Kiwembe herbal pharmacy

Kiwembe herbal pharmacy Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Kiwembe herbal pharmacy, Medical and health, Tanga.

*KIWEMBE HERBAL PHARMAL**MWENDELEZO WA MAKALA NO1 HII NI NAMBA2*TATIZO LA TUMBO KUJAA MAJI*Kuna Aina Ngapi Za Ascites? K...
27/08/2022

*KIWEMBE HERBAL PHARMAL*

*MWENDELEZO WA MAKALA NO1 HII NI NAMBA2

*TATIZO LA TUMBO KUJAA MAJI*

Kuna Aina Ngapi Za Ascites?


Kwa desturi, ascites hugawanywa katika aina kuu 2, transudative na exudative. Mgawanyo huu hutegemea kiwango cha protini kinachoonekana ndani ya maji hayo. Namna bora zaidi iliyotumika ni kutazama kiasi cha albumin kilichopo ndani ya maji (ascitic fluid) kikilinganishwa na kiasi kilichopo ndani ya albumin iliyopatikana ndani ya damu. Hii huitwa Serum Ascites Albumin Gradient au SAAG. Acites iliyotokana na pressure kwenye mishipa mikubwa ya damu ya ini (portal hypertension) huwa juu ya 1.1, na ascites kwa sababu nyingine huwa chini ya 1.1.



Tiba Ya Ugonjwa Wa Maji Kujaa Tumboni


Tiba ya ugonjwa wa maji kujaa tumboni kwa kiasi kikubwa itategemea chanzo halisi cha ugonjwa huu. Kwa mfano, peritoneal carcinomatosis au malignant ascites itatibiwa kwa kufanya upasuaji kuondoa eneo lililoathirika na saratani au kwa chemotherapy, wakati ascites iliyotokana na matatizo ya moyo itadhibitiwa kwa dawa za kutibu chanzo cha moyo kushindwa kufanya kazi vizuri au masharti katika kula.

Endapo maji kujaa tumboni kumetokana na uharibifu wa ini (cirrhosis), mgonjwa atasaidiwa kwa kushauriwa kupunguza matumizi ya chumvi na kumeza vidonge vya kutoa maji yaliyozidi mwilini. Vidonge hivyo vitamfanya atoe haja ndogo mara nyingi zaidi huku vikizuia utunzwaji wa maji mwilini. Pamoja na kuwa hii ni njia bora, aina nyingine za ugonjwa huu hazisikii tiba hii.

Hali ikiwa mbaya sana, operesheni ya kubadilisha ini inaweza kuwa ndiyo uamuzi wa mwisho. Tiba nyingine ni k**a zifuatazo:

Paracentesis

K**a tiba nyingine hazikutoa msaada mkubwa au k**a maji ni mengi sana, paracentesis hutumika. Hii ni njia ambapo daktari huingiza sindano tumboni na kutoa maji yaliyozidi nje ya mwili.









Lengo ni kupunguza msukumo ndani ya tumbo, na kumfanya mgonjwa ajisikie vizuri. Maji yanayotolewa yanaweza kufika lita 5, ingawa kuna wagonjwa wenye hali mbaya zaidi ambao hutolewa maji zaidi ya lita 10.



Shunts

Endapo maji yamejaa tumboni kutokana na kansa, madaktari wanaweza kutumia mpira kuondoa maji kutoka kwenye tumbo na kuyaingiza kwenye mtiririko wa damu.

Daktari huchoma sindano kwenye neva ya shingoni na kuweka shunt kupitia
kifuani. Shunt hiyo huunganisha uwazi wa tumbo na shingo, na kuingia kwenye veni. Na hivyo maji hutiririka kupitia mrija huo hadi kwenye mzunguko wa damu.

Chemotherapy

Chemotherapy inaweza kutumika kudhibiti saratani. Inaweza kufanywa kutumia mpira unaoingizwa tumboni, ingawa hakuna ushahidi wa kuwa njia hii ina matokeo bora.

Swali lakujiuliza jee???kuna dawa za mimea tiba zenye kutibu ugonjwa jawabu lake ndio ziko iko mimea ambayo mgonjwa hupewa anywe lengo atoe maji hayo kwa njia ya mkojo hadi maji yatakapo kwisha tumboni nahii ndio njia sahihi isiyo na madhara kwa mgonjwa nandio njia yakuondoa maji tumboni kwa haraka sana biidhini llahi.

*KIWEMBE HERBAL PHARMACY*

tunatoa huduma za dawa asili za mimea tiba pamoja nakuwashauri kuwaelimisha wenye magonjwa mbali mbali tupigie sasa.

โ˜Ž๏ธ๐Ÿ“žโ˜Ž๏ธ+255652175774/+255787941413 tabibu.m.b.mwarizo.from.tanga.tanzania๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ

*KIWEMBE HERBAL PHARMACY**Ujue Ugonjwa Wa Tumbo Kujaa Maji (Ascites)* *HII NI MAKALA NO1* Katika mada yetu ya leo tutauz...
27/08/2022

*KIWEMBE HERBAL PHARMACY*

*Ujue Ugonjwa Wa Tumbo Kujaa Maji (Ascites)*


*HII NI MAKALA NO1*



Katika mada yetu ya leo tutauzungumzia ugonjwa ambao husababisha maji kujaa ndani ya tumbo na mara nyingine kusababisha mgonjwa apate matatizo katika kupumua. Ni ugonjwa ambao baadaye huweza kusababisha maambukizi ya bakteria katika tumbo โ€“ spontaneous bacterial peritonitis (SBP) na/au kushusha kinga za mwili katika eneo hilo lililojaa maji. Ugonjwa huu huitwa ascites.

Kitaalamu ascites ni ugonjwa wa kujaa maji kusiko kwa kawaida ndani ya tumbo. Maji haya hujaa ndani ya nafasi iliyopo katikati ya tabaka mbili za utando laini ambazo kwa pamoja hujenga peritoneum, mfuko laini ambao hushikilia viungo vya ndani ya tumbo. Kwa kawaida kunakuwepo na maji kiasi ndani ya nafasi hiyo (hadi mililita 20 kwa mwanamke na pungufu ya hapo kwa mwanamme). Kitaalamu maji hayo yanapozidi mililita 25, mgonjwa hutajwa kuwa ana ascites.



Nini Chanzo Cha Maji Kujaa Katika Tumbo?


Kuna sababu nyingi za kujaa maji tumboni, ikiwa ni pamoja na tuberculosis, magonjwa ya figo, matatizo ya kongosho, na kufanya kazi kwa kiwango kidogo kwa tezi ya thyroid.

Chanzo cha maji kujaa ndani ya tumbo kinachobainishwa mara nyingi zaidi ni magonjwa ya ini ya hatua mbaya (cirrhosis). Pamoja na kwamba haijajulikana kwa uhakika ni vipi ascites inatokea, nadharia nyingi zinaamini kuwa kuongezeka kwa pressure kwenye mishipa ya kupeleka damu kwenye ini (portal hypertension) kuna mchango mkubwa zaidi kuliko sababu nyinginezo.

Kanuni ya msingi inafanana na ile inayosababisha edema kwenye maeneo mengine ya mwili ambapo kunakuwa na utofauti wa msukumo kwenye sehemu mbili zinazopakana, sehemu moja ya ndani ikiwa ya msukumo mkubwa na ya nje, kwa hapa ni uwazi wa tumbo, ikiwa na msukumo mdogo. Kuongezeka kwa pressure kwenye mishipa inayolilisha ini na kupungua kwa albumin (protini iliyopo ndani ya damu) vinaweza kuwa visababishi vya tofauti hizi za msukumo na kusababisha maji kujaa ndani ya tumbo.

Visababishi vingine vinavyochangia tatizo la maji kujaa tumboni ni chumvi na kuzuiwa kwa maji. Damu iliyopo ndani ya mzunguko inaweza kuchukuliwa kuwa ni ndogo ikitazamwa na figo kwa sababu ascites inapoanza, hupunguza ujazo wa damu kwenye mzunguko. Hii huzifanya figo kuhifadhi chumvi na maji zaidi kufidia upungufu huo wa damu.

Matatizo mengine yanayohusiana na utofauti wa pressure ya pande mbili ni congestive heart failure na uharibifu wa figo ulio mkubwa ambao huzuia maji ndani ya mwili.

Mara chache sana mwongezeko wa pressure kwenye mishipa ya damu ya ini hutokana na kuzibwa kwa ndani au nje kwa mishipa hiyo, hivyo kusababisha portal hypertension bila uharibifu wa ini (cirrhosis). Mifano ya hali hii ni k**a uvimbe kugandamiza juu ya mishipa hiyo kutoka kwenye uwazi wa tumbo au damu iliyoganda kuziba ndani ya mishipa hiyo na kusababisha mwongezeko wa pressure (mfano, Budd-Chiari syndrome.)

Ascites huweza kujitokeza vile vile kwa sababu ya kansa, ambayo huitwa malignant ascites. Ascites ya aina hii mara nyingi ni ishara ya kansa zilizokomaa ndani ya tishu zilizomo kwenye uwazi wa tumbo, k**a saratani ya utumbo mkubwa, saratani ya kongosho, saratani ya tumbo, saratani ya matiti, lymphoma, saratani ya mapafu, au saratani ya ovari.

Ascites kutokana na kongosho huonekana baina ya watu wenye tatizo sugu la pancreatitis, au uvimbe wa kongosho. Sababu kuu ya pancreatitis sugu ni matumizi ya muda mrefu ya pombe.



Dalili Za Maji Kujaa Tumboni


Kunaweza kusitokee dalili zo zote za maji kujaa tumboni hasa wakati tatizo ni dogo (maji pungufu ya mililita 100-400 kwa mtu mzima). Kadiri maji yatakavyoongezeka, kipimo cha mzunguko wa tumbo na ukubwa wa tumbo vitaongezeka na kuonekana kwa macho. Maumivu ya tumbo, kukosa raha, na kuwamba kwa tumbo kutaonekana. Kukosa pumzi kutajitokeza pale tumbo litakapojaa sana kutokana na kuongezeka kwa pressure kwenye diaphragm na majimaji kuvuka diaphragm na kusababisha maji kuingia kwenye mapafu. Dalili nyingine zaweza kuwa kichefuchefu, kutosikia njaa,
uchovu, kuziba choo na haja ndogo ya mara kwa mara.




Ili usichoke kusoma somo hili nimeligawa mara mbili hii nimakala namba1 makala namba mbili inakuja chini baada ya kumaliza kusoma hii๐Ÿ‘‡โœ๏ธ๐Ÿ‘‡


*KIWEMBE HERBAL PHARMACY*

tunatoa huduma za dawa asili za mimea tiba pamoja nakuwashauri kuwaelimisha wenye magonjwa mbali mbali tupigie sasa.

โ˜Ž๏ธ๐Ÿ“žโ˜Ž๏ธ+255652175774/+255787941413 tabibu.m.b.mwarizo.from.tanga.tanzania๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ

*KIWEMBE HERBAL PHARMACY**SIO KILA ANAEUMWA NA MAUMIVU YA TUMBO CHINI YA KITOVU BASI HUWA NI NGIRI AU CHANGO LA UZAZI**M...
27/08/2022

*KIWEMBE HERBAL PHARMACY*

*SIO KILA ANAEUMWA NA MAUMIVU YA TUMBO CHINI YA KITOVU BASI HUWA NI NGIRI AU CHANGO LA UZAZI*

*MAKALA NO2*

*VISABABISHI VYA MAUMIVU YA TUMBO CHINI YA KITOVU*

2.Kuvimba kwa appendix. Maumivu ya tumbo kwenye kitomfu yanaweza kuashiria ugonjwa wa appendix, kitaalamu hufahamika k**a appendicitis. K**a utahisi maumivu makali ya tumo kitomvuni kisha ghafla yanahamia upande wa kulia wa tumbo kwa chini, huashiria tatizo hili. Tofauti na kuwepo kwa maumivu haya pia mgonjwa ataona dalili flani.

Dalili za ugonjwa wa appendix
1.Kujaa kwa tumbo na kukaza k**a mtu aliye vimbiwa
2.Kichefuchefu
3.Kutapika
4.Kuhisi maumivu ambayo huwa yakiongezeka kila unapokohoa ama unapojongea.
5.Mvurugiko wa tumbo k**a kukosa choo au kuharisha
6.Homa
7.Kukosa hamu ya kula.

Ugonjwa huu ni katika magonjwa ambayo yanahitajika kutibiwa mapema na haraka sana. Endapo mgo jwa atachelewa kutibiwa appendix inaweza kupasuka, na endapo itapasuka inaweza kuhatarisha maisha.

3.Vidonda vya tumbo
Yes maumivu ya tumbo kitomvuni yanaweza kuwa yamesababishwa na vidonda vya tumbo, huwenda vipo kwenye tumbo la chakula ama sehemu ya juu ya utumbo mdogo inayotambulika k**a duodenum. Tofauti na maumivu ya tumbo kwenye kitomvu pia mgonjwa ataona dalili zifuatazo

Dalili za vidonda vya tumbo:
1.mvurugiko wa tumbo
2.Kuhisi tumbo kujaa na kucheua
3.Kichefuchefu
4.Kutapika
5.Kukosa hamu ya kula
6.Kutoa hewa kwa mdomoni kwa sauti

4.Matatizo kwenye kongosho
Huu ni ugonjwa unaosababisha kuvimba kwa kongosho kitaalamu huitwa Pancreatitis. Maradhi haya yanaweza kuja ghafla sana bila ya kuonyesha ishara za awali. Pia zinapoonyesha dalili zake huwa ni k**a:-

Dalili za maradhi ya kongosho
1.Kichefuchefu
2.Kutapika
3.Homa
4.Mapigo ya moyo kuongezeka

5.Kuwa na ngriri ya henia
Ugonjwa huu huwapata wanaume, na hutokea pale ambapo baadhi ya tishu za tumboni zinapoingia kwenye misuli ya tumboni karibu na kitomvu. Kwa watu wazima upasuaji hufanyika ili kutibu tatizo.

6.K**a kuna kizuizi katika utumbo kinachozuia chakula kutembea. Tatizo hili likichelewa kutibiwalinaweza kuwa hatari zaidi. Tatizo hili huweza kusababishwa na:-
1.Mashambulizi ya bakteria
2.Henia
3.Uvimbe
4.K**a kulitokea shida wakati wa kufanyiwa upasuaji.

Dalili
1.Kichefuchefu
2.Kutapika
3.Tumbo kujaa
4.Kupunguwa maji
5.Kukosa hamu ya kula
6.Kukoa choo
7.Homa
8.Kuongezeka kwa mapigo ya moyo

7.Matatizo katika mishipa mikuu ya damu kwenye tumbo (aortic aneurysm). hili ni tatizo la kiafya linalosababishwa na kudhoofu na kutanuka kwa kuta za mishipa mikuu ya damu. Hali hii inaweza kuhatarisha maisha ya mtu k**a mishipa ya damu itapasuka na kupelekea damu kuingia tumboni, hii inaweza kupelekea maumivu makli. Maumivu haya yanaweza kuathiri na viungo vingine.

Dalili nyingine:-
1.Kupata pumzi kwa tabu
2.Kushuka kwa presha ya damu
3.Kuongezeka kwa mapigo ya moyo
4.Kuzimia
5.Udhoifu wa ghafla upande mmoja wa mwili

8.K**a kutakuwa na shida wakati wa mzunguko wa damu katika tumbo (mesenteric ischemia). hii hutokea endapodamu inayotembea kwenye utumbo mdogo itapata usumbufu, kwa mfano ikiganda. Mgonjwa anaweza kusikia maumivu makali ya tumbo. Maumivu haya huandamana na dalili k**a:-
1.Kuongezeka kwa mapigo ya moyo
2.Kuona damu kwenye choo

*KIWEMBE HERBAL PHARMACY*

tunatoa huduma za dawa asili za mimea tiba pamoja nakuwashauri kuwaelimisha wenye magonjwa mbali mbali tupigie sasa.

โ˜Ž๏ธ๐Ÿ“žโ˜Ž๏ธ+255652175774/+255787941413 tabibu.m.b.mwarizo.from.tanga.tanzania๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ

*KIWEMBE HERBAL PHARMACY**SIO KILA ANAEUMWA NA MAUMIVU YA TUMBO CHINI YA KITOVU  BASI YAWEZA KUWA NGIRI AU CHANGO LA UZA...
27/08/2022

*KIWEMBE HERBAL PHARMACY*

*SIO KILA ANAEUMWA NA MAUMIVU YA TUMBO CHINI YA KITOVU BASI YAWEZA KUWA NGIRI AU CHANGO LA UZAZI SIO KWELI*

*Yajue visababishi vya maumivu ya tumbo chini ya kitovu*

*No1 namba2 inakuja*

Maumivu ya tumbo kwenye kitomvu, yanaweza kuwa ni ishara ya maradhi mengi. Mara nyingi maumivu haya yanaweza kuondoka yenyewe baada ya muda. Ila wakati mwingine yanaweza kuwa ni ishara ya shida za kiafya ambazo huhitaji uangalizi wa daktari kwa haraka. Kwa wanaume huwa henia ikisumbuwa sana eneo hili.

Je na wewe ni mwene kusumbuliwa na maumivu ya tumbo kwenye kitomvu? Makala hii ji kwa ajili yako. Hapa tunakwenda kuona sababu za maumivu ya tumbo kwenye kitomvu, dalili na maradhi yanayohusiana na maumivu ya tumbo kitomvuni. Unaweza kutuachia maoni yako hapo chini.

Eneo hili la kitomvuni kitaalamu hufahamika k**a umblical region. Eneo hili la tumbo linahusisha viungo k**a tumbo la chakula, utumbo mdogo, utumbo mkubwa na kongosho. Hivi ni katika viungo muhimu sana katika mmengenyo wa chakula, na afya ya mtu kwa ujumla.

SABABU ZA MAUMIVU YA TUMBO KITOMVUNI NA DALILI ZAKE

1.Kuwepo na uvimbe kwenye njia ya chakula (digestive track) kitaalamu hufahamika k**a gastroenteritis. Hali hii inaweza kusababishwa na virusi, bakteria ama parasite. Mgonjwa anaweza kusikia maumivu na yanaweza kuwa ni makali sana. Mara nyingi maumivu haya yanapoa yenyyewe bila hata kuhitaji matibabau ha huondoka ndani ya siku chache. Ila ni vyema kumuona daktari kwa uchunguzi zaidi.

Dalili zake
Tofauti na kuwa mgonjwa atakuwa anaumwa na tumbo kwenye kitomvu, lakini tumbo hili litafungamana na dalili zifuatazo:-
1.Kuharisha
2.Kichefuchefu
3.Kutapika
4.Homa
5.Kutokwa na
Jasho sana

*KIWEMBE HERBAL PHARMACY*

tunatoa huduma za dawa asili za mimea tiba pamoja nakuwashauri kuwaelimisha wenye magonjwa mbali mbali tupigie sasa.

+255652175774/+255787941413 tabibu.m.b.mwarizo.from.tanga.tanzania๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ

Address

Tanga

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kiwembe herbal pharmacy posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Kiwembe herbal pharmacy:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram