Dr Mabisi

Dr Mabisi Tunaelimisha, tunahamasisha.

Afya yako ni msingi wa maisha bora.
| Tiba | Lishe | Mazoezi | Afya ya Akili |
Wasiliana nasi: emmanuelmabisi5@gmail.com
WhatsApp +255 652 399090

“Eucalyptus” —ndilo jina lake kisayansi, maarufu k**a Mkaratusi, ni miongoni mwa miti maarufu sana katika tiba asili kut...
21/04/2026

“Eucalyptus” —ndilo jina lake kisayansi, maarufu k**a Mkaratusi, ni miongoni mwa miti maarufu sana katika tiba asili kutokana na mafuta na majani yake kuwa na viambato vyenye nguvu za kiafya.

Matumizi ya Eucalyptus Katika Tiba za Jadi

1. Matatizo ya njia ya hewa
- Kutibu kikohozi, mafua, na sinusitis: Maji ya majani ya eucalyptus huchomwa kwenye moto, kisha mvuke huvutwa.

- Pumu (Asthma): Husaidia kupanua njia za hewa kwa kuvuta harufu ya mafuta au mvuke wa majani.

2. Maambukizi ya bakteria na fangasi
- Eucalyptus ina antibacterial na antifungal properties – hutumika kutibu vidonda, majipu, au upele wa ngozi kwa kupaka mafuta ya eucalyptus.

3. Maumivu ya misuli na viungo
- Mafuta ya eucalyptus hupakwa sehemu zenye maumivu k**a arthritis, baridi yabisi, na maumivu ya misuli ili kupunguza uvimbe na maumivu.

4. Homa na malaria
- Majani ya eucalyptus huchochea jasho na hivyo kusaidia kushusha homa. Pia hutumika kuondoa mbu wanaosababisha malaria.

5. Harufu mbaya ya mdomo
- Majani au mafuta yake hutumika k**a mouthwash ya asili, yanaua bakteria wa kinywani.

6. Kuondoa wadudu
- Mafuta ya eucalyptus huondoa kupe, chawa, na mbu – yanatumika k**a dawa ya kupaka au kunyunyiza.

7. Matatizo ya ngozi
- Hutumika kutibu chunusi, vidonda na upele kwa kupaka maji au mafuta ya eucalyptus.

Jinsi ya kutumia:
- Mvuke: Chemsha majani, jifukize na mvuke kwa dakika 5–10.
- Mafuta: Pakaa kwenye sehemu yenye maumivu au upele.
- Maji ya kuoga: Chemsha majani, changanya kwenye maji ya kuoga kwa kusafisha ngozi na kutuliza mwili.

Mdharau asili hufa kikatili

Aloe Vera | Shubiri | Shubiri Mwitu.Huu ni mmea wenye uwezo wa kutibu changamoto nyingi za kiafya kwa binadamu na hata n...
21/04/2026

Aloe Vera | Shubiri | Shubiri Mwitu.

Huu ni mmea wenye uwezo wa kutibu changamoto nyingi za kiafya kwa binadamu na hata ndege....

Leo nitaelezea faida na matumizi yake kwetu sisi.

Shubiri inatatua changamoto hizi:-

>Inatibu Typhoid
>Inasafisha kizazi
>Inasafisha mfumo wa mkojo
>Inatibu minyoo
>Inaondoa sumu mwilini na kuongeza kinga
>Utuliza na kutibu vidonda vya tumbo
>Inatibu bawasiri ya ndani na nje
>Inatibu minyoo
>Inatibu malaria sugu
>Inaondoa chunusi
>Inatibu UTI sugu
>Huondoa tatizo la kukosa choo/kupata choo kigumu
>Inatibu acid reflux
>Inatibu jino
>Inatibu presha ya kushuka
n.k n.k

Namna ya kutumia...

Chukua jani moja au mawili ya aloe vera(shubiri) lisafishe vizuri na ondoa miiba ya pembeni
...kata vipande vidogo vidogo kisha loweka kwenye maji ya vuguvugu lita moja kwa masaa 12

Baada ya masaa 12 kupita utakuwa una kunywa nusu kikombe kutwa mara mbili au mara tatu kwa siku

Utafanya hivo kwa siku 5, 7 hadi 14 kulingana na aina na ukubwa wa tatizo lako na utapona.

Kwa bawasiri ya nje tumia utomvi wake kupakaa kwenye kinyama kila baada ya ya kujisafisha

Kwa chunusi jipakae usoni na uache kwa dakika 30 kisha unajisafisha kwa maji ya vuguvugu... unafanya mara moja kwa siku kwa muda wa siku 7

Niambie ugonjwa/tatizo lingine linalotatuliwa kupitia aloe vera ili nasi tujifunze kutoka kwako..

ujumbe WhatsApp namba +255 652 399 090

Dr Mabisi
Ukiamini Umepona. Asili Haidanganyi

🍃

Umeutambua huu mmea? Tuambie mnaitaje kwa kilugha chenu.Huu mmea kisayansi hujulikana k**a "Rumex usambarensis"  kutoka ...
21/04/2026

Umeutambua huu mmea?
Tuambie mnaitaje kwa kilugha chenu.

Huu mmea kisayansi hujulikana k**a "Rumex usambarensis" kutoka kwenye familia ya Polygonaceae.

Ni mmea mzuri kwa kuongeza hamu ya kula; k**a una mgonjwa hapati hamu ya kula iwe mtoto au mtu mzima basi mpatie chai ya majani haya.
Chai hiyo husaidia pia kukata hali ya kichefuchefu na kikohozi.

Ni mmea wenye matumizi mengi katika tiba za asili k**a vile
✅️Kutibu vidonda vya tumbo
✅️Kutibu tatizo la kukosa choo
✅️Kutibu homa ya njano
✅️Kusaidia matatizo ya nguvu za kiume.
✅️Uvimbe wa mwili (Oedema)
✅️Matatizo ya ngozi

Je wewe umeutumia kujitibu nini? Dondosha comment yako hapo.

Mdharau asili hufa kikatili

Dada zangu na akina mama wajawazito ikifika tarehe za makadrio ya kujifungua;- Chukua  huu mmea wa mzalia nyuma- Chemsha...
21/04/2026

Dada zangu na akina mama wajawazito ikifika tarehe za makadrio ya kujifungua;

- Chukua huu mmea wa mzalia nyuma
- Chemsha vizuri kwa dakika 10
- Chuja na kunywa kikombe kimoja asubui na jioni

✅️Utajifungua vizuri bila upasuaji

TIBA YA MARADHI  YA ZINAAIkiwa unasumbuliwa na maradhi ya zinaa sugu n.kTumia dawa hii utaponaMAHITAJI1.Karafuu2..Tangaw...
21/04/2026

TIBA YA MARADHI YA ZINAA
Ikiwa unasumbuliwa na maradhi ya zinaa sugu n.k

Tumia dawa hii utapona

MAHITAJI

1.Karafuu
2..Tangawizi
3.Mdalasini
4.Kivumbasi
5.Binzari manjano
6.Kitunguu saumu

Hakikisha zisiwe za unga..
kila moja kiwango sawa..

Chemsha vyote kwa pamoja..
Tumia kunywa Kikombe 1 ikiwa vuguvugu kutwa mara 3 siku 21 mpaka 30..

Mafanikio mema..
Tib,dawa na ushauri
+255 652 399 090

Tanga,Dar es salaam.

KUJIVUKIZA UKE (VAGINAL STEAMING)Kujivukiza uke si jambo jipya — Ni njia ya kujitibu na kujijenga kiafya ambayo mababu z...
21/04/2026

KUJIVUKIZA UKE (VAGINAL STEAMING)

Kujivukiza uke si jambo jipya — Ni njia ya kujitibu na kujijenga kiafya ambayo mababu zetu waliitumia mara kwa mara. Walielewa kuwa ndani ya vitu vya asili (moto, maji, mvuke na mimea) kuna uwezo wa uponyaji.

Kujivukiza uke hutumika kusaidia matatizo k**a:
- Uvimbe kwenye mfuko wa uzazi (fibroids)
- Hedhi nzito
- Maumivu ya tumbo la hedhi
- Maambukizi ya bakteria
- Maambukizi ya njia ya mkojo
- Utasa usioeleweka
- Polycystic O***y Syndrome (PCOS)
- Ukavu wa uke
- Huduma baada ya kujifungua
- Majeraha ya kihisia yanayohusiana na mfuko wa - - Uzazi

Vilevile Kujivukiza uke husaidia kupambana na maambukizi ya njia ya mkojo (Urinary Tract Infection) na maambukizi mengine.

Mahitaji:
▪️Karafuu
▪️Majani ya mpera
▪️Sufuria ya maji
▪️Ndoo/beseni

Namna ya kuandaa:
▪️Chemsha maji kisha ongeza karafuu na majani ya mpera kwenye maji yanayochemka.
▪️Chota kikombe kimoja kunywa
▪️Dawa inayobaki mimina kwenye ndoo na ukae kwa juu—kujifukiza.

✅️Husaidia kupambana na maambukizi na kutoa harufu nzuri.

📌Mjamzito asitumie bila ushauri wa daktari.

TIBA ILIYOOMBWA NA WENGIUnahisi k**a kitu kimekwama kooni unakitoa unakutana na kipunje kidogo sana cheupe lakini kinato...
26/02/2026

TIBA ILIYOOMBWA NA WENGI

Unahisi k**a kitu kimekwama kooni unakitoa unakutana na kipunje kidogo sana cheupe lakini kinatoa harufu mbaya—inayokera.

Hii si hali ya kawaida ni ugonjwa wa Mawe ya Tonsils (Tonsil stones au Tonsilloliths)

Mawe ya tonsils (tonsilloliths) ni vipande vidogo vya vitu vilivyokak**aa (hasa chakula, ute na bakteria) vinavyokusanyika kwenye mifuko midogo ya tonsils, hasa za upande wa koo (palatine tonsils).

Aina 3 za tonsils:
1. Palatine – upande wa koo (ndizo wengi huziita "tonsils")
2. Pharyngeal – nyuma ya koo
3. Lingual – chini ya ulimi

Chanzo kikuu cha mawe ya tonsils: Ni chakula, ute na bakteria wanaonaswa kwenye mifuko midogo ya tonsils.

HAPA NAKUORODHESHEA TIBA ASILI ZA KUTUMIA—UTACHAGUA IPI RAHISI KWAKO KUIPATA

1️⃣ S**i ya tufaa (Apple cider vinager) au s**i yoyote yenye tindikali:
—Changanya na maji na tumia kwa gargle (kusukutua kwenye koo) mara mbili kwa siku. Husaidia kuyeyusha mawe madogo na kuua bakteria.

2️⃣ Matunda ya Mwarobaini (Neem fruits)

● Chukua matunda ya mwarobaini
● Kula kwa kufyonza nyama yake na utupe mbegu
● Kula mbegu 5 asubuhi na jioni
● Fanya zoezi hilo kwa siku 7 hadi 14
● Utapona na harufu mbaya ya kinywa itapotea

Hakikisha asubuhi unapoamka kabla ya kupiga mswaki unasukutua na maji ya moto yaliyotiwa chumvi.

3️⃣ MCHANGANYIKO MAALUMU

Mahitaji
● Kitunguu
● Kitunguu swaumu
● Tangawizi
● Limao

Maandalizi ya dawa
▪️Osha viambata vyako na ukate vipande vipande
▪️Weka kwenye sufuria ya maji na uchemshe
✅️Njia nyingine ya maandalizi unaweza kusaga/blend ukapata juisi

Matumizi:
▪️Kunywa kwa kusukutua (gargle) kwenye koo
▪️Tumia asubuhi mchana na jioni kwa siku 7 - 14

4️⃣ MAJANI YA KING GRASS

▪️Chukua majani ya kutosha ya mmea huu (king grass)
▪️Pondaponda na ukamue juisi yake
▪️Kamlia maji ya limao.
▪️Kunywa kwa kusukutua koo (gargle)
▪️Fanya zoezi hili asubuhi na jioni kwa siku 7

Mdharau asili hufa kikatili

15/02/2026
KUNA NGUVU KATIKA MIZIZI YA PAPAI (CARICA PAPAYA)​Kuchemsha mizizi ya papai (Carica papaya) pamoja na pilipili manga hut...
15/02/2026

KUNA NGUVU KATIKA MIZIZI YA PAPAI (CARICA PAPAYA)

​Kuchemsha mizizi ya papai (Carica papaya) pamoja na pilipili manga hutibu:
✅​Bawasiri (Piles)
✅​Malaria
✅​Maumivu ya kiuno
✅​Maumivu ya hedhi
✅​Matatizo ya nguvu za kiume (Erectile issues)
✅​Mvurugiko wa vichocheo mwilini (Hormonal imbalance)
✅​Maambukizi ya vimelea vya “Staphylococcus”

​Maelekezo:
Chemsha mchanganyiko huu kwa muda wa dakika 20 mpaka 30 na unywe kikombe kimoja cha chai mara mbili kwa siku.
Unaweza kuongeza limao kwa ajili ya ladha

📌Mizizi ya papai dume ndiyo yenye ufanisi mkubwa katika tiba

​Faida nyingine:
Mmea huu una uwezo pia kusaidia kwenye matatizo ya figo, k**a vile kuondoa mawe au mchanga (mineral concretions) kwenye figo.

DAWA YA MASIKIO NA MACHOChukua kitunguu swaumu na kitunguu maji menya kisha saga upate juisi yake weka na asali kidogo.Y...
15/02/2026

DAWA YA MASIKIO NA MACHO

Chukua kitunguu swaumu na kitunguu maji menya kisha saga upate juisi yake weka na asali kidogo.

Yeyusha almiti kidogo changanya na juisi yako uliyoandaa.

1.Kwa matatizo ya macho
A. Weka tone 1 kwenye macho muda wa kulala tu kila siku
B.Changanya na unga mdalasini,pakaa kwenye kope...

Ni usku tu wakati wa kulala.

Faida zake
1.Hutibu macho kuuma,
2.Macho kuwasha,
3. kuhisi michanga machoni,
4.kuona giza (uoni hafifu),
5.Macho kutoa tongotongo,
6.Macho kuwa mekundu,

(Wekundu wa macho sio ishara ya uchawi,wala uzee sio ishara ya uchawi..uchawi ni taaluma anayofundishwa mtu kwa kuandaliwa muda mrefu)

2.MASKIO

1.weka tone 1 mas**ioni usku muda wa kulala.

FAIDA ZAKE
1. Huondoa fangasi s**ioni
2.Maumivu ya s**io,
3.Us**ivu hafifu,
4.Mas**io kuunguruma au kupiga kelele,

5.Vidonda mas**ioni.

FAIDA ZA JUMLA ZA JUISI HIYO
1.Kusafisha damu,
2.Kusafisha Tumbo, 3.Kuupa nguvu moyo, 4.Kuondoa uchovu, 5.Maumivu ya kichwa, 6.Matatizo ya moyo kwenda mbio,
7.Kupoteza hisia, 8.Kutopata hedhi,
9.Ukiweka tangawizi tu..inatibu nguvu za kiume,homon imbalance, kusafisha kizazi n.k

Mafanikio mema Mtanzania

Tiba dawa na ushauri
+255 652 399 090

14/02/2026

Unapendelea nini leo kwenye siku ya Valentines day 💓 💖

Address

Ngamiani
Tanga

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dr Mabisi posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Dr Mabisi:

Share