Festo p shine

Festo p shine plumber&plumbing 0622211284

usipende kumweleza kila mtu maisha YakoKwani adui wa mtu ni mtuKuwa makini huenda huyo unaemsimulia ndiye mharibifu wa m...
06/11/2024

usipende kumweleza kila mtu maisha Yako
Kwani adui wa mtu ni mtu
Kuwa makini huenda huyo unaemsimulia ndiye mharibifu wa maisha Yako.

19/10/2024
shida ni utelezi wa maisha usishangae , jasho la mnyonge hulipwa na Mungu mvumilivu hula mbivu
01/10/2024

shida ni utelezi wa maisha usishangae , jasho la mnyonge hulipwa na Mungu mvumilivu hula mbivu

the name of jesus is medicine
24/09/2024

the name of jesus is medicine

(everything you do, you do yourself) don't treat someone bad, it will come back to you if you treat them well and you wi...
14/09/2024

(everything you do, you do yourself) don't treat someone bad, it will come back to you if you treat them well and you will be treated well. good day

16 making the most of every opportunity, because the days are evil. 17 Therefore do not be foolish, but understand what ...
08/09/2024

16 making the most of every opportunity, because the days are evil. 17 Therefore do not be foolish, but understand what the Lord’s will is. 18 Do not get drunk on wine, which leads to debauchery. Instead, be filled with the Spirit,

*JE UPO NDANI YA YESU?*Yohana 15:7 “Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote na...
26/08/2024

*JE UPO NDANI YA YESU?*

Yohana 15:7 “Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa”.

Je unaelewa maana ya kukaa ndani ya YESU(kuwepo ndani ya YESU) ??kwasababu ipo tofauti ya Bwana YESU kukaa ndani yako, na wewe kukaa ndani yake.

Kukaa ndani si Kumpa YESU maisha yako!!!…Ni zaidi ya hapo!.

Je ulishawahi kusikia mtu akisema “fulani nimemtoa ndani yangu kabisa au moyoni”..??

Utakuwa unaelewa maana ya hiyo kauli kwamba huenda katendewa kitendo kibaya sana, au cha kuumiza au kudhalilisha…ikasababisha kumtoa huyo mru moyoni kabisa.

Vile vile kuna mtu utamsikia akisema “mtu fulani yupo sana moyoni mwangu”…

Maana yake mpaka kusema hivyo huenda huyo mtu kamfanyia jambo jema sana au la kugusa moyo wake, au la kumvutia, mpaka kufanya aingie moyoni mwake.

Na Bwana YESU ni hivyo hivyo, kuna watu wapo ndani yake (moyoni mwake)..na kuna watu hawapo kabisa moyoni mwake ijapokuwa wanaweza kukiri wanaye…

Kwanini?..

Jibu: Kwasababu hawajawahi kuugusa moyo wa Bwana hata kumfanya Bwana awaweke moyoni mwake..watu hawa kibiblia hawapo ndani ya YESU na Kristo ingawa wanaweza kukiri kwamba wanaye Kristo moyoni, na Bwana atawakana siku ile kwamba hawajui.

Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.

Yafuatayo ni mambo(Matendo) ambayo mtu anaweza kuyafanya yakaugusa moyo wa Bwana YESU , hata kumfanya mtu huyo awe ndani ya KRISTO (moyoni mwake).

KUSHIRIKI MEZA YA BWANA.
Hili ni jambo la kwanza linalomzamisha mtu kwenye moyo wa KRISTO.

Yohana 6:56 “Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake.

57 K**a vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, nami ni hai kwa Baba; kadhalika naye mwenye kunila atakuwa hai kwa mimi”.

Kamwe usiidharau meza ya Bwana, lakini pia hakikisha unashiriki kulingana na Neno lake..Kwa kufanya hivyo utauteka moyo wa Bwana kwa kiwango kikubwa sana.

2.UMOJA.

Hili ni jambo la pili linalouteka moyo wa Bwana sana na kumzamisha mtu ndani ya moyo wake.

Yohana 17:21 “Wote wawe na umoja; k**a wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.

22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja k**a sisi tulivyo umoja.

23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao k**a ulivyonipenda mimi”.

Hivyo jenga sana desturi ya kutafuta Umoja wa Roho, usipende kukaa peke yako peke yako (huendi kanisani, hushirikiani na wengine..ni hatari kubwa sana).

3.MATOLEO.

Kumtolea Mungu kwa hiari pasipo kulazimishwa wala kushinikizwa, ni kitendo cha tatu kinachougusa sana Moyo wa Bwana (hauwezi kutoka moyoni mwake daima).

Mathayo 26:12 “Maana kwa kunimwagia mwili wangu marhamu hiyo, ametenda hivyo ili kuniweka tayari kwa maziko yangu.

13 Amin, nawaambieni, Kila patakapohubiriwa Injili hii katika ulimwengu wote, tendo hilo alilolitenda huyu litatajwa pia kwa kumbukumbu lake”.

Huyu mwanamke amekuwa ndani ya moyp wa Kristo kwa vizazi vyote, mpaka sasa tunavyozungumza.

Usikwepe matoleo (sadaka) shetani amevuruga sana eneo hili la matoleo kwasababu anajua endapo mtu akipata ufunuo mkamilifu basi ataingia ndani ya Kristo moja kwa moja.

UNYENYEKEVU.
Unyenyekevu ni wa kukiri makosa, na kurudi kitubu na kuyokurudia rudia machafu, ni tendo kubwa sana linamwingiza mtu ndani ya YESU.

Luka 23:40 “Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo?

41 Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa.

42 Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.

43 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi”

Na yapo mambo mengine mengi katika maandiko yanayomwingiza mtu na kumdumisha ndani ya KRISTO.

Zifuatazo ni faida za kuwa ndani ya KRISTO.

Lolote tuombalo tunapata.
Yohana 15:7 “Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa”

2.Tunakuwa viumbe vipya.

2 Wakorintho 5:17 “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya”.

Hasara za kutokuwa ndani ya KRISTO ni kinyume cha faida hizo.

Bwana atusaidie tuingie na kudumu ndani yake.

AMEN

Ee BABA muunba mbingu na nchi,, BABBA Mwenyezi ninakushukuru Kwa ajili ya  asubuhi hii iliyo njemaNipo ianza siku hii ui...
18/07/2024

Ee BABA muunba mbingu na nchi,, BABBA Mwenyezi ninakushukuru Kwa ajili ya asubuhi hii iliyo njema
Nipo ianza siku hii uiliyo mpya ninafurahia wwema wako, Upendo wako na mipango Yako juu ya yangu Ee MUNGU Mwenyezi.
Asante baba Kwa neema,. Rehema na upendeleo wako siku zote juu yamaisha yangu.
Ninakushukuru kwa kua wema wako daima umenizunguka, na kuniweka salama mbele ya maadui zangu.
Ninakushukuru .
kuwa mipango ya adui zangu Haina nafasi
Sina sababu ya kuogopa kwani wewe mungu u. Pamoja nami katika mwili na katika roho
Macho Yako yapo juu yangu na sikio lako lipo wazi kisikiliza maombi yangu.
Ninaomba Ee BABA unipe Amani , Nuru na kibali.
Uniepushe na Kila baya lililosimama mbele yangu.
Uniepushe na Kila mitego iliyotegwa njiani kwa Siri na Kila mahali.
Unipe harifu iliyo Njema niweze kunukia, unifunike Kwa Nuru ya roho wako mtakatifu niweze kung'aa.
Unipe wepesi katika Kila wazo na katika kila jambo katika siku hii ya Leo Ee BWANA.
Kila kinachokula nyuma yangu katika ulimwemngu wa roho, kilowe na moto wa roho mtakatifu Kwa jina la YESU KRISTO Mwana wa MUNGU aliye hai

AMEN🙏

INJILI: Mk.6:7-13Yesu aliwaita wale Thenashara, akaanza kuwatuma wawili wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu; akawak...
13/07/2024

INJILI: Mk.6:7-13
Yesu aliwaita wale Thenashara, akaanza kuwatuma wawili wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu; akawakataza wasichukue kitu cha njiani isipokuwa fimbo tu; wala mkate, wala mkoba, wala pesa za bindoni; lakini wajifungie viatu; akasema, Msivae kanzu mbili. Akawaambia, Mahali po pote mtakapoingia katika nyumba, kaeni humo hata mtakapotoka mahali pale. Na mahali po pote wasipowakaribisha ninyi wala kuwasikia, mtokapo huko, yakung'uteni mavumbi yaliyo chini ya miguu yenu, kuwa ushuhuda kwao. Wakatoka, wakahubiri kwamba watu watubu. Wakatoa pepo wengi, wakapaka mafuta watu wengi waliokuwa wagonjwa, wakawapoza.

Mazungumzo ya wenye kumcha mungu ni ya hekima daima lakini mpumbavi hubadilika k**a mwezi.
04/07/2024

Mazungumzo ya wenye kumcha mungu ni ya hekima daima lakini mpumbavi hubadilika k**a mwezi.

30/06/2024

Kuna misemo mingine siielewagi hata na Wala sitaielewa kabisa .

Mtu anasema eti
Nyumba ni mwanamke lakini kwenye maduka ya ujenzi hutawakuta kule wakiuzwa zaidi ya cement, bati, nondo , misumari , MBAO, tofali, rangi , n.k

Tusidanganyane bwana .

Address

Tanga

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Festo p shine posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share