07/04/2025
Wizara ya Katiba na Sheria kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga inawatangazia wananchi wote kuwa tarehe 08 Aprili 2025 katika Uwanja wa Tangamano, kutafanyika Uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Mkoani Tanga.
Mgeni rasmi katika uzinduzi huu ni Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. DKT. DAMAS NDUMBARO
Uzinduzi huu utafuatiwa na utoaji wa Huduma za Msaada wa Kisheria bila malipo katika Halmashauri zote za Mkoa wa Tanga ikijumuisha Kata, Vijiji na Mitaa kwa kipindi cha siku 9 kuanzia tarehe 08 Aprili, 2025 hadi tarehe 17 Aprili 2025.
Kampeni hii itahusisha utoaji elimu kuhusu masuala mbalimbali ya kisheria k**a vile Ardhi, Haki za Binadamu na Utawala Bora, Mirathi, Ndoa, talaka, Ukatili wa Kijinsia, Madai na Jinai, vilevile itahusisha huduma ya usajili na utoaji vyeti vya kuzaliwa na kifo vitakavyotolewa na RITA, pamoja na vitambulisho vya Taifa, NIDA.
Wananchi wote mnakaribishwa. Usikiapo tangazo hili, Mjulishe na jirani yako.