26/02/2026
TIBA ILIYOOMBWA NA WENGI
Unahisi k**a kitu kimekwama kooni unakitoa unakutana na kipunje kidogo sana cheupe lakini kinatoa harufu mbaya—inayokera.
Hii si hali ya kawaida ni ugonjwa wa Mawe ya Tonsils (Tonsil stones au Tonsilloliths)
Mawe ya tonsils (tonsilloliths) ni vipande vidogo vya vitu vilivyokak**aa (hasa chakula, ute na bakteria) vinavyokusanyika kwenye mifuko midogo ya tonsils, hasa za upande wa koo (palatine tonsils).
Aina 3 za tonsils:
1. Palatine – upande wa koo (ndizo wengi huziita "tonsils")
2. Pharyngeal – nyuma ya koo
3. Lingual – chini ya ulimi
Chanzo kikuu cha mawe ya tonsils: Ni chakula, ute na bakteria wanaonaswa kwenye mifuko midogo ya tonsils.
HAPA NAKUORODHESHEA TIBA ASILI ZA KUTUMIA—UTACHAGUA IPI RAHISI KWAKO KUIPATA
1️⃣ S**i ya tufaa (Apple cider vinager) au s**i yoyote yenye tindikali:
—Changanya na maji na tumia kwa gargle (kusukutua kwenye koo) mara mbili kwa siku. Husaidia kuyeyusha mawe madogo na kuua bakteria.
2️⃣ Matunda ya Mwarobaini (Neem fruits)
● Chukua matunda ya mwarobaini
● Kula kwa kufyonza nyama yake na utupe mbegu
● Kula mbegu 5 asubuhi na jioni
● Fanya zoezi hilo kwa siku 7 hadi 14
● Utapona na harufu mbaya ya kinywa itapotea
Hakikisha asubuhi unapoamka kabla ya kupiga mswaki unasukutua na maji ya moto yaliyotiwa chumvi.
3️⃣ MCHANGANYIKO MAALUMU
Mahitaji
● Kitunguu
● Kitunguu swaumu
● Tangawizi
● Limao
Maandalizi ya dawa
▪️Osha viambata vyako na ukate vipande vipande
▪️Weka kwenye sufuria ya maji na uchemshe
✅️Njia nyingine ya maandalizi unaweza kusaga/blend ukapata juisi
Matumizi:
▪️Kunywa kwa kusukutua (gargle) kwenye koo
▪️Tumia asubuhi mchana na jioni kwa siku 7 - 14
4️⃣ MAJANI YA KING GRASS
▪️Chukua majani ya kutosha ya mmea huu (king grass)
▪️Pondaponda na ukamue juisi yake
▪️Kamlia maji ya limao.
▪️Kunywa kwa kusukutua koo (gargle)
▪️Fanya zoezi hili asubuhi na jioni kwa siku 7
Mdharau asili hufa kikatili