Dr sao AFYA

Dr sao AFYA habari zenu ukurasa huu Ni kwa ajili ya
USHAURI
NA
TIBA
NB:kuhusu Tatizo la AFYA tunatibu
kwa k

Karibu sana
13/08/2021

Karibu sana

MAFUTA MGANDO (Petroleum Jelly) yapo sokoni kwa zaidi ya karne moja na nusu; yameendelea kuaminiwa na madaktari bingwa w...
19/08/2020

MAFUTA MGANDO (Petroleum Jelly) yapo sokoni kwa zaidi ya karne moja na nusu; yameendelea kuaminiwa na madaktari bingwa wa ngozi k**a mafuta rafiki kwa ngozi hasa kwa watu wenye shida za ngozi k**a mzio na vidonda

Zifuatazo ni Faida za Kutumia Mafuta ya Mgando kwa Afya.

✴Mafuta ya mgando hutengeneza mazingira wezeshi ambayo huchochea vidonda hasa michubuko kupona haraka.

✴Hupunguza uwezekano wa maambukizi kwenye vidonda vidogo kwenye ngozi.

✴Mafuta mgando husaidia afya ya ngozi na kupunguza dalili mbaya za magonjwa yatokanayo na mzio wa ngozi k**a pumu ya ngozi na magonjwa mengine k**a psoriasis.

✴Hupunguza uwezekano wa kupata muwasho wa ngozi.

✴Mafuta mgando husaidia kupunguza mzio wa ngozi kwa watoto , Mzio wa ngozi husababisha ngozi za watoto kuwasha na kutoka mapele
Mafuta ya Mgando huweza kutumika kwa mtoto kuanzia wiki 3

✴Mafuta mgando husaidia kuilinda ngozi ya mtoto dhidi ya vipele vya pampers (diaper rash) ambavyo husababishwa na mikojo/kinyesi kuathiri ngozi.

✴Mafuta mgando hayana kemikali zaidi hivyo huwa rafiki kwa ngozi.

✴Mafuta mgando husaidia kupunguza maumivu kwa mtu mwenye bawasiri (hemorrhoid)
Bawasiri huweza kusababisha maumvu wakati wa haja kubwa, mafuta ya mgando husaidia kupunguza hiyo. hali

MUHIMU
Mafuta mgando hayafai kuwa kilainishi wakati wa kufanya mapenzi kwani huweza kuongeza uwezekano wa Kondomu kupasuka.

Ukiwa na swali uliza

Kumbemenda mtoto ni nadharia inayomaanisha kudhoofika kwa afya ya mtoto wakati wa siku za mwanzo kabisa za matumizi ya z...
18/08/2020

Kumbemenda mtoto ni nadharia inayomaanisha kudhoofika kwa afya ya mtoto wakati wa siku za mwanzo kabisa za matumizi ya ziwa la mama yake.

Hudhaniwa kutokana na mama kushiriki tendo la ndoa na mmewe au hata kutoka nje ya ndoa wakati bado ananyonyesha.Imani hii huenda mbali zaidi kwa kueleza kuwa shahawa au mbegu za kiume zinazomwagwa wakati wa tendo la ndoa huingia na kuchanganyikana na maziwa ya mama ambayo baadae hunyonywa na mtoto hivyo kusababisha hali ya kubemendwa kwa mtoto
UKWELI NI UPI?
Haya ni madai ya uongo kwa 100% na hayana hata chembe ya ukweli.Shahawa/manii au hata mbegu za kiume zinazotolewa wakati wa tendo la ndoa huishia safari yake kwenye tumbo la uzazi na huharibiwa huko.Haziwezi kuingia kwenye mfumo wa mzunguko wa damu mwilini hivyo hakuna namna zitaingilia uzalishwaji wa maziwa ya mama
LINI MWANAMKE AFANYE MAPENZI BAADA YA KUJIFUNGUA?
Tendo hili mara nyingi hushauriwa lifanyike wiki 6 baada ya kujifungua.Linaweza pia kufanyika hata baada ya wiki 4 ikiwa tu uchafu na majimaji yenye damu yanayotolewa na mama kupitia uke yatakoma.Tendo hili hutegemea utayari wa mama,uwezo wake katika kulihimili na kasi ya kupona kwa vidonda na mipasuko aliyoipata wakati wa kujifungua.
MUHIMU
Kubemendwa kwa mtoto hakuna uhusiano wowote na kufanya mapenzi.Ukiona afya ya mwanao inadhoofika ni lazima atakuwa na matatizo ya kiafya,au hata hapati matunzo na virutubisho vya kutosha.Inaweza ikawa sababu hapati maziwa ya mama ya kutosha,hanyonyi vizuri,kuanzishiwa vyakula vya ziada mapema hasa kabla ya miezi 6 ya mwanzo,homa za mara kwa mara,nimonia,UTI pamoja na matatizo mengine mengi.Ni vyema akapelekwa hospitalini mapema ili asaidiwe kuliko kuendelea na dhana POTOFU ya kusingizia kuwa tendo la ndoa ndiyo chanzo.

Ukiwa na swali uliza

Hey Tanzanians nawakaribisha sana kwenye ukurasa wangu wa DR sao AFYA KARIBU tujifunze mambo yoote kuhusu afya
12/08/2020

Hey Tanzanians nawakaribisha sana kwenye ukurasa wangu wa
DR sao AFYA
KARIBU tujifunze mambo yoote kuhusu afya

habari zenu ukurasa huu Ni kwa ajili ya
USHAURI
NA
TIBA
NB:kuhusu Tatizo la AFYA tunatibu
kwa k

Address

Temeke

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dr sao AFYA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Dr sao AFYA:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram