Tiba Asili ya Mimea na Chakula

Tiba Asili ya Mimea na Chakula Tibu na Boresha Afya ya Mwili Wako kwa Kutumia Mimea Tiba na Chakula. ๐ŸŒฟ๐Ÿ

Heal and Improve Your Bodyโ€™s Health Using Medicinal Plants and Nutritious Food. ๐ŸŒฟ๐Ÿ

MCHICHA NI ZAIDI YA MBOGAMchicha ni zao la kilimo cha biashara na pia hutumika sana k**a mboga.Wengi wetu tunatumia mchi...
22/09/2025

MCHICHA NI ZAIDI YA MBOGA
Mchicha ni zao la kilimo cha biashara na pia hutumika sana k**a mboga.

Wengi wetu tunatumia mchicha k**a mboga ya kila siku au kujipatia kipato, kiasi kwamba mara nyingi tumeona k**a mboga ya "kawaida" kutokana na upatikanaji wake kwa gharama nafuu, hata kwa watu wa hali ya chini kiuchumi.
Mchicha ni moja ya mboga zilizotulea na kutukuza wengi wetu.
Kutokana na urahisi wake wa kupatikana, tumepuuza thamani yake bila kutambua kuwa ni miongoni mwa mimea yenye nguvu kubwa ya kitabibu.

๐Ÿ‘ฉโš•๏ธ Mara nyingi tunapoenda hospitali na kugundulika tuna upungufu wa damu au changamoto nyingine za kiafya, ushauri wa kwanza tunaopata ni โ€œKula mboga za majani, hasa mchicha.โ€

๐Ÿ”ฌ Mchicha una zaidi ya spishi 75 zinazopatikana duniani kote, hasa kwenye maeneo ya kitropiki, yenye joto, na yenye hali ya wastani.

๐Ÿ’ช Kwa upande wa lishe, mchicha ni hazina kubwa yenye:
โ€ข Nyuzinyuzi (fiber)
โ€ข Protini
โ€ข Vitamini muhimu k**a K, folate na vitamini B
โ€ข Madini muhimu k**a chuma, magnesiamu na potasiamu
โ€ข Antioxidants na mafuta yenye afya
โ€ข Squalene โ€“ mafuta yenye uwezo wa kupambana na uharibifu wa seli na kuongeza kinga ya mwili.

๐ŸŒŸ Zaidi ya hayo, mchicha una aina zote muhimu za amino acids, hivyo ni chanzo bora cha protini.

Nyuzinyuzi zake nyingi husaidia mmengโ€™enyo wa chakula, huku viambato vyake vya antioxidant vikiiweka mboga hii katika kundi la โ€œsuperfoodโ€ โ€“ chakula chenye manufaa makubwa kwa mwili na afya kwa ujumla.

โ“ Kwa nini hatupati faida zote za mchicha licha ya kuutumia mara kwa mara?

Hii inatokana na namna tunavyoandaa mboga hii. Wengi wetu hupika mchicha kwa lengo la kupata ladha zaidi kuliko virutubisho.

๐Ÿ‘‰ Tunapouchemsha kwa muda mrefu sana na kisha kuchanganya na viungo vingi vya kuongeza ladha, tunasababisha vitamini na madini muhimu kupotea kabisa.
โ€ข Kwa hiyo, ili kufaidika zaidi na mchicha:
Pika kwa muda mfupi tu.
โ€ข Usitumie viungo (pika chukuchuku labda weka chumvi tu).
โ€ข Usioshe mboga kwa mda mrefu โ€“ Tumbukiza kwenye maji kisha toa ili kuondoa mchanga.
โ€ข Acha kuanika Majani ya mchicha juani.
โ€ข Pika Majani na fimbo zake zote ni muhimu sana.
โ€ข Pia chai ya unga wa Mbegu za mchicha ni nzuri sana kwa afya ukitumia mara kwa mara.

๐Ÿ’Š Matumizi ya Kitiba
โ€ข Mbali ya virutubisho nilivyotaja pia mmea huu ni astringent (Kukaza tishu na kuzuia kutoka damu au majimaji), anti-parasitic (kuua na kuondoa vimelea/parasiti), na diuretic (kusaidia kuongeza utokaji wa mkojo hivyo kusafisha kibofu cha mkojo).

๐Ÿ‘‰ Kisukari: Wagonjwa wa kisukari wanashauriwa kutumia mbegu na Majani ya mchicha wa lishe au mchicha pori au mchicha kwa ujumla k**a mbadala wa wali, mara kwa mara. Ina sifa za kupambana na kisukari, husaidia kudhibiti sukari mwilini na kuipunguza.

๐Ÿ‘‰ Shinikizo la dmau na Cholesterol (Lehemu): Mbegu na mafuta yake ni bora kwa wenye shinikizo la damu, magonjwa ya moyo na cholesterol kwasababu ya uwepo kwa wingi wa virutubisho na madini k**a chuma, Omega 3, pottasimu na magnesium.

๐Ÿ‘‰ Maumivu na vidonda vya koo, vidonda vya mdomo, fizi kutoa damu na kuuma na kukaza meno yaliyo legea: Kusukutua maji yaliyochemshwa na majani yaliyokaushwa ndani na kusagwa ni tiba nzuri. Chemsha vijiko viwili vya unga wa majani kwenye ujazo wa maji kikombe 1 kwa dakika 10, acha yapoe, kisha sukutua mara tatu au zaidi kwa siku. Unaweza changanya na chumvi yenye madini Joto pia.

๐Ÿ‘‰ Kutokwa damu nyingi wakati wa hedhi na damu za pua au majeraha: Mmea huu ni dawa yenye nguvu ya kugandisha (kuzuia) damu kwasababu ya vitamin K. Chemsha kijiko kimoja cha unga wa mizizi ya mchicha au chimba mizizi minne (4) kata kata kisha chemsha kwenye ujazo wa maji wa kikombe kimoja (1), acha yapoe kisha kunywa. Kwa damu ya nje, nyunyiza unga wa mzizi kwenye eneo lenye jeraha โ€“ husimamisha haraka damu kwenye majeraha madogo mdogo.

๐Ÿ‘‰ Afya ya Uke: Hutumika k**a dawa ya kuosha uke kwa kutibu uchafu usio wa kawaida unaotoka ukeni.

๐Ÿ‘‰ Vidonda na Majeraha: Majani na mbegu za mchicha hutumika kuosha au kufunika vidonda mbalimbali na majeraha ya nje.

๐Ÿ‘‰ Magonjwa ya Ngozi: Maji ya mchicha au kupaka kwenye sehemu ya ngozi hutumika kutibu chunusi, ukurutu (eczema), na upele (hives).

๐Ÿ‘‰ Kuhara: Mchicha unaweza kutumika kuzuia kuharisha na kutoa haja kubwa au mkojo uliochanganyika na damu.

๐Ÿ‘‰ Afya ya Utumbo Mpana na Tundu la Haja Kubwa: Hutumika k**a e***a kwa uvimbe wa utumbo mpana na vidonda vya sehemu ya haja kubwa.

๐Ÿ‘‰ Maambukizi ya uke: Tumia unga wa majani na mzizi kuchemsha (decoction).

๐ŸŒฟ Elimika, Usiwe mtumwa ๐ŸŒฟโœจ

๐ŸŒฟโœจ Mmea wa Lactana Camara (MVUTI) / NYANHUNDA (Kisukuma) โœจ๐ŸŒฟMmea huu una faida nyingi sana katika tiba asilia kwa changam...
21/09/2025

๐ŸŒฟโœจ Mmea wa Lactana Camara (MVUTI) / NYANHUNDA (Kisukuma) โœจ๐ŸŒฟ

Mmea huu una faida nyingi sana katika tiba asilia kwa changamoto mbalimbali za kiafya.

๐Ÿ‘‰ Sio sumu k**a watu wengi wanavyodhani, bali unatakiwa utumike kwa vipimo sahihi. Mfano, mimea k**a Aloe Vera ikitumiwa kupita kiasi bila maelekezo sahihi huleta madhara, Ni vyema utatumika ipasavyo. Pia tambua vyema mmea huu kabla ya kutumia.

Uzoefu Wangu kabla ya Elimu:
โœ… Tangu tukiwa shule ya msingi tulikuwa tunakula matunda yake bila shida yoyote.

โœ… Mama alikuwa akichemsha na kumpa dada yangu mara mbili (2) nusu (1/2) kikombe cha chai alipokuwa kwenye hedhi, kuondosha maumivu makali.

Mmea huu ni Anti-inflammatory (hupunguza maumivu) na pia ni Antioxidant kutokana na kuwa na kiwango kikubwa cha phenolic na flavonoid.

๐Ÿ”น Unapochanganya na majani ya mstafeli (soursop), kisha ukachemsha na kunywa kikombe kimoja cha chai mara mbili kwa siku:
๐Ÿ‘‰ Husaidia kuondoa seli za saratani na uvimbe (cysts).
๐Ÿ‘‰ Ni tiba nzuri pia kwa vidonda vya tumbo.
๐Ÿ“Œ Soma nilivyoeleza zaidi hapa: https://www.facebook.com/100063646042355/posts/1265101525621370/?mibextid=rS40aB7S9Ucbxw6v

๐Ÿง  Kwenye kumbukumbu:
โžก๏ธ Kusanya majani, yakauke kwa joto la kawaida, saga upate unga wake kisha changanya na asali.

๐Ÿ‘‰ Tumia kijiko kimoja asubuhi na jioni ili kusaidia watoto na watu wazima wanaopoteza kumbukumbu.

๐ŸŒธ Kwa uvimbe au saratani:
Chukua majani na maua yake (ujazo wa kiganja kimoja), chemsha kwenye maji lita moja kwa dakika 15, chuja, kisha kunywa nusu glasi asubuhi na jioni kulingana na ukubwa wa tatizo.

TAHADHARI:
โ€ข Usitumike kwa wanawake wajawazito au wanaonyonyesha bila ushauri wa kitaalamu.
โ€ข Epuka kutumia kwa muda mrefu bila ufuatiliaji wa daktari wa tiba mbadala.
โ€ข Angalia dalili za mzio au madhara mengine baada ya matumizi (k**a vile kichefuchefu, kuhara au vipele).
โ€ข Hakikisha mmea umetambuliwa vizuri kabla ya kuandaa dawa.

๐Ÿ’š Elimika, Usiwe mtumwa! ๐ŸŒฟ

CHANGAMOTO ZA UZAZI KWA WANAUME NA SULUHU KUPITIA MIMEA NA LISHE ASILIAUTANGULIZI: Afya ya uzazi kwa wanaume imeendelea ...
09/06/2025

CHANGAMOTO ZA UZAZI KWA WANAUME NA SULUHU KUPITIA MIMEA NA LISHE ASILIA

UTANGULIZI:
Afya ya uzazi kwa wanaume imeendelea kuwa changamoto inayogusa maisha ya familia nyingi kwa namna ya moja kwa moja au isiyo ya moja kwa moja.

TWAKWIMU
Kwa mujibu wa tafiti za afya ya uzazi kwa wanaume:
โ€ข Inakadiriwa kuwa hadi kufikia mwaka huu 2025, zaidi ya wanaume milioni 522 duniani watakuwa wanakabiliwa na tatizo la ukosefu wa nguvu za kiume (Erectile Dysfunction โ€“ ED). Hii ni ongezeko kubwa kutoka wastani wa milioni 152 mwaka 1995 (chanzo: Hopkins Medicine).
โ€ข Tatizo la utasa (infertility) linawakumba hadi asilimia 12 ya wanaume duniani, na huchangia kwa karibu asilimia 50 ya sababu za ndoa nyingi kutopata watoto (chanzo: Parents.com).
โ€ข Matatizo ya nguvu za kiume huongezeka kulingana na umri, ambapo asilimia 52 ya wanaume wenye umri kati ya miaka 40 hadi 70 hukumbwa na changamoto ya kusimamisha uume kikamilifu au kwa muda mrefu (chanzo: Healthline.com).
โ€ข Oligos***mia (upungufu wa mbegu) na Azoos***mia (kutokuwa na mbegu kabisa katika shahawa) ni kati ya matatizo ya kawaida ya uzazi kwa wanaume. Takribani asilimia 1 ya wanaume wote hukumbwa na Azoos***mia, na huathiri hadi asilimia 20 ya wanaume wenye matatizo ya kupata watoto (chanzo: ScienceDirect).
Takwimu hizi zinaonyesha kwa kina kuwa matatizo ya uzazi kwa wanaume hayapaswi kupuuzwa. Ni tatizo la kijamii na kiafya linalohitaji elimu sahihi, msaada wa kitaalamu, na mabadiliko ya kimtindo wa maisha ili kupata suluhisho endelevu.

CHANZO CHA CHANGAMOTO ZA UZAZI KWA WANAUME
1. Mitindo mibaya ya maisha: Kula vyakula visivyo na virutubisho, matumizi ya pombe na sigara, kutofanya mazoezi, na kukaa sana.
2. Mazingira yenye sumu: Mafusho ya viwandani, dawa za kilimo, plastiki zenye kemikali hatari (k**a BPA).
3. Msongo wa mawazo: Unapunguza uzalishaji wa homoni ya testosterone na huathiri hamu ya tendo la ndoa.
4. Magonjwa sugu na dawa: Kisukari, shinikizo la damu, dawa za msongo au za usingizi zinaweza kudhoofisha nguvu za kiume.
5. Joto kupita kiasi kwenye korodani: Kuvaa chupi za kubana, kutumia laptop, kwenye mapaja au kuingia sauna mara kwa mara n.k.
6. Kujichua kupita kiasi:
Kujichua mara nyingi mno, hasa kwa muda mrefu au kwa utegemezi wa picha/filamu za ngono (pornografia), kunaweza kuathiri mfumo wa fahamu na kupunguza hisia za kawaida za kimapenzi, jambo linaloweza kusababisha:
o Kukosa hamu ya tendo la ndoa (Low libido)
o Kufika kileleni haraka (Premature Ej*******on)
o Kushindwa kusimamisha uume (Erectile Dysfunction)
o Kupungua kwa uzalishaji na ubora wa mbegu
o Kushuka kwa homoni ya testosterone
o Msongo wa mawazo na hisia za hatia
Pia, tabia hii inaweza kujenga utegemezi wa kiakili unaoathiri uwezo wa mwanaume kuwa na uhusiano wa kawaida wa kimapenzi.

MAGONJWA YA KAWAIDA YA MFUMO WA UZAZI WA KIUME NA MAELEZO YAO:
1. Erectile Dysfunction (ED): Kushindwa kusimamisha au kudumisha uume ukiwa umesimama.
2. Premature Ej*******on (PE): Kufika kileleni haraka kabla ya muda unaofaa.
3. Delayed Ej*******on: Kushindwa kufika kileleni au kuchelewa sana.
4. Low Libido: Kukosa hamu ya tendo la ndoa.
5. Low S***m Count (Oligos***mia): Mbegu chache chini ya kiwango cha kawaida.
6. No S***m in Semen (Azoos***mia): Hakuna kabisa mbegu kwenye shahawa.
7. Poor S***m Motility: Mbegu hazisogei au haziogelei vizuri.
8. Abnormal S***m Morphology: Muundo wa mbegu si wa kawaida.
9. Low Testosterone (Hypogonadism): Kushuka kwa homoni ya kiume.
10. Varicocele: Kuvimba kwa mishipa ya damu kwenye korodani.
11. Undescended Testicles: Korodani kutoshuka mahali pake kutoka utotoni.
12. Prostatitis: Kuvimba kwa tezi ya kibofu (prostate).
13. Maambukizi ya Zinaa (STIs): Kisonono, kaswende, chlamydia n.k.

CHAKULA, MATUNDA NA MIMEA TIBA KWA MATATIZO YA UZAZI WA KIUME
Chakula tunachokula kina nafasi kubwa katika afya ya uzazi. Vyakula vya asili vina viambata kazi k**a:
โ€ข L-arginine na Citrulline: Kuboresha mtiririko wa damu kwenye uume (tikiti maji, beetroot)
โ€ข Zinc: Uzalishaji wa mbegu (mbegu za maboga, mayai, mbegu za lozi (almond))
โ€ข Selenium: Uboreshaji wa mbegu na kazi ya korodani
โ€ข Vitamin E & C: Kulinda mbegu dhidi ya uharibifu wa sumu (antioxidants)
โ€ข Boron, Magnesium, Omega-3: Kurekebisha homoni na kuboresha libido

ORODHA YA MIMEA NA VYAKULA VYA ASILI VINAVYOBORESHA UZAZI WA KIUME:
Hapa chini nimekuandalia orodha ya kila chakula/mmea na virutubisho muhimu (vitamins, minerals, phytochemicals) vinavyopatikana, pamoja na mchango wake kwenye afya ya uzazi wa mwanaume:

A. Beetroot
Virutubisho Muhimu: Nitrates, Folate (B9), Iron, Vitamin C, Manganese.

Faida kwa Uzazi wa Mwanaume:
Huongeza mzunguko wa damu (nitrate), kusaidia nguvu za kiume na ubora wa mbegu.

B. Mbegu za maboga
Virutubisho Muhimu: Zinc, Omega-3, Magnesium, Iron

Faida kwa Uzazi wa Mwanaume:
Huchochea uzalishaji wa testosterone, huongeza wingi na ubora wa mbegu

C. Lozi (Almond)
Virutubisho Muhimu: Vitamin E, Zinc, Magnesium, Healthy fats

Faida kwa Uzazi wa Mwanaume:
Husaidia kuzuia uharibifu wa mbegu (antioxidant), huongeza libido (hamu ya kufanya tendo la ndoa au msisimko wa kimapenzi).

D. Tango
Virutubisho Muhimu:
Vitamin K, C, Potassium, Silica

Faida kwa Uzazi wa Mwanaume:
Husaidia kupunguza joto kwenye korodani, kurekebisha usawa wa maji mwilini, kuzuia uharibifu wa seli za uzazi kwasababu lina antioxidants k**a Vitamin C na silica zinazosaidia kuzuia uharibifu wa mbegu kwa kulinda dhidi ya sumu na kuimarisha uimara wa seli za uzazi.

E. Tangawizi
Virutubisho Muhimu:
Gingerol, Vitamin C, Magnesium, Potassium

Faida kwa Uzazi wa Mwanaume:
Huchochea hamu ya tendo la ndoa (libido), huongeza mtiririko wa damu kwenye viungo vya uzazi, na husaidia kupunguza uvimbe wa tezi ya prostate.

F. Kitunguu saumu
Virutubisho Muhimu:
Allicin, Selenium, Vitamin B6, C

Faida kwa Uzazi wa Mwanaume:
Huongeza mzunguko wa damu, hupunguza shinikizo la damu, huongeza testosterone.

G. Moringa
Virutubisho Muhimu:
Vitamin A, C, E, Calcium, Potassium, Iron, Zinc

Faida kwa Uzazi wa Mwanaume:
Huchochea uzalishaji wa mbegu, huongeza nguvu za kiume na kinga

H. Ndizi mbivu
Virutubisho Muhimu:
Vitamin B6, Potassium, Magnesium

Faida kwa Uzazi wa Mwanaume:
Husaidia kwenye uzalishaji wa homoni, nguvu na stamina

I. Majani ya mbigili (Tribulus)
Virutubisho Muhimu:
Saponins, Flavonoids

Faida kwa Uzazi wa Mwanaume:
Huongeza testosterone, huimarisha hamu ya tendo la ndoa

J. Tikiti maji (nyeupe ya ndani)
Virutubisho Muhimu:
Citrulline, Vitamin C, A

Faida kwa Uzazi wa Mwanaume:
Husaidia kusimamisha uume kwa kuongeza nitric oxide

K. Asali ya nyuki wadogo
Virutubisho Muhimu:
Fructose, Glucose, Enzymes, Antioxidants

Faida kwa Uzazi wa Mwanaume:
Huchangamsha nishati, huongeza hamu ya tendo la ndoa

L. Mayai ya kuku wa kienyeji
Virutubisho Muhimu:
Vitamin D, E, Zinc, Choline, Protein

Faida kwa Uzazi wa Mwanaume:
Hujenga mbegu bora, huchochea uzalishaji wa testosterone

M. Parachichi
Virutubisho Muhimu:
Vitamin E, B6, Folate, Potassium, Healthy fats

Faida kwa Uzazi wa Mwanaume:
Huongeza libido, huimarisha homoni za uzazi

N. Tende
Virutubisho Muhimu:
Natural sugars, Iron, Potassium, Zinc

Faida kwa Uzazi wa Mwanaume:
Husaidia uzalishaji wa mbegu, stamina, nguvu za mwili

0. Berries
Virutubisho Muhimu:
Antioxidants (anthocyanins), Vitamin C

Faida kwa Uzazi wa Mwanaume:
Huzuia uharibifu wa mbegu, huongeza ubora wa shahawa

P. Ginseng
Virutubisho Muhimu:
Ginsenosides

Faida kwa Uzazi wa Mwanaume:
Huongeza stamina, nguvu, hupunguza uchovu wa akili na mwili

Q. Ashwagandha
Virutubisho Muhimu:
Withanolides, Iron, Alkaloids

Faida kwa Uzazi wa Mwanaume:
Hurekebisha homoni, hupunguza msongo, huongeza ubora wa shahawa

R. Fenugreek (Haba alfajuun)
Virutubisho Muhimu:
Saponins, Iron, Magnesium

Faida kwa Uzazi wa Mwanaume:
Huongeza testosterone, stamina, na libido

S. Kalafuu
Virutubisho Muhimu:
Eugenol, Vitamin K, Manganese

Faida kwa Uzazi wa Mwanaume:
Hurekebisha mzunguko wa damu, huongeza hamu ya tendo

Muarobaini (Neem)
Virutubisho Muhimu:
Azadirachtin, Nimbin, Vitamin E

Faida kwa Uzazi wa Mwanaume:
Husaidia kuondoa maambukizi ya njia ya mkojo na tezi ya prostate

T. Maca
Virutubisho Muhimu:
Macamides, Alkaloids, Iron, Zinc

Faida kwa Uzazi wa Mwanaume:
Huongeza libido, stamina, na uzalishaji wa shahawa

U. Rhodiola
Virutubisho Muhimu:
Rosavins, Salidroside

Faida kwa Uzazi wa Mwanaume:
Hupunguza msongo wa mawazo, huongeza nguvu na hisia za mapenzi.

KUANDAA MCHANGANYIKO WA ASILI
๐Ÿ“Œ Kwa Erectile Dysfunction:
โ€ข Beetroot + Tangawizi + Ndimu โ€“ kunywa kikombe 1 asubuhi na jioni

๐Ÿ“Œ Kwa Low S***m Count:
โ€ข Beetroot + Moringa Powder โ€“ kijiko 1 cha unga wa moringa + juisi ya beetroot, mara 2 kwa siku

๐Ÿ“Œ Kwa Libido na Testosterone:
โ€ข Kitunguu saumu + Asali + Tikiti maji (sehemu nyeupe) โ€“ blend na kunywa kabla ya chakula cha usiku

๐Ÿ“Œ Kwa Uchovu na Kuzorota kwa nguvu:
Parachichi + Tende + Mayai (mayai ya kuchemsha au mabichi) โ€“ kula k**a smoothie au pamojaโ€ pia mchanganyiko huu huongeza nguvu, huimarisha uzalishaji wa homoni na husaidia kuongeza hamasa ya tendo la ndoa.

Faida zaidi:
1. Unaweza Tumia punje 1โ€“2 za kitunguu saumu asubuhi kwa kunywa na maji ya uvuguvugu au changanya na asali kwa matokeo bora zaidi yafuatayo:
โ€ข Kuhimili tendo la ndoa na ufanisi wa viungo vya uzazi.
โ€ข Kupunguza shinikizo la damu (high blood pressure)
โ€ข Kuchochea uzalishaji wa homoni ya testosterone, ambayo ni muhimu kwa nguvu za kiume, misuli, na hamu ya tendo la ndoa (libido).

2. Kula ndizi 1โ€“2 mbivu kwa siku, hasa asubuhi au kabla ya mazoezi au tendo la ndoa, au changanya na tende na parachichi kutengeneza smoothie yenye nguvu,
โ€ข Huchochea uzalishaji wa homoni muhimu za mwili k**a vile dopamine na serotonin, ambazo huathiri moja kwa moja hali ya hisia na hamu ya tendo la ndoa (libido).
โ€ข Huongeza nguvu na stamina, hasa kutokana na wingi wa virutubisho k**a vitamini B6, potasiamu, na wanga wa asili ambao hutoa nishati ya haraka na ya kudumu.
โ€ข Pia zina bromelain, kimengโ€™enya kinachosaidia katika kuongeza nguvu za kiume.

3. Tumia kijiko 1โ€“2 cha Asali ya Nyuki Wadogo (Asali ya Nyuki wa Porini) kila siku asubuhi au usiku kabla ya kulala. Unaweza kuchanganya na kitunguu saumu, tangawizi au tikiti maji kwa ufanisi zaidi.
โ€ข Huongeza hamu ya tendo la ndoa (libido): Asali huongeza kiwango cha nitric oxide, ambayo huchochea mtiririko mzuri wa damu kwenye viungo vya uzazi.
โ€ข Hutoa nishati ya haraka: Fructose na glucose huchangamsha mwili na akili, muhimu kwa stamina wakati wa tendo la ndoa.
โ€ข Huimarisha ubora wa shahawa: Shukrani kwa madini k**a zinc na selenium ambayo huchochea uzalishaji bora wa mbegu.
โ€ข Hupunguza uchovu na msongo: Asali ina amino acids na antioxidants ambazo husaidia mwili kupambana na uchovu wa mwili na akili.

DOZI NA TAHADHARI:
โ€ข Tumia kwa siku 14 mfululizo kisha pumzika kwa siku 3
โ€ข Wale wenye matatizo ya figo, kisukari au presha kali, wasiliane na mtaalamu kabla ya matumizi
โ€ข Epuka kuchanganya dawa za hospitali na tiba asili bila ushauri wa kitaalamu

USHAURI WA MWISHO:
Afya ya uzazi wa kiume inaweza kurejeshwa kwa kuzingatia vyakula sahihi, mimea tiba na kubadili mtindo wa maisha. Hata hivyo, ni muhimu kufanyiwa uchunguzi na kufuata ushauri wa kitaalamu. Epuka kujitibu bila kuelewa tatizo lako. Tiba ya kweli huanza kwa maarifa sahihi.

๐ŸŒฟ Tiba Asili ya Mimea na Chakula โ€“ Afya ya Kweli, Asili ya Kweli.

โ˜• SUPER ROOT COFFEE (SRC)๐ŸŒฟ Nguvu ya asili kwa afya ya uzazi na kurudisha furaha katika ndoa!โ“ Je, unakabiliwa na mojawap...
04/06/2025

โ˜• SUPER ROOT COFFEE (SRC)

๐ŸŒฟ Nguvu ya asili kwa afya ya uzazi na kurudisha furaha katika ndoa!
โ“ Je, unakabiliwa na mojawapo ya changamoto hizi?

๐Ÿ”ธ Idadi ndogo ya mbegu za kiume?
๐Ÿ”ธ Kukosa hamu ya tendo la ndoa?
๐Ÿ”ธ Tezi dume au saratani ya tezi dume?
๐Ÿ”ธ Utasa (infertility)?
๐Ÿ”ธ Uume kuwa legevu wakati wa tendo?
๐Ÿ”ธ Mke kulalamika kutoridhishwa kitandani?

SULUHISHO LAKO LIPO!

Jibu ni Superlife Root Coffee โ€“ SRC โ˜•
๐ŸŒŸ FAIDA ZA SUPER ROOT COFFEE:

โœ… Huongeza uzalishaji wa testosterone na manii
โœ… Huongeza hamu ya tendo la ndoa (libido) kwa jinsia zote
โœ… Huboresha uzalishaji na ubora wa shahawa (s***m count & quality)
โœ… Hurekebisha homoni kwa wanawake na wanaume
โœ… Hupunguza msongo wa mawazo/stress na huchangamsha akili
โœ… Husaidia kupata usingizi mzuri
โœ… Huimarisha afya ya moyo na mishipa ya damu
โœ… Huongeza nguvu, stamina, na ujasiri wa ndani
๐Ÿ’ฐ BEI YA SRC:

๐Ÿ“ฆ Box 1 โ€“ TSh 150,000
๐Ÿ“ฆ๐Ÿ“ฆ Box 2 โ€“ TSh 300,000
โš ๏ธ Angalizo Muhimu:

SRC ni kirutubisho cha asili (natural supplement). Haipaswi kuchukua nafasi ya matibabu ya hospitali bila ushauri wa kitaalamu kutoka kwa daktari wako.

๐Ÿ“ž Mawasiliano:

๐Ÿ“ฑ Phone & SMS: 0654 013 840
๐Ÿ’ฌ WhatsApp: 0786 193 317

๐ŸŒฟ SUPERLIFE COLON CARE PLUS (SCC+)Afya ya Tumbo, Usagaji Chakula, na Kuondoa Sumu โ€“ Kwa Njia ya Asili!SCC+ ni kirutubish...
04/06/2025

๐ŸŒฟ SUPERLIFE COLON CARE PLUS (SCC+)

Afya ya Tumbo, Usagaji Chakula, na Kuondoa Sumu โ€“ Kwa Njia ya Asili!

SCC+ ni kirutubisho asilia chenye viambato vya nguvu k**a:
๐Ÿ”ธ Sinetrol โ€“ husaidia kuchoma mafuta kwa asili
๐Ÿ”ธ Fibersol-2, Chlorophyll, Amla, Probiotics & Multivitamins
๐Ÿ”ธ Psyllium husk, Beetroot, Tufaha Kijani, Mibigili ya Maziwa, na zaidi

๐ŸŒŸ FAIDA KUU ZA SCC+:

โœ… Husafisha damu na ini kwa kina
โœ… Huboresha afya ya utumbo mpana
โœ… Huondoa sumu mwilini (Detoxification)
โœ… Huzuia na kutibu vidonda vya tumbo
โœ… Hutibu saratani ya utumbo mpana
โœ… Huondoa kuvimbiwa na uvimbe tumboni
โœ… Hupunguza mafuta mwilini kwa njia salama
โœ… Hurekebisha kiwango cha sukari kwenye damu
โœ… Huondoa harufu mbaya mdomoni
โœ… Huongeza usagaji bora wa chakula
๐Ÿ’ฐ BEI YA SCC+:

๐Ÿ“ฆ Box 1 โ€“ TSh 177,000
๐Ÿ“ฆ๐Ÿ“ฆ Box 2 โ€“ TSh 354,000

๐Ÿ“ž Mawasiliano:
๐Ÿ“ฑ Phone & SMS: 0654 013 840
๐Ÿ’ฌ WhatsApp: 0786 193 317

โš ๏ธ Angalizo Muhimu:

SCC+ ni kirutubisho asilia. Haitakiwi kuchukua nafasi ya matibabu rasmi. Tafadhali wasiliana na daktari kabla ya kutumia kwa hali yoyote ya kiafya.

๐Ÿ›ก๏ธ SUPERLIFE IMMUNE CARE (SIC)Fursa ya Kuimarisha Kinga ya Mwili Kwa Njia ya Asili!SIC ni kirutubisho bora kilichotengen...
04/06/2025

๐Ÿ›ก๏ธ SUPERLIFE IMMUNE CARE (SIC)

Fursa ya Kuimarisha Kinga ya Mwili Kwa Njia ya Asili!

SIC ni kirutubisho bora kilichotengenezwa kwa mimea yenye nguvu k**a Moringa na Aphanizomenon flos-aquae (AFA) ambavyo vinasaidia kuboresha kinga ya mwili na kuimarisha afya kwa ujumla.

๐ŸŒŸ FAIDA ZA SIC:

โœ… Kuimarisha mfumo wa kinga ya mwili
โœ… Kuongeza kiwango cha nguvu (boost energy)
โœ… Kuboresha afya ya tumbo na utumbo
โœ… Kusafisha ini na kusaidia kutoa sumu mwilini (liver detox)
โœ… Kurekebisha usawa wa kibaolojia mwilini
โœ… Kusaidia kusawazisha viwango vya sukari kwenye damu
โœ… Tajiri kwa antioxidants โ€“ kusaidia kupambana na msongo wa oksidi (oxidative stress)
๐Ÿ’ฐ BEI YA SIC:

๐Ÿ“ฆ Box 1 โ€” TSh 168,000
๐Ÿ“ฆ๐Ÿ“ฆ Box 2 โ€” TSh 336,000

โš ๏ธ Angalizo Muhimu: ni vyema kuelewa kuwa SIC ni kirutubisho asilia, haipaswi kuchukua nafasi ya matibabu ya hospitali bila kushauriana na daktari kabla ya kutumia kwa ajili ya hali yoyote ya kiafya.

๐Ÿ“ž Mawasiliano:

๐Ÿ“ฑ Phone & SMS: 0654 013 840
๐Ÿ’ฌ WhatsApp: 0786 193 317

๐Ÿง  SUPERLIFE NEURON CARE (SNC)Suluhisho la Afya ya Ubongo, Macho, na Mishipa ya FahamuSNC ni mchanganyiko wenye nguvu wa ...
04/06/2025

๐Ÿง  SUPERLIFE NEURON CARE (SNC)

Suluhisho la Afya ya Ubongo, Macho, na Mishipa ya Fahamu

SNC ni mchanganyiko wenye nguvu wa Lutein na Gingko Biloba, viambato vinavyosaidia kuboresha uwezo wa kuona, kumbukumbu, na mzunguko wa damu katika ubongo.
๐ŸŒŸ FAIDA ZA SNC:

โœ… Kutibu Kiharusi (Stroke)

๐Ÿ‘๏ธ Kuimarisha Uwezo wa Kuona (Eye Sight, Cataract, Glaucoma)

๐Ÿง  Kuboresha Kumbukumbu na Utambuzi (Memory & Cognition)

๐Ÿ’ค Kusaidia Usingizi kwa Wenye Tatizo la Kukosa Usingizi

โšก Kutibu Magonjwa ya Ubongo k**a:

Alzheimer

Parkinson

Brain Tumors

Brain Inflammation

๐Ÿ’‰ Kusafisha na Kusaidia Mzunguko wa Damu

๐Ÿ”ฅ Kutibu Ganzi na Baridi ya Mwili (Peripheral Nerve Issues)

๐Ÿ’ฐ Bei ya SNC

๐Ÿ“ฆ Box 1: TSh 168,000

๐Ÿ“ฆ๐Ÿ“ฆ Box 2: TSh 336,000

โš ๏ธ Angalizo Muhimu: ni vyema kuelewa kuwa SNC ni kirutubisho asilia, haipaswi kuchukua nafasi ya matibabu ya hospitali bila kushauriana na daktari kabla ya kutumia kwa ajili ya hali yoyote ya kiafya.

๐Ÿ“ž Mawasiliano:

๐Ÿ“ฑ Phone & SMS: 0654 013 840
๐Ÿ’ฌ WhatsApp: 0786 193 317

STC30 na Faida Zake kwa Afya Yako:STC30 ni kirutubisho (supplement) itokanayo na selo shina za mimeaโ€”hasa kutoka Tufaha ...
04/06/2025

STC30 na Faida Zake kwa Afya Yako:

STC30 ni kirutubisho (supplement) itokanayo na selo shina za mimeaโ€”hasa kutoka Tufaha (Apple) na Zabibu (PhytoCellTecโ„ข). Pia ina GlisODinยฎ, antioxidant yenye nguvu inayojulikana k**a โ€œEnzyme of Life,โ€ ambayo husaidia mwili kupambana na msongo wa oksidi (oxidative stress) na kuimarisha afya ya jumla ya seli.

Faida Kubwa za STC30

โœ… Uimarishaji wa Seli: Huchochea urejeshaji wa seli zilizochakaa na kurekebisha zilizoharibika โ€“ ikichangia mwili kuwa na nguvu, ujana na afya bora.

๐Ÿ›ก๏ธ Kuimarisha Mfumo wa Kinga: Husaidia mwili kujikinga dhidi ya magonjwa kwa kuimarisha kinga ya asili.

โœจ Kupambana na Msongo wa Oksidi: Huzuia uharibifu wa seli kutokana na radicals huru, na hivyo kupunguza kasi ya kuzeeka na magonjwa sugu.

Hivyo STC30 usaidia;

๐ŸŒฟ STC30 โ€“ Kirutubisho Kinachosaidia Katika:

โœ… Kansa

โœ… Kisukari

โœ… Vidonda vya tumbo

โœ… Ganzi ya mwili

โœ… Magonjwa ya moyo

โœ… Magonjwa ya figo

โœ… Kuongeza kinga ya mwili

โœ… Matatizo ya homoni (uzazi)

โœ… Uvimbe tumboni

โœ… Magonjwa ya njia ya mkojo

โœ… Magonjwa ya mapafu

โœ… Magonjwa ya ngozi

โœ… Kusafisha njia zote za taka mwilini na kuondoa sumu

โœ… Magonjwa ya macho pamoja na kichwa kuuma

โœ… Utibu uti wa mgongo uliovunjika

โœ… Utibu Typhoid, anemia, TB

โœ… Husaidia Kuponyesha vidonda ndugu, vya kuungua kwa moto, gesi n.k
โœ… Kupunguza kasi ya kuzeeka kwa seli

โœ… Kusaidia kuamsha seli hai za mwili kufanya kazi

โœ… Kuamsha seli zilizokufa au zilizolala

Muda wa matumizi STC30: Angalau miezi mitatu kwa matokeo bora, na unaweza kuendelea kulingana na hali ya afya.

Bei ya Bidhaa

๐Ÿ“ฆ Box 1: Tsh 154,000

๐Ÿ“ฆ๐Ÿ“ฆ Box 2: Tsh 308,000

Unapotumia STC30, unampa mwili wako msaada wa ndani unaohitaji ili kujirekebisha, kujiimarisha, na kufikia kiwango cha juu cha afya.

โš ๏ธ Angalizo Muhimu: ni vyema kuelewa kuwa STC30 ni kirutubisho asilia, haipaswi kuchukua nafasi ya matibabu ya hospitali bila kushauriana na daktari kabla ya kutumia kwa ajili ya hali yoyote ya kiafya.

๐Ÿ“ž Mawasiliano:

๐Ÿ“ฑ Phone & SMS: 0654 013 840
๐Ÿ’ฌ WhatsApp: 0786 193 317

K**a unachangamoto katika mfumo wako wa mmeng'enyo wa chakula na unapata dalili zifuatazo;1. Kupata maumivu ya tumbo na ...
04/06/2025

K**a unachangamoto katika mfumo wako wa mmeng'enyo wa chakula na unapata dalili zifuatazo;
1. Kupata maumivu ya tumbo na vidonda vya tumbo,
2. Tumbo kujaa gesi na mingulumo,
3. Kuhisi kushiba mda wote (mara kwa mara wakati ujala),
4. Kupata kiungulia,
5. Kupata Maumivu ya chembe ya moyo, na chini ya kifua,
6. Kutopata choo (haja kubwa),
7. Unataka kusafisha tumbo lako,
8. Tumbo kuwaka moto,
9. Kutapika na Kuharisha damu.
Tafuta hii dawa kwenye maduka ya dawa za asili inatwa NYAFYA itakusaidia sana.

04/06/2025

Habari njema!๐Ÿ“š๐ŸŒฟ
Ni furaha na shauku yangu ya kila siku kushirikiana nanyi maarifa kuhusu Tiba Asili ya Mimea na Chakula โ€” namna bora ya kutumia maliasili hizi k**a kinga na tiba dhidi ya changamoto mbalimbali za kiafya.
๐Ÿ‘‰ Kwa sasa tupo hatua za mwisho kabisa katika maandalizi ya kitabu kipya, ambacho kitatolewa hivi karibuni. Kitabu hiki ni zao la utafiti, uzoefu na maono ya kuona jamii yetu inanufaika na elimu sahihi ya mimea tiba na vyakula vyenye nguvu ya tiba.
Kitabu hiki kimejumuisha vipengele muhimu k**a ifuatavyo:
1. Orodha ya makundi ya magonjwa na changamoto mbalimbali za kiafya kwa kulingana na makundi ya watu (watoto, watu wazima, wazee, nk).
2. Uhusiano wa magonjwa hayo na mimea tiba/vyakula vinavyoweza kusaidia kuyazuia au kuyatibu.
3. Picha zenye ubora wa hali ya juu za mimea tiba na vyakula kwa urahisi wa kuitambua.
4. Majina ya mimea hayo kwa lugha ya asili (kabila mbalimbali), majina maarufu duniani, na majina ya kisayansi.
5. Maelezo ya kina kuhusu wapi mimea na vyakula hivyo hupatikana (maduka ya dawa asili, sokoni, maeneo ya miinuko, mashambani n.k).
6. Njia sahihi za kuandaa mimea hiyo (unga, kimiminika, vidonge n.k).
7. Viwango sahihi vya matumizi kwa watoto na watu wazima bila madhara.
8. Maudhi yanayoweza kujitokeza kwa baadhi ya watu baada ya matumizi (side effects).
9. Tahadhari za matumizi kwa makundi maalum k**a wajawazito, wanaonyonyesha, wenye presha au magonjwa ya moyo.
_______________________________________________________________________
๐ŸŒฟ Tiba Asili ya Mimea na Chakula si ushirikina โ€” ni elimu ya kutumia mimea na chakula chenye viambata hai kwa ajili ya tiba na kinga. Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), hadi kufikia mwaka 2008 zaidi ya asilimia 70 ya watu duniani walitegemea mimea k**a tiba yao ya msingi.
Kutambua umuhimu huu, mwaka 2022 WHO ilianzisha Kitengo Maalum cha Tiba Asili (Global Traditional Medicine Centre โ€“ GTMC) kwa ajili ya kukuza tafiti, ubadilishanaji wa maarifa, na ushirikiano wa kimataifa katika sekta ya tiba asilia.
_______________________________________________________________________
๐Ÿ“œ Ushahidi wa kale wa matumizi ya mimea tiba:
1. Misri ya Kale (Papyrus Ebers, 1550 KK): Zaidi ya dawa 700 za mimea zilitajwa.
2. Ugiriki & Roma ya Kale: Hippocrates na Dioscorides waliandika kuhusu matumizi ya mimea katika tiba.
3. Wasumeri: Maelezo ya mimea zaidi ya 250 kwenye jiwe la udongo lenye umri wa miaka 5000.
4. China ya Kale (Pen Tโ€™sao): Mwaka 2500 KK, mimea 365 ya dawa iliorodheshwa.
5. Uhindi wa Kale (Veda): Viungo k**a karafuu, pilipili manga, na kungu vilitumika kwa tiba.
_______________________________________________________________________
Hapa Tanzania, tafiti nyingi zimefanyika chini ya Taasis ya Utafiti wa Tiba โ€“ NIMR, ambapo mimea tiba imetumika kutengeneza dawa mbalimbali zenye ufanisi k**a Nimrcaf, Persivin, Nimrevit, Nimregenin na nyingine nyingi. Hii ni hatua kubwa ya kuthibitisha mchango wa mimea tiba na chakula katika sekta ya Afya. https://surl.li/ccsdgj
๐Ÿ“˜ Tegemea kupokea kitabu hiki hivi karibuni! Tutaweka wazi jinsi ya kukipata na kushiriki elimu hii kwa manufaa ya jamii yetu.
_______________________________________________________________________
Tiba Asilia โ€“ Maarifa Halisi kwa Maisha Bora
๐Ÿ“Œ Endelea kufuatilia ukurasa huu kwa taarifa zaidi.

๐ŸŒฟ Ondoa Tatizo la Kufunga Choo kwa Kutumia Mkunde Pori (Senna occidentalis) ๐ŸŒฟJe, unapata choo mara ngapi kwa wiki?Kwa ka...
31/05/2025

๐ŸŒฟ Ondoa Tatizo la Kufunga Choo kwa Kutumia Mkunde Pori (Senna occidentalis) ๐ŸŒฟ

Je, unapata choo mara ngapi kwa wiki?
Kwa kawaida mtu mwenye afya nzuri anapaswa kupata haja kubwa kati ya mara 3 kwa siku hadi mara 3 kwa wiki, kutegemea aina na kiasi cha chakula anachokula, mda anaokula pamoja shughuli anazofanya, n.k.

Usipuuzie tatizo la kutopata haja kubwa kwa mda mrefu, tumbo kujaa gesi, maumivu ya tumbo, n.k kwani uweza kusababisha kupata Kiungulia (Acid Reflux), Vidonda vya tumbo (gastritis - stomach ulcers), bawasiri, saratani ya utumbo, n.k siku za mbeleni. Kila aliyepata vidonda vya tumbo au bawasiri n.k kuna dalili zilijionesha kwenye mfumo wake wa mmeng'enyo wa chakula lakini kwasababu alipuuzia kwasababu hakuwa na elimu ya uelewa kuhusu afya ya tumbo na mmeng'enyo wa chakula leo unatumia gharama kubwa kutafuta tiba.

๐Ÿ”ฌ Uthibitisho wa Kisayansi kuhusu Mkunde Pori
Tafiti mbalimbali zilizofanyika ulimwenguni kote zimeonesha kwamba mmea wa Mkunde pori (Senna occidentalis) una viambata vya asili zaidi ya 8โ€“12 vyenye manufaa ya kiafya, vikiwemo:

1. Alkaloids
2. Flavonoids
3. Tannins
4. Anthraquinones (hasa sennosides A & B)
5. Saponins
6. Phenols,
7. phlobatannin,
8. xanthoproteins,
9. steroid,
10.cardiac-active glycoside,
11. carbohydrate,
12. protein,
13. fixed oil na vingine vingi.

Viambata hivi vinapatikana kwenye sehemu mbalimbali za mmea k**a majani, mbegu, mizizi, magome, na maganda ya mbegu.

Hivyo uwepo wa viambata kemikali asilia kwenye mmea wa mkunde pori umeufanya mmea huo kuwa na sifa zifuatazo;

๐Ÿ”นUwezo wa kupambana na vijidudu vinavyosababisha maradhi (Antimicrobial properties).
๐Ÿ”นUwezo wa kulinda seli dhidi ya uharibifu wa vioksidishaji (Antioxidants โ€“ upaired molecules and atoms).
๐Ÿ”นUwezo wa kuzuia uvimbe na maumivu ya mwili. (Anti-inflammatory).
๐Ÿ”นUwezo wa kuchochea kupata choo/haja kubwa na kuondoa tatizo la kufunga choo (constipation).

Hivyo, katika somo hili tutaangazia viambata vya msingi na vyenye umuhimu katika kutatua na kutibu changamoto ya kufunga choo.

๐Ÿšฝ Jinsi Mkunde Pori Husaidia Kupata Choo:
Uwepo wa viambata kemikali asilia kwenye mme wa Mkunde pori kiitwacho Anthraquinones glycoside aina ya sennosides A na B ambacho upatikana kwa kiwango kikubwa kwenye Majani ya mmea (leaves), Kikonyo cha Majani (plant leaflets) na ganda lililobeba mbegu za Mkunde pori (pods).

Kiambata hiki asili cha Anthraquinones kwenye mmea wa Mkunde pori kina sifa ya kikemikali katika mfumo wa mmengโ€™enyo wa chakula kwani uchochea mchakato wa utengenezaji wa haja kubwa kiufasaha (stool formation process), kuchochea mjongeo wa taka Mwili izo ndani ya utumbo mpana (bowel movements) na kuchochea kupata choo (Laxative and purgative effects) na hivyo kuondosha changamoto ya kufunga choo (constipation).

Kivipi Kiambata kemikali asili (Anthraquinones glycoside) kwenye mmea wa Mkunde pori kinaondoa tatizo la kufunga choo/kutopata haja kubwa kiufasaha:-

๐Ÿ”นKuchochea ulinganifu wa uzalishaji (hydration) na utunzaji wa majimaji wakati wa utengenezaji wa haja kubwa (Intestinal fluid balance - fluid secretion):
Ukosefu wa kiwango cha kutosha cha majimaji mwilini โ€“ kutokana na sababu mbalimbali k**a vile unywaji wa maji kidogo (chini ya lita 3 kwa siku au vikombe 15), kuharisha, kutapika, kufanya mazoezi mazito au kazi zinazochochea jasho, homa kali, na kukojoa mara kwa mara โ€“ unaweza kusababisha tatizo la kufunga choo. Hali hii hutokea kwa sababu uhaba wa majimaji hufanya kinyesi kuwa kigumu, kikavu, na kigumu kusukumwa nje ya mwili kwa wakati unaofaa.

Moja ya kazi kuu za koloni (sehemu ya utumbo mpana) ni kufyonza majimaji na virutubisho vilivyosalia kwenye mabaki ya chakula. Ikiwa taka mwili hukaa kwa muda mrefu kwenye koloni kabla ya kutolewa, mchakato huu huendelea kufyonza majimaji zaidi kutoka kwenye kinyesi, hivyo kukifanya kiwe kigumu zaidi, chenye mikatiko, na kigumu kujongea au kusukumwa nje ya mwili.

๐Ÿ”น Kuchochea misuli ya utumbo mpana (colon) kutanuka na kusinyaa (stimulation of bowel muscles motility โ€“ contraction and relaxation of colon wall muscles):
Kitendo iko kufanya haja kubwa (stool) kujongea kwa kusukumwa ndani ya utumbo mpana kwenda kwenye puru (re**um) na kutoka nje kupitia sehemu ya kutolea haja kubwa (mkundu/Anus) k**a haja kubwa (f***s).
Jambo la msingi na la kuzingatia, ili mjongeo wa taka mwili kwenye utumbo mpana uwe endelevu na wenye ufanisi unashauliwa kutumia vyakula vyenye nyuzinyuzi, nafaka isiyo kobolewa na vinywaji asilia (k**a maji safi na salama, juisi ya matunda isiyosindikwa, maziwa, n.k).

๐Ÿฅฃ Jinsi ya kuandaa tiba ya asili ya kuvimbiwa kwa kutumia Mkunde pori (Senna occidentalis):
1. Kutumia majani

Mahitaji:

๐Ÿ”นMajani mabichi ya Mkunde pori (ya kijani)
๐Ÿ”นKikombe 1 cha maji safi

Namna ya kuandaa:

๐Ÿ”น Chemsha kikombe kimoja cha maji.
๐Ÿ”น Weka majani 5โ€“7 ya mmea huu kwenye maji ya moto.
๐Ÿ”นFunika na acha yachemke kwa dakika 10.
๐Ÿ”นTumia k**a chai ya dawa (infusion).

2. Kutumia majani yaliyokaushwa (tea powder or decoction):
Tumia majani yaliyosagwa au yaliyokaushwa.

๐Ÿ”นChemsha kijiko kimoja kwenye vikombe 2 vya maji hadi vipungue nusu.
๐Ÿ”นTumia nusu kikombe asubuhi na nusu jioni.

๐Ÿงด Dozi (kipimo kinachopendekezwa):

๐Ÿ”นWatu wazima: Nusu kikombe, Mara 1โ€“2 kwa siku (sio zaidi ya siku 7 mfululizo).
๐Ÿ”นWatoto (zaidi ya miaka 12): Robo kikombe, Mara 1 kwa siku.
๐Ÿ”นWatoto chini ya miaka 12: Haipendekezwi bila ushauri wa daktari au mtaalamu wa tiba asili

โš ๏ธ Tahadhari Kabla ya Kutumia Mkunde Pori (Side effects)
K**a dawa yoyote ya asili, matumizi yasiyo sahihi ya Mkunde pori yanaweza kusababisha madhara yafuatayo:

๐Ÿšซ Kichefuchefu (Nausea),
๐Ÿšซ Kupata maumivu ya tumbo(due to abnorminal cramps - intestine cramps)
๐Ÿšซ kutapika (Vomiting)
๐Ÿšซ kuharisha (Diarrhea)
๐Ÿšซ Shida za ini au figo (Liver and Kidney Concerns)
๐Ÿšซ Mzio kwa Baadhi ya watumiaji (Allergic Reactions) k**a vile upele wa ngozi, kuwasha n.k
๐Ÿšซ Upungufu wa electrolaiti muhimu k**a sodium, potassium n.k.
๐Ÿšซ Matumizi ya muda mrefu yanaweza kusababisha utegemezi wa dawa za kuharisha.

โœ… TAHADHARI - Maelekezo Muhimu ya Matumizi Salama:

Usitumie mmea wa Mkunde pori bila ushauri wa mtaalamu wa Afya
Tumia kwa kufuata kipimo (dose) ulichoelekezwa/fuata maelekezo kwenye lebo ya bidhaa au k**a ilivyoshauriwa na mtaalamu wa afya.

๐Ÿ”น Tumia kwa ushauri wa tabibu au mtaalamu wa afya.
๐Ÿ”น Fuata kipimo sahihi kilichoelekezwa.
๐Ÿ”น Tumia kwa muda mfupi tu.
๐Ÿ”น Kunywa maji mengi (angalau lita 3 kwa siku).
๐Ÿ”น Epuka kwa wajawazito, wanaonyonyesha, na watoto bila ushauri wa kitaalamu.
๐Ÿ”นWeka Mbali na Watoto au matumizi yake kwa watoto yanafuata muongozo wa kitabibu.
๐Ÿ”นNivyema k**a unatumia dawa nyengine za hospitali k**a vile dawa za kutuliza shinikizo la damu, kisukari, kusafisha njia ya mkojo n.k, au unachangamoto za kiafya k**a vile shida za mfumo wa chakula, magonjwa ya moyo, au changamoto ya kutokuwa na uwiano wa elektrolaiti tafadhali tafuta ushauri na muongo wa tabibu.

Nyongeza: Unaweza tumia mmea wa mkunde pori kusafisha tumbo kwa kuondoa vimelea/vijidudu hatari tumboni, kuondoa mabaki ya chakula (taka mwili).

Address

Tanga

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tiba Asili ya Mimea na Chakula posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Tiba Asili ya Mimea na Chakula:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category