Dr Mabisi

Dr Mabisi Tunaelimisha, tunahamasisha.

Afya yako ni msingi wa maisha bora.
| Tiba | Lishe | Mazoezi | Afya ya Akili |
Wasiliana nasi: emmanuelmabisi5@gmail.com
WhatsApp +255 652 399090

15/01/2026

Wanaume eeheee kunakikao chetu huku!!

JINSI YA KUTUNZA SEHEMU ZA SIRI ZA WANAWAKE ILI ZIWE SAFI, ZENYE AFYA, ZINAVYOKAZA NA KUTOA HARUFU NZURI 💃Mahitaji:Karaf...
15/01/2026

JINSI YA KUTUNZA SEHEMU ZA SIRI ZA WANAWAKE ILI ZIWE SAFI, ZENYE AFYA, ZINAVYOKAZA NA KUTOA HARUFU NZURI 💃

Mahitaji:
Karafuu
Ndimu
Tangawizi

Hatua ya 1:
▪️Osha vyote kwa maji safi.
▪️Chukua sufuria safi, weka karafuu na maji safi kisha chemsha kwa dakika 10.

Hatua ya 2:
▪️Kata tangawizi na ndimu vipande vidogo na weka pembeni.
▪️Zima moto baada ya dakika 10.
▪️Ongeza tangawizi na ndimu kwenye mchanganyiko wa karafuu kisha funika kwa dakika nyingine 10.

✅Sasa chai yako ya karafuu iko tayari.

Kunywa kikombe kimoja mara 3 kwa siku.

Kumbuka: Usitumie wakati wa hedhi au ukiwa mjamzito.

DALILI ZA KUSHUKA KWA MFUKO WA UZAZI (UTERINE PROLAPSE)Kushuka kwa mfuko wa uzazi hutokea pale misuli na mishipa ya saka...
13/01/2026

DALILI ZA KUSHUKA KWA MFUKO WA UZAZI (UTERINE PROLAPSE)

Kushuka kwa mfuko wa uzazi hutokea pale misuli na mishipa ya sakafu ya nyonga (pelvic floor) inaponyooshwa na kudhoofika kiasi kwamba haiwezi tena kuushikilia mfuko wa uzazi ipasavyo. Matokeo yake, mfuko wa uzazi hushuka chini au hujitokeza nje ya uke.

Kushuka kwa mfuko wa uzazi kunaweza kusababisha dalili zifuatazo:
▪️ Kuona au kuhisi nyama ikijitokeza nje ya uke
▪️ Kuhisi uzito au mvutano katika eneo la nyonga
▪️ Kuhisi kana kwamba kibofu cha mkojo hakimalizi mkojo wote unapokwenda chooni
▪️ Matatizo ya kuvuja mkojo bila kuthibitiwa (incontinence)
▪️ Kupata shida wakati wa haja kubwa na kulazimika kushinikiza uke kwa vidole ili kusaidia haja kutoka
▪️ Kuhisi k**a umekaa juu ya mpira mdogo
▪️ Kuhisi k**a ngozi ya uke inasugua nguo
▪️ Shinikizo au maumivu katika nyonga au sehemu ya chini ya mgongo
▪️ Matatizo ya kijinsia, k**a kuhisi kwamba uke umekuwa mpana au legevu

Iwapo unapata dalili zozote kati ya hizi, inapendekezwa sana kuzungumza na mtaalamu wa huduma za afya kwa uchunguzi zaidi.

Au piga +255 652 399 090 kwa ushauri..

13/01/2026

Kwa wale wavivu wa kuandaa nyumbani kwao mafuta yapo yaliyoandaliwa Kwa ngozi nyororo uonekane mrembo,,hata k**a una mabaka hii inakwangua kila kitu.

Piga +255 652 399 090

Chukua tango na tangawizi saga kisha kamlia limao,Kunywa glasi 1 kila siku. Husaidia kushusha shinikizo la damu kwa asil...
13/01/2026

Chukua tango na tangawizi saga kisha kamlia limao,Kunywa glasi 1 kila siku.

Husaidia kushusha shinikizo la damu kwa asili, kuharakisha umeng’enyaji,
kuzuia na kuyeyusha mawe kwenye figo,
kusafisha ngozi kuwa safi na ang’avu zaidi

Mdharau asili hufa kikatili

13/01/2026

Eti Anashangaaa ndo ukweli wenyewe huo!!

12/01/2026

Haya haya kina dada changamkia fursa hii!

MBEGU ZA MLONGE (MORINGA SEEDS)Ukitafuna mbegu za mlonge, zinaongeza hamu ya tendo la ndoa (kwa jinsia zote). Hebu tafun...
12/01/2026

MBEGU ZA MLONGE (MORINGA SEEDS)

Ukitafuna mbegu za mlonge, zinaongeza hamu ya tendo la ndoa (kwa jinsia zote). Hebu tafuna angalau mbegu 10 kwa siku, baada ya siku tatu utaona matokeo.

Mbegu za mlonge zimethibitishwa kwa kutibu matatizo k**a vile:-

📌Maumivu ya kichwa: k**a kichwa kinakuuma usimese action wewe tafuna mbegu 5 tu kisha kunywa maji.

📌Kulinda Ini: mbegu za mlonge zinasafisha mafuta yanayoganda kwenye ini na kuongeza utendakazi wa Ini

✓Ni nzuri kwa afya ya moyo
✓Zinarekebisha kiwango cha sukari kwenye damu.
✓Zinapunguza unene (kuondoa kitambi)
✓Ni nzuri kwa afya ya figo (zina uwezo wa kuondoa mawe kwenye figo)

Mdharau asili hufa kikatili

Piga +255 652 399 090 weka oda yako..

KUNYWA MAJI YA MOTO TUMBO LIKIWA TUPU Kwa mujibu wa wanasayansi, kunywa maji ya moto ukiwa na tumbo tupu kuna faida nyin...
11/01/2026

KUNYWA MAJI YA MOTO TUMBO LIKIWA TUPU

Kwa mujibu wa wanasayansi, kunywa maji ya moto ukiwa na tumbo tupu kuna faida nyingi za kiafya na husaidia kuzuia magonjwa.

📌Pia husaidia kutibu matatizo ya hedhi, pumu, maumivu ya kichwa, magonjwa ya macho, maumivu ya mwili, cholesterol nyingi, kufunga choo, matatizo ya moyo, mapigo ya moyo kwenda kasi, kisukari, kifafa, meningitis, kifua kikuu (TB), bronchitis, magonjwa ya figo na njia ya mkojo, kuharisha, kutapika, bawasiri, magonjwa ya sikio, mfuko wa uzazi, koo na pua.

Jinsi ya kutumia
Kila asubuhi, mara tu unapoamka, unapaswa kunywa glasi za maji ya moto. Baada ya hapo unaweza kupiga mswaki; hata hivyo, hupaswi kula au kunywa kitu chochote kwa dakika arobaini na tano zinazofuata.

Baada ya dakika arobaini na tano kupita, utaweza kula au kunywa chochote unachopenda.
Tiba hii haina madhara, haina matokeo yasiyotakiwa, na ni yenye manufaa makubwa sana.

Vyakula vinavyosaidia mfupa uliovunjika kupona na kuungana haraka ni vile vyenye virutubisho muhimu k**a kalsiamu, proti...
11/01/2026

Vyakula vinavyosaidia mfupa uliovunjika kupona na kuungana haraka ni vile vyenye virutubisho muhimu k**a kalsiamu, protini, vitamini D, vitamini C, na madini ya zinki.

Hivi ni baadhi ya vyakula muhimu:
🦴 Vyakula vyenye Kalsiamu
Maziwa, mtindi (yogurt), jibini
Mboga za majani ya kijani (sukuma wiki, spinachi, mchicha)
Samaki wadogo wanaoliwa na mifupa (dagaa, sardine)

🍗 Vyakula vyenye Protini
Mayai
Nyama (hasa ya kuku, ng’ombe)
Samaki
Maharage, dengu, choroko
Karanga, korosho, ufuta

☀️ Vitamini D (husaidia mwili kutumia kalsiamu)
Samaki wa mafuta (samaki wa bahari k**a salmoni, sato)
Mayai (hasa kiini)
Maziwa yaliyoimarishwa
Kupata mwanga wa jua asubuhi 🌞

🍊 Vitamini C (husaidia kutengeneza tishu mpya)
Machungwa, ndimu, maembe
Papai
Pilipili hoho
Nyanya

⚙️ Madini ya Zinki & Magnesiamu
Karanga na mbegu (mbegu za maboga, alizeti)
Nafaka zisizokobolewa (unga wa dona, mchele wa kahawia)
Ndizi, parachichi

🚫 Mambo ya Kuepuka
Pombe
Sigara
Kahawa nyingi (hupunguza ufyonzwaji wa kalsiamu)

💡 Ushauri wa Ziada
Fuata maelekezo ya daktari (k**a kuvaa plasta au kifaa cha kusaidia mfupa)
Kula mlo kamili kila siku
Pumzika vya kutosha

Piga kwa ushauri +255 652 399 090

UVIMBE MAJI KWENYE YAI (OVARIAN CYSTS)Umewahi kuusikia?Inawezekana una uvimbe huo sasa hivi ila wewe hujui....▪️Lakini n...
09/01/2026

UVIMBE MAJI KWENYE YAI (OVARIAN CYSTS)

Umewahi kuusikia?

Inawezekana una uvimbe huo sasa hivi ila wewe hujui....

▪️Lakini ni nini hasa?
▪️Hutokeaje?
▪️Ni hatari au ni saratani?
▪️Je, hurithiwa kifamilia?

📌 Uvimbe maji kwenye yai (ovarian cysts) ni mifuko midogo iliyojaa majimaji inayokua ndani ya yai (o***y) au juu ya uso wake.

Mayai (ovaries) ni tezi ndogo zinazohusika na: Kutengeneza mayai ya uzazi na kutengeneza homoni—Ni sehemu muhimu sana ya mfumo wa uzazi wa mwanamke.

Uvimbe hutokea pale kunapokuwa na hitilafu fulani katika utendaji wa mayai.

Kuna aina mbili za uvimbe maji wa yai:
▪️Uvimbe wa kawaida (Functional cysts)
▪️Uvimbe usio wa kawaida (Non-functional cysts)

🔹 Uvimbe wa kawaida (Functional cysts)
Hutokea kutokana na mabadiliko ya mzunguko wa hedhi.
Hapa pia kuna aina mbili:

1. Follicular cyst: Hutokea pale yai linaposhindwa kutoka wakati wa ovulation (kutoa yai) — Follicle iliyokuwa imebeba yai huendelea kukua na kutengeneza uvimbe.

2. Corpus luteum cyst: Hutokea baada ya yai kutoka. Baada ya ovulation, corpus luteum inapojiziba, majimaji hukusanyika na kusababisha uvimbe — Uvimbe wa aina hii mara nyingi si hatari na hupona wenyewe bila matibabu.

🔹 Uvimbe usio wa kawaida (Non-functional cysts)
Hauhusiani na mzunguko wa hedhi.
Hutokea kutokana na ukuaji usio wa kawaida wa seli kwenye mayai.
Mfano:
▪️Dermoid cyst
▪️Cystadenoma
▪️Endometrioma
Uvimbe huu ni nadra kutokea na hutokana na:
- Seli zinazotengeneza mayai
- Seli za juu ya uso wa yai
- Au ugonjwa wa endometriosis

📌 Je, uvimbe huu ni saratani?
Uvimbe wa saratani ni nadra sana. Zaidi ya 80% ya uvimbe wa mayai si saratani.

📌 Je, uvimbe huu hurithiwa?
Sio uvimbe wote hurithiwa. Endometrioma na dermoid cyst zina uhusiano wa kinasaba, lakini ni nadra.

📌 Dalili zake ni zipi?
Mara nyingi uvimbe hauna dalili, lakini unaweza kuleta:
▪️Maumivu ya nyonga
▪️Kuhisi tumbo limejaa au kuwa zito
▪️Tumbo kujaa gesi (bloating)
▪️Hedhi zenye maumivu au zisizo na mpangilio

📌 Sababu hatarishi (risk factors):
▪️Kutobalansi kwa homoni
▪️Matumizi ya dawa k**a clomiphene au letrozole
▪️Ujauzito
▪️Endometriosis
▪️Maambukizi makali ya nyonga
▪️Historia ya awali ya uvimbe wa mayai

📌 Je, hutibika?
▪️Uvimbe wa kawaida hupona wenyewe
▪️Uvimbe usio wa kawaida hufuatiliwa na dawa hutolewa kupunguza ukubwa wake
▪️Ukikua sana, upasuaji unaweza kufanyika

📌 Nani hupata uvimbe wa mayai?
Wanawake wote walioko katika umri wa kuzaa wana uwezekano wa kupata uvimbe wa mayai.

📌 Je, uvimbe huathiri uzazi?
▪️Uvimbe wa kawaida hauathiri uzazi moja kwa moja unaonyesha uwezo wa kushika mimba
▪️Lakini baadhi ya uvimbe k**a “endometrioma” unaweza kusababisha utasa, hasa kutokana na ugonjwa husika
▪️Uvimbe mkubwa unapofanyiwa upasuaji, huweza kuathiri uzazi

📌 ZINGATIA
- Uvimbe wa mayai mara nyingi si wa kutisha na mingi hupona yenyewe.
- Ikiwa unapata dalili zisizo za kawaida,
tafadhali muone daktari.
- Vipimo vitafanyika na matibabu yataanza kulingana na hali yako.

Elimu haina mwisho—shiriki na wengine ujumbe huu wajifunze

Dawa zipo bila kufanyiwa upasuaji
piga +255 0652 399 090

K**a unasumbuliwa na Vibarango, Mapunye, Fungus (ringworm) za kichwa.▪️Chukua papai bichi▪️Kata vipande vidogo vidogo▪️T...
09/01/2026

K**a unasumbuliwa na Vibarango, Mapunye, Fungus (ringworm) za kichwa.

▪️Chukua papai bichi
▪️Kata vipande vidogo vidogo
▪️Tumia vipande hivyo kujisugulia kichwani
▪️Kaa kwa muda wa dakika 15
▪️Kisha osha na maji ya vuguvugu.
▪️Fanya zoezi hili mpaka utakapopona.

Mdharau asili hufa kikatili

Piga Upate ushauri na matibabubora kabisa
+255 652 399 090

Address

Ngamiani
Tanga

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dr Mabisi posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Dr Mabisi:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram