoprim hutumika k**a muunganiko katika matibabu ta pneumocystis jiroveci kwa wenye VVU, pamoja ya UTI, sulfadoxine na pyrimethamine huunganishwa katika matibabu ya Malaria, toxoplasmosis nk

3. Muunganiko wa dawa katika kundi la penicillin, cephalosporin na kundi la dawa zenye kuzuia β-Lactamase
Penicillin na cephalosporin ni dawa zenye umbo la β-Lactam na huwa katika mazingira hatarishi kuharibiwa na bakteria kwa kutumia kemikali ya β-Lactamase, hivyo basi muunganiko na dawa zenye kuzuia β-Lactamase (clavulanic acid, sulbactam, tazobactam, cloxacillin) huwa yenye matokeo zaidi kwa penicillin kufanya kazi yake. Kwa mfano Ampicillin & cloxacillin, Amoxicillin & clavulanic acid, ceftriaxone & sulbactam, nk
4. Dawa kwaajili ya matibabu ya VVU (UKIMWI)
Muungozo wa matibabu wa sasa unaonesha kuna muunganiko wa aina tatu za dawa za VVU (triple therapy) zinaweza kutengenezwa k**a kidonge kimoja kwa baadhi ya vidonge vya ARV. Kwa mfano dawa mbili zenye kuzuia reverse transcriptase na moja yenye kuzuia nonnucleoside reverse transcriptase au dawa katika kundi la nucleoside pamoja na NNRTI na dawa yenye kuzuia protease au dawa mbili za kundi la nucleoside na dawa yenye kuzuia protease
Katika majaribio, muunganiko wa dawa hizi za ARV umeonesha kuwa na uwezo wa kupunguza kiwango cha virusi hadi kiwango cha mwisho cha kuonekana (kopi 50 za virusi katika mL ya damu). Na husaidia kupunguza uwezekano wa virusi kuzailiana na kutengeneza usugu katika dawa. Matibabu ya mapema ya VVU kwa mtu mwenye upungufu wa CD4 T-cell chini ya seli 350 katika μL ya damu yameonesha kupunguza vifo na magonjwa sugu yatokanayo ya ukimwi

MUUNGANIKO DAWA AMBAO HAUSHAURIWI KUFANYIKA
Dawa zenye kukinzana katika ufanyaji kazi wake hutokea pale zinapounganishwa, muunganiko wenye kukinzana haushauriwi kufanyika hata kidogo. Mara nyingi muunganiko huu umeonekana zaidi dawa zenye kuzuia ukuaji wa bakteria zikitumika pamoja na dawa zenye kuua bakteria. Kwa mfano dawa katika kundi la tetracycline huzuia ukuaji wa bakteria hivyo hukinzana na dawa katika kundi la penicillin ambazo huua bakteria. Kumbuka penicillin hufanya kazi kwa kutegemea ukuaji wa seli za bakteria kwa kuzuia utengenezwaji wa kuta za seli na hatimae kupelekea kuta z seli kuwa dhaifu na baadae seli kufa.

ASANTE KWA KUITEMBELEA SANGULAE ONLINE PHARMACY CARE
Tembelea kurasa zetu za;
​​​​Facebook
​​​​Instagram
​​​​Telegram

UGUMBA AU KUTOSHIKA MIMBA KWA WANANDOA(1) Nini maana ya ugumba au kushindwa kushika mimba?-- Ugumba ni kushindwa kushika...
24/08/2022

UGUMBA AU KUTOSHIKA MIMBA KWA WANANDOA

(1) Nini maana ya ugumba au kushindwa kushika mimba?
-- Ugumba ni kushindwa kushika mimba baada ya miezi 12 ya kufanya tendo la ndoa pasipo kinga au miezi 6 kwa wanawake wenye zaidi ya miaka 35.
Hii maana ya ugumba imerudia kulingana na taarifa ambazo zimeonesha 50% ya ndoa hupata ujauzito ndani ya miezi mitatu, 75% - 82% ndani miezi sita, na 85 - 92% ndani ya miezi 12, lakini hutambua kadri umri uongezekapo ndipo uwezo wa kushika mimba hushuka.

JE SHIRIKA LA AFYA DUNIANI HUSEMA NINI JUU YA UGUMBA
Kulinga na WHO huutambua ugumba k**a ni moja ya kilema na uzingatifu wa huduma bora kwa tatizo hili huangukia katika haki za watu wenye ulemavu.
Karibia wanawake milioni 34, mara nyingi kutoka katika nchi zinazoendelea , ugumba hutokana na matatizo ya kuathiriwa na bakteria sehemu za uzazi ambao hupelekea kutokwa na uchafu na utoaji wa mimba pasipo usalama.

JINSI YA KUMHOJI AU KUMCHUNGUZA MGONJWA

(1) NINI UCHUNGUZI WA AWALI
-- katika ndoa zote zenye kuonesha changamoto hii ya kushindwa kushika mimba, uchunguzi wa awali huhusisha muda sahihi wa kufanya ngono na kujadili visababishi vingine k**a sigara, pombe, caffeine ambayo hupatikana kwenye soda - kahawa - majani ya chai, uzito kupitiliza, matumizi ya uzazi wa mpango, magonjwa yanayohusiana na kutokwa uchafu. Uchunguzi huu wa awali husaidia kutambua k**a changamoto hio chanzo chake ni mwanaume

NB: Uchunguzi huu utahusisha wahusika wote wa ndoa yaani mwanaume na mwanamke.
- Uchunguzi huu utahusisha uchunguzi wa shahawa za mwanaume, kuthibitisha upevukaji wa yai kwa mwanamke, uchunguzaji wa mirija ya uzazi

(2) MATATIZO YA KISAIKOLOJIA AMBAYO HUHUSIANA NA UGUMBA
-- Matatizo ya kisaikolojia huwa ni sababu ya kutoshika ujauzito. Saikolojia hii inaweza kuyumbishwa si na vipimo na matibabu ya tatizo la ugumba bali na kitendo cha kujirudia cha kuwa na matumaini alafu matumaini hayo kupotea tena kwa kila njia mpya inapojaribiwa pasipo mafanikio ya kushika ujauzito. Kutengwa na familia na marafiki husababisha kuathirika zaidi kisaikolojia
-- Matibabu ya kisaikolojia huhitajika kutolewa mapema

(3) SABABU ZILIZOPO UPANDE WA MWANAMKE
Ijapokuwa wanandoa wote wanaweza kuhusika kusababisha tatizo hili lakini mwanamke anapaswa kuchunguzwa zaidi kwasababu ndie hubeba mimba.

👉 Matatizo ya mfumo wa hedhi huwa yenye asilimia kubwa ya kusababisha kushindwa kushika ujauzito. Matatizo hayo ni k**a kasoro katika upevukaji wa yai na kasoro katika tumbo la uzazi, changamoto hizi zinaweza kupelekea mwanamke kutoingia kwenye hedhi au hedhi isioeleweka au hedhi fupi.
-- Kwa uchunguzi wa karibu wa historia ya mgonjwa na vipimo vya maabara inaweza kusaidia kujua kasoro katika (1) tezi kuu (hypothalamic au pituitary) ambapo homoni za FSH, LH na estradiol huwa kwa kiwango cha chini pamoja na kuongezeka au kupungua kwa homoni ya kuzalisha maziwa (Prolactin). (2) Uvimbe kwenye ovari uliojaa maji maji (PCOS); ambao hupelekea hedhi kutokuwa zenye mpangilio, homoni za kiume kuwa nyingi, tatizo hili kufanywa kwa uchunguzi wa picha za miozi (ultrasound). (3) Kasoro zilizopo katika ovari (ambapo homoni ya estradiol huzalishwa katika kiwango cha chini huku FSH kuongezeka katika uzalishaji. Au (4) Kasoro katika tumbo la uzazi

— Uvimbe katika ovari wenye maji maji (Poly cystic ovarian disease); tatizo hili ni kasoro katika ovari (sehemu ya kuzalisha mayai) ambapo hutokea na uvimbe uliojaa maji maji yenye sukari na hupelekea kiwango cha homoni za kiume kuwa kikubwa (hyperandrogenism) pamoja na kiwango cha LH kuongezeka zaidi. Mabadiliko haya ya homoni husababisha changamoto za ukomavu na upevukaji wa mayai na hedhi isioeleweka.
Mtu mwenye tatizo hili la PCOS hukumbwa na changamoto ya kushika ujauzito, mimba kuharibika mara kwa mara, uotaji wa nywele sehemu za usoni - kifuani, uzito usioendana na kimo (uzito mkubwa), changamoto za kisaikolojia zinazotokana na kushindwa kushika ujauzito- muonekano wa kiume usoni na kifuani - na hedhi isiokuwa na mpangilio
PCOS hugundulika kwa kufanya ultrasound - ambayo itaonesha uwepo wa uvimbe na ujazo wa ovari kuwa zaidi ya 10ml. Na kipimo cha homoni hasa LH:FSH ambapo uwiano wake unatakiwa kuwa 1:1 lakini kwa mwenye tatizo hili uwiano wake huwa 2:1 au 3:1 manake kiwango cha LH huzidi kile cha FSH. Lakini hushauriwa kufanya vipimo vya homoni ya kuzalisha maziwa (hyperprolactinemia) ambapo ikiwa nyingi hupelekea mwanamke kujisikia k**a mwenye kunyonyesha au chuchu kuuma, kuvimba na kutoa maziwa au maji maji na huingilia ufanyaji kazi wa homoni za k**e

👉 Magonjwa katika mirija ya uzazi (Tubal disease). Tatizo la PID, matumizi ya uzazi wa mpango wa ndani ukeni, historia ya mimba kutungwa nje ya uzazi, hupelekea mirija ya uzazi kutofanya kazi yake sawa sawa. Kipimo cha Hysterosalpingogram (HSG) au Laparoscopy (kusafishwa mirija) hufanyika mapema kwenye ndoa nyingi.
-- Maambukizi ya bakteria aina ya Chlamydia trachomatis hupuuzwa katika kuchunguzwa kwa undani, hivyo hushauriwa wanandoa wote kutibiwa.

PID ni ugonjwa ambao hutokea sehemu ya uke na uzazi wa mwanamke ambayo huambatana na dalili zifuatazo; (1) Kutokwa na uchafu wenye harufu, uliochanganyika na damu, (2) Maumivu makali wakati wa tendo la ndoa, (3) Maumivu chini ya kitovu, (4) Maumivu ya kiuno, (5) kuwashwa, (6) Kutokwa damu wakati wa tendo, (7) Kukosa hisia ya tendo la ndoa, (8) Maumivu wakati wa kukojoa, (9) Lakini huathiri mzunguko wa hedhi ambapo inaweza kupelekea kutokwa na hedhi isio kawaida. Kumbuka katika ultrasound inaweza kuonesha sehemu ya kizazi ina maji maji yenye bakteria ambayo hudhaniwa kuwa ni uchafu,

👉 Tatizo la tishu/kuta za uzazi kuotea (Endometrosis). Kwa lugha nyepesi ni uwepo wa vinyama vilivyojiotea kwenye kizazi, na uwepo wa hivi vinyama hupelekea kuwa na historia ya kupata maumivu wakati wa ngono (dyspareunia) au maumivu makali ya hedhi (dysmenorrhea). Tatizo hili likiwa la kawaida haliingiliani na upatikanaji wa mimba. Lakini uwepo wa tatizo hili kwa ukubwa husabibisha kasoro katika utengenezaji na upevukaji wa yai, mbegu za kiume kurutubisha yai, na utungwaji wa mimba (mimba kujishikiza katika kuta za uzazi). Endometrosis kitaalamu ni tatizo lililo kimya, ingawa hutolewa kwa njia ya kusafishwa kizazi na mirija yake (laparoscopy)

(4) SABABU ZILIZOPO UPANDE WA MWANAUME
Wanaume nao huwa sehemu ya tatizo la kutoshika mimba kwasababu kuna matatizo mengi ya kiume huhusiana na ugumba kwa mwanamke.

👉Magonjwa yanayohusiana na Korodani na sehemu za kuhifadhia na kusafirisha

👉kasoro au magonjwa katika mfumo wa tezi kuu (hypothalamic - pituitary) ambayo hupelekea kushindwa korodani kufanya kazi yake vizuri

👉Kuna magonjwa ambayo huhusiana na mbegu zenyewe (kasoro katika vinasaba, Y chromosome microdeletions); yawezekana kukosekana (azoospermia) au kiwango kidogo (oligospermia) cha mbegu kwenye shahawa.
-- Kasoro ya kimabadiliko (mutations) katika homoni ya FSH k**a ilivyo kwa wanawake ambavyo kasoro katika FSH hupelekea yai kutokukua na kukomaa hata hivyo kwa wanaume kasoro katika FSH hupelekea uzalishaji mdogo wa mbegu kuwa hafifu zaidi.
-- inakadiriwa kuna 15% za wanaume wenye ugumba unaotokana na shahawa kutokuwa na mbegu na 6% wenye kiwango kidogo cha shahawa.

MATIBABU YA UGUMBA AU KUTOSHIKA UJAUZITO
Ukiacha na athari za uvutaji sigara, pombe, lakini mgonjwa anapaswa kushauriwa juu uzingatifu wa lishe na uzito k**a kiini cha matibabu ya ugumba na ujauzito. Kupungua zaidi au kuwa na uzito zaidi huhusiana na ugumba au ongezeko la athari wakati wa ujauzito
-- Matibabu ya ugumba hupaswa kuangaliwa kulingana na chanzo chake hasa mara baada ya kufanya vipimo. Uzingatifu wa hatua za kimatibabu ni msingi mkuu

👉 Hali ya kuwa na matumaini kwamba kuna kitu kizuri kitakuja kutokea ni msingi wa kisaikolojia kwa wana ndoa.

👉 Kwa tatizo linalohusiana na kasoro za ufanyaji kazi wa ovari zinaweza kutibika kwa; (1) kubadili mtindo wa maisha hasa kwa wanawake wenye uzito mdogo au wenye historia ya kufanya kazi ngumu na mazoezi au uzito mkubwa
- - Matumizi ya dawa zilizopo katika kundi la dopamine agonist (kwa mfano Bromocriptine) zinaweza kutumika kwa wagonjwa wenye kiwango kikubwa cha prolactin homoni
-- Matumizi ya dawa zenye kuongeza ufanyaji kazi wa FSH k**a Clomifene; ni dawa yenye matokeo ya kuongeza upevukaji kwa 60% katika wanawake wenye uvimbe katika ovari. Kumbuka clomifene inaweza kutolewa kwa mwanaume ili kusaidia uzalishaji wa mbegu za kiume

👉 Matibabu ya PCOS; Matibabu bila dawa kwa mwenye changamoto hii ni kwa kufanya yafuatayo. (1) mgonjwa aelezwe chanzo cha tatizo, jinsi tatizo linavoathiri uzazi wake, na jinsi ya kutibu, (2) mgonjwa aelezwe jinsi ya kupunguza uzito kwa kubadili mfumo wa vyakula hasa vyakula vyenye sukari sukari, ufanyaji wa mazoezi
Matibabu kwa kutumia dawa; -changamoto ya hedhi kutokuwa sawa inaweza kuwekwa sawa na moja kati ya dawa zifuatazo; Vidonge vya majira vyenye cyproterone acetate/ co-cyprindiol-dianette ambavyo husaidia kupunguza na homoni za kiume au Norethisterone au Dydrogesterone
- Changamoto ya sukari kuwepo katika ovari hutibiwa kwa kutumia Metformin angalau mwezi mzima
- Changamoto ya yai kutopevuka inaweza kuratibiwa na clomifene

👉 Matibabu ya mfumo wa hedhi huratibiwa kwa kutumia dawa zenye kuongeza homoni mwilini (Hormonal therapy); ambapo dawa huweka katika usawa homoni za hedhi dawa hizo ni k**a Norethisterone, Dydrogesterone (dawa hii hutumika kuweka mfumo wa hedhi sawa, hata kuzuia mimba kuharibika)

👉 Jinsi ya kuhesabu siku za hedhi kwa mtu mwenye siku 28; kwa mfano mwanamke alieingia hedhi tarehe 20/7/2022 hadi 27/7/2022
Siku 10 tangu tarehe ya kuingia hedhi ni salama
—- Kwa mfano wewe hapo tarehe 20/7 hadi 30/7 ulikuwa free ila siku saba ndio ulikuwa hedhi tatu ndio salama (free)

Kuanzia siku ya 11 hadi 20 ni siku ambazo mimba unaweza kushika ambapo siku ya 11 hadi 13 endapo ukifanya ngono isio salama mbegu ya mwanaume huwa hai ndani ya uke hadi siku ya kupevuka yai, siku ya 14 hadi 17 ni hatari zaidi kwasababu yai hupevuka (ovulation period with high chances), siku ya 18 hadi 20 ni siku ambazo yai huwa safarini kuelekea kwenye uzazi na uhatari wa kushika mimba hupungua lakini unaweza kushika ujauzito (low chances)
—— Kwa mfano wewe kulingana na kalenda ya mwezi na mwaka, kuanzia tarehe 31/7 hadi 09/8 ni hatari kwa ujauzito

Kuanzia siku ya 22 hadi 28 yai huwa limeshafika kwenye uzazi na uwezo wake wa kushika mimba hupungua zaidi na ikiwezekana usishike mimba na ni kipindi ambacho humwandaa mwanamke kuingia hedhi
——- kwa mfano wewe hapo kuanzia tarehe 10/8 hadi 17/8 ni siku salama na ambazo zinakutayarisha kuingia hedhi

👉 Tatizo la kuziba mirija hutibiwa kwa kusafishwa sehemu husika

👉 Tatizo la PID hushauriwa kutibiwa kwa aina tatu za dawa; (1) Dawa zenye uwezo katika magonjwa ya zinaa (cover possible gonococcal infection) k**a Ceftriaxone, azithromycin, cefixime, Cefoxitin nk, (2) Doxycycline kwaajili ya bakteria aina ua chlamydial, (3) Dawa zenye kuua bakteria wasiotumia hewa safi wenye tabia ya kuzalisha uchafu, hasa dawa zilizopo katika kundi la Nitroimidazole kwa mfano Metronidazole, Tinidazole, Secnidazole, Ornidazole
Na inashauriwa wanandoa wote kutibiwa ili kupunguza mwendelezo wa bakteria kuwepo na kuathiri, na matibabu haya hushauriwa kufanywa kwa muda wa siku 14

NB: Matibabu mengine yaliainishwa pindi visababishi vikielezwa

ASANTE KWA KUITEMBELEA SANGULAE ONLINE PHARMACY CARE

29/06/2022

Top Trending post

NI TATIZO GANI AMBALO HUPELEKEA KUHISI KIUNGULIA, MAUMIVU YA MAENEO YA CHEMBE YA MOYO HADI MGONGONI AU SHINGONI? (GASTRO...
08/06/2022

NI TATIZO GANI AMBALO HUPELEKEA KUHISI KIUNGULIA, MAUMIVU YA MAENEO YA CHEMBE YA MOYO HADI MGONGONI AU SHINGONI? (GASTROESOPHAGEAL REFLUX DISEASE, GERD).

UTANGULIZI
Maana halisi GERD kwa ujumla ni kuathirika kwa njia ya chakula (Esophagitis) ambako hutokea mara baada ya tindikali au kemikali aina ya gastric acid na pepsin kupanda tokea tumboni kuelekea juu kufuata njia ya chakula. Utembeaji wa kemikali hizi hupelekea kuchoma au kuchubua njia ya chakula na kusababisha mikwaluzo na vidonda sehemu hio

KWA NJIA IPI TATIZO HILI HUTOKEA?
Kuna njia kuu tatu ambazo huhusika kusababisha tindikali au kemikali hizi zipande juu
(1) valvu ya njia ya chakula kulegea mara baada ya tumbo kujaa tindikali au kuongezeka ukubwa mara baada ya chakula (Transient LES relaxations)
(2) Kushuka kwa mgandamizo wa njia ya chakula ambao hupelekea chakula kushuka taratibu au mchanganyiko wa chakula na kemikali kuanza kupanda juu (LES hypotension)
(3) Mabadiliko ya kianatomi ya mfumo wa tumbo na njia ya chakula kwa mfano Kulegea kwa misuli ya tumbo (Hiatus Hernia)

NINI VISABABISHI VYA TATIZO HILI
- unene hasa maeneo ya tumboni
- ujauzito
- Hali ya tumbo kuzalisha tindikali zaidi
- Kukaa chakula tumboni kwa muda mrefu
- Hitilafu za mjongeo wa njia ya chakula
- nk

NJIA YA KIBAIOLOJIA AMBAYO HUSAIDIA KUTATUA TATIZO HILI
Mara baada ya tindikali upanda, mjongeo wa njia ya chakula hurudisha tindikali tena tumbo na mabaki ya tindikali katika njia ya chakula husafishwa kwa mate yenye bicarbonate
- Sababu mbili zinaweza kupelekea tatizo hili kutokea (1) Kubaki kwa tindikali katika njia ya chakula kwa muda mrefu na hii hutokea mara baada ya hitilafu za mjongeo wa njia ya chakula, (2) Uzalishwaji mdogo wa mate ikilonganishwa na mabaki ya tindikali iliopo katika njia ya chakula

DALILI ZA TATIZO HILI
Kiungulia cha muda mrefu au cha mara kwa mara, chakula kutoka tumboni pasipo dalili ya kichefuchefu (yaani kuhisi au chakula kutoka mithili ya kukitapika pasipo dalili ya kichefuchefu). Dalili ambatani ni k**a kushindwa kumeza chakula au maumivu wakati wa kumeza chakula, maumivu ya kifua na mgongo au shingo.

MATIBABU YA TATIZO HILI
Mabadiliko ya mfumo wa maisha ni ya muhimu sana kufanyika ili kupata afadhali na tatizo hili
Mambo matatu huongelewa k**a yafuatayo;-
(1) Epuka vyakula ambavyo hupelekea kupunguza mgandamizo wa wa njia ya chakula k**a vyakula vyenye mafuta mengi, jamii ya pilipilimanga na ikiwezekana kahawa na chai
(2) Epuka vyakula vyenye asili ya tindikali na vyenye kupelekea uzalishaji wa tindikali zaidi k**a jamii ya limau, vyakula vyenye nyanya, viazi, jamii ya maharage, dagaa (kauzu) nk
(3) Kujaribu kuendana na hali ya vyanzo ili kupunguza tatizo hili kwa mfano kula chakula kiasi ila mara kwa mara (yaani kutokula sanaa chakula hadi kupelekea tumbo kuongezeka), usilale, usikimbie mara baada ya chakula
Kwa mgonjwa ambae hupata tabu na kiungulia cha usiku anaweza kutumia kitambaa chochotr ambacho kinaweza kuinua kichwa chake

Matibabu ya dawa mara nyingi huhusisha dawa zenye kuzuia uzalishaji wa tindikali (dawa hizo ni zile za kundi la proton pump inhibitors), na dawa zenye kupunguza hali ya tindikali tumboni (acidity of gastric juices) dawa hizo ni zile katika kundi la Antacid

NB: Kupungua kwa hali ya tindikali (utindikali) hakumaanishi kupungua kwa tatizo hili bali husaidia kuruhusu kuponya sehemu iliochubukua (esophagitis healing). Kwahiyo muunganiko wa dawa zenye kupunguza uzalishaji wa tindikali na zile zenye kupunguza utindikali kwa ile tindikali ambayo imeshazalishwa huonesha matokeo mazuri zaidi.
- Kitu kingine cha msingi zaidi ni kwamba hakuna utofauti mkubwa sana katika kuchagua dawa zenye kuzuia uzalishaji (PPIs) na cha kuzingatia ni katika kuongezeka kwa dozi yake ili kupata manufaa zaidi.

ASANTE KWA KUENDELEA KUTUFUATILIA SANGULAE ONLINE PHARMACY CARE

Address

Rujewa

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sangulae Pharmacy CARE posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Sangulae Pharmacy CARE:

Share